Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110087 articles
Browse latest View live

MWANAMUZIKI JOHN KITIME ANAKUALIKA WEWE KIJANA WA ZAMANI NA WASASA KATIKA BURUDANI YA MUZIKI WA ENZI HIZO PALE SALANDER BRIDGE KILA IJUMAA


MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 22,2017

WANANCHI WAITIKIA WITO WA SERIKALI WA KUSAJILIWA VITAMBULISHO VYA TAIFA

$
0
0
Wananchi wa Wilaya ya Kilolo wameendelea kujitokeza kwa wingi kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ya usajili ambayo ni kujaza fomu za maombi ya Usajili na fomu zao kupitishwa na Serikali za Vijiji wanakoishi.

Zoezi linaenda sambamba na uhakiki wa taarifa za wananchi wanaoomba kupewa vitambulisho vya Taifa chini ya Kamati za Ulinzi na Usalama ngazi ya Mitaa na Vijiji kabla ya kutoa nafasi kwa wananchi kuweka Mapingamizi ya wazi kwa wale waombaji wanaotiliwa shaka uraia wao kabla ya kuendelea na mchakato wa Uzalishaji.

Wilaya ya Kilolo ni Wilaya ya mwisho kukamilisha zoezi hili kwa mkoa wa Iringa na hivyo kutoa fursa ya kuanza kwa matumizi ya Vitambulisho vya Taifa kielektroniki.

Mbali na Iringa mikoa mingine inayoendelea na zoezi hilo ni ya Kanda ya Ziwa ikiwemo; Geita, Shinyanga, Mwanza, Manyara na Singida.
Baadhi ya wananchi wakiwa katika chumba cha usajili tayari kusajiliwa.


Hawa ni baadhi tu ya wananchi waliojitokeza katika zoezi la Usajil Vitambulisho vya Taifa Wilaya ya Kilolo mkoa wa Iringa. Kwa sasa zoezi hili linafanyika kwa awamu ngazi ya Kata ili kutoa fursa kwa wananchi wote wenye sifa kusajiliwa.
Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa akiingiza taarifa za wananchi kwenye mfumo kabla ya kuchukua taarifa za kibaiolojia za wananchi wa Kilolo ambako zoezi kwa sasa linaendelea.
Mmoja wa wananchi akichukuliwa alama za vidole na saini ya kielektroniki ikiwa ni hatua muhimu kabla ya kukamilisha hatua za Usajili Vitambumnbulisho vya Taifa. Mkoa wa Iringa ni moja ya Wilaya zinazo endelea na Usajili kwa sasa kati ya mikoa 11 ya Tanzania.

SPIKA JOB NDUGAI AHUDHURIA MAZISHI YA FAMILIA YA ALIYEKUWA NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA WILAYANI MPWAPWA MKOANI DODOMA

$
0
0
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akiongoza viongozi Mbali mbali wa serikali katika misa ya kuaga miili ya familia ya aliekuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Ndg. Gregory George Teu, uliofanyika leo katika kanisa la Anglikana Tanzania (Dayosisi ya Mpwapwa)iliyopo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akiweka Shada ya maua katika mazishi ya familia ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Ndg. Gregory George Teu, yaliyofanyika leo katka makaburi ya kanisa la Anglikana Tanzania (Dayosisi ya Mpwapwa) iliyopo Mpwapwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akimfariji Mbunge Mstaafu wa Mpwapwa Mjini Mhe. Gregory George Teu (kushoto) kwa Msiba wa familia yake uliotokea tarehe 18 Septemba, 2017 nchini Uganda, kabla ya kuanza kwa mazishi yatafanyika leo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.


Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati)akiwasili katika Msiba wa familia ya Mbunge Mstaafu wa Mpwapwa Mjini Mhe. Gregory George Teu uliotokea tarehe 18 Septemba, 2017 nchini Uganda, ambapo mazishi yatafanyika mapema leo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akiongoza viongozi Mbali mbali wa serikali katika kuaga miili ya familia ya aliekuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Ndg. Gregory George Teu, katika msiba uliofanyika leo nyumbani kwake Mpwapwa Mkoani Dodoma.

