Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

Zawadi za milioni 40 kushindaniwa Rock City Marathon

$
0
0

Washindi wa michuano ya Rock City Marathon inayotarajiwa kufanyika  Octoba 29 mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wanatarajiwa kuondoka na zawadi zenye thamani ya zaidi ya sh milioni 40 pamoja na medali, imefahamika. 


Akizungumzia zawadi hizo jijini Dar es Salaam leo, Mratibu wa mbio hizo kutoka kampuni ya Capital Plus International (CPI), Bw. Bidan Lugoe  alisema pamoja na medali washindi wa kwanza wa mbio za kilomita 42 kwa wanaume na wanawake watajinyakulia sh. Mil 4 kila mmoja, sh.mil 2/-  kwa washindi wa pili na sh. Mil 1/- kwa washindi wa tatu, huku washindi wanne hadi kumi na tano nao pia wakiibuka na zawadi  za medali na pesa taslimu.


Kwa upande wa mbio za  Kilomita 21, Bidan alisema pamoja na medali washindi wa kwanza kwa wanaume na wanawake watajinyakulia sh.  Mil 2/- kila mmoja, sh. Mil 1/-  kwa washindi wa pili na sh. Laki 5/- kwa washindi wa tatu huku pia washindi wanne hadi wa kumi na tano wakiibuka na  zawadi za pesa taslimu na medali kila mmoja.


 “Mbio za kilomita tano tunatarajia kwamba zitaongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe, baadhi ya wakuu wa mikoa kutoka kanda ya Ziwa huku pia zikihusisha wadhamini wa mbio hizi kutoka mashirika mbalimabli yaani(Corporates).’’ Alisema.


Aidha wadhamini ambao pia watashiriki katika mbio hizo ni pamoja na kampuni za Tiper, Puma Energy, Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, New Mwanza Hotel, Real PR Solutions, Efm Radio, EF Out Door, CF Hospital na Afrimax Strategic Partnerships Limited.



Alibainisha kuwa mbio hizo za Km 5 zitahusisha watu wenye ulemavu wa ngozi yaani Albino ambapo washindi kwa upande wa mashirika watapatiwa zawadi za utambuzi ikiwemo medali na vyeti vya ushiriki huku pesa zikielekezwa kwa washiriki wenye ulemavu wa ngozi yaani Albino.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA



Mkutano wa 33 wa ALAT wafanyika leo jijini Dar es Salaam

$
0
0
 Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), Abdallah Ngodu akitoa neno la utangulizi kwa wajumbe wa jumuiya hiyo (hawapo pichani) wakati wa jukwaa la mafunzo kwa wajumbe hao katika mkutano wa 33 wa jumuiya hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
 Mwanyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), Gulamhafeez Mukadam akizungumza na wajumbe wa jumuiya hiyo (hawapo pichani) wakati akifungua jukwaa la mafunzo kwa wajumbe wa jumuiya hiyo katika mkutano wa 33 wa jumuiya hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
 Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mh. Isaya Mwita akisisitiza jambo kwa wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) wakati wa jukwaa la mafunzo kwa wajumbe hao katika mkutano mkutano wa 33 wa jumuiya hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) wakimsikiliza Mwanyekiti wa Jumuiya hiyo Gulamhafeez Mukadam (hayupo pichani) wakati akifungua jukwaa la mafunzo kwa wajumbe hao katika mkutano wa 33 wa jumuiya hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) wakimsikiliza Mwanyekiti wa Jumuiya hiyo Gulamhafeez Mukadam wakati akifungua jukwaa la mafunzo kwa wajumbe hao katika mkutano wa 33 wa jumuiya hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.Picha na Eliphace Marwa - Maelezo

Airtel yasherehekea wiki ya huduma kwa wateja kwa kuzindua OFA KAMBAMBE

$
0
0
Airtel leo wamezindua shamra shamra za wiki ya huduma kwa mteja kwa kuwakaribisha wateja wake wote waliongia madukani kwao kwa kukata keki na kuzindua kifurushi maalum cha sh 1000 cha  OFA KABAMBE kinachodumu kwa siku tatu ikiwa ni  ishara yakuwashukuru wateja wote nchini.

Akiongea katika makao makuu ya Airtel Meneja wa Duka la Airtel Bi Celine Njunju alisema “tunawashukuru wateja na wananchi wote kwa ujumla katika wiki hii ya huduma kwa wateja inayoanza tarehe 2 hadi tarehe 6 mwezi Oktoba duniani kote, kwa upendo kabisa Airtel inakupa kifurushi cha OFA KABAMBE kupitia  Airtel Money kitakachokupa uhuru wa kujichagulia kile unachokipenda kutoka Airtel”.

Ukijiunga na Ofa kabambe ya Airtel Money, kwa Tshs 1000 tu! utapata GB 2, Dakika 110 za kupiga mitandao yote na SMS bila ya kikomo, huku ukiwa na uhuru wa kutumia kifurushi hiki ndani ya siku tatu toka pale ulipo nunua. 
Alieleza kuwa “ili kujiunga  Piga *150*60# chagua 6 kufurahia vifurushi vinavyokupa MB na Dakika kibao pamoja na SMS bila ya kikomo”

 “uhuru ni wako tumia utakavyo ndani ya siku tatu. alisisitiza Bi Celine
kwa upande wake Mkurugenzi  wa kitengo huduma kwa wateja wa Airtel Bi Adriana Lyamba alieleza kuwa “ wiki hii huadhimisha kila wiki ya kwanza ya mwezi oktoba kila mwaka, lakini kwetu  Airtel kila siku tunazingatia swala muhimu la kutoa huduma kwa wateja wetu wote kwa viwango vinavyotakiwa “Mwaka huu Airtel tumeipa wiki hii kauli mbiu Building Trust tukimaanisha kuendelea kuwajengea wateja wote Imani katika huduma tunazotoa” alieleza Bi Lyamba .

