Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110031 articles
Browse latest View live

HOSPITALI YA AGA KHAN YAANZA KUTOA BURE HUDUMA YA UPANDIKIZAJI WA MATITI KWA AKINA MAMA

$
0
0
Hospitali ya Aga Khan imeanza kutoa bure huduma ya kupandikiza matiti kwa akina mama waliopatwa na magonjwa mbalimbali yaliyowapelekea kukatwa kwa kiungo hicho muhimu, ikiwemo wale waliokatwa kutokana na magonjwa ya Kansa, ukatili na kuungua moto.

Akizungumza na waandishi wa habari leo hii Jijini Dar es Salaam, Daktari bingwa wa kitengo cha upasuaji katika hospitali ya Aga Khan, Dr. Aidan Njau amesema huduma iliyoanza leo ni kuhudumia mgonjwa mmoja mmoja ili kusaidia wanawake wengi wenye matatizo hayo ambao wamekuwa wakiishi na maumivu makali hata kujisikia vibaya katika jamii .

“Kwa kuanzia tunaanza na wale wanawake waliokatwa matiti yao, tutatoa nyama kwenye sehemu yake ya mwili na kuipandikiza kwenye sehemu iliyokatwa na kuufanya muonekano wake urudi kama ulivyokuwa" amesema Dk. Njau.

Amesema huduma hiyo, itawafanya watanzania kushuhudia wanawake wakipandikizwa matiti jambo ambalo halijawahi kutokea hapa nchini na kuwaasa wanawake wenye matatizo hayo wajitokeze hospitalini hapo kwa wingi kwa ajili ya kupatiwa huduma hii ya bure.

Amesema, upasuaji huo utafanywa na madaktari wawili ambao ni Daktari bingwa wa kitengo cha upasuaji katika hospitali ya Aga Khan, Dr. Aidan Njau na Daktari bingwa Edwin Mrema kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili wote wakiwa na lengo la kurudisha furaha kwa wanawake wenye matatizo haya waliyokwisha ipoteza.
 Daktari bingwa wa upasuaji wa Hospitali ya Agakhan, Dkt Aidan Njau (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari juu ya huduma ya Upandikizaji wa Matiti kwa wanawake waliokatwa matiti kutokana na majanga mbalimbali ikiwemo karatani ya matiti kulia ni daktari bingwa wa upasuaji kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt Edwin Mrema. 
Dkt Edwin akiwa na baadhi ya wataalam wa magonjwa mbalimbali ya upasuaji

DK.SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI WA OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na Uongozi wa  Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, katika  kikao cha siku moja cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai- Septemba 2017 kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja.

Waziri wa  Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mhe. Mohamed Aboud Mohamed (katikati) alipowasilisha Muhtasari wa  Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai- Septemba 2017, wakati wa kikao cha siku moja cha  Uongozi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)wengine ni  Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abdulhamid Yahya  Mzee (kulia) na Naibu Waziri Mhe.Mihayo Juma N'hunga.

 Baadhi ya Wakurugenzi wa Idara mbali mbali za  Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais  wakimsikiliza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani),alipozungumza na Uongozi wa Ofisi hiyo katika  kikao cha siku moja cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai- Septemba 2017 kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja.

 Viongozi mbali mbali katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais  wakimsikiliza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani),alipozungumza na Uongozi wa Ofisi hiyo katika  kikao cha siku moja cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai- Septemba 2017 kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja. (Picha na Ikulu)

MAVUNDE,LUSINDE NA KUNAMBI WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI NA KUELEZEA MIKAKATI YA DODOMA MPYA.

$
0
0
Dodoma Mjini Anthony Mavunde wampongeza Mh. Rais Dk.John Pombe Joseph Magufuli kwa uamuzi wake kuhamishia Makao makuu ya Serikali Dodoma na hivyo kuongeza fursa za kiuchumi katika mkoa wa Dodoma kupitia uzalishaji wa bidhaa na huduma mbalimbali zitakazotolewa.

Wakizungumza leo katika kipindi cha 360 cha Clouds TV wamesema uamuzi huo ni fursa muhimu kwa wanadodoma ni vyema wakaitumia ipasavyo.Aidha wamempongeza Mh. Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kuivunja CDA na kurudisha mamlaka ya utawala wa ardhi chini ya Manispaa ya Dodoma na kubadilisha mfumo wa umiliki ardhi kutoka katika upangaji(Lease Ground) kwenda kwenye mfumo wa hati ya umiliki.

Wamesema kupitia mfumo huo Dodoma itapata fursa ya kuvutia zaidi wawekezaji wa muda mrefu tofauti ilivyokuwa awali.

Aidha Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi ameelezea mipango mikubwa ya ukuzaji mji wa Dodoma ikiwemo uharakishwaji wa huduma ya vibali vya ujenzi,upimaji wa mae uboreshwa wa miundombinu na huduma za kijamii ili viende sambamba na ukuaji wa haraka wa mji wa Dodoma.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde na Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde akizungumza katika kipindi cha 360 cha Clouds TV.