Wananchi Mbali mbali waliohudhuria katika Msiba wa familia ya aliekuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Ndg. Gregory George Teu uliotokea tarehe 18 Septemba, 2017 nchini Uganda, katika mazishi yaliyofanyika leo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.

PICHA NA OFISI YA BUNGE

Tamasha la Utamaduni Tukuyu Ni Chachu ya Kukuza Na Kuendeleza Utamaduni Nchini

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel amewataka Watanzania kuenzi na kuimarisha utamaduni wao ili kuepukana na chamgamoto ya utamaduni kutoka nchi za magharibi unaoletwa ukuaji wa sayansi na teknolojia.

Prof. Elisante ametoa kauli hiyo leo Tukuyu wakati wa ufunguzi wa tamasha la Ngoma za jadi linaloratibiwa na Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson inayojishughulisha na masuala ya kukuza na kuendeleza utamaduni nchini.

Prof. Elisante amewahakikishia vijana kuwa kuwekeza mahali salama, hivyo waendelee kukuza sanaa yao iweze kujijengea jina na kutambulika ndani na nje ya nchi.“Vijana muendelee kuthamini utamaduni wetu, tusiposimamia, kuwekeza na kuthamini utamaduni wetu, utamaduni wan chi za magharibi utawachukua vijana wetu na kuacha tunu yetu ya asili tangu enzi za babu zetu” alisema Prof. Elisante

Prof. Elisante amewahakikishia waandaaji wa tamasha hilo kuwa Serikali ipo sambamba nao na kuwataka wapanue wigo wa tamasha hilo ili liweze kuwa na matawi na kuwafikia watu wengi zaidi nchi nzima.Akifungua tamasha hilo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala amesema limekuwa kichocheo cha kukuza na kuendeleza utamaduni wa Mtanzania hatua inayoongeza fursa ya ajira kwa vijana mkoani Mbeya. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyevaa mashuka ya Kimasai) akiongea na washiriki wa tamasha la Ngoma za jadi linaloratibiwa na Taasisi ya Tulia Trust leo wilayani Tukuyu mkoani Mbeya. Wa kwanza kushoto ni Mwasisi wa taasisi hiyo ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala akifungua tamasha la ngoma za jadi leo wilayani Tukuyu mkoani humo ambapo amesisitiza Watanzania kukuza na kuendeleza utamaduni wa Mtanzania hatua inayoongeza fursa ya ajira kwa vijana mkoani humo.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akipokea zawadi ya CD kutoka kwa Mchungaji Damian Matipa wa Kanisa la Uponyaji Mbeya Mjini yenye nyimbo za kumpongeza Naibu Spika kwa kazi anazofanya.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel mara baada ya kuwasili Tukuyu mkoani Mbeya.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiteta jambo na Mkuu wa Majeshi Mtaafu Jenerali Davis Mwamunyange wakati wa tamasha la Ngoma za jadi linaloratibiwa na Taasisi ya Tulia Trust leo wilayani Tukuyu mkoani Mbeya.
Ngoma ya Bugobo gobo kutoka Bujara mkoani Mwanza
Baadhi ya viongozi wakiwa wamebeba moja ya vifaa Bugoyangi (nyoka) vinavyotumiwa na kikundi cha kucheza ngoma cha Bujora mkoani Mwanza.
Picha na Eleuteri Mangi, WHUSM, Tukuyu, Mbeya.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

HAFLA YA CHAKULA CHA JIONI ILIOANDALIWA NA KINANA KWA AJILI YA KIONGOZI WA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA VIETNAM MJINI DODOMA JANA SEPTEMBER 21,2017

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Alhaj Adamu Kimbisa akimtolea ufafanuzi wa zawadi ya kinyango Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam uku katibu Mkuu wa (CCM) akishuhudia zoezi hilo,wakati wa hafla ya Chakula cha Jion ilioandaliwa na kinana.
 Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza kabla ya Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam kukabidhiwa zawadi na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Alhaj Adamu Kimbisa wakati wa hafla ya Chakula cha Jion.
 Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza na balozi wa Vietnam Nguyen kim Doanh.
 Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akifurahia jambo na wageni wake toka chama cha Kikomunisti cha Vietnam (VCP) jana wakati wa hafla ya chakula cha jion.
 Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha jion.

