Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

TPB Bank Plc, Multichoice kuwapatia Watanzania DStv kwa Mkopo

$
0
0
 BENKI ya TPB imeingia kwenye makubaliano rasmi na kampuni ya Multichoice Tanzania inayotoa huduma za DStv ambapo wafanyakazi umma, wateja na hata wale wasio wateja sasa wanaweza kupata ving’amuzi vya DStv kwa mkopo na kisha kulipia kidogo kidogo.

Hafla hiyo ya kusaini makubaliano imefanyika leo jijini Dar es Salaam, ambapo Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya TPB Sabasaba Moshingi pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande wamesaini hazi za makubaliano. 

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi alisema kwa sasa Watanzania wanaotaka kumiliki ving’amuzi vya DStv, wataweza kupata mkopo maalum kutoka TPB utakaowawezesha kufungiwa huduma za DStv na kisha kulipa kwa awamu kwa kati ya miezi mitatu hadi mwaka mmoja.

Alisema kuwa benki yake siku zote imekuwa ikijitahidi kubuni huduma mbalimbali kwa ajili ya kuwawezesha Watanzania wengi zaidi kupata huduma muhimu na pia katika kuboresha hali zao kiuchumi na kijamii. 
 Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya TPB Sabasaba Moshingi (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande (kushoto) wakibadilishana nyaraka za makubaliano mara baada ya kusaini.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya TPB Sabasaba Moshingi (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande (kushoto) wakisaini makubaliano ya ushirikiano, ambapo kwa sasa wafanyakazi umma, wateja na hata wale wasio wateja wanaweza kupata ving’amuzi vya DStv kwa mkopo na kisha kulipia kidogo kidogo. Nyuma yao ni mashahidi kutoka pambe zote mbili.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

IGP SIRRO AFUNGA MKUTANO WA URRA SACCOS MKOANI MOROGORO

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro pamoja na Viongozi wengine wa Chama cha kuweka na kukopa cha Jeshi la Polisi (URA SACCOS) wakiimba wimbo wa maadili ya ofisa wa Polisi wakati wa hafla fupi ya kufunga Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama hicho uliokuwa ukifanyika mkoani Morogoro ambapo aliwataka Viongozi hao kuhakikisha kuwa Mikopo inawafikia walengwa kwa wakati ili waweze kuboresha maisha yao.(Picha na Jeshi la Polisi)
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha kuweka na kukopa cha Jeshi la Polisi (URA SACCOS) wakimsikiliza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro( hayupo pichani) wakati wa ufungaji wa mkutano huo uliokuwa ukifanyika mkoani Morogoro ambapo aliwataka Viongozi hao kuhakikisha kuwa Mikopo inawafikia walengwa kwa wakati ili waweze kuboresha maisha yao.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro pamoja na Viongozi wengine wa Chama cha kuweka na kukopa cha Jeshi la Polisi (URA SACCOS) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa SACCOS hiyo wakati wa hafla fupi ya kufunga mkutano huo uliokuwa ukifanyika mkoani Morogoro.(Picha na Jeshi la Polisi)

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA VIONGOZI WA KUU WA OFISI YA MAKAMU WA RAIS.

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Joseph K. Malongo na Naibu Katibu Mkuu Bi. Butamo K. Philip ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba (wa pili kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Joseph K. Malongo(kulia) na Naibu Katibu Mkuu Bi. Butamo K. Philip  (kushoto) ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Rais Magufuli akutana na Rais Shein na Balozi wa Japan Ikulu Jijini Dar es Salaam

$
0
0


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Japan nchini Mhe. Masaharu Yoshida alipokutana na na kufanya mazungumzo naye Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 22, 2017. PICHA NA IKULU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein walipokutana na kufanya mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 22, 2017

NAIBU WAZIRI WA UJENZI KWANDIKWA ARIDHISHWA NA HUDUMA ZA VIVUKO JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

NAIBU Waziri wa Ujenzi Elias Kwandikwa amefanya ziara katika kivuko cha Kigamboni na kujionea namna mashine mpya za kieletroniki zilivyoweza kufungwa na kumtaka  mhandisi aanze kuzifanyia majaribio kabla ya mwaka huu kuisha ili Januari 2018 zianze kutumika.

