Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109922 articles
Browse latest View live

BancABC yazindua akaunti mpya ya Hundi ya Jiongeze .

$
0
0

Lengo ni kufikia Watanzania wengi na waweze kuwa na kaunti za hundi kwa bei nafuu.
Dar es Salaam Tanzania, BancABC imeendelea kuwa Benki inayojiogeza hapa nchini kwa kua wabunifu wa hali ya juu kwenye utoaji huduma zao pamoja na kuboresha huduma hizo za kibenki ili kuwawezesha wateja kupata huduma za kwa urahisi na hivyo kuwa suluhisho kwenye sekta ya fedha.

Katika kuendelea kudhihirisha ubunifu wa bidhaa zao, BancABC leo imezindua akaunti mpya inayoitwa Jiongeze Hundi akaunti kwa lengo la kupunguza makato ya huduma za uendeshaji akaunti ya mwezi kwa mwezi kwa wateja wote watakaofungua Akaunti ya Jiongeze na Benki hiyo hapa nchini.

Akaunti ya Jiongeze inamfanya mteja aweze kuendesha akaunti ya kibiashara au ya mshahara mara nyingi bila makato ya mwisho wa mwezi kwa muda wa mwaka mmoja na hivyo kufanya wateja wa BancABC kuweza kufanya miamala mingi ya kibenki kwa Uhuru na urahisi zaidi.
 Meneja wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa BancABC,Joyce Malai (kulia) akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa akaunti mpya ya Hundi ya Jiongeze isiyo na makato yeyote ya mwisho wa mwezi. Kushoto ni Meneja Masoko wa benki hiyo Upendo Nkini.

Meneja wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa BancABC,Joyce Malai (kulia) na  Meneja Masoko wa benki hiyo, Upendo Nkini, wakionyesha bango la   uzinduzi wa akauti mpya ya Hundi ya Jiongeze isiyo na makato ya mwisho wa mwezi wakati wa hafla ya kuzindua akaunti hiyo jijini Dar es Salaam jana.


TCRA YAWAASA WAMILIKI WA MITANDAO YA KIJAMII KUCHUJA HABARI ZAO KWA WEREDI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Wamiliki wa mitandao ya kijamii wameaswa kuchuja habari zao ambazo wamekuwa wakizipata na kuzisambaza kwa jamii kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa Redio ama televisheni za Mitandaoni.

Hayo ameyasema leo Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui , Valerie Msoka wakati alipokutana wamiliki wa mitandao ya Kijamii pamoja na waandishi wa habari, Valerie amesema kuwa upashanaji wa habari lazima kuangalia na usalama wa nchi pamoja kuacha uchochezi ambao unachonganisha na jamii au mamlaka.

Amesema kuwa takribani miaka mitano kulikuwa hakuna fursa za kupata matangazo ya televisheni kupitia mitandao ya kijamii, lakini sasa imeenea kwa watanzania wengi na inaendelea kuongezeka kadri ya teknolojia inavyokuwa, hivyo kunahitajika kuwepo umuhimu wa kusimamia huduma ya mitandao hiyo ili iweze kuleta tija kwenye taifa na si vinginevyo.

Valerie amesema kuwa TCRA kupitia kamati ya maudhui inatambua na kuthamini kuwepo kwa fursa ya upashanaji wa habari na serikali iliamua kuruhusu huduma hiyo wakati miongozo na taratibu stahiki zikiendelea kutayarishwa.
 
Amesema vyombo vya habari katika mitandao ya kijamii vya Radio, Televisheni na bado teknolojia inaendelea kukua na haviwezi kuzuia kutokana na mfumo wa upashanaji wa habari. Mwenyekiti huyo anasema habari zingine hazina tija kwa jamii na zingine zinaleta uchochezi ndani ya jamii na wakati mwingine kuingilia faragha za watu ambazo ambazo hazitakiwa kufikia jamii kama sehemu ya habari.

