Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110113 articles
Browse latest View live

KIJANA ANAYEDAIWA KUUA MTU ASIYEJULIKANA AFIKISHWA MAHAKAMANI

$
0
0
Na Karama Kenyunko wa Blogu ya Jamii

Kijana wa miaka 22, anayeishi Ipililo Maswa mkoani Shinyanga leo Novemba 24, 2017 amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kumuua mtu asiyejulikana.
 Kwa mujibu wa chanzo cha Habari cha uhakika kijàna huyo ambaye alikamatiwa katika kituo cha mabasi cha Ubungo jijini Dar es Salaam na alikutwa akiwa na viungo vya binadamu ambavyo ni sehemu za mbalimbali za siri za mwanamke na nyara za serikali.
Mshtakiwa Nkonja amesomewa mashtaka yake mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha.
Wakili wa serikali Nassoro Katuga akisoma hati ya mashtaka amedai kati ya Oktoba Mosi na 30 mwaka huu katika eneo la Kahama Shinyanga na Kituo cha Mabasi cha Ubungo jijini Dar es Salaam, alimuua mtu ambaye bado hajafahamika.
Hata hivyo, mshtakiwa hakutakiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Decemba 8, mwaka huu. Upelelezi bado haujakamilika

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa akutana na Msajili wa UN-MICT

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy akizungumza na Msajili wa Mfumo wa Kimataifa wa kumalizia mashauri masalia ya iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ya Rwanda (MICT), Dkt. Olufemi Elias alipotembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Novemba 2017. 
Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Caroline Chipeta na Maafisa mambo ya nje wakifuatilia mazungumzo. 
Maafisa walioambatana na Msajili wa UN-MICT wakifuatilia mazungumzo. 

DR. NTUYABALIWE FOUNDATION YAKABIDHI CHUMBA CHA MAKTABA SHULE YA MSINGI MUUNGANO

$
0
0
Taasisi ya Dr Mtuyabaliwe imekabidhi Chumba cha maktaba, ilichokikarabati na kukisheheni vitabu, kwa shule ya Msingi Muungano iliyopo Manispaa Temeke, ambayo tangu kuanzishwa kwake miaka 30 iliyopita  haikuwahi kuwa na maktaba.

Akikabidhi Maktaba hiyo Mkurugenzi na Muasisi wa Taasisi ya Dr Ntuyabakiwe Jacquiline Mengi amesema Taasisi hiyo, iliyoanzishwa mwaka 2015 kumuenzi marehemu baba yake aliyekuwa mpenzi mkubwa wa kusoma vitabu, inahimiza usomaji wa vitabu kwa wanafunzi,ikiwa ni kuunga mkono  jitihada za serikali za kutoa elimu bora nchini:
Katika salaamu zao za shukrani Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa Bw. Bakari Makele, Mwalimu Mkuu Esther Matowo na Dada mkuu Veronika Mruma wameshukuru kwa msaada huo na kuahidi kuitunza na kuitumia ipasavyo.

Wakati wa hafla hiyo Mwakilishi Taasisi ya Sema-Tanzania Itanisa Mbise alikabidhi kwa Dada Mkuu wa shule Veronica Mruma nakala 100 za jarida linalochapishwa na Taasisi hiyo kwa matumizi ya maktaba hiyo.
Makabidhiano ya Makataba hiyo kwa shule ya Msingi Muungano yamefanyika wakati ambao Wizara ya elimu imeingiza somo la Maktaba katika mtaala wa elimu baada ya kuona umuhimu wake katika kufanikisha utoaji wa elimu katika shule za msingi.
Dr Ntuyabaliwe Foundation ni taasisi pekee binafsi nchini inayojihusisha na utoaji wa misaada ya vitabu vya maktaba kwa shule za msingi nchini, na hadi sasa imekwishatoa misaada kama huo kwa shule mbili za msingi za jiji la Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Jacqueline Mengi akisoma moja ya vitabu vya hadithi kwa baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Muungano waliowakilisha wenzao katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Jacqueline Mengi akikata utepe kuashiria uzikizundua rasmi eneo la kuhifadhia vitabu ndani ya maktaba hiyo.
Mkurugenzi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Jacqueline Mengi pamoja na walimu na wajumbe wa kamati ya shule wakikagua vitabu katika maktaba hiyo katika shule ya Msingi Muungano iliyopo Manispaa Temeke

