Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110016 articles
Browse latest View live

BAKHRESA FOOD PRODUCT WAENDESHA WARSHA KUHUSIANA NA MBINU BORA ZA KILIMO KWA WAKULIMA

$
0
0


Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Hassan Sanga akizungumza na wakulima,wasafirishaji wa matunda katika warsha ya siku moja iliyoanadaliwa na Bakhresa Food Product –kitengo cha kuchata matunda leo Mkuranga Mkoa wa Pwani.
.Mkurugenzi wa Mahusiano wa Makampuni ya Bakhresa, Hussen Sufian Ally akizungumza na wakulima,wasafirishaji wa matunda kuhusu mbinu bora za uvunaji na usafirishaji wa matunda bila kupoteza ubora wake, leo Mkuranga Mkoa wa Pwani.
Sehemu ya wakulima na wasafirishaji wa matunda wakifatilia mada mbalimbali katika warsha hiyo uliyo anadaliwa na Bakhresa Food Product –kitengo cha kuchata matunda leo Mkuranga Mkoa wa Pwani.
Wakulima na wasafirishaji wa matunda wakitembele maeneo mbalimbali ya kiwanda hicho. Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya jamii.

TANZANIA NA SWEDEN ZAADHIMISHA MIAKA 40 YA USHIRIKIANO WA MASUALA YA UTAFITI

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa maadhimisho ya miaka 40 ya ushirikiano wa masuala ya utafiti baina ya Tanzania na Sweden na namna walivyoweza kufanikiwa kupata wataalamu mbalimbali wa tafiti. 


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo amesema kuwa ushirikiano uliopo baina ya  nchi ya Tanzania na  Sweden umeweza kuleta tafiti zenye tija kwa taifa na kufanikisha kupatikana kwa watafiti mbaimbali.

Hayo  ameyasema leo katika maadhimisho ya miaka 40 ya ushirikiano wa masuala ya utafiti baina ya Tanzania na Sweden yaliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa masuala ya utafiti nchini.

Dkt Akwilapo amesema kuwa, ushirikiano huo umeweza kuwasaidia katika kufanya tafiti zenye tija na maamuzi yanayoendana na tafiti kwa njia bora, wameweza kunufaika kwa kuweza kupata watafiti mbalimbali ambao wengi wao walikuwa wanafunzi.
"Kwa kipindi cha miaka 40 ya ushirikiano wetu baina ya Tanzania na Sweden tumeweza kupata watafiti wengi sana ambao kwa sasa wameweza kuhitimu katika ngaza za uzamivu (PHD) kwenye masuala mbalimbali ambapo wamweza kupatikana na kufanya tafiti mbalimbali kipindi wanasoma,"amesema Dkt Akwilapo.

Kwa upande wa  Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dugushilu Mafunda amesema amesema kuwa baada ya kuwezeshwa kwa kipindi ca miaka 10 wameweza kupata watafiti ambao kwa sasa hivi wanawafundisha watu wengine namna ya kufanya tafiti pia tafiti hizo zimejikita zaidi katika sayansi na teknolojia.

Mafunda ameongeza lengo kubwa ni kuhakikisha taasisi zijiendeshe, kuweza kuzipa taasisi nguvy ya kwenda kufanya tafiti sehemu mbalimbali na wanashukuru kwa sasa serikali ya Tanzania wanatilia mkazo suala la sayansi na teknolojia.

Mkurugenzi Mkuu wa taasisi ya utafiti ya nchini Sweden,  SIDA nchini Sweden Karin Jamtinameweka wazi kuwa kwa sasa Tanzania wameweza kukua katika masuala ya utafiti na zaidi wameshapata wataalamu kutoka kwa wanafunzi waliokuwa wanafanya utafiti kwenye miaka ya nyuma na hilo limeweza kusaidia zaidi kwenye kutoa elimu.

 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dugushilu Mafunda akielezea namna ushirikoano huo baina ya Tanzania na Sweden ulivyoweza kusaidia kuwapata wataalamu na utafiti pia kuweza kuwasadia taasisi kujindesha zenyewe ikiwemo kufanya tafiti sehemu tofauti za nchi na nje ya nchi.
Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akifuatilia mkutano wa maadhimisho ya miaka 40 ya ushirikiano wa masuala ya utafiti baina ya Tanzania na Sweden ulioanza leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa taasisi ya utafiti ya nchini Sweden, SIDA nchini Sweden Karin Jamtin akizungumza na wanahabaru namna jinsi taasisi yao ya nchini Sweden walivyoweza kushirikiana na Tanzania kupitia vyuo na serikali kwenye masuala ya utafiti wa mambo mbalimbali.
Wadau wa masuala ya sayansi na teknolojia wakiwa wanatembelea mabanda yaliyopo katika ukumbi wa mkutano ikiwa ni katika maadhimisho ya miaka 40 ya ushirikiano wa masuala ya utafiti baina ya Tanzania na Sweden yalioanza leo Jijini Dar es Salaam

YANGA NA SIMBA ZAPIGWA FAINI, SIMBA YAPEWA ONYO KALI KWA KOCHA WAKE MSAIDIZI

$
0
0
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imepitia ripoti za michezo yote ya Ligi Kuu Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja Pili (SDL) na kufanya uamuzi ufuatao.