Akizungumza baada ya kumaliza ziara yake na kujionea namna wafanyakazi wanavyotoa huduma kwa abiria wanaofika kwa ajili ya usafiri kwa kivuko kutoka Kigamboni na Kivukoni, Naibu Waziri Kwandikwa amesema kuwa amefurahishwa na huduma zinazotolewa na zaidi amezungumza na baadhi ya wananchi na wote wameonekana kufurahishwa. 

" Nimezungumza sehemu mbalimbali na kujionea namna watoa huduma wanavyotoa huduma zao kwa abiria na pia nimezungumza na takribani wananchi kumi wanaotumia usafiri wa kivuko na wote wameonekena kufurahishwa na huduma zenu ,"alisema Naibu Waziri Kwandikwa.


Naibu Waziri wa Ujenzi Elias Kwandikwa akizungumza na mhudumu wa kukata tiketi katika kituo  cha Kivukoni wakati alipofanya ziara kuangalia namna abiria wanavyopata huduma zao, juu akikata tiketi ya kuingia ndani.
 Naibu Waziri wa Ujenzi Elias Kwandikwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza ziara yake katika kivuko cha Kivukoni na Kigamboni na kujionea uendeshaji wa huduma bora kwa abiria kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TAMESA).
Naibu Waziri wa Ujenzi Elias Kwandikwa akizungumza na Mhandisi wa kivuko Ally Daudi na akipewa maelezo ya maendeleo ya vivuko vyote vilivyopo chini ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TAMESA).
Naibu Waziri wa Ujenzi Elias Kwandikwa akikagua mashine za kieletroniki za tiketi zilizofungwa katika Kivuko cha Kigamboni na Kivukoni wakati wa ziara yake iliyofanyika leo Jijini Dar es salaam.

NENO ZITO LA PATROBAS KATAMBI WA BAVICHA (CHADEMA) KWA WATANZANIA

LAWRENCE MASHA - MWANA MPOTEVU NIMERUDI NYUMBANI

ALBERTO MSANDO - HII NDIO CCM NILIYOITAKA


Prof. KITILA MKUMBO ATOA WOSIA MZITO KWA UPINZANI WA TANZANIA

TAMBWE KAMILI GADO, YANGA KUENDELEA KUWAKOSA TSHISHIMBI, NGOMA NA KAMOSOKU

$
0
0

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KIKOSI cha Yanga kimeendelea na mazoezi yake leo katika Uwanja wa Uhuru kujiandaa na mchezo wa raundi ya 11 ya ligi kuu Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons ya Jijini Mbeya.

Mchezo huo unatarajiwa kufanyika kwenye Uwanja wa Chamazi kutokana na mabadiliko yaliyofanya na bodi ya ligi baada ya Uwanja wa Uhuru kuwa na shughuli za kijamii.

Katika mazoezi hayo, mshambuliaji Mrundi, Amissi Joselyn Tambwe aliyekosekana uwanjani kwa kipindi kirefu toka kuanza kwa ligi msimu huu leo amejumuika na wenzake na kufanya mazoezi kikamilifu kwa mara ya kwanza pamoja na wenzake ikiwa ni baada ya muda mrefu.

Kurejea kwa Tambwe katika mazoezi ya pamoja chini ya Kocha George Lwandamina  kuna uwezekano  kwenye mchezo wa wiki hii akajumuishwa kwenye mchezo dhidi ya TZ Prisons siku ya Jumamosi.

Kocha wa Yanga, Mzambia George ‘ Lwandamina amesema kwamba kati ya majeruhi wake wanne, wengine ni Tambwe pekee amefanya mazoezi ukiachilia  kiungo Thabani Kamusoko na mshambuliaji, Donald Ngoma nna kiungo Papy Kabamba "Tshishimbi" ambapo alikosa mchezo wa wiki iliyopita dhidi ya Mbeya City.


