Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

ZIARA YA KAMISHNA WA EU NEVEN MIMICA YALETA NEEMA KWA TANZANIA

$
0
0
 NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

ULE msemo wa kiswahili wa "mgeni njoo mwenyeji apone", unaweza kutumika kufatsiri neema ambayo taifa limepata kufuatia ziara ya siku mbili nchini ya Kamishna wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) anayeshughulikia mahusiano ya Kimataifa na Maendeleo, Mhe. Neven  Mimica, pichani juu.
Mhe. Mimica alianza ziara yake Novemba 2, kwa kutiliana saini makubaliano na Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mjpango, ambapo EU imeahidi kutoa kiasi cha Euro milioni 50 ambazo zitatumika kupeleka umeme vijijini.
Serikali inapambana kuhakikisha vijiji elfu 12 (12,000) ambavyo bado havina umeme nchini vinapata huduma ya umeme ifikapo 2020.Kwa mujibub wa Afisa Habari wa EU hapa nchini Bi.Susanne Mbise, msaada huo wa Euro milioni 50 utasaidia kupeleka umeme kwenye vijiji 3,000.
Ziara ya Kamishna Mimica, ililenga kutembelea shughuli mbalimbali ambazo EU imekuwa ikifadhili,
Miongoni mwa maeneo ambayo Kamishna Mimica alitembelea ni pamoja na bandari ya Dar es Salaam, ambapo akiongea na uongozi wa bandari hiyo, Kamishna Mimica a,lieleza utayari wa EU katika kusaidia kub oresha bandari hiyo kwani ina msada mkubwa sio tu kwa Tanzania bali pia kwa nchi majirani.
Kamishna Mimica pia ametembelea kituo kinachosaidia vijana cha Nafasi Art Space kilichoko  Mikocheni jijini Dar es Salaam ambapo aliweza kusikiliza maoni yao na kujadiliana nao masuala mbalimbali yahusuyo changamoto za ajira na pia ukatili dhidi ya mtoto wa kike. "Kamishna Mimica amesema EU itatoa Euro  milioni 500 ili kusaidia kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto". amesema Bi. Mbise.
Kamishna huyo wa EU, alikutana na kujadiliana na makampuni makubwa ya kibinafsi ili kuona jinsi sekta binafsi inavyofanya shughuli zake hapa nchini na ziara hiyo ilimuwezesha pia kukutana na viongozi wa asasi za kiraia hapa nchini.
 Kamishna wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) anayeshughulikia mahusiano ya Kimataifa na Maendeleo, Mhe. Neven  Mimica, (kushoto), akiwa na balozi wa EU nchini, Mhe.Roeland van der Geer, wakati amkizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa ziara yake ya siku mbili nchini Novemba 3, 2017.(PICHA NA HABARI/K-VIS BLOG;Khalfan Said)
 Mhe. Mimica, akipokewa na Kaimu Mkurugezni Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, (TPA), Bw. Lazaro twange, alipotembelea bandari ya Dar es Salaam, Novemba 3, 2017. EU ni mdau mkubwa katika kjuisaidia TPA kuimarisha miundombinu yake.
 Mhe. Mimica akizun gumza na uongozi wa juu wa TPA.
 Mhe. Mimica akipeana mikono na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Mhe. Dotto James, baada ya kusaini makubaliano ambapo EU itatoa Euro milioni 50 kusaidia usambazaji umeme vijijini. Takriban vijiji 3,000 kote nchini vitafaidika na msaada huo. Serikali inapambana kuwafikishia umeme wana vijiji wa vijiji 12,000 a,mbavyo bado havijapata umeme na mpango huu umepangwa kukamilika 2020.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Usajili Vitambulisho vya Taifa watinga Manyara, Singida

$
0
0
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeanza zoezi la usajili wa watu katika wilaya zote za mikoa ya Manyara na Singida ambalo linalenga kuwapatia Vitambulisho vya Taifa. 