Bi Lyamba aliendelea kusema “wiki hii pia Airtel tutakuwa na matukio mengi maalumu kwa wateja wetu lakini muhimu zaidi tunawakaribisha wote mtembelee katika ofisi zetu za huduma kwa wateja ili muendelee kujipatia huduma bora kama vile kusajili laini mpya, kujipatia simu na vifaaa vya mawasiliano original kwa bei nafuu na vitakuwa na ofa kabambe maalum kwa ajili yako, pia utaelekezwa jinsi yakutumia huduma zetu kama Airtel Money, Airtel Yatosha, huduma ya kukopa kwa Airtel Money yaani Timiza na nyingine nyingi.

Meneja wa duka la Airtel Makao Makuu Bi Celine Njuju akiongea na wateja leo wakati Airtel ilipozindua wiki ya huduma kwa wateja pamoja na kuzindua kifurushi cha OFA kabambe kinachopatikana kupitia Airtel Money kwa shilingi 1000 tu na kudumu kwa siku 3. kifurushi hiki pia kinampatia mteja GB 2, dakika za maongezi 110 kwenda mitandao yote pamoja na sms bila kikomo uzinduzi wa wiki.

Katikati ni Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Airtel Bi Adriana Lyamba akikata keki kuashiria uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja inayoazimishwa duniani kote kuanzia octoba 2 hadi oktoba 6 huku akiwa amezungukwa na baadhi ya wafanyakazi wa Airtel pamoja na  wateja wa Airtel waliotembelea duka la Airtel Moroco kujipatia huduma.
 Mmoja kati ya wateja wa Airtel Bw, Kassim Nguya akimlisha keki Mkurugenzi wa huduma kwa mteja Bi Adriana Lyamba maalum kwa kuashiria uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja ambayo huanzimishwa kila mwaka mwezi oktoba tarehe 2 hadi 6. airtel pia imezindua kifurushi cha OFA kabambe ambapo kwa  shilingi 1000 mteja anapata  GB 2, dakika za maongezi 110 kwenda mitandao yote pamoja na sms bila kikomo.
 Baadhi ya wateja wa Airtel waliotembelea duka ya Airtel Makao makuu leo wakilishwa keki na Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Airtel Bi Adriana Lyamba leo ikiwa ni kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoazimishwa duniani kote kuanzia octoba 2 hadi 6. Airtel mwaka huu wamesherehekea wiki hio wakiwa na kauli mbiu yao ya BUILDING TRUST yaani kuwajengea wateja Imani kwa kuwapatia huduma zenye viwango. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MFUMO WA ‘DROPWALL’ KUSAIDIA TAKWIMU MASHULENI

$
0
0
MFUMO mpya wa kieletroniki wa ‘Dopwall’ umezinduliwa nchini na unatajwa kuwa utasaidia kupunguza mdondoko wa elimu kwa wananchi wa kike nchini.

Licha ya hali hiyo pia inatajwa kuwa mdondoko wa wanafunzi kwa shule bado ni tatizo nchini ambapo kwa kipindi cha mwaka 2015 wanafunzi 61,488 waliripotiwa kuacha masomo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi Mkurugenzi Mkuu Kampuni ya Eagle Analytics, Rose Funja, alisema kuzinduliwa kwa mfumo huo kusaidia wazazi na walezi kujua hali ya maendeleo ya shule wanasoma watoto wao ikiwemo kuwa na uwezo wa kuhoji kupitia vikao vya wazazi na bodi za shule.

“Serikali kupitia wizara mbalimbali ikiwemo Serikali za Mitaa wameboresha ukusanyaji wa taarifa mbalimbali za kielimu ambazo ni msingi wa mapambano dhidi ya mdondoko wa wanafunzi. Pamoja na jitihada hizo matumizi ya taarifa kama hizo katika kuboresha utendaji wa kila siku wa watumishi wa umma na ufanyaji wa maamuzi hayatoshelezi au hakuna kabisa katika idara za serikali,” alisema Funja
Meneja Ufuatiliaji na Tathimini mradi wa Data kwa Maendeleo ya Jamii wa Tume ya Sayansi na Teknolojia, Dk. Geofrey Chambua akiongea mbele ya wanahabari jijini Dar es Salaam wakati wakimtambulisha mfumo mpya wa kieletroniki wa ‘Dopwall’. Pembeni ni Mkurugenzi Mkuu Kampuni ya Eagle Analytics, Rose Funja ambao ni wasimamizi wa mfumo huo. 
Mkurugenzi Mkuu Kampuni ya Eagle Analytics, Rose Funja ambao ni wasimamizi wa mfumo huo akifafanua machache mbele ya wanahabari jijini Dar es Salaam jinsi mfumo huo unavyofanyakazi. Pembeni ni Meneja Ufuatiliaji na Tathimini mradi wa Data kwa Maendeleo ya Jamii wa Tume ya Sayansi na Teknolojia, Dk. Geofrey Chambua.


