Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109591 articles
Browse latest View live

UNHCR YAWAWEZESHA WAKIMBIZI WENYE MAHITAJI MAALUM KUKABILIANA NA CHANAGAMOTO ZA MAISHA NDANI YA KAMBI YA NDUTA WILAYA KIBONDO MKOANI KIGOMA

0
0
Ujumbe wa Wanahabari na wafanyakazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la  Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR)  Wakiwa na Maofisa wa Shirika la Help Age International wakizungumza na Kikongwe cha Miaka 80 ambaye anapata huduma za kijamii kutoka UNHCR Kupitia  Shirika la Help age ndani ya Kambi ya Wakimbizi ya Nduta Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma. Wazee na Walemavu katika Kambi hizo za wakaimbizi wamekuwa na Changamoto kubwa ya kuweza kujipatia mahaitaji ya kila siku na kufanya shughuli zingine za kuwaingizia kipato hili waweze kujikimu hivyo UNHCR Kupitia Mashirika Saidizi imekuwa ikitoa  Msaada kwa makundi hayo maalum
Afisa wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) wa Masuala ya Ustawi wa Jamii, Grace Atim akionyesha Jiko la Mafuta ya taa linalotumiwa na  Kikongwe wa Miaka 80 ndani ya nyumba yake iliyopo ndani ya kambi ya wakimbizi ya Nduta Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma jiko hilo limekuwa msaada kwake kwani hawezi tena kutembea umbali mrefu ndani ya kambi kwenda kutafuta nishati ya kupikia.
 Mmoja wa walemavu waishio ndani ya kambi ya Wakimbizi ya Nduta ambaye ana uwezo wa kufanya kazi za useremala, akieleza namna ambavyo Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) kwa kushirikiana na Help Age International walivyomuwezesha kuendeleza shughuli hizo kwa lengo la kuweza kijikimu kimaisha baada ya kujengewa uwezo. 

 
 Mmoja wa wazee wanaowezeshwa na  Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) kupitia taasisi ya Help Age Interanational jinsi ya kusuka viti vya asili akipokea maelekezo kutoka kwa Afisa wa Masuala ya Ustawi wa Jamii (UNHCR), Grace Atim. Lengo la kutoa mafunzo mbalimbali kwa nadharia na vitendo kwa wakimbizi waishio ndani ya kambi za wakimbizi ni ili kuwawezesha kuwa na shughuli za kujiongezea kipato pindi watakaporejea katika nchi zao.
Watumishi wa Shirika la Help Age International wakiwa wanaingia katika moja ya nyumba ya Mkimbizi mwenye mahitaji maalumu ndani ya kambi ya Nduta iliyopo Wilayani Kibondo mkoani Kigoma. Watumishi hao wamekuwa wakitembelea nyumba za watu wenye mahitaji maalum kila siku hili kubaini ni changamoto gani wanakabiliana nazo ndani ya kambi hiyo 


Baadhi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum wakimsikiliza mwalimu katika kambi ya Wakimbizi ya Nduta Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma

RPC AIPONGEZA SGA KWA WELEDI, KUJALI WAFANYAKAZI

0
0
Kampuni ya SGA Security imeadhimisha miaka 33 tangu ianze shughuli zake nchini Tanzania huku ikiwatunuku wafanyakazi walioitumikia kampuni hiyo kwa muda mrefu na kupongezwa na Jeshi la Polisi kwa hatua hii. Shughuli ya kuwatambua wafanyakazi hawa ilihudhuriwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, SACP Jumanne Muliro katika ofisi za SGA Masaki ikiwa ni moja ya majukumu yake kuhakikisha makampuni 
binafsi ya ulinzi na usalama yanaendeshwa kwa viwango vinavyotakiwa.

 Kampuni hiyi iliunda kikundi maalumu kijulikanacho kama ‘Club 20’ ambacho kinajumuisha wafanyakazi walioitumikia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 20. Kwa sasa kampuni ya SGA Security imeajiri wafanyakazi zaidi ya 5,100 Tanzania na kuifanya iwe moja ya makampuni makubwa ya usalama nchini. SACP Muliro aliipongeza SGA kwa kujali masilahi ya wafanyakazi na kuongoza kwa mfano huku akisisitiza kuwa makampuni mengi ya ulinzi na usalama hayafuati utaratibu uliowekwa ikiwemo mafunzo, usimamizi na mishahara huku akitoa wito kwa makampuni mengine kuiga mfano wa SGA. 
 Mgeni rasmi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni SACP Jumanne Muliro akizungumza jambo kabla ya kukabidhi tuzo kwa wafanyakazi wa kampuni ya SGA katika kuadhimisha miaka 33 tangu kuanzishwa kwake katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya ofisi za SGA.