RAIA WA UHOLANZI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUISHI NCHINI BILA KIBALI

$
0
0
Raia wa uholanzi, Monique Honsbeek Amanzi, ameieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, rafiki yake wa kiume ambaye ni askari polisi kitengo cha Trafiki amemchania hati yake ya kusafiria.

Amanzi (28), amedai hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa alifikishwa mahakamani hapo kujibu tuhuma zinazomkabili za kuishi nchini bila ya kuwa na kibali.

Akisomewa mashtaka yake na wakili wa serikali kutoka ofisi za Uhamiaji, Nivatus Mlay amedai, Septemba 11 mwaka huu (2017) katika makao makuu ya ofisi za uhamiaji mshtakiwa huyo, akiwa raia wa Uholanzi alikutwa akiishi nchini bila ya kuwa na kibali.  Baada ya kumaliza kusomewa tuhuma zake hizo. 

Aliulizwa kama ni kweli au la, ndipo Amanzi akadai kuwa, alikuwa na hati yake ya kusafiria ambayo rafiki yake huyo wa kiume trafki aliyemtaja kwa jina la Letiko Kulwa wa Makumbusho Victoria aliichana na hivyo kumfanya asijue kama visa yake ilikuwa imeisha.

Amedai, alikuja nchini akitokea uholanzi akiwa na mumewe Ibrahim Abasa, na watoto wao wawili lakini baadae waliachana ndipo akampata trafiki huyo ambaye walizaa nae mtoto mmoja lakini alifariki.

Amedai ameishatoa taarifa katika kituo cha polisi miaka miwili iliyopita juu ya kuchanwa kwa hati yake lakini RB aliyopewa ameipoteza. Pia alishaenda kutoa taarifa Uhamiaji lakini hakupata msaada wowote.
Kesi hiyo itatajwa Septemba 27 mwaka huu.

WAZIRI KAIRUKI AZINDUA BODI YA PILI YA UONGOZI INSTITUTE

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki amesema kuwa wakurugenzi walioteuliwa katika bodi ya Taasisi ya Uongozi  ni watu makini na wenye uzoefu wa muda mrefu katika nafasi mbalimbali ,hivyo watatoa ushauri mzuri kwenye taasisi hiyo.

Waziri Angellah aliyasema hayo katika uzinduzi wa bodi ya pili ya Taasisi  ya Uongozi uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini  Dar es Salaam. Amesema bodi ya wakurugenzi wa taasisi hiyo wamepita katika utumishi na wazalendo katika sehemu zao mbalimbali ambapo watakuwa msaada mkubwa kwa taasisi hiyo katika  kutoa ushauri.

Amesema kuwa Uongozi Institute ilianzishwa kwa ajili ya kuwajengea uwezo viongozi wa Afrika katika kuangalia maendeleo endelevu ya bara la Afrika  hivyo wajumbe wa bodi ni wa kimataifa na wanatambulika.

Angellah amesema kuwa walioteuliwa na Rais Dk.John Pombe Magufuli watatimiza majukumu yao na wataendelea kupewa ushirikiano pamoja na viongozi wengine wa Afrika katika kuwa na ajenda ya kuandaa viongozi.

Amesema uongozi Institute inatakiwa kutimiza mambo matatu moja ni bidhaa ya huduma iliyo na kiwango bora, kuangalia rasilimali  ya kuweza  kufanya taasisi hiyo ikue katika kuangalia vyanzo vya mapato pamoja na kujengea uwezo wa kuendelea kutekeleza ajenda ambazo zimeibuliwa.

Walioteuliwa katika bodi hiyo Mwenyekiti ni Balozi wa Finland Inchini Afrika Kusini, Kari Alanko , Makamu wa Rais Profesa Idris Kikula wengine ni Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora  Dk. Laureane Ndumbaro,  Katibu Mtendaji wa SADC Dk. Stergomena Tax, Profesa Penina Mlama wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Christina Duarte Waziri wa Zamani wa Fedha , Mipango na Utumishi wa Cape Verde, Mkurugenzi wa Nodic Afrika ya nchini Sweeden Lina Soiri, pamoja Mkurugenzi wa zamani wa shule ya utawala ya nchini Uingereza , David Walker.