PRECISION AIR YAANZA SAFARI RASMI ZA SERENGETI KUPITIA ARUSHA

$
0
0
SHIRIKA la ndege la Precision Air (PW) jana lilizindua safari zake za Serengeti mkoani Mara, kupitia Uwanja wa Ndege wa Arusha.

Uwepo wa safari hizo za ndege utasaidia usafirishaji wa watalii kutoka nchi mbalimbali duniani na ndani ya Tanzania kutembelea hifadhi ya Serengeti kirahisi jambo ambalo litachangia ukuaji wa uchumi nchini.

Pichani juu ni Wafanyakazi wa Ndege ya PrecisionAir na abiria  wakishuka katika Ndege kwenye Uwanja wa Seronera jana walipozind
 Wafanyakazi wa Ndege ya PrecisionAir wakivinjari katika Uwanja wa Seronera jana.
 Wafanyakazi wa Ndege ya PrecisionAir wakiwa katika picha ya pamoja katika uwanja wa Seronera.
 Ndege ya PrecisionAir ikiwa katika Ofisi za Uwanja wa ndege wa Seronera. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Mawakala wa mashindano ya urembo wabanwa

$
0
0
Uongozi wa Kampuni ya Lino International Agency Limited inayoandaa mashindano ya Mrembo wa Tanzania (Miss Tanzania) kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa nchini (Basata) imefanya marekebisho ua Kanuni, Sheria na Taratibu za mashindano ya urembo nchini.

Marekebisho hayo yamefanywa ili kuyafanya mashindano ya Miss Tanzania nchini kuwa bora zaidi na kuondoa changamoto ambazo wadau wake wamekuwa wakizipata.

Afisa Habari wa Lino Internationa Agency Limited, Hidan Ricco amesema kuwa kutokana na kuwa katika mchakato wa kuandaa na kukamilisha taratibu hizo mpya, wamesabisha kuchelewa kupata kibali kutoka Basata cha kuanza mchakato wa mashindano ya mwaka huu ya Miss Tanzania.

Ricco alisema kuwa wapo mawakala ambao tayari wamefanya mashindano na wengine ambao wanakusudia kufanya mashindano na vile vile wapo wengine ambao waliteuliwa kwa mujibu wa sheria ambazo wanatakiwa kuzifuata kabla ya kufanya shindano.

Aliyataka masharti hayo kuwa ni pamoja na kusajiliwa na kulipa ada ya Basata, kukabidhi zawadi za washiriki wote siku 14 kabla ya shindano kwa afisa utamaduni wa ngazi husika na vile vile kutoa taarifa siku saba baada ya mashindano.

“Uongozi wa Kampuni ya Lino International Agency Kimited hautosita kuchukua hatua za kinidhamu kwa wakala ambaye atashindwa kufuata kanuni, sheria na taratibu za mashindano ikiwa amoja na shindano husika,” alisema Ricco.

Aliwaomba waandaaji (mawakala) kuzingatia mashari hayo ambao lengo lake ni kuondoa malalamiko ambayo yamekuwa yakisababisha malumbano mbalimbali miongoni mwa wadau na kampuni yao kunyooshewa kidole.

“Tunasisitiza, wakala ambaye atakwenda kinyume na taratibu zetu atachukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa pamoja na kutotambua shindano lake, hivyo ni wajibu wa wakala kuhakikisha anafuata taratibu hizi kwa lengo la kuboresha mashindano,” alisema.

DK.SHEIN AWAAPISHA MAJAJI WA MAHKAMA KUU YA ZANZIBAR,NA VIONGOZI WENGINE

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bw. Khamis Ramadhan Abdala kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar  katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bibi Aziza Iddi Suwedi kuwa  Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar  katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bw. Kubingwa Mashaka Simba  kuwa  Katibu wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika  hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,kabla alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha  Bw. George Joseph Kazi kuwa  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika  hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar, kabla alikuwa Mrajis wa Mahakama Kuu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Katibu wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya kuwaapisha rasmi leo katika hafla iliyofanyika  ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar (Picha na Ikulu).

UTAFITI WA KILIMO KUFANYIKA NCHI NZIMA KUANZIA KESHO

$
0
0

Na: Veronica Kazimoto.

Serikali kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inatarajia kufanya Utafiti wa Kilimo wa mwaka 2016/17 nchi nzima kuanzia kesho tarehe 3 Oktoba hadi tarehe 3 Novemba, 2017. 

Akizungumza leo wakati wa kufunga mafunzo ya wadadisi watakaokusanya Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 mkoani Dodoma, Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Maria Mashingo amesema lengo la utafiti huo ni kutoa makadirio ya kiasi cha uzalishaji wa mazao makuu, idadi ya mifugo, mazao yatokanayo na mifugo na maeneo ya kilimo katika mikoa yote ya Tanzania.

"Ningependa kuwasisitizia washiriki kuwa, dhumuni kubwa la utafiti huu wa  kilimo ni kutoa makadirio ya uzalishaji wa mazao makuu ya kilimo na maeneo yake yaliyolimwa pamoja na taarifa za mifugo katika mikoa yote ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania", amesema Dkt. Mashingo.

