Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110149 articles
Browse latest View live

VIJANA WATAKIWA WASIPISHANE NA FURSA KWENDA NJE YA NCHI NA KUWAACHIA WAGENI

$
0
0

VIJANA wametakiwa wasipishane na fursa kwa kwenda nchi ya nchi kuzitafuta wakati wenzao wa nchi hizo wakija kunufaika nazo hapa nchini.

Rai hiyo imetolewa na Kamishina wa Polisi Mussa Ali Mussa wakati akihutubia kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Siku ya Amani Duniani-Tanzania yaliyofanyika leo Viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam.

"Vijana acheni mipango ya kwenda kuzitafuta fursa nje ya nchi kwani wenzenu kutoka nchi hizo wamekuwa wakija kunufaika nazo hapa nchini" alisema Mussa. Alisema serikali imeweka mazingira mazuri hivyo ni vizuri hali hiyo ikatumika kwa ajili ya kufanya shughuli za maendeleo hasa katika wakati huu nchi ikiingia katika uchumi wa viwanda.

Aliwataka wazazi na walezi kutoa malezi bora kwa watoto wao ili kuwaepusha kujiingiza katika makundi yasiofaa.Katika hatua nyingine Kamishna Mussa alisema amani ya nchi itadumishwa na kila mtu na kuwa watu waondoe dhana ya kuwa amani hiyo italetwa na vyombo vya dola ikiwemo polisi.

Alisema suala la amani si la mtu mmoja bali ni la kila mtu jeshi la polisi kazi yake ni kuilinda na kumkamata mtu yeyote anayeonekana kusababisha viashiria vya kutoweka kwa amani hiyo.Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa na Mkuu wa Shirika la UN linaloshughulikia wahamiaji la IOM,  Dk. Quasim Sufi alisema amani ni jambo la muhimu kwa nchi na mustakari wa maendeleo.

Alisema bila ya amani hakuna kitu kitakacho weza kufanyika na ndio maana UN imekuwa ikisisitiza amani duniani kote.Sheikh Hemed Bin Jalala alisema amani ndiyo msingi wa dini zote ya kiislam na kikristo na kuwa amani haipaswi kuchezewa kwani ndio neema tuliyopewa na mwenyezi mungu.

Jalala alisema amani ni msingi wa dini uliojengwa kiimani na kutakiwa kuihubiri na kuwa wale wanaohubiri vita na machafuko wanatoka katika dini ya mashetani.Afisa Habari Kitemgo Cha Habari cha Umoja wa Mataifa-UNIC, Stella Vuzo aliwataka vijana kuendelea kuidumisha amani iliyopo nchini kwani wao ndio rahisi kurubuniwa kutokana na kuwa wengi.

"Katika maadhimisho ya siku ya amani duniani tunapenda kuwashirikisha vijana kutokana na wingi na umuhimu wao katika kutunza amani" alisema Vuzo.Alisema vijana watumie fursa ya amani iliyopo nchini katika kufanya shughuli zao za  maendeleo badala ya kukaa bure.

Vuzo alisema Kauli Mbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu ni  " Pamoja Katika Kudumisha Amani: Heshima, Usalama na Utu kwa wote"

Maadhimisho hayo yameandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na taasisi mbalimbali kama  Global Peace Tanzania, Global Network of Religions for Children- GNRC, Chama cha Scout Tanzania, Asasi ya Vijana wa Umoja wa mataifa YUNA Tanzania, wanafunzi na wananchi.
  Kamishna wa Polisi Mussa Ali Mussa, akiwa amebeba mfano wa picha ya ndege wa kuashiria amani, kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Siku ya Amani Duniani-Tanzania yaliyofanyika leo Viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam.
 Maandamano ya kuadhimisha siku hiyo yakifanyika.
 Wanafunzi wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
 Wawakilishi mbalimbali na viongozi wa dini  wakiwa wamebeba mfano wa ndege huyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Makala Maalum ya Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki 2017 (JAMAFEST),Kampala-Uganda

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 24,2017

TOYOTA RAV 4 FOR SALE

$
0
0
Toyota RAV 4. 
Colour-Silver. 
Year of Manufacture 2000. 
Engine Capacity 1990. 
Fuel-Petrol.

Call
+255 658 870 112




MZIKI MNENE EFM, HAUJAWAACHA SALAMA KWA WAKAZI WA KINONDONI

$
0
0
Na Agness Francis Blogu ya jamii
Katika tamasha la tamasha la muziki Mnene lililokonga nyoyo za mashabiki  ambalo limefanyika  katika ukumbi wa New Msasani Jijini Dar es Salaam  ambapo wasanii kama Chidi Benzi, Nuhu Mziwanda, Izzo Business, Bob Junior, Makomando pamoja na Kayumba Asosiye  mshindi wa BSS walitoa burudani ya kutosha  kwa wakazi hao wa Kinondoni.

