Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live

ASKOFU SANGU AWATAKA VIJANA WASIKUBALI KUTUMIWA KULETA CHUKI, FITINA NA MAFARAKANO

0
0

Na Stella Kalinga, Simiyu

Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la SHINYANGA Liberatus Sangu amewataka Vijana kutokubali kutumiwa kuleta vurugu, chuki na mafarakano hapa nchini.

Askofu Sangu ametoa wito huo wakati wa Ibada ya Sakramenti ya Kipaimara iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu John Mjini Bariadi.“Maandiko Matakatifu yanasema Vijana wana nguvu; kwa hiyo nawasihi vijana popote pale mlipo muwe chimbuko la Upendo, furaha na amani; watu wengine wasitumie nguvu zenu vijana kuleta chuki, fitina na mafarakano, muwe macho” alisema Askofu Sangu.

Askofu Sangu amewaasa waumini wa Kanisa hilo kuishi maisha mema ambayo hayatakuwa chanzo cha mateso kwa watu wengine katika familia, jumuiya , jamii wanaoishi na Taifa kwa ujumla.Aidha, amewataka Watanzania wote kupinga na kukemea mauaji ya watu wenye ualbino kwa kuwa wanayo haki ya kuishi kama watu wengine na watu wote wameumbwa kwa mfano wa Mungu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ametoa wito kwa Kanisa kuwa na mtazamo wa kuisaidia nchi katika kupambana na tatizo la ajira hususani kwa vijana.Ameongeza kuwa ni vema Kanisa liyavae maneno ya Mhe.Rais kuhusu Ujenzi wa Tanzania ya Uchumi wa Kati na kuona namna linavyoweza kushiriki katika kufikia Tanzania Mpya, kwa kuimarisha Idara za Kanisa na Vyama vya Kitume na kuzijenga idara na vyama hivyo katika mtazamo wa Kiujasiriamali.
Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la SHINYANGA Liberatus Sangu akiongoza Ibada ya Sakramenti ya Kipaimara katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu John Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na Waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu John Mjini Bariadi katika Ibada ya Sakramenti ya Kipaimara iliyoongozwa na Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la SHINYANGA Liberatus Sangu.
Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la SHINYANGA Liberatus Sangu akiwapaka mafuta vijana wa Kipaimara katika Ibada ya Sakramenti ya Kipaimara iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu John Mjini Bariadi.
Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la SHINYANGA Liberatus Sangu akiwabariki vijana wa Kipaimara katika Ibada ya Sakramenti ya Kipaimara iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu John Mjini Bariadi.


BANDARI YA TANGA YANG’ARA KILIMANJARO CUP

0
0
TIMU ya Mpira wa Kikapu ya Bandari Tanga ambayo inashikilia Ubingwa wa Mashindano ya Kilimanjaro Cup mwaka jana inashiriki tena Mashindano hayo kutetea ubingwa huo mwaka huu katika mashindano yanayoendelea kwenye viwanja KCMC mjini Moshi.

Kitendo cha timu hiyo kuendelea kufanya vizuri katika mashindano hayo kwa mara nyengine kinaonyesha namna kinavyotumia vema fursa hiyo kuitangaza Bandari ya Tanga.

Katika kuhakikisha suala hilo linakwenda kwa vitendo leo timu ya Bandari Tanga wameibuka na ushindi wa vikapu 64-57 dhidi ya timu ya Baptist katika mechi iliyokuwa na upinzani mkubwa huku Bandari Tanga ikipambana ili kuhakikisha inatetea Ubingwa wake na kuondoka na ushindi huo.

Awali akizungumza wakati akizundua mashindano hayo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwira amezitaka timu shiriki kutumia fursa ya mashindano hayo kutangaza utalii wa nchi ikiwemo mlima Kilimanjaro.“Baada ya mashindano haya timu zote shiriki zitakwenda kupanda mlima Kilimanjaro ili kuweza kuhamasisha wanamichezo na wananchi wengine kuweza kutalii mlima huo “Alisema Mkuu huyo wa mkoa.

