Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU WABUNGE WA CUF WALIOVULIWA UBUNGE


MTANDAO WA UTEPE MWEUPE (WHITE RIBBON) WAZUNGUMZA NA WAKAZI WA KIJIJI CHA MAORE JUUU YA VIFO VTOKANAVYO NA UZAZI KWA KINAMAMA NA WATOTO WACHANGA

$
0
0
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

WANANCHI katika kijiji cha Maore wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro,wamesema tatizo la vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi pamoja na watoto wachanga vinachangiwa na upungufu wa watumishi katika zahanati ya kijiji pamoja na ufinyu wa wodi ya wazazi iliyopo.

Wakitoa maoni yao katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Taasisi ya Utepe mweupe (White Ribbon)  kujadili vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga katika kijiji cha Maore wilayani Same wananchi hao wameiomba serikali kuangalia namna ya kutatua changamoto hizo.

Mbali na changamoto hizo wakazi wa Maore wameeleza pia changamoto kubwa inayowakabili wanafunzi wa kike kupata ujauzito pindi wawapo shuleni kuna changiwa na wazazi kushindwa kuwaeleza ukweli  watoto wao kuhusu kuanza mahusiano wawapo shuleni .
Mratibu wa Mtandao wa Utepe Mweupe kitaifa  (The White Ribbon Alliance ) Rose Mlay akizungumza na wananchi katika kijiji cha Maore wilayani Same wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Taasisi ya Utepe mweupe (White Ribbon)  kujadili vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga .
Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Maore wilayani Same akifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokuwa yakiendelea kuhusu vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga .
Mganga Mkuu wa wilaya ya Same,Dkt Godfrey Andrew akizungumza wakati wa mkutano na wananchi ulioandaliwa na Mtandao wa Utepe Mweupe (White Ribbon) kujadili  vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga .

WAZIRI MBARAWA ATAKA BODI YA TPA KUFANYA MAAMUZI KWA WAKATI

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa wajumbe wa Bodi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA), na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Mhandisi Deusdedit Kakoko, kukamilisha Skana mpya (haipo pichani), ambayo inajengwa kwa ajili ya ukaguzi wa mizigo inayoingia Bandarini hapo ambayo haijakamilika hadi sasa.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amesema anasikitishwa na utendaji wa Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kutofanya maamuzi kwa wakati hali ambayo inachangia malalamiko kuongezeka Bandarini hapo. Aidha, Mbarawa amesema Serikali inapeleka Naibu Mtendaji Mkuu mpya wa shughuli za Uendeshaji Bandarini hapo kutokana na aliyekuwepo kushindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo.

Profesa Mbarawa amesema hayo leo wakati wa ziara ya kushtukiza aliyoifanya bandarini ikiwa ni siku chache baada ya Rais John Magufuli, na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kufanya ziara ya kustukiza na kubaini madudu bandarini hapo.   Ziara ya Waziri Mbarawa ni mwendelezo wa ziara mbalimbali bandarini hapo kubaini uendeshaji na utendaji wa shughuli zinazotolewa na Mamlaka hiyo.
Muonekano wa Skana mpya ambayo inajengwa kwa ajili ya ukaguzi wa mizigo inayoingia Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), ambayo haijakamilika hadi sasa.

“Nimelazimika leo kuwaita Watendaji na Bodi ya TPA ili kuwaeleza kasoro zenu ambapo inaonesha wazi kuwa asilimia kubwa ya mambo yanayotokea humu ni kuwa mnakuwa wazito katika kutoa maamuzi”, amesema Profesa Mbarawa.   Amesema katika bandari hiyo ipo mizigo ya kahawa ambayo imefika bandarini tangu mwaka 2014 huku kukiwa hakuna sababu za kueleweka za wenye mali kutochukuwa mizigo yao.  

Profesa Mbarawa amesema hahitaji wasaidizi ambao wanakaa katika vikao na kulipana posho ila wanapaswa kufanya kazi ya kuangalia shughuli zote za bandari.   “Kama hamtabadilika nitaendelea kuja katika bandari hii ili kuchukua hatua pale ambapo inaonekana kwani haipendezi kila kukicha malalamiko kutokea,” amesisitiza Waziri Mbarawa.  
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Profesa Ignatus Rubaratuka (Wakwanza kushoto), wakati akikagua shehena ya kahawa iliyohifadhiwa Bandarini hapo kwa muda mrefu.

