Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110117 articles
Browse latest View live

PROF KITILA MKUMBO ATANGAZA KUJIUNGA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)


WAZIRI MKUU AKUTANA NA MABALOZI WA TANZANIA KATIKA NCHI ZA MISRI NA ZAMBIA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi wa Tanzania nchini Misri, Balozi Meja Jenerali Issa Suleiman Nassoro na Balozi Abdulrahman Kaniki wa Zambia, ambapo amewataka wakaimarishe mahusiano baina ya nchi zote mbili.

Amekutana na Mabalozi hao Balozi leo (Alhamisi, Novemba 16, 2017) katika Ofisi ya Waziri Mkuu iliyopo Barabara ya Reli na Mahakama mijini Dodoma na kuwasisitiza wakaboreshe shughuli za Kidiplomasia kati ya Tanzania na nchi za Misri na Zambia.

Pia Waziri Mkuu amewataka Mabalozi hao wakahakikishe wanatangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini, ukiwemo mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama, fukwe pamoja na fursa za uwekezaji zilizopo nchini hususan katika sekta ya viwanda.

Amesema licha ya kutangaza fursa za uwekezaji na vivutio vya utalii pamoja na kuboresha biashara baina ya Tanzania na nchi za Misri na Zambia pia wakawashawishi wawekezaji waje wawekeze katika sekta mbalimbali nchini ikiwemo ya viwanda.

Waziri Mkuu amesema Tanzania ni nchi salama yenye amani na utulivu wa kisiasa, pia Serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji jambo ambalo litawawezesha wawekezaji watakaokuja kuwekeza nchini kupata tija.

Pia Waziri Mkuu amewataka Mabalozi hao wahakikishe wanakwenda kutafuta masoko ya bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini.Hata hivyo, Waziri Mkuu amewataka Mabalozi hao kwenda kukutana na kufanya mazungumzo na Watanzania waishio kwenye nchi hizo na kuwasisitiza waishi kwa kuzingatia sheria za nchi husika. Pia wawaunganishe pamoja na kuwashauri waje kuwekeza nchini.

Kwa upande wao Mabalozi hao wamesema watahakikisha wanayafanyia kazi maelekezo yote waliyopewa na Waziri Mkuu ikiwa ni pamoja na kwenda kutafuta wawekezaji ili wawe kuwekeza katika sekta ya viwanda na kuboresha ushirikiano baina ya Tanzania na nchi hizo. 


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
S. L. P. 980,
DODOMA.

ALHAMISI, NOVEMBA 16, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi Meja Jenerali Issa Suleiman Nassoro wa Misri  (katikati) na Balozi Abdulrahman Kaniki wa Zambia Ofisini kwake mjini Dodoma Novemba 16, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi Meja Jenerali Issa Suleiman Nassoro wa Misri  (katikati) na Balozi Abdulrahman Kaniki wa Zambia Ofisini kwake mjini Dodoma Novemba 16, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Michoro ya watoto kutoka Tanzania wazawadiwa Finland.

$
0
0
Michoro mitatu iliyochorwa  na watoto kutoka Tanzania hivi karibuni ilitunukiwa tuzo ya heshima ya vyeti vya stashahada ya maonesho na Taasisi ya Sanaa za watoto na vijana ya Hyvinkää, Finland.

Bryton Manyewa(10), Neev  Mistry (9) wa shule ya Academic International Primary na Mandela Mtaya (5) wa shule ya chekechea ya Upendo Montessori ndiyo waliofanikiwa kupata tuzo hiyo kwa upande wa Tanzania baada ya  kushiriki shindano la michoro liloitwa 'Pamoja' lililotayarishwa na taasisi hiyo ya nchini Finland.

Zaidi ya michoro 6800 toka katika nchi 66 duniani zilishiriki shindano hilo ambapo majaji ambao walikuwa ni wachoraji magwiji a sanaa wa nchi hiyo walichagua michoro 670 kushiriki katika maonesho yaliyoanza Oktoba mwaka huu na yatamalizika 18 Januari 2018 kwenye ukumbi wa Taasisi hiyo inayojihusisha na elimu ya Sanaa kwa watoto na vijana ukuzaji wa muingiliano wa utamaduni wa nchi mbalimbali. 