Mkuu huyo wa mkoa alitumia nafasi hiyo kuwataka vijana kuchangia damu kwa wahitaji ambapo katika viwanja hivyo sehemu iliyotengwa kwa ajili ya kuchangia damu kwa hiari.Mashindano hayo yanaendelea kwa wiki nzima katika viwanja vya Baptist na KCMC Mkoani Kilimanjaro.Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.
Mchezaji wa timu ya Bandari Tanga akiruka juu kuwania mpira wakati wa mchezo wa Mashindano ya Kilimanjaro Cup yanayoendelea kwenye viwanja wa KCMC na Baptist ambapo mechi hiyo ilikwisha kwa Bandari Tanga kuibuka na ushindi wa vikapu 64 dhidi ya 57 
Wachezaji wa timu za Bandari Tanga na Baptist wakiwania mpira wakati wa mchezo wa Mashindano ya Kilimanjaro Cup yanayoendelea kwenye viwanja wa KCMC na Baptist ambapo mechi hiyo ilikwisha kwa Bandari Tanga kuibuka na ushindi wa vikapu 64 dhidi ya 57 
Kikosi cha timu ya Mpira wa Kikapu ya Bandari Tanga .


Usiku wa Kilimanjaro ndani ya Sweden 14 October 2017

0
0

Kutakuwepo: Wasanii wa aina tofauti na Disko, Sanaa za ufundi, Vyakula vya ki Afrika vyenye asili ya Tanzania, pamoja na 
Wataalamu watakaoelezea utalii wa Tanzania.
Venue: Kulturhuset Örebro. Järnvägsgatan 8
70362 Örebro.
Time: 15:00 -- middle of the night
At the door: 250 sek
Kuponi ya chakula na kinywaji 350 sek
Tiketi ya kikundi watu 6 ni 150 sek per each.
Unaweza kununua tiketi yako mapema online via..
Otherwise Contact @biorn_records
@mmbandokennedy

SIMUTV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

Serikali Mtandao - Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Mkurugenzi Mkuu wa FAO kuzuru Tanzania, kufanya maqzungumzo na viongozi waandamizi wa Serikali, wadau

0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, (FAO), José Graziano da Silva(pichani), Jumanne wiki hii ataanza ziara rasmi nchini Tanzania ambapo anategemewa kufanya mikutano na mazungumzo na maofisa waandamizi wa serikali na wadau.

Bw. Graziano da Silva anategemewa kukutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein.

Mkurugenzi Mkuu wa FAO amepanga kufanya mikutano na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi (Tanzania Bara), Dkt. Charles Tizeba, na Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Zanzibar, Hamad Rashid Mohamed.

Ziara hii ya Mkurugenzi Mkuu inakuta wakati FAO ikiadhimisha miaka 40 toka kuanza shughuli zake hapa Tanzania. Wakati wa ziara hii, Bw. Graziano da Silva atakutana na uongozi na wafanyakazi wa FAO hapa Tanzania kabla ya kuhudhuria hafla maalum hapa Dar es Salaam kusherehekea maadimisho hayo. Hafla hiyo itahudhuriwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Samia Suluhu Hassan.

Mwakilishi Mkazi wa FAO hapa nchini, Bw. Fred Kafeero, amethibitisha kuwa Bw.  Graziano da Silva atakuwa hapa nchini kufuatia mwaliko wa Serikali ya Tanzania. “Mkurugenzi Mkuu wa FAO atabadilishana mawazo na Serikali ya Muungano wa Tanzania kwenye masuala makuu yanayohusiana na uhakika wa chakula na maendeleo ya kilimo, ikijumuisha juhudi za FAO kitaifa na kikanda,” alisema. Bw. Graziano da Silva pia atajadili mambo mengine yanayohusiana na ushirikiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na FAO, pia masuala mengine ya umuhimu kati ya pande hizo mbili, aliongeza. Mbali ya Maafisa wa Serikali, Mkurugenzi Mkuu atakutana na wadau wengine wa FAO hapa nchini wakiwa ni pamoja na asasi za kiraia, taasisi za elimu, na taasisi za utafiti.

Baadae Mkurugenzi Mkuu ataenda Zanzibar ambapo, miongoni mwa mambo mengine, anategemewa kuweka jiwe la msingi katika jingo la Mradi wa Kuzalisha vifaranga vya samaki unaofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Korea kupitia Shirika lake la Maendeleo ya Kimataifa KOICA.  Pia Bw. Graziano da Silva atapata fursa ya kutembelea mradi wa kilimo cha mwani na pia kuona maonesho ya bidhaa mbali mbali zilizotengenezwa na wanawake wanaojihusisha na kilimo cha mwani.