“Ni jambo la kupongezwa sana kwa kuwa kampuni yenye wafanyakazi zaidi ya 50 walioitumikia kampuni kwa zaidi ya miaka 20,” alisema. Alisema SGA ndio ilikuwa kampuni ya kwanza ya binafsi ya ulinzi na usalama kuanziswa Tanzania na imedhihirisha kuwa kuwajali wafanyakazi ndio chanzo cha mafanikio. 
“Nimefahaishwa kuwa wafanyakazi walioitumikia SGA kwa zaidi ya miaka kumi ni zaidi ya 1,500 jambo ambalo linastahili pongezi,” alisema huku akisisitiza kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na makampuni binafsi ya ulinzi na usalama kuhakikisha mkoa unakuwa salama na kuongeza kuwa walinzi wanafanya kazi kubwa katika kuzuia ujambazi. 
Naye Mtendaji Mkuu wa SGA Group, Jules Delahaije aliupongeza uongozi wa SGA nchini kwa kuhakikisha wafanyakazi wanaitumikia kampuni kwa muda mrefu na pia kwa kuwatambua na kuwatunuku waliofanya kazi muda mrefu. Aliwapa wafanyakazi hao ngao maalumu za kuonesha utumishi wao kwa zaidi ya mika 20. 
“Tukiwa na wafanyakazi zaidi ya 18,000 duniani kubwa kwetu ni watu. Tumewekeza sana katika mafunzo na pia tumehakikisha tunawalipa wafanyakazi wetu vizuri kabisa ikilinganishwa na makampuni mengine ili tuwajengee mazingira bora ya kazi na pia tuwe nao kwa muda mrefu,” alisema.
   
Mkurugenzi Mkuu wa SGA Group, Bw. Jules Delahaije akizungumza jambo wakati wakati wa hafla ya kukabidhi tuzo kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo wakati wa kuadhimisha miaka 33 tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo ambapo RPC wa Kinondoni, Jummane Muliro alikuwa mgeni rasmi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MWENYE TAARIFA KUPOTEA KWA MWANDISHI WA MWANANCHI ATULETEE-POLISI

0
0
JESHI la Polisi nchini limesema yoyote mwenye taarifa zitakazosaidia kupatikana kwa mwandishi wa habari wa kujitegemea wa Kampuni ya Mwananchi Communication(MCL)mkoani Pwani Azory Gwanda ambaye kwa sasa hajajulikana alipo azipeleke kwenye jeshi hilo ili zifanyiwe kazi.

Kauli hiyo imetolewa Dar es Salaam leo na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai(DCI)Robert Boaz ambapo amesema wanaendelea na upelelezi kutokana na taarifa walizonazo lakini bado wanaendelea kupokea taarifa,hivyo kwa mtu ambaye atakuwa nazo ni vema akawapelekea.

Amesema hayo wakati anajibu swali la waandishi wa habari waliotaka kujua Polisi wamefikia wapi katika kumtafuta mwandishi huyo.

“Jeshi la Polisi tunaendelea kufanya upepelezi kupitia taarifa tulizonazo ambazo hatuwezi kuzisema, lakini tutoe rai kwa mwenye taarifa zaidi zitakazaotusaidia kwenye upepelezi wetu atuletee.

“Ni mapema mno kusema Gwanda ametekwa au amejiteka, kikubwa tuacheni polisi tuendelee na kazi yetu ya kufuatilia,”amesema.

Ameongeza kuwa jamii isubiri upepelezi utakapikamilika utatoa majibu sahihi na kuan mifano ya matukio ambayo yametokea huko nyuma ambapo jamii iliamini mtu fulani ametekwa kumbe amejiteka mwenyewe. Hivyo waachwe wafuatilie na ukweli utajulikana.

NBS Wachukulieni Hatua Wanaotoa Takwimu za Uongo-Rais Dkt Magufuli

RC MAHENGE ATEMBELEA DAMPO LA KISASA MANISPAA YA DODOMA, ASEMA DODOMA LAZIMA IWE SAFI ZAIDI

0
0
NA RAMADHANI JUMA,OFISI YA MKURUGENZI

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge amesema Mji wa Dodoma hauna sababu ya kuwa mchafu kwa sababu Manispaa ya Dodoma imetekeleza mradi wa ujenzi wa dampo la kisasa na litakalodumu kwa miaka mingi ijayo.