Mechi namba 54 (Simba 4 v Njombe Mji 0).



Klabu ya Simba imepewa Onyo Kali kutokana na Kocha wake Msaidizi Masoud Djuma kuanza kufundisha bila kuwa na vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini. Uamuzi huo umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(13) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha.



Pia klabu hiyo imetakiwa kufikia Novemba 10 iwe imewasilisha Bodi ya Ligi nakala ya vibali hivyo, na kukumbushwa kuwa mahitaji ya nyaraka hizo ni kwa mujibu wa Kanuni za Ligi, lakini pia sheria za nchi.



Vilevile klabu ya Simba imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa timu yake kuwasilisha orodha ya wachezaji wake (team match list) nje ya muda wa kikanuni. Kitendo cha timu hiyo ni kukiuka Kanuni ya 14(2k) ya Ligi Kuu. Adhabu dhidi yao imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu.



Klabu ya Njombe Mji imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na kuonesha vitendo vinavyoashiria imani za ushirikina katika mechi hiyo wakati ikiwasili uwanjani. Adhabu dhidi ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Klabu.



Mechi namba 56 (Stand United 0 v Yanga 4). Klabu ya Stand United imetozwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kutokana na golikipa wao kuvaa jezi yenye namba tofauti na ile iliyosajiliwa, kitendo ambacho ni ukiukaji wa Kanuni ya 60(11) ya Ligi Kuu kuhusu Usajili. Adhabu dhidi yao imezingatia Kanuni ya 60(12) ya Ligi Kuu.



Mechi namba 57 (Azam FC 1 v Mbeya City 0). Mwamuzi Shakaile Ole Yanga Lai amefungiwa miezi mitatu kwa kutoripoti na kuchukua hatua dhidi ya kitendo cha Kipa Owen Chaima wa Mbeya City kumpiga kofi mshambuliaji wa Azam FC. Kitendo cha Mwamuzi huyo ni ukiukaji wa Kanuni ya 38(1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Waamuzi wakati adhabu dhidi yake imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 38(5) ya Ligi Kuu.



Naye Kamishna wa mechi hiyo, David Lugenge amefungiwa miezi mitatu kwa kushindwa kuripoti tukio hilo. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 39 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Kamishna.



Mechi namba 58 (Yanga 1 v Simba 1). Klabu ya Yanga imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na mashabiki wake kurusha uwanjani chupa zinazosadikiwa kuwa na mikojo. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 42(1) kuhusu Udhibiti wa Klabu.

RUNGU LA ADHABU LATEMBEA LIGI DARAJA LA KWANZA (FDL) NA LA PILI (SDL)

$
0
0

Mechi namba 16 Kundi A (Friends Rangers 1 v African Lyon 1). Klabu ya African Lyon imepewa Onyo Kali kwa timu yake kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mechi ikiwa na maofisa pungufu, kitendo ambacho ni kinyume na Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Kwanza. Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza.

Mechi namba 20 Kundi A (Mgambo JKT 1 v Mshikamano 0). Klabu ya Mgambo JKT imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kuingia uwanjani baada ya filimbi ya mwisho ya mchezo kupulizwa. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.

Mechi namba 21 Kundi A (Kiluvya United 2 0 v Mshikamano 1). Klabu ya Kiluvya United imepigwa faini ya sh. 100,000 (laki moja) kwa kutohudhuria kikao cha maandalizi ya mechi, kitendo ambacho ni kinyume na Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Kwanza. Faini hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza.

Mechi namba 24 Kundi A (Friends Rangers 0 v JKT Ruvu 3). Klabu ya Friends Rangers imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kusababisha mchezo kusimama kwa dakika tano baada ya kumpiga jiwe Mwamuzi Msaidizi. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.



Mechi namba 28 Kundi A (Mgambo JKT 2 v Ashanti United 1). Klabu ya Mgambo JKT imepewa Onyo Kali kutokana na timu yake kuchelewa kufika uwanjani kwa dakika 13. Adhabu hiyo ni utekelezaji wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo.