Aidha, Katibu Mkuu huyo ametoa wito kwa wakuu wote wa kaya watakaochaguliwa kushiriki kwenye utafiti huu, kutoa ushirikiano wa kutosha na hususan kutoa taarifa sahihi kuhusu hali ya uzalishaji wa mazao, huduma zinazotolewa na Maafisa Ugani na aina ya mbegu wanazotumia na kubainisha changamoto wanazokumbana nazo katika shughuli zao za kila siku.
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)  Dkt. Albina Chuwa akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 mkoani Dodoma. Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017. 
 Mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Maria Mashingo akihutubia wakati wa kufunga mafunzo ya wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 mkoani Dodoma. Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017. 
 Baadhi ya wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa kufunga mafunzo ya utafiti huo mkoani Dodoma. Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017. 
 Mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Maria Mashingo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa NBS, Chuo cha Mipango na baadhi ya wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17.  Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MBUNGE WA ILALA MUSSA ZUNGU AKAGUA UJENZI WA BARABARA ZA OLYMPIO NA MFAUME, UPANGA MASHARIKI, DAR ES SALAAM, LEO

$
0
0

Mbunge wa Ilala Mussa Zungu (kushoto)

NA BASHIR NKOROMO

MBUNGE wa Ilala, Dar es Salaam, Mussa Azzan Zungu, amesema ameridhishwa na kiwango cha ujenzi wa Barabara ya Olympio, katika kata Upanga Mashariki, huku akilalamikia ujenzi wa Barabara ya Mtaa wa Mfaume ambayo ujenzi wake umekwama. 

Zungu amesema hayo leo alipokagua maendeleo ya ujuenzi wa barabara hizo ambazo zinajengwa kwa kiwango cha lami chini ya usimamizi na gharama za Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam.

"Kama mnavyoiona, barabara hii ya Olympio inayojengwa na kampuni ya kigeni ya China Railway Seventh Group (CRSG), imejengwa kwa kiwango kizuri kabisa, lakini hii ya Mtaa wa Mfaume yenye urefu wa mita 900, ambayo mkandarasi wake ni kampuni ya CASCO abayo ni ya mzawa mwenzetu 

imekwama kumalizika, Sasa tunamtafuta Mwenyekiti wa Halmashauri tujue nini hasa kimesababisha ujenzi wa barabara huu kukwama", amesema Zungu.

Amesema, wakati barabara ya Olympio yenye urefu wa mita 740  ujenzi wake umekamilika kwa kiwango kikubwa tangu Septemba 30, mwaka huu, ujenzi wa barabara ya  Mfaume umekwama hadi sasa kutokana na Mkandarasi kusimamishwa kuendelea kutokana na kuonekana anaijenga kwa viwango vya chini.

Wakala wa Ujenzi wa barabara ya Olympio kutoka kampuni ya CRSG Zhou Cunfei, alisema licha ya ujenzi kukamilika kwa asilimia 95, kampuni hiyo inamalizia sehemu chache zilizobaki na inainatarajia kuikabidhi rasmi Januari 2, mwakani.

  Mbunge wa Ilala Mussa Azan Zungu akikagua ujenzi wa Barabara ya Olympio, Upanga Mashariki jijini Dar es Salaam, leo. Wapili kulia ni Wakala wa Ujenzi wa barabara hiyo kutoka kampuni ya CRSG ya China, Zhou Cunfei

NAIBU WAZIRI MABULA ASEMA JUKUMU LA KUPANGA MIJI KWENYE HALMASHAURI HALIEPUKIKI

$
0
0

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii 

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri kuweka utaratibu wa kupanga miji kama sehemu ya kazi yao kuliko kukurupuka na mashinikizo ya makundi ya watu.

Naibu Waziri Mabula amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa madhimisho ya siku ya Makazi Duniani iliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee.

“Halmashauri ndio zinajukumu kubwa la kupanga miji lakini cha ajabu Halmashauri nyingi zimekuwa zikipima miji kwa mashinikizo ya makundi hali inayofanya kuibuka kwa miji holela mingi katika makazi yetu” Amesema Mabula.Waziri Mabula ameongeza kuwa siku ya makazi inatukumbusha umuhimu wa kuwa na makazi bora yanayoendana na miundombinu ya huduma za kijamii.

Ameweka wazi kuwa kwa sasa Wizara yake imeweza kurasimisha nyumba zaidi ya 2000 katika eneo la Kimara na Mbezi lakini haijamaanisha kuwa zoezi hilo litaweza kuendelea nchi nzima katika maeneo ambayo yamejengwa kiholela.

Ametaja kuwa serikali itaendelea kusimamia mpango kabambe(Master Plan) wa miji yote hivyo hawatakuwa na msamaha kwa wote watakaokwenda kinyume na utaratibu wa mpango huo .
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Angelina Mabula akizungumza na wadau wakati wa maadhimisho ya siku ya Makazi Duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi , John Lupala akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri
Wajumbe kutoka Ushirika wa Nyumba (Mwenge) wakijadili jambo katika Mahadhimisho ya siku ya Makazi Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Karimjee Dar es Salaam.
Wajumbe wa Ushirika wa Viguta wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri , Angelina Mabula

Kesi ya Mke wa Bilonea Msuya yaendelea kupigwa kalenda.

