Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live

JAFO AKUNWA NA UJENZI WA MIRADI MVOMERO

$
0
0
Waziri wa Nchi, ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi)Selemani Jafo amewapongeza viongozi na watendaji wa wilaya na Halmashauri ya wilaya ya Mvomero kwa usimamizi wa Miradi ya maendeleo. 

Jafo aliyasema hayo alipokuwa ziarani wilayani huko ambapo alifanikiwa kutembelea ujenzi wa hospitali ya wilaya, shule ya kidato cha tano na sita ya kumbukumbu ya Sokoine, mradi wa ujenzi wa barabara ya lami, kituo cha mafunzo ya kilimo na mifugo, pamoja na mradi wa umwagiliaji. 

Katika ziara hiyo,Jafo ameagiza kuanza kwa utoaji wa huduma ya matibabu kwa wagonjwa katika hospitali ya wilaya ya Mvomero ifikapo keshokutwa Desemba 13,mwaka huu wakati serikali ikitafuta fedha kwaajili ya ujenzi wa jengo la upasuaji, maabara, wodi ya watoto na majengo mengine ambayo yatagharibu zaidi ya sh.milioni 700 ambapo matarajio ni kupata fedha hizo na kukamilisha majengo hayo kabla mwezi Machi 2018. 

Pia Jafo ameagiza kuongezeka kwa kasi ya kukamilisha madarasa, bwalo la chakula na mabweni katika shule ya sekondari ya Sokoine Memorial kabla mwezi April 2018 ili shule hiyo iweze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano hapo mwakani kwani serikali imepeleka fedha zote za ujenzi zaidi ya sh.billioni 1.6.

Aidha Jafo amewataka viongozi na watendaji kuendelea kushikamana ili kuwaletea wananchi maendeleo.

.Jengo la utawala na wagonjwa wa nje ya Hospitali ya Mvomero.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akikagua shule ya kisasa ya Sokoine Memorial inayojengwa na serikali ya wilaya Mvomero.
.Jengo la kituo cha Mafunzo ya kilimo na mifugo kinachomaliziwa kujengwa wilayani Mvomero.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akikagua ujenzi wa miundombinu wilayani Mvomero.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiwa na viongozi wa mkoa na wilaya ya Mvomero wakati wa ukaguzi wa miradi ya maendeleo


WAZIRI UMMY AFANYA Ziara Zahanati ya Mhandu na Segese wilayani Msalala

$
0
0
Na.WAMJW-Msalala

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto aweka historia kwa kutembelea Zahanati ya Mhandu kata ya Chela Wilayani Msalala ambapo tangu Uhuru wa Tanzania kijiji hicho hakijawahi kutembekewa na Kiongozi wa Kitaifa.

Waziri Ummy Mwalimu yupo ziara ya kikazi Wilayani Msalala kujionea Utekelezaji wa Mpango wa Malipo kwa Ufanisi(RBF) ambapo ulianza Januari 2016 kwa Mkoa wa Shinyanga

RBFni Mpango wa malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya ngazi ya msingi ambapo vituo vinapewa maeneo ya utekelezaji na kupimwa kuona kama wamekidhi na kufikiwa malengo hivyo kituo huhakikiwa na hatimaye kutolewa fedha kulingana na matokeo ya idadi za huduma zilizotolewa na ubora kulingana na miongozo ya utoaji wa huduma za Afya.Fedha zinazopatikana zinafanya maboresho ya vituo ikiwemo miundombinu ya kituo,madawa na vifaa tiba

Waziri Ummy Mwalimu ameipongeza halmashauri ya wilaya hiyo kwa kufanya vizuri katika kutekeleza Mpango huo hata hivyo aliwataka watendaji kufanya uhakiki na kujiridhisha kwamba huduma za Afya zitolewazo zinakidhi viwango kulingana na miongozo ya Afya ndipo malipo yatolewe
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akimsalimia mgonjwa aliyekuwa anasubiri huduma katika Zahanati ya Segese wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akisisitiza jambo kuhusu upatikanaji wa dawa katika Zahanati ya Mhandu wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akiangalia friji la kuhifadhia chanjo kwa ajili ya watoto katika Zahanati ya Segese wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akipata maelekezo juu ya upatikanaji wa dawa kutoka kwa mtoa huduma kushoto katika Zahanati ya Segese wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akifurahia jambo na baadhi ya wazee wa kijiji cha Segese wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.PICHA NA WIZARA YA AFYA –KAHAMA.