Amesema wadau wa mitandao ya kijami na watumiaji wa mitandao hiyo wanahakikisha wanahabarisha kwa kuzingatia habari zizojenga umoja wa kitaifa, mshikamano na ushirikiano baina ya watanzania bila kujenga hofu , kuchochea chuki na uhasama baina ya watanzania. Aidha amesema habari za matusi katika mitandao ya kijamii hayavumiliki ,kwani zinakiuka misingi ya uandishi na uhuru na wajibu wake.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui wa TCRA, Valerie Msoka akizungumza na wadau wa mitandao ya kijamii juu uchujaji wa habari ambazo zinatakiwa  kuwafikia jamii na zinazolenga uimarishaji wa usalama wa nchi na mshikamano watanzania, leo jijini Dar es Salaam.Picha na Michuzi Jr-Michuzi Media Group.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui wa TCRA, Valerie Msoka (katikati) akipitia taarifa wakati wa mkutano wa wadau wa mitandao ya kijamii ambao wanasambaza taarifa leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Maudhui, Abdul Ngalawa na Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka.
Kaimu Mkurugenzi wa Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka akizungumza katika mkutano wa wadau wa mitandao ya kijamii ambao wasambazaji wa taarifa kwa jamii leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya waandishi wa habari na wamiliki wa mitandao ya Kijamii wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam.


Mmoja wa wamiliki wa Mitandoa ya Kijamii, kutoka Jamii Media Maxence  Mello akichangia jambo katika suala zima la uchujaji wa Habari katika mitandano ya Kijamii, katika mkutano uliowahusu Wamiliki wa radio, Televisheni za mtandaoni na mitandano mingine ya kijamii uliondaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),mapema leo jijini Dar
Mmoja wa wamiliki wa Mitandao ya Kijamii,kutoka Mtembezi Media,Antonio Nugaz akichangia jambo katika suala zima la uchujaji wa Habari katika mitandano ya Kijamii,ndani ya mkutano uliowahusu Wamiliki wa radio,Televisheni za mtandaoni na mitandano mingine ya kijamii uliondaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),mapema leo jijini  Dar

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UZINDUZI WA AWAMU YA PILI YA MRADI WA KULIJENGEA UWEZO BUNGE

Msisubiri Muda wa Kuchukua Leseni Kuisha - Dkt. Abbasi

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akielezea jambo wakati wa zoezi la kukabidhi Leseni za machapisho kwa Kampuni ya The Guardian Ltd leo Jijini Dar es Salaam ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa matakwa ya sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 kifungu kidogo namba 5(e). Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi anayeshugulikia Usajili Patrick Kipangula na kulia ni Mhariri Mkuu wa The Guardian Ltd Jesse Kwayu. Kampuni hiyo inamiliki magazeti ya Nipashe, Nipashe Jumapili, Sema Usikike,The Guardian, The Guardian On Sunday, Kulikoni, Lete Raha, This Day, Alasiri na Taifa Letu.
  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi Leseni za machapisho Mhariri Mkuu wa Kampuni ya The Guardian Ltd Jesse Kwayu (kulia) ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 kifungu kidogo namba 5(e).Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi anayeshugulikia Usajili Patrick Kipangula. Kampuni hiyo inamiliki magazeti ya Nipashe, Nipashe Jumapili, Sema Usikike,The Guardian, The Guardian On Sunday, Kulikoni, Lete Raha, This Day, Alasiri na Taifa Letu.
  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi Leseni za machapisho Meneja wa Sheria na Uhusiano  wa Kampuni ya The Guardian Ltd Bw. Emmanuel Matondo(kulia) ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 kifungu kidogo namba 5(e). Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi anayeshugulikia Usajili Patrick Kipangula. Kampuni hiyo inamiliki magazeti ya Nipashe, Nipashe Jumapili, Sema Usikike,The Guardian, The Guardian On Sunday, Kulikoni, Lete Raha, This Day, Alasiri na Taifa Letu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Serikali yaanza Kujenga Mitambo ya FM Kuimarisha Usikivu Redio ya Taifa

$
0
0
Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma

Serikali imeanza kutekeleza Mpango wa kujenga mitambo ya FM nchini kuimarisha usikivu maeneo mbalimbali ili wananchi waweze kupata matangazo kutoka redio yao ya Taifa (TBC).