Aidha, Waziri Mbarawa ameitka bodi na menejimenti kuhakikisha kuwa inatatua changamoto iliyopo katika bandari ya kushusha na kupakia mizigo kutoka Zanzibar na kuingia Tanzania Bara ambapo wafanyabiashara wanalalamikia utaratibu unaotumika kuwahudumia.   Amesema haingii akilini kuona mizigo inayotoka au kwenda Zanzibar kutozwa kodi baada ya masaa huku inayotoka nje ya Tanzania ikitozwa baada ya siku saba.   

Kuhusu ujio wa Naibu mtendaji Mkuu mpya Mbarawa aliitaka Bodi na menejimenti kumpa ushirikiano ili aweze kutoa matokeo chanya kwenye bandari.   “Tunaleta Naibu Mtendaji Mkuu mpya ambaye atasimamia operesheni, naomba apewe ushirikiano ili kusaidia Serikali huyu ambaye anakaimu tunamuondoa ameshindwa kwenda na kasi yetu,” amefafanua Profesa Mbarawa.  
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akikagua shehena ya kahawa iliyohifadhiwa tangu mwaka 2014 hadi sasa katika ghala iliyopo katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Dar es Salaam. Pembeni yake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka hiyo, Profesa Ignatus Rubaratuka akishuhudia ukaguzi huo.

Akizungumza baada ya ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya TPA Ignas Rugaratuka, amesema wamejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa wanaitendea haki nafasi waliyopewa kwa kusimamia mabadiliko ndani ya bandari.   Amesema tangu waingie wamekuwa wakipambana kuhakikisha kuwa mapungufu ya TPA yanaisha ambapo wamefanikiwa kurekebisha kwenye utawala kwa kutoa mafunzo kwa watumishi na kuzuia wizi ambao ulikuwa umekithiri.   

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko, amesema kuwa tangu aingie katika mamlaka hiyo wamekuwa wakifanya jitihada za kurekebisha mapungufu na kumuahidi waziri kuwa ataongeza jitihada zaidi.

  “Kama ni mabadiliko tumefanya makubwa sana hasa katika utawala na uongozi ila kila anayehusika katika sekta hiyo anapaswa kutoa msaada,” amesema Mkurugenzi Mkuu.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, alipofika Bandarini hapo leo wakati wa ziara ya kushtukiza kuangalia uendeshaji wa huduma Bandarini hapo.

Rais Magufuli amteua Bi Stelli Chagi kuwa Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba wa Wilaya

UTEUZI: RAIS DKT. MAGUFULI AMTEUA BI. STELLA CHAGI KUWA MSAJILI WA MABARAZA YA ARDHI NA NYUMBA WA WILAYA

WAZIRI MKUU, KASSIM MAJALIWA MGENI RASMI MAHAFALI YA 33 YA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda,  baada ya kuwasili kwenye Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania mjini Singida ambapo alikuwa mgeni rasmi, Novemba 30, 2017.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika mjini Singida Novemba 30, 2017. Kushoto ni Mkuu wa Chuo Kikuu hicho na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda.

 Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa (mwenye miwani mbele) akiwa na wahitimu wenzake katika Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika mjini Singida, Novemba 30, 2017.
 Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda akimtunuku Shahada ya Uzamili Katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera (Master Of Education in Administration, Planning and Policy Studies), Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa (kushoto) katika Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika mjini Singida, Novemba 30, 2017. Wapili kulia ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Watatu kulia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinoloji, Profesa Joyce Ndalichako. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akitelemka kutoka kwenye jukwaa baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamili Katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera (Master of Education in Administration, Planning and Policy Studies) na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Waziri Mkuu MStaafu, Mizengo Pinda (kulia)  huku  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishuhudia. 
 Mke wa  Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa   akipokea ua kutoka kwa mwanae, Saad Majaliwa Kassim baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamili katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera (Master of Education in Administraion, Planning and Policy Studies) katika Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika mjini Singida Novemba 30, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

KATIBU MKUU SIHABA NKINGA AFUNGUA BARAZA LA WAFANYAKAZI IDARA KUU MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO.