Maonesho hayo yanaweza pia kutazamwa katika mfumo wa Kidijitali kupitia tovuti ya Taasisi hiyo www.artcentre.fi

Katika miaka ya nyuma, kwa ufadhili wa ubalozi wa Finland nchini, baadhi ya watoto kutoka Tanzania waliweza kuhudhuria mafunzo ya Sanaa yanayotolewa na taasisi hiyo
 

Kwa mara ya kwanza upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) wafanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

$
0
0
16/11/2017 Jumla ya wagonjwa 20 wamefanyiwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa upasuaji wa aina hiyo kufanyika hapa nchini.

Akiongea na Waandishi wa Habari leo jijini Dar Salaam Daktari bingwa wa magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge alisema upasuaji huo unafanyika katika kambi ya matibabu ya Moyo inayofanywa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na madakatari kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saudi Arabia.

Dkt. Kisenge alisema kuwa kambi hiyo inaenda sambamba na utoaji wa elimu na kubadilishana ujuzi wa kazi kati ya wafanyakazi wa Taasisi hizo mbili ikiwemo aina mpya ya upasuaji wanaoufanya kitu ambacho kinawajengea uwezo zaidi. ”

“Faida ya upasuaji huu ni kumwezesha mgonjwa kutoka chumba cha upasuaji akiwa anatembea na baada ya masaa manne kama hali yake inaendelea vizuri anaweza kuruhusiwa.“Tofauti na upasuaji wa kutumia mshipa wa paja ambao tulikuwa tunaufanya, baada ya upasuaji mgonjwa ni lazima akae Hospitali kwa zaidi ya masaa 24 ili kuangalia maendeleo ya afya yake”, alisema Dkt. Kisenge.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya IIRO Ali Al Masoud alisema kambi hiyo inaendelea vizuri kwani kwa siku wanatibu wagonjwa 10 na baada ya matibabu afya zao zinaimarika tofauti na ilivyokuwa kabla ya matibabu.Dkt. Masoud aliongeza kuwa wamekuja na utaalam mpya wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono ambapo kabla ya hapo matibabu yaliyokuwa yanafanyika ni ya kutumia mshipa wa damu wa kwenye paja.

Alifafanua, “Hivi sasa tunafanya upasuaji wa Moyo wa bila kufungua kifua kitu ambacho wenzetu hawa walikuwa wanakifanya. Sisi tumewaongeza utaalam mpya wa kutumia mshipa ya mkononi badala ya mshipa wa paja.

Naye Bader Alanezi ambaye ni Mtaalamu wa magonjwa ya Moyo na mishipa ya damu kutoka IIRO alimalizia kwa kusema kuwa wamepata muda wa kujifunza vitu vingi na kupata uzoefu mpya wa baadhi ya magonjwa na mambo ya kiteknolojia ambayo katika nchi yao hakuna.

Jumla ya wagonjwa 40 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ya siku tano ambayo imeanza tarehe 14 hadi tarehe 18 mwezi huu.

Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saud Arabia wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab katika kambi ya matibabu ya moyo inayoendelea kwenye Taasisi hiyo. Jumla ya wagonjwa 40 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ya siku tano.


Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge na mwenzake wa Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saud Arabia Ali Al Masoud wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab katika kambi ya matibabu ya moyo inayoendelea kwenye Taasisi hiyo. Jumla ya wagonjwa 40 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ya siku tano.

Zoezi la kumfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab likiendelea. Picha na JKCI

CHUO KIKUU MZUMBE WAMUENZI BABA WA TAIFA HAYATI MWL. JULIUS KAMBARAGE NYERERE KWA KONGAMANO

ZIMAMOTO MBEYA WAFAIDI MAFUNZO YA KUJAZA NA KUTUMIA MITUNGI YA HEWA SAFI (SCABA) TOKA UJERUMANI

SERIKALI YAELEZA VIGEZO VITAKAVYOTUMIKA KUCHAGUA MAENEO YATAKAYOTUMIKA KUENDESHA AFCON U17 2019

RC GEITA - AUAGIZA UONGOZI WA HALMASHAURI YA MJI GEITA KUPELEKA WAKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI KATA YA MGUSU WILAYANI GEITA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Modest Apolinary kupeleka Wakaguzi wa ndani wa Hesabu za Serikali Kata ya Mgusu ili wakakague na kujiridhisha na mapato na matumizi ya fedha mbalimbali katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Mgusu na Mtaa wa Machinjioni Wilayani Geita.

Mheshimiwa Robert amesema hayo wakati wa ziara yake Halmashauri ya Mji Geita yenye lengo la kuzindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na Zahanati ambapo baada ya uzinduzi kufanyika wananchi wa mtaa wa machinjioni walimueleza kero ya kutopata taarifa ya mapato na matumizi ya michango wanayochangia kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa muda mrefu katika mtaa na kata ya Mgusu.