Hata hivyo Michuzi Blog imezungumza na msanii Kayumba Asosiyee ambaye mpaka hivi sasa yupo chini ya meneja wake Mkubwa Fella ametanabaisha kuwa kuwepo kwa tamasha  hilo la Mziki nene linasaidia kukuza  vipaji vya wasanii chipukizi vilivyolala.

Vile vile msanii huyo amesema  kuwa changamoto ya muziki wa sasa mchuano umekuwa mkali sana kwa sababu mashabiki wanajua muziki mzuri, inabidi kupambana ili kuhakikisha unatoa kitu chenye ubora, na amewaahidi mashabiki wake wake mkao wa kula anatarajia kutoa ngoma yake hivi karibuni.                      
Mwanamuziki wa kizazi kipya Chidi Benzi akiwaburudisha mashabiki wake na kuwa acha midomo wazi Kwa kazi nzuri alioifanya katika tamasha la muziki Mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya  Izzo Business akifanya yake jukwaani    kuwaburudisha mashabiki  wake na wapenzi wa hip hop waliojitokeza Kwa wingi katika tamasha hilo la muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya Nuhu Mziwanda akizima kiki na kuwasha muziki katika kuhakikisha wakazi wa Kinondoniwanapata Burundi  kabambe akiimba  nyimbo yake mpya ambayo inajulikana kama  bao  la ushindi katika tamasha hilo la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya  kundi La Masada sita  wakitia burudani Kwa kuimba na kucheza kuwaburudisha wazi wa maeneo hayo  ambao hawakuachwa salama Kwa shoo nzuri iliofanywa na wadada hawa katika tamasha la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.

Mashabiki na wakazi wa Kinondoni waliojitokeza Kwa wingi kushuhudia shoo ya kukata na shoka kutoka Kwa wasanii Mbalimbali wa hapa nchini wakitoa burudani  kwao katika tamasha la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salama. Picha na Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.

TAMASHA LA SANAA NA UTAMADUNI LA KIMATAIFA BAGAMOYO LADHAMIRIA KULETA TIJA ZAIDI KWA WASANII WA NDANI NA NJE YA NCHI

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kulia) akimsikiliza mjasiriamali wa kazi za sanaa kutoka Dar es Salaam Bibi. Magreth Kabonge (kushoto) alipotembelea banda lake kabla ya kufungua Tamasha la 36 la Sanaa na Utamaduni la kimataifa Bagamoyo jana katika Taasisi ya TaSUBa. Kulia ni Mtendaji Mkuu Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbert Makoye.

Bodi ya Ushauri ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) imeagizwa kukaa na kufanya tathmini ya kina kuandaa mpango mkakati mzuri wa namna ya kuliendesha tamasha la Sanaa na Utamaduni ili liweze kuwa na tija zaidi kwa wasanii na Taasisi kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe wakati wa uzinduzi wa tamasha la 36 la Sanaa na Utamaduni la kimataifa Bagamoyo jana katika Taasisi hiyo mjini Bagomoyo. “Tangu kuanzishwa kwa tamasha hili mwaka 1982, Tamasha limeendelea kuwa kivutio kikubwa kwa wasanii na wadau wa sanaa ndani na nje ya nchi na wananchi kwa ujumla hivyo ni vyema Bodi ya ushauri ya TaSUBa ikapanga mikakati yenye tija zaidi kwa maslahi ya wasanii wetu na Taasisi yetu” amesema Mhe. Mwakyembe.

Aidha Mhe. Mwakyembe ameipongeza Bodi, Menejimenti, wafanyakazi na wanachuo wote wa TaSUBa kwa kazi kubwa wanayoiofanya kila mwaka ya kuandaa na kuendesha Tamasha hilo kwa kipindi cha miongo mitatu na nusu mfululizo na kuwataka kutembea kifua mbele kwa rekodi hiyo iliyotukuka ndani na nje ya nchi.

Mhe. Mwakyembe amesema kuwa lengo la Tamasha hilo ni pamoja na kutunza na kuenzi sanaa na utamaduni wa mtanzania, kutengeneza jukwaa ambalo wanafunzi wa TaSUBa wanalitumia kupima kiwango chao cha umahiri katika sanaa kwa mwaka, kukutanisha watu wa tamaduni mbalimbali kutoka sehemu tofauti duniani ili kuonyesha utajiri wao wa sanaa na utamaduni, pamoja na kutengeneza jukwaa ambalo ni kiungo cha kujenga mahusiano ya wasanii wa ndani na nje ya nchi kupitia maonyesho ya sanaa na kubadilishana uzoefu na uwezo katika kuendeleza tasnia ya sanaa.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbert Makoye amesema kuwa taasisi inajivunia mafanikio makubwa wanayoendelea kuyapata kupitia tamasha hilo kwani kwa sasa tamasha linajumuhisha wasanii wa ndani na nje ya nchi pamoja na wanafunzi waliosoma katika taasisi hiyo miaka ya nyuma na waliopo mafunzoni.

