Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

PROFESA MBARAWA: UJENZI WA JENGO LA TATU LA ABIRIA UMEGHARIMU SHILINGI BILIONI 560

$
0
0


Waziri wa ujenzi  uchukuzi na mawasiliano  Profesa Makame Mbarawa amefanya  ukaguzi   wa maendeleo ya ujenzi wa jengo la 3 la abiria la kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere   (JNIA)  ambao unatarajia kukamilika ifikapo mwakani .
 Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali Jijini Dar es Salaam katika viwanja vya ndege Juliuas  Nyerere  (JNIA) profesa Mbarawa amesema kuwa  ujenzi huo ambao umefikia asilimia 67 kukamilika umegharimu  takribani shilingi bilioni 560 katika ujenzi wake hadi sasa.
Aidha waziri huyo ametanabaisha kuwa  jengo hilo la 3 la abiria litakuwa na uwezo wa kuhifadhi ndege kubwa 11 ambapo huchukua abiria mia 300 hadi 400 na  ikiwa kwa ndege ndogo daraja c ni 21  nazo huchukua abiria 120-160 kwa kila moja.
Hata hivyo profesa Mbarawa amesema kuwa abiria wataondokana na changamoto ya kuchukua muda mrefu  katika kitengo cha uhamiaji pale wanapolazimika kufanyiwa ukaguzi  kutakuwa na mabadiliko ya kisasa  ya wahudumu  24  watakaokuwa wanahudumia abiria hao kwa muda usiopungua dakia 20 ili kuondokana na usumbufu pamoja na kuboresha huduma hizo .
Vile vile Mkurugenzi wa viwanja vya ndege vya mikoa Richard Mayongela  ( DRA)  amesema kuwa abiria watapata huduma za viwango vya kimataifa ikiwa pia na  kufungwa  mitambo ya kisasa ili kudhibiti uhalifua utakojitokeza ikiwemo kusafirisha nyaraka za serikali bila kibali maalumu.
Mkurugenzi mayongela amemalizia kwa kusema  kuwa kutakuwa na fursa za wafanya biashara  mara baada ya jengo hilo kumalizika na kuwataka  wawekezaji kuchangamkia  fursa hiyo ikiwa ni mojawapo ya kuiingizia kipato mradi huo .
 aziri wa ujenzi  uchukuzi na mawasiliano  Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali kuhusu maendeleo ya mradi wa ujenzi wa jengo la 3 la abiria Jijini Dar es Salaam katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere   (JNIA).
 Mkurugenzi wa viwanja vya ndege vya mikoa Richard Mayongela  ( DRA) akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali wa hapa nchini kuhusu uwanja huo utakavyokuwa wa kisasa na huduma bora leo Jijini Dar es Salaam katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere   (JNIA).
Wadau mbalimbali hapa nchini waliohudhuria mkutano huo wa maendeleo ya ujenzi wa jengo la 3 la abiria Jijini Dar es Salaam katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere   (JNIA).
 Waziri wa ujenzi  uchukuzi na mawasiliano  Profesa Makame Mbarawa akikagua ujenzi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo la 3 la abiria Jijini Dar es Salaam katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere   (JNIA).
 Waziri wa ujenzi  uchukuzi na mawasiliano  Profesa Makame Mbarawa akiteta jambo na Mkurugenzi wa viwanja vya ndege vya mikoa Richard Mayongela  ( DRA) Jijini Dar es Salaam katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere   (JNIA).

MAHARAMIA WA KAZI ZA WASANII KUFIKISHWA MAHAKAMANI WIKI IJAYO

$
0
0

Maharamia wa kazi za wasanii zaidi ya 200 waliokamatwa katika zoezi laukamataji kazi feki za sanaa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wiki ijayo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Auction Mart, Alex Msama amesema kuwa kwa sasa anaishukuru serikali kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakiuonyesha kwa kuwa bega kwa bega kwa vile wamekuwa wakinyonya wasanii.

"Ndugu zangu waandishi nimewaita hapa kuwaeleza juu ya zoezi la kumkamata maharamia wa kazi za sanaa bado linaendelea vizuri na sasa wanatarajia kufikishwa mahakamani wiki ijayo ili waweze kusomewa mashtaka yao," Alisema Msama.

Msama alisema kuwa mpaka sasa msako huo umefanikisha kukamata vifaa vya zaidi ya bilioni 1 ambavyo ikiwemo kopyuta, laptop na cd feki.Aliongeza kuwa watanzania lazima walipe kodi na wauze kazi zilizo na stika za mapato (TRA) ili wasanii wapate mapato na serikali ipate mapato.

"Wamachinga acheni kulalamika, mnaopoenda kununua Filamu za nje na ndani hakikisheni Filamu hiyo ina Stika ya TRA, ukiuza yenye Stika mtu hatokukamata", amesema Msama.Msama aliwaomba Watanzania watambue awamu hii ya Tano ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli haitaki ujanja ujanja, lazima kufanya kazi kwa bidii ili upate kipato halali.