Mwalimu Mkuu ya Msingi ya Muungano, Esther Matowo akisoma risala kwa mgeni rasmiwakati wa zoezi la uzinduzi wa maktaba shuleni hapo leo. wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Jacqueline Mengi na wapili kulia ni Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Temeke, Bakari Makele.

Mkurugenzi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Jacqueline Mengi akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi waliowakilisha wenzao. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AFANYA MKUTANO NA WAHARIRI ILI KUONGEZA UELEWA WA MIFUMO MIPYA KUHUSU UAGIZAJI WA MBOLEA KWA PAMOJA

$
0
0

Na Mathias Canal, Dar es salaam
Wanahabari kote nchini wametakiwa kutoa ushirikiano kwa Wizara ya Kilimo ili ifanikiwe katika jitihada zake za kuhakikisha kwamba Tanzania inafikia lengo la Azimio la Maputo la kumwezesha mkulima kufikia matumizi ya kilo 50 za virutubisho kwa hekta badala ya hali ya sasa ambapo anatumia kilo 19 tu au asilimia 38 ya lengo la Maputo.

Mwito huo umetolewa Leo Novemba 24, 2017 na Naibu waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa wakati akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini kwenye Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es salaam.

Mkutano huo ulikuwa na dhamira ya kujifunza na kuongeza uelewa kwa wahariri juu ya Mifumo mipya iliyoanzishwa na Serikali kuhusu Uagizaji wa Mbolea kwa Pamoja (Bulk Procurement System - BPS) na Usimamizi wa bei Elekezi ya Mbolea (Indicative Pricing Structure - IPS) kwa lengo la kumwezesha Mkulima kupata mbolea bora na kwa bei nafuu ili kuongeza matumizi ya mbolea yatakayo chochea, ongezeko la uzalishaji nchini ili kukidhi mahitaji ya familia na kuuza ziada ndani na nje ya nchi.
Mgeni Rasmi-Naibu waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini kwenye Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es salaam, Leo Novemba 24, 2017.
Mgeni Rasmi-Naibu waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini kwenye Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es salaam, Leo Novemba 24, 2017.
  Baadhi ya wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi-Naibu waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa wakati akizungumza kwenye Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es salaam, Leo Novemba 24, 2017.
  Baadhi ya wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi-Naibu waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa wakati akizungumza kwenye Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es salaam, Leo Novemba 24, 2017.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TUTAMALIZA KERO YA MAJI TUNDURU-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa miradi miwili ya maji katika vijiji viwili vya Rahaleo na Mbungulaji kwenye kata ya Kalulu yenye thamani ya sh. Milioni 112 na kuahidi kumaliza kero ya maji wilayani Tunduru.

Amesema Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, hivyo amewaomba wananchi kuendelea kuwa na imani na Serikali yao.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Novemba 24, 2017) mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa miradi ya maji katika vijiji hivyo kwa lengo la kumaliza changamoto ya umatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika maeneo hayo.

Amesema ujenzi wa miradi hiyo ni utekelezaji wa Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani yenye lengo la kuwafikishia wananchi huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

“Nataka maji haya yaende kwa wananchi si wananchi wayafuate, hivyo mara baada ya kukamilika ujenzi wa mradi huu Halmashauri ijenge mtandao wa mabomba yatakayosafirisha maji kutoka eneo la mradi hadi kwenye vioksi na kuyafikisha katika makazi ya wananchi.”