Nae Afisa Afisa Mtendaji Mkuu wa Uongozi Institute, Profesa Joseph Semboja  amesema kuwa chombo hicho kilianzishwa katika kuwajengea viongozi wa Afrika ambao waliridhia kuundwa kwa chombo hicho.

Amesema kuwa Taasisi hiyo imetoa mafunzo mbalimbali tangu kuanzishwa kwake na itaendelea kutoa mafunzo kwa watumishi.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki akizungumza katika uzinduzi wa bodi ya pili ya Wakurugenzi wa Uongozi Institute , uliofanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Uongozi Insitute, Profesa Joseph Semboja akizungumza katika uzinduzi wa bodi ya Uongozi Institute  juu ya taasisi hiyo inavyofanya kazi  katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Uongozi Institute ,Balozi wa Finland Inchini Afrika Kusini, Kari Alanko akitoa shukurani kwa Waziri Kairuki  mara baada ya kuzinduliwa  bodi hiyo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki akigawa vitabu vya miongozo kwa wajumbe wa Bodi hiyo.
 Sehemu watendaji mbalimbali wa serikali waliohudhuria uzinduzi wa bodi ya pili ya oungozi institute.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki akiwa katika picha ya pamoja na bodi ya ya wakurugenzi ya Uongozi Institute, jijini Dar es Salaam.

KAMISHNA WA UTAWALA POLISI MAKAO MAKUU AKIFUNGA MAFUNZO UTAWALA

$
0
0
 Naibu Kamishna wa utawala polisi makao makuu DCP Leonard .l. Paulo alie katikati akiongozana na wenyeji wake mkuu wa chuo cha polisi kidatu baada ya kuwasili chuoni hapo ACP, Zarau .H Mpangule alie mkono wa wa kushoto na alieko kulia ni Kamanda wa polisi Msitafu DCP  Venance Tossi.  Picha na Jeremia.
 Kamanda wa polisi Msitafu DCP Venance Tossi  wakijadili jambo na Naibu Kamishna wa utawala polisi makao makuu DCP Leonard .l. Paul.
Naibu Kamishna wa utawala polisi makao makuu DCP Leonard .l. Paul akilakiwa au kupokelewa kwa shangwe na  wakanguzi waliokuwa wanaitimu mafunzo yao katika chuo cha polisi Kidatu. 

TIMU YA NDANTO FC YATWAA KOMBE LA MICHUANO YA 'TULIA CUP 2017'

$
0
0
 Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Davis Mwamunyange, akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya Ndanto Fc, Peter Mwakingwa, baada ya kushika nafasi ya nafasi ya kwanza na kutwaa kombe la fainali za 'Tulia Cup 2017' kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya. Picha na Muhidin Sufiani (MAFOTO MEDIA GROUP)
 Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Davis Mwamunyange, akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya Isange, Frank Asilih, baada ya kushika nafasi ya pili katika fainali za 'Tulia Cup'kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya.
 Beki wa timu ya Isange Fc, Zawadi Andombwisye (kushoto) akichuana kuwania mpira na mshambuliaji wa Ndanto Fc, Erick Mwangoye, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5.
 Beki wa timu ya Ndanto Fc,Fidelis Yeo (kulia) akiwania mpira na mshambuliaji wa Isange Fc, Hussein Thom, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5.
  Wachezaji wa Isange Fc, Shadrack Kandrum (kushoto) na Hussein Thom (kulia) wakimdhibiti Mandela Chaile, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS ABBAS: AIDHA UHURU AU HAKI KAMILI KWA WOTE, KATIKA NCHI YA PALESTINA YA KIHISTORIA

$
0
0
Rais wa Palestina “Mahmoud Abbas” amesisitiza kuwa uhuru  wa nchi yake upo karibu hauepukiki na kwamba uvamizi wa Israeli unafikia mwisho, akisema: "Aidha upatikane uhuru au haki kamili ya wote katika nchi ya Palestina ya kihistoria."