Hata hivyo, zoezi laukamataji Kazi feki za sanaa litaendelea katika Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni zoezi la nchi nzima.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Auction Mart, Alex Msama akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam.
Mzigo ambao mpaka sasa umeshakamatwa ukiwa umeifadhiwa.Picha/Habari na Kajunason/MMG-Dar es Salaam. 

WAZIRI MPINA AITAKA KAMPUNI YA GAME TRACKING SAFARIS (TGTS) KUONDOKA KWENYE RANCHI YA UVINZA KABLA YA JANUARI 2018

$
0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina ameutaka uongozi wa Kampuni ya Game Tracking Safaris(TGTS) kuangalia na kupitia nyaraka walizonazo ili kuona uhalali wa umiliki wa eneo la hekta 20000 kwenye vitalu tisa vilivyomo kwenye Ranchi ya Uvinza inayomilikiwa na Kampuni ya Ranchi za za Mifugo za Taifa (NARCO)kabla ya Selikali kuwatoa kwa nguvu ifikapo tarehe 1/1/2018.

Waziri Mpina ametoa maelekezo hayo leo alipotembelea Ranchi ya Uvinza kuangalia shughuli mbalimbali katika Ranchi hiyo ambapo ametoa muda wa hadi Januari mosi mwakani kwa mwekezaji huyo kuondoka katika eneo hilo endapo atabaini kuwa amekuwa akikaa kimakosa kuanzia katika vitalu namba 41 hadi 49.

Aidha Waziri Mpina amesema endapo Mwekezaji huyo ataendelea kubaki baada ya tarehe Mosi Januari, Serikali itamuondoa kwa nguvu na atatakiwa kulipa gharama zote za fidia na usumbufu.“Ninakuagiza angalia taarifa mbalimbali ulizonazo kuhusu umiliki wa eneo hili kama utaona umeendelea kukaa hapa bila kufuata taratibu tafadhali uondoke mara mmoja ili kupisha Serikali kuendelea na shughuli zake” alisisitiza Mpina

Waziri Mpina amemuagiza Meneja Mkuu wa NARCO, Profesa Philemoni Wambura kuwaandikia barua ya kuwaondoa wawekezaji wote katika Ranchi hiyo ambao hawajaendeleza kwa zaidi ya asilimia 40 na kwamba wawekezaji ambao wamewekeza kwa zaidi ya asilimia arobaini wanatakiwa kukamilisha malipo yote kabla ya Januari mosi mwakani.

Alionya wawekezaji kuacha tabia ya kuidanganya serikali kwamba wanauwezo wa kuwekeza katika vitalu ili wapewe lakini wanabadili matumizi baada ya kupewa. Aliongeza kwamba Serikali imegundua baadhi ya wawekezaji wanaopewa vitalu wanawakodisha wafugaji kutoka nchi jirani na kujipatia faida wakati Serikali haipati chochote.

Awali, Meneja wa (TGTS) Audax Kalulama akizungumza kwa simu na Waziri Mpina kutoka Arusha amesema kwamba eneo hilo wanamiliki kihalali na kuomba muda ili wawasiliane na Wizara ya Mifugo kuonyesha taarifa za umiliki wa eneo hilo.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh.Luhaga Mpina akizungumuza na Meneja wa Kampuni ya Game Tracking Safaris(TGTS) Audax Kalulama katika simu alipotembelea Ranchi ya Uvinza leo na kuamuru mwekezaji huyo kuondoka kabla ya Januari Mosi mwakani kutokana na Mwekezaji huyo kukaa katika eneo hilo kinyume cha Sheria.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh.Luhaga Mpina (katikati) kitoa maamuzi ya kuitaka Kampuni ya Game Tracking Safaris(TGTS) kuondoka katika eneo la hekta 20000 kwenye vitalu tisa vilivyomo kwenye Ranchi ya Uvinza ifikapo tarehe 1/1/2018.
Sehemu ya Ranchi ya Uvinza.
.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh.Luhaga Mpina (katikati) akiwasikiliza walinzi wa Kampuni ya Game Tracking Safaris(TGTS) hawapo pichani wakitoa maelezo alipotembelea Ranchi ya Uvinza .