UYUI WAZIPOKEA KWA MIKONO MIWILI MBEGU BORA ZILIZOFANYIWA UTAFITI KUTOKA COSTECH-OFAB

$
0
0
 Wanakikundi cha Upendo kilichopo Kijiji cha Magiri Kata ya Magiri katika Halmshauri ya Wilaya ya Uyui mkoani Tabora wakiwa pamoja na watafiti kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha ARI-Maruku mkoani Kagera na Mwanahabari Coleta Makulwa wa RFA (wa pili kushoto), baada ya kukabidhiwa mbegu bora za Viazi lishe aina ya Kabode kwa ajili ya kuzipanda kwenye shamba darasa katika kata hiyo wilayani humo leo.
 Mbegu hizo zikiinuliwa juu baada ya kukabidhiwa.
 Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa, akimkabidhi mbegu za mihogo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Uyui, Hadija Makuwani kwa ajili ya kupanda katika shamba darasa katika Kijiji cha Isikizya wilayani humo. Wengine ni wakulima wa kijiji hicho.
 Wanakikundi cha Mapambano katika Kijiji cha Iberamilundi wakifurahi mbegu bora ya mihogo baada ya kukabidhiwa.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KOMBE LA SHIRIKISHO LA ASFC KUENDELEA KESHO KATIKA VIWANJA SABA

$
0
0
Michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam yaani Azam Sports Federation Cup (ASFC), inaendelea kesho Alhamisi Novemba 9, 2017 kwa michezo saba ambako Dar City itacheza na Majimaji Rangers ya Lindi.


Mchezo huo utafanyika kwenye Uwanja wa Bandari jijini Dar es Salaam huku Real Mojamoja ya Iringa ikiwa wenyeji wa African Wanderers kwenye Uwanja wa Samora mkoani Iringa wakati Shupavu na Sabasaba zitachuana mjini Morogoro.



Mashujaa ilikwisha kupata mpinzani ambaye ni Buseresere ambaye kabla aliifunga Isoko katika hatua ya awali. Mchezo huo utafanyika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.



The Mighty Elephant itacheza na Makanyagio kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea. Namungo na Villa Squad nazo zinacheza kesho kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara .




RC GEITA ASHIRIKIANA NA WANANCHI KUCHIMBA MSINGI NA UJENZI WA KITUO CHA AFYA MGANZA WILAYANI CHATO

$
0
0
Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi Mkuu wa Mkoa wa Geita amezindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa Zahanati Wilayani Chato ili kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa na Zahanati Wilayani humo.

Mhandisi Robert Gabriel amezidua kampeni hiyo kwa kushirikiana na wananchi kuchimba msingi kwa ajili ya ujenzi wa vymba vya madarasa viwili pamoja na Ofisi katika shule ya msingi Ilyamchele ambayo inaongezeko la wanafunzi 2,212 kutoka 1,700. Darasa la pili linawanafunzi 407 ambao wanasoma kwa awamu mbili hivyo, kufanya shule hiyo kuwa na mahitaji ya vyumba vya madarasa 28.

Akizungumza na wananchi baada ya kuchimba msingi Mkuu wa Mkoa amesema kuwa Serikali inataka watoto wa Ilyamchele wafanane na watoto wa maeneo mengine kwa kukaa katika vyumba vizuri vya kisasa vyenye miundombinu ya kutosha na walimu wa kutosha. Hivyo, ametoa wito kwa wananchi wote kushirikiana na viongozi wote katika utekelezaji wa miradi hii ili kumaliza uhaba wa vyumba vya madarasa na Zahanati.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akishiriki kujenga ukuta katika kituo cha afya Mganza Halmashauri ya Wilaya Chato.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amendelea na ziara hadi kijiji cha Mganza ambapo ameshiriki katika ujenzi wa kituo cha afya Mganza ili kuona hali ya wananchi kupata huduma katika vijiji inaimalika kwa kujenga Zahanati na vituo vipya vya afya.

Miradi hii inatekelezwa na vikundi vya mafundi walioungana kwa kujitolea kufanya kazi hiyo pasipo kuwa na malipo isipokuwa kupatiwa chakula wanapokuwa katika eneo la kazi. Wananchi na wadau wanashiriki kwa kuleta maji, mchanga, sementi, kokoto na kushiriki katika ujenzi.

Mafanikio haya yanatokana na juhudi za Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa baada ya kuwasili mkoani Geita baada ya uteuzi wake aliamua kutoa semina kuhusu mikakati na njia za kumaliza tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa na Zahanati kwa Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala Wilaya, Wakurugenzi, Maafisa Tarafa, Maafisa elimu wa Wilaya na Makatibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya zote.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel akichanganya mchanga na simenti kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Mganza (Chato) alipofanya ziara ya kikazi ya kuhamasisha wananchi kushiriki katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo Wilayani humo.

H.E. PAUL KAGAME TOURS EAC PARTNER STATES STAND AT WTM IN LONDON

$
0
0
EAC Headquarters, Arusha, Tanzania, 8th November 2017: H.E Paul Kagame, President of the Republic of Rwanda on Monday 6th November, 2017, toured the EAC Partner States stand at the World Travel Market (WTM) and recognized the joint tourism promotion efforts by the Partner States. The President was at the World Tourism Market to receive his World Tourism Awards given in recognition of his efforts to foster sustainable tourism development in Rwanda. The award exemplified the commitment by East African leaders in promoting sustainable tourism.