Aliyasema hayo baada ya kutembelea dampo la kisasa la Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma lililopo eneo la Chidaya Kata ya Matumbulu takribani umbali wa kilometa 12 kutoka katikati ya Mji wa Dodoma.

Katika ziara hiyo fupi, Mkuu huyo wa Mkoa alioongozana na Katibu Tawala wa Mkoa huo Rehema Madenge pamoja na Mkuu wa Idara ya Mazingira na Usafishaji wa Manispaa hiyo Dickson Kimaro aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (katikati mbele) akiwa na Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa ya Dodoma Barnabas Faida (kulia) na Meneja wa Dampo la Kisasa la Manispaa hiyo John Chiwanga (kushoto) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.
Moja ya magari maalum kwa ajili ya kubeba uchafu ya Manispaa ya Dodoma likipimwa uzito kabla ya kuingia kumwaga uchafu katika Dampo hili la kisasa lilipo eneo la Chidaya Kata ya Matumbulu katika Manispaa hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (kushoto) akiwa katika sehemu ya Dampo la kisasa la Chidaya Manispaa ya Dodoma iliyoanza kutumika huku akipata maelezo kutoka kwa Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa hiyo Barnabas Faida (kulia) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.
Sehemu ya pili ya Dampo la kisasa la Chidaya katika Manispaa ya Dodoma linalotumia Teknolojia ya kuzika taka ardhini ambayo bado haijaanza kutumika kwa sasa.

INASIKITISHA! MAKOSA YA UBAKAJI, KUNAJISI YASHIKA KASI MWAKA 2017,

0
0
Said Mwishehe,Blogu ya jamii

INASIKITISHA!Ndivyo unavyoweza kuelezea baada ya Jeshi la Polisi nchini kusema kuwa mwaka huu wa 2017 matukio ya ubakaji na kunajisi watoto yameongezeka na kushika kasi ikilinganishwa na mwaka 2016

Imefahamika sababu ya kuongezeka kwa matukio hayo ni ushirikina, tamaa ya mwili na mmomonyoko wa maadili kwenye jamii ya Watanzania

Akizungumza Dar es Salaam leo, kwenye Makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai(DCI) Robert Boaz amefafanua makossa dhidi ya binadamu yanayojumuisha mauaji, kubaka,kulawiti , wizi wa watoto, kutupa watoto, kunajisi na kusafirisha binadamu yameripotiwa

“Katika kundi hili makosa ambayo yameonekana kuongezeka ni makosa ya kubaka na kunajisi.Zipo sababu nyingi lakini kubwa ni ushirikina, kukosekana kwa maadili na tamaa ya mwili.

“Jeshi la Polisi tutaendelea kufuatilia wanaojihusisha na matukio hayo na kisha sharia ichukue mkondo wake.Tunaomba jamii nayo ishirikiane na jeshi lao kutoa taarifa dhidi ya wanaojihusisha na matukio ya aina hiyo,”amesema.

Ameongeza takwimu zinaonesha makosa ya kubaka na kunajisi yameongezeka. Novema mwaka 2016 makosa ya kubaka yaliyoripotiwa yalikuwa 6,985 ikilinganishwa na makosa 7,460 ambayo yameripotiwa mwaka huu.

China Yaunga Mkono Juhudi Za Rais Magufuli

0
0
Na Mwandishi Maalum, Beijing

China imeahidi kushirikiana na Tanzania kikamilifu katika miradi ya kipaumbele ambayo Serikali ya AwamuyaTano imepanga kuitekeleza ili kufikia azma yake ya uchumi wa viwanda ifikapo 2020 na baadaye uchumi wa Kati ifikapo 2025.

Hayo yalibainishwa leo jijini Beijing na Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming na baadaye kukaririwa tena na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipango (NDRC), Bw. Ning Jizhe walipofanya mazungumzo kwa nyakati tofauti na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Mahiga aliainisha na kufafanua namna Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Maguful iilivyokusudia kuwashirikisha wadau mbalimbali kwenye utekelezaji wa miradi ya kipaumbele ambayo inalenga kuchochea agenda ya uchumi wa viwanda. 

Miradi hiyo ni pamoja na kuendeleza nishati ya umeme ambapo Serikali imedhamiria kuzalisha umeme wa megawatts 5000 ifikapo mwaka 2020 ili kuharakisha utekelezaji wa agenda ya uchumi wa viwanda ambayo haitaweza kufanikiwa kama hakutakuwa na umeme wa kutosha na wauhakika.

Kutokana na uhalisia huo, Serikali imepanga kujenga kituo cha kuzalisha umeme wa megawatts 2100 kwenye mto Rufiji na kujenga njia za kusambaza umeme huo kutoka Rufiji, Chalinze hadi Dodoma na nyingine kutokaChalinze, Kilimanjaro hadi Arusha. 