MICHUZI TV: DC GONDWE AAMURU KUKAMATWA WALIOKULA MILIONI 12 ZA MRADI WA TREKTA

DK.MAHENGE: HALMASHAURI ZIHAKIKISHE ASILIMIA 10 YA FEDHA ZA VIJANA, WANAWAKE NA WALEMAVU ZINATUMIKA KUTEKELEZA MKAKATI WA SERIKALI YA VIWANDA.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amezitaka Halmashauri za Wilaya, Mji na Manispaa Mkoani Dodoma kuhakikisha zinatenga asilimia kumi (10%) ya makusanyo yao ya ndani kwa ajili ya vijana, wanawake na Walemavu kuanzisha miradi ya viwanda vidogo na vya kati.

Lengo ni kuitikia kampeni ya Serikali inayoitaka Mikoa kuanzisha viwanda kama ilivyozinduliwa hivi karibuni na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mheshimiwa Seleman Jafo.

Akizungumzia hilo, ameonya tabia ya baadhi ya Halmashauri kutotoa asilimia kumi (10%) ya makusanyo yake ya ndani au kutoa kiasi kidogo kwa ajili ya vijana, wanawake na walemavu na kuwa utaratibu unaotumika sasa wa Halmashauri kukopesha fedha hizo wakati mwingine sio muafaka sana badala yake Halmashauri zitumie fedha hizo kuwafungulia vijana, wanawake na walemavu viwanda vidogovidogo na kuwakabidhi waendeleze uzalishaji na kuviendesha.

CHUO KIKUU ARDHI MARUFUKU KUKODI MAKAMPUNI-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekipiga marufuku Chuo Kikuu Ardhi kukodi makampuni ya kufanya kazi mbalimbali kwa niaba yake.

Amesema kitendo hicho kinaharibu kazi na sifa ya chuo hicho kwa kuwa baadhi ya makampuni wanayoyapa kazi hayakidhi vigezo.Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Novemba 23, 2017) kwenye ufunguzi wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Chuo Kikuu Ardhi.

“Kama kuna umuhimu wa kufanya kazi na kampuni ni bora muanzishe kampuni ya kwenu itakayofanya kazi vizuri ili kujiepusha na matatizo.”Pia Waziri Mkuu amekiagiza chuo hicho kufanya tafiti zenye kuleta majibu ya maswali na changamoto mbalimbali zinazolikabili Taifa na Dunia.

Ametaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni mabadiliko ya tabia nchi, ujenzi holela, uharibifu wa mazingira na majanga ya asili kama mafuriko.Amesema Serikali inaamini kuwa matokeo ya kazi zinazofanywa na chuo hicho zikiwemo tafiti ni chachu ya maendeleo ya taasisi za elimu ya juu.

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kifo cha Mzee Kleist Sykes

MATUMIZI YASIYO YA LAZIMA YADHIBITIWE

$
0
0
Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo  amewataka watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima kwenye Halmashauri ili kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Waziri Jafo ameyasema hayo wakati wa Ufunguzi wa kongamano la siku mbili la Chama cha Wahasibu Tanzania(TAA) lililojumuisha wataalam wa Hesabu na wafanya maamuzi kutoka katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Katika Kongamano hilo ambalo Linafanyika kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa Chama hicho mwaka 1983 limelenga kujenga uwezo kuhusu Uwazi na Uwajibikaji kwa Viongozi waandamizi wa Mamlaka ta Serikali za Mitaa katika Matumizi ya Fedha za Umma.

Waziri Jafo amesema kuwa Bajeti kubwa ya Serikali inapelekwa kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa takribani asilimia 20.7 ya Bajeti ya Serikali huelekezwa katoka Halmashauri hivyo ni eneo ambalo linapata  Fedha nyingi na zinahitajo uangalizi mkubwa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selamani Jafo akifungua kongamano ya Chama cha Wahasibu Tanzania  linalohusu uwazi na uwajibikaji kwa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa linalofanyika Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu Tanzania Fred Msemwa akitoa neno la utangulizi wakati wa ufunguzi wa Kongamano linalohusu uwazi na uwajibikaji kwa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Washiriki na wajumbe wa chama cha Wahasibu Tanzania wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya Ufunguzi wa Kongamano lililofunguliwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za MItaa Mhe.Selemani Jafo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe.Selemani Jafo(kulia) akizungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu Tanzania Fred Msemwa wakati wa Ufunguzi wa Kongamano linalofanyika Mjini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe.Selemani Jafo(Katikati mbele) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chama cha wahasaibu Tanzania pamoja na wawwezeshaji wa Kongamano hilo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

NAIBU WAZIRI ULEGA AFANYA ZIARA KATIKA KISIWA CHA MAFIA

$
0
0
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amefanya ziara katika Kisiwa cha Mafia kwa ajili kukagua shughuli za uvuvi pamoja na kumuona Samaki aina Papa Potwe.