Pia ametoa wito kwa wazee wa vijiji hivyo kwa kushirikiana na vijana kuhakikisha wanalinda mradi huo kwa kutokata miti kwenye maeneo yote yanayozunguka vyanzo vya maji ili kuepusha ukame. Ameagiza ipandwe miti kwenye maeneo hayo ili kuhifadhi mazingira.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewataka watumishi wa umma kuhakikisha wanatekeleza ipasavyo majukumu yao ikiwa ni pamoja na kufanya kazi ya kuwatumikia wasnanchi bila ya ubaguzi wa dini, rangi na itikadi za vyama.

Amesema Serikali haitaki kusikia mwananchi anakwenda kufuata huduma katika ofisi zao na kuzungushwa kwa muda mrefu bila ya kuhudumiwa. “Serikali hii haitaki wananchi wake hususan wanyonge wasumbuliwe tukikubaini tunakuondoa.”

Waziri Mkuu ameongeza kwamba “Serikali hii haidekezi wala kuwaonea aibu watumishi wasiowajibika katika kuwatumikia wananchi. Serikali hii haitamuhifadhi mtu atakayeshindwa kufanya kazi, tunataka kazi tu na asiyefanya kazi na asile ndiyo maana tunawaondo watumishi wazembe wote.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, NOVEMBA 24, 2017.

RAIS DKT MAGUFULI KUHUDHURIA SHEREHE ZA KUAPISHWA MHE.UHURU KENYATTA WA KENYA.

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi vifo vya watu 12 wa ajali Singida

OSHA YAAGIZWA KUWEKA MIKAKATI MAHUSUSI YA KIUTENDAJI

$
0
0
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Eric Shitindi, ameuagiza Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kuweka mikakati mahususi ya kiutendaji itakayosaidia kuboresha mazingira ya biashara na kukuza ajira nchini. 

Mtendaji Mkuu huyo wa Wizara ametoa agizo hilo alipokuwa akiwahutubia watumishi wa OSHA katika kikao chao cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Shitindi alifafanua kwamba mikakati hiyo inapaswa kujikita katika kuimarisha mifumo ya kiutendaji itakayolenga katika kuboresha huduma zitolewazo kwa wateja na taasisi hiyo ya umma ili kuwaondolea usumbufu watu mbali mbali wanaofanya shughuli mbali mbali za kiuchumi hapa nchini.

“Wakati mwingine tunashindwa kujipanga vizuri katika utekelezaji wa kazi zetu na hivyo kuwasababishia usumbufu mkubwa wateja. Kwa mfano unakuta mkaguzi mmoja wa Usalama na Afya mahali pa kazi anapita katika eneo fulani la kazi asubuhi na mwingine anakuja katika eneo hilo hilo mchana wakati watu hawa wangeweza kufika katika eneo la kazi kwa pamoja na kukamilisha kazi zao za kaguzi kwa wakati mmoja,” alisema Shitindi.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Eric Shitindi, akiwahutubia watumishi wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) katika kikao chao cha baraza la wafanyakazi mjini Tanga kilichofanyika leo Ijumaa Novemba 24,2017.
Watumishi wa OSHA wakifuatilia hotuba ya Mgeni Rasmi, Eric Shitindi, wakati wa kikao chao cha baraza la wafanyakazi kinachofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Watumishi wa OSHA wakifuatilia hotuba ya Mgeni Rasmi, Eric Shitindi, wakati wa kikao chao cha baraza la wafanyakazi kinachofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Eric Shitindi, akiwa katika picha ya pamoja na menejimenti ya OSHA nje ya ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga. Mtendaji Mkuu huyo wa Wizara alikuwa Mgeni Rasmi katika kikao cha baraza la wafanyakazi wa Wakala huo.


MAVUNDE AWANEEMESHA WAJASIRIAMALI DODOMA

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Dodoma mjini Anthony Mavunde leo amekabidhi mashine mbalimbali kwa wajasiriamali wa vikundi 31 na kuwataka kuhakikisha wanazitumia kwa kujiongezea kipato na kuenda sambamba na azma ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa Viwanda.