MIILI YA ASKARI 14 WA JWTZ WALIO UWAWA WAKILINDA AMANI NCHINI DRC YAWASILI.

TAZAMA MAPOKEZI YA MIILI YA MASHUJAA WETU,WANAJESHI 14 WA JWTZ WALIOUWAWA CONGO

TTB Yamkabidhi Bendera Balozi wa Utalii Nchini Marekani

$
0
0
Mshindi wa Pili katika Mashindano ya Miss Tanzania U.S.A. mwaka 2017, Neema Olory (wa pili toka kushoto) akikabidhiwa Bendera ya Taifa na Meneja wa Masoko toka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Geofrey Meena (kushoto) kama ishara ya kuwa balozi wa Utalii nchini Marekani, kulia ni Mwanzilishi wa Kampuni ya Coutious on Tanzania Justa Lujwengana na wa pili kulia ni Afisa Uhusiano Mkuu toka Bodi hiyo Geofrey Tengeneza. Meneja wa Masoko toka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Geofrey Meena (kushoto) akimkabidhi Mshindi wa Pili katika Mashindano ya Miss Tanzania U.S.A. mwaka 2017, Neema Olory baadhi ya vitabu vinavyoelezea vivutio mbambali vya utalii vilivyopo Tanzania mara baada ya kumkabidhi Bendera ya Taifa kama ishara ya kuwa balozi wa Utalii nchini Marekani Mshindi wa Pili katika Mashindano ya Miss Tanzania U.S.A. mwaka 2017, Neema Olory akionesha baadhi ya vitabu vinavyoelezea vivutio mbambali vya utalii vilivyopo Tanzaniakwa waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kukabidhiwa Bendera ya Taifa kama ishara ya kuwa balozi wa Utalii nchini Marekani mapema hii leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Eliphace Marwa – Maelezo).

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA,SADIFA JUMA ANYIMWA DHAMANA,KESI YAKE KUSIKILIZWA TENA DESEMBA 19.

$
0
0
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM), Sadifa Juma Khamis amepandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Mkoa wa Dodoma kwa makosa mawili yanayohusu rushwa.

Sadifa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Donge alifikishwa Mahakamani hapo majira ya 4:55 asubuhi na maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru)akiwa katika gari lenye namba za usajili T994 BEM.

Akisoma kesi hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Joseph Fovo, Wakili wa serikali kutoka Takukuru Biswaro Biswaro alisema katika kesi hiyo ya jinai namba 232 ya mwaka 2017, mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Desemba 9, mwaka huu akiwa nyumbani kwake maeneo ya Kata ya Mnadani Manispaa ya Dodoma.

Alisema katika kosa la kwanza Sadifa anadaiwa kuwa akiwa nyumbani kwake alitoa rushwa ya vinywaji kwa wajumbe ili wamchague mgombea wa nafasi ya Makamu mwenyekiti wa UVCCM Rashid Mohamed Rashid.

Biswaro alisema kosa la pili analokabiliwa nalo Sadifa ni kutoa ahadi ya kuwalipia gharama za usafiri wajumbe hao kutoka Dodoma –Kagera kama zawadi kwao baada ya kumpigia kura mgombea huyo.

Wakili huyo aliwataja wajumbe hao kuwa ni Kadogo Shabani, Abdallah Hamimu, Octavian Andrea, Didas Zimbihile, Tasinta Nyamwiza, John Lufunga, Mtwawafu Kantangayo, Haleluya Ivody, Deocres Kagunila, Emmanuel Shitobelo, Happiness Rynyogote, Adolf Andrew, Adinani Musheruzi, Editha Domisian na Hashim Abdallah.

Biswaro alisema mshtakiwa huyo alitenda makosa hayo kinyume na Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007 kifungu cha 15(1)(b) na (2).

Hata hivyo alisema upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na upande wa jamhuri unaweka pingamizi la dhamana kwa mshtakiwa.Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Hakimu Fovo alimhoji mshtakiwa huyo ambapo alikana kutenda makosa yote mawili.


Sababu za kuzuiliwa dhamana 

Wakili Biswaro alisema sababu za kuzuia dhamana ya mshtakiwa huyo kutokana na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi UVCCM ni wa siku mbili mfululizo 10-11 Desemba 2017 na matokeo bado hayajatangazwa hivyo kuna uwezekano wa kuingilia uchaguzi huo.