Aidha Dkt. Makoye amewashukuru wakazi wa Bagamoyo kwa ushirikiano ambao wamekua wakiuonyesha katika kushirikiana na Taasisi kuendeleza na kuthamini sanaa na utamaduni wa mtanzania.

Naye Chifu wa Unyanyembe na Mwenyekiti wa Chama cha Machifu Tanzania Mhe. Msagati Fundikira amewapongeza watendaji wa TaSUBa kwa kutoa wataalamu wazuri katika fani ya sanaa na utamaduni kwani kwa ufanya hivyo wamekua wakiendeleza na kudumisha utamaduni wa mtanzania kwa vizazi vya leo.


Tamasha hili la 36 la Sanaa na Utamaduni la kimataifa la Bagamoyo lenye kauli mbiu isemayo “Sanaa na Utamaduni katika kupiga vita madawa ya kulevya” limeshirikisha wasanii kutoka Kenya, Ufaransa, Uingereza, Zimbabwe na Mayyote na kuudhuriwa na mabalozi mbalimbali akiwemo balozi wa Malawi, balozi wa Palestina, balozi wa uholanzi, pamoja na wawakilishi kutoka ubalozi wa Zambia, Saudi Arabia, Msumbiji, Japani, Ujerumani, Marekani, India, Shirikisho la Urusi, Angola na Kenya.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akiangalia moja ya kazi za sanaa iliyotengenezwa na mbunifu kutoka Arusha Bi. Joyce Lema (kushoto) alipotembelea banda lake kabla ya kufungua Tamasha la 36 la Sanaa na Utamaduni la kimataifa Bagamoyo jana katika Taasisi ya TaSUBa.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akionyesha picha yenye mfano wa sura yake iliyochorwa na kalamu ya risasi na mwanafunzi kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Bw. Baraka Jeje (kushoto) alipotembelea banda lake kabla ya kufungua Tamasha la 36 la Sanaa na Utamaduni la kimataifa Bagamoyo jana katika Taasisi ya TaSUBa.
Baadhi ya wanafunzi kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) wakiimba wimbo wa taifa wakati wa uzinduzi wa Tamasha la 36 la Sanaa na Utamaduni la kimataifa Bagamoyo jana katika Taasisi hiyo.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

NEW HIT IN TOWN: Lady Jaydee - IMissYou

MSANII LULU DIVA KUSHIRIKISHWA NGOMA MPYA NA MZIMBABWE

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Lulu Abbas maarufu kama "Luludiva" amekuwa akiendelea kujikusanyia lundo la mashabiki wa kazi zake kwa muda mfupi aliokaa kwenye game, ndani na nje ya nchi kutokana na jitihada zake katika muziki, huku nyimbo zake zikifanya vizuri katika media mbalimbali za hapa nchini, Afrika Mashariki, Nigeria, South Africa na Congo

Kwa Mara ya kwanza amefanikiwa kupata collabo ya kimataifa, akishirikishwa na msanii maarufu kutoka nchini Zimbambwe ambaye yupo chini ya label ya Military touch inayomilikiwa na msanii Jah Prayzah aliyefanya nyimbo na Diamond Platnum.

Akizungumza na Ripota wa Globu ya Jamii, Lulu diva ameyazungumza haya, "Jah Prayzah najuana naye toka naenda South Africa kufanya video ya  nyimbo yangu ya pili ya Usimwache, aliniambia anakuja Tanzania akifika tuonane na alipofika alinitafuta na kuniomba nifanye collabo na msanii wake Exq ambaye yupo chini yake" alisema Lulu diva.

Aliendelea kusema kuwa "Alinisikilizisha nyimbo nikaiona ni nzuri na mimi naweza fanya kitu kizuri, kwa hiyo sikusita kutoa jibu nilikubali hapo hapo sababu niliona nitapata faida hasa kwa kuongeza kundi lingine la mashabiki kutoka Zimbabwe". 

Lulu diva alisema kuwa walifikia muafana na muandaaji huyo na kufanya nyimbo hiyo na muda wowote itaanza kusikika katika redio na televisheni mbalimbali hapa nchini.  hiyo anawaomba mashabiki wake wawe tayari kusikia na kuona.

Nyimbo hiyo imefanywa na Maproducer wakubwa watatu ambao ni
Producer wao: Tamuka huku kwa upande wa Tanzania ni: Abbydady, Tuddy Thomas.

WATU WAHAMASIKA KUPIMA AFYA KATIKA TAMASHA LA NGOMA ZA ASILI - RUGWE

$
0
0
WATU zaidi ya 800 wamejitokeza kupima afya ya magonjwa yasiyoambukiza katika Viwanja   vya Tandale Wilayani Rungwe ambapo Tamasha la Ngoma za asili linalojulikana kwa Tulia Traditional Dances Festival 2017 lililoandaliwa na Naibu Spika Dk. Tulia Ackson linafanyika.

