Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Yamuachia huru mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfed Lwakatare

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfed Lwakatare baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP). Kuwasilisha hati ya kuondoa shauli hilo kwa kuwa hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi yake.

Lwakatare ambaye kesi yake imedumu kwa zaidi miaka minne alikuwa akikabiliwa na tuhuma za kula njama kutenda kosa

Akiwasilisha hati hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Thomas Simba, wakili wa serikali mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi ameeleza kuwa wanaomba kesi hiyo iondolewe chini ya kifungu cha 91(1) cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai kilichofanyiwa marekebisho 2002 sababu (DPP) hana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba amesema ameifuta kesi hiyo na mshtakiwa(Lwakatare) yupo huru.Mapema, DPP aliondoa maombi yake dhidi ya Lwakatare, kuhusiana na shtaka la ugaidi katika Mahakama ya Rufaa.

Katika maombi hayo DPP aliomba kibali cha kufungua mapitio kuhusiana na uamuzi wa Mahakama Kuu kumfutia Lwakatare mashtaka ya ugaidi.

Katika kesi hiyo, Lwakatare na mwenzake Ludovick Rwezaura, walikuwa wakikabiliwa na jumla ya mashtaka manne likiwemo la kula njama za kufanya vitendo vya kigaidi kwa lengo la kumdhuru kwa sumu aliyekuwa Mhariri wa gazeti la Mwananchi, Denis Msacky.

TULIA TRADITIONAL DANCE FESTIVAL LAFANA

$
0
0
TAMASHA la ngoma za kitamaduni lililopewa jina la Tulia Traditional Dance Festival, limeanza kwa mbwembwe mjini Tukuyu, mkoani Mbeya jana, likishirikisha vikundi zaidi ya 100 kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini ambapo litafikia tamati kesho.  

Akizungumza tamasha hilo akiwa Tukuyu jana, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson ambaye ndiye mwasisi wake, alisema kuwa anajisikia furaha kuona tukio hilo limepokewa vizuri mno na wakazi wa Tukuyu na mkoani Mbeya, lakini pia na Tanzania kwa ujumla.

“Maandalizi yanaendelea vizuri na mwitikio umekuwa mkubwa mno kuonyesha jinsi Watanzania wanavyothamini tamaduni zao. Matamasha kama haya ni muhimu mno kwani hutoa fursa ya kutangaza utamaduni wetu wa kitanzania na kuwa moja ya kivutio badala ya kutegemea vivutio vya kiutalii vilivyozoeleka kama Mlima Kilimanjaro, mbuga na hifadhi za wanyama na vinginevyo.

“Nawaomba wabunge waandae matamasha kama haya katika maeneo yao ili baadaye washindi watakaopatikana, waweze kushiriki katika tamasha letu hili ili kulifanya kuwa la kitaifa zaidi, hii itasaidia kuwaonyesha vijana wetu wa kizazi cha sasa kufahamu tamaduni zao, kuona mababu zao walikuwa wakifanya nini.

“Kwa serikali, iandae na kuunga mkono matamasha ya utamaduni kama sehemu ya kuenzi utamaduni wetu kwani vijana wengi wamekuwa wakibobea katika tamaduni za kigeni kutokana na kutofahamu tamaduni zao,” alisema.
 Kikundi cha ngoma ya asili ya Sindimba toka mkoa wa Mtwara,Wakicheza ngoma hiyo jana wakati wa mashindano ya ngoma za asili yaliyodhaminiwa na Vodacom Tanzania PLC ya”Tulia Traditional dances festival 2017”yanayofanyika kwa siku tatu katika viwanja vya tandale mjini Tukuyu wilaya ya Rungwe mkoa wa Mbeya.
 Wakazi wa Tukuyu wilaya ya Rungwe mkoa wa Mbeya wakifatilia mashindano ya ngoma za asili yaliyodhaminiwa na Vodacom Tanzania PLC ya”Tulia Traditional dances festival 2017” yanayofanyika kwa siku tatu katika viwanja vya Tandale mjini humo.
 Majaji wa mashindano ya ngoma za asili yaliyodhaminiwa na Vodacom Tanzania PLC ya”Tulia Traditional dances festival 2017” wakifatilia kwa karibu mashindano hayo yanayofanyika kwa siku tatu katika viwanja vya tandale mjini tukuyu wilaya Rungwe mkoani Mbeya.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakimfanyia mahojiano Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC, Rosalynn Mworia kuhusiana na mashindano hayo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MRISHO MPOTO KUTUMBUIZA TAMASHA LA UTALII NCHINI CHINA.

$
0
0
 Msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto akiwa katika picha nchini China mara baada ya kuwasili kuiwakilisha Tanzania katika Tamasha la Utalii Duaniani. 
 Msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto amewasili nchini China leo katika eneo ambalo litakuwa likionesha utalii ikiwa ameenda huko kwaajili ya kuwakilisha nchi katika tamasha la Utalii Duniani ambalo litafanyika kuanzia Leo Septemba 21,2017.
Msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto akiwa na mwenyeji wake katika viwanja ambavyo Tamasha la Utalii linafanyika nchin China.

Msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto amewasili nchini China Jumatano hii kwaajili ya kuiwakilisha Tanzania katika Tamasha la Utalii Duaniani. 

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Kitendawili’, aliondoka nchini Tanzania siku ya Jumatatu akiwa ameambatana na kikundi chache cha ngoma kikiwa na jumla ya watu sita pamoja na yeye mwenyewe.
Akiongea na mwandishi wetu akiwa nchini humo baada ya kuwasili katika eneo ambalo litafanyika tamasha hilo, Mpoto amesema Alhamisi hii wataanza kufanya maonyesha hayo katika tamasha hilo ambalo linayakutanisha mataifa mbalimbali duniani.

“Kama nilivyowaambia watanzania wakati naondoka Tanzania, tumekuja China kwaajili ya watanzania, tumekuja kuwawakilisha wao, tunatangaza utalii wa ndani, lugha zetu za makabila zaidi ya 120, lugha yetu hadhimu ya Kiswahili, mbuga zetu za wanyama kwahiyo sisi tutawaambia Tanzania ni nchi ambayo ina kila kitu kama ukiamua kuitembelea,” alisema Mpoto.

Aliongeza,“Tumejiandaa vizuri kufanya kile kitu tulichokipanga, watanzania wananijua mimi ni mtu gani kwenye hizo anga, Kiswahili ni lugha yangu kwahiyo naweza kusema tumejipanga kuuonyesha ulimwengu tuna kitu gani ambacho tumewaletea na bila shaka kila ambaye amekuja katika eneo hili atondoka na meseji ya Tanzania ni sehemu sahihi ya kuitembelea,”

Pia amewataka watanzania kuwaunga mkono wasanii ambao wanafanya jitihada mbalimbali za kuitangaza Tanzania katika nyanja mbalimbali za utalii kwa kuwa utalii ni moja kati vyanzo vizuri vya mapato nchini.

“Uwepo wangu mimi hapa sio kwaajili ya familia yangu, hiki ninachokifanya hapa ni kwaajili ya watanzania, yule mtalii ambaye atakuja Tanzania baada ya kusikia meseji yangu ile pesa anayolipa kwaajili ya kutalii ndio ile ambayo inajenga hospitali na kununua dawa. Kwahiyo mimi ningewataka watanzania kuwa wazalendo kwenye mambo ya msingi ambayo bila shaka yanaleta tija kwaajili ya watanzania wote," alisema Mpoto.
Muimbaji huyo amesema kila mtanzania anaweza kuitangaza nchini yake kwa mazuri hivyo wamewaka watanzania kuwa wazalendo na kudumisha amani iliyopo.

KUMBUKUMBU YA MWAKA MMOJA WA KIFO CHA CASSIUS O. MDAMI

$
0
0

Tangu umetuacha tumetafakari mengi tukidhani umesafiri utarudi lakini kumbe haikuwa hivyo. Kuwa kwako mbali na familia kumetufanya kujifunza mengi kuhusu maisha na kutafakari muda ambao tulikuwa pamoja katika maisha ya hapa duniani wakati wa furaha na uchungu.

 Unakumbukwa na mke wako Rose na watoto wako Martina, Grace, Gideon, Gonsalver na Gibson. Umetimiza mwaka sasa tangu umetuacha; pengo lako ni kubwa katika kila kona ya maisha na hata katika Tasnia ya Habari uliyoitumikia katika muda mwingi wa maisha yako kwa kutuonyesha kwa vitendo maana ya kuipenda na kuithamini kazi katika maisha. 

Tumekosa simulizi za kusisimua za Utalii wa Ndani, ulichimba na kuchimbua mengi ambayo kama si kwa jitihada zako binafsi tusingeyajua kamwe… tumebaki na msemo wako maarufu “Falsafa ya Ufagio ni Unyenyekevu”. Faraja yetu ni Mungu aliye Baba wa Yatima na mume wa Wajane (Kutoka 22:22-24). Tunaamini katika Ufufuo na Uzima na siku moja tutafurahi nawe mbinguni (Yohana 11:25-26). 

Mungu akupe pumziko la Milele, upumzike kwa Amani - Amina

WAFANYAKAZI WA KUJITOLEA WA PEACE CORPS WAPATAO 57 WAAPISHWA KUHUDUMU NCHINI KWA MIAKA MIWILI

$
0
0
 Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Dk. Inmi Patterson aliwaapisha wafanyakazi wa kujitolea wa Peace Corps wapatao 57 kuhudumu nchini Tanzania katika kipindi cha miaka miwili katika hafla iliyofanyika katika ofisi za Peace Corps jijini Dar es Salaam. 