Akizungumza na wanavikundi hao na wakazi wa Dodoma, Mavunde amesema mashine hizo zimenunuliwa kupitia fedha za mfuko wa jimbo na kwamba dhamira yake ni kuhakikisha wananchi wanajikwamua kiuchumi kwa kubadili maisha yao.

“Leo Tumegawa mashine hizi mkazitumie zibadilishe maisha yenu msizifungie stoo zikajaa vumbi na msipozitumia kwa malengo yaliyokusudiwa hamuwezi kufikia malengo yenu,Mashine hizi zikaunge mkono falsafa ya Rais ya uanzishaji wa viwanda ili kufikia uchumi wa viwanda,”amesema Mavunde

Hata hivyo amewahakikisha kuwa amejipanga kuhakikisha anawakwamua wananchi wake kiuchumi kupitia fursa mbalimbali na kwamba anakuja na mradi wa kuchimba mabwawa ya kufugia samaki.

“Kuna teknolojia imekuja ya kufuga samaki ambayo unaweza kufuga nyumbani, hiyo ndo mipango ya ofisi ya Mbunge ya kuwawezesha wananchi kiuchumi na pia kwa upande wa kilimo nimetafuta wataalamu kutoka India tunaangalia eneo la Nzasa kulitumia kwa majaribio ya kilimo cha mboga mboga na ufugaji samaki,”amesema
Mbunge wa jimbo la Dodoma mjini Anthony Mavunde akiwa na viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani katika hafla ya kukabidhi mashine mbalimbali kwa vikundi vya wajasiriamali.
Mbunge wa jimbo la Dodoma mjini Anthony Mavunde akikabidhi mashine kwa wajasiriamali.
Mashine zilizokabidhiwa kwa vikundi vya wajasiriamali


Waziri wa Afya Aupongeza Mfuko wa Abbott

$
0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeupongeza mfuko wa Abbott kutokana na juhudi kubwa za kusaidia kuboresha huduma ya afya katika sekta ya afya nchini.

Kauli hiyo imetolewa Leo na Waziri wa wizara hiyo, Ummy Mwalimu kabla ya kukabidhi kadi za bima ya afya kwa watoto 139 wanaoishi katika mazingira magumu.Mfuko huo kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na benki ya ABC, leo wamekabidhi kadi kwa watoto hao kupitia Waziri Ummy Mwalimu.

“Napenda kuupongeza Mfuko wa Abbott kwa kuwezesha watoto hawa 139 kupata kadi za bima ya afya, hongereni sana. Nimeambiwa Kadi hizi mmezilipia na zitaisha baada ya mwaka mmoja, hivyo naomba muendelee kuzilipa endapo haitawezekana Serikali italipa, lakini naamini kwamba hamtashindwa kuendelea kuiunga mkono Serikali,” alisema Waziri Ummy Mwalimu.

Baada ya Waziri huyo kutoa kauli hiyo, Mkurugenzi wa Miradi endelevu wa Mfuko wa Abbott, Dkt. Festo Kayandabila alisema kuwa wako tayari kuwasaidia watoto hao.Mfuko wa Abbott umekuwa ukiisaidia Hospitali ya Taifa Muhimbili katika juhudi zake za kuboresha huduma za afya. Mfuko huo umesaidia kukarabati Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali pamoja na kukarabati Jengo la maabara kuu.
Mkurugenzi wa Miradi Endelevu wa Mfuko wa Abbott, Dkt. Festo Kayandabila akieleza jinsi mfuko wa Abbott ulivyoshiriki kuwapatia watoto wanaoishi katika mazingira magumu kadi za bima ya afya. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati wa benki ya ABC, Joyce Malai na Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Kurasini, Rabikira Mushi.