Akijibu kero hiyo Mkuu wa Mkoa amesema "Kama kuna kiongozi wa mtaa au Kata amekula fedha za wananchi hafai kuwa kiongozi serikali itamchukulia hatua kali za kisheria na atarejesha fedha hizo!, Mkurugenzi leta timu ya ukaguzi wa hesabu za Serikali ili ikague na kujiridhisha kama kuna fedha yoyote iliyochukuliwa pasipo maelezo yanayojitosheleza hatua zichukuliwe haraka kwa wote watakaobainika kuhusika". 

 Mheshimiwa Robert ameongeza kuwa ukaguzi huo ufanyike kuanzia mwaka 2014 hadi 2017 kisha apate taarifa hiyo ofisini. Akiwa katika Halmashauri hiyo Mkuu wa Mkoa amepongeza jitihada zinazofanywa na wananchi za kushiriki katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo licha ya kuwepo changamoto nyingi katika maeneo yao.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akizungumza na wananfunzi wa Shule ya Msingi Shinamwendwa (Halmashauri ya Mji Geita) alipokwenda kushiriki kuchmba msingi wa ujenzi wa nyumba pacha ya Walimu shuleni hapo.
Akina mama wa mtaa wa Machinjioni Kata ya Mgusu Halmashauri ya Mji Geita wakishiriki katika ujenzi wa jengo la utawala kwa kubeba maji kupeleka eneo la mradi.Wananchi wwameamua kujenga Shule ya Sekondari kwa kuwa Kata hiyo haina hata shule moja hivyo watoto wanaofaulu ulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya elimu ya Sekondari katika Kata za jirani.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akishiriki kujenga msingi wa vyumba vya madarasa shule ya Sekondari Mgusu baada ya kuzindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na Zahanati Halmashauri ya Mji Geita.Kata ya Mgusu inakabiliwa na changamoto ya kutokuwa na Shule ya Sekondari. 
Mhandisi Modest Apolinary Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita kitoa ufafanuzi kuhusu ramani ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mgusu kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita Robert Gabriel kulia ni Herman Kapufi Mkuu wa Wilaya ya Geita. 


TUME YA KUREKEBISHA SHERIA YATEMBELEA MAKAZI YA WAZEE YA NYABANGE NA KITUO CHA KULELEA WATOTO CHA JIPE MOYO MKOANI MARA

$
0
0
Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa akiongea na Wazee katika Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nyabange yaliyopo Butiama mkoani Mara wakati wa Tume ilipotembelea makazi hayo ikiwa ni sehemu ya Utafiti wa Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania.
Sehemu ya wazee katika Makazi ya Wazee wasiojiweza ya Nyabange yaliyopo Butiama mkoani Mara wakimsikiliza katibu Msaidzi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa.
Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa akimkabidhi zawadi ya Sabuni Mkuu wa Makazi ya Wazee wasiojiweza ya Nyabange iliyopo Butiama mkoani Mara Bw. Edward Mbaga wakati Tume ikifanya Utafiti mkoani humo. Kushoto ni Mhadhiri Msaidizi Chuo cha Ustawi wa Jamii Bw. Paulo Mwangosi

MAGAZETI YA IJUMAA LEO NOVEMBA 17,2017

Huu ndiyo Mrejesho kuhusu Missafricausa 2017.

$
0
0
Hadi wanaingia ukumbini kura zilikuwa:-

D.R.Congo: 8683
Cape Verde: 3248
Tanzania: 2268

Baada ya wawakilishi wa nchi 15 za Africa kushindanishwa haya ndio matokeo :-

Cameroon
Nigeria
Tanzania

Mwakilishi wa Tanzania Lylian Muttakyawa, ametoka na tuzo ya mshindi wa 3 na kubwa zaidi kawa Miss Congeniality.Tunashukuru mno mno, Watanzania kwa support yenu ya kura.
Tafadhali sambaza shukrani hizi.
Mungu awabariki. 




 

WANAODURUFU KAZI ZA SANAA KUFIKISHWA MAHAKAMANI.

$
0
0

 Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart imethibitisha kuwa Watuhumiwa wote waliokwamatwa kushiriki kufanya biashara ya kazi feki za sanaa watafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Msama Auction Mart, Alex Msama amesema kuwa Watuhumiwa hao watapelekwa Mahakamani kutokana na kuwa na kesi ya kujibu.