RITTA KABATI KUKARABATI SHULE YA MSINGI KIHESA

0
0
 Na Fredy Mgunda,Iringa.

Mbunge wa viti maalam mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati amefanya ziara kwenye baadhi ya shule za msingi za manispaa ya Iringa kwa lengo la kubaini changamoto zilizopo na kuanza kuzitafutia ufumbuzi kwa lengo la kuboresha mazingira ya wanafunzi kusomea.

Akizungumza mara baada ya kumaliza zira hiyo ya wiki moja Kabati alisema kuwa amefanya ziara katika shule ya msingi Kihesa,Igereke,Mtwira na shule ya Kibwabwa na kubaini changamoto nyingi ambazo anaanza kuzitafutia ufumbuzi hivi karibuni.

“Nimejionea mwenyewe changamoto zilizopo na naona kama changamoto kwa asilimia kubwa zinafanana hivyo ni kazi yangu kuanza kutafuta njia ya kuanza kuzitatua changamoto hizo”alisema Kabati.

ACACIA YAFANYA TAMASHA LA AJIRA KUWAPA FURSA WAFANYAKAZI WALIOACHISHWA KAZI MIGODI YA BUZWAGI NA BULYANHULU

0
0

Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Acacia kupitia migodi ya dhahabu ya Buzwagi na Bulyanhulu imefanya tamasha la ajira kwa kuwakutanisha waliokuwa wafanyakazi wa migodi hiyo na makampuni zaidi ya 20 kwa ajili kubalishana mawazo na kupeana mawasiliano na taarifa ili wafanyakazi hao wapate kazi.

Tamasha hilo limefanyika leo Jumatano Desemba 20,2017 katika ukumbi wa Umoja uliopo katika mgodi wa Buzwagi uliopo wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkufunzi katika Idara ya Saikolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Dk Chris Mauki.

Akizungumza wakati wa tamasha hilo,Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu alisema lengo la tamasha la ajira lilioandaliwa na Acacia ni kuwaonesha fursa za ajira waliokuwa wafanyakazi wa kampuni ya Acacia kwa kuwakutanisha na makampuni mbalimbali katika kipindi cha kuelekea kufunga migodi hiyo.

“Tumekutana hapa ili kuonesha fursa za ajira kwa wafanyakazi wetu waliobobea katika kazi za migodini, kuna maisha mengine baada ya mgodi,tumealika kampuni ambayo yanachukua mawasiliano na CV na kama kuna nafasi za ajira basi watapatia ili maisha yaendelee nje ya mgodi”,aliongeza Busunzu.

“Tulialika makampuni zaidi ya 40, 15 yalikubali kushiriki,na 11 leo yamehudhuria,lakini pia wafanyakazi zaidi ya 260 wamehudhuria kwa ajili ya kuonana na makampuni haya,Acacia inaamini tamasha hili litakuwa na mafanikio makubwa tuliyotarajia”,alieleza.

Mgeni rasmi Mkufunzi katika Idara ya Saikolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Dk Chris Mauki akizungumza katika Tamasha la Ajira lililoandaliwa na Kampuni ya Uchimbaji madini ya dhahabu ya Acacia lililofanyika leo Jumatano Desemba 20,2017 katika mgodi wa Buzwagi na kukutanisha pamoja makampuni zaidi ya 10 na wafanyakazi zaidi ya 260 walioachishwa kazi katika mgodi wa Buzwagi na Bulyanhulu wakati Acacia ikielekea kufunga migodi hiyo.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akielezea lengo la kufanya tamasha la ajira lililokutanisha pamoja makampuni na wafanyakazi wa Acacia ili kupeana fursa za ajira. Kulia Meneja Uendelevu mgodi wa Buzwagi George Mganza,kushoto ni Dk. Chris Mauki.

Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akiwasisitiza waliokuwa wafanyakazi wa Acacia kutumia fursa ya tamasha hilo kutafuta maisha nje ya migodi.

Washiriki wa tamasha la ajira wakimsikiliza Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu .

SHONZA AFUNGA MASHINDANO YA MICHEZO YA VYUO VIKUU LEO UDOM MJINI DODOMA

0
0
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana shonza akijiandaa kufunga kikapu wakati wa kufunga mashindano ya Michezo ya Vyuo Vikuu yaliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dodoma leo.
.Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akikagua timu ya mpira wa pete ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) wakati wa fainali za Michezo ya Vyuo Vikuu Mjini Dodoma Leo..