Tanzania ilijiunga na FAO mwaka 1962, na mwaka 1977 FAO ilifungua ofisi zake hapa Tanzania. Katika miaka 40 ya uwepo wake, FAO imeisadia Serikali ya Tanzania katika kupanga na kutekeleza sera, mikakati na mipango ya kilimo hapa nchini. Kazi ya FAO imejikita katika kuboresha usalama wa chakula na lishe pamoja na maisha ya wakulima wadogo na hivyo kuwa chachu ya kukua kwa uchumi kupitia sekta ya kilimo. 

MAGAZETI YA JUMATATU SEPT 4, 2017

Kwa Simu Toka London: Vibanda Simu Mitaani vingalipo London


MFAHAMU JAPO KWA UCHACHE JAJI DAVID MARAGA -MSABATO MWENYE IMANI KALI

0
0
.....'I am a God fearing person who believes in, and endeavours to do, justice to all irrespective of their status in society.....' 

Mzaliwa wa Januari 12, 1951, Jaji wa Mahakama ya juu nchini Kenya, David Maraga na wenzake wanne wameweka historia kwa kubatilisha uchaguzi wa urais wa mwezi Agosti na kuamuru kurudiwa ndani ya siku 60 zijazo. (Land Mark Case).

Wakenya na wadau wengine kwingineko duniani wamempongeza Jaji Maraga kwa kuwa jasiri kutengua uchaguzi wa mtu aliyemchagua rais Uhuru Kenyatta mbali na kurudisha imani katika idara huru ya mahakama.

Magazeti kadhaa ya Kenya yamemtaja jaji Maraga kuwa mtu wa maadili kutokana na hatua yake ya kuwa muumini shupavu wa kanisa la Seventh Day Adventist Church (SDA).

Aliripotiwa akiliambia jopo lililokuwa likimhoji kwamba iwapo atachaguliwa kuwa jaji mkuu nchini Kenya hatosimamia kesi siku ya Jumamosi , ambayo ni siku ya kupumzika kwa waumini wa kanisa hilo.

Wengine wamedai kwamba huenda hii ndio sababu kikao cha kwanza cha kesi ya kupinga uchaguzi wa rais Uhuru Kenyatta kilianza mwendo wa saa moja usiku siku ya Jumamosi baada ya siku ya Sabato kuisha........kama mna kumbukumbu hii pia iliwahi kutokea kwa Waziri mkuu wa zamani wa Israel Bwana Ariel Sharon ambaye aliondoka mkutanoni majira ya saa kumi na mbili baada ya sabato kuingia kuhu akimwacha Clinton kutoamini macho yake (Wayahudi na sabato huwaelezi kitu).........

Wafaransa pia hawatamsahau Benjamin Netanyahau kwani baada ya kuandaa itifaki zote za kumpokea walijikuta wakiambiwa kwamba hangeweza kwenda nchini humo Ijumaa jioni HADI SABATO ITAKAPOKWISHA ...........yaaani kesho yake jumamosi tena baada ya jua kuzama.
Imeripotiwa kuwa wakati alipokuwa akikaguliwa alikabiliwa na madai kwamba alikula hongo lakini yeye aliwashangaza wengi kwa kutangaza katika runinga za taifa akiapa kwa kushikilia kitabu kitukufu cha Biblia kwamba hajawahi kuchukua hongo katika maisha yake. Jaji Maraga alifuzu kama wakili miaka 40 iliyopita kutoka chuo kikuu cha Nairobi kabla ya kuhudumu kama wakili wa kujitegemea.

4th ANNIVERSARY

0
0
Rev. Martin E. Urassa (25th Dec. 1934 – 04th Sept. 2013)

Today is the fourth  anniversary of our dear father’s passing away on 4th September 2013 at KCMC Referral Hospital and was laid to rest at Machame Nkuu on 10th September 2013.  Dad we still remember your wisdom, advice and fatherly role you played to the family, your students, parisheners of Nkuu Machame and many more people you served as a teacher and later pastor for 30 years.  

We cherish your wisdom and continue remembering you for all the good things we received from you.

Deeply missed by your wife Mrs. Tryphosa Martin Urasa and children: Oswald, Benet, Evans, Beatrice, Joyce and Alwisa, inlaws, grand children, brothers and relatives. 