WALK FOR AFRICAN MOTHERS THIS SATURDAY, 4TH NOVEMBER

$
0
0
Nurse Students benefited through the SU4AM programme at Makole Health Facility in Dodoma Region. In 2017/19 the programme aims to raise a minimum of Tsh 300million to support training of 400 nurse students that shall include midwifery Certificate level as well as upgrading midwifery course

With the theme “More Midwives for Safe Delivery!” Amref Health Africa Tanzania in Partnership with Bank M has organized a ‘Stand up for African Mothers’ Charity Walk which is expected to take place this Saturday, November 4thfrom 6.30-10.00am at the Green Grounds Oysterbay, Dar es Salaam. The Stand up for African Mothers (SU4AM) programme has been running for the past seven years with the major aim of training more midwives for safe delivery. The Vice President Hon. Samia Suluhu will be leading a four (4) km walk which will start and finish at the Green Grounds Oysterbay.

Speaking about the preparations for this year’s SU4AM Charity Walk, Amref Health Africa Tanzania Country Director Dr. Florence Temu said, “The Stand Up for African Mothers is an international programme launched by Amref Health Africa in October 2011 to draw attention to the plight of African mothers and to mobilize citizens worldwide, to support African Mothers get the basic medical care they need during pregnancy and childbirth. In 2017/18 up to 2018/19 the programme aims to raise a minimum of Tsh300 million to support training of a total of 400  nurse students  that shall include midwifery Certificate level as well as upgrading midwifery course at Diploma level. This will eventually contribute towards the reduction of maternal and child mortality in Africa. Let us Stand up for African Mothers; contribute Tanzanian Shillings 25,000/= or more that will directly support the training of midwives. You will be provided with a ticket and t-shirt for the walk, you are all welcome”.


She also thanked Bank M once again for coming on board as the main sponsor. “Bank M has consistently supported thisprogramme for five years.  We are extremely grateful to Bank M for their ongoing support, solid contribution to improving the lives of Tanzanians across the country and for partnering with us to help create lasting health change in Africa. We call upon other supports from different areas to join us and contribute to train more midwives for safe delivery,” concluded Dr. Temu.We also thank many other partners who have joined this noble course in different ways, including individuals, residences and citizens of the United Republic of Tanzania, she added.

Bank M’s CEO, Ms. Jacqueline Woiso commented that Bank M’s partnership with Amref Health Africa has been a great milestone in achieving our Corporate Social responsibility initiatives. “This project, which aims to improve maternal health services throughout Tanzania, reflects our bank’s mission to support the community and promote a healthy and sustainable workforce in the country. Bank M will continue supporting this cause as we believe in the expertise and accountability of Amref Health Africa and more importantly, we believe in the impact of this project on the vulnerable section of our society” said Ms. Woiso.

MAGAZETI YA JUMAMOSI LEO NOVEMBA 4,2017

KUMBUKUMBU YA MIAKA 5 YA KIFO CHA MARTHA TUNU PATRICK MOMBO

$
0
0
LEO, NOVEMBA 4,  NI  MIAKA MITANO  TANGU MPENDWA WETU MARTHA TUNU PATRICK MOMBO ULIPOTANGULIA MBELE YA HAKI NA KUTUACHIA MAJONZI NA PENGO LISILOZIBIKA DAIMA. KAMWE HATUWEZI KUSAHAU UPENDO WAKO, BUSARA ZAKO NA UCHESHI WAKO               

 UNAKUMBUKWA SANA NA FAMILIA NA UKOO WA BALOZI PATRICK CYPRIAN MOMBO, NDUGU NA JAMAA ZETU WOTE   

 RAHA YA MILELE UMPE, EE BWANA NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE. ASTAREHE KWA AMANI. AMINA

Kipindi cha Maoni ya Watanzania MIAKA MIWILI YA RAIS DK MAGUFULI

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA


NKAMBAKU AKANA KUHAMA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM).

BOT YAWAJENGEA UWEZO WA KUTAMBUA NOTI BANDIA WATU WENYE ULEMAVU WA KUTOSIKIA WILAYANI CHATO

$
0
0
NA JOEL MADUKA,CHATO.

Benki kuu ya Tanzania (BOT)imekutana na kundi la watu wenye ulemavu wa kutokusikia na wale ambao hawaoni Wilayani Chato lengo likiwa ni kuwapatia na elimu ya utambuzi wa Noti bandia Wilayani humo.

Akizungumza kwenye semina ambayo imefanyika kwenye ukumbi wa KKKT Wilayani Humo,Meneja msaidizi wa idara ya uhusiano wa BOT, Vicky Msina alisema elimu wanayoitoa imelenga kuwawezesha viziwi kutambua alama za usalama zilizopo katika noti ili kuzitofautisha na noti bandia wanapokuwa katika shughuli zao kwani mtu yeyote akikutwa na noti bandia ni kosa la jinai, hivyo wanawapa mafunzo ili wasikumbwe na kadhia hiyo.