“Naomba Mahakama itambue uchaguzi bado unaendelea na mshitakiwa hadi sasa hajakabidhi uongozi bado ni mwenyekiti,”alisema

Aidha alisema sababu nyingine ni kuwa mashahidi wengi ni viongozi ambao ni Mwenyekiti na Makatibu na endapo akiachiwa kwa dhamana ana kila aina ya ushawishi anaweza kuvuruga upelelezi.

Kufuatia maelezo hayo, Wakili wa utetezi Godfrey Wasonga alipinga kuzuiwa kwa dhamana na kudai kuwa ni haki ya mtu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Alibainisha kiapo cha kuzuia dhamana hicho kilichowasilishwa mahakamani ambacho kimetolewa na Emma Kuhanga (Kamanda wa Takukuru Dodoma) hakina mashiko.

“Uchaguzi wa UVCCM umeshaisha na mshindi tayari ameshapatikana na hakuna uchaguzi mwingine wa kuingilia au kama kuna uchaguzi utafanyika kiapo kingesema,”alisema Wasonga

Alihoji sababu za kupelekwa kesi ambayo haijakamilika upelelezi na kuzuia dhamana kwa mshtakiwa na kwamba mshtakiwa huyo hataweza kuingilia uchunguzi kwa sababu walizozitoa.“Hawa mashahidi atawezaje kuwashawishi wakati mtu ameshatoka madarakani?mteja wangu ni mbunge ni mtu makini na anaaminiwa asihukumiwe kwa kuwekwa ndani kwasababu zisizo na mashiko,”alisema Wasonga.

Aliomba Mahakama itupilie mbali pingamizi hilo na mshtakiwa apewe dhamana kwa kuwa hataweza kuingilia uchaguzi na uchaguzi mwingine wa Umoja huo ni hadi mwaka 2022.

Kutokana na mvutano huo, Hakimu Fovo aliahirisha kesi hiyo hadi desemba 19, mwaka huu na kwamba Mahakama ndipo itatoa maamuzi kuhusu suala hilo na mshtakiwa ataendelea kuwa rumande.

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

Natoa Wiki Sita Mradi wa Maji Kivindo-Muheza Uwe Umekamilika-Waziri Jafo.

$
0
0
Waziri wa nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametoa wiki sita kwa Mkandarasi wa mradi wa maji Kivindo Wilayani Muheza kukamilisha mradi huo na uanze kutoa huduma kwa wananchi.

Waziri Jafo ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake Wilayani Muheza ambapo alikagua miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo.

Alisema Mradi huo kwas asa umefikia asilimia 90 ya utekelezaji wake na Mkandarasi umeahidi hapa mbele ya wananchi kwamba utaukamilisha ndani ya muda niliokupa ambao ni wiki sita kuanzia hivi sasa.

“Sitegemei kuskia sababu zozote zitakazofanya mradi huu usikamilike ndani ya wiki sita ni mategemeo yangu wananchi wataanza kufaidi matunda ya mradi huu baada ya muda mfupi tu kuanzia sasa, Mkandarasi fanya kazi yako” Alisema Jafo.

Katika ziara hiyo Waziri Jafo amefanikiwa kutembelea Miradi ya afya na elimu katika kituo cha afya Mkuzi na Ubwari pamoja na kutembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Msingi Kilulu. 

Waziri Jafo amewapongeza wadau mbalimbali wanaoshirikiana na Serikali katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika Maeneo ya Umma. Hususan ni Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMRI) kwa kutoa mifuko 50 ya Saruji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miundombinu katika kituo cha Afya Ubwari.

Halkadhalika Waziri Jafo ametoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kuendelea kushirikiana na Serikali katika kufanikisha ajenda ya maendeleo kwa wananchi.
Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwa katika kituo cha Afya Ubwari wakati wa ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto.
Waziri Jafo akiwa katika Ukaguzi wa Miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Muheza.
Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI akiwa na baadhi ya viongozi katika Halmashauri ya Wilaya ya Muheza.
Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI akiwa na baadhi ya vijana waoashiriki kuchimba mitaro ya mradi wa Maji Kivindo.

MAKALA SHERIA:KUBADILI HATI KUTOKA JINA LA MAREHEMU KWENDA MSIMAMIZI WA MIRATHI.

$
0
0
Na  Bashir  Yakub.