Tamasha la waandishi wa habari mkoa wa Arusha kufanyika Nyerere Day

0
0
Katibu wa TASWA-ARUSHA Mussa Juma wa nne kutoka kulia akiwa pamaoja na wadhamini wa muda mrefu wa bonanza la wanahabari mkoani Arusha mara baada ya kumaliza mkutano na wanahabari ambapo wametangaza kuwa bonanza la mwaka huu litafanyika siku ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere.


Wanahabari zaidi ya 400 wanatarajia kushiriki katika Tamasha la vyombo vya habari, Kanda ya kaskazini, litakalofanyika kuanzia Octobar 14 siku ya kumbukumbu ya mwalimu Julius Nyerere hadi octobar 15 mwaka huu.

Siku ya kumbukumbu ya mwalimu Nyerere kutakuwa na kongamano kujadili mchango wa hayati baba wa Taifa, katika masuala ya kiuchumi, kisiasa na michezo na baadaye octobar 15 kutakuwa na michezo katika uwanja wa General Tyre katika jiji la Arusha.

Tamasha hilo ambalo hufanyika kila mwaka linaandaliwa na Taasisi ya Arusha Media kwa kushirikiana na chama cha waandishi wa habari za michezo na burudani mkoa Arusha(TASWA- Arusha chapter).

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu wa TASWA mkoa Arusha, Mussa Juma, alisema tamasha hilo litashirikisha wanahabari 400 kutoka mikoa ya Arusha,Manyara, Kilimanjaro na Jijini Dar es Salam.

Juma alisema katika kongamano hilo mada mbali mbali zitatolewa na wabobezi katika masuala ya kiuchumi, kisiasa na michezo na wanahabari watapata fursa kutambua zaidi mchango wa hayati baba wa Taifa katika michezo.

"Mwaka huu, tumeamua kuanza na kongamano ili kukumbushana wanahabari masuala mbali mbali ambayo ni muhimu kwa mustakabali wa taifa letu"alisema

Akizungumzia maandalizi ya Bonanza, mratibu wa bonanza hilo Andrea Ngobole amesema katika tamasha hilo wanahabari na timu waalikwa watashiriki katika michezo ya soka, kuvuta kamba, mbio za magunia, riadha, kukimbiza kuku .

"maandalizi yanakwenda vizuri lakini tunaomba wadhamini zaidi kujitokeza ili kufanikisha tamasha na Kongamano la wanahabari mwaka huu"alisema.

Alisema katika michezo timu ambazo tayari zimethibitisha kushiriki ni TASWA Dar es Salaam ambao ndio mabingwa watetezi, timu za Radio Sunrise,timu za vyuo vya Uandishi habari Arusha, Arusha one Radio, Triple A Radio, Radio 5, ORS Radio ya mkoa Manyara na TASWA Arusha.

"tutangaza zawadi hivi karibuni na pia wageni waalikwa kama ambavyo hufanyika kila mwaka"alisema.
Waandishi wa Habari kutoka chuo cha uandishi wa Habari Arusha wakifurahia ushindi wao katika moja ya mabonanza yaliyopita jijini Arusha ambapo chuo hicho kimekuwa kikishriki bonanza hili toka mwaka 2008 na mwaka huu wamethibitisha kushiriki tena.

Baadhi ya Waandishi wa habari za michezo wakifatilia burudani katika moja ya bonanza la wanahabari za michezo jijini Arusha. 
Wakufunzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha wakifuatilia mwenendo wa Mchezo kati ya Sunrise Redio na Chuo cha AJTC 
Mwandishi wetu,Arusha

Warembo vyuo vikuu kupambana Septemba 29

0
0
Warembo wa vyuo vikuu vya Tanzania “Miss Higher Learning Institution 2017” watapanda jukwaani  Septemba  29,  kwenye ukumbi wa King Solomoni, Namanga jijini. Mashindano hayo yameandaliwa na kampuni ya Glamour Bridal Tanzania baada ya kupewa idhini ya waandaaji wa Miss Tanzania, Lino International Agency kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa Tanzania (Basata).