Ameendelea kusema ni kosa kuuza Kazi za Wasanii hao ambazo hazina Stika ya TRA, kwani zinawakosesha Mapato Wasanii hao na Serikali kwa ujumla.

Amesema wataendelea na zoezi hilo kwa kupita maeneo yote kuhakikisha wanadhibiti uuzwaji wa kazi hizo feki.Kwa jana zoezi letu liliendelea maeneo ya Mbande, Mbagala, Buza Tandika na Chanika", amesema Msama.

Amesisitiza kuwa kazi za nje na ndani lazima ziwe na Stika ya TRA, pia amesema ni marufuku kuweka nyimbo za Wasanii, Kuburn CD na kuweka kwenye Flash.
Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart inashirikiana na Jeshi la Polisi kwa ajili ya usalama, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuendelea na kuikamisha shughuli hiyo,ambayo pia inatarajiwa kufanyika katika mikoa mbalimbali.
  Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart ya jijini Dar es salaam,Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari katika kituo kikuu cha Kanda Maalum Dar es salaam jana kabla ya kuanza kwa zoezi la kukamata wauzaji wa CD Feki katika maeneo mbalimbali ya ikiwemo eneo hatarishi kwa bishara hiyo la Kariakoo .
Baadhi ya watuhumiwa wakipandishwa kwenye gari na vifaa vyao.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart ya jijini Dar es salaam,Alex Msama akikagua baadhi ya CD kwenye moja ya duka.
Mmoja wa watuhumiwa akichukuliwa na na Askari baada ya kugundulika akiuza katika duka lake.
"Mfano huyu mmiliki wa duka hili, Leseni yake imeisha tangu 2014 mpaka leo na hajui taratibu zozote za kupata leseni mpya wala TIN number,bado anaendelea na biashara yake,kinyume cha sheria",alisema Alex Msama.

ZOEZI LA KUANDIKISHA WANANCHI KUPATA VITAMBULISHO VYA TAIFA LINAENDELEA KATIKA MIKOA YA MANYARA NA SINGIDA

$
0
0

Mkuu wa Kitengo cha Biashara Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa,Thomas William, akizungumza na kipindi cha Hello Tanzania cha Uhuru FM,kuhusu zoezi la uandikishaji wananchi kwaajili ya vitambulisho vya Taifa katika Mikoa ya Manyara na Singida.
Ndugu Thomas atazungumzia zoezi hilo linavyoendelea katika mikoa mingine siku ya jumatatu tarehe 20-11-2017 katika kipindi Hello Tanzania cha Uhuru FM saa 02:00 kamili Asubuhi.

JK AWATAKA WASANII WA BONGO MOVIE KUJIONGEZA NA KUACHA KULALAMIKIA SERIKALI

$
0
0
 Rais Mstaaafu wa Awamu ya Nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Televisheni  inayoshughulika na masuala ya filamu za Kitanzania kwa Wasanii wa Bongo Movie JTV, ambayo itapatikana kupitia king'amuzi cha Star Times ambapo amewataka wasanii hao kujiongeza ili wafanye kazi kama wasanii kutoka nchi za Magharibi.
 Waziri wa habari Sanaa Utamaduni na Michezo Dk Harisson Mwakyembe akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dk Jakaya Kikwete katika uzinduzi wa Televisheni ya Jtv  itakayooneshwa kwenye king'amuzi cha Star Times
 Mkurugenzi wa Jtv, Jason Msimbe akizungumza wakati wa hafla ya kumkaribisha  Rais Mstaaafu wa Awamu ya Nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete, kwenye uzinduzi wa televisheni yake
 Baadhi ya Wasanii walioshiriki katika uzinduzi wa Tlevisheni mpya ya Jtv ambayo itakuwa inaonesha filamu za kitanzania kupitia King'amuzi cha Star Times
 Rais Mstaaafu wa Awamu ya Nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete, akiteta jambo naWaziri wa habari Sanaa Utamaduni na Michezo Dk Harisson Mwakyembe na Mkurugenzi wa JTv Jason Msimbe
Rais Mstaaafu wa Awamu ya Nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wasanii wa Bongo Movie walioshiriki uzinduzi wa Televisheni ya Jtv

