Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live

SERIKALI YATEKELEZA AMRI YA MAHAKAMA YA KUMPELEKA HARBINDER SINGH HOSPITALI YA MUHIMBILI KWA MATIBABU

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii

Upande wa Jamhuri umetekeleza amri iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kumpeleka  mmiliki wa IPTL, Harbinder Singh Sethi kutibiwa kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili 

Wakili wa serikali, kutoka Takukuru, Leornad Swai ameeleza hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Huruma Shaidi na kuongeza kuwa, mshtakiwa alifanyiwa vipimo na atapelekwa tena hospitalini hapo kuchukua majibu baada ya wiki moja. 

Sethi ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya uhujumu Uchumi anashtakiwa pamoja na  James Burchard  Rugemarila ambapo wanakabiliwa na mashtaka  12 ya  uhujumu uchumi ikiwemo  kutakatisha fedha na kuisababisha serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.

Baada ya taarifa hiyo Wakili wa utetezi Respicius Didas alilalamikia kucheleweshwa kwa upelelezi na kudai kuwa washtakiwa walifika mahakamani kwa mara ya kwanza Juni 19 kipindi chote hicho wamekuwa wakiteseka kwa kukaa ndani na upande Wa Jamuhuri kila wakija wanasema upelelezi bado na kuongeza kuwa wateja wake kuendelea kuwa ndani kinaathari ndani yake.

Akijibu hoja ya kuchelewa kukamilika kwa upelelezi,  wakili Swai amedai, kesi inayowakabili watuhumiwa ni ya kughushi ambayo upelelezi wake unachukua muda mrefu na sheria iko wazi kwa hilo lakini tutajitahidi kukamilisha upelelezi.

MTANDAO WA WANAWAKE WENYE ULEMAVU TANZANIA WAZINDULIWA LEO.

$
0
0
WANAWAKE wenye ulemavu Tanzania wamezindua mtandao wa wanawake wenye ulemavu Tanzania ambao utakuwa ukiwasaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazo wakabili.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mtandao huo jijini Dar es Salaam leo 
Katibu wa jumuiya ya wanawake na watoto wenye ulemavu Tanzania na diwani manispaa ya Ilala, Nuru awadhi amesema kuwa mtandao huo utakuwa karibu zaidi na wanawake walemavu wa Tanzania ili kujua changamoto za kiuchumi zinazo wakabiri.

 Mtandao huo ambao upo chini ya mwavuli wa shirikisho la watu wenye ulemavu tanzani(SHIVYAWATA) amaesema kuwa mtandao huo utalenga zaidi katika kuwainua kiuchumi wanawake walemavu pamoja kuwasaidi kupata mikopo mbalimbali kutka taasisi za kifedha ambazo zitajitokeza kuwasaidi kutokana na hali zao. 
Katibu wa jumuiya ya wanawake na watoto wenye ulemavu Tanzania na diwani manispaa ya Ilala, Nuru awadhi akizungumza na wanawake walemavu wakati wa uzinduzi wa Mtandao wa wanawake wenye ulemavu ambapo wanakauli mbiu ya Fursa kwa wanawake wenye ulemavu ni chachu ya maendeleo.

 Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mtandao wa wanawake walemavu amesema kuwa ''Nia yetu ni kuwaunganisha wanawake walemavu ili kutatua changamoto mbalimbali zinazotukabili".
 
Mbunge wa viti maaluum wa watu wenye ulemavu, Amina Moleli akifungua pazia kwaajili ya uzinduzi wa mtandao wa wanawake nyenye ulemavu Tanzania  uzinduzi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa jumuiya ya wanawake na watoto wenye ulemavu Tanzania, Doris Kulanga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mtandao wa wanawake wenye ulemavu jijini Dar es Salaam leo. amesema kuwa  mtandao huo utasaidia kupunguza changamoto mbalimbali zinazo wakabiri wanawanye wenye ulemavu kwa kushirikiana pamoja na kupendana ili kuleta mabadiliko yaliyo na tija kwa wanawake.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