$
0
0

Na Karama Kenyunko
WAKILI wa utetezi katika kesi ya mauaji inayomkabili mke wa marehemu bilionea Msuya, Miriam Mrita (41) na mfanyabiashara Revocatus Muyela (40), ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumuita Afisa wa upelelezi makosa ya jinai wa Temeke,(RCO) aje aeleze upelelezi wa kesi hiyo umefikia wapi.

Wakili Peter Kibatala amedai hayo leo mbele ya Hakimu  Mkazi Thomas Simba baada ya wakili wa Serikali Estazia Wilson kudai kesi hiyo leo ilikuja kwaajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika.

Hakimu Simba amekubaliana na ombi hilo la upande  wa  utetezi na kusisistiza kuwa RCO aitwe mahakamani hapo Kesi hiyo imeahirishwa hadi Octoba 16,2017 kwa ajili ya kutajwa.

Februari 23, mwaka huu, washtakiwa hao waliachiwa huru na mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey  Mwambapa kisha wakakamatwa tena na baadaye kusomewa mashtaka hayo ya mauaji upya.

Katika kesi hiyo namba 5/2017 inadaiwa Mei 25, mwaka jana maeneo ya Kibada Kigamboni Jijini Dar es Salaam, kwa makusudi washtakiwa walimuua dada wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya. 

VODACOM TANZANIA YASHEREHEKEA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA NA WATEJA WAKE

$
0
0
 Mkuu wa kitengo cha maduka ya rejareja ya Vodacom Tanzania PLC, Brigita Stephen akikata utepe kuashiria uzinduzi wa dawati la huduma kwa wateja wa kampuni hiyo”Service desk”lililopo soko la makumbusho jijini Dar es Salaam katika kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoanza kufanyika leo dunia nzima,Wanaoshuhudia kutoka kushoto Meneja wa kampuni hiyo,Fredrick Laini,Mteja na mkazi wa Makumbusho,Alex Kisanga.
 Alex Kisanga(kulia)Ambaye ni Mteja wa kwanza kufika katika dawati la huduma kwa wateja wa Vodacom Tanzania PLC,”Service desk”lililopo soko la makumbusho jijini Dar es Salaam,Akionyeshwa baadhi ya bidhaa zilizopo katika dawati hilo baada ya kuzinduliwa rasmi na Mkuu wa kitengo cha maduka ya rejareja ya kampuni hiyo, Brigita Stephen(katikati)na Meneja wa kampuni hiyo,Fredrick Laini,katika kuazimisha wiki ya huduma kwa wateja inayoanza leo na  kufanyika dunia nzima.
 Mteja wa Vodacom Tanzania PLC,Dkt. Mdimu Ngoma akishirikiana na Mkuu wa kitengo cha maduka ya rejareja wa kampuni hiyo, Brigita Stephen,kukata keki ikiwa ni ishara ya kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoanza leo na kufanyika dunia nzima.

WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA ILIVYOFANA BENKI YA CRDB TAWI LA KARIAKOO JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
BENKI ya CRDB tawi la Kariakoo lasherekea wiki ya huduma kwa wateja ambayo inafanyika kila mwaka kwa wiki nzima kuanzia leo Oktoba 2 hadi Oktoba 6,2017.

Akizungumza katika uzinduzi wa wiki ya Huduma kwa wateja, Meneja wa benki ya CRDB tawi la Kariakoo, Diana Mtalo jijini Dar es Salaam leo amesema wiki hii ni wiki ya huduma kwa wateja na ni wiki ya kuwahudumia wateja pamoja na kuwahamasisha wateja wajitokeze kufungua akaunti katika benki hiyo katika tawi la Kariakakoo jijini Dar es Salaam.

Amesema wateja ambao hawana akaunti katika benki hiyo waende wakafungue ili kuweza kujipatia huduma kedekede zilizopo katika benki hiyo ikiwa pamoja na kujipatia mikopo.
Meneja wa benki ya CRDB tawi la Kariakoo, Diana Mtalo akizungumza na wateja wa Benki ya CRDB tawi la Kariakoo jijini Dar es Salaam na kuwashukuru pamoja na kuwaomba kufungua akaunti za benki katika Tawi hilo kwani wanatoa mikopo mbalimbali katika tawi hilo. Wiki ya Huduma kwa mteja huadhimishwa kila mwaka kwaajili kusherekea pamoja na kuwahudumia wateja wao inavyopaswa.
Baadhi ya Wateja wa Benki ya CRDB tawi la Kariakoo wakifungua Shampeini kwaajili ya kusherekea pamoja wiki ya huduma kwa wateja ambalo huadhimishwa kila mwaka. 
Meneja wa benki ya CRDB tawi la Kariakoo, Diana Mtalo pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Kariakoo wakigonganisha glasi za shampeni kwaajili ya kudherekea wiki ya huduma kwa mteja ambayo huadhimishwa kila mwaka.
Wateja wa benki ya CRDB tawi la Kariakoo wakilishwa keki ikiwa ni kuadhimisha ufunguzi wa wiki ya huduma kwa wateja jijini Dar es Salaam leo.
Wateja na wafanyakazi wa beki ya CRDB tawi la Kariakoo wakiwa katika picha ya pamoja ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka.

DC WA UBUNGO AMEWATAKA WAMILIKI WA VYOMBO VYA MOTO KUZINGATIA SHERIA ZA BARABARANI

$
0
0
MKUU wa Wilaya ya Ubungo,Kisare Makore amewataka wamiliki wa vyombo vya moto kuzingatia sheria za barabarani ili kuepuka ajali zinazosababishwa na madereva wazembe na kuwataka kufanya kazi kwa kuzingatia sheria zilizopo.