Mara  kadhaa nimezungumzia   kuhusu  namna  bora  na  ya  kisheria  ya  kuuza  na  kununua  nyumba  au  kiwanja    kutoka  kwa msimamizi  wa  mirathi  baada  ya   mmiliki  halisi  kufariki.


Leo  tena makala haya yataeleza  kubadili  jina kutoka  jina  la  marehemu  kwenda  kwa  msimamizi  wa  mirathi. Kubadili  huku  kunaweza  kuwa  na  lengo  la  kuuza, kupangisha  , kugawa  kwa  warithi  au  hata  kubadili tu  kwa maana  ya  kubadili  bila  malengo haya juu.


Maelezo  katika  makala  haya yatatoka Sheria  ya  Usajili  wa  Ardhi  sura  ya 334 na  kanuni zake  za  mwaka  1954, pamoja  na Sheria ya  usimamizi  wa  Mirathi sura ya 352 na  kanuni zake  za mwaka 1963.


UTARATIBU  NI  HUU.


1.Lazima  kwanza ufungue  mirathi na  apatikane  msimamizi  wa  mirathi.  Tumeeleza  mara  nyingi utaratibu  wa  kufungua  mirathi . Tulisema kuwa,  kwa  marehemu  aliyekuwa  mkristo  utafungua  mahakama  maalum ya  wilaya(district delegate)  au mahakama kuu  ,  na  kwa  marehemu  aliyekuwa  muislam  au  aliyeishi  kimila  bila  dini   utafungua  mahakama  ya  mwanzo  au  Mahakama  kuu.

Kwahiyo hoja  hapa  ni  kuwa  hatua  ya  kwanza   lazima  awepo  msimamizi wa mirathi.

2. Msimamizi wa  mirathi  atakapokuwa  amepatikana  basi  atapewa  fomu  namba 4 na 5 za  usimamizi  wa mirathi. Fomu  hizi  zinatolewa  na  mahakama  na  ni  uthibitisho  kuwa   fulani  ni  msimamizi  wa  mirathi halali.  Hoja hapa hakikisha  unazo hizo  fomu   mkononi.

3. Ukishakuwa  na  fomu  hizo  mkononi  basi  utatakiwa  kutafuta  na  kujaza  fomu  nyingine iitwayo  fomu  ya  uwakilishi  maalum  wa  marehemu kisheria( Lega personal representative). Fomu  hii  ni  namba 20  kwenye  kanuni  za  usajili wa ardhi.


                KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com



MAGAZETI YA JUMANNE LEO DECEMBER 12,2017

NSSF YASHIRIKI MAONYESHO YA VIWANDA DAR

$
0
0
Afisa Masoko wa Nssf Riziki Kibwasali (kushoto), akizungumza na baadhi ya wateja waliotembelea banda lao wakati wa maonyesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja vya Saba saba jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko wa Nssf Riziki Kibwasali (kushoto),akiwaonyesha fomu baadhi ya wateja waliotembelea banda lao wakati wa maonyesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja vya Saba saba jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko wa NSSF, Salama Mbarak (kushoto), akizungumza na baadhi ya wateja waliotembelea banda lao wakati wa maonyesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja vya Saba saba jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko na UhusianoNSSF, Aisha Sango (kulia), akizungumza na baadhi ya wateja waliotembelea banda lao wakati wa maonyesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja vya Saba saba jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wateja wakiuliza maswali iliwaweze kupata kadi ya bima ya matibabu  walipotembelea banda la Nssf wakati wa maonyesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja vya Saba saba jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wateja wakijaza fomu kwa ajili ya kupata kadi ya bima ya matibabu walipotembelea banda la Nssf wakati wa maonyesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja vya Saba saba jijini Dar es Salaam.

KIWANDA CHA SARUJI TANGA (SIMBA CEMENT) YATOA MIFUKO 760 KUCHANGIA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA SHULE YA MSINGI PONGWE JIJINI TANGA

$
0
0

Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akipanga tofali kwenye msingi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya msingi ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na wasioona ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo.
Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akiweka sawa tofati katika msingi wa moja ya vyumba vipya vitatu vya madarasa kwenye shule ya Msingi ya ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo

Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akizungumza katika halfa hiyo iliyofanyika leo kwenye shule ya Msingi Pongwe Jijini Tanga.