TAASISI YA DORIS MOLLEL YAZINDUA FILAMU YA MTOTO "NJITI" JIJINI DAR

$
0
0
Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", Waziri wa Madini, Angella Kairuki (katikati) akiwa na Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem (kulia) pamoja na Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel (DMF) na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti", Doris Mollel baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi huo, uliofanyika katika ukumbi wa sinema wa Cinemax, Dar Free Market, jijini Dar es salaam leo. Filamu hiyo ambayo inaelezea maisha ya Mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati "Njiti" imeandaliwa na Taasisi ya Doris Mollel, imelenga kutoa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati.
Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", Waziri wa Madini, Angella Kairuki akitoa hotuba yake, ambapo alitoa pongezi nyingi kwa Taasisi ya Doris Mollel kwa kufanikisha kupatikana kwa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati kupitia filamu hiyo.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", ambayo inaelezea maisha ya Mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati "Njiti" iliyoandaliwa na Taasisi ya Doris Mollel, imelenga kutoa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati.
Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel (DMF) na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti", Doris Mollel akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika katika ukumbi wa sinema wa Cinemax, Dar Free Market, jijini Dar es salaam leo. 
Sehemu ya wageni waliohudhulia hafla hiyo.

DC HANDENI AZINDUA RASMI ZOEZI LA USAJILI, UTAMBUZI NA UFUATILIAJI WA MIFUGO (KUPIGA CHAPA)

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni akipiga chapa Ngo'mbe Kama ishara ya uzinduzi wa zoezi hilo
 Baadhi ya wafugaji walioleta mifugo yao kwaajili ya upigaji chapa ya moto
 Mifugo ikiwa imefungiwa tayari kwa zoezi la upigaji chapa.

MUHIMBILI YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO NJITI DUNIANI

$
0
0
Serikali imesema imeweka mikakati endeleveu  ya kupunguza vifo vya watoto njiti kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya afya nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Huduma za Kinga katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Neema Rusibamayila katika Siku ya Kimataifa ya Watoto Njiti ambayo huadhimishwa kila mwaka Novemba 17.

“Tanzania inakabiliwa na tatizo kubwa la vifo vya watoto wachanga chini ya mwezi mmoja hivyo kutokana na hali hii tunapaswa kudhibiti vifo kwa watoto wachanga,” alisema  Dkt. Rusibamayila.

Alisema takwimu zinaonyesha asilimia 13 hadi 17 ya watoto wote wanaozaliwa Tanzania ni njiti na kwamba kutokana na hali hiyo Serikali kupitia Wizara ya Afya, imekuwa ikiratibu progamu mbalimbali   za kupunguza  vifo vya watoto wachanga na wa chini ya miaka mitano.

Mkurugenzi huyo alisema moja ya program hizo ni kumsaidia mtoto kupumua baada ya kuzaliwa, kupanua huduma za watoto wachanga kwa kujenga wodi za watoto wachanga katika hospitali za manispaa na wilaya pamoja na kutoa mafunzo kwa wa hudumu wa afya jinsi ya ya kuhudumia watoto wachanga.
  Kaimu Mkuurugenzi wa Kinga katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Janneth Mghamba akizungumza kwenye maadhimisho ya mtoto Njiti Duniani ambayo huadhimishwa Novemba 17 kila mwaka. Kushoto ni Mkurugenzi wa Tiba Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Hedwiga Swai.
  Mkurugenzi wa Tiba Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Hedwiga Swai akizungumza na kinamama pamoja na wataalamu wengine wa afya katika siku ya mtoto njiti duniani. Kulia ni Kaimu Mkuurugenzi wa Kinga katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Janneth Mghamba, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Afya ya Uzazi na Mtoto katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Felix Bundara na Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Watoto, Dkt. Merry Charles.
 Baadhi ya kinamama wenye watoto njiti wakiwa kwenye maadhimisho hayo leo Muhimbili. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

KATIBU MKUU WIZARA YA KATIBA AKUTANA NA WADAU WA KIMATAIFA KATIKA MASUALA YA KISHERIA

$
0
0
 Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Griffin Mwakapeje (aliyesimama) akifafanua jambo katika kikao kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome na wadau wa kimataifa katika masuala ya sheria wakati wakibadilishana mawazo kuhusu sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya ugaidi Tanzania.
 Baadhi ya washiriki wa majadiliano ya sheria mbalimbali nchini kati ya  Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome na wadau wa kimataifa katika masuala ya sheria .
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akisisitiza jambo kwa wadau wa kimataifa katika masuala ya sheria walipomtembelea leo (17/11/2017) ofisini kwake mjini Dodoma.

Serikali Yawakaribisha wawekezaji kutoka China kuja kuwekeza kwenye miradi mbalimbali ya madini nchini.

