Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

Make your collaboration firm, higher education institutions told

$
0
0
The State University of Zanzibar (SUZA) has on 5 th October, 2017 hosted a joint seminar between the Committee of Vice Chancellors, Principals and Provosts in Tanzania (CVCPT) and the Association of Commonwealth Universities (ACU) with the theme ‘Collaborative Approaches to Globalization Growth’.

The seminar which was held at Maruhubi Campus and officially opened by Honourable Riziki Pembe Juma, the Zanzibar Minister of Education and Vocational Training incorporated the senior leaders from higher education institutions in Tanzania and some stakeholders from the Commonwealth countries.

In her opening remarks, Hon. Riziki urged the universities to cooperate since they cannot grow with quality in isolation. “I commend the ACU to come a long way with a mission to link more of our universities to the rest of the world”, the Minister informed. She also called upon members of the CVCPT to reflect upon the theme of the seminar and critically evaluate individual institutions in order to see various ways which can help to build quality of higher education systems in our institutions. This will help to deliver quality education to our young generation, she fleshed out.
Prof. Idris Rai contributes during a session.

On the question of international exposure through study abroad programmes, Hon. Riziki advised each institution member of CVCPT to identify its selling proposition a niche that it can call itself the leader nationally, regionally and globally so eventually we may attract foreign students to come and learn from us, this can better be done through collaborations with foreign institutions, she added.

She requested the CVCPT members who are not members of the Association of Commonwealth Universities to consider the benefits critically and if they can add value to their institutional development they shouldn’t hesitate to join. Earlier, Prof. Idris Rai, the Vice Chancellor of the State University of Zanzibar and Deputy Chair of the CVCPT said in his welcome remarks that collaborations are the key factors in developing higher learning institutions.

Taking the example of SUZA, Prof. Rai enlightened that collaborations have enabled SUZA to effectively develop its staff as they have been instrumental in transforming from college to university culture and they have been vital in building institutional reputation around the globe. Through collaborations SUZA has currently over seventy partnership agreements with institutions from various countries of the world, Prof. Rai clarified.
Participants pay attention to ACU’s Director of Programmes.

Supporting Honourable Minister’s request, Prof. Rai informed that SUZA has joined the Association of Commonwealth Universities to learn, to look for benchmarks outside the country amidst growth, to collaborate, to contribute to higher education development and to develop SUZA as one of the regional leaders in higher education. Prof. Rai commended ACU for its initial suggestion to hold the event jointly with CVCPT and thanked the Chair and the CVCPT members for their proposal which enabled SUZA to host this seminar and the first CVCPT meeting to be held in Zanzibar under SUZA’s hostage.

Introducing the Association of Commonwealth Universities, the Director of Programmes, Mr. Ben Prasadam-Halls, mentioned the key purpose of his association as to advance international cooperation in the fields of higher education and to help its members to develop their capabilities in human resources as well as through various programmes to promote academic mobility among the Commonwealth countries. This seminar explored issues which focused on the role of regional collaboration in meeting the challenges of internationalization and quality of institutions.
Hon. Riziki Pembe Juma (seated centre) with seminar participants.

TAS TAIFA WAOMBA ELIMU ITOLEWE KULINDA WATU WENYE UALBINO VIJIJINI NA MIJINI, ALIYEKATWA MKONO ASIMULIA

$
0
0
Mmoja wa viongozi wa Chama cha watu Wenye Ulemavu wa Ngozi Tanzania(TAS) Rehema Athuman ( kulia) akimjulia hali Mzee Nassoro Msingili (75) mkazi wa kijiji cha Nyarutanga, Kata ya Kisaki, wilaya ya Morogoro ambaye alikatwa sehemu ya mkono wake wa kushoto ambaye juzi aliletwa kutoka kituo cha Afya Duthumi na kulazwa hosipitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro kuendelea na matibabu zaidi. ( Picha na John Nditi).

Na John Nditi, Morogoro

CHAMA cha watu Wenye Ulemavu wa Ngozi Tanzania(TAS) kimewaomba  viongozi wa dini, siasa na wadau mbalimbali kujikita kutoa elimu kwa wananchi  ili waweze kubadili mitazamo na kuacha kuwadhuru  wenye ualbino  kutokana na imani za kishirikina  na wambue  nao ni binadamu sawa na  walivyo wengine.

Mwenyekiti wa TAS Taifa, Nemes Temba  alisema hayo hivi karibuni ( Okt 5)  mjini hapa baada ya kumjulia hali mwenzao Nassoro Msingili (75) ambaye ni mkazi wa kijiji cha Nyarutanga,  Kata ya Kisaki , wilayani Morogoro  mwaka huu baada ya kufanyiwa ukatili  Oktoba 3, mwaka huu na baadhi ya  watu kumkata mkono  wa kushoto na kutokomea nao.

Temba alisema,   kitendo cha Mzee Msingili kukatwa mkono kimewaumiza  wao kama  watu wenye ualbino na taifa kwa ujumla na kukemea  vikali  kitendo hicho kwa kuwa kufuatia tayari ameongezewa  ulemavu mwingine zaidi ya ualbino aliokuwa nao.