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kyerwa Innocent Sebba Bilakwate kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, lililohoji ni lini Serikali itawapatia Wananchi wa Kyerwa haki yao ya kusikiliza Redio TBC ili kujua yanayoendelea katika nchi yao kama ilivyokuwa hapo awali kabla ya kubadilisha teknolojia ya habari badala ya sasa kusikiliza Redio Rwanda na Uganda.

Mpango huo unatekelezwa na Serikali kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ambao umeanza kutekelezwa katika wilaya za Kibondo, Nyasa, Longido, Tarime pamoja na Rombo na utaendelea katika wilaya nyingine ikiwemo Kyerwa kadiri bajeti inavyoendelea kuimarika.

“Kwa sasa kama ilivyobainishwa katika Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya mwaka 2017/2018, Serikali inaendelea kubadilisha mfumo wa urushaji matangazo kupitia satelaiti uweze kuwa wa kisasa ili kuboresha usikivu wa radio ya Taifa TBC hatua itakayosaidia wananchi kuendelea kupata habari kupitia viongozi wao” amesema Naibu Waziri Wambura.

Naibu Waziri Wambura amebainisha kuwa zipo wilaya 84 nchini ambazo usikivu wa TBC umeshuka na kusababisha baadhi ya maeneo kukosa matangazo ya redio kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa baadhi ya miundombinu ya radio, uwepo wa milima na uharibifu wa vifaa kutokana na radi wakati wa mvua.

Aidha, Naibu Waziri Wambura amewataka Wabunge na wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kutoa taarifa endapo kutatokea uharibifu wa vifaa vya kusaidia upatikanaji na usikivu wa matangazo ya radio ya taifa TBC katika maeneo yao ili yaweze kufanyiwa marekebisho mapema na wananchi waendelee kupata habari mbalimbali za Kitaifa na Kimataifa.
Wilaya ya Kyerwa iko katika Mkoa wa Kagera ambapo matangazo ya Redio yanapatikana kupitia mtambo wa TBC ulioko katika Manispaa ya Bukoba ambao unasafirisha mawimbi ya Redio katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo. 

KLM Customers worldwide receive flight information through WhatsApp

$
0
0
KLM Royal Dutch Airlines and WhatsApp have started a unique test for a new service by offering customers with booking confirmation, check-in notification, boarding pass, flight status updates all around the world. They have joined forces as ways of creating value for customers and businesses with hassle free service ready-to-hand in the next few days. 

The WhatsApp official business application account will allow customers to ask questions in ten different languages. KLM is one of the very first airline companies worldwide to come up with a verified WhatsApp account. 

“KLM is proud to be the world’s first airline with a verified WhatsApp account. This unique partnership underlines our position as an aviation pioneer. We want to make it possible for KLM to connect with customers in a fast and personal way on WhatsApp” says KLM President & CEO Pieter Elbers.

Mr Pieter Elbers adds “We offer to our customers worldwide as a reliable way to receive their flight information and ask questions 24/7 (24 hours a day, seven days a week). This truly is a major next step in our social media strategy.”

KLM flight information is easy to find through the verified App, it gives easy access to information, making it available at the airport, en route or at home. Customers can contact KLM’s social media service agents directly. The service is available to customers who book tickets or check in via KLM.com and opt-in to receive information via WhatsApp.  

Messages are secure and can only be read by the customer and KLM. Customers can easily recognise and verify their information by using the official WhatsApp business application. This means that customers will see a green checkmark badge next to the KLM contact name on WhatsApp. 

KLM has gained a reputation as a pioneer in the field of social media services and campaigns since 2009. The airline has over 25 million fans and followers on various social media platforms. Through these channels, KLM receives over 100,000 mentions every week, and 15,000 can be questions or remarks.

The questions and remarks are personally answered by more than 250 service agents, who form the world’s largest, dedicated social media team. Apart from WhatsApp, the airline has also been using other social media, including Facebook, Messenger, Twitter, LinkedIn, WeChat and KakaoTalk (Korean). 

KLM offers a one-stop-shop in nine languages in Dutch, English, German, Spanish, Portuguese, French, Chinese, Japanese, Korean and Italian. KLM was the world’s first airline to offer customers the option of receiving flight documents and status updates via Messenger, Twitter and WeChat. 