MLATA AAGIZA MAKAMBI YA UVCCM KUWAJENGEA NYUMBA VIKONGWE WANAOISHI KWENYE NYUMBA ZINAZOTISHIA MAISHA YAO

$
0
0

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida,Marther Moses Mlata ameuagiza umoja wa vijana wa Chama hicho kutumia muda wanapokuwa kwenye makambi ya vijana kuwasaidia wazee  wanaosihi katika nyumba zinazotishia maisha yao kwa kuwajengea na kuwakabidhi wazee hao ili waweze kujihakikishia usalama wa maisha yao.
Mlata ambaye pia ni mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Singida alitoa agizo hilo wakati alipokuwa akimpokea mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Singida,Dk.Denisi Nyiraha alipokwenda kujitambulisha kwenye ofisi za chama hicho Mkoa wa Singida.
Aidha Mwenyekiti huyo aliyemaliza muda wake aliweka bayana kwamba kumekuwa kukifanyika makambi mengi sana na kambi hizo zimekuwa zikiwasaidia vijana kujifunza mambo mengi sana,lakini wakati vijana hao wanapokuwa makambini na kugundua kuna nyumba ya mkongwe mmoja inayokaribia kudondoka,watumie makambi hayo kuwasaidia wazee kama hao kunusuru maisha yao.
“Ukiwa kule unamuona ndani anavyozunguka,ninaomba makambi yale kama vijana tusaidieni wazee wale wasiangukiwe na nyumba zao na fanyeni taratibu yeyote mmeweka kambi mkifanya mafunzo yenu,lakini hakikisheni mnafyetua matofali na kuweka harambee kumjengea nyumba mpya na kumwambia bibi au babu ingia hapa”alisisitiza Mlata.  
Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Singida,Dk.Denisi Nyiraha aliahidi kuunda kamati ndogondogo kuanzia ngazi ya wilaya hadi Mkoa ili kurahisisha majukumu ya mwenyekiti wa wilaya na Mkoa ikiwa ni pamoja na kuibua mipango mipya na endelevu ya kukuza na kujenga jumuiya.
Mwenyekiti huyo alisema ili kufanikisha azma hiyo ni wajibu wa kila wilaya ianze kujiandaa kuunda kamati ya sera na mipango kwenye ngazi ya Mkoa hadi katika ngazi za wilaya na kuitaja kamati nyingine atakayounda ni kamati ya uchumi itakayokuwa na wajibu wa kwenda kubaini vyanzo vya jumuiya katika ngazi hizo.
“Kwa hiyo kamati hii itakuwa na wigo mpana na kwa mfano nitolee majukumu ya kamati hii ya uchumi ngazi ya mkoa,tutaunda chombo kitakachokwenda kufanya auditing,kitakachoenda kufanya upembuzi yakinifu kwenye miradi yote kwenye ngazi ya Mkoa”alisisitiza Dk.Nyiraha.
Hata hivyo Dk.Nyiraha alitumia fursa ya kikao hicho kutoa angalizo kwa kiongozi yeyote yule iwapo alishiriki kwa njia yeyote ile katika matumizi mabovu ya miradi na iwapo kuna fedha ambazo bado anazo aliagiza azirudishe bado mapema.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo wale wote waliohusika kuhujumu mali za chama,mali za umoja wa vijana wajiandae kuzirejesha maana hawatafumbiwa macho na kwamba miradi yote ya chama kuanzia ngazi ya wilaya ambayo imetaifishwa na vyombo tofauti tofauti waliombwa kuvirejesha haraka iwezekanavyo,
Hata hivyo katika risala wa chipukizi iliyosomwa kwa Mwenyekiti huyo wa UVCCM,imeeleza changamoto zinazowakabili vijana hao kuwa ni pamoja na kutokuwa na sare za kijani na suruwali nyeusi na wanatarajia kuwa ombi lao watatekelezewa.

SERIKALI YAMPA SIKU 100 MKANDARASI KUKAMILISHA UJENZI MRADI WA MAJI CHALINZE

Waziri Jenista Mhagama-Maadhimisho ya Uhuru ya Mwaka Huu Kuwa ya Aina Yake

Mkazi wa Arusha ashinda milioni 86 ya M-bet

$
0
0
Mkazi wa Arusha, Sagi Thomas (37) amejishindia kitita cha sh milioni 86 kwa kubashiri kwa usahihi mchezo maarufu kwa ‘Perfect 12’ unaondeshwa na kampuni ya mchezo wa kubahatisha ya M-Bet.

Thomas alikabidhiwa kitita chake jana na Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley. Malley alisema kuwa Thomas alifanikiwa kubashiri sahihi jumla ya mechi 12 kati ya 17 na kuwa mshindi wao wa droo ya 17 tokea kuanzishwa kwa mchezo wa Perfect 12. Alisema kuwa serikali imejipatia jumla ya Sh milioni 15.5 kutoka kiasi hicho cha fedha ambacho ni asilimia 18 kwa mujibu wa sheria.

“Kama tulivyosema hapo awali, M-Bet ni nyumba ya washindi na leo tumedhihirisha usemi wetu ambapo Thomas anajisindia mamilion ya fedha kwa kutumia kiasi cha She elfu moja tu, hii imedhihirisha kuwa tunawaomba mashabiki wa soka kuendelea kucheza mchezo wetu ili kujishindia fedha,” alisema Malley.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha zake, Thomas alisema kuwa atazitumia fedha hizo kwa kuanzisha vitega uchumi na vilevile kuwaendeleza kielimu ndugu zake.

“Nina furaha sana, mimi ni mwajiriwa wa serikali, leo hii nina faraja kubwa kuona kiasi cha Sh 1,000 tu kimeniwezesha kushinda mamilioni ya fedha, M-Bet imebadilisha maisha yangu” alisema Thomas. Meneja wa Tehama wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha (GBT), Kabora Mboya aliwashukuru M-Bet kwa kuendelea vyema na shughuli zake mbali ya kuwazawadia washindi mara kwa mara.
 Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley (kushoto) akimkabidhi hundi mshindi wa mchezo wa Perfect 12, Sagi Thomas (kulia) ambaye amejishindia kitita cha sh milioni 86. Katikati ni Meneja wa Tehama wa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha (GBT), Kabora Mboya.
 Mshindi wa mchezo wa Perfect 12 Sagi Thomas 'akipozi' na mfano wa hundi mara baada ya kukabiziwa jana. Kalinga alijishindia kitita cha sh milioni 86.