Alisema kuwa  kwa wastani asilimia kubwa  ya  suala la mauaji, kukatwa viungo na kunyanyaswa kwa watu wenye ualbino ni ya kishirikina   ambao unapaswa kukemewa na kupingwa vita na kila Mtanzania.

Hivyo alimwomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk  John  Pombe Magufuli  kulitolea tamko la kukemea vikali vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa watu wenye ualbino nchini ili waweze kuishi kwa  amani sawa na watanzania wengine.

waandishi wa Habari mjini Morogoro  juu ya wao kukemea vikali kitendo cha ukatili alichofanyiwa albino mwenzao Nassoro Msingili (75) mkazi wa kijiji cha Nyarutanga Kata ya Kisaki wilaya ya Morogoro vijijini Oktoba 3 mwaka huu.

“ Natoa  wito kwa viongozi wa dini, siasa na wadau mbalimbali  washiriki kutoa elimu kwa wananchi  ili wabadili  mitazamo na kuacha kuwadhuru albino kwa imani za kishirikina  na badala yake atambue  kuwa  albino nao ni binadamu kama walivyo watu wengine” alisema Temba.

Hata hivyo aliiomba Serikali kufanya jitihada kwa kushirikiana na wadau wengine kuweza kupata takwimu sahihi za ualbino ili kuweza  kuwalinda  na kupatia huduma muhimu .

Msingili (75) alikatwa mkono wa kushoto mnamo Oktoba 3 ,mwaka huu majira ya saa 6 usiku katika kijiji cha Nyarutanga , kata ya Kisaki,  wilayani Morogoro baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana  wakati akiwa amelala nyumbani ,na kulazwa  katika Kituo cha afya Duthumi  ambapo juzi alihamishiwa  Hospitali ya Rufaa  ya mkoa wa Morogoro  kwa  ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.

Akizungumza na gazeti hili juzi , akiwa wodi ya majeruhi katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro, Msingili alisema kuwa wakati akivamiwa usiku alikuwa peke yake kwa kuwa ndugu zake walikuwa wamehamishia makazi ya muda shambani  kuvuna nafaka.

Alisema kuwa akiwa amelala usiku watu wasiofahamika walimvamia nyumbani kwake na walimpiga na kitu butu kama rungu kichawani na alipojihami kwa kuinua mgomo wake wa kushoto juu ghafla akikatwa na panga na  watu hao kutokomea na sehemu ya mkono wake wa kushoto.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Leonce Rwengasira,alisema kufuatia tukio hilo Polisi inawashirikia watu wawili kwa tuhuma hizo ambao majina yao yamehifadhiwa kwa ajili upelelezi bado unendelea kufanyika na watafikishwa mahakamani wakati wowote ule.

BREAKING NEWZZZZ: RAIS DKT MAGUFULI AFANYA MABADILIKO MADOGO KATIKA BARAZA LA MAWAZIRI LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitangaza mabadiliko madogo katika baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 7, 2017. Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi pamoja na maafisa waandamizi wa Ofisi ya Rais walikuwapo. Picha na Ikulu



BENKI YA CRDB TAWI LA KARIAKOO WAWAPA ZAWADI WATEJA MAALUMU PAMOJA NA KUFANYA USAFI KUADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA.

$
0
0
BENKI ya CRDB tawi la Kariakoo washeherekea wiki ya Huduma kwa wateja wa kufanya usafi maeneo mbalimbali ya kariakoo pamoja na kuwapa wateja wake zawadi mbalimbali ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza ya Oktoba duniani kote.

Akizungumza mara baada ya kufanya usafi Meneja wa benki y CRDB tawi la Kakriakoo, Diana Mtalo amaesma kuwa wiki hii ni maalumu kwa wateja wote wa benki ya CRDB hasa tawi la Kariakoo.

Pia amesema kuwa kwa sasa benki ya CRDB wa watatoa mkopo kwa wateja wajasiliamali wa  kati kwa kuwapa mkopo ambao watapewa kwa siku saba tuuna mteja ataanza kunufaika na mkopo.
 Meneja wa benki ya CRDB kwa wateja wadogo wadogo, Jesca Nyachiro akizungumza na wateja wa benki ya CRDB tawi la Kariakoo jijini Dar es Salaam wakati wakisheherekea pamoja wiki ya huduma kwa wateja ambayo huadhimishwa kila mwaka wiki ya kwanza ya Oktoba. 
Mteja wa benki ya CRDB na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Tripple "S" Investment Limited, Geofrey  Rwenyagira akizungumza na wafanyakazi pamoja na wateja wa benki ya CRDB tawi la kariakoo jijini Dar es Salaam wakati walipokuwa akizungumzia changamoto mbalimbali pamoja na mafanikio aliyoyapata. Pia aliwaasa wafanyakazi wa beni hiyo kuvumiliana katika furaha na matatizo mbalimbali ya wateja wake.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Kariakoo wakiwa katika picha pamoja na wateja waliohudhulia hafla fupi ya kuwashukuru pamoja na kuwapa zawadi mbalimbali wateja wake.
 Mteja wa benki ya CRDB na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Tripple "S" Investment Limited, Geofrey  Rwenyagira akishirikiana na Meneja wa benki ya CRDB kwa wateja wadogo wadogo, Jesca Nyachiro kukata keki kwaajili ya kuwashukuru wateja maalumu wa Tawi la Kariakoo katika wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza ya Oktoba.
Meneja wa benki ya CRDB kwa wateja wadogo wadogo, Jesca Nyachiro akilishwa keki na meneja wa Benki ya CRDB tawi la Kariakoo,Diana Mtalo wakati wa kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza ya Oktoba.
 meneja wa Benki ya CRDB tawi la Kariakoo,Diana Mtalo akita zawadi kwa wateja wa mda mrefu pamoja na wateja maalumu wa benki ya CRDB tawi la Kariakoo jijini Dar es Salaam.Ikiwa ni Kusherekea pamoja wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza ya Oktoba duniani kote.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Kariakoo wakifanya usafi maeneo mbalimbali yaliyo karibu na Benki hiyo jijini Dar es Salaam leo.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