MAMA JANETH MAGUFULI NA MAMA SHEIN WATEMBELEA VITUO VYA WATOTO YATIMA NA WAZEE ZANZIBAR LEO

$
0
0
 Mama Janeth Magufuli na Mama Mwanamwema Shein wakiwa na baadhi ya watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha yatima cha Mazizini Unguja ambako wake hao wa Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Zanzibar walitembelea ambapo Mama Magufuli alitoa msaada wa vyakula mbali mbali na mafuta ya kupikia na sukari leo Oktoba 13, 2017.
 Mama Janeth Magufuli akiwa ameongozana na Mama Mwanamwema Shein katika kituo cha yatima cha SOS eneo la Mombasa mjini Unguja ambako wake hao wa Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Zanzibar walitembelea ambapo Mama Magufuli alitoa msaada wa vyakula mbali mbali na mafuta ya kupikia na sukari leo Oktoba 13, 2017.
 Mama Janeth Magufuli akiwa na Mama Mwanamwema Shein wakimsalimia Bibi anayelelewa katika kituo cha Wazee eneo la Welezo ambako wake hao wa Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Zanzibar walitembelea ambapo Mama Magufuli alitoa msaada wa vyakula mbali mbali na mafuta ya kupikia na sukari leo Oktoba 13, 2017.
 Mama Janeth Magufuli akiwa ameongozana na Mama Mwanamwema Shein wakisalimia baadhi ya wazee wanaolelewa katika kituo cha Welezo Unguja wakati wake hao wa Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Zanzibar walitembelea ambapo Mama Magufuli alitoa msaada wa vyakula mbali mbali na mafuta ya kupikia na sukari.
 Mama Janeth Magufuli akiwa ameongozana na Mama Mwanamwema Shein akikabidhi msaada wa vyakula kwa ajili ya wazee wanaolelewa kituo cha Welezo Unguja wakati wake hao wa Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Zanzibar walitembelea ambapo Mama Magufuli alitoa msaada wa vyakula mbali mbali na mafuta ya kupikia na sukari leo Oktoba 13, 2017. 
 Mama Janeth Magufuli akiwa ameongozana na Mama Mwanamwema Shein akitoa misaada katika kituo cha yatima cha wazee cha Sebleni Unguja wakati wake hao wa Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Zanzibar walitembelea ambapo Mama Magufuli alitoa msaada wa vyakula mbali mbali na mafuta ya kupikia na sukari leo Oktoba 13, 2017. 
 Mama Janeth Magufuli akiaga baada ya kutembelea katika kituo cha kulelea Wazee cha Sebleni Unguja wakati alipotembelea hapo na kutoa  msaada wa vyakula mbali mbali na mafuta ya kupikia na sukari leo Oktoba 13, 2017.

 PICHA NA IKULU

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MAGAZETI YA JUMAMOSI LEO OCTOBER 14,2017

HILI HAPA SULUHISHO KWA MADAKTARI WANAO UMIA KAZINI.

$
0
0
Mganga Mkuu mkoani Mwanza Dkt.Leonard Subby.
Madaktari pamoja na Waganga nchini wametakiwa kutumia weledi wa taaluma yao katika kuhudumia wagonjwa hususani wafanyakazi wanaoumia kazini kwa kuhakikisha wanapata huduma kwa wakati.



Mganga Mkuu mkoani Mwanza Dkt.Leonard Subby ameyasema hayo leo wakati akifunga mafunzo ya siku tano kwa madaktari na waganga kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa yaliyoandaliwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi nchini WCF na kufanyika katika ukumbi wa BOT Jijini Mwanza.

Amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo Madaktari pamoja na Waganga ili kutambua namna bora ya kufanya tathimini kwa mfanyakazi aliyeumia akiwa kazini.


Dkt.Abisalam Omary ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za tiba na tathimini WCF, amesema mfuko huo unawajengea uwezo madaktari hao ili kufanya tathmini sahihi kwa wagonjwa wanaoumia kazini ama wasaidizi wao.
Rehema Kabongo ni Meneja wa Mafao ya Fidia Mfuko wa Fidia Kwa wafanyakazi (WCF) anasema kuwa "Tangu mpango huo ulipoanza mwaka 2015 kila uchwao maajiri wamekuwa wakifumbuka macho na kuona haja ya kujiunga na mfuko wa fidia kwa wafanyakazi kiasi kwamba wengi kwa makundi wameanza kujiunga na mfuko"


"Bado tunapata changamoto katika kutoa elimu kwa sababu mfuko huu bado ni mpya lakini tumejipanga kuhakikisha tunawafikia mmoja mmoja au kwa makundi ili kufikia malengo tuliyojiwekea yenye tija kwa matabibu wetu"

“Tunataka hawa  madaktari wawe na ujuzi wa kutosha utakaowawezesha kufanikisha azma yetu, na tumeamua kuwa mafunzo ya aina hii yatakuwa endelevu ikiwa ni pamoja na kuwapatia muongozo utakaowasaidia kutekeleza majukumu yao ya kufanya tathmini,” alisema.
Mbali na madaktari na watumishi walio katika sekta ya afya wengi wa wafanyakazi waliopatwa na matatizo hayo kazini wanatoka sekta mbali mbali kama migodi, viwanda na usafirishaji. 