$
0
0
 Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika kikao kilichofanyika mjini Morogoro Novemba 30, 2017.
 Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala na Rasilimali Watu kutoka Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. James Kibamba(kulia) akiwasilisha mapendekezo ya marekebisho ya Muundo wa Utumishi wa Idara ya Ustawi wa Jamii uliopitiwa na kujadiliwa na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto lililofanyika mjini Morogoro Novemba 30, 2017.
 Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu kutoka Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Deodatha Makani (kushoto) akifafanua masuala ya Kiutawala kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Idara kuu ya Mendeleo ya Jamii, Jinisa, Wazee na Watoto lililofanyika mjini Morogoro Novemba 30, 2017.
 Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabikira Mushi (kulia) akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Idara kuu ya Mendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto lililofanyika mjini Morogoro Novemba 30, 2017.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi TV: SERIKALI YAWATAKA WATENDAJI BANDARINI KUWA NA MAAMUZI Michuzi TV


CHINA YAAHIDI KUFADHILI UJENZI WA RELI KWA KIWANGO CHA KIMATAIFA (SGR)

$
0
0
Benny Mwaipaja, Dar es Salaam.

BALOZI wa China hapa nchini, Wang Ke amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango na kuahidi kuwa nchi yake iko tayari kushawishi taasisi za fedha ikiwemo Benki ya EXIM ya nchini humo kushiriki ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa baada ya kufanyika kwa upembuzi yakinifu wa mradi huo.

Alisema kuwa kutokana na ukubwa wa mradi huo, unaokadiriwa utagharimu Dola za Marekani bilioni 7.6 hadi kukamilika kwake, utahitaji kufanyiwa upembuzi yakinifu ili kukidhi masharti ya kupata mkopo kupitia Benki ya Exim na taasisi nyingine zitakazotaka kujenga mradi huo muhimu. 

“Mradi huu ni muhimu na wa kihistoria kwa nchi hizi mbili, China ingependa kuona mradi huo unaboreshwa ili uweze kutoa huduma ya kusafirisha mizigo na abiria na kwamba kuimarika kwake kutaokoa miundombinu ya barabara kwa kuwa shehena kubwa ya mizigo itasafirishwa kupitia reli hiyo.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), wa pili kulia akieleza kuhusu fursa zilizopo katika Sekta ya Utalii wakati wa  Mkutano kati yake na Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke, (hayupo pichani), Jijini Dar es Salaam, kulia ni Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. John Rubuga.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), wa tatu kulia akiwa katika mkutano na  Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke (wa pili kushoto) ambapo walikubaliana kuendeleza ushirikiano katika Biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande hizo mbili, mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akieleza kuhusu kuwa na uwiano wa kibiashara kati ya Tanzania na China kwa manufaa ya pande hizo mbili wakati wa mkutano kati yake na Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke, (hayupo pichani), Jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa China hapa Nchini Bi. Wang Ke, (katikati) akiongoza maafisa wake wa ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini wakati wa mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), Jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

BBC SWAHILI: Tanzania yavuma kwa miundombinu Afrika Mashariki

MWAMUZI MTANZANIA KUCHEZESHA KOMBE LA DUNIA KWA WANAWAKE 2018 NCHINI URENO

$
0
0
Mtanzania Jonesia Rukyaa Kabakama ameteuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), kuchezesha fainali zijazo za Kombe la Dunia kwa wanawake (Algarve Cup) zitakazofanyika nchini Ureno, mwezi Februari, mwakani.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka TFF, Jonesia, ambaye ni mwanamke, ameteuliwa kupuliza filimbi katika fainali hizo ambazo hukutanisha timu mahiri zilizofanya vema katika michuano ya kila Bara.
Lakini kabla ya kwenda Ureno, Jonesia anatarajiwa kushiriki semina maalumu iliyoandaliwa na FIFA. Semina hiyo itafanyika Doha, Qatar kuanzia Februari 12- 16, mwakani.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limempongeza Mwamuzi Jonesia kwa kuteuliwa na FIFA kuchezesha fainali za Kombe la Dunia na kuhudhuria semina hiyo muhimu kwa maendeleo ya mpira wa miguu.
Waamuzi wengine walioteliwa kutoka Afrika Lidya Abebe wa Ethiopia, Glady Lengwe wa Zambia na Salima Mukansanga wa Rwanda.

WATEULIWA KUUNDA KAMATI NDOGONDOGO ZA MAANDALIZI YA AFCON U17/2019 YATAYOFANYIKA NCHINI

$
0
0
Ukiacha Kamati Kuu ya kuratibu michuano ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON U17/2019) kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limefanya uteuzi mwingine.

Uteuzi huo umeegemea zaidi kwa Wajumbe wa Kamati Kuu ya Maandalizi (LOC) wakiwamo viongozi wakuu wa TFF na wanafamilia wengine ambao kwa pamoja watafanya kazi ya kuandaa michuano hiyo itakayofanyika Tanzania mwaka 2019.