UTT AMIS yatoa elimu na kutoa huduma kwa wawekezaji wa zamani na wapya katika maonyesho ya Tasisi za Fedha jijini DSM.

$
0
0
Afisa Masoko wa UTT AMIS akitoa elimu na kutoa huduma kwa wawekezaji wa zamani na wapya wa UTT AMIS katika maonyesho ya Tasisi za Fedha Mnazi Mmoja jijini DSM.
Afisa Masoko wa UTT AMIS akitoa elimu na kutoa huduma kwa wawekezaji wa zamani na wapya wa UTT AMIS katika maonyesho ya Tasisi za Fedha Mnazi Mmoja jijini DSM.

Afisa Masoko wa UTT AMIS akitoa elimu na kutoa huduma kwa wawekezaji wa zamani na wapya wa UTT AMIS katika maonyesho ya Tasisi za Fedha Mnazi Mmoja jijini DSM.

WAFANYAKAZI WA BIMA YA BRITAM WATOA MSAADA KATIKA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA CHAKUWAMA.

$
0
0
WAFANYAKAZI wa bima ya Britam ambayo hutoa bima za magari, bima za nyumba, bima za wakandarasi, bima za usafiri wa majini pamoja na bima za safari bima za afya pamoja na nyingine nyingi leo wametembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam.

Wafanyakazi hao wametoa vitu mbalimbali kama vile Unga kilo 300
Maharage 250,Sukari kilo 200,sabuni za unga,Karatasi nyeupe (limu bunda)200,Daftari boksi 500, Mafuta ya kula lita 100,chumvi pamoja na vifaa mbalimbali vya shule.

Vitu hivyo vyote vimegharimu shilingi milioni Saba ambayo wameona wagawane faida waliyoipata katika kushaherekea wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza ya Oktoba duniani kote.

Kwa upandewa  Katibu mtendaji wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA, Hasan Khamis  amewashukuru uongozi kampuni ya bima ya Britam  kwa kuwaona wao kwani kunavituo vingi hapa nchini "Tunashukuru kwa kutuona sisi CHAKUWAMA na kwa kuona mchango wetu.
Mkuu wa operesheni wa Bima ya Britam, Farai Dogo akimkabidhi msaada wa vitu mbalimbali Katibu Mtendaji wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA, Hasan Khamis  kilichopo Sinza jijinini Dar es Salaam leo ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza Oktoba duniani Kote.
Meneja masoko wa bima ya Britam,Godfrey mzee akimkabidhi Katibu Mtendaji wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA, Hasan Khamis msaada huo ni shukrani kwa wateja wa bima iyo ambapo wameona watoe faida kwa watoto yatima wanaolelewa katika kituo kilichopo sinza jijini Dar es Salaam.
 Wafanyakazi wa bima ya Britam wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakikabidhi vitu mbalimbali kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo sinza jijini Dar es Salaam. 
Katibu mtendaji wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWA, Hasan Khamis akizungumza na wafanyakazi wa bima ya Britam na kuwaelezea historia ya kituo hicho pamoja na changamaoto pamoja na mafanikio waliyoyapata.
Pia amewashukuru wafanyakazi wa bima ya Britam kwa kuwapa msaada huo.
 Baadhi ya wafanyakazi wa bima ya Britam wakimsikili katibu Mtendaji wa kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Bima ya Britam wakiwa katika picha ya  pamoja jijini Dar es Salaam leo.

WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI WAMETAKIWA KUSIMAMIA WELEDI KATIKA KAZI ZAO

$
0
0
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Amina Khamis Shaban akizungumza wakati wa mahafali ya 8 ya  Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugazi (PSPTB), Yaliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Ununuzi na Ugavi katika Sherehe ya Mahafali ya nane ya bodi  yaliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam
 Makamu Mkuu wa Chuo cha Ushirika  Moshi(MOCU), Neema Kumburu  akipokea cheti cha chuo hicho kuongoza katika utoaji wa masomo hayo mwaka wa pili Mfululizo
 Hotuba ya Mkurugenzi Mtendaji wa bodi ya wataalamu wa Ununuzi na Ugavi akitoa nasaha kabla ya kumkaribisha mgeni Ramsi katika Mahafali ya 8 ya chuo hicho
 Makamu Mwenyekiti wa bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi,Ahmed Kilima akitoa hotuba ya Shukrani wakati wa kufunga  mahafali ya 8 ya  bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugazi (PSPTB), Yaliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

 Wahitimu wa Shahada ya Utaalamu wa Ununuzi na  Ugavi (PSPTB) wakisoma Kiapo Mbele ya Mgeni Rasmiwakati wa mahafali ya 8 ya  bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugazi (PSPTB), Yaliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

RAIA WA COMORO WAISHIO TANZANIA WALIOMBA JESHI LA POLISI KUSAIDIA KUPATIKANA KWA NDUGU YAO

$
0
0
JUMUIYA ya raia wa Comoro waishio Tanzania wameiomba Serikali kupitia Jeshi la Polisi nchini kusaidia kupatikana kwa ndugu yao Ammar Abdousoi Madou (26) aliyepotea na kutoweka kusikojulikana tangu tarehe 29 Juni mwaka huu.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo (jana) Jijini Dar es Salaam, Mwanasheria wa Jumuiya hiyo, Larifou Said alisema taarifa za kupotea kwa Madou ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kampala nchini Uganda ziliifikia familia yake tarehe 29 Juni, mwaka huu.

Said anasema familia ya Madou ilipokea taarifa za kushikiliwa kwa Madou na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha tarehe 27 Juni, mwaka huu kutoka kwa rafiki wa karibu wa Madou anaeishi Mkoani Arusha na baadae kuelezwa kuwa aliachiwa huru tarehe 29 Juni mwaka huu, ingawa tangu kipindi hawajaweza kuonana nae hadi sasa.

Anasema pamoja na familia hiyo kufanya jitihada mbalimbali za kufanikisha upatikanaji wa ndugu yao ikiwemo kufanya Mawasiliano ya mara kwa mara na vyombo vya usalama ikiwemo kuwasiliana na Idara ya upelelezi ya Jeshi la Polisi kwa ajili ya kufahamu undani na sababu ya kukamatwa kwa Madou.

Mwanasheria wa Jumuiya ya Raia wa Comoro waishio Tanzania, Larifou Said akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu tukio la kupotea kwa Mwanafunzi Raia wa nchi hiyo Ammar Abdousoi Madou (pichani) ambapo waliliomba Jeshi la Polisi kusaidia upatikanaji wa ndugu yao huyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TAIFA STARS YATOKA SARE YA 1-1 NA TIMU YA MALAWI

$
0
0
Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' imetoka sare ya 1-1 na timu ya Taifa ya Malawi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika leo katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaam.

Mchezo huo ulioanza kwa kasi kwa kila upande uliweza kudumu kwa dakika 40 kwa timu ya Malawi kupata goli la kuongoza likifungwa na Robert Ng'ambi.

Goli hilo liliweza kudumu mpaka mapumziko.

Kipindi cha Pili kilianza kwa Tanzania kutafuta goli la kusawazisha ambapo dakika ya 57, Simon Msuva akiisawazishia Tanzania goli na kupelekea matokeo kuwa 1-1.

Mpira ulianza kuwa wa vurugu baada ya Kocha wa Malawi kutolewa nje Na mwamuzi Israel Nkongo ikiwa ni kwa kufanya kosa la kuingia ndani ya uwanja na kubishana na mwamuzi wa akiba.

Ikiwa ni katika kutafuta goli la ushindi Beki wa kulia Erasto Nyoni aliweza kuzawadiwa kadi nyekundu na kisha baadae Mzamiru Yassin nae aliweza kupewa kadi nyekundu baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.

Mpaka mpira unamalizika Taifa Stars 1- 1 Malawi.
Nahodha wa timu ya Taifa, Mbwana Samatta akiondoka na mpira mbele ya Mabeki wa Malawi.


Mmoja wa Wachezaji wa timu ya Tanzania (Taifa Stars) akimchomoko mchezaji wa timu ya Taifa ya Zambia,ambapo mpaka sasa kipindi cha pili timu hizo zimefungana sare ya 1-1 na mpira unaendelea katika uwanja wa Uhuru,jijini Dar.
 Kikosi cha timu ya Taifa Stars
 Waziri wa Habari,Utamaduni ,sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe akiikagua timu ya Taifa Stars kabla ya mchezo wa kirafiki wa Kimataifa dhidi ya timu ya Malawi kuanza jioni ya leo katika uwanja wa Uhuru,jijini Dar
 Wimbo wa Taifa Ukipigwa
Kikosi cha timu ya Malawi.

JERRY MURO NDANI TA MKASI NA SALAMA JABIR

BARAZA KUU LA WAFANYAKAZI TANESCO LAUNGA MKONO JITIHADA ZA RAIS MAGUFULI

$
0
0
BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) limeazimia kuunga mkono jitihada za Rais Dkt John Magufuli za kuifanya Tanzania kuwa nchi ya watu wenye kipato cha kati kwa kufanya kazi kwa umahiri,uzalendo na ufanisi.