Mkuu huyo wa Wilaya ameyasema hayo wakati wa uwekaji saini wa mkataba kati ya Chama Cha Madereva na wamiliki pikipiki mkoa wa Dar es Salaam (CMPD) na Kampuni ya Tanzania Motorcycle and Bajaji Association (TAMOBA)

Kwaajili ya kuzisajili pikipiki na bajaji katika mfumo wa Tanzania tracking technology and security monitoring system utakaowawezesha kujua pikipiki iliyoibiwa ipo eneo gani na kuweza kupatikana kwa haraka zaidi.

Aidha Makore amesema madereva wa pikipiki na bajaji walikuwa na wasiwasi wa kuibiwa vyombo vyao hivyo ila TAMOBA imeleta usalama mzuri kisasa kwa kuwa madereva hao watafanya kazi zao wakiwa hawana wasiwasi wa kuibiwa pikipiki zao na mali zao wawapo katika majukumu yao hayo pamoja na abiria wao.

Kwaupande wake Afisa Utumishi wa TAMOBA,Erasto Lahi amesema kwamba kampuni hiyo inatoza Shilingi mia moja kwa siku kwaajili ya kulinda pikipiki na bajaji

“Mtu aliye katika mfumo huu atapata msaada wa kulindwa muda wote masaa 24, hivyo mmiliki wa chombo muda wowote akihitaji taarifa za chombo kilipo, kilipopita na kinapoelekea atazipata, pia mfumo huu utaunganishwa na Jeshi la Polisi moja kwa moja ili kuharakisha zaidi huduma za kiusalama”alisema Lahi.


Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Kisare Makore (wapili kushoto) kwakushirikiana na viongozi mbalimbli akizindua ofisi za Chama Cha Madereva na wamiliki pikipiki mkoa wa Dar es Salaam (CMPD)
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Kisare Makore akizungumza katika hafla ya kusaini makubaliano ya usajili wa pikipiki na bajaji katika mfumo wa Tanzania tracking technology and security monitoring system utakaowawezesha kujua pikipiki iliyoibiwa ipo eneo gani leo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TAMOBA,Joseph Kimisha akizungumza baada ya kusaini makubalino na Chama Cha Madereva na wamiliki pikipiki mkoa wa Dar es Salaam (CMPD) kwajili ya usajili wa pikipiki na bajaji katika mfumo wa Tanzania tracking technology and security monitoring system.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TAMOBA,Joseph Kimisha na Mwenyekiti wa Chama cha Madereva na wamiliki pikipiki mkoa wa Dar es Salaam (CMPD),Michael Massawe wakisani hati za makubaliano kwajili ya usajili wa pikipiki na bajaji katika mfumo wa Tanzania tracking technology and security monitoring system.

 Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

TANZIA: TANGAZO LA KIFO CHA CLINTON ALEX KAMWELA

$
0
0
Familia ya Kamwela ya Katengele, Ileje, mkoani Mbeya inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao Clinton Alex Kamwela kilichotokea jana Jumapili saa mbili Usiku Iwambi, Mbeya. Mipango ya mazishi inafanyika hapo hapo nyumbani kwa Bw. Ernest Kamwela. Mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho Jumanne Oktoba 2, 2017 huko Katengele, Ileje. Habari ziwafikie ndugu, jamaa, marafiki na majirano popote walipo.


Benki ya NMB yazindua wiki ya huduma kwa wateja, yaahidi kuboresha huduma

$
0
0
Benki ya NMB Tanzania imezindua wiki ya huduma kwa wateja ambapo imeahidi kuboresha zaidi huduma kwa wateja wake wa sasa na kuwafikia wananchi ambao bado hawajapata huduma za kibenki katika maeneo mbalimbali nchini.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Tanzania, Ineke Bussemaker katika uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja na kusema kila mwaka wamekuwa wakiboresha huduma mbalimbali ambazo zinatolewa sasa na kuanzisha zingine mpya na wamejipanga kuhakikisha wanaendelea kuboresha huduma hizo.

“Kila mwaka ni mzuri sababu kunakuwa na jambo tofauti pamoja na hilo pia tupo katika nafasi nzuri kama benki namba moja Tanzania, ni jambo la kujipongeza sababu tulipo sasa sio sawa na miaka 12 iliyopita,

“Tumejipanga kuhakikisha tunaboresha huduma zetu na zaidi kidigitali ili kuahisha huduma za kifedha kuwepo karibu zaidi na wateja wetu, huduma ya kidigitali inahitaji huduma ya intrnet ambayo kwa sasa nchini ipo vizuri na simu ya kisasa (smartphone) ambazo hata gharama zake kwa sasa zipo chini," amesema Ineke na kuongeza.

“Tumekuwa tukitoa huduma boa lakini pamoja na hilo hatuwezi kuwafikia wateja wote ndiyo maana tumekuwa na mawakala zaidi ya 3,500 nchi nzima ambao wamekuwa wakitoa huduma kwa wateja wetu."