MRADI MKUBWA WA KUSOMA BILA MWALIMU KWA KUTUMIA TABLETI WAZINDULIWA MUHEZA

$
0
0

Mradi wa majaribio wa miezi 15 wa watoto waliokosa shule, kujifunza wenyewe kwa kutumia teknolojia ya kisasa inayotumia tableti umezinduliwa mkoani Tanga.

Mradi huo uliozinduliwa katika kijiji cha Zenith ya Kati, wilayani Muheza ni sehemu ya mradi mkubwa wa miaka mitano wa majaribio duniani chini ya Global Learning Xprize wenye lengo la kutatua matatizo ya kujifunza.

Mradi huo hapa nchini unaendeshwa kwa pamoja na Shirika la Mpango wa Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na XPrize ambao wametoa tableti husika.

Aidha kuwezekana kuwapo kwa mradi huo kumetokana pia na makubaliano kati ya serikali ya Tanzania kupitia Wizara yake ya elimu na TAMISEMI na mashirika.

Katika utoaji elimu huo watoto wanaohusika ni wa miaka kuanzia 9 hadi 11 na watajifunza kwa kutumia program tano zilizowekwa katika tableti zitakazomuwezesha kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Ofisa Elimu wa mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu akivishwa skafu na kukaribishwa katika hafla ya kukabidhi tableti kwa ajili ya mradi wa kutumia teknolojia kujifunza, kuandika kusoma na kuhesabu uliozinduliwa Muheza jana. Mradi huo wa majaribio unafadhiliwa na Global Learning Xprize kwa kupitia UNESCO na WFP. Kushoto ni Mwakilishi wa Unesco ambaye pia anasimamia mradi wa Global Learning Xprize, Faith Shayo.
Mwenyekiti wa kijiji cha Zeneth wilayani Muheza, mkoani Tanga, Juma Killo akitoa salamu kwa XPrize, UNESCO, WFP na wageni waalikwa katika hafla hiyo. Wa pili kulia ni Mwakilishi wa Unesco ambaye pia anasimamia mradi wa Global Learning Xprize, Faith Shayo, Afisa Miradi wa UNESCO, Nadia Marques (wa tatu kushoto), Ofisa Elimu wa wilaya ya Pangani, Mbwana Mohamed (wa tatu kulia), Kaimu Ofisa Elimu Lushoto, Beatus Kipfumo (wa pili kulia) na Mwakilishi wa WFP mkoa wa Tanga, Xavery Njovu (kulia).
Mradi huo wa Tanga ambao utagusa watoto 2,400 kutoka katika vijiji 167 vya wilaya za Handeni, Korogwe, Lushoto, Muheza, Mkinga na Pangani unatoa changamoto kwa timu ya wabunifu kuwezesha watoto walio na fursa ndogo ya kuingia katika elimu darasani kujifunza stadi za msingi za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) kwa kutumia tableti wakijifunza wenyewe.

Akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo katika kijiji cha Zenith, Muheza Mkoani Tanga, Mwakilishi wa Unesco ambaye pia anasimamia mradi huo Faith Shayo alisema kwamba mradi huo unaendana na majukumu ya Unesco ya kuhamasisha elimu jumuishi katika kuhakikisha kwamba watoto wote wa Tanzania wakiwemo wa jamii za pembezoni zilizo nyonge zinapata fursa.

Alisema UNESCO inatekeleza majukumu yake kwa kuisaidia serikali ya Tanzania kuwezesha kutoa elimu bora kwa wananchi wake wote na hata wale ambao hawana uwezo wa kupata elimu kutokana na mazingira yao au maeneo yao.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TARIME NA BUNDA WASHUKURU MFUKO WA HDIF KWA KUOKOA MAISHA YA MAMA NA MTOTO KUPITIA UFADHILI WAO

$
0
0

  Kiongozi msaidizi wa Mfuko wa Ubunifu na Maendeleo ya Watu (HDIF), Joseph Manirakiza akimkabidhi barua ya makabidhiano ya mradi na vifaa mganga mkuu wa hospital ya Shirati, Dr. Bwire Chiragi kwa muda wa miaka miwili hospitali hiyo imepata ufadhili wa kuendesha mradi wa kuokoa maisha ya mama na mtoto (saving mothers project) katika wilaya za Bunda na Tarime mkoani Mara.
 Mganga mkuu wa hospitali ya Shirati,  Dr. Bwire Chiragi akisaini makabidhiano ya mradi wa kuokoa maisha ya mama na mtoto (saving mothers project) katika wilaya za Bunda na Tarime mkoani Mara. Katikati ni kiongozi msaidizi wa Mfuko wa Ubunifu na Maendeleo ya Watu (HDIF), Bw Joseph Manirakiza na Kulia ni Katibu wa hospitali ya Shirati, Ogottu Obala.
 Msaidizi kiongozi wa Mfuko wa Ubunifu na Maendeleo ya Watu (HDIF) , Joseph Manirakiza (katikati) akifafanuliwa jambo na viongozi wa hospitali ya Shirati iliyopo mkoani Mara, kulia ni Mganga mkuu wa Hospitali hiyo, Dr. Bwire Chiragi na kushoto Katibu wa hospitali hiyo, Juma Ogottu Obala