Rais Abbas Jumatano jioni akihutubia Mkutano wa 72 wa Umoja wa Mataifa, ameongeza kusema kwamba, imepita miaka ishirini na minne tangu kusainiwa kwa Mikataba ya mpito ya Oslo, ambayo ilionesha ukomo wa uvamizi wa Israeli na kuwapa matumaini Wapalestina, ya kuanzishwa kwa Dola yao huru, huku akihoji " Tuko wapi sasa na matumaini haya?."

Amesema:"Tumekubali uwepo wa Dola ya Israeli  kupitia mipaka ya mwaka 1967, lakini Israeli kutokubali uwepo wa Dola ya Palestina kunatupa maswali mengi. Badala ya kuzingatia sababu, inafanya juhudi kuteka misimamo ya kimataifa kwa masuala yasiyo na uzito wowote, yatokanayo na sera zake za kikoloni. Tunapoitaka na kutakiwa na jumuiya ya kimataifa kukomesha uvamizi wake, inadai ni uchochezi na kukosekana  ushiriki wa Palestina na kuwekwa kwa masharti yasiyowezekana."

Rais Abbas ameongeza kusema kuwa,anaelea machafuko ni Utawala wa kivamizi wa Israeli katika ardhi yetu,uvamizi ambao umefikia zaidi ya nusu karne,huku zaidi ya miaka kumi sasa tumekubaliana  kuunda kamati ya pande tatu ambazo ni Marekani,Israeli na Palestina, ili kumaliza suala la uchochezi.Kamati  imefanya kazi kwa muda, lakini tumekuwa tunatoa wito wa kufufuliwa wa kamati hiyo hatupati mrejesho. Hivi ni nani anaekaribisha hilo na kufanya juhudi ya kulifanya liwepo?.

Amesema pia,kuendelea kwa uvamizi ni aibu kwa Israeli na Jumuiya ya Kimataifa,ni wajibu wa Umoja wa Mataifa kumaliza uvamizi huo ili kuwezesha jamii ya Palestina kuishi kwa uhuru na ustawi katika ardhi yake,huku mji mkuu wake ukiwa ni Jerusalemu ya Mashariki.

"Kukomesha uvamizi na vitendo vyake vya kidhalimu, vitakuwa na athari kubwa mno katika kupambana na udaidi pia mashirika yake kukosa karatasi muhimu ambazo huzitumia kwa kuuza fikra zao."Tunatilia mkazo la kukaliza uvamizi ili kukamilisha juhudi zetu katika kukabiliana na mashirika hayo ya kigaidi,kwani Wapalestina wapo dhidi ya ugaidi wa ndani,kikanda na wa kimataifa.

HOSPITALI YA TEULE MUHEZA YAPATIWA MSAADA WA MASHUKA

$
0
0

HOSPITALI ya Teule wilayani Muheza Mkoani Tanga imepata msaada wa mashuka 50 kwa ajili ya kukabiliana na uhaba uliopo kutokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya wagonjwa wanao kwenda kupata matibabu kutoka maeneo mbalimbali hasa vijijini.

Hatua ya uhaba huo unatokana na uchakavu wa wa mashuka unaotokana na kufubaa unaosababishwa na maji wanayotumia kufulia kutokana na uhaba wa maji hali iliyopelekea kuwepo uhitaji kila wakati ili kuweza kukithi mahitaji ya wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu.

Hayo yalibainishwa jana na Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Muheza, Boniphace Mhabe wakati akipokea msaada wa mashuka 50 kutoka kampuni ya Suba Agro Trading na Engineering ambao ni mzalishaji wa mbegu bora zamahindi kwa kushirikiana na Cimmity taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mahindi na Ngano.

Shuka hilo zilitolewa kwa ajili ya wodi ya wakina mama wajawazito kwenye hosptali ya Teule Muheza,Hospitali ya wilaya ya korogwe na ile ya wilaya ya Handeni lengo kubwa likiwa kuwaondolea changamoto zinazowakabili.