Akizungumzia hili, Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya (NHIF) Afya Ofisi ya Mbeya, Isaya Shekifu alisema pamoja na kuenzi utamaduni wamegundua kuwa watu wengi hawana utamaduni wa kufika Hospitalini kwa ajili ya kupima afya zao kwa ajili ya kupata ushari na tiba ya magonjwa yasioambukiza ambayo ni tishio kubwa kwa afya za wengi.

Alisema Mfuko uliona utumie fursa ya mashindano ya Ngoma za asili kwa ajili ya kuwafikia watu wengi ili waweze kupima na kupatiwa ushauri na elimu juu ya magonjwa mbalimbali ikiwemo Sukari, shinikizo la damu na unene ulipitiliza.
Alisema wananchi wengi wamehamasika na kujitokeza kupima na kupata ushauri kutoka kwa madaktari waliopo katika viwanja hivyo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa NHIF, Bi. Anjela Mziray alisema pamoja na kupima afya katika mashindano hayo ambayo huduma hutolewa bure pia Mfuko unahamasisha na kusajili watoto wa chini ya umri wa miaka  18 na huduma ya bima ya afya. Huduma hii inajulikana kwa jina la Toto Afya Kadi.

Alisema zoezi la kuandikisha linafanyika kiwanjani hapo na kadi kutolewa ndani ya muda mfupi kwa mchango wa shilingi 50,400 tu kwa mwaka kwa kila mtoto ambapo mtoto atapata matibabu kwa mwaka mzima katika Zahanati,Vituo vya Afya na Hospitali zote zilizosajiliwa na Mfuko huo Tanzania nzima.
Aidha alitoa wito kwa wazazi na Walimu kuchangamkia fursa hiyo kwa kuwa shule nyingi za bweni zinakabiliwa na changamoto ya matibabu kwa wanafunzi hivyo kila mwanafunzi akiwa na Bima ya afya itamrahishia kupata matibabu kwa uhakika akiwa shuleni na hata wakati wa likizo.

Nao baadhi ya Wateja waliojitokeza kupata huduma katika Banda la Bima ya Afya, Staford Mwakasapa na Mwalimu Elizabeth Sekile ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Wilaya ya Rungwe wamepongeza utaratibu huo na kuongeza kuwa huduma kama hiyo inapaswa kusambazwa katika kila mikusanyiko.
Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa NHIF, Anjela Mziray akizungumza na waandishi wa habari.

Walisema watu wengi hawana utaratibu wa kwenda Hospitali kupima afya zao hadi waugue hivyo huduma ya kutembelea na kutoa elimu napaswa kusogezwa na kuwa endelevu ili kuokoa afya za wananchi.

Hata hivyo walitoa wito kwa Serikali kuhakikisha wateja wenye kadi za matibabu ya Bima ya Afya wanapata huduma zote zinazostahili ikiwemo upatikanaji wa Vifaa tiba pamoja na madawa kwa wagonjwa.

TANZIA: MSANII MOHAMED IDI MTURUMA AKA MUDDY ALIYEKUWA ANAISHI UJERUMANI AMEFARIKI NCHINI SPAIN

$
0
0
Marehemu Mohamed Idi Mturuma aka Muddy enzi za uhai wake.

Umoja wa Wa Watanzania Ujerumani kwa ushirikiano na watanzania wanaoishi England na Spain kwa masikitiko makubwa sana tulipata msiba wa ndugu yetu mtanzania mwenzetu mcheza sarakasi Mohamed Idi Mturuma aliekuwa akiishi koloni Ujerumani na kufariki nchini spain alikokwenda kikazi.

Aliaga dunia tarehe 19.09.17 Kwa ushirikiano wa Watanzania wanaoishi nchi hizo tumeazimia kufanya kila liwezekanalo ili kuweza kusafisrisha mwili wa Marehemu ndugu yetu Mohamed Idi Mturuma kwenda kuzikwa nyumbani Tanzania Umoja wa Watanzania Ujerumani (UTU.e.V ) Unawatangazia watanzania wote wanaoishi popote pale Duniani kuunga mkono azma yetu kwa kutoa michango ya hali na mali ili tumsafirishe mwenzetu.