Mfuko huo umeingia mkataba na watoa huduma za afya kwenye hospitali na  vituo vya afya  zaidi ya 6,000 nchi nzima ambapo zitahudumia wafanyakazi hao.

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

Miili ya Askari JWTZ Kurejeshwa Nchini

OPERESHENI YA KUWAPIMA MACHO WAKAZI WOTE WA SINGIDA KUANZISHWA.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa kuanzisha operesheni maalumu ya kuwapima macho wakazi wote Mkoani hapa hususani watumishi wa serikali.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo mapema jana wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afya ya Macho Duniani ambapo asilimia 94 ya watu wenye upofu Mkoani Singida wanasumbuliwa na matatizo ya macho ambayo yanazuilika.

Amesema ili watumishi wa umma waweze kutoa huduma iliyo bora wanatakiwa kuwa na uoni mzuri hivyo kuwapima ni hatua kubwa itakayosaidia kutibu na kuzuia upofu mapema.

“Mganga Mkuu wa Mkoa sasa tunataka uanzishe operesheni tupimwe wote macho, inasikitisha kusikia hao wote waliopata upofu takribani watu elfu 25 wangeweza kupona endapo wangegundulika mapema kwakuwa matatizo yaliyowasababishia upofu yanazuilika”, amesema Dkt Nchimbi na kusisitiza kuwa,“Halmashauri zote tengeni bajeti za kununua dawa za macho pamoja na kuhakikisha wananchi wenu wote wanapimwa macho ili magonjwa yanayozuilika yapewe matibabu mapema, watendaji msione fahari kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa macho wakati mngeweza kuwasiadia”, ameeleza Dkt Nchimbi.

Awali, Dkt Nchimbi amepokea kifaa cha kisasa aina ya Auto Perimeter Glautefield Lite kutoka kwa Shirika la Sight Saver, chenye uwezo wa kuona taswira na matatizo ya macho vizuri, ambacho kwa nchi nzima kinapatikana mkoani Singida peke yake.Amesema kifaa hicho kitawasaidi madaktari bingwa wa macho Mkoani hapa kutoa huduma bora huku akiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili wapatiwe huduma kwani uwepo wa kifaa hicho bila kutumika kitakuwa hakina manufaa.

Dkt Nchimbi ameongeza kuwa, kutokunywa maji ya kutosha husababisha uoni hafifu ambao hupelekea upofu unaozuilika, hivyo amelishauri shirika la Sight Savers kuweka mpango wa kuboresha upatikanaji wa maji na kufanya utafiti hasa maofisini endapo watumishi wanakunywa maji ya kutosha kwakuwa yanasaidia kuzuia upofu.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akipokea kifaa cha kisasa cha vipimo vya macho aina ya Auto Perimeter Glautefield Lite kutoka kwa Shirika la Sight Saver, aliyeshika kipaza sauti ni Meneja Mipango na Uendeshaji wa Shirika la Sight Savers Nchini Mhandisi Koronel Kema.
Daktari wa macho akimfanyia uchunguzi wa macho mmoja kati ya wagonjwa waliojitokeza katika maadhimisho ya Siku ya Afya ya Macho Mkoani Singida.
Mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho Said Mwiru akimuonyesha Mkuu wa Mkoa wa Singida (hayupo pichani) kuwa anaweza kuona na kuwatambua watu kwa kutumia jicho alilofanyiwa upasuaji. Kabla ya upasuaji huo Mwiru amesema jicho hilo lililkuwa halioni.
Baadhi ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa macho wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Singida (hayupo pichani) katika maadhimisho ya Siku ya Afya ya Macho Duniani, akina mama hao wamefanyiwa upasuaji kwa hisani ya shirika la Sight savers.