“Ni muda sasa walituomba kuwapa mafunzo na hii ni kutokana na wengi wao kutokujua noti bandia wamekuwa wakijikuta wanabambikiwa na pia wanapo kwenda benki kupeleka fedha zao wahudumu huwadharau na wakati mwingine kwa wale wanao kwenda kuchukua fedha hupatiwa noti chafu jambo ambalo lilitusukuma kuwaelimisha juu ya hatua za kufuata ilikupatiwa haki zao za msingi kwenye huduma hizo,”alisema Msima.

Mwenyekiti wa Kituo cha Sanaa na Utamaduni kwa Viziwi Tanzania (Kisuvita), Habibu Mrope alisema kuna tatizo kubwa la kutotambua noti bandia kwa Walemavu hali ambayo imechangia kuwarudisha nyuma kwani wanapokutwa na noti hizo huchukuliwa hatua za kisheria.
Bw,Patrick Fata ambaye ni Mhelimishaji kutoka BOT akielekeza na kutoa elimu namna ambavyo unaweza kutambua Noti bandia. 
Bw,Patrick Fata ambaye ni Mhelimishaji kutoka BOT,akisisitiza swala la alama za fedha ambazo zinakuwepo kwenye noti. 
Kifaa ambacho kinatumika kuangalizia noti bandia na ile ambayo ni ya harari. 
Noti ambazo zinakuwa zimeharibiwa zikiwa kwenye mafungu fungu lenye rangi nyekundi ni elfu kumi na yenye rangi ya blue ni elfu tano. 


DC SHINYANGA AKUTANA NA WAKULIMA WA PAMBA SHINYANGA VIJIJINI KUHAMASISHA KILIMO CHA KISASA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro jana Ijumaa Novemba 3,2017 amewatembelea wakulima wa zao la pamba katika kijiji cha Sayu kata ya Pandagichiza halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kuwahamasisha kulima zao hilo kwa njia za kitaalamu/kisasa ili kilimo hicho kiwe na tija kwa ajili ya kujikomboa kiuchumi.

Akizungumza katika kikao na wananchi wa kijiji hicho ambacho ni maarufu kwa kilimo cha pamba,Matiro aliyekuwa ameambatana na wataalamu wa zao la pamba,aliwataka wakulima wa zao hilo wilayani humo kulima kisasa kwa kufuata kanuni 10 za kilimo ikiwemo kulima kwa kutumia kamba.

Alisema wananchi katika wilaya hiyo wamekuwa mstari wa mbele katika kulima zao la pamba lakini wamekuwa hawapati faida kutokana na kulima njia zisizo za kitaalamu.

“Tunataka kufanya kilimo biashara ili kiwe na tija,hatupati mazao ya kutosha kutokana na kutolima kitaalamu,naomba mwaka huu tuwasikilize wataalamu wetu wanatuambia nini,nataka tubadilishe maisha yetu kupitia pamba”,alisema Matiro
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sayu kata ya Pandagichiza leo akiwahamasisha kufuata njia za kisasa kulima zao la pamba-Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisisitiza wananchi kulima mazao ya biashara pamoja na yale ya chakula
Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Charles Maugira akizungumza katika kikao hicho
Mkaguzi wa pamba wilaya ya Shinyanga,Benjamini Madama akitoa elimu kwa wakulima wa pamba juu ya njia ya kisasa ya kulima zao hilo
Mkaguzi wa pamba wilaya ya Shinyanga,Benjamini Madama akionesha kamba zinazotakiwa kutumika katika kilimo cha pamba.

WANAWAKE BARANI AFRIKA WAKUTANA TANZANIA KUJADILI AMANI YA BARA LA AFRIKA

$
0
0
Aliyekuwa katibu Mkuu wa Mkutano wa Beijing , Getrude Mongela akizungumza wakati wa mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Muasisi wa Mkutano wa Wanawake juu ya Amani na kutatua matatizo Barani Afrika, Dkt. Basirat Nahibi akizungumza juu ya suala la wanawake wa bara la Afrika kukutana kujadili na kuandaa upatanishi juu ya mgogoro wa kisiasa unaondelea nchini Kenya.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko Kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Balozi Amina Salum Ali akizungumza katika mkutano huo kwa niaba ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu
Mwanahabari Mwanamke mkongwe nchini Radhia Mwawanga akichangia hoja katika mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana
Mhariri wa jarida la mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani afrika, Fatma Othman Moma akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Mwaka mmoja na nusu sasa, Kitilya na wenzake waendelea kusota rumande

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii. 

 Ikiwa ni mwaka mmoja na nusu sasa tangu kufikishwa mahakamani kwa aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, (TRA) Harry Kitilya na wenzake wawili upande wa mashtaka umeieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa shauli hilo bado haujakamilika.