Meanwhile, the EAC High Commissioners/ Ambassadors in London, Heads of Tourism Boards for Partner States, and the Secretariat staff held a pre- WTM meeting on 5th November 2017 at the Uganda High Commission premises.

H.E Paul Kagame greeting Uganda’s Minister of Tourism, Wildlife and Antiquities Prof. Ephraim Kamuntu at the Uganda WTM stand.

The objective of the meeting was to provide the High Commissioners and Ambassadors with information on the current status of the Tourism sector in the EAC region and on the agreed priorities for the next financial year and in the 5th EAC Development Strategy, as well as to review the programme of the EAC joint event with Partner States at the World Travel Market.

The meeting was co-chaired by the EAC Deputy Secretary General in charge of Productive Sectors, Hon. Christophe Bazivamo and the Uganda High Commissioner, H.E Julius Moto. 

H.E Moto welcomed the participants to the meeting and observed that tourism sector was quite significant for EAC economies and therefore it required concerted promotional efforts. He further noted that joint participation at the World Travel Market was quite critical given that it was the largest international trade fair with an attendance of about 50,000 people. “This offers the EAC as a region and the Partner States an opportunity to market their tourism products and therefore the need to gear marketing efforts towards high spending tourists to ensure maximum benefits for the region” noted Uganda’s High Commissioner in the UK.

The EAC team meeting the UN World Tourism Organization Director of Programme for Africa on 7th November, 2017.

The EAC Deputy Secretary General in charge of Productive and Social Sectors highlighted major undertakings and progress made in the EAC integration process that include; EAC being recognized as one of the fastest growing regions in Sub-Saharan Africa and the largest regional economic blocs with the largest single market in Africa with a total population of about 170 million.

The EAC official briefed the Envoys on how EAC had become a fully-fledged Single Customs Territory since 2014 with major benefits such as reduced turnaround times in clearance and transportation of goods across borders. Other milestones include implementation of Common Market Protocol and significant removal of non-tariff barriers to trade; and the development of the EAC International e-passport and Partner States such as Kenya and Burundi have started issuing the passport.

Other High Commissioners/ Ambassadors in attendance were; H.E. Ernest Ndabashinze, Ambassador of Burundi in the United Kingdom (UK); H.E Lazarus O. Amayo, Kenya’s High Commissioner in UK; H.E Asha-Rose Migiro, High Commissioner of the United Republic of Tanzania in UK; Mr. David Ruvibi from Rwanda High Commission, and Maker A. Deng from the Embassy of South Sudan.

The EAC Deputy Secretary General in charge of Productive and Social Sectors, Hon. Christophe Bazivamo, and the Ugandan High Commissioner, H.E Julius Moto co-chairing the meeting.

The EAC team also met the UN World Tourism Organization Director of Programme for Africa, Ms. Elcia Grandcourt on 7th November 2017, with whom they discussed possible areas of technical co-operation in tourism. These will include development of quality assurance mechanisms for the tourism sector, harmonization of tourism statistics, and development of a regional tourism marketing strategy. 

The two institutions will enter into an MoU on technical co-operation. The possibility of staging an EAC-UNWTO joint conference in East Africa was also discussed. The objective would be to build capacity of key tourism stakeholders.
Group photo opportunity.

SERIKALI KUPATA MABILIONI YA SHILINGI KUTOKANA NA ALMASI ILIYOKAMATWA UWANJA WA NDEGE WA JNIA

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Waziri wa Madini, Angela Kairuki amesema kuwa serikali inataraji kupata mrabaha zaidi katika madini ya Almasi yaliyokamatwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere kutoka kwa Kampuni ya Williamson Diamond iliyokuwa ikitaka kutoroshwa madini nchini kwenda Ubelgiji.

Waziri Kairuki amesema hayo alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari wakati akitoa ripoti ya Wizara ya Madini juu ya mzigo huo wa Almasi kutoka kampuni ya Williamson Diamonds.

“tarehe 20/10/2017 almasi hizo zilisafirishwa kwenda ubelgiji na serikali ilituma maafisa wake kusimamia uuzwaji wa alamasi hizo ambapo tarehe 7/11/2017 almasi hizo ziliuzwa kwa dola za Marekani 10,261,227.76 hivyo thamani hii ni ongezeko la Dola za Marekani 2,069,582.77 sawa na asilimia 20.16%”amesema.

Amesema kutokana na ongezeko hilo baada ya almas kuuzwa serikali itapata mrabaha zaidi ambao ni mwisho kiasi cha Dola za Marekani 124,174,.97 na ada ya ukaguzi Dola za marekani 20,695.83 ambayo jumla yake ni dola za Marekani 144,870.80 sawa na shilingi Milioni 325.525 hivyo jumla ya mapato yote ya serikali kutokana na mauzo ya almasi hizi ni Dola za Marekani 718,288.95

Aidha Waziri Kairuki amesema katika mzigo huo waliweza kuikuta Almasi moja yenye rangi ya pinki ambayo ni adimu kupatikana na yenye uzito wa karatani 5.92 na kuuzwa kwa dola za marekani 2,005,555.00 sawa na shilingi Bilioni 4.51 .