SPIKA JOB NDUGAI ATEMBELEWA NA BALOZI WA UINGEREZA NCHINI LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA

$
0
0
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akisalimiana na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (kushoto) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. katikati ni Mwakilishi Mkazi wa DFID hapa nchini, Ndg. Beth Arthy.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (katikati) na Mwakilishi Mkazi wa DFID hapa nchini, Ndg. Beth Arthy,  pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akimsikiliza Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (katikati) na kulia ni  Mwakilishi Mkazi wa DFID hapa nchini, Ndg. Beth Arthy,  pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akiagana na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (kushoto) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. katikati ni Mwakilishi Mkazi wa DFID hapa nchini, Ndg. Beth Arthy
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati)akiwa katika picha ya pamoja na ugeni kutoka ubalozi wa Uingereza uliomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. ulioongozwa na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (watatu kulia).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

TRA YAONGEZA UFANISI WA UKUSANYAJI KODI YA MAJENGO

$
0
0
Serikali imeeleza kuwa katika mwaka wa fedha 2016/17 Mamlaka ya Mapato Nchini, (TRA) imekusanya Kodi ya Majengo kwa ufanisi zaidi ikilinganishwa na kipindi ambacho kodi hiyo ilikuwa ikikusanywa na Halmashauri. 

Hayo yameelezwa Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri waFedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Cecilia Paresso(CHADEMA), aliyetaka kujua baada ya TRA kupewa jukumu la kukusanya kodi za majengo basala ya Halshauri za Miji, Manispaa na Majiji, ufanisi wake umefikiwa kiasi gani ikilinganishwa na mapato yaliyokuwa yakikusanywa na Halmashauri zenyewe. 

Katika swali hilo Mhe. Paresso alisema kuwa kodi hiyo ilikuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa mapato ya Halmashauri hizo yaliyokuwa yakitumika katika kutekeleza majukumu ya kutoa huduma kwa wananchi. 

“Baada ya TRA kupewa jukumu la kukusanya kodi ya majengo majukumu ya Halmashauri hizo hayajapungua, je Serikali imejipanga vipi kufidia vyanzo hivyo?,” alihoji.Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alisema ufanisi wa TRA katika kukusanya kodi ya majengo umeongezeka kwa asilimia 20.6 kutoka Sh. bilioni 28.28 mwaka 2015/16 hadi Sh. Bil 34.09 mwaka 2016/17.

Dkt. Kijaji alifafanua kuwa Serikali inatambua kuwa kodi ya majengo imekua ikichangia kwa kiasi kikubwa mapato ya Halmashauri husika katika kutekeleza mipango ya utoaji huduma za jamii na imeweka utaratibu wa kibajeti ambao unaziwezesha Halmashauri hizo kupata fedha za makusanyo ya kodi ya majengi iliyokusanywa na TRA ili kuziwezesha kutimiza majukumu yao.

“Utaratibu uliopo ni kwamba, Halmashauri zinatakiwa kuomba fedha hizo kutoka Serikali Kuu kwa kuzingatia makisio ya bajeti zao, kwa mantiki hiyo Halmashauri zinashauriwa kuzingatia utaratibu huo ili ziweze kupata fedha hizo,”alisema Dkt. Kijaji.

Alisisitiza kuwa hatua ya Serikali kuhamisha jukumu hilo la kukusanya kodi TRA halikulenga kuzinyang’anya Halmashauri vyanzo vya mapato bali ni kuimarisha ukusanyaji wake kwani takwimu zilizoainishwa hapo juu zinadhihirisha kuwa TRA imefanya vyema katika kukusanya mapato hayo ikilinganishwa na Halmashauri.

Imetolewa na: 
Benny Mwaipaja
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango

Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika

$
0
0
Tanzania imekuwa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Masuala ya Kisera ya Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (African Minerals and Geosciences Center (AMGC) ambao unafanyika jijin Dar es Salaam. 