Wakati jina namba moja ni Mwenyekiti wa kila kamati ndogo wajumbe wengine katika kamati hizo ni kama ifuatavyo:

Miundombinu (Infrastructure)
  1. 1.Paul Makonda (Mwenyekiti)
  2. 2.Yusuph Singo
  3. 3.Sunday Kayuni
  4. 4.Leslie Liunda
  5. 5.Nassoro Idrissa
  6. 6.Mohamed Kiganja
  7. 7.Mhandisi Davis Shemangale

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MWANZA AKANUSHA TAARIFA ILIYOPO KATIKA GAZETI LA MWANANCHI LA TAREHE 30/11/2017.

$
0
0
LEO TAREHE 30.11.2017 KAMANDA WA POLISI MKOA WA MWANZA NAIBU KAMISHINA WA POLISI AHMED MSANGI (PICHANI), AMEKANUSHA TAARIFA ILIYOPO KATIKA GAZETI LA MWANANCHI LA TAREHE 30/11/2017, TOLEO NAMBA 6334, UKURASA WA TATU, INAYOSEMA KUWA AMETHIBITISHA JUU YA KUWEPO HEWA YA SUMU NDANI YA UKUMBI WA CITY MALL AMBAPO KULIKUWA KUKIFANYIKA MKUTANO MKUU WA UCHAGUZI WA VIJANA WA CCM (UVCCM) MKOA WA MWANZA.


AIDHA KAMANDA MSANGI ANASEMA, UKWELI NI KUWA ALIPIGIWA SIMU NA MWANDISHI WA GAZETI HILO TAREHE 29/11/2017 MAJIRA YA SAA 15:00 MCHANA ALIYETAKA KUTHIBITISHIWA TAARIFA YA KUWEPO HEWA YA SUMU NDANI YA UKUMBI WA CITY MALL  AMBAPO KULIKUWA KUKIFANYIKA MKUTANO TAJWA HAPO JUU. 


KAMANDA ALIMJIBU KUWA HANA TAARIFA NA HAWEZI KUTHIBITISHA KWANI HAJAPATA TAARIFA YEYOTE KUHISIANA NA YALIYOTOKEA KATIKA MKUTANO HUO, NA YEYE YUPO KWENYE KIKAO CHA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA OFISI YA MKUU WA MKOA.

PIA KAMANDA HAKUFIKA ENEO TAJWA KAMA TAARIFA HIYO  INAVYOSEMA, HIVYO INAONEKANA MWANDISHI WA TAARIFA HIYO ALIAMUA KUANDIKA MANENO HAYO KWA MANUFAA YAKE BINAFSI HIVYO JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINAOMBA GAZETI HUSIKA KUREKEBISHA. PIA ANAOMBA WAELEWE KUWA MATUKIO YA AINA KAMA HIYO YANAHITAJI YAWE NA MAJIBU YA KITAALAMU TOKA KWA WANASAYANSI PINDI YANAPOTOKEA. 

AIDHA JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINANAEDELE KUOMBA USHIRIKIANO TOKA KWA WAANDISHI WA HABARI KWA KUFANYA KAZI KWA PAMOJA ILI KUWEZA KUENDELEA KUDUMISHA USALAMA NA ULINZI KATIKA MKOA WETU. PIA JESHI LINAWAOMBA WAANDISHI WA HABARI KUFANYA KAZI KWA KUFUATA TAALUMA YA UANDISHI WA HABARI, UWELEDI NA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI ILI KUEPUSHA HABARI ZA AINA KAMA HII AMBAZO ZINALETA PICHA MBAYA KWA JESHI NA MKANGANYIKO KWA JAMII.

IMETOLEWA NA;
DCP: AHMED MSANGI
KAMANDA WA POLISI (M) MWANZA.

Mama wa mitindo Bi. Asya Idarous Khamsin Kutikisa Desemba 9 huko Oakland California Nchini Marekani.

$
0
0
 Mkongwe katika mitindo nchini Tanzania na Marekani maarufu kama Mama wa mitindo Bi. Asya Idarous Khamsin anatarajiwa kuonyesha mitindo yake mbalimbali ya ubunifu wa mavazi katika sherehe ya maalum  ya Watanzania itakayofanyika tarehe 9 Desemba,2017 huko Oakland California Nchini Marekani.