 Baadhi ya Baiskeli 124  zilizotolewa na Mfuko wa Ubunifu na Maendeleo ya Watu (HDIF) uliochini ya UKAIDS kwa ajili ya kuwasaidia wauguzi katika Wilaya ya Bunda na Tarime.
 Mama Prisca  Koboko  Ambae ni muuguzi toka Tarime akielezea jinsi mradi wa kuokoa maisha ya mama na mtoto ulivyowawezesha kuwafikia wakina mama.

NAIBU WAZIRI MADINI ATEMBELEA MACHIMBO YA JASI MKOANI SINGIDA

$
0
0
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo hapo jana alifanya ziara kwenye machimbo ya Jasi (Gypsum) ya Mkoani Singida na kuzungumza na Wafanyabiashara na Wachimbaji wa Madini hayo ambapo aliwahakikishia ushirikiano wa dhati wa kufikia malengo waliyojiwekea.
Alitembelea maeneo ya machimbo ya Madini ya Jasi na Viwanda vidogo vya uongezaji thamani ya madini hayo ikiwemo viwanda vya kusaga madini ya Jasi ambayo unga wake unasafirishwa nje ya Mkoa huo, viwanda vya kutengeneza chaki vilivyopo Itigi na kiwanda cha utengenezaji wa mapambo ya majumbani kilichopo Singida Mjini.
Naibu Waziri Nyongo yupo Mkoani Singida kwenye ziara ya siku Tatu ya kutembelea maeneo mbalimbali ya uchimbaji wa madini Mkoani humo ili kujionea shughuli zinazofanywa kwenye maeneo hayo na kuzungumza na wachimbaji wa madini ili kubaini changamoto zinazowakabili kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wake. 
Kwa mujibu wa wachimbaji wa madini hayo, Madini ya Jasi hutumika kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kutengenezea chaki, hospitalini kwa watu waliovunjika na kutengeneza viungo bandia, kutumika kutengenezea saruji, urembo majumbani, hutumika kama insulation kwenye majengo makubwa kwa kuwa Jasi huzuia moto, kutengenezea midoli na masanamu, kutengeneza meno bandia na pia hutumika kama mbolea
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) akishuhudia upakiaji wa Madini ya Jasi katika kijiji cha Kihanju, Itigi yanayosafirishwa kuelekea kwenye Kiwanda cha Saruji cha Mbeya Cement ikiwa ni moja ya malighafi ya kutengenezea Saruji.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kushoto) akiwasikiliza wachimbaji na wafanyakazi wa machimbo ya Jasi, yaliyopo katika Kijiji cha Kihanju, Itigi, Mkoani Singida alipofanya ziara kwenye machimbo hayo.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kushoto) akitazama hatua ya uchomaji wa Madini ya Jasi kwenye kiwanda cha kampuni ya mzawa cha RSR kilichopo katika Kijiji cha Sanjaranda, Itigi kabla ya kusagwa kuwa unga na baadaye kusafirishwa hadi Dar es Salaam kwa ajili ya kuuzwa na mwingine kutumika katika Kiwanda cha kutengenezea mapambo ya Majumbani, katika kiwanda kilichopo Singida mjini.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akitazama Chaki zinazozalishwa na Kiwanda cha Dobercolor kilichopo katika Kijiji cha Majengo, Itigi ambazo huuzwa ndani na nje ya Mkoa huo huku lengo likiwa ni kuuza nje ya Tanzania.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


IGP SIRRO AKAGUA NA KUSHIRIKI MAZOEZI YA UKAKAMAVU NA ASKARI WA MKOA WA TABORA.