Wizara kuongeza wigo wa matumizi ya kiswahili Afrika Mashariki

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba leo akiongea na Wanachama wa Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki (CHAKAMA) amesema Wizara inaendelea na jitihada za kuhimiza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika Nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo hadi sasa tayari baadhi ya nchi wanachama zimeshaweka lugha ya Kiswahili katika mitaala ya Elimu katika shule za Msingi na Sekondari hatua ambayo itawezesha kuongeza wigo wa matumizi ya lugha hii katika Jumuiya yetu.

Mhe. Dkt Kolimba akizungumza katika kongamano hilo amewapongeza Viongozi na Wanachama wa Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki kwa kuwahusisha baadhi ya Ofisi za Balozi zilipo nchini katika hatua za kufanikisha Kongamono hilo. Kwa namna ya pekee alitumia fursa hiyo kumpongeza Balozi wa Kuwait nchini Mhe.Jaseem Al Najem na Watumishi wa Ubalozi huo kwa kukubamwaliko wa kushiriki Kongamano na kwa mchango waliotoa kufanikisha Kongamano hilo.

Tokea mwaka 2004 hadi sasa Kiswahili kimekuwa lugha ya kwanza ya Afrika kutumika katika vikao vya Ngazi ya Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika, hii ni kufuatia jitihada na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Jitihada hizo ilikuwa ni pamoja na kugharamia wakalimani kwa fedha za ndani, na mwaka 2008 Wizara iliishawishi Kamisheni ya Umoja wa Afrika kuchukua jukumu hilo.

Aidha Mhe. Dkt. Kolimba amewahakikishia Viongozi na Wanachama wa CHAKAMA kuwa nia ya Serikali ya kufungua vituo vya kufundishia lugha ya kiswahili sehemu mbalimbali nje ya mipaka ya Tanzania bado iko palepale, "tayari tulishafungua kituo kimoja mwaka 2012 katika Ofisi za Kamisheni ya Umoja wa Afrika huko Addis Ababa, Ethiopia" amesema Mhe. Dkt. Kolimba.

CHAKAMA imehitimisha Kongamano lake leo lililofanyika kwa muda wa siku mbili mjini Dodoma ,likiwa na kauli mbiu ya "Kiswahili na Maendeleo ya Afrika Mashariki" chama hiki kinaundwa na nchi Wanchama za Jumuiya ya Afrika pia kinahusisha wanachama kutoka nchi mbalimbali za Afrika zikiwemo Ghana na Zimbabwe.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba akihutubia washiriki wa kongamano la Chama cha Kiswahili Afrika Mashariki lililofanyika katika Hoteli ya African Dream mjini Dodoma 
Naibu Waziri Mhe.Dkt. Susan Kolimba akimkabithi cheti cha ushiriki mmoja wa wajumbe wa Kongamo la CHAKAMA 
Naibu Waziri Mhe.Dkt. Kolimba akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kongamano 

WATOTO 139 WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU WAKABIDHIWA KADI ZA BIMA YA AFYA MUHIMBILI

$
0
0
Serikali ameipa siku 60 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kuandaa mpango utakaowawezesha wateja wa hiari kulipia fedha kidogo kidogo kwa ajili ya kupata kadi ya bima ya afya.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu kabla ya kukabidhi kadi za bima ya afya kwa watoto 139 wanaoishi katika mazingira magumu. Kazi hizo zimetolewa na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na Mfuko wa Abbott na Benki ABC.

Waziri Ummy Mwalimu ameuagiza mfuko wa NHIF kuhakikisha ndani ya siku 60 inaweka utaratibu ambao utasaidia wateja wa hiari wanapata kadi za bima ya afya ndani ya muda mfupi kwa kuwa wengi wao hawana fedha taslimu Sh 50,400 za kulipia kwa wakati mmoja.