Akizungumza katika ufungaji wa baraza hilo mwishoni mwa wiki mjini Tanga Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi,Dr.Alexander Kyaruzi alisema bodi hiyo ipo tayari kutoa ushirikiano katika kuhakikisha shirika linafikia malengo yake muhimu.

Alisema malengo hayo ambayo yanahitajika katika kuhakikisha uchumi wa viwanda unafikiwa kwa kasi kubwa kutakapotokana na kuwa na umeme wa uhakika ambao unaweza kusukuma gurudumu la maendeleo.Aidha alisisitiza juu ya umuhimu wa utunzaji wa miundombinu ya shirika hilo ili iweze kusaidia kutoa huduma zake wakati wote bila kuwepo kwa vikwazo vya namna yoyote ile.

Hata hivyo aliwaasa wafanyakazi wa shirika hilo kuhakikisha wanakuwa walinzi wa miundombinu hiyo ili isiweze kuibiwa ikiwemo kuhakikisha haihujumiwi na watu wanaoweza kufanya hivyo.Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.
KAIMU Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka akizungumza wakati wa ufungaji wa baraza kuu la 47 la wafanyakazi mjini Tanga 
KAIMU Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka akizungumza wakati wa ufungaji wa baraza kuu la 47 la wafanyakazi mjini Tanga 
KAIMU Mkurugenzi Mtendaji TANESCO, Dkt.Tito E. Mwinuka ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo kulia akiwa na Katibu wa Baraza Kuu la Wafanyakazi,Asmaa Myale wakisikiliza kwa umakini hoja za wafanyakazi.

ARUSHA WAANZA USAJILI VITAMBULISHO VYA TAIFA WAANZA KWA KISHINDO

$
0
0
Wananchi wa Kata za Themi, Sekei na Sombetini Wilaya ya Arusha mjini leo wameanza zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa kwa kishindo; huku baadhi wakihangaika huku na huko kutoa nakala ya viambatisho vyao ili kujisajili kwa wakati.

Akizungumza katika Usajili huo Afisa Usajili wa Wilaya hiyo Bi. Juliet amesema wamepanga kukamilisha usajili wa Kata hizo ndani ya siku 9; na kwamba wananchi wote wanaoishi katika Kata hizo kujitokeza kwa wingi ili wasajiliwe.

Misururu ya wananchi imeonekana katika Kata za Themi na Sekei; huku baadhi wakihangaika kujaza fomu za maombi ya Usajili. Katika hali iliyoonyesha ushirikiano na kujizatiti kwa viongozi katika kuhakikisha wananchi hao wanahudumiwa, ofisi za Mitaa leo zilifungwa kwa muda na huduma zote kuhamia katika makao makuu ya Kata ili kuwaidhinishia wananchi fomu zao pamoja na kuwagongea mihuri kuthibitisha makazi yao.

Zoezi la Usajili kwa Wilaya ya Arusha Mjini linatazamiwa kukamilika ndani ya miezi miwili; ambapo wananchi wataweza kupata namba za Utambulisho (NIN) wakati hatua za uzalishaji Vitambulisho zikiendelea. Wilaya nyingine mkoani humo ambazo usajili unaendelea ni Karatu, Longido, Arumeru na Monduli.
Mmoja wa Wageni Wakaazi mkoani Arusha na mkazi wa Kata ya Sekei akikamilisha Usajili wa Vitambulisho vya Taifa. Zoezi la Usajili kwa mkoa wa Arusha linahusisha wananchi wenye umri wa miaka 18 na kuendelea na Wageni Wakaazi wenye kuishi halali nchini.
Watumishi wa NIDA wakiingiza taarifa za wananchi kwenye mfumo kutumia mashine maalumu ya Usajili ambayo pia inauwezo wa kuhifadhi si tu taarifa za kawaida pia alama za kibaiolojia na picha za waombaji wa Vitambulisho wakati wa Usajili.
Ofisi ya Kata ya Themi ambako zoezi la Usajili limeanza rasmi, na kukutanisha mamia ya wananchi kupata huduma.

Afisa Uhamiaji kutoka Ofisi ya Uhamiaji makao makuu Arusha akihakiki uraia wa mmoja wa wananchi katika Kata ya Themi aliyefika kujiandikisha.