Wafanyakazi hawa wa kujitolea wa Kimarekani watakaofanya kazi katika sekta ya elimu watapangiwa kuhudumu katika wilaya za Iringa, Mufindi, Same, Kyela, Masasi, Maswa, Singida Vijijini, Lushoto, Chamwino, Hai, Rombo, Wete, Rungwe, Njombe, Iringa Vijijini, Sumbawanga, Kusini Unguja, Kaskazini Unguja, Hanang, Mbeya, Nachingwea, Hanang, Iramba, Kiomboi, Mbeya Rural, Shinyanga na Singida Mjini.
Mgeni rasmi katika hafla hii alikuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Leonard D. Akwilapo. Hafla hii ilihudhuriwa pia na wafanyakazi wa kujitolea wa Peace Corps wanaoendelea kuhudumu na wale waliohudumu hapo zamani pamoja na maafisa kutoka mashirika mengine yanayojihusisha na wafanyakazi wa kujitolea. 

Akizungumza na wafanyakazi hao wa kujitolea Kaimu Balozi Patterson alisema: "Wakati ambapo kuna uwezekano kwamba mnaweza kuwa Wamarekani wa kwanza kuishi na wafanyakazi wenzenu au majirani wa Kitanzania, ni wazi kwamba kwa Watanzania hao nyinyi mtaendelea kuwa wawakilishi wa Watu wa Marekani."

Peace Corps ni taasisi ya Serikali ya Marekani iliyoanzishwa na Rais John F. Kennedy mwaka 1961 ambayo hivi sasa inahudumia zaidi ya wafanyakazi wa kujitolea zaidi ya 7,000 katika zaidi ya nchi 70 duniani. Kwa zaidi ya miaka 50, Peace Corps imekuwa taasisi inayoendesha shughuli za mabadilishano ya kiufundi na kitamaduni zisizoegemea mrengo wowote wa kisiasa na kidini. Peace Corps ina dhamira ya kukuza amani na urafiki duniani kwa kutekeleza malengo matatu yafuatayo:

• Kutoa wafanyakazi wa kujitolea wa Kimarekani watakaochangia kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika nchi itakayohitaji wafanyakazi hao;
• Kukuza uelewa kuhusu Wamarekani miongoni mwa watu katika jamii zinazohudumiwa na Wafanyakazi wa kujitolea;
• Kuimarisha uelewa wa Wamarekani kuhusu dunia na watu wake.

Zaidi ya wafanyakazi wa kujitolewa wa Peace Corps 2,500 wamehudumu nchini Tanzania toka mwaka 1961.  Peace Corps hutoa wafanyakazi wa kujitolea wa Kimarekani wenye utaalamu katika nyanja mbalimbali ambao hupangiwa kufanyakazi katika jamii wakifundisha katika shule za sekondari (hisabati, sayansi na Kiingereza), wakitoa elimu ya afya na utunzaji wa mazingira.

UMOJA WA MASOKO MKOA WA DAR ES SALAAM WACHANGIA VYAKULA KWA AJILI YA WAFYATUAJI TOFALI

$
0
0
MUUNGANO wa Umoja wa Masoko ya Mkoa wa Dar es Salaam (MUMADA) wakiongozwa na Mwenyekiti wao Mohamed Mwekya wamekabidhi kilo za mchele 2835, Kilo 600 za Maharage pamoja Chumvi kwa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kwa lengo la kuunga mkono jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika ujenzi wa ofisi za walimu.


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mwenyekiti wa MUMADA, Mwekya amesema kuwa wao kama wafanyabishara wameguswa na harakati za RC Makonda katika kuboresha elimu hususani mazingira ya walimu, hivyo wameamua kutoa mchango wao huo ambao wana imani utasaidia.

Mwekya amesema wataendelea kushirikiana na na serikali katika shughuli mbalimbali za maendeleo na kuwataka wadau wengine wa maendeleo waunge mkono jitihada hizo zenye lengo ya kuboresha elimu kwa walimu kukaa ofisi zenye hadhi na taaluma yao.

Nae Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Mwajuma Magwiza amesema kuwa mchango huo utakwenda kwa shughuli iliyokusudiwa na wana imani kila mmoja akijitolea watatimiza lengo la kujenga ofisi 19 za walimu katika wilaya ya Kinondoni.
 Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Mwajuma Magwiza akipokea msaada vya vyakula kutoka kwa Mwenyekiti wa MUMADA, Mohamed Mwekya ikiwa kuunga mkono jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika ujenzi wa ofisi za walimu.

 Sehemu ya msaada vyakula kwa ajili ya watu wataofyatua tofali kwa ajili ya ujenzi ofisi za walimu.

.Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Mwajuma Magwiza akiwa katika ya pamoja na Muungano wa Umoja wa Masoko ya Mkoa wa Dar es Salaam (MUMADA) leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)




ZAIDI YA MILIONI 400 KUTUMIKA MRADI MKUBWA WA MAJI KUTOKA ENEO LA PONGWE JIJINI TANGA HADI WILAYANI MUHEZA

$
0
0

WANANCHI wa wilaya ya Muheza mkoani Tanga wataondokana na adha ya huduma ya maji baada ya Serikali kutenga fedha zaidi ya milioni 400 kwa ajili mradi mkubwa wa kutoa maji kutoka eneo la Pongwe Jijini Tanga hadi wilayani Muheza.