“Natoa siku 60 kwa NHIF kuhakikisha inaweka utaratibu wa kuwawezesha watu kupata kadi ya bima ya afya kwa kulipa fedha kidogo, kidogo kwa mfano mteja wa hiari anaweza kulipia Sh 5,000 au Sh 10,000 hadi atakapokuwa amefikisha Sh50,400 ambayo inatakiwa na NHIF,” alisema waziri huyo.
Waziri wa Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu akimkabidhi kadi ya bima ya afya, Irene Paul kwa niaba ya watoto wenzanke 139 ambao wanaishi katika mazingira magumu. Kadi hizo zimetolewa na Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kushirikiana na mfuko wa Abbott na benki ya ABC. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati wa benki ya ABC, Joyce Malai, Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Kurasini, Rabikira Mushi na Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Miradi Endelevu wa Mfuko wa Abbott, Dkt. Festo Kayandabila na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali wa hospitali hiyo, Dkt. Juma Mfinanga.
Baadhi ya walezi wa watoto wanaoishi katika mazingira magumu wakishuhudia jinsi watoto hao wanavyokabidhiwa kadi za bima ya afya leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo.
Waziri wa Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu akizungumza kabla ya kukabidhi kadi za bima ya afya kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu.
Baadhi ya watoto waliokabidhiwa kadi za bima ya afya na Waziri wa Afya wakionyesha kadi hizo kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Muhimbili leo.

Upasuaji wa Kihistoria Kupandikiza Figo Wafanyika Muhimbili

$
0
0

Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na Hospitali ya BLK ya New Delhi, India imefanikiwa kufanya upasuaji wa kihistoria wa kupandikiza figo (Renal Transplant) ikiwa ni mara ya kwanza nchini.

Upandikizaji wa figo umefanywa na madaktari bingwa wa Mhimbili na Hospitali ya BLK Novemba 21, mwaka huu na taarifa za wataalamu hao zimeeleza upasuaji huo umekuwa wa mafanikio makubwa na kwamba utakuwa endelevu.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema kufanyika kwa upasuaji huo ni moja ya mkakati wa Serikali wa kuendelea kuboresha na kuanzisha huduma bora za kibingwa nchini.

“Serikali inaendelea na juhudi za kuboresha huduma za afya nchini chini ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli zikiwamo za kibingwa nchini na kupunguza rufaa za wagonjwa wanaohitaji huduma hizo nje ya nchi,” amesema Ummy Mwalimu.

Amesema upasuaji figo katika Hospitali ya Muhimbili utasaidia kupunguza gharama kubwa ambazo serikali imekuwa ikitumia kupeleka wagonjwa nje ya nchi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari kuhusu upasuaji wa kihistoria wa kupandikiza figo ambao umefanyika Novemba 21, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ikiwa ni mara ya kwanza upasuaji huo kufanyika nchini. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo Profesa Lawrence Museru, Dkt. Rajesh Pande, Dkt Sunil na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya figo Muhimbili, Dkt. Jacqueline Shoo wakiwa kwenye mkutano huo leo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru akizungumza kwenye mkutano huo. Kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Dkt. Rajesh Pande na Dkt Sunil wakifuatilia mkutano huo.

Wataalamu wa figo wa Muhimbili ambao wameshiriki katika upasuaji huo wa kihistoria wakiwa kwenye mkutano huo leo.

ZIARA YA WANAMKIKITA NCHINI THAILAND

$
0
0
 Wajumbe kutoka Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita/Living Green) wakiwa na furaha baada ya kulakiwa na wenyeji wao walipowasili hivi karibuni  katika Jiji la Bangkok, Thailand tayari kwa ziara ya utalii wa kilimo cha kisasa na ufugaji pamoja na fursa la biashara.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita, Adam Ngamange (kushoto) na  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mtandao huo, Dk. Kissui S. Kissui wakiwawsili kwenye uwanja wa ndege jijini Bangkoko, Thailand
 Wakiwa na wenyeji wao

Bondia Ibrahimu Class wa Tanzania na Bondia Koo’s Sebiya wa Afrika ya Kusini Wapima Uzito Tayari kwa Pambano