Kwa mujibu wa Mama wa Mitindo, Bi. Asya Idarous Khamsin ameweka wazi kuwa, onyesho hilo litakuwa la aina yake kwani watu watakaojitokeza watashuhudia mitindo mipya kabisa ya mavazi ambauyo itaonyesha kwenye jukwaa maalum siku hiyo sambamba na Chakula maalum cha kuchangia watu wenye tatizo la ugonjwa wa Kansa nchini Tanzania.
“9 Desemba,2017  tumewaandalia onyesho maalum la mavazi. Watu wajitokeze kwa wingi kushuhudia mavazi ya ubunifu. Pia kutakuwa na ‘fundraising dinner’  ya kukusanya fedha kwa ajili ya (partnering to tackle cancer to Tanzania) ambayo inafanyika kila mwaka.
Sherehe hizo ni pamoja na kusherehekea Shamla shamla za Uhuru wa (Tanganyika) ambayo sasa ni Tanzania” Alieleza Asya Idarous Khamsin.

BBC DIRA YA DUNIA ALHAMISI NOVEMBA 30, 2017


MAGAZETI YA IJUMAA LEO DECEMBER MOSI,2017

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU ARDHI (ARU) WAKABIDHIWA ZAWADI ZAO

$
0
0


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Profesa Evaristo Liwa akiwa amemkabidhi cheti cha shukrani mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho aliyefanya vizuri kwenye masomo yake, wakati wa hafla ya kuwakabidhi zawadi wahitimu waliofanya vizuri iliyofanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam Novemba 30 2017. Kushoto ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Profesa Gabriel Kassenga na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Robert Kiunsi. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs)

Sehemu ya wanafunzi wa chuo Ardhi University wakifuatilia matukio katika hafla ya kukabidhiwa vyeti na zawadi mbalimbali baada ya kufanya vizuri katika masomo kwa mwaka 2017 hafla iliyofanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam Novemba 30 2017.
Sehemu ya wanafunzi wa chuo Ardhi University wakifuatilia matukio katika hafla ya kukabidhiwa vyeti na zawadi mbalimbali baada ya kufanya vizuri katika masomo kwa mwaka 2017 hafla iliyofanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam Novemba 30 2017.
Sehemu ya wanafunzi wa chuo Ardhi University wakifuatilia matukio katika hafla ya kukabidhiwa vyeti na zawadi mbalimbali baada ya kufanya vizuri katika masomo kwa mwaka 2017 hafla iliyofanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam Novemba 30 2017.

SERIKALI HAIJARUHUSU KOZI ZA FOUNDATION CHUO KIKUU HURIA

$
0
0
SERIKALI haijatoa ruhusa kwa Chuo Kikuu Huria (OUT) kiendelee kutoa kozi ya ‘Foundation’ kama ambavyo imedaiwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii.

Baadhi ya mitandao ilitoa taarifa yenye kichwa cha habari kisemacho: Waziri Mkuu aruhusu kozi za 'Foundation' Chuo Kikuu Huria kwa madai kuwa alitoa ruhusa hiyo jana (Alhamisi, Novemba 30, 2017) wakati akiwa mkoani Singida ambako alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu hicho.

Akizungumza na mamia ya wakazi wa mji wa Singida waliohudhuria mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye viwanja vya Kanisa Katoliki mjini Singida, Waziri Mkuu alisema Serikali bado inafanyia maboresho Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014.

“Kwa sasa Serikali inafanya maboresho ya Sera ya Elimu na Mafunzo kwani sera tuliyonayo haifafanui vizuri jinsi ya kuwasaidia vijana wetu wajiendeleze kwa njia ya mfumo wa elimu huria na masafa,” alisema.

“Programu kama zilizoelezwa na Makamu Mkuu wa Chuo za Foundation, zinahitaji pia kufafanuliwa kwenye sera yetu, ambayo kwa sasa wataalamu wetu wanaendelea kuiboresha. Pindi itakapokamilika, tutaitolea taarifa kwa Chuo Kikuu Huria na wataalamu wataweza kushirikiana na sekta zote ili kuhakikisha jambo hili linakwenda vizuri,” alisema.

Mapema, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Prof. Elifas Tozo Bisanda alisema wamepokea barua kutoka kwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia ikiwaarifu juu ya nia ya Serikali kutaka kurejeshwa kwa kozi za Foundation katika chuo hicho.

“Tayari tumekwisha wasilisha mtaala wa Foundation ulioboreshwa ili kukidhi matakwa ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), na tunasubiri mrejesho kutoka Kamisheni baada ya kikao chao, mapema mwezi ujao,” alisema Prof. Bisanda.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
S. L. P. 980,
DODOMA.