Hatua hiyo ina lenga kuondoa changamoto ya uhaba wa maji wilayani Muheza ambayo ilikuwa kikwazo cha maendeleo kwa wananchi kutokana na kutumia muda mwingi kusaka huduma hiyo badala ya kufanya shughuli za kujiingizia kipato.

Akizungumza jwakati wa kukabidhi mabomba yatakayotumika kwa mkandarasi wa mradi huo katika eneo la Pongwe Jijini Tanga, Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu alisema mradi huo utakuwa ndio mkombozi mkubwa kwa wananchi.

Alisema mradi huo ambao ni mkubwa ni moja kati ya ahadi za Rais John Magufuli alipofanya ziara mkoani Tanga ambapo alihaidi kuhakikisha wakazi wa mji huo wanaondokana na changamoto ya uhaba wa maji.

"Kwanza nimshukuru mh Rais kwa kutekeleza ahadi yake mapema jambo ambalo limetupa faraja kubwa sisi wakazi wa Muheza na vitongoji vyake lakini niwaambie katika mradi huu nitakuwa mkali sana na nitafuatilia kila mwezi kuhakikisha unajengwa kwa viwango kutokana na thamani ya fedha"Alisema.
Mhandisi wa Mradi wa Maji kutoka eneo la Pongwe Jijini Tanga hadi wilayani Muheza kutoka kampuni ya Koberg Construction Co.Limited Mhandisi Stepheni Kingili kushoto akitoa maelekezo kwa Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu namna watakavyoanza kutekeleza mradi huo kuanzia kesho(leo) wakati wa halfa ya makabidhiano ya vifaa vya mradi huo yaliyofanyika ofisi ndogo za mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) eneo la Pongwe
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa akiingia kwenye halfa hiyo
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajaabu wa pili kutoka kulia akiongozana na baadhi ya viongozi kukagua mabomba yatakayotumikaa kwenye mradi huo kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Luiza Mlelwa na kushoto ni Mhandisi wa Mradi huo ambao utatoa maji Pongwe Jijini Tanga Hadi wilayani Muheza
Moja kati ya vifaa mbalimbali vitakayotumika kwenye mradi huo.

PROF. MBARAWA AZUNGUMZA HAYA WAKATI WA UZINDUZI WA BODI YA WAKURUGENZI YA TTCL


MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA NMB

$
0
0
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha ofisini kwake Mkurugenzi Mtendaji wa NMB Bi. Ineke Bussemaker ambapo walifanya mazungumzo, Ikulu jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa NMB Bi. Ineke Bussemaker ambaye alifika Ofisini kwa Makamu wa Rais leo,Ikulu jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

ZITTO KABWE AHOJIWA NA KAMATI YA BUNGE LEO

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini Mheshimiwa Zitto Kabwe akitoa maelezo mbele ya Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge leo mjini Dodoma mbunge huyo alipoitwa kuhojiwa juu ya Shutma za kudharau Mhimili wa Bunge. (Picha Ofisi ya Bunge)
Mweyekiti wa Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge Mheshimiwa Kapteni Mstaafu George Mkuchika akiongoza Mahojiano ya Kamati hiyo leo Bungeni Mjini Dodoma ambapo Mheshimiwa Zitto kabwe aliitwa  kuhojiwa juu ya shutma za kudharau Mamlaka ya Bunge.

TACAIDS: UKIMWI BADO NI CHANGAMOTO

$
0
0
Na Fatma Salum – MAELEZO.

Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) imeendelea kuiasa jamii kuhusu kubadili tabia ili kuepuka maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwani ugonjwa huo bado ni janga kwenye nchi yetu.
Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa tume hiyo Bw.Jumanne Issango alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu mafanikio na changamoto za tume tangu ilipoanza kutekeleza majukumu yake.
“UKIMWI bado ni changamoto katika maendeleo ya Taifa letu na umeendelea kuathiri kila sekta, kila imani, matajiri na masikini nchini kote hivyo ni wajibu wa kila mmoja kujitathmini mwenendo wake na kuacha tabia hatarishi ambazo zinachangia kuongeza maambukizi ikiwemo uasherati, ngono zembe, ulevi na kadhalika,” alisema Issango.
Alieleza kuwa kwa miaka ya karibuni hali ya maambukizi ya UKIMWI imeendelea kupungua ingawa kuna tofauti kwenye mikoa, wilaya na makundi ya kijamii.Issango alibainisha kuwa kiwango cha maambukizi Tanzania Bara ni asilimia 5.3 na takwimu hizo ni kutokana na Utafiti wa Viashiria vya UKIMWI mwaka 2012.
 
Kaimu Mkrugenzi Mkuu wa TACAIDS Bw.Jumanne Issango akieleza jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa mkutano kuhusu changamoto na mafanikio katika kupambana na virusi vya ukimwi nchini kulia ni Kaimu Mkurugenzi Muitiko wa kitaifa wa TACAIDS Bi.Audrey Njelekela mkutano uliofanyika katika ukumbi wa ofisi za TACAIDS leo Jijini Dar es Salaam. (Picha na Paschal Dotto-MAELEZO) 

SHIDA YA MAJI LONGIDO KUWA HISTORIA-MAJALIWA

$
0
0

CHANGAMOTO ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama wilayani Longido mkoani Arusha kuwa historia baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya sh. bilioni 15.8. 