MBULU WAMPONGEZA KAMOGA KWA KUFANIKISHA MAENDELEO

0
0
Wakazi wa Kata ya Masieda Wilaya yards Mbulu Mkoani Manyara, wamemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Hudson Kamoga kwa jitihada zake binafsi zilizofanikisha kupata ufadhili wa kumalizia madarasa ya shule ya msingi Umbur. 

Ofisa mtendaji wa Kijiji cha Masieda Yasenti Lazaro akizungumza wakati Kamoga akizindua madarasa matatu ya shule hiyo alisema wananchi wa eneo hilo wanashukuru kwa kuwezesha umaliziaji wa jengo la darasa la shule hiyo. 

Lazaro alisema shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2014 na kusajiliwa mwaka 2015 ina wanafunzi 335 na vyumba vinne vya madarasa. Alisema bado wanakabiliwa na upungufu wa vyumba vitatu vya madarasa na nyumba za walimu kwani hivi sasa kuna nyumba moja pekee ya walimu wanne waliopo shuleni hapo. 

Mwenyekiti wa CCM Kata ya Masieda, Nicomed Nada ameshukuru Rais John Magufuli kumteua Kamoga kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kwani anawatumikia wananchi kwa kuacha alama ya maendeleo. Nada alisema Kamoga ni mbunifu kwenye suala la maendeleo na amekuwa akipigania vipaumbele vya wananchi wa wilaya hiyo kwenye elimu, afya na maji. 

Alisema Kamoga ni mbunifu wa maendeleo kwani alifika kwenye shule hiyo na kubaini tatizo la ukosefu wa madarasa, akazungumza na wadau wa maendeleo waliowezesha jambo hilo. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga alisema baada ya kutembelea shule hiyo na kubaini changamoto ya darasa, wakati Halmashauri haikuwa na fungu la kulimaliza, alizungumza na mdau wa maendeleo waliyejitoa sh10 milioni, kwa ajili ya kumalizia ujenzi huo. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga akipokea zawadi ya mbuzi baada ya wananchi wa Kijiji cha Masieda kumpatia kama shukrani ya kuwezesha umaliziaji wa jengo la darasa la shule ya msingi Umbur ambapo aliwapa shilingi milioni saba alizopata kwa wadau ambapo kati ya shilingi milioni 10 alizozipata saba alitoa kwa shule hiyo na nyingine milioni tatu zikapelekwa kwenye vijiji vya Mamagi na Genda ili kufanya utafiti wa upatikanaji wa maji. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga akizindua madarasa matatu ya shule ya msingi Umbur, ambapo moja kati ya madarasa hayo alimalizia ujenzi wake kwa kutumia fedha alizozipata kwa wadau wa maendeleo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuari ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Starnley Kamoga akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Masieda.
Mzee wa jamii ya wairaq John Tluway wa Kijiji cha Masieda Wilayani Mbulu Mkoani Manyara akimpa zawadi ya majani, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Hudson Kamoga baada ya kuzindua madarasa matatu ya shule ya msingi Umbur.

DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE

0
0

Na Kitengo cha Mawailiano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile ameshiriki kazi ya ujenzi wa shule ya msingi Chambasi Wilayani Kisarawe ikiwa ni zoezi la kuamsha ari ya wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo Dk. Ndugulile amesema kuwa kwa kipindi kirefu dhana ya wananchi kujitolea katika kufanya kazi za maendeleo imepungua kwa kiasi kikubwa na kuiachia Serikali ikitoa kila kitu kutekeleza miradi ya maendeleo hata kama inawezekana kazi hizo kutekelezwa na wananchi.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa kwa kipindi cha sasa cha Serikali ya Awamu ya Tano ya Hapa kazi tu wananchi hawana budi kujitoa katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneno hayo ili kuisaidia Serikali na kujisaidia wao wenyewe kujiletea maendeleo.

“Msisubiri kila kitu kifanywe na Serikali vingine mnaweza kufanya weneyewe hongereni sana ninyi ni mfano wa kuigwa kwa vijiji vingine katika hili” alisema Dkt. Ndugulile.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kuchanganya mchanga wa kutengeneza zege kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao katika wilaya ya Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kutengeneza tofali wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kubeba ndoo ya zege wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Bibi.Sihaba Nkinga akishiriki kubeba ndoo ya zege wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.