Awali, mkutano huo ulianza kwa kuwakutanisha Wakurugenzi wa Bodi ya kituo hicho na kufuatiwa na mkutano wa tarehe 13 Agosti, 2017, uliowashirikisha Makatibu Wakuu kutoka nchi Wanachama wa kituo husika.

Akizungumza na Vyombo vya Habari wakati wa Mkutano wa Makatibu Wakuu, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe alisema lengo la kukutana ni kufanya tathmini na kuendeleza yale yaliyopangwa kutekelezwa na nchi wanachama ikiwemo kupanga mipango ya mwaka ujao na bajeti ya utekelezaji wa mipango hiyo.

Profesa Mdoe alisema kuwa yapo mambo ambayo waliyokubaliana katika mkutano wa 36 yakiwemo ujenzi ya Maabara ya kisasa kwa ajili ya nchi za Maziwa Makuu ambayo itasaidia katika shughuli za madini ikiwemo za uchunguzi wa madini, kukiwezesha kituo hicho kufanya shughuli zake vizuri na kusaidia nchi wanachama katika sekta husika.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja ya Mkutano wa MakatibU Wakuu kutoka Nchi Wanachama wa Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC). Wengine katika picha ni wawakilishi kutoka Nchi wanachama pamoja Makamishna na Wakuu wa Vituo vya Madini. 
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (katikati) baada ya kufugua kikao cha Makatibu Wakuu kutoka Nchi Wanachama wakiwa katika Kituo cha Afrika Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC). Wengine ni Kamishna wa Madini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (kushoto) na Assa Mwakilembe (kulia).
Baadhi ya wawakilishi wa Bodi ya Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC), wa kwanza kutoka kulia ni Mwenyekiti wa UNECA, Dkt. Koja Busia, Mwenyekiti wa Bodi, Masresha Gebreselassie, Mwenyekiti wa AUC, Frank Mugyenyi na Mkurugenzi Mkuu wa AMGC, Ibrahim Shaddad.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (anayeongea). Wengine ni washiriki katika kikao hicho.

Serikali Imeanza Kujenga Mitambo ya FM Kuimarisha Usikivu Redio ya Taifa

$
0
0

Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma

Serikali imeanza kutekeleza Mpango wa kujenga mitambo ya FM nchini kuimarisha usikivu maeneo mbalimbali ili wananchi waweze kupata matangazo kutoka redio yao ya Taifa (TBC).

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kyerwa Innocent Sebba Bilakwate kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, lililohoji ni lini Serikali itawapatia Wananchi wa Kyerwa haki yao ya kusikiliza Redio TBC ili kujua yanayoendelea katika nchi yao kama ilivyokuwa hapo awali kabla ya kubadilisha teknolojia ya habari badala ya sasa kusikiliza Redio Rwanda na Uganda.

Mpango huo unatekelezwa na Serikali kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ambao umeanza kutekelezwa katika wilaya za Kibondo, Nyasa, Longido, Tarime pamoja na Rombo na utaendelea katika wilaya nyingine ikiwemo Kyerwa kadiri bajeti inavyoendelea kuimarika.

“Kwa sasa kama ilivyobainishwa katika Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya mwaka 2017/2018, Serikali inaendelea kubadilisha mfumo wa urushaji matangazo kupitia satelaiti uweze kuwa wa kisasa ili kuboresha usikivu wa radio ya Taifa TBC hatua itakayosaidia wananchi kuendelea kupata habari kupitia viongozi wao” amesema Naibu Waziri Wambura.

Naibu Waziri Wambura amebainisha kuwa zipo wilaya 84 nchini ambazo usikivu wa TBC umeshuka na kusababisha baadhi ya maeneo kukosa matangazo ya redio kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa baadhi ya miundombinu ya radio, uwepo wa milima na uharibifu wa vifaa kutokana na radi wakati wa mvua.

Aidha, Naibu Waziri Wambura amewataka Wabunge na wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kutoa taarifa endapo kutatokea uharibifu wa vifaa vya kusaidia upatikanaji na usikivu wa matangazo ya radio ya taifa TBC katika maeneo yao ili yaweze kufanyiwa marekebisho mapema na wananchi waendelee kupata habari mbalimbali za Kitaifa na Kimataifa.