Akizungumza na Wavuvi , Watendaji wa Kisiwa hicho, Ulega amesema kuwa sekta ya Uvuvi inatakiwa ilete maendeleo ikiwa rasilimali hizo zitatumika ipasavyo.Ulega ameiagiza  Halmashauri ya Mafia ndani ya siku saba kuhakikisha wavuvi wapate barafu kwa kuuziwa bei ya chini ili kuweza kupata mapato.

Amesema kuwa wananchi wa Mafia hawaelewi maana ya Hifadhi ambapo wanatakiwa kupewa elimu ili kuondokana na mgogoro wa hifadhi.
Ulega amesema Halmashauri  inashindwa kupata mapato ya kujiendesha kutokana  na kutokuwa wabunifu juu ya kutengeneza mapato ikiwa pamoja  kuwasumbua wananchi kwa vitu visivyo na mapato.

Aidha amesema kuwa Rais Dk. John Pombe Magufuli amefuta ushuru kwa wafanyabiashara wanaochukua biashara kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Amesema kuwa hakuna sheria ndogo inayozidi sheria Mama juu ya Halmashauri Mafia kutunga sheria ndogo ya kuchukua ushuru wa mazao ya bahari yanayotoka wilaya moja kwenda nyingine wakati sheria hiyo ilishafutwa.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akiwa katika boti kuelekea katika kisiwa cha Mafia ikiwa ni ziara ya kuangalia shughuli za maendeleo ya Uvuvi katika kisiwa hicho ambacho kinategemea kipato chake kwa ajili ya mazao ya baharini .
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza na wavuvi pamoja na watendaji wa Halmashauri ya Mafia juu ya usimamizi wa shughuli za uvuvi ambazo zinafanyika katika kisiwa cha Mafia
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akikagua kiwanda cha uchakataji samaki kilichopo Mafia ambacho ni kiwanda cha uchakataji samaki kwa ajili ya usafirishaji .
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akipokea ripoti kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Shaib Ahmed Nnunduma (kulia) jinsi shughuli za Uvuvi zinazofanyika katika Kisiwa hicho .
 Watalii wakimuangalia samaki aina ya Papa Potwe ambaye anapatikana Tanzania kwa miezi mitano wakati sehemu nyingine anakaa miezi miwili.picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii Mafia

UFUNGAJI WA MAFUNZO YA UDHIBITI USAMBAAJI MAFUTA BAHARINI WAFANYIKA ZANZIBAR.

$
0
0
 Injinia Mratibu wa maswala ya Mazingira Baharini kutoka ZMA Halfani Hamad Hassan kulia akitoa maelezo kuhusiana na zoezi la vitendo la Udhibiti wa Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini katika Mkutano wa kufunga mafunzo hayo uliofanyika Hoteli ya Marumaru Forodhani mjini Unguja.
 Mkuu wa Kituo cha Huduma za Dharura Norwey Helge Munkas Andersen kushoto akionesha namna ya zoezi zima la mafunzo ya  Udhibiti  Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini katika Mkutano wa kufunga mafunzo hayo uliofanyika Hoteli ya Marumaru Forodhani mjini Unguja.
 Mkuu wa Kituo cha Huduma za Dharura Norwey Helge Munkas Andersen akijibu baadhi ya maswala yalioulizwa katika Mkutano wa  Ufungaji  mafunzo ya  Udhibiti  Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini  uliofanyika Hoteli ya Marumaru Forodhi mjini Unguja.
 Naibu Katibu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji,  Shomari O,Shomari akitoa hotuba ya ufunguaji wa  mafunzo ya  Udhibiti  Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini yaliochukua muda wa siku Tatu hafla iliofanyika  Hoteli ya Marumaru Forodhani mjini Unguja.
Naibu Katibu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Shomari O,Shomari (kulia) akimkabidhi cheti cha Ushiriki wa mafunzo ya Udhibiti  Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini Injinia Mratibu wa maswala ya Mazingira Baharini kutoka ZMA Halfani Hamad Hassan katika ufungaji wa mafunzo hayo katika Hoteli ya Marumaru Forodhani mjini Unguja.