Shukran nyingi kwa msanii Mussa FAB Moses Kutoka England ambaye alisafiri mara baada ya msiba kutokea kwenda Spain kwa ajili ya kusaidia mchakato wa kuandaa kusafirisha mwili wa marehemu. Mussa Fab Moses anategemea kusafiri na mwili wa Merehem kwenda Tanzania kwa Mazishi

Watanzania wanaoishi England mnaweza kuwasiliana moja kwa moja na Saidi Kanda ili kuwasilisha michango yenu namba ya kiganjani +447404066607

Watanzania wanaoishi Tanzania mnaweza kuwasiliana na Eddy Sengo ili kuwasilisha michango yenu namba ya kiganjani +255656210725

Watanzania wanaoishi Ujerumani mnaweza kuwasiliana na Makamo mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania Ujerumani (UTUe.V) Malumbo Salim Malumbo namba ya simu +49 1522 4082848

Mwili wa Marehemu ulisaliwa msikitini siku ya ijumaa iliyopita tarehe 22.09.17 na kupelekewa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti kwa ajili ya kusubiria safari.

UMOJA NI NGUVU; PENYENIA PANA NJIA; TUKITAKA TUTAWEZA KWA KUDRAZA MWENYEZIMUNGU INSHALLAH WABILAHI TAWFIQ

UMOJA WA WATANZANIA UJERUMANI (UTU e.V)
 Waumini wa kiisalam nchini spain wakijiandaa kuusalia mwili wa marehem Mohamedi Idi Mturuma nchi spain.
 Waumini wakiislam wakielekea msikitini kuusalia mwili wa marehemu Mohamedi Idd Mturuma.
baadhi ya marafiki  zake marehemu Mohamedi Idi Mturuma baada ya kutoka kuusalia mwili wa marehemu.

SERIKALI KUTATUA CHANGAMOTO YA KODI SHULE BINAFSI

$
0
0
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 10 ya Shule ya Sekondari Baobab, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akihutubia Jumuiya ya Shule ya Sekondari Baobab, wakati wa mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa Kidato cha Nne wanaotarajiwa kufanya mitihani yao siku chache zijazo.

Benny Mwaipaja, WFM, Pwani

SERIKALI imeahidi kuyafanyiakazi malalamiko ya wamiliki wa shule za binafsi nchini kuhusu kodi mbalimbali wanazotozwa kwa kuwa Serikali inathamini mchango mkubwa wa taasisi binafsi za elimu katika mapambano dhidi ya adui ujinga.

Ahadi hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, wakati wa sherehe za mahafali ya kumi ya kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Baobab, iliyoko Mapinga, Wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani.

Dokta Kijaji amesema kuwa tayari Serikali imeondoa baadhi ya kodi kwa shule hizo ikiwemo kodi ya mabango, Usalama mahali pa kazi-OSHA, Ada ya zimamoto, na kwamba kikosi kazi kilichoundwa na Serikali kupitia upya kodi zingine zinazoonekana kuwa kikwazo katika utoaji wa elimu, kinaendelea na kazi na matokeo yake yataonekana hivi karibuni.

“Niko kwenye kikosikazi kinachoshughulikia changamoto za kodi kwenye shule za watu binafsi ninaamini suluhisho litapatikana kutokana na Serikali kuthamini mchango wenu mkubwa katika kuwapatia vijana wetu elimu” alisema Dkt. Kijaji

Alieleza kuwa katika Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2017/2018, suala hilo litazingatiwa na kuwataka wamiliki wa shule binafsi nchini kuwa watulivu wakati jambo hilo linafanyiwakazi tena kwa umakini mkubwa.

Awali Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari Baobab, Bw. Halfan Swai, pamoja na kuiomba Serikali ifute kodi mbalimbali wanazotozwa kwa kuwa hawafanyibiashara bali wanaisaidia Serikali kutoa huduma kwa jamii, ameomba pia isaidie  kuangalia viwango vya riba vinavyotozwa na taasisi za fedha nchini kwa kuwa zinawawekeka katika mazingira magumu wanapohitaji mikopo ya kuendeleza shule zao.

Wanafunzi 149, (wavulana 14 na wasichana 135)  wa Shule hiyo wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao ya kidato cha nne hivi karibuni, wameahidi kufanya vizuri katika mitihani yao kwa kuwa wameandaliwa vizuri na walimu waliobobea katika ufundishaji pamoja na mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia shuleni hapo.

Dokta Ashatu Kijaji, mbali na kuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo, yeye na familia yake wameshuhudia mtoto wao Samira, akiagwa wakati wa mahafali hayo yaliyohudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wazazi, ndugu na jamaa wa wanafunzi hao.
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 10 ya Kidato cha Nne ya Shule ya Sekondari Baobab, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akimkabidhi zawadi mmoja wa wanafunzi mwenye ulemavu aliyefanya vizuri katika baadhi ya masomo wakati wa sherehe ya kuwaaga, iliyofanyika shuleni hapo.
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 10 ya Kidato cha Nne ya Shule ya Sekondari Baobab, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), (Katikati), akikabidhi keki kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Baobab, iliyoko Mapinga, Bagamoyo, mkoani Pwani, ikiwa ni alama ya kusherehekea siku yao ya kuagwa shuleni hapo.