Kuwapatia Vitambulisho wananchi kutasaidia kutambulika pale wanapotaka kugawiwa pembejeo za Kilimo, kupata leseni za udereva na biashara, kusajili namba za Simu, kumiliki Ardhi, kupata mikopo, kufungua akaunti benki na matumizi mengineyo yanayohitaji utambulisho.

Mratibu wa Usajili wa mikoa ya Manyara na Singida, Thomas William ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara amesema watu wengi wanajitokeza kusajiliwa baada ya kuelimishwa kuhusu umuhimu wa Vitambulisho vya Taifa.
Wakazi wa Sinai na Magugu, Babati, Manyara wakishiriki kwenye zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa.

PROFESA MBARAWA AWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE WA MKOA WA GEITA

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisalimia wananchi wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa mkoa wa Geita unaojengwa wilayani humo kwenye sherehe zilizofanyika leo Jumamosi Novemba 4, 2017. Uwanja huo ambao utakuwa na njia yenye urefu wa kilomita 3, unajengwa na makandarasi wazalendo.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiwa na Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani ambaye ni Mbunge wa Chato wakifunua kitambaa kuashiria  uwekaji wa jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa mkoa wa Geita unaojengwa wilayani humo kwenye sherehe zilizofanyika leo Jumamosi Novemba 4, 2017. Uwanja huo ambao utakuwa na njia yenye urefu wa kilomita 3, unajengwa na makandarasi wazalendo.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiwa na Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani ambaye ni Mbunge wa Chato wakifunua kitambaa kuashiria  uwekaji wa jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa mkoa wa Geita unaojengwa wilayani humo kwenye sherehe zilizofanyika leo Jumamosi Novemba 4, 2017. Uwanja huo ambao utakuwa na njia yenye urefu wa kilomita 3, unajengwa na makandarasi wazalendo.


Wabunge wa Mkoa wa Geita wakipanda mti wakati wa sherehe za   uwekaji wa jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa mkoa wa Geita unaojengwa wilayani humo kwenye sherehe zilizofanyika leo Jumamosi Novemba 4, 2017. Uwanja huo ambao utakuwa na njia yenye urefu wa kilomita 3, unajengwa na makandarasi wazalendo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiwa na Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani ambaye ni Mbunge wa Chato pamoja na viongozi waandamizi wa Wizara na mkoa wakikata utepe kuashiria  uwekaji wa jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa mkoa wa Geita unaojengwa wilayani humo kwenye sherehe zilizofanyika leo Jumamosi Novemba 4, 2017. Uwanja huo ambao utakuwa na njia yenye urefu wa kilomita 3, unajengwa na makandarasi wazalendo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mhandisi Patrick Mfugale (kushoto) akipata maelezo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa mkoa wa Geita unaojengwa wilayani Chato. Uwanja huo ambao utakuwa na njia yenye urefu wa kilomita 3, unajengwa na makandarasi wazalendo.


MAMA SAMIA SULUHU ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI YA KUCHANGIA MAFUNZO YA WAUGUZI NA WAKUNGA

$
0
0


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu amesema kuwa moja ya chanzo kikubwa cha vifo vya akina mama wakati wa kujifungua ni kutokana na kutokwenda kujifungua kwenye vituo vya afya.
Hayo ameyasema leo wakati matembezi ya Hisani yenye lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kugharamia mafunzo ya uuguzi na ukunga na kusema sababu kubwa ji ni kukoseakana kwa wataalamu wa kuwahudumia akina mama katika vituo wanapokwenda kujifungua.
Mama Samia amesema ushiriki mkubwa baina ya Amref na serikali katika kuhakikisha wanatoa mafunzo kwa wakunga na mpango huo utasaidia katika kuongeza wataalamu kwenye vituo.
Katika matembez hayo mama Samia ameweza kuwa balozi wa wakunga ikiwa ni baada ya kushiriki kwenye matembezi kwa mara ya pili mfululizo pia ameweza kutoa cheti cha ushiriki kwa makampuni na taasisi mbalimbali.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu akimkabidhi cheti cha ushiriki kwa Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu na Ushauri wa Kiufundi wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya  Dkt Aifena Mramba wakati wa matembezi ya Hisani yenye lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kugharamia mafunzo ya uuguzi na ukunga yaliyofanyika leo Jijini Dar es salaam.
   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu akiwa sambamba na Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee wakiwa katika matembezi ya Hisani yenye lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kugharamia mafunzo ya uuguzi na ukunga yaliyofanyika leo Jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkaazi wa AMREF Florence Temu baada ya kumalizika kwa matembezi ya Hisani yenye lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kugharamia mafunzo ya uuguzi na ukunga yaliyofanyika leo Jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu akipokea zawadi kutoka kwa mwakilishi wa chama cha wakunga ikiwa ni baada ya kukubali kuwa balozi wa Wakunga.

 Wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wakionyesha furaha baada ya kumaliza kwa matembezi ya Hisani yenye lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kugharamia mafunzo ya uuguzi na ukunga yaliyofanyika leo Jijini Dar es salaam.

Wafanyakazi mbalimbali wa asasi za kiraia.
Picha zote na Zainab Nyamka.



WATANZANIA WASOGEZEWA MBELE FURSA ZA UWEKEZAJI NA MAENDELEO BANK

$
0
0
Wito umetolewa kwa wananchi kote nchini kuweza kujijengea utamaduni wa kuwekeza katika mfumo wa hisa na hasa katika hisa za Benki ya Maendeleo 

Wito huo kwa umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo, Ibrahim Mwangalaba jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kusogezwa mbele kwa zoezi lao la kuuza hisa za benki hiyo.Mwangalaba alisema njia kubwa ya kuwasaidia wananchi katika kujikwamua kimaisha ni kuchangamkiakia fursa zinazojitokeza ikiwemo ya kununua hisa za benki hiyo.Zoezi la uuzwaji wa hisa za benki hiyo ambalo lilianza Septemba 21, mwaka huu na lilikuwa limalizike leo sasa litandelea hadi Desemba 4, mwaka huu ili Watanzania wengi waweze kunufaika nalo.

Aliongeza kuwa lengo lao ni kuuza hisa zaidi ya mil.17 kwa Watanzania wapatao 170,000 kutoka mikoa yote ya Tanzania.Benki ya Maendeleo ni ya Watanzania wote, hivyo tumeona ni vema zoezi hilo lifanyike nchi nzima kwani awali tulikuwa tayari tumewafikia Watanzania kutoka mikoa 13 pekee na sasa tutatumia muda ulioongezwa kufika mikoa yote," alisema Mwangalaba.

Hisa moja inauzwa kuanzia sh.600 na kima cha chini cha kumiliki hisa ni 100.

MRADI WA UJENZI WA JENGO LA ABIRIA LA TATU UMEKAMILIKA KWA ASILIMIA 66-SERIKALI

$
0
0
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa (alietangulia) akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wakitembelea mradi wa jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha,Julius Nyerere leo jijini Dar es Salaam.


Serikali imesema mradi wa ujenzi wa jengo la abiria la tatu  umekamilika kwa asilimia 66 na kwamba mradi huo utakamilika Septemba, mwakani kama ilivyopangwa kwa kuwa kwa saasa hakuna kikwazo chochote.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Ujenzi), Elias Kwandikwa wakati alipotembelea mradi huo leo, jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa serkali imeshamlipa mkandarasi fedha anazodai na kwa sasa hawana deni.


"Awamu hii ya pili tunajenga uwanja huu kwa fedha zetu za ndani, hii ni ishara tunaelekea kuzuri kwamana itafika mahali tutakuwa na miradii kama hii kwa fedha zetu wenyewe," amesema Kwandikwa.
Msimamizi wa Mradi huo  Mhandisi,Barton Komba(kulia) akimfafanulia jambo Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa wakiwa kwenye eneo la mradi huo leo jijini Dar es Salaam.


LIONS CLUB OF DAR ES SALAAM TANZANITES PROMOTES PEACE VIA ART

$
0
0
 The winner from  International School of  Tanganyika (IST) Sreelakashmi Jayasankaran (11).