Kitilya pamoja na aliyekuwa miss Tanzania mwaka 1996, ambaye pia alikuwa Ofisa wa benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Graham Solomon ambao walifikishwa mahakamani hapo kwa Mara ya kwanza April 1, mwaka jana wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa USD Mil.6 

Mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa kesi hiyo leo Novemba 3 ilifikishwa kwa ajili ya kutajwa ambapo Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi ameileza mahakama kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Alidai kuwa bado wanasubiri awamu ya pili ya upelelezi kutoka nchini Uingereza na kuomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi November 10, mwaka huu.

Katika kesi hiyo, washtakiwa wote wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya March 2013 na September 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola za Marekani 550 milioni  kwa  serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard Uingereza.

Pia wanadaiwa kuwa  March 2013 jijini Dar es Salaam walijipatia Dola za Marekani 6 milioni, wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa mkopo  na zililipwa kupitia  Kampuni ya Egma T Ltd.

DK. HAMISI KIGWANGALLA AMEAGIZA RASIMU YA SERA MPYA YA MISITU IKAMILIKE NDANI YA MWEZI HUU WA NOVEMBA

$
0
0
Waziri wa Maliasili, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwasili katika ukumbi wa Hoteli ya Morena mjini Dodoma jana kwa ajili ya kufungua warsha ya siku moja ya wadau sekta misitu. Warsha hiyo ililenga kujadili maboresho ya Rasimu ya Sera mpya ya Misitu na Nyuki, pamoja na changamoto na mikakati mbalimbali ya kuboresha sekta hiyo.

Na Hamza Temba - WMU
............................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ameagiza kukamilishwa haraka kwa rasimu mpya ya Sera ya Taifa ya Misitu ya mwaka 2016 ili kuwezesha upatikanaji wa Sera, Sheria na Kanuni mpya za usimamizi wa rasilimali za misitu nchini kwa ufanisi zaidi.


Ameagiza wataalamu wa Wizara hiyo kukamilisha rasimu hiyo mwezi huu wa Novemba na iwasilishwe kwake mapema mwezi ujao (Desemba) ili aweze kupata ushauri zaidi wa wataalamu wengine huru kabla ya kuwasilishwa kwenye Baraza la Mawaziri na baadaye kutungiwa Sheria na Kanuni za utekelezaji.


Dk. Kigwangalla ametoa agizo hilo jana mjini Dodoma wakati akifungua warsha ya siku moja ya wadau wa misitu iliyolenga kujadili maboresho ya Rasimu ya Sera mpya ya Misitu na Nyuki, pamoja na changamoto na mikakati mbalimbali ya kuboresha sekta hiyo.
Waziri wa Maliasili, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akizungumza wakati wa ufunguzi wa  warsha ya siku moja ya wadau sekta misitu iliyofanyika mjini Dodoma jana. Warsha hiyo ililenga kujadili maboresho ya Rasimu ya Sera mpya ya Misitu na Nyuki, pamoja na changamoto na mikakati mbalimbali ya kuboresha sekta hiyo.

“Natoa agizo mchakato huu ukamilike ndani ya mwezi huu wa 11, tarehe moja mwezi wa 12 mlete rasimu ambayo nyie wataalamu mmeridhika nayo, muiwasilishe kwangu mimi na Mhe. Naibu Waziri, na siku hiyo mtakayoiwasilisha kwetu mniletee timu ya wataalamu watakaonishauri kwenye maeneo mbalimbali.


“Pamoja na hao wataalamu washauri nataka watu wengine huru wahusike kwenye kunishauri, ili nipate picha ya watu wengine huru kabla hatujatengeneza andiko ambalo tutalipeleka kwenye kikao cha baraza la Mawaziri, waje wanishauri maeneo yanayotaji maboresho, kuongeza ubunifufu au kukazia zaidi”. Aliagiza Dk. Kigwangalla.


Waziri wa Maliasili, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mauzo wa Kampuni ya Charcoal Briquettes ltd, Abdala Seushi kuhusu majiko banifu ya mkaa muda mfupi baada ya kufungua warsha ya siku moja ya wadau sekta misitu iliyofanyika mjini Dodoma jana. Warsha hiyo ililenga kujadili maboresho ya Rasimu ya Sera mpya ya Misitu na Nyuki, pamoja na changamoto na mikakati mbalimbali ya kuboresha sekta hiyo.

Alisema amelazimika kuharakisha zoezi hilo ili Sera hiyo ikamilike haraka iweze kushughulikia changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo ikiwemo ongezeko la watu linalosababisha misitu mingi kuteketezwa kwa ajili ya mahitaji mbalimbali ya kijamii na kiuchumi kupitia shughuli za kilimo na uanzishwaji wa makazi mapya.