Wilaya ya Kyerwa iko katika Mkoa wa Kagera ambapo matangazo ya Redio yanapatikana kupitia mtambo wa TBC ulioko katika Manispaa ya Bukoba ambao unasafirisha mawimbi ya Redio katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akijibu swali la Mbunge wa Kyerwa Innocent Sebba Bilakwate leo Bugeni Mjini Dodoma lililohoji ni lini Serikali itawapatia Wananchi wa Kyerwa haki yao ya kusikiliza Redio TBC ili kujua yanayoendelea katika nchi yao kama ilivyokuwa hapo awali kabla ya kubadilisha teknolojia ya habari badala ya sasa kusikiliza Redio Rwanda na Uganda.Picha na Frank Mvungi, MAELEZO, Dodoma.

TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA -WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ipo salama na imara na kwamba mtu yeyote atakayejaribu kutaka kuvuruga amani atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Septemba 13, 2017) alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Bw. Mousa Farhang jijini Dar es Salaam.

“Hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote kutoka popote atakayejaribu kuvuruga amani yetu. Nawaomba wananchi muwe makini na muendelee kuidumisha amani yetu.”Amesema kwa sasa Serikali ipo katika mapambano dhidi ya vitendo vya ufisadi, rushwa, biashara haramu ya dawa za kulevya pamoja na wahujumu uchumi.

Waziri Mkuu amesema licha ya Tanzania kuwa ni nchi ya amani na yenye utulivu wa kisiasa, wameendelea kuwahamasisha wananchi wake kudumisha mshikamano.Amesema mbali ya kuimarisha amani nchini, pia Serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji jambo ambalo litawawezesha watakaokuja kuwekeza nchini kupata tija.

Hivyo ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchini Iran ili waje kuwekeza kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya kuchakata mazao ya kilimo.Pia amewakaribisha raia wa Iran kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko nchini Tanzania kama mlima wa Kilimanjaro, fukwe, mali kale na mbuga za wanyama.

Kwa upande wake, Balozi Farhang ameipongeza Serikali kwa kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi na kupambana na dawa za kulevya na ufisadi.Balozi huyo amesema Serikali ya Irani ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi pamoja na vitendo vingine vya kihalifu.

Balozi Farhang ametumia fursa hiyo kuiomba Serikali ya Tanzania ifungue Ofisi ya Ubalozi nchini Iran ili kuimarisha uhusiano huo, ambapo Waziri Mkuu amekubali.Pia Bw. Farhang amesema aliwahi kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti na Ngorongoro na kusema kwamba ni maeneo mazuri ambayo hajawahi kuyaona tangu azaliwe.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMATANO, SEPTEMBA 13, 2017.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na Balozi wa Iran. Mousa Farhang nakufanya mazungumzo ya kikazi leo Septemba 13/2017.Ofisini kwake Magogoni Dar es salaam. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