The Lions club of Dar es Salaam Tanzanites organized a Peace Poster competition on saturday 4.11.2017. The Lions Club International focuses on this activity to promote peace in the world for the past 30years. The event organized by Lions Club of  Dar es Salaam Tanzanites, 2 schools participated - The Aga Khan Mzizima Secondary School and The International School of Tanganyika.
They had 20 participants present their master pieces, which were judged by Mr. Paul Ufford (UNICEF member), Mr. Muzu Suleimanji (a renowned artist from Tanzania) and Mr. Pranay Shah a Professional from the Digital Media World- DTP).

It was a breathtaking moment to see the beautiful art works on display, which clearly portrayed the talent of our future generation – tomorrow’s leaders.

Each art work uniquely spoke about how important it is to them to have a peaceful world to live in, where everyone, every religion, caste, color and creed lived with love, peace and harmony.

The Peace Posters chosen here will go for further competition to the Lions District and Lions Club International that is in Chicago USA. The Grand Prize winner chosen in the International has a chance of winning up to 5000USD- This finale winner will be announced in February 2018.

The winners of the local level competition, from International School of Tanganyika was Sreelakashmi Jayasankaran and the winner from Aga Khan Mzizima Secondary School was Magenta Jumwa . We wish them all the best for further competition.

RC WA MTWARA AMUAGIZA MKURUGENZI WA BODI YA KOROSHO NA MENEJA WA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA KUANDIKA BARUA YA KUJIELEZA KWANINI WALIIDANGANYA OFISI YAKE.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amemuagiza Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho CBT Hassan Jarufu pamoja na Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika MAMCU Kuhakikisha wanaandika Barua ya Kutoa Maelezo kwa nini Waliidanganya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuhusiana na Mkataba, Idadi ya Ununuzi wa Magunia ya Kubebea Korosho katika Kikao Kilichoketi Novemba,mosi  Mwaka huu.


Katika Kikao hicho Bodi ya Korosho Kupitia MAMCU walisema, wameagiza magunia Million1 kupitia Kampuni ya DIRMAN HOLDING LTD na Ndipo mkuu wa Mkoa akaagiza Kuletewa mkataba Huo na kubaini kuwa Baadhi ya wajumbe wa Mamcu Hawaujui Mkataba na Haujulikani Thamani yake laki pia Mkataba ni magunia Laki6.5 na sio Million1 walizozisema katika kikao Hicho.Hata hivyo magunia hayo mpaka sasa hayajulikani idadi kamili iliyoletwa

Katika Mkutano na waandishi wa Habari Ofini kwake, Mkuu wa mkoa Byakanwa amesema kutokana na Udanganyifu huo Ofisi yake imeamua Bodi ya Korosho isilipe Pesa yeyote kwa kampuni ya DIRMA HOLDING LTD kwa kushindwa kuleta magunia kwa wakati,kwani ilitakiwa kuleta Septemba 30/2017lakini mpaka sasa bado hajakamilisha na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya Mzabuni huyo.

Aidha Ameiagiza Bodi kuhakikisha inasambaza magunia ndani ya Kipindi cha Wiki Mbili zijazo ili malalamiko ya wakulima yaweze kuondoka.

Kutokana na Udanganyifu Huo Mkuu wa Mkoa anatarajia Kuunda kamati ili kuweza kuchunguza taratibu zinazotumika kuingia mikataba na wote waliohusika na kamati hiyo itaishauri nini cha kufanya kwa wahusika.

UZINDUZI WA UPIMAJI WA AFYA WATOTO WA KITUO CHA MAZIZINI UNGUJA.