UZALENDO NA UTAIFA KAMPENI KUZINDULIWA LEO NA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI

$
0
0


LEO ni siku ya Uzinduzi wa kampeni ya Uzalendo na Utaifa. Uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa Chimwaga Dodoma,  kwa ratiba itakayoanza saa 9 mchana na kuisha saa 3 usiku.. Kati ya matukio yatakayokuweko ni maandamano yatakayoshirikisha wasanii mbalimbali na pia kazi za sanaa, baada ya watu wote kufika na kutulia Chimwaga kutakuweko na wimbo maalumu wa Uzalendo, filamu ya kihistoria, hotuba za viongozi wastaafu, uzinduzi wa kitabu, na kisha Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania atatoa vyeti vya udhamini hatimae chakula. Wimbo hapo juu ni kazi ya wanamuziki Anania Ngoliga na John Kitime wakipiga gitaa na rimba kuisifia nchi yao,

NIC YAMKABIDHI MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR MILIONI 20 ZA BIMA YA MAISHA

$
0
0
Makamu wa pili wa Rais katika serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Alli Iddi akipokea mfano wa hundi ya malipo yake ya bima ya maisha iliyoiva kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa NIC Bw. Sam Kamanga. Sherehe hizo zilifanyika jana jumatano mjini Zanzibar mbele ya Baraza la Wawakilishi wakati wa mafunzo ya bima yaliyotolewa na timu ya wataalam kutoka Makao Makuu wakishirikiana na tawi la Zanzibar.Kwa kawaida bima ya maisha huiva baada ya miaka kumi. Wawakilishi Zanzibar Zuberi Ali Maulid.
Makamu wa pili wa Rais katika serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Alli Iddi kushoto akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa NIC Bw. Sam Kamanga. kbla ya kupokea hundi ya Shilingi milioni 20 kutoka kwa Mkurugenzi huyo baada ya bima ya Maisha ya Makamo huyo wa Rais kuiva.Sherehe hizo zilifanyika jumatano wiki hii mjini Zanzibar mbele ya Baraza la Wawakilishi katikati ni Spika wa Bunge la Wawakilishi la Zanzibar Zuberi Ali Maulid 
Mtendaji wa NIC Bw. Sam Kamanga akizungumza katika hafla hiyo 

ALICHOSEMA NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA BAADA YA KUTEMBELEA MAPOROMOKO YA MTO KIMANI KATIKA PORI LA AKIBA MPANGA KIPENGELE

$
0
0

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akionyeshwa njia ya kuelekea kwenye maporomoko ya maji ya mto Kimani na Kaimu Meneja wa Pori la Akiba la Mpanga Kipengele, Stanslaus Odhiambo (katikati) alipotembelea maporomoko hayo katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akionyeshwa maporomoko ya maji ya mto Kimani na Kaimu Meneja wa Pori la Akiba la Mpanga Kipengele, Stanslaus Odhiambo (katikati) alipotembelea maporomoko hayo jana katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune kwenda eneo la maporomoko ya maji ya mto Kimani ambayo yapo ndani ya Pori la Akiba la Mpanga Kipengele katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) akiangalia maporomoko ya maji ya mto Kimani alipotembelea Pori la Akiba la Mpanga Kipengele katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, David Kanyata (kushoto) na baadhi ya wafanyakazi wa Pori la Akiba la Mpanga Kipengele alipotembelea  maporomoko ya maji ya mto Kimani ambayo yapo ndani ya pori hilo katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70
Maporomoko ya Maji ya Mto Kimani ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika Pori la Akiba la Mpanga Kipengele katika Wilaya ya Makete mkoani Njombe. Maporomoko hayi yana urefu wa mita zaidi ya 70.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune wakiangalia moja fuvu la mnyamapori katika moja ya pango ambalo ambalo Chief Mkwawa alilitumia kujificha wakati wa vita na wakoloni alipotembelea Pori la Akiba la Mpanga Kipengele katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. 
Picha ya pamoja. (Picha na Hamza Temba)

RC KILIMANJARO,ANNA MGWIRA ATANGAZA RASMI KUHAMIA CCM

$
0
0

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwira baada ya kutangaza rasmi kuhamia Chama cha Mapinduzi, katika ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete, mjini Dodoma Desemba 8, 2017.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

WATENDAJI NA WATAALAMU WA WILAYA YA HANDENI WATAKIWA KUSIMAMIA SUALA LA ELIMU YA MADHARA YA UKEKETAJI

$
0
0
Watendaji na wataalamu wa Wilaya ya Handeni wametakiwa kusimamia na kuweka suala la elimu ya madhara ya ukeketaji kuwa ajenda rasmi kwenye vikao vyao ngazi ya Kata na Tarafa ili kukomesha kabisa vitendo vya ukeketaji kwa watoto wa kike wa jamii ya wafugaji hususani pindi mradi wa “KIJANA WA LEO” unaofadhiliwa na shirika la Amref kukoma.

.Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe ametoa rai hiyo leo alipohudhuria sherehe za uvushwaji rika wa wasichana 170 wa jamii ya wafugaji(Ndito) zilizofanyika Kata ya Malezi katika mtaa wa Kwamadule.

Mh. Gondwe alisema kuwa ni haki ya binti anapokuwa mtu mzima na kuvushwa rika asiweze kunyanyaswa kijinsia, kwasababu athari za ukeketaji zinafahamika ikiwa ni pamoja na kuwa ni kitendo ambacho ni kinyume na maagizo ya Mungu lakini pia uvunjwaji wa haki za binadamu..

Ameongeza kuwa jamii ya wafugaji inatamaduni zilizoshiba na wanachangia kwa kiasi kikubwa kuingizia pato na fedha za kigeni Taifa, ni utamaduni bora unaotambulisha Tanzania kwa zaidi ya makabila 120.Watu wanapenda tamaduni za kimasai na jamii za wafugaji wengine lakini mila ambazo ni potofu zinazoleta maumivu katika jamii zitokomezwe.

“ sherehe na kila kitu kifanyike, watoto wafundishwe lakini ukeketaji hapana ili tumuokoe binti huyu na maumivu makali kwa sababu morani wamekubali kuoa wananwake ambao hawajakeketwa na kwasasa wanaoa hata jamii zingine ambazo wanawake hawajakeketwa” alisema Mkuu wa Wilaya.
  Mkuu wa Wilaya ya Handeni akizungumza na Mangariba na kuwapongeza kuelimika kuacha vitendo vya ukeketaji kwa watoto wa kike.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe akikaribishwa kwenye sherehe za uvushaji rika.
 mangariba wakionesha namna ambavyo  huwakamata wasichana (ndito) wa kimasai kuwapeleka kwenye chumba cha ukeketaji.
 ​Mmoja wa wazee wa kimila akishukuru Amref kwa Elimu waliyopewa juu ya uvuhsaji rika wasichana kwa kufanya sherehe na mila zao bila kukeketa.​
​mmoja wa wsichana waliovushwa rika bila kukeketwa akipokea cheti cha kufuzu mafunzo ya kuzuia ukeketaji na mafunzo ya afya ya uzazi​.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Aliyedaiwa kuuibia DCB bank aachiwa huru

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya Jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru mfanyabiashara Manfred Sangawe aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya wizi wa fedha zaidi ya Shilingi milioni 130 za benki ya DCB.

Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi amemuachia huru mshtakiwa huyo, baada ya Wakili wa Serikali, Mwanaamina Kombakono kuomba aachiwe chini ya kifungu cha 91(1)  cha sheria ya Makosa ya Jinai,(CPA) kwa kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi yake.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, mahakama iliridhia ombi hilo na kumuachia huru Sangawe.

Mbali na Sangawe,  wenzake sita akiwamo John Sarakikya, Hidergard Mahrurus na wafanyakazi wa benki hiyo, Suzan Kaboko na Belinda Chaula bado wanaendelea kukabiliana na kesi hiyo yenye mashtaka 14 yakiwamo ya kula njama, kughushi na wizi na ipo katika hatua ya usikilizwaji wa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka.

Katika shtaka la kula njama, washtakiwa hao wote wanadaiwa tarehe tofauti kati ya Septemba mosi na Novemba 16, 2015 Dar es Salaam, walikula njama na watu wengine kuidanganya benki hiyo kuhusu Shilingi milioni 313.

Pia, washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka ya kughushi barua na fomu za kuhamisha fedha za kiwango tofauti wanadaiwa kuyatenda katika benki hiyo tawi la Arnautoglou.

Washtakiwa hao wanadaiwa kuiibia benki hiyo viwango tofauti vya fedha ambavyo vinafikia zaidi ya Sh 139 milioni.

VIDEO: MAHAKAMA YA TANZANIA YAENDELEA NA PROGRAMU YA MABORESHO YA HUDUMA ZA MAHAKAMA

KESI YA UTAKATISHAJI FEDHA: RUGEMALILA ADAI UNAHITAJIKA USHIRIKIANO BAINA YAKE NA UPANDE MASHITAKA KUMBAINI MWIZI WA BILIONI 309 ZA SERIKALI.

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Mfanyabiashara James Rugemarila anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha amedai mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa unahitajika ushirikiano baina yake na upande wa mashtaka ili kumbaini mwizi wa Bil 309 za serikali wanazodaiwa kuiba.

Katika kesi hiyo, Rugemarila, anashtakiwa pamoja na mmiliki wa IPTL, Harbinder Singh Sethi ambapo wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi likiwemo la utakatisha fedha na kuisababisha serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na Bil 309.

Rugemarila amedai hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Mwendesha Mashtaka kutoka Takukuru, Leornad Swai kuieleza mahakama kuwa kesi leo imekuja kwa kutajwa na upelelezi bado haujakamilika.