Kampuni ya LG Electronics Yatoa Msaada wa Sare za Shule

$
0
0
Meneja Mkuu Masoko, wa kampuni ya LG Electronics, Tawi la Afrika Mashariki, Moses Marji (kulia) na Ofisa wa LG, Mohamed Ibrahim, wakimvisha sare mpya ya shule, mwanafunzi, Issa Abas, mwenye ulemavu wa ngozi, albinism katika Shule ya Msingi ya Uhuru Mchanganyiko jiji Dar es Salaam, jana, wakati kampuni hiyo ya LG Electronics imetoa msaada wa sare za shule kwa Shule ya Msingi ya Uhuru Mchanganyiko kama sehemu ya Wajibu wa Jamii wa Kampuni kwa lengo la kusaidia watoto wenye ulemavu nchini Tanzania, kufuatia shule hiyo ya Uhuru Mchanganyiko kukabiliwa na changamoto mbalimbali katika kuwaelimisha watoto wenye ulemavu ambao wana mahitaji maalum.
Meneja Mkuu Masoko, wa kampuni ya LG Electronics, Tawi la Afrika Mashariki, Moses Marji (kulia) na Ofisa wa LG, Mohamed Ibrahim, wakimvisha sare mpya ya shule, mwanafunzi, Kelvin Joseph, mwenye ulemavu wa kutosikia, katika Shule ya Msingi ya Uhuru Mchanganyiko jiji Dar es Salaam, jana, wakati kampuni hiyo ya LG Electronics imetoa msaada wa sare za shule kwa Shule ya Msingi ya Uhuru Mchanganyiko kama sehemu ya Wajibu wa Jamii wa Kampuni kwa lengo la kusaidia watoto wenye ulemavu nchini Tanzania, kufuatia shule hiyo ya Uhuru Mchanganyiko kukabiliwa na changamoto mbalimbali katika kuwaelimisha watoto wenye ulemavu ambao wana mahitaji maalum.
Meneja Mkuu Masoko, wa kampuni ya LG Electronics, Tawi la Afrika Mashariki, Moses Marji (katikati mwenye kofia) , katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Uhuru Mchanganyiko jiji Dar es Salaam, jana, wakati kampuni hiyo ya LG Electronics imetoa msaada wa sare za shule kwa Shule ya Msingi ya Uhuru Mchanganyiko kama sehemu ya Wajibu wa Jamii wa Kampuni kwa lengo la kusaidia watoto wenye ulemavu nchini Tanzania, kufuatia shule hiyo ya Uhuru Mchanganyiko kukabiliwa na changamoto mbalimbali katika kuwaelimisha watoto wenye ulemavu ambao wana mahitaji maalum.

JESHI LA POLISI LAFUNGA MAFUNZO YA UTAYARI KATIKA CHUO CHA POLISI KIDATU

$
0
0
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi (DCP) Leonard Paulo (katikati), akiwa ameongozana na Naibu Kamishna wa Polisi mstaafu (DCP) Venance Tossi (Kushoto) na Mkuu wa chuo cha Polisi Kidatu kilichopo mkoani Morogoro, kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Zarau Mpangule, wakati alipowasili katika chuo hicho kwa ajili ya kufunga mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo askari wakati wanapotekeleza majukumu yao. Picha na Jeshi la Polisi.
Naibu Kamishna wa Polisi mstaafu (DCP) Venance Tossi (Kushoto), akizungumza jambo na Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi (DCP) Leonard Paulo (katikati), muda mfupi kabla ya kufunga mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo askari wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi (DCP) Leonard Paulo, akifanya mazoezi ya viungo na baadhi ya askari wanaoshiriki Mafunzo ya Utayari na kujengewa uwezo wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi, mafunzo yanayofanyika katika Chuo cha Polisi Kidatu Kilichopo mkoani Morogoro. Picha na Jeshi la Polisi.

Kwa simu Toka London: Kutana na Mwanamke anayeongoza Timu ya Mpira

WAMILIKI WA SHOWROOM WAONYESHWA ENEO LILILOTENGWA KWAAJILI YA BIASHARA YA MAGARI KIGAMBONI

$
0
0
Wamiliki wa Showroom za kuuza Magari leo wamepelekwa Kigamboni kwenye eneo maalumu lililotengwa kwaajili ya Kuuza Magari (Dar es Salaam Automobile Zone) kwaajili ya kukagua  eneo hilo na kuonyeshwa namna ya kumilikishwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa amesema eneo hilo litamilikishwa kwa Wamiliki wa Showroom kwa Muda wa Miaka Mitatu ya Mwazo Bure kisha Baada hapo watawekewa utaratibu wa Malipo.