$
0
0
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ametoa wito huo Novemba 16, 2017 Jijini Dar es Salaam alipokutana na Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Wang Ke na ujumbe alioambatana nao Wizarani hapo kutoka kwenye Ubalozi huo ili kujadiliana masuala mbalimbali ya madini ikiwemo fursa za uwekezaji.

Waziri Kairuki alisema Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi za madini na hivyo zipo fursa lukuki za uwekezaji ambazo zinaweza kutumiwa na kampuni za nchini China kwa manufaa ya pande zote mbili.

“Rasilimali za madini ni nyingi na hivyo zipo fursa mbalimbali ambazo zinaweza kutumiwa na kampuni za China na wakati huo huo kuchangia katika uchumi na pato la Taifa kwa ujumla,” alisema Waziri Kairuki.

Waziri Kairuki vile vile alisema yapo maeneo ambayo wawekezaji wanaweza kushirikiana na Serikali ambapo alitaja baadhi yake kuwa ni uchimbaji wa madini kwa kushirikiana na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), tafiti za utambuzi wa maeneo yenye madini kwa kushirikiana na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) na Chuo cha Madini (MRI).

Aidha, aliongeza kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha madini yanayochimbwa nchini yanaongezwa thamani kabla hayajasafirishwa ili kukuza uchumi wa Taifa na wakati huo huo, kuongeza mapato ya Serikali na kuzalisha ajira zaidi.
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kulia) akizungumza na Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke na ujumbe alioambatana nao (hawapo pichani) walipomtembelea Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kulia) akimsikiliza Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke alipomtembelea Ofisini kwake jijini Dar es Salaam ili kujadili masuala mbalimbali.
 Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke (kulia) akiwa na ujumbe wake kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania walipomtembelea Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (hayupo pichani) ili kujadili masuala mbalimbali ya Sekta ya Madini.

 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa pili kutoka kulia) akijadiliana jambo na ujumbe kutoka Ubalozi wa China nchini ulioongozwa na Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke (katikati).

USAID funded projects in Iringa voiced how keen their, in transforming people live

$
0
0
The United State Agency for International Development (USAID) funded projects in iringa has demostrated how their bringing impacts to the lives of the people in Iringa. This expression was made by USAID funded NGO’s and local CSO’s to the newly USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas who conducted a field visit in Iringa to assess the implementation of USAID funded Project activities.

Andy who was accompanied by his deputy Mission Director Helen Pataki and other USAID staff expressed his appreciation to the regional administration and local authorities for the support their giving to all implementing partners funded by USAID in the region and thanks them for their work their doing for the people of Iringa.    

Explaining on how they engage the local authorities and the entire community to fight the spread of the HIV/AIDS in Iringa, the Chief of Party with Sauti Project a Jhpiego’s lead program Dr. Albert Komba said despite the fact that the project works in 14 region countrywide, in Iringa Municipal they targets all Vulnerable groups including young girls by  linking them into services like Behavior Change Communication Sessions, Economic Empowerment groups, Screening for Gender Based Violence and cancelling on usage of Alcohol and Drugs.

“we are working to ensure we reduce the spread of HIV/AIDS because the groups we are targeting like these adolescence girls and female sex workers are more vulnerable and engaging them in the fight against HIV will lead to an HIV/AIDS free generation in Iringa” said Dr. Komba
 The Chief of Party of the Sauti Project a Jhpiego’s lead program Dr. Albert Komba elaborating a point to the USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas when he visited projects interventions conducted to reduce HIV/Aids prevalence to the vulnerable groups in Iringa. The program is conducting Behavior Change Communication Sessions, Screening for Gender Based Violence and cancelling on usage of Alcohol and Drugs to the Vulnerable groups including young girls.
 Scholina Charles (22) a young girl from umoja groups in iringa giving her testimony to the USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas and his delegation on the risk she went through before joining the Sauti project to fight HIV/ AIDS. Looking center is the Sauti Project Chief of Party Dr. Albert Komba .
 The USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas,  Deputy Mission Director Helen Pataki (second right), Jhpiego Country Director (right) and Sauti Project Chief of Party Dr. Albert Komba (left) following a Behavior Change Communication Sessions conducted by Zera Mingo (23) to the young adolescences girls as part of HIV/ AIDS intervention to reduce HIV/Aids prevalence to the vulnerable groups in Iringa.

FOR MORE NEWS CLICK HERE
Viewing all 110117 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>