$
0
0
Bondia Ibrahimu Class wa Tanzania (kulia) akimkabidhi kitabu kinachoonyesha vivutio tulivyonavyo Tanzania bondia Koo’s Sebiya wa Afrika ya Kusini (kushoto) baada ya kupima uzito tayari kwa kushiriki katika pambano la kimataifa la ngumi litakalofanyika kesho katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam
Mabondia Ibrahim Maukola (kushoto) na Ibrahim Tamba (kulia) wakionyesha uwezo wao baada ya kupima uzito kwa ajili ya kuonyesha pambano la ngumi kati yao kabla ya pambano la kimataifa kati ya Bondia Ibrahimu Class wa Tanzania na Bondia Koo’s Sebiya wa Afrika ya Kusini litakalofanyika kesho katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Idara ya Michezo Bw. Yusuph Singo (kulia) akizungumza wakati wa kuwapima uzita mabodia Ibrahimu Class wa Tanzania na Koo’s Sebiya wa Afrika ya Kusini wanaotarajia kupambana kesho katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam


RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI MGENI RASMI MAADHIMISHO MIAKA 56 YA UHURU

WAHITIMU IFM WAASWA KUJIEPUSHA NA RUSHWA NA UFISADI

$
0
0

Benny Mwaipaja, Dar es Salaam

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amewaonya wahitimu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM kuacha tamaa ya kutaka kupata mali za haraka haraka na kutojihusisha na vitendo vya rushwa na ufisadi wawapo kazini ili waweze kuisadia nchi kufikia maendeleo ya haraka.

Dokta Mpango aliyasema hayo wakati akiwatunuku vyeti vya kozi mbalimbali wahitimu 2692 wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM, wakati wa mahafali ya 43 ya Chuo hicho yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.

Alisema kuwa moja ya changamoto zinazoikabili jamii hivi sasa ni mmomonyoko wa maadili katika utumishi wa Umma hali iliyosababishwa na suala la rushwa na ufisadi kuota mizizi na kuwa tatizo kubwa katika jamii.

“Katika miaka ya karibuni kumekuwa na matatizo mengi ya matumizi mabaya ya fedha za umma ikiwemo watumishi hewa, wanafunzi hewa na pembejeo hewa, nawataka wahitimu mkafanyekazi zenu kwa kuzingatia maadili na kuepuka tabia ya kutaka utajiri wa harakaharaka” Alisisitiza Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango alitumia fursa hiyo pia kuelezea mafanikio makubwa yaliofikiwa nchini katika sekta ya fedha katika kukuza uchumi na kupunguza umasikini kwa kuimarisha upatikanaji wa huduma, mikopo ya mitaji ya kuwekeza katika Sekta mbalimbali na kuhakikisha kuwa sekta hiyo inabaki imara.
Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha-IFM, waliofanya vizuri zaidi katika masomo yao wakipokea zawadi ya hundi kifani yenye thamani ya shilingi 1,200,000 ambayo ni sehemu ya zawadi lukuki walizopewa wakati wa Mahafali ya 43 ya Chuo hicho, yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini Dar es Salaam.
Mhitimu Bi. Elizabeth Mnzava akipokea zawadi ya cheti kutoka kwa Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 43 ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) baada ya kufanya vizuri katika masomo yake.
Meza Kuu wakiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa pili kushoto) wakiimba Wimbo wa Taifa wakati wa Mahafali ya 43 ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha- IFM, yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini Dar es Salaam ambapo wanafunzi 2692 wamehitimu kozi mbalimbali katika Nyanja za Fedha, Uhasibu, Bima, TEHAMA na Hifadhi ya Jamii. Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho Prof. Lettice Rutashobya na wa Pili kulia ni Mkuu wa Chuo hicho Prof. Tadeo Satta.

Wanachama wa Shirikisho la waganga wa Tiba Asili Tanzania (SHIVYATIATA)wawajia juu viongozi wao

$
0
0
Na David John

BAADHI ya wanachama wa Shirikisho la waganga wa Tiba Asili Tanzania (SHIVYATIATA) wamewajia juu viongozi wa Shirikisho huku wakihoji uhalali wao wa kuendelea kufanya kazi.