$
0
0
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akitoa hutuba yake wakati wa hafla ya Uzinduzi wa huduma maalum ya Upimaji wa Afya za Watoto iliyofanyika leo katika Kituo cha kulelea Watoto Mazizini Wilaya ya Magharibi “A” Unguja Mkoa wa Mjini Magharibi (kulia) Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Vijana,Wanawake na Watoto Mhe.Moudline Cyrus Castico na Mke wa Balozi Mdogo wa China Mhe.Mama Liu Jie (kushoto) , [Picha na Ikulu.] 04/11/2017.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akimpakata Mtoto Yussuf Abdalla Abdilah akifanyiwa uchunguzi wa Dr.Qin Qin (kulia) kutoka china akiwa ni miongoni mwa Madakatri wa kujitolea akati wa hafla ya Uzinduzi wa huduma maalum ya Upimaji wa Afya za Watoto iliyofanyika leo katika Kituo cha kulelea Watoto Mazizini Wilaya ya Magharibi “A” Unguja Mkoa wa Mjini Magharibi,[Picha na Ikulu.] 04/11/2017.
Mke wa Balozi Mdogo wa China aliyepo Zanzibar Mama Liu Jie (katikati) akimpakata mtoto wakati wa hafla ya Uzinduzi wa huduma maalum ya Upimaji wa Afya za Watoto iliyofanyika leo katika Kituo cha kulelea Watoto Mazizini Wilaya ya Magharibi “A” Unguja Mkoa wa Mjini Magharibi,(kulia) Dr.Guo Yulan akiendelea na zoezi hilo,wakiwepo na Viongozi wengine Dr.Wang Hao,Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Vijana,Wanawake na Watoto Mhe.Moudline Cyrus Castico,Katibu Mkuu Bi.Fatma Gharib Bilali na Naibu Wazuiri wa Afya Mhe,Harusi Said Suleiman, [Picha na Ikulu.] 04/11/2017.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na Mke wa Balozi Mdogo wa China aliyepo Zanzibar Mama Liu Jie (katikati) pamoja na Viongozi wengine wakiwa picha ya pamoja na Madaktari wa Kichina wakati wa hafla ya Uzinduzi wa huduma maalum ya Upimaji wa Afya za Watoto iliyofanyika leo katika Kituo cha kulelea Watoto Mazizini Wilaya ya Magharibi “A” Unguja Mkoa wa Mjini Magharibi,[Picha na Ikulu.] 04/11/2017.

TUME YA UCHAGUZI YATEUA MADIWANI 2 WA VITI MAALUM

MBEGU YA MAHINDI YA WEMA 2109 NA MIHOGO ILIYOTOLEWA NA COSTECH WILAYANI MBOGWE MKOANI GEITA KUONGEZA CHACHU YA KILIMO

$
0
0
Na Dotto Mwaibale, Mbogwe, Geita.

MAKAMU Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita, Nsika Sizya amesema mbegu bora ya mahindi ya WEMA 2109 na mihogo aina ya Mkombozi waliyokabidhiwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB) itaongeza chachu ya kilimo wilayani humo.

Sizya aliyasema hayo wilayani humo jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi na kukabidhi mbegu bora za Mahindi ya Wema yanayostahimili ukame na mihogo kwa ajili ya mashamba darasa kwa wakulima wa vijiji vinne vya Mponda kilichopo Kata ya  Luganga, Kijiji cha Ushetu kilichopo Kata ya Ushirika, Kijiji cha Lwazeze kilichopo Kata ya Ngemo na Kijiji cha Iponya kilichopo Kata ya Iponya.

Alisema changamoto kubwa waliyokuwa nayo wakulima katika Halmshauri hiyo ni kukosekana kwa mbegu bora za mihogo na mahindi ambapo alisema kwa kupata mbegu hizo kutaongeza ari na chachu ya kilimo kwa wananchi.

Aliishukuru CSTECH na OFAB kwa kuwapelekea mradi huo katika wilaya hiyo na kuupokea kwa shangwe kwa kuzingatia kuwa mihogo ni zao la biashara na chakula ambapo aliwataka wananchi kubadilika na kufanya kilimo chenye tija kama wataalamu wanavyowaelekeza.
 Mkulima wa Kijiji cha Lwazeze, Charles Kangai akichimba mashimo kwa ajili ya upandaji mbegu ya mahindi ya WEMA.
 Mtafiti wa Mazao ya Mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani Kagera, Jojianas Kibula, akielekeza jinsi ya upandaji wa mbegu hiyo ya mihogo aina ya Mkombozi.
 Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita, Nsika Sizya, akipanda mbegu ya mihogo katika shamba darasa katika Kijiji cha Iponya.