"Vitanda vipo vingi lakini tatizo kubwa ni mashuka na hili linatokana na asilimia kub wa kuchakaa kutokana na maji lakini pia wakati mwengine yanabadilika rangi jambo ambalo limekuwa changamoto kwao.
Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Muheza,Boniface Mhabe kushoto akipokea msaada wa mashuka 50 kutoka kwa Afisa Masoko na Mauzo wa Kampuni ya Sub Agro Trading anda Engineering,Neema Ng'unda kwa ajili ya wodi ya wakina mama wajawazito kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza jana ilkiwa ni kutambua mchango mkubwa wa wanawake katika kilimo wa pili kutoka kushoto ni Afisa Mauzo wa Suba Agro Trading yenye makao makuu yake mjini Arusha,Shillaga Samweli .


WAZIRI UMMY ALAANI KITENDO CHA MWALIMU KUMPA MIMBA MWANAFUNZI WA DARASA LA SABA WILAYA YA KALAMBO MKOANI RUKWA

NAIBU KATIBU MKUU, NISHATI NA MADINI AKUTANA NA BALOZI WA SWEDEN NCHINI

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini, Katarina Rangnitt (kushoto) katika kikao chake kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini zilizopo jijini Dar es Salaam tarehe 22 Septemba, 2017. Kikao hicho kilishirikisha wataalam kutoka Idara ya Nishati, Wizara ya Nishati na Madini, na Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (PURA).
Sehemu ya wajumbe wa kikao hicho wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (hayupo pichani).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (PURA), Chalers Sangweni (kulia) na mjiolojia kutoka mamlaka mamlaka hiyo, Simon Nkenyeli (kushoto) wakifuatilia majadiliano mbalimbali katika kikao hicho.
Mtaalam wa Masuala ya Nishati kutoka Ubalozi wa Sweden Nchini, Jorgen Eriksson (kushoto) akieleza jambo katika kikao hicho. Kulia ni Balozi wa Sweden Nchini, Katarina Rangnitt.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi  Juliana Pallangyo (katikati) na Balozi wa Sweden Nchini, Katarina Rangnitt ( wa nne kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kikao hicho.  

WAFANYAKAZI WASHAURIWA KUPIMA AFYA MARA BAADA YA KUSTAAFU.

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO Dodoma.

Wafanyakazi nchini wameshauriwa kupima afya zao mara tu wanapostaafu ili kujihakikishia ikiwa hawajaathirika na kazi ambazo wamekuwa wakizifanya.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Eric Shitindi alipokuwa akifungua semina ya viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) na viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi juu ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, leo Mjini Dodoma.

“Kumekuwa na mazoea kwa wafanyakazi kupima Afya pale tu wanapoajiriwa na kutotilia maanani upimaji afya zao mara wanapostaafu ili kujua ikiwa kazi wanazozifanya zimewaathiri kwa kiasi gani,” amesema Shitindi.

Ameendelea kwa kusema kuwa, upimaji wa afya mara baada ya kustaafu utasaidia watumishi kujua afya zao na ikiwa watakuwa wameathirika upitia kazi walizokuwa wakizifanya basi mwajiri atawajibika mkulipa fidia mtumishi huyo.
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi. Khadija Mwenda akiongea na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati wa Ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi Leo Mjini Dodoma.Kulia ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule
 Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi akiongea na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati wa Ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi ambapo aliwashauri wafanyakazi nchini kupima afya mara wanapostaafu ili kujihakikishia kama hawajaathirika na kazi walizokuwa wanafanya.Katikati ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule na Kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi. Khadija Mwenda 
 Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule akiongea naViongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati wa Ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi, kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi na kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi. Khadija Mwenda.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

IN MEMORY OF MWALIMU CLARA GASPAR MAREALLE

$
0
0
04 AUGUST 1930 – 22 SEPTEMBER 2009

Days, weeks, months and years came and gone. It is now 8 years since you left us, desolate and bereft. Mama your bountiful, unconditional and unwavering Love and support to your husband, children, grandchildren and family members gardened you unprecedented admiration from the Marealle and Lyimo Clans, then and always! You left a foot print in this earthly world of ours. We loved you Mama, and will forever Love You.