Amesema Wamiliki hao watatakiwa kutoa kiasi cha Shilingi 300,000 kama dhamana ya kuonyesha nia. Amesema kuwa ukubwa wa eneo lilitengwa kwaajili ya Showroom ni Square Meter 750,000 ambapo lipo eneo lingine la ziada lenye ukubwa wa kiasi cha Square Meter zaidi ya 300,000.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya Kigamboni Rahel Mhando amesema mradi huo ni fursa kubwa ya Maendeleo kwa Wilaya hiyo. Amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kwa kubuni Mpango huo ambao pia utafanya Wilaya ya Kigamboni kuwa kwenye mpangilio Mzuri.

Nae Salim Chicago ambae ni mmiliki wa Showroom amesema Mpango huo utawapa unafuu wa kupata huduma zote ikiwemo TRA, TPA,BIMA,SUMATRA,Kituo cha Polisi na huduma za Kibank ndani ya eneo moja. Aidha amesema Mpango huo utawarahisishia kupata Wateja wengi na wa uhakika kutoka ndani na Nje ya Nchi.
Hata hivyo amesema utaratibu huo utawawezesha kulipa kodi ya Serikali na kuwabana wale Wafanyabiashara wanaofanya biashara za magari kwenye maeneo bubu.

Ikumbukwe kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda alitoa agizo la kuwataka wenye Showroom na Yard za kuuza Magari kuhakikisha wanahamia Kigamboni kwenye eneo maalumu lililotengwa kwaajili ya Showroom kabla ya Mwezi January Mosi mwakani.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa (wakwanza kushoto) akizungumza na wamiliki wa Showroom za kuuza Magari katika eneo maalumu lililotengwa kwaajili ya Kuuza Magari (Dar es Salaam Automobile Zone).
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa (katikati) akiwaonesha wamiliki wa showroom eneo lililotengwa kwaajili ya biashara ya magari Kigamboni jijini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

DC MTATURU AWASIHI VIJANA KUDUMISHA NIDHAMU NA MSHIKAMANO

$
0
0

Na Mathias Canal, Singida

Vijana wametakiwa kusimamia misingi ya Nidhamu ndani na nje ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi kwa kuhuisha mshikamano ili kulinda misingi ya Utaifa na uwajibikaji kwani wao ndio nguvukazi ya Taifa na ushindi wa Chama Cha Mapinduzi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya siasa Wilaya wakati akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi kwenye mkutano wa uchaguzi wa viongozi wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa shule ya Sekondari Ikungi.

Mhe Mtaturu alisema kuwa Dhana ya Demokrasia ni jambo muhimu linalohitaji kuheshimiwa na kuenziwa ndani ya Chama na  Jumuiya zake hivyo kuimarisha nidhamu, mshikamano na upendo ndio silaha pekee itakayoleta heshima ndani ya jumuiya ya vijana wa CCM ili iweze kusonga mbele zaidi na kuwa na mafanikio makubwa katika kuimarisha kipato cha vijana.

Alisema kuwa Nia ya UVCCM ni kujenga na kudumisha haiba  njema ya kuendelea kuheshimu misingi ya demorasia ya kweli, yenye kuchunga  adabu na kufuata nidhamu, miiko na maadili kwa kila mwanachama anayetaka kutumia haki ya kuchagua au kuchaguliwa.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Siasa Wilaya akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi ulioketi kuchagua uongozi wapya watakaoiongoza jumuiya hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Siasa Wilaya akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi ulioketi kuchagua uongozi wapya watakaoiongoza jumuiya hiyo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi wakimsikiliza mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kabla ya kuchagua uongozi wapya kuongoza jumuiya hiyo ngazi ya Wilaya.

UTHIBITISHO WA MALIPO YA TSH MIL 43 KWENDA NAIROBI HOSPITAL KUSAIDIA MATIBABU YA MH TUNDU LISSU

MZIKI MNENE EFM, HAUJAWAACHA SALAMA KWA WAKAZI WA KINONDONI

$
0
0
Na Agness Francis Blogu ya jamii.

Katika tamasha la tamasha la muziki Mnene lililokonga nyoyo za mashabiki  ambalo limefanyika  katika ukumbi wa New Msasani Jijini Dar es Salaam  ambapo wasanii kama Chidi Benzi, Nuhu Mziwanda, Izzo Business, Bob Junior, Makomando pamoja na Kayumba Asosiye  mshindi wa BSS walitoa burudani ya kutosha  kwa wakazi hao wa Kinondoni.

Hata hivyo Michuzi Blog imezungumza na msanii Kayumba Asosiyee ambaye mpaka hivi sasa yupo chini ya meneja wake Mkubwa Fella ametanabaisha kuwa kuwepo kwa tamasha  hilo la Mziki nene linasaidia kukuza  vipaji vya wasanii chipukizi vilivyolala.