Waziri Mkuu ameweka jiwe hilo la msingi leo (Alhamisi, Septemba 21, 2017) kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji  wa Longido Mjini pamoja na kijiji cha Oltepesi  ambao chanzo chake ni kutoka mto Simba wilaya ya Hai mkoani Kilimanajro.
Amesema Serikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini watapata huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

Pia Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge kupeleta wataalamu wilayani Longido ambao watashirikiana na Halmashuri za wilaya ya Longido na tarafa ya  Loliondo  kutafuta vyanzo vingine vya maji ili wananchi waweze kupata maji  ya kutosha.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka  jiwe la msingi la Mradi wa maji wa Longido mkoani Arusha Septemba 21, 2017. Wapili kushoto ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji,  Mhandisi Gerson Lwenge na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo. Kulia ni Mbunge wa Hanang Dkt. Mary Nagu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia baada ya kuweka jiwe la msingi la Mradi wa maji wa Longido mkoani Arusha Septemba 21, 2017. Wapili kushoto ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji,  Mhandisi Gerson Lwenge na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo. Kulia ni Mbunge wa Hanang Dkt. Mary Nagu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi baada ya kuwasili kwenye eneo la uwekaji jiwe la Msingi la Mradi wa Maji wa Longido mkoani Arusha, Septemba 21, 2017. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa Longido kabla ya kuweka jiwe la Msingi la Mradi wa maji wa Longido Mkoani Arusha Septemba 21,  2017. 
 Baadhi ya Wananchi wa Longido wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Mjaliwa wakati alipozungumza kabla ya kuweka jiwe la Msingi la Mradi wa maji wa Longido Mkoani Arusha, Septemba 21, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WANAOPISHA MRADI MKUBWA WA UCHIMBAJI MADINI YA ‘KINYWE’ KIJIJI CHA EPANKO KUFAIDIKA KWA KUJENGEWA NYUMBA ZA KISASA ENEO MBADALA

$
0
0

Na John Nditi, Ulanga.
KAMPUNI ya TanzGraphite imesema itawajengea nyumba zenye hadhi ya juu kaya za  kijiji cha Epanko, wilayani Ulanga , mkoani Morogoro  zinazohama kwa kupisha mradi mkubwa wa uchimbaji wa madini ya Kinywe (Graphite) na itahakikisha kuwa,  maisha ya watu wanaohama yanabaki kama ilivyokuwa awali ikiwa na  kuboreshwa zaidi.

Meneja Mahusiano wa TanzGraphite, Bernard Mihayo , alisema hayo kwenye taarifa ya Kampuni hiyo  katika  kikao cha tisa cha kikosi kazi kilichokutana  Septemba 14, mwaka huu  mjini Mahenge , wilayani humo.

Kikao hicho kilichokuwa ni cha kujadili na kupokea mrejesho wa vikao vya wananchi kuhusu mpango wa uhamishaji makazi (RAP) kupisha mradi wa madini ya kinywe wa Epanko kilihudhuriwa na  wajumbe  wa vitongoji vya  Kazimoto, Epanko A, Itatira , Mbera, Epanko B na Luli .

 Wawakilishi wengine ni kutoka   ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro, Ofisi ya madini mkoa , Ofisi ya  wilaya ya Ulanga , halmashauri na wadau wengine wa mradi huo.

Madini ya Graphite ‘Kinywe’ kwa sasa yanahitajika kwa wingi duniani kutokana na matumizi ya  kutengeneza vitu mbalimbali ikiwemo betri za simu , kompyuta mpakato ‘laptop’  na penseli .
 Kiongozi wa wa kimila wa kabila la Wapogoro wa kijiji cha Epanko , wilaya ya Ulanga, mkoani Morogoro  (Mbuyi ), Redemta Masura ( wapili kushoto) akiwa na viongozi  wa Kijiji hicho wakipitia  taarifa  ya mpango wa uhamishaji makazi kupisha mradi wa madini ya Kinywe wa Epanko , wakati wa kikao cha tisa cha Kikosi Kazi iliyowashirikiasha wajumbe wa kutoka vitongozi sita wa kijiji hicho , viongozi kiserikali na kijamii kilichofanyika hivi karibuni mjini Mahenge.
 Baadhi ya viongozi wa serikali wa wilaya ya Ulanga na mkoa wa Morogoro wakiungana na vitongoji vya kijiji cha Epanko wakiwemo na wakimila na kijamii  kupitia   taarifa  ya mpango wa uhamishaji makazi kupisha mradi wa madini ya Kinywe wa Epanko katika kikao cha tisa cha Kikosi Kazi cha mpango wa uhamishaji makazi  kupisha mradi wa madini ya Kinywe wa Epanko kilichofanyika hivi karibuni mjini Mahenge.
 Baadhi ya viongozi wa kamati ya Kikosi kazi  kutoka serikali  za vitongoji vya kijiji cha Epanko wakiwemo wa kimila na kijamii  wilayani  Ulanga  wakijumuika na wa ngazi ya wilaya hiyo na mkoa wa Morogoro kupitia   kwa pamoja taarifa  ya mpango wa uhamishaji makazi kupisha mradi wa madini ya Kinywe wa Epanko  kilichofanyika hivi karibuni mjini Mahenge.
Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Lucas Mwaisaka (kulia) akimkabidhi  Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Epanko, Kata ya Nawenge, wilayani Uanga, Eliza Liwemba, ( kushoto) Mpango wa Uhamishaji Makazi (RAP) wa Mradi wa Madini wa Epanko  wakati wa kikao cha tisa cha Kikosi Kazi cha mpango huo kilichowashirikisha wajumbe wa kutoka vitongozi sita wa kijiji hicho , viongozi kiserikali  ya wilaya  na  mkoa ambacho kilifanyika hivi  karibuni mjini Mahenge. ( Picha na John Nditi).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