MAGAZETI YA JUMAPILI LEO OCTOBER 8,2017

MASAUNI ATEMBELEA MRADI WA UMWAGILIAJI GEREZA LA KILIMO IDETE, ATAKA MKANDARASI ACHUKULIWE HATUA KALI KWA KUUTELEKEZA UJENZI WA MRADI HUO WA MABILIONI

$
0
0
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka (kushoto), pamoja na Maafisa wengine wa Jeshi hilo, wakitoka katika Gereza la Kilimo Idete lililopo Ifakara, mara bada ya Naibu Waziri huyo kupokeataarifa ya Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji uliosimama baada ya Mkandarasi kuutelekeza mradi huo wenye thamani ya shilingi Bilioni 2.5. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi hilo kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia),
Karani wa Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, Mkaguzi wa Jeshi la Magereza, Juma Mtega, akimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto),chanzo cha ujenzi wa mradi huo. Masauni alifanya ukaguzi wa mradi huo wa mabilioni ya fedha ambao Mkandarasi aliutelekeza mwaka 2016. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi la Magereza kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.
Mkuu wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka, akimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), sehemu mbalimbali za Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, wakati Masauni alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi huo wa zaidi ya shilingi Bilioni 2.5 uliosimama baada ya Mkandarasi wa mradi huo, kuutelekeza mwaka 2016. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi hilo kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akitoa maelekezo kwa viongozi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro ya kumchunguza na kumchukulia hatua za kisheria endapo itathibitika Mkandarasi aliyesimamisha Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, alifanya makosa kwa kusimamisha ujenzi wa mradi huo wa mabilioni ya fedha, tangu mwaka jana 2016. Wapili kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mkoa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

NHIF YATOA HUDUMA ZA UPIMAJI KWENYE BONANZA LA MICHEZO JIJINI TANGA LEO

$
0
0

Afisa Mdhibiti wa Viwango na Ubora Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoani Tanga,Dkt Lwi Kupaza akiangalia taarifa za moja ya wakazi wa Jiji la Tanga ambao walijitokeza kupima uzito,sukari na presha wakati wa bonanza la michezo ambalo limefanyika leo kwenye viwanja vya shule ya sekondari Popatlaly kushoto ni Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu
Daktari wa NHIF kushoto akimpima presha Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu wakati wa bonanza la michezo 
Afisa Mdhibiti Viwango na Ubora Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Dkt Lawi Kupaza akichukua maelezo ya Ofisa wa Polisi kutoka Ofisi ya RCO,Saidi Mwagara wakati wa bonanza hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga (RPC) Benedict Wakulyamba akiwaongoza askari wa Jeshi hilo kuwavuta kamba Bandari Tanga wakati wa Bonanza hilo leo
Ofisa Uhamiaji wa Mkoa wa Tanga,Crispin ngonyani akiwaongoza idara hiyo kuvuta kamba kwenye bonanza hilo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

PSPF YAWAZAWADIA WAFANYAKAZI WAKE KWENYE KILELE CHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA DUNIANI

$
0
0
 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, amewapongeza wafanyakazi wa Mfuko huo, kwa kazi nzuri wanayofanya ya kuwatumikia wateja, (wanachama) wa Mfuko.

Bw. Mayingu ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwatunuku tuzo na zawadi wafanyakazi waliofanya vizuri zaidi katika kipindi cha Wiki ya Huduma kwa Wateja, iliyoanza Oktoba 2 na kumalizika Oktoba 6, 2017.

Wiki hiyo ambayo huadhimishwa kila mwanzo wa wiki ya mwezi Oktoba kila mwaka, hulenga kuwakumbusha wafanyakazi wajibu wao wa kuwahudumia wateja kwa kuzingatia weledi wa utoaji huduma bora kwa mteja.

"Wakati nikiwa Iringa nimepokea pongezi nyingi za Wanachama wetu, wakiwapongeza nyinyi wafanyakazi kwa kuwahudumia vizuri, hongereni sana na niwaombe muendele kutoa huduma bora kwa wateja wetu kwani huo ndio wajibu wetu." Alisema Bw. Mayingu katika hafla hiyo iliyofanyika Oktoba 6, 2017 kwenye ukumbi wa makao makuu ya PSPF, Jubilee Tower jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, akiwahutubia wafanyakazi na wadau wa Mfuko, wakati wa hafla ya kuwatunuku tuzo na kuwakabidhi zawadi wafanyakazi "waliochomoza" kwa utoaji huduma bora zaidi katika kipindi cha Wiki ya Huduma kwa Wateja, 2017, iliyofikia kilele Oktoba 6, 2017.
 Bw. Mayingu akimkabidhi tuzo, Elizabeth Shayo.
  Bw. Mayingu akimkabidhi tuzo, Bi.Valley Malinga
Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, (PSS), Bi. Mwanjaa Sembe, (wapili kushoto), akiwa na maafisa waandamizi wa Mfuko huo.
 Baadhi ya wafanyakzi wa PSPF

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

RC NCHIMBI AAGIZA KUVUNJWA KWA BODI YA USHIRIKA MSAI WILAYANI IRAMBA, NDANI YA WIKI MBILI

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula, asimamie kuvunjwa kwa bodi ya Ushirika wa Kijiji cha Msai Wilayani Iramba ndani ya wiki mbili, kutokana na tuhuma za ubadhirifu wa zaidi ya shilingi milioni 50.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo mwishoni mwa wiki alipokuwa katika mkutano na wakulima wa Pamba wa Kijiji cha Msai, ambao wamemueleza kutokuwa na imani na viongozi wa bodi hiyo kutokana na upotevu wa fedha hizo na wakiwa hawajachukuliwa hatua yoyote.