BOFYA HAPA KWA HABARI NA PICHA ZAIDI

WIZARA YA UJENZI YARIDHISHWA NA KASI YA JNIA-TBIII

$
0
0
WIZARA ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, imeridhishwa na ujenzi wa mradi wa jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), ambapo unatarajiwa kukamilika Septemba 2018. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya Ujenzi), Mhe. Elias Kwandikwa wakati alipotembea maendeleo ya mradi huo unaojengwa na Mampuni ya ujenzi ya Bam International ya Uholanzi.

Mhe. Kwandikwa alisema mradi huo umefikia asilimia 66, ambapo wizara imekuwa ikihakikisha mkandarasi analipwa kwa wakati ili uweze kukamilika kama ilivyotarajiwa, na kukamilika kwake kutatoa picha ya kuelekea kwenye Tanzania mpya.

“Hivi karibuni nilitembelea kiwanja cha KIA (Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro), nikaridhishwa na maendeleo ya ukarabati unaoendelea pale, na nikaona ni vyema pia kutembelea hili jengo na nimeliona na nimeridhishwa na kasi ya ujenzi unaoendelea, ninaamini kama wakandarasi walivyosema basi hadi kufikia Septemba 2018 litakuwa limekamilika kabisa,” alisema Mhe. Kwandikwa.

Hata hivyo, Mhe Kwandikwa alisema serikali inajenga awamu ya pili ya mradi huo kwa kutumia fedha za ndani, lakini pia kwa kushirikiana na wadau wengine, ambapo ni ishara nzuri kuwa siku zijazo kutakuwa na miradi mingi zaidi.

“Tunajenga mradi huu kwa fedha zetu za ndani, lakini pia kwa kushirikiana na wadau wengine, hii ni ishara nzuri kwamba sasa tunakokwenda tunao uwezo wa kuwa na miradi mingi zaidi kama hii tuliojenga kwa kutumia fedha zetu wenyewe,” alisema Mhe. Kwandikwa.

Hata hivyo, msimamizi wa Mradi huo, Mhandisi Barton Komba alisema, mkandarasi wa ujenzi huo ameshalipwa fedha zake zote, hivyo kwa sasa hadai serikali na anafanya kazi yake vizuri, ili kukamilisha na kukabidhi jengo pindi litakapokamilika. “Mpaka mwezi wa tisa mwakani utakuwa umekamilika kabisa, lakini pia jengo hili limejengwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa na litatoa huduma kwa watu wote hata ndugu zetu wenye mahitaji maalumu, ,” alisema Mhandisi Komba.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elias Kwandikwa (wa tatu kushoto) akielekea kwenye ukaguzi wa ujenzi wa jengo la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere. Wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Mtengela Hanga.
Msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), Mhandisi Barton Komba (kulia) akimwonesha kitu Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elias Kwandikwa (wa pili kulia), wakati alipotembelea na kukagua ujenzi wa jengo hilo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elias Kwandikwa (wa pili kulia), akizungumza na Mhandisi Barton Komba (wa tatu kushoto) wakati wakitoka kwenye ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa mradi wa jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.

NHIF YATOLEA UFAFANUZI MADAI YA KUKOSEKANA HUDUMA YA MATIBABU KATIKA KITUO CHA AGAKHAN, ARUSHA

MPANDA MILIMA MASHUHURI DUNIANI, JUANITO OIZARZABAL APANDA MLIMA KILIMANJARO

$
0
0
Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakijiandaa kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro.


Na Dixon Busagaga, Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

MPANDA milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal raia wa Ureno na wenzake wawili wameanza safari ya siku tano ,kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia lango la Kilema ikiwa ni aina mpya ya utalii iliyoanza kushika kasi katika hifadhi hiyo.

Hatua hiyo inatokana na jitihada za shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kueendelea kupanua wigo wa vivutio katika Hifadhi zake 16,kwa kuanzisha aina mpya ya bidhaa za utalii ili kushindana na nchi nyingine duniani katika uuzaji wa safari kwa watalii.

Miongoni mwa bidhaa hizo ni pamoja na zile zilizoanzishwa katika Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimajaro (KINAPA) ya kuzunguka mlima kwa kutumia Parachuti pamoja na kupanda Mlima kwa kutumia Baiskeli, utalii ambao umeanza kushika kasi.

Juanito Oiarzabal ambaye tayari ameweka rekodi nyingi duniani na kuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu kijulikanacho kama World Guinness Book amepanda mlima Kilimanjaro na wenzake wawili ,Eduardo Pascuaz na Ramon Abecia kwa kutumia Baiskeli .

Mkurugenzi wa Utali wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA ) Ibrahim Musa amesema Oiarzabal atakuwa Mreno wa kwanza kuweka rekodi ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia baiskeli na kwamba aina hi ya utalii na rafiki kwa mazingira ya Hifadhi.

Mkurugenzi wa kampuni ya Safari Bike Africa inayoratibu wa changamoto hii a kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli,Mario Martos amesema hatua hii ni mwanzo wa kufungua aina hii ya utali katika Hifadhi za Taifa za Arusha na Saadan.

Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kupitia Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro limeweka utaratibu wa kufanya vipimo kwa wapandaji wa Mlima kwa wanao tumia Baiskeli pia kabla ya kuanza safari ya kuelekea kileleni.

Juanito na wenzake wawili wameianza safari ya siku tano ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia baiskeli wakipita lango la Kilema ambapo wanatarajia kupita katika Kilele cha Mawenzi kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea kilele cha Uhuru.
Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu wa safari hiyo ambaye pia ni mkurugenzi wa kampuni ya Safari Bike Africa ,Mario Martos pamoja na waongoza watalii ,Ally Chuwa na Elvas Mlengwa kabla ya kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro
Eduardo Pascuaz akifunga kofia ngumu kabla ya safari ya kuelekea Kilele cha Uhuru kuanza.
Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakijiandaa kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro.

TPDC yaguswa na Maendeleo ya Jamii

$
0
0
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeanza kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii katika mwaka wa fedha 2017/2018 ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika uboreshwaji wa Sekta mbalimbali kama Elimu, Afya, Maji na Utawala Bora.

Hayo yamezungumzwa na Meneja wa Mawasiliano wa TPDC, Marie Msellemu katika tukio la kukabidhi hundi za fedha kwa ajili ya kusaidia uimarishwaji wa Chama cha Maafisa Uhusiano Tanzania pamoja na kukabidhi fedha za kuwezesha ununuzi wa mafuta na dawa kwa Chama cha Wanawake Albino cha Ndugumbi lilofanyika tarehe 03 Novemba, 2017 Makao Makuu ya TPDC.

“Leo tunayo furaha ya kuanza rasmi shughuli zetu za uwajibikaji kwa jamii kwa kuhakikisha afya bora kwa ndugu zetu kutoka kikundi cha Wanawake Albino cha Ndugumbi kwa kuwapatia fedha za kuweza kufanya manunuzi ya dawa na mafuta ya kupaka ili kuimarisha afya ya ngozi zao na kujikinga dhidi ya maradhi ya Kansa na hivyo kurudisha tabasmu kwao na kuona kuwa Shirika lao la Mafuta la taifa linawajali na liko pamoja nao katika mapambano dhidi ya maradhi ya Kansa.”  Msellemu alieza katika tukio hilo.
Meneja Mawasiliano wa TPDC akikabidhi hundi kwa Uongozi wa Chama cha Maafisa Uhusiano Tanzania.

Baada ya kupokea msaada wa fedha kutoka TPDC, Mwamvua Kambi ambaye ni Katibu wa Ndugumbi ametoa shukrani kwa TPDC kwa kuwajali na kuwasikiliza kilio chao maana kilio chao kikubwa ni Kansa ya Ngozi ambayo kwa dawa na mafuta watakazonunua zitasaidia kupunguza mionzi ya Jua ambayo ni hatarishi kwa afya za ngozi zao na kwa msaada walioupata ni mkubwa na unawatosha pamoja na wenzao katika kikundi.”

Aidha Meneja Mawasiliano alieongezea kuwa kwa kutambua umuhimu wa kuboresha masuala ya Utawala Bora nchini, Shirika linaamini kuwa kwa kukisaida Chama cha Maafisa Habari wa Tanzania kitakua kimeimarisha eneo la Utawala Bora ambapo kupitia Kongamano la Maafisa habari ambalo litalenga kwenye kuimarisha mchango wao katika kuijenga Tanzania ya Viwanda wataendelea kufanya kazi kwa bidii kwa kuelimisha Umma wa Watanzania juu ya uwajibikaji wa kizalendo katika kuiletea Nchi Yetu Maendeleo ya kweli katika Sekta ya Viwanda.

David Mwaipaja ambaye ni Mratibu wa chama ametoa shukrani kwa mchango wa TPDC, “Tunashukuru saana kwa utayari mliounyesha wa kuhakikisha Chama cha Maafisa Uhusiano kinafikia Malengo yake na kiukweli matokeo makubwa kwa mlichokifanya leo hayataonekana leo hii lakini nafasi kubwa ya kushukuru itapatikana siku ya Mkutano Utakaolenga kuangalia Nafasi ya Maafisa Uhusiano katika Kuelekea Tanzania ya Viwanda ambapo mtapata nafasi ya kueleza umuhimu wenu au mchango wenu katika kuijenga Tanzania ya Viwanda”.
Meneja Mawasiliano wa TPDC akikabidhi hundi kwa Chama Ndugumbi Albino kwa ajili ya kuwezesha manunuzi wa mafuta ya ngozi.