JPM aunda Tume ya 'Makinikia' ndani ya Chama cha Mapinduzi kufuatilia mali ya chama hicho nchi nzima

0
0




Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na Katibu Mkuu wa (CCM) Abdulrahman Kinana wakati alipokuwa akiwasili katika eneo la Mkutano na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya (CCM) NEC uliofanyika mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wajumbe Halmashauri Kuu ya Taifa ya (CCM) NEC (hawaonekani pichani) katika eneo la Mkutano mjini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu wa (CCM) Abdulrahman Kinana
Makamu Mwenyekiti wa CCM kwa upande wa Zanzibar Rais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Philip Mangula mara baada ya kuwasili katika eneo la mkutano wa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya (CCM) NEC uliofanyika mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wajumbe Halmashauri Kuu ya Taifa ya (CCM) NEC mjini Dodoma. Wa pili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM kwa upande wa Zanzibar, Rais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein aliyeketi pamoja na Katibu Mkuu wa (CCM) Abdulrahman Kinana.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wajumbe Halmashauri Kuu ya Taifa ya (CCM) NEC mjini Dodoma.
Wajumbe mbalimbali wa NEC wakizungumza katika mkutano huo uliofanyika mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasikiliza wajumbe mbalimbali wa NEC walipokuwa wakijitambulisha katika mkutano huo wa NEC mjini Dodoma.

JAFO AAGIZA MANISPAA DODOMA IPIME HARAKA VIWANJA NA AMFAGILIA MBUNGE MAVUNDE KWA KUWAJALI WANANCHI

0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi kuhakikisha wanapima viwanja haraka ili kuufanya mji wa Dodoma uendane na kasi ya ongezeko la idadi ya watu wanaohamia Dodoma na kuufanya mji uliopangwa kwa utaratibu unaoeleweka.

Jafo ameyasema hayo leo katika hafla fupi ya kuweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Shule ya Sekondari Iyumbu-Dodoma Mjini,ambapo pia ametumia nafasi hiyo kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwatumikia na kuwaletea maendeleo wananchi wake na kuahidi kuendelea kumpa ushirikiano katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wake wa Jimbo la Dodoma Mjini.

Mbali na hilo, Jafo ameagiza fedha kiasi cha sh.milioni 10 zilizopo kwenye akaunti ya kata hiyo ambazo zilitakiwa kutumika kupaulia darasa la shule ya sekondari Iyumbu kutumika kujenga madarasa manne.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akizungumza na wananchi kata ya Iyumbu
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza na wananchi katika kata ya Iyumbu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akifurahi jambo na Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde

SHONZA AFUNGA MICHEZO YA VYUO VIKUU TANZANIA (TUSA) MJINI DODOMA

0
0
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akimvisha medali golikipa wa timu ya mpira wa miguu ya Chuo Kikuu cha Zanzibar Ahmad Suleiman wakati wa kufunga fainali za Michezo ya Vyuo Vikuu iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dododma leo Tarehe 20/12/2017. Chuo Kikuu cha Zanzibar waliibuka washindi wa mpira wa  miguu kwa wanaume.
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akisalimiana na wachezaji wa timu ya mpira wa kikapu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) wakati wa kufunga fainali za Michezo ya Vyuo Vikuu iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dododma leo Tarehe 20/12/2017. OUT waliibuka washindi wa mchezo wa kikapu kwa wanaume dhidi ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akizungumza na washiriki wa Michizo ya Vyuo Vikuu (Hawapo Pichani) wakati akifunga fainali za Michezo hiyo iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dododma leo Tarehe 20/12/2017. Waliokaa kulia kwake wa kwanza ni Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Antony Mavunde,Wa pili ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma Prof. Idris Kikula na Mtangazaji wa Clouds Fm Ndg. Shafii Dauda. 
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akijiandaa kufunga kikapu wakati wakufunga Michezo ya Vyuo Vikuu kwenye Mchezo wa Fainali ya mpira wa kikapu kati ya timu ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Tanzania (OUT) na Chuo Kikuu cha Dododma (UDOM) iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dododma leo Tarehe 20/12/2017, wa Pili kushoto ni Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Antony Mavunde. OUT waliibuka washindi wa mchezo wa kikapu kwa wanaume. PICHA NA:OCTAVIAN KIMARIO-WHUSM