Mshauri wa Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange, akipanda mbegu ya mihogo aina ya Mkombozi kwenye shamba darasa katika Kijiji cha Iponya.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS DKT. MAGUFULI AKIWA MAPUMZIKONI CHATO MKOANI GEITA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia picha kwenye simu pamoja na Mama yake mzazi Suzana Magufuli (katikati) pamoja na mdogo wake Monica wa kwanza (kushoto). Rais Dkt. Magufuli yupo mapumzikoni katika Kijiji cha Lubambangwe Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia picha kwenye simu aliyokuwa akioneshwa na Mama yake mzazi Mama Suzana Magufuli nyumbani kwao katika kijiji cha Lubambangwe Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza radio pamoja na Mama yake mzazi Suzana Magufuli wa pili kutoka (kushoto) mdogo wake Monica wa kwanza (kushoto), na Dada yake Asteria wa kwanza (kulia). Rais Dkt. Magufuli yupo mapumzikoni katika Kijiji cha Lubambangwe Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza radio pamoja na Mama yake mzazi Suzana Magufuli wa pili kutoka (kushoto) mdogo wake Monica wa kwanza kushoto. Rais Dkt. Magufuli yupo mapumzikoni katika Kijiji cha Lubambangwe Chato Mkoani Geita. PICHA NA IKULU

WANAFUNZI WATAKIWA KUTUMIA MITANDAO KUPATA MAARIFA

$
0
0
Wanafunzi wa Chuo cha Kodi (ITA) jijini Dar es Salaam, wametakiwa kutumia vyema teknolojia ya mawasiliano hususan mitandao ya kijamii kujifunza ili kupata maarifa badala ya kuitumia kwa mambo ambayo hayatawasaidia katika masomo.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo wakati akiwakaribisha wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho kwa mwaka wa masomo 2017/18.Amesema vijana wengi wanatumia mitandao ya kijamii kwa masuala ya kijamii kwa kiwango kikubwa kuliko kuitumia kujifunza na kupata maarifa kwa mambo ambayo yatawasaidia kukuza kiwango cha elimu.

“Elimu ipo kila mahali siku hizi: katika vitabu, mitandao na tuna mambo mengi ambayo yanasaidia sana kujifunza tofauti na ilvyokuwa miaka 30 iliyopita. Ni wajibu wa wanafunzi kuitumia vyema mitandao hususan simu kujifunza na kupata maarifa”, alisema Prof. Jairo.

Mkuu huyo wa chuo amesema kwamba chuo cha kodi kinatumia mfumo wa kujenga umahiri kwa mwanafunzi ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi wa hali ya juu na ambao umelenga kumuwezesha mwanafunzi kujifunza badala ya kufundishwa. Ameongeza kwamba mfumo huo ndio utaratibu unaotumika ulimwenguni ili mwanafunzi anapohitimu awe na uwezo wa kujua nini cha kufanya katika fani yake na kwa Chuo cha Kodi ajue jinsi ya kukusanya kodi.
Wanafunzi wapya katika Chuo cha Kodi wakifuatilia kwa makini maelezo ya Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo 
Mkuu wa Chuo cha Kodi (ITA) Prof. Isaya Jairo (aliyesimama) akizungumza na wanafunzi wapya waliojiunga na Chuo hicho kwa muhula wa masomo wa kuanzia 2017/18. Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Huduma za Fedha Emmanuel Foya na Kaimu Naibu Mkuu wa Chuo Utawala, Fedha na Mipango Emmanuel Masalu. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs) 
Wanafunzi wapya katika Chuo cha Kodi wakifuatilia kwa makini maelezo ya Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo 