 Msellemu anansisitiza kuwa “kwa Mwaka huu wa fedha TPDC inatarajia kutekeleza ujenzi wa kituo cha Afya Tunduru, ujenzi wa vyoo kwa wananfunzi wenye ulemavu Shule ya Msingi Shangani na vyoo kwa Shule ya Msingi Kilwa Kivinje, ujenzi wa Zahanati katika kijiji cha Mingoji pamoja na kufadhili zoezi la upimaji wa afya kupitia Taasisi ya Moyo katika kuendesha zoezi la upimaji afya litakalofanyika Wilayani Luangwa Mkoani Lindi.”

Msellemu amefafanua kuwa hii si mara ya kwanza kwa TPDC kutekeleza jukumu lake la msingi katika uwajibikaji kwa jamii inayoizunguka ila ni mwanzo tu wa shughuli hizo kwa mwaka huu wa fedha.

“TPDC tumekuwa na utaratibu wa kutekeleza majukumu yetu kwa jamii toka huko nyuma ambapo tuliweza kuchangia madawati na viti kwa shule za Msingi na Sekondari kwa Mikoa ya Lindi, Mtwara na Dar es Salaam, ujenzi wa madarasa, mabweni, vyoo, ofisi za serikali za mitaa na n.k”.

TPDC kama Shirika la Mafuta la Taifa linao wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria za Nchi na kama Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015 inavyoelekeza namna ya utekelezaji wa wajibu wa Sekta ya Mafuta na Gesi kwa jamii, Shirika litaendelea kutekeleza wajibu huo kwa lengo la kuhakikisha manufaa ya Gesi Asilia nchini yanapatikana kwa wananchi si kwa kutokana na mapato ya gesi asilia pekee kwa Serikali lakini pia kwa kuboresha Sekta za Elimu, Afya, Maji, Utawala Bora, Miundombinu na kadhalika.
Viongozi wa Chama cha Maafisa Uhusiano Tanzania na Chama cha Ndugumbi pamoja na Meneja na Maafisa wa TPDC mara baada ya makabidhiano ya Hundi katika Ofisi za TPDC Dar es Salaam.

TADB YATINGA HONG KONG KUTAFUTA FURSA ZA UWEKEZAJI KWENYE MITAJI NA MIRADI MIKUBWA YA KILIMO NCHINI KUPITIA "ONE BELT ONE ROAD"

$
0
0
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania hivi karibuni ilipiga hodi mjini Hong Kong kujadiliana na Taasisi mbali mbali za Hong Kong na China kuhusiana na fursa za upatikanaji wa fedha kwa ajili ya mitaji na uwekezaji kwenye Sekta ya Kilimo nchini Tanzania.

Katika ziara hiyo iliyoratibiwa na Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki na Katibu Mkuu wa Taasisi ya Kuhamasisha Ushirikiano kati ya China na Tanzania Bwana Joseph Kahama, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB Bwana Francis  Assenga walikutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa makampuni na taasisi kadhaa zikiwamo  Benki ya China; China Capital Fund Management (Hong Kong);  First Shanghai Capital Ltd; Mwakilishi wa China Africa Industrial Forum Ndugu Wenbao Tan ambaye ni Naibu Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa Kituo cha Biashara cha China.

Wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa Japan International Cooperation Foundation Bwana Takashi Kawasaki na Mkurugenzi wa China Biodiversity Conservation and Green Development Foundation Prof. Frederick Charles Dubee.

Miongoni mwa yaliyojiri katika mazungumzo hayo ni jinsi Tanzania inavyoweza kunufaika na fursa zilizopo kwenye Mikakati ya 'Silk Road Economic Belt and the 21st-century Maritime Silk Road', ujulikanao kama 'One Belt and One Road Initiative' (OBOR) ambapo kwa mujibu wa Mkakati huo, Tanzania ndio lango kuu la kuingilia Afrika kwa fursa hizo za kiuchumi na kibiashara toka Asia ambapo Tanzania inakuwa kama kiungo muhimu hivyo kuweza kunufaika zaidi ya nchi nyingine.

Miongoni mwa fursa hizo ni pamoja na kukuza uwekezaji kwenye miundombinu ya aina zote, viwanda vikubwa na vya kati, biashara kati ya Afrika na Asia, na Huduma mbalimbali.