MAGAZETI YA ALHAMIS LEO DECEMBER 21,2017

Dkt. Mahiga ahutubia Chuo Kikuu cha Mambo ya Nje cha China

0
0
Wziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Chuo cha Mambo ya Nje cha China kabla ya wawili hao hawajaelekea kwenye ukumbi kuhutubia wanafunzi. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augastine Mahiga akihutubia wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mambo ya Nje cha China. Dkt. Mahiga alieleza ushirikiano wa Tanzania na China ulipoanza hadi leo na kuwasihi wanafunzi hao waangalie namna y kuuimarisha kutokana na nafasi zao. 
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mambo ya Nje cha China wakisikiliza Hotuba ya Dkt. Mahiga. Wanafunzi hao ambao walikuwa wadadisi sana walifurahi sana kutokana na elimu ya siku moja waliopata kutoka kwa Mbobezi wa masuala ya Diplomasia. 
Dkt. Mahiga akiendelea na hotuba yake huku Mkuu wa Chuo akisikiliza kwa makini. Mkuu huyo alikiri kuwa kutokana na hotuba hiyo amejifunza vitu vingi sana. 
Ujumbe uliomsindikiza Waziri Mahiga, kutoka kulia ni Bw. Benedict Msuya, Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Gerald Mbwafu, Katibu wa Waziri na Kanali Remigius Ng'umbi, Mwambata Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China. 
Mstari wa Mbele kutoka kushoto ni Kamishna msaidizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Malmeltha Mtagwaba, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Thomas Kashililah, Naibu Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji kutoka Wizara ya Vwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Joseph Buchweishaija, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha wa Zanzibar, Bw. Khams Omar na Balozi wa Tnzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki wakifuatilia hotuba hiyo. 

Muuza mpunga wa Kisaki ashinda milioni 86. 2 ya M-Bet

0
0
Mkazi wa Mvua, Kisaki mkoani Morogoo, Fredy Masawe (35) ameishinda Sh milioni 86.2 kwa kubashiri kwa usahihi mchezo maarufu kwa ‘Perfect 12’ unaondeshwa na kampuni ya mchezo wa kubahatisha ya M-Bet.

Masawe ambaye ni shabiki wa timu ya Manchester United ya Uingereza alifanikiwa kubashiri kwa usahihi mechi 12 kati ya 17 za mchezo na kufanikiwa kuwa mshindi pekee wa droo ya 20 ya mchezo.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley alisema kuwa Masawe ni mshindi wa tatu kwa mwezi huu kupaza zawadi kiasi kikubwa cha fedha na serikali kupata ya jumla ya Sh milioni 15 kutoka kiasi hicho cha fedha ambacho ni asilimia 18 kwa mujibu wa sheria. “M-Bet ipo kwa ajili ya kuwanufaisha mashabiki wa soka hapa nchini, watashindi kibao wamefanikiwa kubadili maisha baada ya kujishindia fedha nyingi na sasa amekuwa mtu wa kipato kingine tofauti na alivyokuwa awali,” alisema Malley.

Alisema kuwa kiasi cha Sh 1,000 tu kimeweza kumnufaisha Masawe ambaye sasa ataweza kuendesha maisha yake tofauti na kuanzisha biashara mbalimbali. Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha zake, Masawe alisema kuwa atazitumia fedha hizo kwa kupanua biashara yake ya kuuza mpunga.

“Sikuamini nilipoambiwa kuwa nimeshinda kiasi hiki cha fedha, kule kwetu Mvua, tumeweka eneo la kubashiri mchezo huu chini ya mwembe, nimebeki mara nyingi sana, na kupata fedha ndogo ndogo, sikukata tamaa kwa kukosa kushinda na leo nimekuwa mshindi, kwa fedha hizi pia nitamalizia nyumba yangu ya kuishi na kuwa ya kisasa, ” alisema Masawe.

Mke wa Masawe, Elizabeth Chifungo (26) alisema alikuwa anamzui mume wake kucheza mchezo huo kwa kuamini kuwa alikuwa anapoteza fedha. “Nilimzuia sana, akakataa na kuendelea kucheza, nimeamini kuwa michezo hii ya kubashiri ni ya ukweli, nawaomba watanzania kuendelea kubashiriki, kwa ushindi huu, nami nitaongeza mtaji wa biashara yangu,” alisema Elizabeth.
Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley (kulia) akimkabidhi hundi mshindi wa mchezo wa Perfect 12, Fredy Masawe (katikati) ambaye amejishindia kitita cha sh milioni 86.2. anayeshuhudia ni baba wa Mshindi huyo, Geofrey Masawe.
Mshindi wa mchezo wa Perfect 12 Fredy Masawe (kushoto) akiwa na mkewe, Elizabeth Chifungo wakifurahia mara baada ya kukabdhiwa zawadi yake. Masawe alishinda kitita cha sh milioni 86.2

TANGAZENI MAFANIKIO YA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI-MWAMANGA.