PICHA NA YUSSUF SIAMI/MAELEZO ZANZIBAR.

Bondia Mtanzania kutetea ubingwa wa GBC dhidi ya bondia wa Afrika Kusini

$
0
0
 Bondia Mtanzania Ibrahim Class Mgendera, anatarajia kutetea ubingwa anaoushikilia wa mkanda wa dunia wa Baraza la Ngumi Duniani (Global Boxing Council – GBC) uzito wa “Lightweight dhidi ya bondia kutoka nchini Afrika Kusini

Pambano hilo la kimataifa la ngumi za kulipwa ambalo limedhaminiwa na kampuni ya simu ya Vodacom PLC pamoja na kampuni ya Azam, litafanyika jijini Dar es Salaam Novemba 25 2017 kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Mgendera anashikilia ubingwa wa mkanda wa dunia wa Baraza la Ngumi Duniani (Global Boxing Council – GBC) uzito wa “Lightweight”ambao alioutwaa nchini Ujerumani tarehe 1 Julai, 2017 kwa kumpiga Jose Forero wa Panama. Bondia huyo atakuwa ni kibarua kigumu cha kutetea taji hilo mbelea ya KOOS SIPHO SIBIYA kutoka AFRIKA YA KUSINI

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi,Yusuph Singo alisema maandalizi ya pambano hili yalianza siku tarehe 5 August siku ya hafla ya kumpongeza bingwa huyo ambapo mgeni  alikuwa ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Harrison Mwakyembe ambapo Uongozi wa  bondia hiyo ilimwelezea Waziri mwenye dhamana na michezo kwamba, mkanda huo unapaswa kutetewa katika kipindi cha miezi mitatu tangu alipoupata na tayari kulikuwa na ofa mezani za kuutetea mkanda huo kutoka katika nchi za Marekani, Ujerumani na Ufilipino.
 Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC, Matina Nkurlu (kushoto)akiongea na Waandishi wa habari (hawapo pichani)  katika ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam,  wakati  wa kuwatambulisha  Bondia Mtanzania Ibrahim  Mgendera(Katikati) anayetarajia kutetea ubingwa wake wa mkanda wa dunia wa Baraza la Ngumi Duniani (Global Boxing Council – GBC) uzito wa “Lightweight dhidi ya bondia kutoka Afrika ya Kusini KOOS SIPHO SIBIYA(hayupo pichani)  Pambano hilo la kimataifa la ngumi za kulipwa  limedhaminiwa na Vodacom Tanzania na Azam TV na  litafanyika  jumamosi  kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam,Kulia ni Mkuzaji wa Vipaji  vya ngumi Tanzania, Joe Anea.
 ondia Mtanzania,Ibrahim Mgendera(Kushoto)atakaye utetea ubingwa wake wa mkanda wa dunia wa Baraza la Ngumi Duniani (Global Boxing Council – GBC) uzito wa “Lightweight” (kushoto) na bondia kutoka nchini Afrika Kusini,KOOS SIPHO SIBIYA wakitambulishwa na Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC,Matina Nkurlu kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa mkutano na vyombo vya habari  uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, pambano hilo  la kimataifa la ngumi za kulipwa limedhaminiwa na Vodacom Tanzania,Azam TV litafanyika siku ya jumamosi katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kushoto)akishuhudia mabondia Ibrahim Mgendera kutoka Tanzania na kocha wake (wapili kushoto)na bondia kutoka nchini Afrika Kusini,KOOS SIPHO SIBIYA na kocha wake(wapili kulia)wakitambulishwa kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa mkutano na waandishi hao uliofanyika Habari Maelezo jijini Dar es Salaam,  pambano hilo  la kimataifa la ngumi za kulipwa limedhaminiwa na Vodacom Tanzania PLC, AzamTV litafanyika siku ya jumamosi katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam,Katikati ni mwamuzi wa mpambano huo wa Kimataifa  kutoka nchini Ujerumani, Arno Pokrandt.