Rugemarila alidai upelelezi wa tuhuma zao ulianza tangu 2014 na sio miezi sita iliyopita kama alivyoeleza.Amedai kuwa anahitaji apate ushirikiano kutoka kwa upande wa Jamhuri ili wamjue na kumtaja ni nani mwizi wa Bil.309 za serikali.Aidha amedai kuwa hajawahi kupata nafasi ya kuzungumza na mawakili wake tangu alipotoka mahakamani hapo tarehe iliyopita.

"Nashindwa kupata ushauri, wala sijui nini kinaendelea kuhusu kesi yangu, hivyo angalau naomba waruhusiwe mawakili angalau wawili badala ya 10 ili wawe wananielezea kuhusu ilipofikia hii kesi,".Awali kabla ya kutoa hoja hizo, Wakili wa utetezi Balomi alidai kuwa suala la upelelezi katika kesi hiyo linachelewesha, huku ikizingatiwa linakiuka misingi ya haki ya kikatiba kwa washtakiwa.

" Ni miezi 6 sasa, tunaambiwa upelelezi haujakamilika, Wakili wa serikali anashindwa hata kutuambia umefikia wapi na umebaki muda gani kukamilika,".Pia Wakili Balomi amedai kuwa hali ya washtakiwa kiafya sio nzuri hasa Seth, hivyo upelelezi ukamilishwe kwa haraka ama wawe wanaelezwa hatua ulipofikia.Akijibu hoja hizo Wakili Swai alidai kuwa, upande wa utetezi ndio umekuwa ukikwamisha mchakato wa upelelezi kwani wamekuwa wakinyimwa baadhi ya nyaraka.

Swai aliongeza kudai, kuchelewa kwa upelelezi huo pia kunasababishwa na ushahidi mwingine kuwepo nje ya nchi.Kesi hiyo imeahirishwa hadi December 22, 2017 upande wa mashtaka umetakiwa kukamilisha upelelezi.

KUMBILAMOTO AGAWA JEZI KWA TIMU NNE ZILIZOINGIA NUSU FAINALI YA VINGUNGUTI SUPER CUP

$
0
0
  Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto, akikabidhi jezi kwa kiongozi wa timu ya Freemason Fc ya Vingunguti, Sudi Rashid
  Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto, akikabidhi jezi kwa kiongozi wa timu ya Guantanamo Fc ya Vingunguti ,Abdul Mgohela
  Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto, akikabidhi jezi kwa kiongozi wa timu ya Msako FC ya Kigogo Kani Masumbola  wakati wa hafla ya kukabidhi jezi kwa timu nne zilizo ingia nusu fainali ya Vingunguti Super Cup
  Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto, akikabidhi jezi kwa kiongozi wa timu ya Relini Fc wa Vingunguti Halidi Kitapagala.

Kesi ya Uhujumu Uchumi dhidi ya Dkt.Ringo Tenga na wenzake yapigwa kalenda hadi Desemba 15.

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeipiga kalenda hadi Desemba 15/2017 kesi ya uhujumu uchumi na kusababisha hasara ya USD 3.7 milioni ambayo ni sawa na bilioni nane. inayowakabili vigogo wanne wa Kampuni ya Six Telecoms Limited na kampuni yenyewe.

Hatua hiyo imekuja baada ya wakili wa upande wa mashitaka, Jackline Nyantori kuieleza mahakama kuwa, upelelezi dhidi ya kesi hiyo bado haujakamilika na wanajitahidi kukamilisha mapema.

Wakili wa utetezi Masumbuko Lamwai akizungumza kuhusu upelelezi amedai, kesi wanayokabiliwa nayo washtakiwa siyo mpya, kwani ilishafikishwa mahakamani hapo kama kesi ya uhujumu uchumi Namba 2 ya mwaka 2016.

Amedai, upande wa mashtaka wanazo taarifa zote juu ya shauli hilo sababu mashtaka wanayoshtakiwa nayo ni juu tarrif za simu ambazo ni electronic na ziko recodedi hivyo hamna ushahidi wowote ambao bado haujakamilika.

"Wateja wetu wana umri mkubwa wametumikia nchi hii kwa muda mrefu, wanaambiwa upelelezi bado wakati mambo yote yako wazi, hii ni kuonesha kuwa hawana nia nzuri nao, wanataka tu kuwaweka ndani, tunaomba waambiwe wakamilishe upelelezi twenda mahakama kuu kusikiliza kesi.

Kufuatia hoja hizo, Wakili Nyantori amedai, siyo kweli kwamba hiyo kesi ni ya pili, kesi ya uhujumu uchumi Namba 2/2016 washtakiwa wa zamani ambao wapo kwenye kesi hii mpya ni wawili tu lakini hii mpya wako wanne, pia katika kesi hiyo kulikuwa na mashtaka mawili na hii mpya mashtaka ni matano, kwa hiyo ni kesi mbili tofauti. Tutajitahidi kukamilisha upelelezi.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 15 mwaka huu, washtakiwa wamerudishwa rumande.Washtakiwa katika kesi hiyo ni Mhandisi na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Six telecoms, Hafidhi Shamte, Mfanyabiashara na Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Peter Noni, Mwanasheria na Mhadhiri na Mkurugenzi wa hiyo kampuni Dr ,Ringo Tenga, Mkuu wa fedha wa kampuni hiyo Noel Chacha na Kampuni ya Six Telecoms Limited. 