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro wa tatu toka kulia alishiriki  mazoezi ya utayari na kuwatia hamasa Askari wa  Mkoa wa Tabora,  katika ziara yake ya siku moja mkoani humo, hatua hiyo ni kutokana na kuwataka askari wa Jeshi la Polisi kuwa na utayari wakati wote .  Picha na Jeshi la Polisi.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro akiwa amembeba Joshua mtoto wa muumini wa kanisa la Siroham mkoani Tabora kabla ya uzinduzi wa zahanati ya Polisi iliyojengwa kwa hisani ya kanisa hilo.  Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro wa tatu kutoka kushoto akiangalia  mmoja wa askari wa Jeshi la Polisi akiwa katika mazoezi ya utayari kupita juu ya kamba mkoani Tabora .  Picha na Jeshi la Polisi.

KIWANDA CHA SARUJI TANGA (SIMBA CEMENT) YATOA MIFUKO 760 KUCHANGIA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA SHULE YA MSINGI PONGWE JIJINI TANGA

$
0
0
 Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akipanga tofali kwenye msingi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya msingi ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino)  na wasioona ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo
 Mkurugenzi  Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akijenga tofati katika vyumba vipya vitatu vya madarasa kwenye shule ya Msingi ya
ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na wasioona  ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa
 Mkurugenzi  Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akiweka  tofati katika vyumba vipya vitatu vya madarasa kwenye shule ya Msingi ya
ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na wasioona ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa.
 Mkurugenzi  Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akiweka sawa tofati katika msingi wa moja ya vyumba vipya vitatu vya madarasa kwenye shule ya Msingi ya  ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na wasioona ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

BOHARI YA DAWA (MSD) MSHINDI WA PILI SEKTA ZA UMMA KATIKA TUZO YA MWAJIRI BORA 2017

$
0
0
Na Dotto Mwaibale

BOHARI ya Dawa (MSD) imeibuka kidedea kwa kuwa mshindi wa pili (2) kwa upande wa Sekta za Umma katika tuzo ya Mwajiri Bora mwaka 2017 zinazoandaliwa na Chama cha Waajiri nchini ( ATE). 

Akizungumza katika hafla ya utoaji tuzo hizo, Mgeni rasmi Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema uanzishwaji wa vipengele vipya katika tuzo hizo unazipa fursa za kipekee taasisi za serikali kupata nafasi ya kushiriki na kushinda. 

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa MSD, Bi.Victoria Elangwa amesema tuzo hiyo ni matokeo ya maboresho ya kiutendaji kwa MSD ambayo yanafanyika kulingana na Mpango Mkakati wa MSD wa mwaka 2017 -2020.

Ameongeza kuwa hatua hiyo ya MSD kupata tuzo ya Taasisi ya Umma inayofanya vizuri ni motisha kwa wafanyakazi na MSD kwa ujumla kufanya kazi kwa bidii zaidi.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Bohari ya Dawa (MSD), Victoria Elangwa (kulia), akipokea tuzo ya mshindi wa pili Sekta za Umma katika Tuzo ya Mwajiri Bora 2017 katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam jana.
Wafanyakazi wa MSD wakiwa kwenye hafla hiyo.
Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Mhagama, akimkabidhi cheti cha ushiriki wa tuzo hizo Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Bohari ya Dawa (MSD), Victoria Elangwa. Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Anthony Mavunde.
Wafanyakazi wa MSD wakifurahia ushindi huo wakiwa na tuzo zao.

GCAM CREDIT SCORING TEAM MEETS TADB BOARD OF DIRECTORS

$
0
0

By Our Reporter,

A delegation from Group Credit Agricole of Morocco (GCAM) has met the Tanzania Agricultural Development Bank (TADB)’s Board of Directors in order to brief the Board the purpose of their visit.

Speaking with TADB’s Board of Directors, Mr. Jalal Bouchama who is GCAM’s Director of Engineering and Agro business said that his team is in the country to facilitate to develop a Credit Scoring System that means to be used in scoring small holder’s farmer’s projects in Tanzania.

“We intend to develop Credit Scoring System that will speed up the process of identifying viable projects through scoring small holder’s farmer’s projects in Tanzania,” he said.

According to Mr. Bouchama, since its inception in 2004 the Credit Scoring System has assisted Morocco to advance its agriculture and socio-economic development in rural areas by identifying visible agricultural and rural development projects in Morocco.

On her part, Chairperson of TADB’s Board of Directors, Madame Rosebud Kurwijila said the Bank appreciates GCAM visit in the country hoping once the System will be operationalized will enhance TADB to achieve Government’s intentions in supporting Tanzania’s agricultural development.