Vile vile msanii huyo amesema  kuwa changamoto ya muziki wa sasa mchuano umekuwa mkali sana kwa sababu mashabiki wanajua muziki mzuri, inabidi kupambana ili kuhakikisha unatoa kitu chenye ubora, na amewaahidi mashabiki wake wake mkao wa kula anatarajia kutoa ngoma yake hivi karibuni.                      
Mwanamuziki wa kizazi kipya Chidi Benzi akiwaburudisha mashabiki wake na kuwa acha midomo wazi Kwa kazi nzuri alioifanya katika tamasha la muziki Mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya  Izzo Business akifanya yake jukwaani    kuwaburudisha mashabiki  wake na wapenzi wa hip hop waliojitokeza Kwa wingi katika tamasha hilo la muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya Nuhu Mziwanda akizima kiki na kuwasha muziki katika kuhakikisha wakazi wa Kinondoniwanapata Burundi  kabambe akiimba  nyimbo yake mpya ambayo inajulikana kama  bao  la ushindi katika tamasha hilo la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya  kundi La Masada sita  wakitia burudani Kwa kuimba na kucheza kuwaburudisha wazi wa maeneo hayo  ambao hawakuachwa salama Kwa shoo nzuri iliofanywa na wadada hawa katika tamasha la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.

Mashabiki na wakazi wa Kinondoni waliojitokeza Kwa wingi kushuhudia shoo ya kukata na shoka kutoka Kwa wasanii Mbalimbali wa hapa nchini wakitoa burudani  kwao katika tamasha la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salama. Picha na Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.

DK.SHEIN AWAAPISHA VIONGOZI MBALI MBALI LEO

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Dkt,Idris Muslim Hija kuwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais,hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,kabla ya Uteuzi huo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,[Picha na Ikulu.] 24/09/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bw.Joseph Abdalla Meza kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi,hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,kabla ya Uteuzi huo alikuwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais,[Picha na Ikulu.] 24/09/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bw.Juma Ali Juma kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara,Viwanda na Masoko,hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,kabla ya Uteuzi huo alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bw.Bakari Haji Bakari kuwa Katibu Mtendaji wa Bazara la Biashara la Zanzibar hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,kabla ya Uteuzi huo alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara,Viwanda na Masoko,[Picha na Ikulu.] 24/09/2017.

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TPA YAKAMATA BOTI ILIYOTUMIKA KUIBA MAFUTA BAHARINI

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari-TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko (kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), kuhusu mafuta yanavyopakuliwa kutoka kwenye meli, alipotembelea bandarini hapo ili kupata maelezo kuhusu mchakato wa kupata mita mpya za kupimia mafuta (Flow Meters), Jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko (kushoto) akimuonesha Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), namna maharamia wa mafuta walivyoharibu miundombinu ya bomba la mafuta baharini, baada ya kufanikiwa kukamata boti moja na vifaa vyake lililokuwa likitumiwa na wahalifu hao kuiba mafuta.
Boti Jeupe lililonaswa na kikosi maalumu cha kuzuia uhalifu cha Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) juzi wakati wahalifu wakijiandaa kutoboa bomba na kuiba mafuta kwenye kina kirefu cha Bahari ya Hindi. Wahalifu walifanikiwa kutokomea kusikojulikana baada ya kujitosa baharini, Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwapongeza askari wa doria waliofanikisha kukamata boti moja pamoja na vifaa vyake muhimu ikiwemo injini baada ya kuwadhibiti maharamia waliotaka kutoboa bomba na kuiba mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mmoja wa maafisa wa TPA walioongoza zoezi la kupambana na wahalifu wanaoiba mafuta kwenye bomba la mafuta akionesha vilipuzi vilivyokamatwa vilivyokuwa vitumiwe na wahalifu waliokuwa wakijaribu kuiba mafuta kwenye bomba la mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam.
Kaimu Kamisha na Kodi za Ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Elijah Mwandumbya, akitoa maelezo kwa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), kuhusu hatua zilizochukuliwa kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali upande wa mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko, akitoa maelezo walipokuwa wakiagana na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb)Katika ziara hiyo Waziri Mpango amepongeza juhudi mbalimbali zinazofanywa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania na Mamlaka ya Mpato katika kudhibiti ukwepaji kodi.
Mmoja wa maafisa wa TPA walioongoza zoezi la kupambana na wahalifu wanaoiba mafuta kwenye bomba la mafuta akionesha vilipuzi vilivyokamatwa vilivyokuwa vitumiwe na wahalifu waliokuwa wakijaribu kuiba mafuta kwenye bomba la mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam.



Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (mbele), akiwa ametoka kukagua mitambo ya kupitisha mafuta kutoka kwenye Meli ili kujihakikishia kama hakuna namna ya ubadhilifu au hujuma kwa mapato ambayo Serikali inatakiwa kuyapata.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa pili kulia)na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko (kulia) na wengine, walipotembela Bandari ya Dar es Salaam, kitengo cha Mafuta, kukagua flow meters na tukio la kukamatwa kwa boti lililokuwa likitumika kuhujumu bomba la mafuta.


Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango
Viewing all 110149 articles
Browse latest View live




Latest Images