RC GEITA AUNGA MKONO JITIHADA ZA UJENZI WA SHULE NA ZAHANATI KATA YA LUTEDE NA KAKUBILO WILAYANI GEITA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameunga mkono jitihada za ujenzi wa Zahanati na Shule kata za Ludete na Kakubilo Halmashauri ya Geita kwa kuchangia matofali yenye thamani ya shilingi 2,400,000/= na kufanikisha harambee ya mifuko ya Saruji zaidi ya 420.

Mhandisi Robert Gabriel ameunga mkono jitihada za wananchi  baada ya kutembelea kata hizo na kuridhishwa na kazi za ujenzi wa Zahanati za vijiji na Shule zinazofanywa na wananchi kwa kujitolea kufanya kazi bila malipo, kuchangia vifaa mbalimbali vya ujenzi na kuchimba misingi.

Akiwa Kata ya Ludete Mkuu wa Mkoa amesema " Nimefurahi sana kuona namna mnavyoshiriki katika utekelezaji wa miradi hii niwaombe mshiriki kuanzia mwanzo hadi mwisho na msikubali mtu yeyote kuwavunja moyo kwa kuwa maendeleo ya Ludete yataletwa na wananchi wenyewe hivyo mimi ninawachangia matofali 1000 kwa ajili ya Zahanati na mengine 1000 ya kujenga vyumba vya madarasa shule ya Sekondari Ludete".

Mheshimiwa Herman Kapufi Mkuu wa Wilaya ya Geita akitoa maelekezo kwa viongozi wa Halmashauri ya Geita na kata ya kakubilo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel katika Halmashauri hiyo kuhamasisha ujenzi wa Zahanati na vyumba vya madarasa.
 Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akishirikiana na wananchi wa Kata ya Ludete Wilayani Geita kumwaga zege kwa ajili ya lenta kwenye ujenzi wa madarasa 10 ya shule ya msingi Ludete yenye wanafunzi 6,616  alipokwenda kuzindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.

 Mhandisi Robert Gabriel akishirikiana na mafundi kupandisha ndoo yenye zege kwa ajili ya uwagaji wa leta katika majengo 10 ya vyumba vya madarasa shule ya Msingi Ludete Wilayani Geita.

 Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa Geita akikabidhi fedha shilingi 2,400,000/= kwa Diwani wa Kata ya Ludete Sebastian Mranda kwa ajili ya ujenzi wa boma la Zahanati ya Kijiji na Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari katika hiyo.
 Wananchi wa kijiji cha Ludete Kata ya Ludete Wilayani Geita wakishiriki katika uchimbaji wa msingi kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati katika kijiji hicho kwa lengo la kuunga mkono jitihada za mkuu wa mkoa wa Geita za kila kijiji kuwa na Zahanati.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

BANK OF AFRICA-TANZANIA CELEBRATES 19th ANNIVERSARY IN STYLE

$
0
0
The guest of honor; Honorable Charles Mwijage, Minister of Industries, Trade and Investment giving out the speech at the Bank’s 10 years’ anniversary event, yesterday at Serena Hotel.
CEO and Managing Director of BANK OF AFRICA- TANZANIA, Mr. Ammishaddai Owusu-Amoah giving out his very exciting and energetic speech during the 10 years’ corporate anniversary event, which took place yesterday at Serena Hotel.
Deputy Managing Director of BANK OF AFRICA –TANZANIA, Mr. Wasia Mushi giving out his opening remarks and introducing the entire BANK OF AFRICA team present at the 10 years’ corporate anniversary event, which took place yesterday at Serena Hotel.
CEO and Managing Director of BANK OF AFRICA- TANZANIA, Mr. Ammishaddai Owusu-Amoah hands over a copy of his speech to the guest of honor; Honorable Charles Mwijage, Minister of Industries, Trade and Investment.
The guest of honor; Honorable Charles Mwijage, Minister of Industries, Trade and Investment together with Board Chairperson of BANK OF AFRICA-TANZANIA, Ambassador Mwanaidi S. Maajar and CEO and Managing Director of BANK OF AFRICA- TANZANIA, Mr. Ammishaddai Owusu-Amoah; in group photo with a section of esteemed clients of the Bank who attended the corporate 10 years anniversary dinner gala.

Viewing all 110000 articles
Browse latest View live




Latest Images