PRINCE AGHA KHAN AZINDUA STEMPU ZA POSTA ZENYE KUMBUKUMBU ZA TAASISI YAKE JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Kiongozi Mkuu wa Dhehebu la Shia Ismailia, Prince Agha Khan (kulia), akiangalia picha za stempu zenye kumbukumbu ya Taasisi yake wakati alipokuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere, kabla ya kuzizindua jijini Dar es Salaam jana. Walioshika bango lenye picha za stempu hizo kulia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi na kushoto ni Meneja Mkuu Rasilimali za Shirika la Posta Tanzania (TPC), Macrice Mbodo. Anayeangalia kushoto ni Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda.
Kiongozi Mkuu wa Dhehebu la Shia Ismailia, Prince Agha Khan (kulia), akikabidhiwa bango lenye  picha za stempu zenye kumbukumbu ya Taasisi yake na kaimu postamasta  Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Macrice Mbodo, wakati wa uzinduzi wa stempu hizo jijini jana. Anayeangalia kushoto ni Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda.
Meneja Mkuu Rasilimali za Shirika la Posta Tanzania (TPC), na kaimu Postamasta Mkuu Bw.Macrice Mbodo (kulia), akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wa Shirika hilo, kwenye ofisi ya Posta uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere mara baada ya kumalizika uzinduzi huo.

Dc Sofia Mjema awaongoza mamia ya vijana wa UVCCM wilaya ya ilala katika zoezi la kufanya usafi hospitali ya Mnazi mmoja

$
0
0
Katika kuazimisha siku ya kumbukumbu ya kifo cha mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema leo ameongoza umomoja wa Vijana CCM, Wilaya ya Ilala kufanya usafi na kugawa misaada ya kijamii katika Hospital ya Mnazi mmoja Jijini Dar es salaam.

Akizungumza baada ya zoezi hilo Mhe. Mjema amesema , Wameamua kufanya usafi na kugawa zawadi hizo ili kumuenzi Babawa Taifa na amewapongeza vjiana wote walijitokeza katika shuguli hiyo kwani nitendo la uzalendo amabalo linawafanya watu wengi kumkumbuka mwalimu Nyerere kwa uadilifu wake alivyo litumika Taifa enzi ya uhai wake.

Kwa upande wake Mganga mfawidhi wa Hospital hiyo Helmani Gonyani, amewashukuru vija wa umoja huo kwa kutembelea hospitali hiyo na kufanya usafi na kuwataka tena iwapo wata pata nafasi siku nyingine wafanye hivo kwani wamefariji wagonjwa na kuhamasisha umoja wa kitaifa.
Mkuuwa wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema aliye vaaqkilemba ,aliye upande waq kushoto ni Diwani wa kata ya Ilala Mhe. Saad Kimji akifagia na vijana wa Umoja wa Vijana CCM Wilaya ya Ilala katika Hospital ya Mnazi mmoja jijini Dar es salaam leo katika kuelekea madhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha hayati Mwalimu JK nyerere.
Mmoja wa viongozi wa umoja wa vijana CCM ilala akimpati zawadi ya Sabuni mama mzazi Ruth Eliya aliye jifungua jana katika Hospital ya mnazimoja ,aliye upande wamisho kulia ni Mkuuwa Wilaya ya Ilala Mhe.Sophia Mjema .

RC RUVUMA ATOA AGIZO NZITO KWA TANESCO MKOA NA WILAYA

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma DKT BILINITH MAHENGE amemwagiza meneja wa shirika la umeme wilaya ya namtumbo na mkoa wa Ruvuma kuhakikisha wanapeleka huduma ya umeme katika chuo cha mifugo na kilimo MAHINYA kilichopo katika wilaya ya hiyo. HABARI KAMILI HII HAPA VIDEO YAKE

Injinia Manyanya afanya ziara yake ya kwanza ya kikazi akiwa Wizara ya Viwanda

$
0
0
Naibu Waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya afanya ziara yake ya kwanza ya kikazi akiwa Wizara ya Viwanda kwa kutembelea kongano la ngozi na bidhaa za ngozi katika eneo la zuzu Mkoani Dodoma.