Rest in Eternal Bliss Mama.

MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI WAKANUSHA TAARIFA YA UZUSHI INAYOSAMBAZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII

SSRA Yatakiwa kusimamia Michango ya Wanachama

$
0
0

Na. Zawadi Msalla. 

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mh. Alli Karume ameitaka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kusimamia kwa ukaribu michango ya Wanachama kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii  ili itumike kwa malengo yaliyokusudiwa kwa mujibu wa Sheria zilizoanzisha mifuko hiyo. 

Wito huo umetolewa jana mjini Kigoma na Waziri Karume alipotembelea banda la SSRA kwenye maonesho ya wiki ya Bahari duniani yanayoendelea kwenye viwanja vya shule ya msingi Mlole Mkoani humo.

Waziri Karume alisema SSRA inawajibu mkubwa wa kumlinda mwanachama wake ili kuhakikisha hapati matatizo pale anapotakiwa kupata mafao yake.Pia alisisitiza kuwa Itakuwa ni jambo la kuumiza sana inapotokea mwanachama mwenye matumaini ya kupata mafao yake atakapoambiwa mfuko umefilisika na hivyo mafao anayoyatarajia hawezi kuyapata.

Aidha Mhe. Karume aliipongeza SSRA kwa elimu wanayoendelea kuitoa kwa jamii juu ya umuhimu wa kujiunga na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na  jinsi wanavyo simamia maboresho mbalimbali yanayoendelea katika sekta hiyo. 
Hata hivyo alisema bado SSRA inawajibu mkubwa wa kutoa elimu kwa jamii ili kushawishi wananchi kuona umuhimu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwani wapo wananchi wengi wasio fahamu umuhimu wa  mifuko hiyo na wengi wao hupata shida inapofikia kipindi cha uzeeni.
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Alli Karume  akipata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na SSRA kutoka kwa Afisa Uhusiano wa Mamlaka Bw. Sabato Kosuri alipotembelea banda hilo  wakati wa maadhimisho ya siku ya Bahari Duniani yaliyofanyika mkoani Kigoma.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

BARAZA LA TAIFA LA UJENZI NI MUHIMU KATIKA KUTOA TAARIFA MBALIMBALI ZA SEKTA YA UJENZI NCHINI –PROFESA MBARAWA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Serikali  imesema kuwa Baraza la Taifa la Ujenzi ni muhimu kwa taifa pamoja na kwa wananchi katika kutoa taarifa mbalimbali zinazohusu  sekta ujenzi nchini.

Hayo ameyasema leo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa wakati akifungua warsha ya Baraza la Taifa la Ujenzi kujadiliana la maboresho ya baraza hilo, uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere leo jijini Dar es Salaam, Profesa Mbarawa amesema kuwa hakuna mtu ambaye anajua gharama ya mraba wa mita moja ambapo kazi hiyo ilitakiwa kufanywa na baraza hilo.

Amesema kuwa wakati mtu anataka kujenga nyumba anaweza kupata gharama katika baraza la ujenzi na kuachana na ujenzi wa mazoea ambao unachukua gharama kubwa.

Mbarawa amesema  bidhaa zinaingia nchini lakini hakuna anayejua gharama na ubora na kutofautisha na bidhaa zingine za ambapo kazi hiyo baraza la taifa la ujenzi linatakiwa kufanya.

Amesema kuwa kama mambo hayaendi sawa kutokana na sheria yuko tayari kubadilisha sheria  ili baraza lifanye kazi yake kwa maendeleo ya taifa.

Aidha Mbarawa amesema warsha hiyo italeta mapendekezo ya kina kutokana na wadau waliopo katika sekta ya ujenzi ili iweze kuleta matokeo chanya.

Nae  Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano-Ujenzi, Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema warsha hiyo watajadili  katika kuborseha baraza hilo.

Amesema kuwa wadau wa sekta ya ujezi watakuwa huru na wazi katika uchangiaji masuala mbalimbali ikiwa na malengo ya kuborsesha sekta ya ujenzi.