Alimaliza kwa kusema kuwa anawakikishia Watanzania kuwa serikali itaendelea kuisimamia kwa makini rasilimali zetu za madini ili kuhakikisha kuwa nchi yetu inanufaika ipasavyo.
Waziri wa Madini, Angela Kairuki akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya ripoti ya faida iliyopata serikali katika Madini ya Almas kutoka mgodi wa Wiliamson Diamonds Ltd iliyokamatwa uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila akitoa ufafanuzi wa kitaalmu juu ya madini hayo yaliyouzwa huko ubelgiji.
Kamishana wa Madini, Mhandisi Benjamini Mchwampaka akizungumzia juu ya madini hayo yanavyoweza kuliongezea pato taifa.

KIGAMBONI MARATHON KURINDIMA DISEMBA 2, 2017 WILAYANI KIGAMBONI

MICHUZI TV: Rais Dkt Magufuli akipata maelezo ya kilimo cha miwa alipotembelea kiwan...

BENKI YA DUNIA YAIPATIA TANZANIA MKOPO NAFUU WA BILIONI 340 KUENDELEZA UTALII UKANDA WA KUSINI

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (wa pili kulia) na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi, Burundi na Msumbuji, Bi. Bella Bird, wakisaini Mkataba wa Mkopo wenye masharti nafuu wa Sh. Dola za Marekani milioni 150 sawa na Shilingi bilioni 340 kwa ajili ya Mradi wa kuibua fursa za Utalii Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, huku Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi (wa pili kulia waliosimama-tai nyekundu) akishuhudia, katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.

 Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi, Msumbiji na Burundi Bi. Bella Bird (kushoto) wakibadilishana Mkataba wa Mkopo wenye masharti nafuu wa Sh. bilioni 340 kwa ajili ya Mradi wa kuibua fursa za Utalii katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi, Msumbiji na Burundi Bi. Bella Bird (kushoto) wakionesha Mkataba wa Mkopo wenye masharti nafuu wa Sh. bilioni 340 kwa ajili ya Mradi wa kuibua fursa za Utalii katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, baada ya kusainiwa katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa-TANAPA, Bw. Allan Kijazi na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi, Burundi na Msumbuji, Bi Bella Bird, wakisaini Makubaliano ya utekelezaji wa Mkataba wa Mradi wa kuibua fursa za Utalii Ukanda wa Kusini mwa Tanzania utakao gharimu Shilingi bilioni 340 zilizotolewa kama mkopo wenye masharti nafuu na Benki hiyo kwa Tanzania, Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia nyuma ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, (wa pili kulia waliosimama akifuatiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi, Jijini Dar es Salaam.

BOFYA HAPA KWA HABARI ZAIDI

RAIS DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA WANANCHI WA WILAYA YA MISENYI NA KUTEMBELEA KIWANDA CHA SUKARI CHA KAGERA SUGAR, MISENYI MKOANI KAGERA

$
0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanachi wa Wilaya ya Misenyi(hawaonekani pichani) wakati akielekea katika kiwanda cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo Wilayani hapo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiandika wakati wananchi wa Misenyi walipokuwa wakiwasilisha Kero zao mara baada ya kusimama wakati akiwa njiani kuelekea katika Kiwanda cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo wialayani humo.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipokewa kwa shangwe na Mamia ya wananchi wa Misenyi mara baada ya kuwasili Wialayani hapo akitokea Bukoba mjini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasikiliza wananchi wa Misenyi wakati wakitoa kero zao mbalimbali mara baada ya kuwasili.
 Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akizungumza katika eneo hilo la Misenyi.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli pamoja na  Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu wa pili kutoka kushoto , Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba wa kwanza (kulia) wakisikiliza mtaalamu wa Kilimo (haonekani pichani) aliyekuwa akielezea mambo mbalimbali katika mashamba ya miwa katika Kiwanda hicho cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo Misenyi mkoani Kagera.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

RC MPYA DODOMA DKT. MAHENGE AWATEMBELEA VIONGOZI WA BARAZA LA WAZEE DODOMA, WAMUAAHIDI USHIRIKIANO

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Dkt. Binilith Mahenge amemtembelea na kufanya mazungumzo na mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Dodoma Balozi Mstaafu Job Lusinde ambapo mwenyekiti huyo wa Wazee amemuhakikishia Dkt. Mahenge ushirikiano kutoka kwa Wazee wakati wote wa uongozi wake Mkoani Dodoma.