MKUTANO WA WATAALAMU WA SEKTA YA MAENDELEO YA JAMII KUFANYIKA DODOMA KUANZIA NOVEMBA, 2017

TASWA FC YAIADHIBU POLISI FC MABAO 5-0 UWANJA WA UHURU

$
0
0
  MSHAMBULIAJI wa Taswa Fc, Said Seif (kushoto) akiruka kumkwepa beki wa Polisi Fc, Andew Thomas, wakati wa mchezo wa kirafiki katika Maadhimisho ya 10 ya Mtandao wa Polisi yaliyoanza jana Nov 4 katika Uwanja wa Uhuru Dar esSalaam, yakitarajia kumalizika Nov 9 mwaka huu. Katika mchezo huo Taswa Fc ilishinda mabao 5-0. Picha na Muhidin Sufiani.


 DCP Mary Nzuki wa Jeshi la Polisi, akimkabidhi Ngao ya ushindi Nahodha wa Taswa Fc, Willbert Moland, baada ya Taswa kuibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Polisi katika mchezo wa kirafiki wa Maadhimisho ya 10 ya Mtandao wa Polisi yaliyoanza jana Nov 4 katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, yakitarajia kumalizika Nov 9 mwaka huu. Picha na Muhidin Sufiani.

WAZIRI UMMY AZINDUA MAABARA HAMISHIKA ZA TFDA

MAGAZETI YA JUMAPILI LEO NOVEMBA 5,2017

DK. KIGWANGALLA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA ZIWA MANYARA NA KUKAGUA SHUGHULI MBALIMBALI ZA UHIFADHI NA UTALII

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Noelia Myonga kuhusu hifadhi hiyo alipoitembelea jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akiongozwa na Mhifahdi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Noelia Myonga kwenda kuangalia kivutio cha Maji ya Moto ya Asili ndani ya hifadhi hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akigusa maji ya moto ya asili ambayo ni kivutio cha kipekee cha utalii kilichopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. Maji hayo yanakadiriwa kuwa na nyuzi joto 80 ambapo imeelezwa kuwa baadhi ya watalii huweza kuchemsha mayai katika maji hayo. Nyuma yake anayeshuhudia ni Mhifadhi Mkuu wa hifadhi hiyo, Noelia Myonga.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akionyeshwa maeneo ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara na Mhifadhi Mkuu wa hifadhi hiyo, Noelia Myonga alipoitembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. 
Ndege aina mbalimbali wanapatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.
Mtoto wa Tembo katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Maginga Business Holdings Company Ltd yadaiwa kukwamisha ujenzi wa barabara ya Namelock –Sunya

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo (katikati) akimskiliza Meneja wa TARURA Wilaya ya Kiteto Eng.Gerald Matindi akielezea hali ya ujenzi wa barabara ya Namelock-Sunya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(kwanza kushoto) akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magesa, Mbunge wa Kiteto Mhe.Emanuel Papiyani na Mwenyekiti wa Ccm Wilaya wakikagua ujenzi wa barabara ya Namelock –Sunya eneo linalojengwa na Mkandarasi Maginga Business Holdings Company Ltd ya mjini Dodoma.

Muonekano wa barabara ya Namelock –Sunya eneo linalojengwa na Mkandarasi Maginga Business Holdings Company Ltd ya mjini Dodoma ambaye yuko site kwa miezi minne sasa lakini hali ya ujenzi wa barabara hiyo ikiwa hairidhishi.
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa kata ya Engusero –Wilayani Kiteto wakati wa ziara yake ya kazi Wilayani hapo.

Celebrate Tanzania Independence Day and Annual Fundraising Dinner in Oakland - California, Dec 9th.

$
0
0
Tanzanian Community Organization (TCO) in the BayArea cordially invites you to celebrate & commemorate the Independence of Tanzania 56th Anniversary and Annual Fundraising Dinner. It will be a time to celebrate all aspects of Tanzanian culture, delicious East African food, music, dancing, and great Tanzanian & AfroBeats Music & More... KARIBUNI SANA.
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images