Wamesema kuwa viongozi hao muda wao wa kuongoza ulishapita na wanachama walishatoa msimamo wa kuwataka kujiudhuru ili kupisha kufanyika kwa uchaguzi mwaka kesho.

Akizungumza kwa niaba ya wezake mmoja wa wanachama hao Rajabu Hassan amesema wamepata taarifa kwamba kuna baadhi ya viongozi wa shirikisho hilo wamekwenda mjini Dodoma kusimamia uchaguzi wa shirikisho vyama kwa ngazi ya mkoa kinyume cha taratibu.

Amesema maamuzi ya Halmashauri kuu ya shirikisho hilo ilikuwa kuwa chaguzi zote ambazo zitafanyika ngazi za wilaya na mikoa zisimamiwe na wajumbe wa halmashauri kuu na si viongozi wakuu na hiyo nikutokana wao walipewa kuendesha shirikisho kwa muda ambapo muda wao umekwisha kimsingi.
Hassan Rajabu mmoja mwanachama wa shirikisho la vyama vya waganga wa tiba asili Tanzani.

Kanzi Data Ya Kuhifadhi Taarifa Za Wadau Wa Tasnia Ya Filamu Kuleta Maslahi Katika Tasnia

$
0
0

Na: Genofeva Matemu – WHUSM

Wadau wa tasnia ya filamu nchini wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiunga katika vyama vilivyopo chini ya Shirikisho la filamu ili waweze kuingia katika mpango wa Kanzi Data inayolenga kuhifadhi taarifa za wasanii na kuinua maslahi ya tasnia kupitia tuzo na mashindano mbalimbali yatakayoandaliwa.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe wakati wa kusaini mkataba wa kanzi data itakayohifadhi taarifa za wasanii wa filamu kati ya Kampuni ya Cogsnet na Shirikisho la Filamu leo Jijini Dar es Salaam.

“Ni wajibu wetu kuhamasisha wadau wa tasnia ya filamu kuingia katika mfumo wa kanzi data kwani mpango huu umedhamiria kuboresha na kuendeleza maslahi ya tasnia ya filamu na kuleta maendeleo ya msanii mmoja mmoja” amesema Mhe. Mwakyembe

Awali Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo amesema kuwa tasnia ya filamu imekua ikikosa fursa nyingi kutokana na wadau kutokua katika kanzi data inayowatambua vizuri hivyo ujio wa kanzi data hii utakua mkombozi kwa tasnia.
Rais wa Shirikisho la Filamu Bw. Simon Mwakifwamba (wapili kushoto waliokaa) pamoja na mwanasheria wa kampuni ya Cogsnet Bw. Thomas Herman (katikati waliokaa) wakisaini mkataba wa kutengeneza Kanzi Data itakayohifadhi taarifa za wanatasnia ya filamu kati ya kampuni ya Cogsnet na Shirikisho la Filamu leo Jijini Dar es Salaam. Waliosimama katikati ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe
Rais wa Shirikisho la Filamu Bw. Simon Mwakifwamba (kulia) akikabidhiana mkataba na mwanasheria wa kampuni ya Cogsnet Bw. Thomas Herman (kushoto) baada ya kusaini mkataba wa kutengeneza Kanzi Data itakayohifadhi taarifa za wanatasnia ya filamu kati ya kampuni ya Cogsnet na Shirikisho la Filamu leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe (waliokaa katikati) katika picha ya pamoja na wadau wa tasnia ya filamu baada ya kusaini mkataba wa kutengeneza Kanzi Data itakayohifadhi taarifa za wanatasnia ya filamu kati ya kampuni ya Cogsnet na Shirikisho la Filamu leo Jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo.Picha na: Genofeva Matemu – WHUSM


KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA IJUMAA

Viewing all 110113 articles
Browse latest View live




Latest Images