Wote kwa pamoja wanadaiwa kuhujumu miundombinu ya mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kutoza garama chini ya kiwango, kushindwa kulipa ada za udhibiti na kutakatisha 3,282,741.12 

Pia washtakiwa hao wanadaiwa kuisababishia TCRA hasara ya USD 3,748,751.22, sawa na Sh 8 bilioni za kitanzania.

Wateja 20 wapokea zawadi kemkem za pesa kwa kufanya miamala kupitia Tigo Pesa

$
0
0
 Meneja wa Wateja wa Kampuni ya Tigo, Mary Rutta (kulia) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuwatangaza na kuwazawadia washindi 20 wa promosheni ya ‘Tumia Tigo Pesa na Ushinde,’ inayoendelea katika msimu huu wa Krismasi na Mwaka mpya, iliyofanyika leo kwenye ofisi zao, Makumbusho jijini Dar sa salaam. Kushoto ni Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Tigo, Woinde Shisael.

Huduma ya kutuma na kupokea fedha inayoongoza nchini Tanzania, Tigo Pesa leo imewatangaza na kuwazawadia washindi 20 wa promosheni yake ya ‘Tumia Tigo Pesa na Ushinde,’ inayoendelea katika msimu huu wa Krismasi na Mwaka mpya ambapo wateja wanajishindia mamilioni ya pesa.

Washindi wanne (4) wamepata bahatiya kushinda zawadi za kila siku za shilingi milioni moja kila mmoja, huku wengine 16 wakijaza mifuko yao na donge nono la shilingi laki tano (TZS 500,000) kila mmoja. each. Jumla ya shilingi milioni 12 zimetolewa kama zawadi kwa wiki hii.

Washindi wa zawadi za TZS 1 milioni ni wafanyabiashara Neema Fredrick Mosha, Fredrick Joseli Mponzi , Sefu Athumani Sefu na Hadija Mohamed Lukulumbale ambaye ni mama nitilie.
Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Tigo, Woinde Shisael akizungumza katika mkutano huo.

Washindi wa zawadi za TZS 500,000 ni Michael Joseph Moshi, Moses Muhonga Amuli, Saidi Khatib Kiko, Sylvester Michael Madaga, Aziza Ramadhani Ngozi, Evelyne Gwamaka Mwakyembe, Tumsifu Harold Temu na Sikudhani Constantine Mwenda. Wengine walioshinda TZS 500,000 ni Queentina Msafiri Mbwambo, Hilary Andrew Massawe, Ashura Ally Salim, Halima Saidi Shaabani, Fatuma Ally Makumbo, Halima Saidi Sangiwa, Jenifer Samuel Apolinale na James John Mkanula.

‘Tunatarajia kupata jumla ya washindi 153 katika kipindi cha mwezi mmoja wa promosheni hii. Bado tuna zawadi za thamani ya TZS 108 milioni kutoa kwa washindi 133,’ Meneja wa Wateja wa Tigo, Mary Rutta alisema wakati akikabidi zawadi kwa washindi Dar es Salaam leo. Alibainisha kuwa pamoja na zawadi za kila siku, promosheni hiyo ya ‘Tumia Tigo Pesa na Ushinde,’ itakuwa na zawadi kubwa za mwezi TZS 15 milioni, TZS 10 milioni na TZS 5 milioni.

Afisa Vigezo wa Tigo, Abdallah Nguba (kushoto) pamoja na Meneja wa Wateja wa Tigo Mary Rutta (kati) wakifanya droo ya kuwapata washindi wa promosheni inayoendelea ya 'Tumia Tigo Pesa na ushinde,' ambapo wateja wa Tigo wanapata fursa ya kushinda hadi milioni 15 kila wanapotumia Tigo Pesa. Jumla ya wateja 20 walijishindia kati ya shilingi laki tano na milioni moja leo. Kulia ni Afisa wa Bodi ya Michezo ya Bahati na Sibu Tanzania, Jehud Ngolo.

‘Kushiriki katika promosheni hii ni rahisi na ni wazi kwa wateja wote wa Tigo Pesa ambao wanahitaji kutumia huduma ya Tigo Pesa kwenye simu zao ili kupata nafasi ya kushinda. Kadri unavyotumia huduma ya Tigo Pesa ndivyo unavyojiongezea nafasi ya kushinda,’ alisema. Tigo Pesa inajivunia kufanya miamala ya zaidi ya TZS 1.7bn kila mwezi kupitia mtandao wake mpana wa mawakala zaidi ya 70,000 waliosambaa nchini kote.