Wakulima hao wamemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa fedha zaidi ya milioni 50 zilitolewa na seikali kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la ghala la ushirika wa kijijini hapo lakini hakukuwa na ujenzi wowote uliofanyika huku wakifuatilia hawapewi majibu sahihi.

Wamesema wana ushirika walijitahidi kutuma mwenyekiti wa Kijiji hicho kufuatilia upotevu huo bila mafanikio jambo lililowakatisha tamaa ya kuendelea na ushirika.

Dkt Nchimbi amesema “moja ya Muhimili wa mafanikio ya kilimo cha pamba ni ushirika ulio imara, tunakoelekea kwenye kilimo cha pamba chenye tija hawa wasiowaaminifu kwenye bodi watatukwaza na kutukwamishwa, kama bodi haifanyi kazi vizuri kwanini iendelee?, Mkuu wa Wilaya naimani kwa utendaji wako mzuri hili halitachukua zaidi ya wiki mbili”.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akiwaelekeza wakulima wa pamba kijiji cha Msai wilayani Iramba, vipimo vya kati ya tuta na tuta, shimo na shimo kwa kutumia kamba na vijiti ili waweze kupanda kitaalamu na kuvuna kwa wingi.
Wakulima wa pamba kijiji cha Msai wilayani Iramba, wakishiriki kwa vitendo mafunzo yya kupima urefu kati ya tuta na tuta, shimo na shimo kwa kutumia kamba na vijiti ili waweze kupanda kitaalamu na kuvuna kwa wingi.
Katibu Tawala Wilaya ya Iramba Pius Songoma akishiriki kuwaelekea wakulima wa pamba kijiji cha Msai wilayani Iramba, vipimo vya kati ya tuta na tuta, shimo na shimo kwa kutumia kamba na vijiti ili waweze kupanda kitaalamu na kuvuna kwa wingi.
Konyo Mjika ambaye ni mkulima hodari wa pamba wilaya ya Iramba kutoka kijiji cha Msai akimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Singida kwa zawadi ya kilo tano za mbegu ya pamba aliyopewa.
Zakaria Marko Mwakilishi wa Kampuni ya Biosustain itakayosambaza mbegu za pamba tani 300 mkoani Singida akizungumza na wakulima wa zao hilo Katika kijiji cha Msai Wilayani Iramba.


BENKI YA CRDB YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA WILAYANI CHATO

$
0
0

Na Binagi Media Group.

Katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja mwaka huu 2017, benki ya CRDB jana simetoa semina kwa wateja wake katika wilaya ya Chato mkoani Geita na pia kupokea maoni yao ili kuboresha zaidi huduma zake.


Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wakubwa Goodlack Nkini aliwahakikishia wateja wa benki hiyo huduma ya mikopo kwa muda wa siku saba na hivyo kuwahimiza wafanyabiashara kuitumia benki fursa hiyo kukuza mitaji yao ya biashara.


Aidha alisisitiza kwamba benki hiyo itaendelea kutoa huduma bora kwa wateja wake ikiwa ni benki inayoongoza kwa kutoa mikopo hapa nchini huku pia jamii ikiendelea kunufaika na benki hiyo kupitia gawio la faida ambalo hutolewa kila mwaka ili kusaidia shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo afya na elimu.


“Tunaomba tuendelee kushirikiana pamoja ambapo CRDB ni benki ya muda mrefu iliyo salama na imara kufanya nayo kazi ikiongoza kwa zaidi ya miaka 10 sasa kwa kutoa huduma bora na zenye riba nafuu nchini”. Alisisitiza Nkini kwenye semina hiyo iliyojumuisha pia wateja wa CRDB kutoka Geita, Muleba, Ngara na Bihalamulo.
Meneja wa CRDB tawi la Chato, Msigwa Mganga alisema benki hiyo imeendelea kuwafikia wateja wake kote nchini kupitia huduma mbalimbali ikiwemo Fahari Huduma, Simu Banking pamoja na Internet Banking na hivyo kuwa benki yenye mtandao mkubwa unaowawezesha wateja wake kupata huduma za kibenki popote walipo.


“Huduma zetu ni bora kuliko benki nyingine yoyote nchini hivyo natoa rai wateja wetu kutumia huduma zetu ikiwemo mikopo kwa ajili ya mitaji ya biashara zao kwani tunao uwezo mkubwa wa kuwahudumia”. Alidokeza Meneja wa CRDB tawi la Mwanza, Wambura Calystus.

 Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wakubwa Goodlack Nkini, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji CRDB. Meneja wa CRDB tawi la Mwanza, Wambura Calystus akizungumza kwenye semina hiyo. Meneja wa CRDB tawi la Chato, Msigwa Mganga akizungumza kwenye semina hiyo. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KIGOMA YAKUTANA NA WADAU WAKE WA HAKI JINAI KUJADILI NAMNA YA KUSUKUMA MASHAURI

$
0
0
Na Mary Gwera, Mahakama-Kigoma 

KAIMU Hakimu Mkazi Mfawidhi-Mahakama ya Hakimu Mkazi/Mkoa-Kigoma, Mhe. Flora A. Mtarania amewasihi Wadau wa Haki Jinai wa mkoa huo kushirikiana na Mahakama ili kumaliza mashauri yote yaliyofunguliwa mwaka huu ifikapo Desemba mwaka huu. 