Aidha Mhe. Waziri amewaagiza watendaji wa wizara kufanya juhudi za haraka za uendelezwaji wa eneo hilo kwa hakuna sababu ya kuchelewa ambapo mhe. Naibu waziri ametoa muda wa miaka miwili hilo eneo liwe limeanza kuwekewa miundombinu na huduma nyingine.

Pia mhe. Waziri ametembelea eneo la SIDO lililotengwa kwa ajili ya kongano la alizeti ambapo pia amewaagiza watendaji kufanya juhudi za haraka kuharakisha mchakato wa uendelezwaji wa eneo hilo, Mhe. Naibu waziri alihitimisha ziara yake kwa kutembelea ofisi za SIDO na kutembelea ajasiliamali walioko chini ya SIDO na kujionea shughuli za ujasiriamali zinazofanywa katika eneo hilo.

Mhe. Naibu waziri ataendelea na ziara ya kutembelea taasisi zilizo chini ya wizara kuanzia wiki ijayo na kujionea utendaji wa kila taasisi.
 Darasa maalumu la mafunzo ya uzalishaji na utengezaji wa bidhaa za ngozi lililopo Kizota, mkoani Dodoma.
 Naibu waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stellah Manyanya akishuhudia bidhaa mbalimbali zinazotengezwa na wanafunzi wanaojifunza utengezaji wa bidhaa za ngozi pembeni ni ndugu. Stephano Ndunguru, meneja wa mafunzo SIDO, Dodoma.

 baadhi ya bidhaa za ngozi zinazotengezwa na wanafunji wanaojifunza utengezaji wa bidhaa za ngozi. 
 Naibu waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stellah Manyanya akiangalia bidhaa zinazotengezwa na wajasiriamali wa SIDO.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

DKT MABULA AAHIDI WATAALAMU WA KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI SINGIDA.

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeahidi kutoa timu ya wataalamu watakao suluhisha mgogoro wa mpaka kati ya Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida na Wilaya ya Hanang’ Mkoani Manyara.

Naibu Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angelina Mabula ametoa ahadi hiyo wakati wa ziara yake Mkoani Singida katika kijiji cha Singa tarafa ya Kinampundu Wilayani Mkalama ambapo amesema Wizara yake itatoa wataalamu watakaoweza kutatua mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya miaka 30.

“Kwakuwa pande zote mbili za Mkalama na Hanang’ zimekutana mara kadhaa bila mafanikio, nitaleta wataalamu wafike eneo la mpaka ili wataalam hao wawasomee alama moja baada ya nyingine, kila mmoja wenu afahamu eneo lake mwisho ni wapi, nadhani hapo tutakuwa tumewasaidia wananchi wetu”, amesema Dkt Mabula.

Amesema wananchi wa Kijiji hicho cha Singa wasiwe na wasiwasi endapo baada ya kuonyesha mpaka wao mashamba yao yakionekana yapo wilaya ya Hanang’ wataruhusiwa kuendelea kuyamiliki ila watatakiwa kwenda kujitambulisha katika Uongozi wa Wilaya hiyo.

Aidha Dkt Mabula amesema timu hiyo ya wataalamu itahakikisha inasuluhisha migogoro yote ya mipaka ya wilaya hiyo ambayo ngazi ya wilaya imeshindikana kutatuliwa.

Amewashauri wananchi hao kutouza au kugawa ardhi yao ovyo ovyo kwakuwa ardhi ni mali na mtaji popote pale hata kama ni vijijini hivyo watunze ardhi yao na kuiongezea thamani kwa kuipima na kuwa na hati ya umiliki.
Naibu Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angelina Mabula akizungumza na wataalamu wa ardhi, viongozi na watendaji wa halmashauri ya Wilaya na Manispaa ya Singida [hawapo pichani], Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi. 
Naibu Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angelina Mabula akizungumza na wananchi wa kijiji cha Singa tarafa ya Kinampundu Wilayani Mkalama, Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhandisi Jaksoni Massaka.
Naibu Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angelina Mabula akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Ardhi wa Wilaya ya Iramba Lugano Sanga kuhusu utuzanji wa nyaraka za idara hiyo.
Naibu Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angelina Mabula akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi hati ya kumiliki kiwanja chake kilichopo Mjini Dodoma.

TANZANIA YANG’ARA KATIKA TUZO ZA SAFARI ZA KITALII AFRIKA.