0
0

Na Estom Sanga- TASAF

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF- bwana Ladislaus Mwamanga amewaagiza Maafisa Ufuatiliaji na Waratibu wa Mfuko huo ngazi ya halmashauri za Wilaya nchini kote kushirikiana na Vyombo vya Habari kutangaza mafanikio ya utekelezwaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kwenye maeneo yao.

Bwana Mwamanga amesema serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF- imefanikiwa kuzikifia kaya za wananchi waliokuwa wanakabiliwa na hali ya umaskini wa kipato ambao wameanza kukabiliana na kadhia hiyo kwa kuwekeza kwenye shughuli za kiuchumi na kuboresha maisha yao.

Akizungumza katika siku ya pili ya kikao kazi cha watumishi, Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF ametoa mfano wa Mafanikio yaliyoanza kupatikana tangu kaya za walengwa kujumuishwa kwenye shughuli za Mpango, amesema kumekuwa na mwitikio mkubwa katika uundwaji wa vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana miongoni mwa walengwa na hivyo kukuza mitaji yao na kuibua shughuli za kiuchumi hususani biashara ndogo ndogo.

Aidha bwana Mwamanga amesema walengwa wa TASAF wameanza kuboresha makazi kwa kuezeka nyumba zao kwa mabati baada ya kuanzisha miradi midogo midogo ya kiuchumi kutokana kutokana na ruzuku inayotolewa na serikali kupitia TASAF huku kukiwa na mwitikio chanya katika sekta za elimu, afya na lishe kwa kaya za Walengwa.

Kutokana na mafanikio hayo,Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF amesema jitihada hizo zilizofanywa na serikali kupitia TASAF zinapaswa kuwekwa bayana na hivyo kuwaagiza Watendaji wote walioko kwenye halmashauri za Wilaya kushirikiana na Vyombo vya habari kutangaza mafanikio hayo ili kuwawezesha wananchi kutambua jitihada za kukabiliana na umaskini .

Aidha Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF amesisitiza watumishi wa Mfuko huo kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu mkubwa ili Mfuko huo uendelee kuaminiwa na Serikali na Wadau wengine wa Maendeleo kwa manufaa ya taifa kwa ujumla.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF amesema mwelekeo wa siku zijazo za utekelezaji wa shughuli za taasisi hiyo ni kuhakikisha kuwa walengwa wake wanatumia vyema fursa hiyo kwa kushiriki kwenye shughuli za ujenzi wa miradi ya Maendeleo na kujiongezea kipato kama njia mojawapo ya kuboresha maisha yao.
Mmoja wa Walengwa wa TASAF katika halmashauri ya mji wa Tabora, akimwonyesha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika nyumba aliyoanza kuijenga baada ya kujiongezea kipato kwa kuanzisha mradi wa biashara ya mboga na matunda kwa kutumia fedha za ruzuku kutoka TASAF. Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF bwana Ladislaus Mwamanga (aliyeshika kipaza sauti) akizungumza wakati wa kikao kazi cha watumishi wa taasisi hiyo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Watumishi wa TASAF wakimsikiliza meneja wa miradi ya kutoa Ajira, Mhandisi Barnabas Jachi aliyeshika kipaza sauti) alipokuwa akielezea manufaa ya miradi ya ajira za muda katika kuongeza kipato cha walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.
Baadhi ya Watumishi wa TASAF wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi (hayupo pichani )alipozungumza kwenye kikao kazi cha taasisi hiyo kinachojadili pamoja na mambo mengine namna uboreshaji wa huduma zake kwa wananchi.

WAUGUZI NI CHACHU YA HUDUMA ZA AFYA

0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi na Ukunga kutoka Wizara ya Afya Gustav Moyo akiwasilisha mada wakati wa mafunzo ya maadili kwa wauguzi wakuu wa Mikoa na hospitali za Kitaifa na za Rufaa za kanda unaoendelea chuo cha Uuguzi Mirembe Mkoani Dodoma.
Wauguzi wakuu toka mikoa mbalimbali wakifuatilia mada zinazowasilishwa kwenye mafunzo hapo.mafunzo hayo yana lenga kuwakumbusha uadilifu na maadili ya uuguzi wakati wa utoaji huduma za afya nchini.
Baadhi ya wauguzi wa mikoa wakijadili kwenye makundi mikakati ya nini kifanyike katika kutekeleza majukumu yao ili kuondokana na malalamiko ya taaluma yao kutoka kwa wananchi.
Wauguzi wakuu wakiendelea na kazi kwenye makundi.
Mkurugenzi wa Uuguzi na Ukunga Gustav Moyo akiongea na wauguzi wakuu wa mikoa kwenye mafunzo hayo.
Viewing all 109591 articles
Browse latest View live


Latest Images