Mwenyekiti wa Baraza hilo, Profesa Mayunga Mkunya amesema kuwa kufanyika kwa baraza hilo ni matokeo kile kitachojadiliwa kuwezesha katika kujenga baraza.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano , Profesa Makame Mbarawa akizungumza katika ufunguzi wa warsha ya kujadili mabaoresho ya baraza la taifa la Ujenzi lililofanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano-Ujenzi, Mhandisi Joseph Nyamhanga akizungumza juu ya baraza la Taifa la Ujenzi linavyofanya kazi leo katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Ujenzi,  Profesa Mayunga Mkunya akizungumza juu warsha hiyo itavyoleta matokeo yaliyotokana na majadiliano na wadau leo katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya wadau ya wakiwa kwenye Warsha ya Baraza la Taifa la Ujenzi kujadiliana maboresho ya baraza hilo, iliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa warsha ya baraza la Taifa la Ujenzi leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere leo jijini Dar es Salaam.  

Wanafunzi wang’ara shindano la Genius CUP.

$
0
0
Mkurugenzi wa shule ya Feza Ibrahim Yunus kushoto na kulia Mwalimu Mkuu wa Feza Boys, Saimon Albert  wakiwa kwenye picha ya pamoja na mshindi wa kwanza hadi watatu wa mashindano hayo. Wa kwanza kushoto ndiye Perfect Ndyetabura  aliyeibuka mshindi wa kwanza kutoka shule ya msingi Hazina  na Hamza Azaeli mwenye miwani aliyeibuka mshindi wa pili naye akitokea shule ya Hazina na watatu anatoka shule ya Feza.

WANAFUNZI wa shule ya Msingi Hazina ya jijini Dar es Salaam, wameibuka washindi kwenye mashindano ya Genius CUP, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mwanafunzi aliyeshika nafasi ya kwanza  kwenye mashindano hayo ni Hamza Azaeli na Perfect Ndyetabura ambao wote wanatoka shule ya msingi Hazina.

 Mashindano hayo yaliyoshirikisha shule mbalimbali nchini yaliandaliwa na  shule ya Feza na kushirikisha shule kutoka mikoa na kuitaja baadhi ya mikoa iliyoshiriki kuwa ni Tanga, Mwanza, Dodoma, Mbeya, Mtwara, Pwani, Arusha na Zanzibar.

Mratibu wa mashindano hayo kutoka shule ya Feza, Ashrak Habibu, alisema wanafunzi hao walionyeshana umwamba kwenye masomo ya sayansi na hisabati.

Katika hafla ya kukabidhi vyeti hivyo, iliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Kimataifa ya Feza, Salasala jijini Dares Sallam, Mkurugenzi wa shule hiyo, Ibrahim Yunus alisema mashindano hayo ya kimasomo yajulikanayo kama Genius Cup, yaliandaliwa kwa pamoja na shule hizo kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Tume ya Sayansi na Teknolojia.

“Lengo letu ni kuwaandaa wanafunzi ili watakapomaliza masomo yao wawe na taaluma ya kisayansi, hasa kwa kuwa nchi inaelekea katika uchumi wa viwanda, hivyo inahitaji vijana wanasayansi na mashindano haya hufanyika kila mwaka hapa nchini,” alisema mkurugenzi huyo.

 Mbali na kupewa vyeti, wanafunzi watatu waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya Hisabati walitunukiwa kiasi cha fedha 200,000 kwa mshindi wa kwanza (150,000) mshindi wa pili na laki moja kwa mshindi wa tatu.

Akizungumzia  mafanikio ya wanafunzi hao, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,  Patrick Cheche, alisema wanafunzi wa shule hiyo wamekuwa wakifanya vyema kwenye mashindano mbalimbali kutokana na maandalizi mazuri wanayoyapata.


 “Walimu wanafanyakazi kwa moyo sana, wazazi wa wanafunzi wamekuwa wakitoa ushirikiano mzuri sana kwa shule na uongozi wa shule unawajali sana walimu, hayo kwa pamoja yamekuwa yakisaidia wanafunzi wetu kufanya vizuri kwenye mashindao mengi,” alisema Mwalimu Patrick

Viewing all 110087 articles
Browse latest View live




Latest Images