“We do appreciate your visit hoping that we will work together to achieve Bank’s main objectives that are bestowed by our Government in efforts to bring about economic growth and poverty reduction in the country,” she said.

Tanzania Agricultural Development Bank (TADB) and Group Credit Agricole of Morocco (GCAM) signed a memorandum of Understanding (MoU) IN October 2016.The MoU intends to promote productive investments in the agriculture sector and development of agro-industrial value chains in the respective countries.

According to the signed MoU, these objectives will be achieved through promotion of financing and support systems, especially for smallholder’s farmers.The delegation from GCAM led by Director of Engineering and Agro business, Mr. Jalal Bouchama, other members include Chief of Agroindustry Department, Mrs. Sanae Benmali, Director of Credit Information System, Mr. Abdessamad Danguir and Ms. Sara Nachid, IT Developer.
Chairperson of TADB’s Board of Directors, Madame Rosebud Kurwijila (left) talks with a delegation from Group Credit Agricole of Morocco (GCAM) on the right side when the delegation meets with Bank’s Board of Directors.
TADB Acting Managing Director, Mr. Francis Assenga (standing) briefs Bank’s Board of Directors on importance of GCAM visit in the country. Looking on is delegation from Group Credit Agricole of Morocco (GCAM) and TADB’s Manager for Credit Appraisal, Mr. Samuel Mshote (left).
Chairperson of TADB’s Board of Directors, Madame Rosebud Kurwijila (left) emphasizes on the need of the Credit Scoring System in Banks’s operations to delegation from Group Credit Agricole of Morocco (GCAM) (not in picture). According to Madame Kurwijila the System is important in supporting Tanzania’s agricultural development. Right is Bank’s Board Director, Madame Rehema Twalib.
GCAM delegation together with TADB’s TADB Acting Managing Director, Mr. Francis Assenga (second left) and TADB’s Manager for Credit Appraisal, Mr. Samuel Mshote (left) attentively listen to Chairperson of TADB’s Board of Directors, Madame Rosebud Kurwijila (not in picture)
Head of delegation from Group Credit Agricole of Morocco, Mr. Jalal Bouchama (right) who is a Director of Engineering and Agro business hints the role of GCAM on agriculture and socio-economic development in Morocco to the TADB’s Board of Directors (not in picture).
Some members of TADB’s Board of Directors listen to Head of delegation from Group Credit Agricole of Morocco, Mr. Jalal Bouchama (not in picture). From left is Madame Rehema Twalib, Mr. Dome Malosha and Mr. Hassan Mbululo. Others are Mr. Joanes Kerenge and Mr. Joseph Mutashubilwa.

TATU MZUKA YAWATUNUKU WASHINDI WA WAWILI WA SH. MILIONI 10

$
0
0
Mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka umetoa  washindi wa wawili wa sh. Milioni  10  katika droo maalumu ya mwisho wa mwaka ili kuwapa wachezaji wa droo hiyo kufurahia sikukuu za mwisho wa mwaka .

Akizungumza na waandishi habari wakati wa kukabidhi hundi hizo  kwa washindi hao , Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba amesema droo hiyo inachezwa majira ya saa tatu na nusu usiku ambayo inakwenda hadi mwishoni wa mwaka.

Kemi amesema  kuwa washindi wote waliopewa hundi ni kutokana na kushinda mchezo huo kwa kufuata taratibu zilizowekwa za  mchezo,Amesema Watanzania waendelee kuchangamkia fursa ya mchezo huo na kuibuka washindi na kufurahi  msimu wa sikukuuu na ziku zinazoendelea.

Kemi amesema kuwa droo ya walioshinda ni maalumu na wakiona umuhimu wataweza kuitumia na droo zingine zikiendelea.Mshindi wa Tatu Mzuka wa Sh.milioni 10, Samson Mwamwenda amesema  hakuamini kama ameshinda kutokana na kusikia watu wanashinda.

Amesema kuwa amecheza kwa wiki mbili akipata sh.2000  na mara ya mwisho akapata sh.10,000 lakini ameweza kushinda milioni 10.
 Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akimkabidhi hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka ,Samson Mwamwenda,mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .
 Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akimkabidhi hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka ,Godfrey Madeje,mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .

Viewing all 110078 articles
Browse latest View live




Latest Images