TaSUBa KUFANYA TAMASHA LA 36 LA KIMATAIFA BAGAMOYO

$
0
0
Na. Neema Mathias- MAELEZO

Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) imeandaa tamasha la 36 la Kimataifa kuanzia tarehe, 23 hadi 30, Septemba litakalofanyika katika viwanja vya taasisi hiyo mjini Bagamoyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo Dkt.Hebert Makoye alisema kuwa tamasha hiyo litakuwa na kauli mbiu isemayo ‘sanaa na utamaduni katika kupiga vita madawa ya kulevya’.

“Kauli mbiu hii ni mahsusi katika kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli za kupiga vita matumizi na usambazaji wa dawa za kulevya nchini” alisema Dkt. Makoye.

Aliongeza kuwa wakati wa tamasha elimu ya kudhibiti matumizi ya dawa za kulevya itatolewa ikiwalenga hasa vijana ambao ndio waathirika wakuu wa dawa hizo ambapo kutakuwa na midahalo na makongamano kuhusu athari za matumizi ya dawa hizo.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) (wa pili kushoto) akiongea na Waandishi wa habari kuhusu kufanyika kwa Tamasha la Kimataifa la 36 linalohusu Sanaa na Utamaduni Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) 21 Septemba, 2017 Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tamasha la Sanaa na Utamaduni toka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) (kushoto) akitolea ufafanuzi kwa Waandishi wa habari kuhusu kufanyika kwa Tamasha la Kimataifa la 36 linalohusu Sanaa na Utamaduni Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) 21 Septemba, 2017 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Waandishi wa habari wakichukua taarifa wakati wa Mkutano wa Waandishi wa habari uliohusu kufanyika kwa Tamasha la Kimataifa la 36 linalohusu Sanaa na Utamaduni Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) 21 Septemba, 2017 Jijini Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM


………………………………..

DOKTA MPANGO AIHIMIZA WAINGEREZA KUKUZA ZAIDI BIASHARA NA UWEKEZAJI NCHINI

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam.

Tanzania imetoa rai kwa Serikali ya Uingereza kubadili mfumo wa uhusiano wake kwa kujikita zaidi katika masuala ya biashara na uwekezaji badala ya kutoa misaada ya kawaida ili nchi iweze kukuza uchumi wake kwa haraka zaidi.

Wito huo umetolewa Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango, alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wabunge kutoka mabunge ya uingereza (Baraza la Mamwinyi na Bunge la Wawakilishi).

Dokta Mpango amesema kuwa kiwango cha mtaji ambacho Serikali ya Uingereza imewekeza nchini hadi sasa ni Paundi bilioni 2.5 lakini kwa upande wa biashara kati ya nchi hizo mbili, hali si nzuri.

"Mwaka 2015 Tanzania iliuza nje bidhaa zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 22.5 na kununua bidhaa kutoka Uingereza zenye thamani ya Dola milioni 150, kiwango ambacho ni kidogo sana na tunahitaji kufanya biashara zaidi" Alisisitiza Dkt. Mpango.

Alielezea hatua mbalimbali ambazo Serikali inazichukua kuimarisha uchumi wa viwanda na kuelezea changamoto kubwa ikiwa na namna ya kuendeleza kilimo kwa ajili ya kupata malighafi za viwanda na kuwainua wananchi kiuchumi kwa kuwa kilimo ndicho kinaajiri idadi kubwa ya Watanzania.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (wa tatu kushoto), akiongoza majadiliano na Ujumbe wa Wabunge watano pamoja na maafisa kadhaa kutoka nchini Uingereza, walipomtembela na kufanya naye mazungumzo Jijini Dar es Salaam.