Aidha Ineke amesema moja ya changamoto ambayo benki imekuwa ikikutana nayo kwasasa ni huduma za kifedha kupatikana kupitia mitandao hivyo wateja wengine kutumia mitandao yao kuhifadhi pesa lakini wamejipanga kuja na njia mbadala ikiwa na huduma bora zaidi ambazo zitawashawishi wananchi kutumia benki kutuma fedha.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Tanzania, Ineke Bussemaker akizungumza katika uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja katika hafla iliyofanyika leo makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NMB Tanzania wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Tanzania, Ineke Bussemaker (hayupo pichani) katika hafla ya uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Tanzania, Ineke Bussemaker akizindua Wiki ya Huduma kwa Wateja, kwa kuliruhusu gari la huduma kwa wateja kuzunguka kutoa huduma maeneo mbalimbali.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Airtel yasherehekea wiki ya huduma kwa wateja kwa kuzindua OFA KAMBAMBE

$
0
0
Meneja wa duka la Airtel Makao Makuu Bi Celine Njuju akiongea na wateja leo wakati Airtel ilipozindua wiki ya huduma kwa wateja pamoja na kuzindua kifurushi cha OFA kabambe kinachopatikana kupitia Airtel Money kwa shilingi 1000 tu na kudumu kwa siku 3. kifurushi hiki pia kinampatia mteja GB 2, dakika za maongezi 110 kwenda mitandao yote pamoja na sms bila kikomo uzinduzi wa wiki.

Katikati ni Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Airtel Bi Adriana Lyamba akikata keki kuashiria uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja inayoazimishwa duniani kote kuanzia octoba 2 hadi oktoba 6 huku akiwa amezungukwa na baadhi ya wafanyakazi wa Airtel pamoja na  wateja wa Airtel waliotembelea duka la Airtel Moroco kujipatia huduma.
 Mmoja kati ya wateja wa Airtel Bw, Kassim Nguya akimlisha keki Mkurugenzi wa huduma kwa mteja Bi Adriana Lyamba maalum kwa kuashiria uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja ambayo huanzimishwa kila mwaka mwezi oktoba tarehe 2 hadi 6. airtel pia imezindua kifurushi cha OFA kabambe ambapo kwa  shilingi 1000 mteja anapata  GB 2, dakika za maongezi 110 kwenda mitandao yote pamoja na sms bila kikomo.

 Baadhi ya wateja wa Airtel waliotembelea duka ya Airtel Makao makuu leo wakilishwa keki na Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Airtel Bi Adriana Lyamba leo ikiwa ni kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoazimishwa duniani kote kuanzia octoba 2 hadi 6. Airtel mwaka huu wamesherehekea wiki hio wakiwa na kauli mbiu yao ya BUILDING TRUST yaani kuwajengea wateja Imani kwa kuwapatia huduma zenye viwango. 

 Baadhi ya wateja wa Airtel waliotembelea duka ya Airtel Makao makuu leo wakilishwa keki na Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Airtel Bi Adriana Lyamba leo ikiwa ni kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoazimishwa duniani kote kuanzia octoba 2 hadi 6. Airtel mwaka huu wamesherehekea wiki hio wakiwa na kauli mbiu yao ya BUILDING TRUST yaani kuwajengea wateja Imani kwa kuwapatia huduma zenye viwango. 




JUKUMU LA KUPANGA MIJI KWENYE HALMASHAURI HALIKWEPEKI- MABULA

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii 
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri kuweka utaratibu wa kupanga miji kama sehemu ya kazi yao kuliko kukurupuka na mashinikizo ya makundi ya watu.

Naibu Waziri Mabula amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa madhimisho ya siku ya Makazi Duniani iliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee.

“Halmashauri ndio zinajukumu kubwa la kupanga miji lakini cha ajabu Halmashauri nyingi zimekuwa zikipima miji kwa mashinikizo ya makundi hali inayofanya kuibuka kwa miji holela mingi katika makazi yetu” Amesema Mabula.Waziri Mabula ameongeza kuwa siku ya makazi inatukumbusha umuhimu wa kuwa na makazi bora yanayoendana na miundombinu ya huduma za kijamii.

Ameweka wazi kuwa kwa sasa Wizara yake imeweza kurasimisha nyumba zaidi ya 2000 katika eneo la Kimara na Mbezi lakini haijamaanisha kuwa zoezi hilo litaweza kuendelea nchi nzima katika maeneo ambayo yamejengwa kiholela.

Ametaja kuwa serikali itaendelea kusimamia mpango kabambe(Master Plan) wa miji yote hivyo hawatakuwa na msamaha kwa wote watakaokwenda kinyume na utaratibu wa mpango huo.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Angelina Mabula akizungumza na wadau wakati wa maadhimisho ya siku ya Makazi Duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi , John Lupala akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri.
Wajumbe kutoka Ushirika wa Nyumba (Mwenge) wakijadili jambo katika Mahadhimisho ya siku ya Makazi Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Karimjee Dar es Salaam.
Wajumbe wa Ushirika wa Viguta wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri , Angelina Mabula.

Umoja wa wanawake wanasiasa wapinga udhalilishaji wa wanawake katika mitandao ya kijamii.

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
UMOJA wa Wanawake wa Wanasiasa (WCP-Ulingo) umesema  wanawake wamekuwa wanadhalishwa utu wao katika mitandao ya kijamii Si michuzi Media na kutaka vyombo vya dola kuchukua hatua dhidi ya wanaofanya hivyo.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa Sekretarieti ya Umoja huo, Angelina Mtahiwa amesema kuna uovu unafanywa baadhi ya mitandao ya kijamii katika kuwachafua wanawake katika nafasi zao hali ambayo inarudisha nyuma wanawake kuogopa kujihusisha masuala mbalimbali kwa jamii.