SERIKALI WILAYANI GEITA KUWACHUKULIA HATUA KALI WATAKAO HUJUMU ZOEZI LA VITAMBULISHO VYA TAIFA

$
0
0

Na Joel Maduka-Geita

Serikali Wilayani Geita imesema haitamuhurumia yeyote atakayehujumu zoezi la uandikishaji kwa ajili ya vitambulisho vya Taifa.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo wa zoezi la kuwasajili wananchi kwenye halmashauri ya mji wa Geita, Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi alisema kituo chochote ambacho zoezi hilo halitaenda vizuri, hatua zitachukuliwa dhidi ya Mwenyekiti na mtendaji wa mtaa husika.

“Hatutakuwa na huruma na mtu yoyote ambaye hatahusika na kuhujumu zoezi hilo na kama tukisikia mwenyekiti wa mtaa na mtendaji kunatatizo ambalo limetokea tutakushughulikia hapo hapo na kama ni mwenyekiti wa mtaa sio kukushughulikia tu nitafuta nafasi yako tutachagua kiongozi mweningine hatutaki watu wasio na maadili kwenye Wilaya yetu.”Alisisitiza Kapufi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Geita, Mhandisi Modest Apolinary amewasisitiza wananchi kutumia nafasi hiyo kwa kuwa haitajirudia tena.“Ni waombe tu wananchi kwamba hii nafasi ambayo mmepewa ni nafasi ya kipekee sana haitajirudia tena kwa hiyo ni zamu ya wananchi wote kuhakikisha kwamba mnajitokeza kwa wingi kujiandikisha ili muweze kupata vitambulisho vyenu”Alisema Modest.

Mratibu wa NIDA Mkoani Geita Bw Emmanuel Ernest amesema wameanza usajili tarehe 23 August mwaka huu na kwamba wamesajili awamu 6 zenye jumla ya kata 12 na wananchi waliojiandikisha ni Laki moja, elfu 36 na 643 sawa na asilimia 75.33 na kwamba matarajio ni kuandikisha watu Laki moja elfu 81 na 374 hivyo waliobaki ni watu elfu 44 na 731.

Akielezea faida na umuhimu wa kitambulisho cha Taifa Mratibu alisema kuwa kitasaidia serikali kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato(kodi)pamoja na kuongeza idadi ya wanaotakiwa kulipa kodi,pia vitasaidia kupunguzia serikali gharama za kusafirisha daftari la wapiga kura,na kuwa daftari lenye taarifa sahihi za watu na mahali walipo.

Bi,Rosemary Yusuf ambaye ni mwananchi wa msalala road alisema vitambulisho vya Taifa vitawasaidia kwani watatambulika kuwa wao ni watanzania harari.
Mgeni Rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Geita,akizindua zoezi la usajili wananchi kwaajili ya kupatiwa vitambulisho vya Taifa , kwenye halmashauri ya Mji wa Geita ,Mratibu wa NIDA Mkoani Geita,Emmanuel Ernest akitoa maelekezo ya namna ya kutumia kifaa cha usajili. 
Mratibu wa NIDA Mkoani Geita,Emmanuel Ernest akizungumzia madhumuni ya uandikishaji wananchi kwaajili ya kupatiwa vitambulisho vya Taifa kwenye halmashauri ya mji wa Geita. 
Watoto wa kituo cha Brith light wakiimba wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo na mgeni rasmi pamoja na baadhi ya wadau wakiwatunza. 
Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi kulia ni Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Geita,Constatine Molandi akifuatiwa na diwani wa kata ya kalangalala,Sospeter Mahushi wakiwa kwenye zoezi la uzinduzi wa vitambulisho. 
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Geita Mhandisi Modest Aporinaly akizungumza na wananchi juu ya umuhimu wa zoezi la uandikishwaji vitambulisho vya Taifa. 
Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akisisitiza viongozi wa mitaa ambao wataonekana kuhujumu zoezi la usajili wananchi kwenye vitambulisho vya Taifa watachukuliwa hatua kali. 
Wananchi ambao wamejitokeza kujiandikisha wakiwa kwenye mstaari wakisubilia shughuli za kujisajili kwaajili ya kupata vitambulisho vya Taifa.

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM ) RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO WA TISA WA UMOJA WA WANAWAKE TANZANIA (UWT) MJINI DODOMA

$
0
0
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM , Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wajumbe wa mkutano  Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kabla ya kufungua mkutano wao wa Tisa uliofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma. 
 Wajumbe wa mkutano wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakishangilia kabla ya ufunguzi wa  mkutano huo wa tisa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma.
 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira akivalishwa Kitambaa kichwani mara baada ya kutangaza kuhamia Chama cha Mapinduzi CCM katika Mkutano wa tisa wa (UWT) uliofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma.
 Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira mara baada ya kuhamia rasmi katika Chama cha Mapinduzi CCM katika mkutano wa wa tisa wa UWT uliofanyika mjini Dodoma.
 Mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira mara baada ya kutangaza kuhamia Chama cha Mapinduzi CCM katika mkutano wa tisa wa UWT uliofanyika mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiimba  nyimbo za CCM pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan wa pili kutoka (kushoto), Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wa pili kutoka (kulia), Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli wakwanza kulia mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa tisa wa UWT uliofanyika mjini Dodoma.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live




Latest Images