Dkt. Mahenge alimtembelea Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Balozi (Mstaafu) Lusinde kwa lengo la kujitambulisha kama Mkuu mpya wa Mkoa wa Dodoma na kuahidi kuwa atakutana na Baraza zima la Wazee la Mkoa wa Dodoma hivi karibuni, aidha, Dkt. Mahenge alipata pia fursa ya kumtembelea Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Pinda nyumbani kwake Zuzu nje kidogo ya Mji wa Dodoma na kujionea shughuli za kilimo na ufugaji wa kisasa wa mifugo, nyuki na samaki.

Balozi (Mstaafu)Lusinde amebainisha kumfahamu Mheshimiwa Dkt. Mahenge kwa muda mrefu akiwa kwenye nafasi mbalimbali za uongozi na kumpongeza kwa jitihada zake za kuongoza na kutumikia wananchi kwenye nafasi mbalimbali alizowahi kutumika hivyo kumuhakikishia ushirikiano kutoka kwa baraza la wazee.

 “Wakati wote wa uongozi wako hapa Mkoani Dodoma, Baraza la Wazee litakuunga mkono na kukupatia ushirikiano mkubwa ili uweze kutekeleza majukumu yako hususani ya kusimamia shughuli za maendeleo kwenye Mkoa wa Dodoma” alisisitiza Balozi Lusinde wakati wa mazungumzo yake na Mkuu wa Mkoa Dkt. Mahenge
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (kulia) akifanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Dodoma Balozi Mstaafu Job Lusinde alipomtembelea nyumbani kwake Uzunguni Mjini Dodoma, Balozi Lusinde amemuhakikishia Dkt. Mahenge ushirikiano kutoka kwa wazee.
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akimtembeza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge kwenye mradi wake mpya wa ufugaji samaki wakati Dkt. Mahenge alipomtembelea Mhe. Pinda nyumbani kwake Zuzu nje kidogo ya mji wa Dodoma.
 Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda (kushoto) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge wakati Dkt. Mahenge alipomtembelea Mhe. Pinda nyumbani kwake Zuzu nje kidogo ya mji wa Dodoma. 
 Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akimtembeza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge kwenye mradi wake mpya wa ufugaji samaki wakati Dkt. Mahenge alipomtembelea Mhe. Pinda nyumbani kwake Zuzu nje kidogo ya mji wa Dodoma.

MAGAZETI YA ALHAMIS LEO NOVEMBA 9, 2017

RC Wangabo amuagiza RPC awapumzishe DTO na Msaidizi wa RTO kupisha uchunguzi

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa George Kyando kuwaweka pembeni Mkuu wa Usalama barabarani wa Wilaya Inspector Suleiman Africanus pamoja na Msaidizi wa Mkuu wa Usalama barabarani Mkoa Inspector Michael Mwakasungula ili kupisha uchunguzi kufuatia tuhuma kadhaa zilizoelekezwa dhidi yao.

Agizo hilo amelitoa wakati akijibu kero za madereva wa bajaji na bodaboda wapatao 4352 kwa mkoa mzima waliowakilishwa na wenzao wa mjini Sumbawanga baada ya kukutana nao na kusikiliza vilio vyao katika Mkutano uliofanyika katika Viwanja vya Nelson Mandela mjini Sumbawanga.

Madereva 13 walipata nafasi ya kumuelezea Mh. Wangabo kero wanazopata wakiwa barabarani huku miongoni mwa kero hizo ambazo ni pamoja na kupokea rushwa, uonevu usio wa lazima barabarani na kuwaweka mahabusu kwa visingizio mbalimbali zilielekezwa kwa maafisa hao wa usalama barabarani.

“Hawa wawili hawa na tuhuma mlizozitoa huenda zina ukweli, RPC nakuagiza nenda kazichunguze hizi tuhuma zote zilizotolewa hapa kwa kina na nyinyi muwe mashahidi kwenda polisi kutoa shuhuda zenu, halafu uchukue hatua stahiki, lakini wakati huo huo unapozichunguza hizi tuhuma wao uwaweke pembeni, uwape kazi nyingine,”

Amesema kuwa hakuna mtendaji wa serikali ambaye amepangiwa sehemu akae milele na milele na kuwa mtumishi asijidanyanye kwamba bila ya yeye kazi za serikali haziwezi kwenda huku akijitolea mfano kuwa yeye ni Mkuu wa Mkoa wa 15 tangu kuanzishwa kwa Mkoa huu mwaka 1974, wote walionitangulia wamepiga kazi wameondoka nae ataondoka.

Aidha, Mh. Wangabo amewasisitiza madereva hao kusomea sheria za barabarani na kupata leseni ilikupunguza ajali za barabarani katika Mkoa wa Rukwa huku akiwapongeza kwa takwimu zinzoonyesha kupungua kwa ajali hizi ukilinganisha na mwaka 2016.

Katika kulisisitiza hilo Mh. Wangabo alimualika mwalimu wa mafunzo ya usalama barabarani ili kutoa mafunzo hayo ya siku 3 bure kwa madereva hao kwa lengo la kutokuwa na ajali katika Mkoa wa Rukwa.huku akimpa miezi 7 kamanda wa polisi mkoa kuhakikisha bodaboda wote 4352 wanakuwa na leseni na vitambulisho.