Aidha, Bwana Assenga alikutana pia na akina mama wa shirika lisilo la kiserikali la kukuza uchumi kwa akina mama wa Hong Kong wanamiliki pia Shule ya Sekondari kama mchango wao kwenye huduma za jamii.
Bwana Francis Assenga katikati mwenye suti ya khaki ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB akipanda miti katika Shule ya Sekondari ya China Foundation mjini Hong Kong kuashiria kuunga mkono Mapinduzi ya Mkanda wa Kijani (Green Belt Revolution) wakati wa Maadhimisho ya Miaka 35 ya shule hiyo ambapo Bwana Assenga alialikwa kama Mgeni Maalum wa Shule hiyo. Wageni wengine Maalum waliotoka nchi mbali mbali ni pamoja na Bwana Joseph Kahama ambaye aliyealikwa kama sehemu ya Jopo la Washauri wa Shule hiyo kwa miaka takriban 8 sasa na Mkurugenzi Mtendaji wa Japan International Cooperation Foundation Bwana Takashi Kawasaki (Mwenye Suti bila Tai Kulia kabisa) toka Tokyo, Japan na Mkurugenzi wa China Mfuko wa Uhifadhi Mazingira na Maendeleo ya Mkanda wa Kijani Profesa Frederick Charles Dubee (Mwenye Mvi na Tai katikati) toka Hienola, Finland.
Kikao kati ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Kampuni ya kutafuta mitaji na uwekezaji ya Hong Kong iitwayo China Alpha Fund Management (HK) kilichofanyika katika Jengo la Two Exchange Square mjini Hong Kong hivi karibuni ambacho kiliongozwa na Mwenyekiti wa Kampuni ya Utafutaji Mitaji na Uwekezaji ya Hong Kong Bwana James Wang (Katikati). TADB iliwakilishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bwana Francis Assenga (Mwenye Shati la Bluu na Tai) na kushoto kwake ni Bwana Joseph Kahama ambaye ni Katibu Mkuu wa China-Tanzania Friendship Promotion Association. Kushoto wa Kwanza ni Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Wawekezaji wa China Alpha Fund Management (HK) Ltd Bi. Kandice Au.
Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania Bwana Francis Assenga mwenye tai nyekundu kulia kabisa akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Benki ya China Hong Kong baada ya kumalizika kwa Kikao chao mnamo tarehe 20 Oktoba 2017. Kulia kwa Bwana Assenga ni Meneja Mkuu wa BOC Hong Kong Bwana Chan Man Stephen; Katibu Mkuu wa Taasisi ya Ushirikiano kati ya China na Tanzania Bwana Joseph Kahama; na Watendaji wa Benki hiyo Bi. Yiu Oi Yin Doris, ambaye ni Mkuu wa Idara ya Biashara inayoshughulikia Taasisi za Fedha; na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji wa Mahusiano na Mabenki, Bwana Wong Chee Him Steve, wakiwa Makao Makuu ya Benki ya China mjini Hong Kong.
Kaimu Mkurigenzi Mtendaji wa TADB Bwana Francis Assenga (Kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Shule ya Sekondari ya China Foundation Secondary School (CFSS) Bwana Au Kwong Wing, zawadi toka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania wakati Bwana Assenga alipokaribishwa kama Mgeni Maalum wa Shule kwenye Maadhimisho ya Miaka 35 ya Sekondari hiyo Mjini Hong Kong hivi karibuni ambapo pamoja na mambo mengine aliwahimiza wanafunzi wa shule hiyo kuhifafhi mazingira na kujikita kwenye teknolojia mbali mbali za kilimo cha kisasa.

MAKAMU WA RAIS AONGOZA MATEMBEZI YA HISANI KWA AJILI YA KUSOMESHA WAUGUZI

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, leo ameshiriki katika Matembezi ya Hisani ya Kilomita Nne na Nusu yenye lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kugharamia mafunzo ya uuguzi na ukunga.

Akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza katika viwanja vya Green Ground- Oysterbay mara baada ya matembezi hayo, Makamu wa Rais alisema takwimu za vifo vya kina mama zimeongezeka, hivyo wazo la kusaida kuongeza idadi ya wakunga ambao watasaidia kupunguza vifo hivyo ni zuri sana. 

Makamu wa Rais alisema “nimefarijika kusikia kuwa mwaka 2016 matembezi haya ya hisani yalikusanya wastani wa shilingi milioni 290 pesa ambayo iliwekwa katika fungu la kusomesha wauguzi wakunga wapya 75 katika mafunzo ya ngazi ya cheti” . Makamu wa Rais alionesha kufurahishwa na malengo yaliyowekwa kwa miaka miwili ijayo ya kukusanya kiasi cha shilingi milioni 300 kwa ajili ya kusomesha wakunga wauguzi 400 katika ngazi ya cheti na diploma kwa njia ya masafa. 

Makamu wa Rais alisisitiza kuwa moja ya chanzo cha vifo vya kina mama na watoto wakati wa kujifungua ni ukosefu wa wataalam wa kuwahudumia. Takwimu za Tanzania zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 60 ya akina mama hawaendi kujifungua katika vituo vyetu vya kutolea huduma kutokana na kukosekana kwa wataalam wa kuwahudumia akina mama hao. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Ssuluhu Hassan akizungumza jambo na Waziri wa Afya Mh.Ummy Mwalimu, huku wakitembea mapema leo wakati akiongoza a matembezi ya hisani kwa ajili ya kusomesha Wauguzi Wakunga , matembezi hayo ya kilometa 4.5 yalianzia kwenye viwanja  vya Green Grounds, Oysterbay jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais). 
 Matembezi yakiendelea.


 Picha ya pamoja na Washiriki wa Matembezi hayo ya Hisani .

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Viewing all 110031 articles
Browse latest View live




Latest Images