$
0
0

Sekta ya Utalii nchini imezidi kujiimarisha katika masoko ya kitalii ulimwenguni hivyo kuendelea kushinda tuzo mbalimbali katika biashara ya Utalii.

Katika hafla ya 24 ya Utoaji Tuzo ya kila mwaka ya Safari za Kitalii Afrika kwa mwaka 2017 iliyofanyika Kigali nchini Rwanda wiki hii, Tanzania imejinyakulia tuzo mbali mbali ambazo zimedhihirisha kuimarika kwa sekta ya Utalii nchini.

Katika hafla hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Kitalii ya Radisson Blu mjini Kigali, kwa mwaka wa pili mfululizo, Mlima Kilimanjaro umeshika nafasi ya kwanza kuwa kivutio kikuu cha utalii barani Afrika.

Kwa upande wa huduma za hoteli, Tanzania ‘imekomba’ tuzo za juu tano za ubora ambapo hoteli ya kifahari ya Diamonds La Gemma Dell’Est iliyoko ncha ya Kaskazini Magharibi ya Kisiwa cha Zanzibar imenyakua nafasi mbili za juu.

Katika tuzo hizo, Hoteli ya Thanda iliyoko katika kisiwa cha Shungimbili wilaya ya Mafia imetununikiwa Tuzo ya Hoteli Bora za Visiwa cha Maraha mwaka 2017 ikiwa ni mwaka wa pili mfululizo kunyakua tuzo hiyo.

Hoteli ya Kisiwa cha Mnemba kilichoko Kaskazini Mashariki ya Pwani ya Zanzibar imepata Tuzo za Hoteli bora za Visiwa vyenye Faragha huku hoteli ya Four Seasons Safari Lodge ya Serengeti imejinyakulia Tuzo ya Hoteli Bora za Mbugani.

Tuzo za Safari za Kitalii zilianzishwa mwaka 1993 kwa lengo la kutambua, kuwazawadia na kusherehekea mafanikio ya wadau katika sekta ya utalii.

Hivi sasa Tuzo hizo zinatambuliwa ulimwenguni kuwa kiwango cha ubora katika sekta hiyo ambapo washindi wanafikia viwango ambavyo wengine wanashindana kuvifikia.

Kila mwaka hafla za Tuzo za Safari za Kitalii hufanyika ulimwenguni kote kwa kuwatukutanisha watu mashuhuri katika matukio ya kikanda kutambua na kusherehekea mafanikio ya mtu moja moja na makundi.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUAHIRISHWA KWA MNADA WA TANZANITE


Article 5

TAARIFA KWA UMMA KUANZA KWA KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE

Article 3

Kamati ya Amani ya viongozi wa dini yakemea matumizi mabaya mitandao

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Dar es Salaam imekemea wale wanaotumia mitandao ya Kijamii,kumtukana Rais na kusisitiza kuwa wanaofanya hivyo wanawakosea watanzania kwa kitendo wanachokifanya.

Akizungumza  wakati wa warsha ya siku moja ya kamati ya Amani ya viongozi wa dini Dar es Salaam iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCR kwa lengo la kuwaelimisha matumizi salama ya mitandao

Mweneyekiti wa Kamati hiyo, Shekh Alhad Mussa Salum amesema Rais Dk. John Pombe Magufuli amekuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya , ufisadi, wizi na ubadhirifu katika mali za umma hivyo wanaotumia mitandao vibaya ni kuwakosea watanzania .

Katika Mkutano huo Shekh wa Mkoa , Alhad Salum amempongeza Rais John Magufuli kwa juhudi ambazo amezichukua katika kuifanya nchi kuwa maadili kwa viongozi wa Umma pamoja na wananchi.

Amesema si suala jema kwa kiongozi wa nchi kutakanwa kwenye mitandano ,kwa kufanya hivyo ni sawa na kutukanwa watanzania waliomuweka madarakani ambapo kuwa jambo hilo halikubaliki.“Simu yako ndio pepo yako na ndiyo moto wako, ukitumia vibaya bila shaka itakupeleka motoni licha ya kuwa kiongozi wa dini pamoja na waumini wako wataingia motoni ,” amesema .

Amsema wananchi wanawajibu wa kuheshimu sheria za mitandao na za nchi na kusisitiza kuwa mmomonyoko wa maadili na kuharibika kwa tabia miongoni mwa jamii kwa kiasi kikubwa, kumechangiwa na simu hizo hivyo lazima zitumike kwa utaratibu.