Kwa upande wake kamanda wa polisi Mkoa ACP George Kyando ameeleza kuwa kwa ajali za bajaji na bodaboda mwaka 2016 kulikuwa na ajali 18 huku 11 zikisababisha vifo vya watu 20 wakati mwaka 2017 kuemtokea ajali 9 huku 5 zikisababisha vifo vya watu 7.

Yona Mwangoka ni mmoja wa madereva wa bodaboda aliyedai kuwa na ushahidi wa video unaoonyesha ukusanyaji wa shilingi 40,000 kuwapa polisi ili kuachiwa kwa makosa mbalimbali huku risiti zao zikionesha shilingi 30,000, fedha ambazo zilikusanywa na kiongozi wa boda boda baada ya boda boda hao kukamatwa kwa kosa la kumpiga askari wa usalama barabarani tukio lililotokea siku mbili kabla ya Mkutano huo. 
 Baadhi ya Bajaji zikiwa zimepaki katika uwanja ulipofanyikia Mkutano wa madereva wa Bajaji na Bodaboda na Mkuu wa Mkoa. 

 Kamanda wa polisi Mkoa wa Rukwa ACP George Kyando akitoa elimu ya usalama barabarani na kujibu baadhi ya kero zilizotolewa na madereva wa Bodaboda na bajaji wa Manispaa ya Sumbawanga. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akizungumza na madereva wa Bodaboda na Bajaji wa Manispaa ya Sumbawanga katika uwanja wa Nelson Mandela.
baadhi ya bodaboda zikiwa zimepaki uwanja wa Nelson Mandela Mjini Sumbawanga.

KATIBU MKUU WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO BW. DOTO JAMES AWATOA HOFU WATANZANIA KUHUSU DENI LA TAIFA

$
0
0
Benny Mwaipaja, Dar es Salaam

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James amewatoa hofu watanzania kuhusu ongezeko la Deni la Taifa akisisitiza kuwa Deni hilo ni himilivu.

Bw. James amesema hayo Jijini Dar es Salaam kwa vyombo vya habari wakati wa hafla fupi ya kutia saini Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Shilingi bilioni 340 uliotolewa na Benki ya Dunia kwa ajili ya Mradi wa kuendeleza utalii kwa vivutio vilivyoko katika ukanda wa kusini mwa Tanzania ujulikao kama Resilient Natural Resource for Tourism and Growth (REGROW)

Alikuwa akitolea ufafanuzi kuhusu baadhi ya watu na vyombo vya habari vinavyozungumzia Deni la Taifa kwa kutumia neno Deni la Taifa “linapaa”

Katibu Mkuu huyo ambaye pia ndiye Mlipaji Mkuu wa Serikali alisema kuwa Deni la Taifa ni himilivu kwa kutumia viwango vya kitaifa na kimataifa kwamba ili nchi iwe katika hatari ya kukua kwa Deni lake la Taifa inabidi lifikie asilimia zaidi ya 50 lakini kwa Tanzania kiwango cha deni hilo ni asilimia 32.

“Deni letu lingekuwa linapaa, hata Benki ya Dunia wasingekubali kutukopesha kwa maana hiyo tukitaka kukopa tutafanya hivyo kwa kuwa tuko chini katika viwango vya ukopaji kwa asilimia zaidi ya 18” alisema Bw. Doto James.

Kwa hiyo nawaomba hili mlichukue muuelimishe umma wa watanzania kwamba deni la Taifa ni stahimilivu, nchi inakopesheka vizuri.Novemba 7, 2017, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiwasilisha Bungeni mjini Dodoma Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Mwongozo wa Maanndalizi ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka 2018/2019 alisema kuwa Deni la Taifa limefikia dola za Marekani milioni 26,115.2 mwezi Juni mwaka 2017.

Dkt. Mpango alieleza kuwa ongezeko hilo ni sawa na asilimia 17 ikilinganishwa na dola milioni 22,320.76 katika kipindi kama hicho mwaka 2016.Alisema ongezeko hilo lilichangiwa na mikopo mipya iliyochukuliwa ili kugharamia miradi ya maendeleo kama vile: Standard Gauge Railway; Strategic Cities; mradi wa usafirishaji Dar es Salaam (DART) na kupanua upatikanaji wa maji safi Dar es Salaam. 

Deni hilo la Taifa linajumuisha deni la Serikali lililofikia dola za Marekani milioni 22,443.70 na deni la sekta binafsi la dola za Marekani milioni 3,671.50. Pamoja na ongezeko hili, viashiria vyote bado vinaonesha kuwa deni la Taifa ni himilivu kwa kipindi cha muda mfupi, wa kati na mrefu huku uwiano kati ya deni na Pato la Taifa umefikia asilimia 31.2 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 56.