NEWS ALERT: MWANZILISHI WA DOGODOGO CENTRE NA NYUMBA YA SANAA MAREHEMU SISTER JEAN PRUITT KUZIKWA JUMATANO IJAYO JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Mazishi ya mwanzilishi wa Kituo cha Kulelea watoto wa mitaani cha Dogodogo Centre na Kituo cha Sanaa na Utamaduni cha Nyumba ya Sanaa Marehemu Sister Jean Pruitt aliyefariki Septemba 10, 2017 huko Karatu mkoani Arusha yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatano ijayo jijini Dar es salaam. 
Kwa mujibu mmoja wa vijana waliolelewa naye, Ndugu Amos, mwili wa Sister Jean unatarajiwa kuwasili jijini Dar es salaam siku ya Jumanne ama Jumatano hiyo hiyo wiki ijayo. Taarifa za taratibu na ratiba kamili zitatolewa mara baada ya maandalizi kukamilika. 
Sister Jean Pruitt aliletwa Tanzania mwaka 1969 na na taasisi ya kidini ya Marekani ya Maryknoll Sisters kufanya kazi na Kanisa Katoliki, akianza kushughulika na taasisi ya Misaada ya Catholic Relief Services, akishughulika zaidi na maendeleo ya afya ya vijana na watoto wa Tanzania. 
 Toka awasili nchini miaka hiyo, alianzisha taasisi nyingi zilizosaidia sana wasanii, walemavu na watoto na vijana walio katika mazingira magumu. 
Mwaka 1972 alianzisha kituo cha utamaduni cha Nyumba ya Sanaa jijini Dar es salaam ambacho kikaja kuwa mojawapo ya taasisi mashuhuri alizoanzisha na zilizofanikiwa sana. 
 Uwanja ilipojengwa Nyumba ya Sanaa hivi sasa ni makao makuu ya benki ya NMB, ambao kwa kutambua umuhimu wake, wametenga sehemu moja kwa ajili ya Nyumba ya Sanaa. Lakini sio kubwa kama ilivyokuwa yenyewe kabla ya kuvunjwa, jambo ambalo Sister Jean alililalamikia sana sana, hasa ikizingatiwa yeye binafsi aliomba eneo hilo toka kwa Rais wa wakati huo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, na alipolipata lilisaidia sana kukuza sanaa ua utamaduni wa Mtanzania. 
 Mwaka huo huo wa 1972 alianzisha tawi la Caritas, na mwaka 1988 alikuwa mwanzilishi mwenza wa chama cha Urafiki wa Tanzania na Msumbiji (TAMOFA). 
 Mwaka 1992 Sister Jean alianzisha kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Dogodogo Centre kukabiliana na ongezeko la watoto hao jijini Dar es salaam. Alifanikiwa sana na watoto na vijana na watoto wengi waliolelewa hapo hivi sasa ni watu wazima wakifanya shughuli zao. 
 "Ni majonzi makubwa sana kwangu na jamii ya Tanzania kwa ujumla wake maana mchango wake ni mkubwa mno kwa familia nyingi hapa nchini" anasema Amos ambaye alilelewa hapo Dogodogo Centre toka mwaka 2002 hadi mwaka 2009. Hivi sasa yeye ni producer mashuhuri wa vipindi vya TV.
Marehemu Siter Jean Pruitt
17 October 1939–10 September 2017

Kusoma habari zake zaidi BOFYA HAPA

TANZANITE WAKABIDHIWA BENDERA YA TAIFA,TAYARI KUWAKABILI NIGERIA SEPT 17

$
0
0
 
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Waizara ya Michezo, Yusuph Singo  akiwa anamkabidhi bendera ya taifa kwa nahodha wa timu ya wanawake chini ya miaka 20 Tanzanite Stars kuelekea nchini Nigeria kwa ajili ya mchezo wa kimataifa wa kuwania kucheza Kombe la Dunia. katikati ni Kocha Mkuu wa timu hiyo Sebastian Mkoma na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Wilfred Kidau na baadhi ya viongozi wengine kutoka TFF.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Timu ya Taifa ya Wanawake wenye umri wa miaka 20 'Tanzanite Stars' leo imekabidhiwa bendera ya Taifa na Mkurugenzi wa Michezo kabla ya safari ya kuelekea Nigeria kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Ufaransa, 2019.

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Waizara ya Michezo, Yusuph Singo amewakabidhi bendera ya taifa kwa timu hiyo  inayoondoka leo usiku kuelekea nchini Nigeria kwa ajili ya mchezo wa kimataifa wa kuwania kucheza Kombe la Dunia.

Akiwakabidhi bendera mbele ya Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Wilfred Kidau, Singo amesema kuwa ana imani kubwa sana na kikosi cha wachezaji hao wanaoelekea nchini Nigeria na amewataka warejee nyumbani wakiwa kifua mbele na ushindi.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Waizara ya Michezo, Yusuph Singo akizungumza kabla ya kukabidhi bendera ya timu ya Taifa leo Jijini Dar es salaam , Kulia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Wilfred Kidau, Mkurugenzi wa Ufundi Salum Madadi (kwanza kulia) na Mjumbe wa kamati ya Utendaji TFF Lameck Nyambaya.