Aidha amesema viongozi wa dini, makanisa na misikiti wanatakiwa kufanya kazi ya Mungu kwa kuwaokoa watu kwa kuwaelimisha  matumizi sahihi ya mitandao.

Naye Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Joshua Mwangasa amewataka Aidha kwa upande wa viongozi wa dini kuwaelimisha waumini wao kuhusu matumizi bora ya mitandao ya kijamii ili kuepuka kuvunja sheria ya makosa ya kimtandao kwa kuzingatia maadili na utu.
Kwa mujibu wa Mwangasa, kila mtanzania yupo kwenye hatari ya kuingia au kuingizwa kwenye makosa ya kimtandao hivyo ni vema wananchi kuwa makini kwa kukataa kusambaza jumbe zisizo na maadili au kutoa taarifa polisi kuhusu mtu anayesambaza jumbe hizo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Mhandisi James Kilaba akizungumza na kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa wa Dar es Salaam juu matumizi ya mitandao jinsi ya kutumia viongozi wa dini katika mkutano ulifanyika jana jijini Dar es Salaam.
 Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Joshua Mwangasa akizungumza Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam namna ya kutumia mitandao na Jeshi la polisi linavyofanya  kazi kwa wahalifu wa mitandao,jana jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam, Shekh Alhad Mussa Salum (katikati) akiwa na Katibu Kamati ya Amani , Padri John Solomon  (kulia) na Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba  wakisiliza mada katika mkutano wa TCRA na Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam.
Sehemu ya kamati ya amani ya Mkoa wa Dar es Salaam

LAPF YAFUNGUA OFISI YA KANDA YA MAGHARIBI MKOANI GEITA

$
0
0
Naibu waziri wa ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Josephat Sinkamba ameziagiza halmashauri zinazodaiwa kwa kutokupeleka michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kutathmini kiasi wanachodaiwa na wakati wa maandalizi ya bajeti wahakikishe wanakwenda na mikakati ya kiasi walicholipa wanachodaiwa na namna ya kulipa madai kwenye mifuko hiyo.

Agizo hilo limetolewa leo wakati Bw Sinkamba akizindua ofisi za mfuko wa penisheni wa LAPF kanda ya magharibi ambayo itahudumia Mikoa ya Kagera, Kigoma na Geita na Wilaya ya Sengerema na Halmashauri ya Buchosa.

Amesema miongoni mwa maeneo yanayodaiwa na mifuko ya hifadhi ni pamoja na watumishi wa Halmashauri hususani watendaji wa kata na vijiji na kwamba ni vema Halmashauri zikajua kiasi wanachodaiwa na kuandaa mikakati ya kulipa na kupeleka taarifa ya malipo kwa TAMISEMI.

Mkurugenzi Mkuu wa LAPF Bw Eliud Sanga, ameeleza katika kuendelea kuboresha huduma ya mfuko huo wamekuwa wakilipa mafao mapema zaidi kwa mwanachama anayekaribia kustaafu na kwamba wamejidhatiti kutoa huduma bila usumbufu kwa wastaafu wanapohitaji mafao yao.Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga amesema wanaamini kwa mashirika kuendelea kuweka ofisi za kanda ni njia mojawapo ya kukuza mji wa Geita na kufikia azma ya kuufanya mji huo kuwa Manispaa.
Naibu waziri wa ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Josephat Sinkamba Akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Kushoto Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga ,Kulia Mkurugenzi Mkuu wa LAPF Bw Eliud na wa pili kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Geita Mji Constatine Kanyasu wakikata utepe kwaajili ya kuzindua ofisi za LAPF kanda magharibi .
Philip Ngika ni Mstaafu aliyestaafu hivi karibuni na kupatiwa mafao yake kiasi cha zaidi ya Milioni 72 na Naibu waziri wa TAMISEMI. 
Mwanachama wa LAPF ambaye amenufaika na fao la uzazi na kupatiwa kiasi cha zaidi ya Shilingi Laki sita 
Mkurugenzi Mkuu wa LAPF Bw Eliud Sanga,Akimkabidhi Mgeni rasmi Naibu waziri wa TAMISEMI madawati 100 ambayo yametolewa kwenye halmashauri ya mji wa Geita. 

Viewing all 110078 articles
Browse latest View live




Latest Images