 Baadhi ya wabunge wa mabunge ya Uingereza wakiwa katika kikao na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt, Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto), akisisitiza jambo alipokutana na kufanya mazungungumzo na wabunge kutoka nchini Uingereza waliomtembelea Jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Kaimu Kamishna wa Fedha za Nje, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Mamelta Mutagwaba.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), akizungumza na Wabunge kutoka Nchini Uingereza waliomtembelea katika Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na kuipongeza nchi hiyo kwa kuisadia Tanzania katika masuala mbalimbali, amesisitiza ushirikiano wa nchi hizo mbili ujikite zaidi katika masuala ya biashara na uwekezaji.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa pili kushoto) na Kiongozi wa Ujumbe wa Wabunge kutoka Uingereza, Mhe. David Linden (katikati) na Wabunge wengine kutoka Uingereza, Maafisa Waandamizi kutoka Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa Mkutano katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Prof, Mbarawa Aitaka Bodi Mpya ya TTCL Kujipanga

$
0
0

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Mkame Mbarawa ameitaka Bodi Mpya ya Wakurugenzi ya kampuni ya mawasiliano nchini (TTCL) kuhakikisha kuwa inasimamia vyema kazi na majukumu yake ili kuiwezesha kampuni hiyo kujiendesha kibiashara na kuimarisha huduma za mawasiliano hapa nchini.

Wito huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo ambapo aliwasisistiza kuwa wachape kazi ili kurahisisha huduma mbalimbali za kimawasiliano hapa nchini na kuhakikisha kuwa wanaendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano yenye sera ya hapa kazi tu.

“Nataka bodi mjue tunakwenda wapi katika kampuni hii lakini pia tunahitaji kufanya kazi kwa juhudi, kushindana na makampuni mengine ya simu, mhakikishe mapato makubwa yanatoka kwenye data halikadhalika tujue mnapaswa mjue strenght (nguvu) yenu iko wapi maana tusipojibu maswali haya hatuwezi kufanya ushindani na makampuni mengine,” alifafanua Prof. Mbarawa.

Aidha Prof. Mbarawa alisema kuwa, Serikali imeweka sera nzuri za uwekezaji katika sekta ya mawasiliano kiasi ambacho kimeongeza mapato pamoja na ushindani wa huduma ya mawasiliano na kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi na maendeleo hapa nchini.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo mbele ya wajumbe wa Bodi ya Kampuni ya Simu ya TTCL katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Bodi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano) Dkt. Maria Sasabo na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Mhandisi Omary Nundu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Simu za Mkononi ya TTCL Mhandisi, Omary Nundu akielezea jambo wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Bodi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Mawasiliano) Dkt. Maria Sasabo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya mawasiliano) Dkt. Maria Sasabo akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Bodi ya Kampuni ya Simu ya Mkononi ya TTCL leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa TTCL, Bw. Waziri Kindamba, Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL Mhandisi Omary Nundu na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa.
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya TTCL wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Bodi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.Picha na Frank Shija – MAELEZO



Three schools in Mwanza benefit from the Tigo E-schools Project

$
0
0
Mwanza 21st September,  2017- Leading digital lifestyle company, Tigo Tanzania has today provided digital education content to three (3) secondary schools in Mwanza as part of its Tigo e-schools program and the Tigo Fiesta 2017 – Tumekusomaa cultural festivities.
   
As part of its Tumekusoma (‘we understand you’) initiative, which underscores Tigo’s dynamic reputation as the telecom brand that best understands and responds to the needs of its customers, Tigo will be providing the digital education content to 52 secondary schools located in 12 of the 15 regions where the Tigo Fiesta 2017 –Tumekusomaa festival will take place.

Speaking during the handover event at Mwanza Secondary School, Tigo Zonal Director for Lake Zone, Ali Maswanya said that the digital drive would enhance the learning experience of students and prepare them to be part of the global digital village. 
‘We are living in a digital world and Tigo e-schools project is equipping students to be part of the digital world,’ Maswanya said, revealing that the other secondary schools in Mwanza that have benefitted from the Tigo E-schools project are Pamba Secondary School and Mirongo Secondary School. 

In 2016, Tigo entered into a partnership with the Ministry of Communications, Works and Infrastructure to facilitate the roll-out of internet access points in the country’s secondary schools to complement the Government’s eSchools project for a period of 2 years.

As part of the agreement, the Ministry identified and provided a list of schools without computer labs to be connected and also guided the implementation of the project. Tigo sponsored the infrastructural development in the schools across the country, including wiring classrooms and installation of wireless LAN with internet access points. The third phase of this project is the current installation of learning materials that students can access directly from the computer labs, thus digitizing their learning experience.

“Through our corporate responsibility initiative, we are now implementing the Government’s vision to transform the country into a knowledge-based economy by the year 2025.  Our company is committed to ensure that most of the secondary schools have access to the internet in Tanzania, and also to learning materials so that they can be amply prepared for opportunities that come with the digital transformation that is currently sweeping the globe”, Tigo’s Lake Zone Director said.

Theschools that will benefit from the project are Arusha Day, Ilbouru and Arusha Secondary Schools in Arusha region; Mwanza, Pamba and Mirongo Secondary Schools in Mwanza region; Tabora Girls and Milambo Secondary Schools in Tabora; and Mpwapwa Secondary School in Dodoma.