Mkurugenzi wa Glamour Bridal Tanzania Muba Saedo alisema kuwa wanatarajia kufanya mashindano yenye upinzani wa hali ya juu kutokana na idadi ya vyuo mbalimbali vilivyothibitisha.
Mbali ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii (ISW), mashindano hayo yatashirikisha vyuo vya Taasisi ya Uhasaibu Dar es Salaam (TIA), IFM, CBE, UDOM, Tumaini – Makumira na Taasisi ya Uhasibu wa Arusha (IAA) na Chuo Kikuu Cha Ardhi.

Saedo alivitaja vyuo vingine kuwa ni Mzumbe, Chuo Kikuu cha Iringa, Tanzania Aviation University College na Magogoni. Alisema kuwa bado wanapokea maombi kutoka vyuo mbalimbali na mwisho wa kuthibitisha ni Septemba 11.

“Kwa sasa tunapokea warembo ili kuweza kushiriki katika mashindano haya, kuna vyuo vilifanya mashindano na vingine  vilifanya uteuzi wa ndani na kutuletea majina kutokana na kuepuka gharama za kufanya mashindano,”

“Mpaka sasa kuna warembo ambao wamejitokeza kuwania nafasi tatu za kushiriki mashindano ya Miss Tanzania mwaka huu, kwa vile tunahitaji mashindano bora yenye ushindani wa hali ya juu, bado tunawakaribisha wasichana wanaosoma vyuo mbalimbali kuwasiliana na waandaaji ili kujaribu bahati yao,” alisema Saedo.

Kwa mujibu wa Saedo warembo wanaotaka kushiriki katika mashindano hayo wanatakiwa kuomba kupitia instagram page @higher­_learning_miss_tz_2017 au kupitia mubasaedo4me@gmail.com, msaedo@glamourbridal@gmail.co.tz na jmsendo@glamourbridal.co.tz.
Miss Higher Learning Institutions 2016 , Laura Kwai akipunga mkono baada ya kutangazwa kutwaa taji hilo kwenye Ukumbi wa King Solomoni jijini Dar es Salaam. Kushoto ni mshindi wa pili Evelyn Andrew pamoja na mshindi wa tatu Clara Nyaki.

MAJARIBIO ZAIDI YA MAKOMBORA YAANDALIWA KOREA KASKAZINI

0
0
Korea Kusini imesema kuwa kuna dalili kuwa Korea Kaskazini inapanga majaribio zaidi ya makombora hususan makombora ya masafa marefu.
Maafisa wa ulinzi wamekuwa wakilishauri bunge mjini Seoul baada ya Korea kulifanyia jaribio bomu la nyuklia mwishoni mwa wiki.
Korea Kusini imejibu kwa kufanya majaribio kwa kurusha makombora kwa kutumia ndege na kutoka ardhini.

Marekani imeonya kuwa tisho lolote kwake na kwa washirika wake litapingwa vikali kijeshi. Korea Kusini imesema kuwa ililifanyia majaribio bomu la haidrojeni ambalo linaweza kuwekwa kwa kombora la masafa marefu.

Baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kufanya kikao cha dharura baadaye leo kujadili hatua za kuchukua.
Chang Kyung-soo, ambaye ni afisi kutoka wizara ya ulinzia aliliambia bunge, "tunaendelea kuona dalili za uwezekano wa makombora zaidi ya masafa marefu. Pia tunaweza kutabiri kuwa Korea Kaskazini huenda ikarusha kombora la masafa marefu.

Wizara hiyo pia ililiambia bunge kuwa huenda Marekani ikapeleka manowari wa nyuklia ya kubeba ndege katika rasi ya Korea.

Chanzo: BBC Swahili

Waziri Mkuu awapongeza NSSF, PPF na magereza mradi wa kiwanda cha sukari cha Mbigiri mkoani Morogoro

0
0
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amepongeza hatua ya mifuko ya hifadhi ya jamii hapa nchini kuwekeza kwenye sekta ya viwanda huku akitoa wito kwa jamii hususani vijana kuhakikisha wanaonyesha uzalendo kwa kujitolea kwa vitendo kuunga mkono jitihada hizo zinazolenga kutatua tatizo la ajira na kuinua uchumi wa taifa.