"Wachezaji, mnapokwenda kule mnatakiwa mfahamu kuwa mna jukumu la kuipeperusha bendera tya Tanzania na kutuwakilisha Watanzania zaidi ya milioni 50 na hii ni  fursa kubwa kwa sola ketu kujitangaza  kimataifa kama mnavyoona siku hizi wachezaji wa Tanzania wameanza kuchukuliwa kwa wingi kwenda nje," alisema Singu.

Kocha wa Tanzanite, Sebastian Mkoma alitamba kuweza kuiondoa kwneye  mashindano timu ya Nigeria ambapo mchezo huo umepangwa kufanyika  17 mwaka huu na mshindi wa mchezo huo atakutana na Morocco.

"Tumejiandaa vizuri ingawa tulikosa mechi za kirafiki za kimataifa, tutahakikisha tunapata matokeo mazuri," alisema Mkoma
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Waizara ya Michezo, Yusuph Singo kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu TFF na Kikosi cha Tanzanite Stars kinachotarajiwa kuondoka usiku wa leo kuelekea nchini Nigeria.

MICHUZI TV: WAZIRI MKUU MAJALIWA ASEMA TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA

MICHUZI TV: WAZIRI MKUU MAJALIWA ASEMA TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA


MICHUZI TV: WAZIRI MKUU MAJALIWA ASEMA TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA

TAMASHA LA KIMATAIFA LA 36 LA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO KUANZA SEPTEMBA 23-30, 2017

TFF YATOA MIPIRA 300 KWA VITUO VYA KUKUZIA SOKA LA VIJANA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa mipira 300 kwa viongozi wa vituo na wilaya katika Jiji la Dar es Salaam ikiwa ni mpango wa kuinua soka la vijana.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya TFF anayewakilisha Kanda ya Dar es Salaam na makamu mwenyekiti wa soka la Vijana Lameck Nyambaya amekabidhi mipira hiyo kwa lengo la vituo vinavyopatikana jiji la Dar es Saaalm kuweza kuwasaidia na pia kuona soka la vijana linafanikiwa.
Nyambaya alisema TFF watahakikisha mipira hiyo inatumika vizuri ili kutimiza lengo la kuibua na kuwa na vipaji vingi vya mpira ambavyo watakuja kuwa msaada kwa timu za vijana na timu ya taifa. 
"Tunaigawa mipira hii kwa vituo vya soka na mimi binafsi nitahakikisha kunakuwa na matumizi sahihi na sio vinginevyo.
Kutokana na ukubwa wa jijini hili, nilimuomba Rais wa TFF atupatie mipira 200 ambayo ametupatia na mimi mwenyewe nitaongeza mipira 100," alisema Nyambaya.
Hivi karibuni, TFF ilianzisha kampeni ya kugawa jumla ya mipira 3,100 ya soka nchi nzima kwa ajili ya soka la vijana.

Mipira hiyo imekabidhiwa kwa viongozi wa wilaya za Kinondoni, Ilala, Temeke, Kigamboni na Ubungo.

Mjumbe wa kamati ya utendaji ya TFF anayewakilisha Kanda ya Dar es Salaam, Lameck Nyambaya akizungumza na waandishi wa habari na viongozi wa wilaya kabla ya kukabidhi mipira kwa ajili ya kuwapatia viongozi wenye vituo vya kukuza vipaji vya mpira, kushoto ni makamu mwenyekiti wa chama cha soka Dar es salaam (DRFA) Salum Mwaking'inda.




Mjumbe wa kamati ya utendaji ya TFF anayewakilisha Kanda ya Dar es Salaam na Lameck Nyambaya akikabidhi mpira kwa Makamu Mwenyekiti
wa chama cha soka Dar es salaam (DRFA) Salum Mwaking'inda 
na kuwakabidhi viongozi wa wilaya 
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya TFF anayewakilisha Kanda ya Dar es Salaam, Lameck Nyambaya akiwa anachezea moja ya mipira aliyokabidhi leo kwa viongozi wa wilaya za Jijini Dar es salaam.

Mshindi wa Apple iPad kwenye tournament ya kwanza ya karata (Albastini)

Introducing Nyimbo MPYA ya Jay Maiko Ft. Come Dash – "Sio Mbali"

Viewing all 109922 articles
Browse latest View live




Latest Images