Others are Iringa and Kleruu Secondary School in Iringa region; Matalawe and Songea Girls Secondary Schoosl in Songea Region; Njombe and Mpechi Secondary School in Njombe region; Morogoro Municipal and Mzumbe Secondary Schools in Morogoro; and Handeni and Shemsanga Secondary Schools in Tanga.
Other schools to benefit from the digital education tools provided through Tigo e-Schools’ project are,  Lyamungo Secondary School and Machame Girls Secondary School in Moshi; Newala Day Secondary School and Masasi Day Secondary School in Mtwara while in Dar es  Salaam the schools to benefit include  Mbagala, Kibamba, Benjamin Mkapa and Makumbusho Secondary Schools.  

‘Tigo is proud to be partnering with the Ministry of Communications, Works and Infrastructure and the schools to enable the youth and the wider communities to tap into the global mainstream of information and knowledge, where they will learn, expand their creativity and collaborate with peers across the world,’ Maswanya noted.

The e-Shools project is one of Tigo’s strategic social investment projects and to date Tigo has connected over 52 public secondary schools with internet and provided 77 computers to secondary and higher learning institutions across the country.

MZIGO WA RWANDA WAONGEZEKA BANDARINI

$
0
0
Shehena ya Rwanda kupitia bandari ya Dar es Salaam katika kipindi cha miaka mitano imekuwa ikiongezeka kwa wastani wa asilimia 9.9 kwa mwaka kutoka tani 630,000 mwaka 2012/2013 mpaka tani 950,000 mwaka 2016/2017.

Haya yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Mhandisi Deusdedit Kakoko alipokutana na balozi wa Rwanda nchini Tanzania Mhe. Eugene Kayihura aliyetembelea TPA leo.

Kakoko amesema kwamba kwa sasa shehena yote ya mizigo inayokwenda na kutoka Rwanda na nchi zingine za jirani inahudumiwa ndani ya bandari ili kurahisisha uondoshaji na usalama wa mizigo hiyo.

Mkurugenzi Mkuu amesema katika mkakati wake wa kuimarisha uhusiano zaidi na wateja, Serikali kupitia TPA imetenga eneo kwa ajili ya kuhifadhia mzigo wa Rwanda katika bandari Kavu ya Kwala, Ruvu na kuwataka wafanyabiashara wa nchini Rwanda kuitumia bandari Kavu ya Isaka kwa ajili ya mizigo yao ili kuwapunguzia safari ya kusafiri hadi Dar es Salaam.

TPA tayari imeshakamilisha ujenzi wa ofisi yake nchini Rwanda kwa ajili ya kuhudumia wateja wake toka nchini humo. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu, ofisi hiyo ya TPA nchini Rwanda imekamilika na kinachosubiriwa ni ufunguzi baada ya kukamilisha taratibu zote ili ianze kazi rasmi.

“Ufunguzi wa ofisi hiyo utasaidia sana kuimarisha huduma kwa wateja wetu wa Rwanda ambao wanatumia Bandari ya Dar es Salaam,” amesema Kakoko. Naye Balozi wa Rwanda nchini, Mhe. Eugene Kayihura ameishukuru TPA na Serikali ya Tanzania kwa kuwapatia eneo la kuhifadhia mizigo iendayo Rwanda.

Balozi Kayihura amesema kwamba biashara kati ya Tanzania na Rwanda imekuwa ikiongezeka kwa kasi katika siku za hivi karibuni mara baada ya TPA kuimarisha huduma zake. “Kwa sasa Bandari ya Dar es Salaam imekuwa ikihudumia asimilia 90 ya mizigo yote inayoingia na kutoka Rwanda hivyo kuweka rekodi ya ukuaji wa haraka sana wa mizigo ya Rwanda inayohudumiwa nchini,” amesema Mhe. Balozi Kayihura.

Amesema kwamba ziara yake aliyoifanya bandarini ni sehemu ya juhudi za Rwanda kuimarisha uhusiano wa kibiashara na Tanzania haswa kwa kupitia huduma bora zitolewazo na Bandari ya Dar es Salaam kwa sasa.

Katika mkakati wake wa kuhakikisha inakuwa karibu na wateja wake, TPA hivi karibuni ilishiriki katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa nchini Rwanda ambapo pamoja na mambo mengine ilikutana na wafanyabiashara wa nchi hiyo ambao walionesha kuridhishwa na huduma za bandari ya Dar es Salaam.

BBC DIRA YA DUNIA ALHAMISI SEPTEMBA 21, 2017

SEKRETARIETI YA CCM CHINI YA KINANA YAFANYA MAZUNGUMZO NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA VIETNAM MJINI DODOMA

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM abdulrahman Kinana akisalimiana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Chau Van Lam alipowasili kwa ajili ya mazungumzo na Sekretarieti ya CCM chini ya Kinana, jana katika ukumbi wa Kamati Kuu ya CCM, ndani ya Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete nje kidogo ya mji wa Dodoma. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM-zanzibar Jumanne Mabodi. Katikati ni katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga.
Kiongozi huyo akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Jumanne Mabodi
Kiongozi huyo akiendelea kusalimia viongzi wa CCM
Mazungumzo yakianza
Mazungumzo yakiendelea
Mazungumzo yakiendelea

Viewing all 110000 articles
Browse latest View live




Latest Images