Waziri Mkuu Majaliwa alitoa rai hiyo mwishoni mwa wiki mkoani Morogoro mara tu baada ya kuongoza zoezi la upandaji wa miwa ikiwa ni ishara ya kuunga mkono mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha sukari unaofahamika kama Mkulazi II unaotekelezwa kwa ubia kati ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF na PPF kupitia kampuni Hodhi ya Mkulazi Holding unaofanyika katika gereza la Mbigiri, Dakawa mkoani Morogoro.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mkulazi ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara alipotembelea shamba la kubwa la miwa linaloandaliwa ikiwa ni sehemu ya mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha sukari unaofahamika kama Mkulazi II unaotekelezwa kwa ubia kati ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF na PPF kupitia kampuni Hodhi ya Mkulazi Holding unaofanyika katika gereza la Mbigiri, Dakawa mkoani Morogoro.

"Pamoja na kutoa pongezi kwa mifuko yetu ya hifadhi ya jamii hapa nchini kwa kuitikia vema wito wa serikali ya awamu ya tano katika uwekezaji wa viwanda vyenye tija kwa taifa, kipekee nitoe wito kwa jamii hususani vijana kuhakikisha wanaunga mkono jitahada hizi kwa kujitolea ujuzi na maarifa katika kufanikisha adhma hii ya serikali inayolenga kuwanasua kutoka kwenye uhaba wa ajira,'' alitoa wito.

Wito huo wa Waziri Mkuu ulikuja kufuatia kuguswa na uzalendo ulioonyeshwa na vijana wasomi sita kutoka mikoa mbalimbali walioamua kuweka kambi kwenye eneo hilo Mbigiri wakilala chini ya miti lengo likiwa ni kuunga mkono jitiahada za ujenzi wa kiwanda hicho kwa kushiriki bila malipo katika hatua mbalimbali za ujenzi wa kiwanda hicho ikiwemo kubuni mchoro uliotumika katika moja ya jengo litakalotumika kujengwa kiwanda.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw.William Erio wakati wa ziara hiyo.

"Vijana hawa ambao kwa sasa wamepatiwa maturubai ya kujihifadhi wamekuwa mfano wa kuigwa na wenzao nchi nzima na nitazifikisha salamu zao kwa muheshimiwa Rais ajue jitiahada zake zinatafsiriwa vyema sana na vijana wazalendo wa taifa hili,'' alisisitiza.

Akizungumzia mradi huo Waziri Mkuu alisema pamoja na kumaliza tatizo la uhaba wa sukari hapa nchini, pia utapunguza tatizo la ajira sambamba na kukuza uchumi wa nchi. 

Ili kuhakikisha wananchi wanakuwa kwenye nafasi ya kushiriki kikamilifu katika kuzalisha malighafi kwa ajili ya kiwanda hicho Waziri Mkuu aliutaka uongozi wa mkoa huo kuhakakikisha wanapita wilaya nzima ya Kilosa unapotekelezwa mradi huo kuhakikisha hakuna mashamba pori zoezi litakaloambatana na unyang'anyaji wa mashamba yasiyoendelezwa kutoka kwa wamiliki wake na kisha kukabidhiwa kwa wananchi wayatumie kwa kilimo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kushoto) pamoja na Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama (katikati) wakiongoza zoezi la upandaji wa miwa ikiwa ni ishara ya kuunga mkono mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha sukari unaofahamika kama Mkulazi II unaotekelezwa kwa ubia kati ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF na PPF kupitia kampuni Hodhi ya Mkulazi Holding unaofanyika katika gereza la Mbigiri, Dakawa mkoani Morogoro. Kulia, akishirikiana nao ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk Steven Kebwe.

"Na kwa wale wananchi wanaolima kwenye eneo la magereza utumike utaratibu mzuri waweze kupata mashamba kwenye eneo la magereza waendelee na kilimo hiki cha miwa ili kulisha kiwanda licha ya kuwa umiliki wa ardhi utabaki kuwa ni wa jeshi la magereza,'' alifafanua.

Mradi huo unaolenga kuzalisha tani 50 za sukari kwa mwaka ni sehemu ya mradi mkubwa unaotekelezwa na mifuko hiyo katika eneo la Ngerengere, Wilaya ya Morogoro Vijijini unaofahamika kama Mkulazi I ambao unaolenga kuzalisha tani 200,000 za sukari kwa mwaka sambamba na kutoa ajira zaidi ya 100,000 katika hatua ya awali.