Amesema mitandao ya jamii itumike katika kujenga nchi kuelimisha  masuala ya kijamii ili nchi iweze kusonga mbele kiuchumi pamoja kuwatoa  wanawake katika kushiriki nafasi mbalimbali sio kutumika katika mitandao kwa ajili ya kudhalilishwa.

Nae Mjumbe wa Sekretarieti hiyo, Swaum Rashidi amesema kwa sasa wanawake wamekuwa wakishiriki shughuli za kuchumi , siasa, biashara  na kuwa sehemu ya mchano katika kuchangia maendeleo ya taifa.

Swaum amesema wanawake wakidharishwa katika mitandao ya kijamii inawafanya kuwa woga pamoja na kupata wakati mugumu katika familia zao.

Aidha amesema kuwa watu wanaotengeneza taarifa mbaya za wanawake kupitia mitandao ya kijamii wachukuliwe hatua ili hali hiyo isiweze kujirudia.

Aidha Swaum amesema kuwa hawawezi kumtaja mwanamke ambaye amesdhalilishwa na katika mitandao kwani kufanya hivyo ni kuendeleza udhalilishaji huo.
 Mjumbe wa Sekretarieti wanawake wanasiasa WCP-Ulingo, Angelina Mtahiwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya udhalilishaji wa wanawake baadhi ya mitando ya jamii si Michuzi Media, kulia ni  Mjumbe  Swaum Rashidi, kushoto  ni Mjumbe Diminatha Rwechungura.
 Mjumbe wa WCP- Ulingo, Swaum Rashidi akizungumzia juu mitandao ya jamii inavyotakiwa kutumika katika maendeleo na sio kuchafua watu kulia ni anawakilisha  Walemavu WCP –Ulingo Agness Mgaya , kushoto ni  Mjumbe wa Sekretarieti wanawake wanasiasa WCP-Ulingo, Angelina Mtahiwa.
Mjumbe wa Sekretarieti wanawake wanasiasa WCP-Ulingo, Angelina Mtahiwa (katikati )akionesha a mfano wa kutomtaja jina mwanamke jina aliyedhalilishwa katika mitandao ya kijamii kama vyombo vyaha habari vinavyoficha picha za wahusika katika matukio ya udhalilishaji leo jijini Dar es Salaam.

The Rotary Club of Bahari Dar es Salaam inaugurates a Mission Green environmental conservation project

$
0
0
The Rotary Club of Bahari Dar es Salaam on Saturday September 30th, 2017 inaugurated  an environmental conservation project along Barack Obama Road in the City, with over  200 indigenous trees and shrubs planted in the ocean front area across the Aga Khan Hospital, to provide a clean shaded recreational area for residents and to maintain the natural beauty of the waterfront.

This was part of a greater Mission Green Initiative for Rotary District 9211, which encompasses Tanzania and Uganda, with the goal of planting one tree for every Rotarian in the District. The plans for the park were developed in conjunction with municipal authorities, and water for the project has been generously donated by Aga Khan Hospital.

President Amyn Lalji of the Rotary Club of Bahari le  the team in the groundbreaking ceremony under the theme “Greening East Africa one tree at a time: Mission Green” spearheaded by Rotary International District 9211 Governor Kenneth Wycli­ff Mugisha whose aim is to mobilize the community and resources for the restoration and protection of the environment. District 9211 consist of Uganda and Tanzania.

Recognizing the importance of the environment to people’s livelihood in East Africa and the adverse effects the very same livelihood has had on the environment, District Governor Ken Mugisha has chosen the environment to be at the center of his agenda

The annual increment of the urban population in both Uganda and Tanzania was 5.4% in 2015. (World Bank 2015) In comparison, the average for ALL developing countries is just over 3%. The proportion of our population that use wood products in form of charcoal and ‑rewood as fuel for food preparation is too high. As high as 90% in Uganda’s case.

The forest subsector contributed up to 5.2% of the GDP in Uganda and 3.4% in Tanzania. The forest cover as a %ge of land area between 1990 and 2015 declined by 10% in Tanzania and 12% in Uganda During the period 1990 - 2005, total forest and woodland area decreased by 24.7% in Uganda and a whopping 37.4% in Tanzania (rainforests.mongabay.com).

 Chief Guest Permanent Secretary Vice President's Office Professor Faustine kamuzora flags off the initiative by planting a tree along Barack Obama Road in the City, with over  200 indigenous trees and shrubs planted in the ocean front area across the Aga Khan Hospital, to provide a clean shaded recreational area for residents and to maintain the natural beauty of the waterfront.
 President Amyn Lalji of the Rotary Club of Bahari leads the team in the groundbreaking ceremony 
 President Amyn Lalji of the Rotary Club of Bahari speaks during the groundbreaking ceremony 
Rotary Dar Marathon Chair Catherinerose Baretto plants a tree during the ceremony. The five-year project started in  January 2017 to December 2021 as the  District wide project (Uganda and Tanzania)  with the purpose of protectin  the environment and reduce the adverse effetc of climate change and improve the income levels of susceptible groups.
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live


Latest Images