MAVUNDE AMKABIDHI KITITA CHA MILIONI 60 MSHINDI WA DROO YA 14 YA TATUMZUKA MJINI DODOMA.

$
0
0
Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Mheshimiwa Anthony Mavunde leo amemkabidhi kitita cha shilingi Milioni 60 mshindi wa droo ya Tatumzuka Bwana Robert Changadiko ambaye alijishindia kiasi hicho katika ‘Jackpot’ ya wiki hii katika droo ya kusisimua iliyoonyeshwa siku ya jumapili kupitia vituo vya runinga kote nchini.

Bwana Changadiko ambaye anafanya kazi kama fundi minara mjini Dodoma alielezea furaha yake juu ya ushindi huo ambao hakuutegemea na akaishukuru Tatumzuka kwa kutimiza hitaji lake la pesa wakati alipokuwa akizihitaji zaidi.

"Niliamua kucheza Tatu Mzuka kutokana na matatizo niliyokuwa nayo ya kifedha ambapo nilihitaji fedha za haraka ili kukidhi mahitaji hayo. Kwakweli nina furaha kubwa sana na nashukuru kwamba nilijaribu bahati na ikatimia” alisema.Mavunde alimpongeza mshindi kwa kushinda kiasi hicho na Tatu Mzuka kwa ajili ya kuendelea kutengeneza mamilionea na kubadilisha maisha ya watu.

Naibu Waziri Kazi, Vijana na Ajira (kushoto) Mh. Antony Mavunde (Mbunge), akimkabidhi mshindi wa 14 wa mchezo wa tatu Mzuka Bw. Robert A. Changadiko(45), hundi ya shilingi milioni sitini , Mjini  Dodoma.
Mshindi wa droo ya 14 ya Tatu Mzuka Bw.Robert A. Changadiko (kulia)aliyejishindia donge nono la shilingi milioni sitini wiki hii, akiwa na rafiki yake bwana Bw. Daudi Mwangoto (katikati), ambaye alizawadiwa shilingi milioni moja kutoka katika promosheni ya cheza na washkaji shinda na washkaji ya Tatu Mzuka, kushoto ni Bw.Edwin Kawito ni mshindi wa Tatu Mzuka droo ya kumi (10) aliyejishindia shilingi milioni sitini.
Mshindi wa shilingi milioni sitini kutoka kijiji cha Msembata (Dodoma)Bw.Robert A. Changadiko mwenye umri wa maika 45, ambaye ni fundi minara,akifurahia ushindi wake.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Mfumo wa kutengeneza na kusambaza filamu za Kitanzania (Bongohoodz) wazinduliwa

$
0
0
 
Kampuni za utengenezaji filamu za Mashauri Studios na Novitech kwa kushirikiana na Clouds Plus pamoja na Shirikisho la Filamu Tanzania imezindua rasmi mfumo wa kutengeneza, kutangaza, kuonyesha na kusambaza filamu za kitanzania ujulikanao kama Bongohoodz. 

Akizungumza na waandishi wa habari, mwanzilishi mwenza wa Bongohoodz ambaye pia ni mtayarishaji wa filamu na Mkurugenzi wa Mashauri Studios, Paul Mashauri, mfanyabiashara ambaye katika miaka ya hivi karibuni alimua kuwekeza katika filamu alisema Bongohoodz inakuja kuwasaidia waandaaji wa filamu nchini kutatua tatizo la wizi wa kazi za sanaa hasa DVDs kutokana na usambazaji wa sinema feki unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu.

 “Baada ya kutoa sinema kazaa sokoni ikiwa ni pamoja na One Month Date mwaka 2014, Maisha ni Siasa na Bongo na Fleva mwaka 2015 tumegundua kuwa wizi wa kazi za sanaa ‘piracy’ ni mkubwa sana.

 Lakini kupitia Bongohoodz, watayarishaji wa sinema nchini hawatahitaji tena kusubiri mapato yao au uwekezaji wao urudi kwa kuuza DVDs, "Kimsingi hata katika nchi zilizopiga hatua katika sinema unazungumzia Hollywood (Marekani), Bollywood (India), China Film Industry (China) na Nollywood (Nigeria), mapato makubwa yanatokana na uonyeshaji wa sinema katika majumba ya sinema au ‘theaters’ wao wanaita ‘Box Office’. 

Kwa sababu wizi wa kazi za sanaa upo dunia nzima," alisema Mashauri na kuongeza. "Lakini mapato ya kwanza wanayopata waandaaji wa sinema au ‘production houses’ yanatoka ‘Box office’ au katika nyumba za kuonyesha sinema. Ndio maana sisi tutasema, kwanini tusionyeshe sinema hizi nchi nzima katika matamasha makubwa ambapo watanzania watapata kuona sinema zinazoburudisha na kufundisha kwa bei nafuu kabisa huku wakifurahia vyakula mbalimbali, muziki, kisha filamu?” 

Viewing all 110016 articles
Browse latest View live




Latest Images