Mhe. Mtarania aliyasema hayo mapema mwishoni mwa wiki iliyopita Oktoba 06 katika kikao maalum cha Kusukuma Mashauri ‘Case Flow Management Meeting’ kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mahakama hiyo ya Mkoa. 

“Mpaka sasa Mahakama ya Mkoa-Kigoma kuna jumla ya mashauri 24 ambayo bado hayajatolewa maamuzi ‘pending cases’ huku 16 yakiwa mashauri ya Madai na nane (8) ya Jinai, na kwa upande wa Mahakama za Wilaya kuna jumla ya mashauri 103 ambayo bado hayajakamilika huku mashauri 79 yakiwa ya Jinai na 24 mashauri ya Madai,” alisema Mhe. Mtarania. 

Alisema kuwa kesi hizo ambazo zina wastani wa kati ya miezi mitatu (3) hadi miezi sita (6) tangu kufunguliwa kwake Mahakamani zimekuwa zikikwama kwa sababu mbalimbali ambazo ni pamoja na kutopatikana kwa Mashahidi hali inayopelekea haki kutopatikana kwa wakati, upelelezi kutokamilika kwa wakati, fedha za Mashahidi kutotosheleza uhitaji na kadhalika. 

Aliongeza kuwa ni vyema Suala ya mchakato wa usikilizwaji wa kesi hadi ukamilikaji wake lifanyike kwa ushirikiano kati ya Mahakama na Wadau wa Haki Jinai ili haki ipatikane kwa wakati stahiki. 

Aidha; Mhe.Mtarani alisema kuwa lengo la vikao vya pamoja na Wadau wa Mahakama ni kujadili namna ya kusukuma mashauri ili yaweze kumalizika kwa wakati, kupeana mikakati ya kushughulikia mashauri na kuhakikisha kuwa kila mtu anatimiza wajibu wake katika mchakato mzima wa usikilizaji wa mashauri. 

Mhe. Mtarania aliendelea kusema kuwa vikao hivi hufanyika kila baada ya miezi mitatu na hiki ni kikao cha tatu (3) kufanyika kwa mwaka huu, huku akieleza kuwa kabla ya kikao hiki cha ngazi ya Mkoa kufanyika huwa kuna vikao vya kusukuma Mashauri ambavyo hufanyika kwa ngazi za Mahakama za Wilaya ili kuwasilisha mipango yao katika kikao cha Wadau cha Mkoa. 

“Kimsingi kwa hatua tuliyofikia sasa vikao hivi vimesaidia kumaliza mashauri yaliyokuwa yalikaa muda mrefu Mahakamani kutokana na sababu mbalimbali zilizosababishwa na Wadau,” alieleza Mhe. Mtarania. 

Kikao kilihudhuriwa na Kaimu Hakimu Mkazi Mfawidhi ambaye ndiye Mwenyekiti, Mwanasheria wa Serikali Mfawidhi, Mahakimu Wafawidhi wa Wilaya za Kasulu na Kibondo, Mkuu wa Takukuru-Mkoa, Afisa Uhamiaji wa Mkoa, Mkuu wa Upelelezi (RCO), Afisa Ustawi wa Jamii, Mwenyekiti wa Chama cha Mawakili wa Kujitegemea na Mtendaji wa Mahakama-Kigoma. 

Hata hivyo, Wajumbe wa Kikao hicho waliazimia kufanya kazi kwa kushirikiana ili ifikapo Desemba 30, kesi ambazo hazijakamilika ziwe zimekamilika. 
Kaimu Hakimu Mkazi Mfawidhi-Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mhe. Flora Mtarania akiongoza kikao cha Kusukuma Mashauri ‘Case Flow Management Meeting’kilichofanyika katika Ukumbi wa Mahakama ya Mkoa Kigoma.
Mtendaji-Mahakama ya Mkoa Kigoma, Bw. Humphrey Paya (kulia) akichangia jambo katika kikao hicho.
Wajumbe wakiwa katika kikao hicho (katikati) ni Hakimu Mkazi Mfawidhi-Mahakama ya Wilaya-Kasulu, wa kwanza kulia ni Mtendaji wa Mahakama-Kigoma, Bw. Humphrey Paya na wa kwanza kushoto ni Mwakilishi kutoka Ofisi ya Ustawi wa Jamii, Manispaa ya Kigoma.
Wajumbe wakiwa katika kikao.
Muonekano wa sehemu ya jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi-Kigoma,hata hivyo jengo hilo ni chakavu hivyo linahitaji ukarabati ili liendelee kukidhi mazingira ya bora ya kutolea haki kwa wananchi.

MABADILIKO MADOGO YA BARAZA LA MAWAZIRI LAGUSA PANDE ZOTE ZA NCHI

Viewing all 110028 articles
Browse latest View live


Latest Images