IJUMAA, DESEMBA MOSI, 2017    

RC MAKONDA AJITOLEA KUFANIKISHA MATIBABU YA AHMED ALBAITY

Waziri Mpina Aagiza Mikataba Ya Wawekezaji Wa Vitalu Vya Ranchi Ya Taifa Vyenye Jumla Ya Hekta 68238 Kuvunjwa Mara Moja

$
0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina ameagiza Mtendaji Mkuu wa Ranchi za Mifugo za Taifa, Profesa Philemoni Wambura kuvunja mikataba ya wawekezaji wa vitalu vyenye jumla ya hekta 68,238 kwenye ranchi ya Mkata na Dakawa ndani ya mwezi mmoja baada kushindwa kuviendeleza vitalu vya ranchi na kushindwa kulipia kwa muda mrefu.Mpina ameyasema hayo jana wakati alipotembelea katika ranchi ya Mkata na Dakawa kwa lengo la kukagua shughuli mbalimbali zinazofanyika katika ranchi hizo.

Amezitaja kampuni za wawekezaji ambazo zilizomilikishwa vitalu zinatakiwa kuvunja mkataba kwa kushindwa kuendeleza upande wa ranchi ya Mkata katika Wilaya ya Kilosa kuwa ni pamoja na Kadolo Farm Company Ltd kitalu namba 418 yenye hekta 4005,Bagamoyo Farm kitalu namba 419 yenye hekta 3672.96, A to Z Animal Feeds Company Ltd kitalu namba 420 yenye hekta 3692.97 na Ereto Livestock Keepers kitalu namba 422 yenye hekta 4020.54.

Katika Wilaya ya Mvomero kampuni zilizoshindwa kuendeleza vitalu ni pamoja na kampuni ya Overland kitalu namba 415 yenye hekta19446.28, Katenda yenye hekta 2500, Mollel yenye hekta 2500 na Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa (Mtibwa Sugar) chenye hekta 20000 walizomilikishwa toka mwaka 1999 na kushindwa kukiendeleza na kukilipia kwa miaka 18.

Mpina amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kilosa kumaliza mara moja migogoro inayoendelea baina ya wakulima na wafugaji. Aidha Waziri Mpina amemtaka Diwani wa kata yaTwatwatwa, Katibu Tawala wa Halimashauri ya Wilaya ya Kilosa pamoja na jamii ya wafugaji kumaliza migogoro inayowasumbua kwa muda mrefu kwa njia ya mazungumzo kabla ya kukimbilia muhimili wa mahakama bila sababu yoyote.

Mpina amesema kama vyombo vya Serikali vingetumika vizuri kuanzia ngazi ya kijiji kungepunguza migogoro ya wakulima na wafugaji katika wilaya hiyo. Wilaya ya Kilosa ni miongoni mwa Wilaya zinaongoza kwa kuwa na migogoro mingi baina ya wakulima na wafugaji hapa nchini.

Kwa upande mwingine, Waziri Mpina amezitaka Halimashauri zote nchini kutotunga sheria kandamizi dhidi ya wafugaji. Akitolea mfano, wa sheria ndogo ya Halimashauri ya Mvomero ya kutoza faini ya shilingi 25, 000/=kwa kila mfugo kuingia katika Wilaya hiyo bila kufuata taratibu badala ya shilingi elfu kumi iliyoelekezwa katika Sheria ya Magonjwa ya Wanyama namba 17 ya Mwaka 2003.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT) Magembe Makoye amesema upatikanaji wa ardhi kwa ajili ya wafugaji kutasaidia kuondoa migogoro baina ya pande hizo na kuendelezwa kwa ranchi hizo za taifa kutawasaidia wafugaji kupata shamba darasa litakalo wasaidia kufuga kwa kisasa na kupata mbegu bora za mifugo.
Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina (mwenye Kofia) akiwa kwenye picha pamoja na Viongozi wa Wilaya ya Mvomero na Viongozi wa Chama cha Wafugaji Tanzania alipotembelea ranchi ya Dakawa jana.
Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina (mwenye Kofia) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Muhamed Utaly kulia akitoa maelezo ya kuhusu eneo la hekta 20000 zilizoshindwa kuendelezwa na mwekezaji Mtibwa Sugar kwa lengo la ufugaji. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo bwana Stan Rau hapo jana.
Meneja wa ranchi ya Mifugo ya Mkata, Iddi Sadalah akimuonyesha Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina (mwenye Kofia) banda la Mbuzi linalokadiriwa kuchukua mbuzi 800 kwa wakati mmoja katika ranchi ya Mkata jana.
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live




Latest Images