Nchi sita kushiriki mashindano ya kuogelea ya Kanda ya Tatu Afrika

0
0
Jumla ya nchi sita zimethibitisha kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya kanda ya tatu ya Afrika (Cana zone 3) yaliyopangwa kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Oktoba 19 -21.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Chama Cha kuogelea nchini (TSA), Leena Kapadia amezitaja nchi hizo kuwa ni Afrika Kusini, Zambia, Kenya, Uganda, Djibouti na wenyeji Tanzania.

Kapadia amesema kuwa walitarajia kuona nchi nyingi zaidi zinashiriki katika mashindano hayo, lakini kutokana na uhaba wa fedha zimeshindwa kufanya hivyo.

“Tumezipa nafasi zaidi kutafuta fedha ili kushiriki, tutafunga mlango wa kuthibitisha wiki moja kabla ya mashindano,” alisema Kapadia.
 Alisema kuwa Tanzania itashirikisha waogeleaji 60 wakigawanywa kwa timu mbili (Tanzania A na B) chini ya makocha wao, Alex Mwaipasi na Michael Livingstone.

Nchi ambazo zimeongezewa muda wa kuthibitisha kushiriki katika mashindano ni Ethiopia, Eritrea, Somalia, Rwanda, Sudani Kusini ambazi zipo kanda ya tatu na za kanda ya nne ni Angola, Botswana, Comoro, Madagascar, Lesotho, Malawi, Mauritius, Seychelles, Msumbiji, Namibia, Zimbabwe na Swaziland.

Alisema kuwa kwa kamati yao inatafuta wadhamini kwa ajili ya kufanikisha mashindano hayo. Wanahitaji kiasi cha Sh 100 milioni ili kufanya mashindano hayo kwa hadhi inayostahili.

Alisema kuwa wanatarajia waogeleaji zaidi ya 200 kushiriki katika mashindano hayo ambayo Tanzania ni mabingwa watetezi.

Mbali ya Kapadia, kamati hiyo pia unaundwa na wajumbe ambao ni Inviolata Itatiro, Geeta Gokarn, Phillip Saliboko, Imani Dominic, Hetal, Linges Ramasamy, Thauriya Diria, Amina Karume, Nitesh Patel, Nelly Coehlo na Mary Mugurusi.

MANJI NA WENZAKE KUHOJIWA POLISI

0
0
Mfanyabiashara Yusuph Manji, akitoka Mahakamani baada ya Hakimu Mkazi, Huruma Shahidi kuruhusu yeye na wenzake watatu wanaokabiliwa na tuhuma za uhujumu uchumi kupelekwa polisi kuhojiwa ili kukamilisha upelelezi.

Manji aliyeletwa mahakamani hapo kwa hati ya kuwatoa mahakamani (remove order) anaenda kuhojiwa kufuatia barua ya maombi mahakamani hapo kutoka kwa ZCO, pia mahakama imewaamuru kesho kabla ya muda wa kazi kuisha wawe wamerudishwa mahakamani hapo.

Mbali ya Manji washtakiwa wengine ni Deogratius Kisinda, Abdallah Sangey na Thobias Fwere.

Manji na wenzake hao wamekabidhiwa kwa Detective  Koplo Dotto ambaye ametakiwa mpaka kesho ndani ya saa za kazi wawe wamerudishwa mahakamani.

habari kamili itafuata baadaye kidogo.

VIDEO: AFRICAN GUY INTERVIEWS WHITE PEOPLE

MAHAKAMA KUAMUA KAMA LISU ANA KESI YA KUJIBU AU LA OKTOBA 4 MWAKA HUU.

0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.

 MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imesema October 4 mwaka huu, itatoa uamuzi kama Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lisu(Pichani) anayekabiliwa na kesi ya uchochezi ana kesi ya kujibu au la.

 Hakimu Mkazi Godfrey Mwambapa amesema hayo leo baada ya upande wa mashtaka uliokuwa ukiongozwa na wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi kufunga ushahidi wao kwa kuita mashahidi watano.

Kabla ya hayo, Lissu alidai kuwa, kwa ushahidi uliotolewa mahakamani hapo ameona kabisa kuwa hana kesi ya kujibu. Hata hivyo, Hakimu Mwambapa amesema ni jukumu la Mahakama kuamua kama mshtakiwa anakesi ya kujibu au la.
Aidha Mahakama imezitaka pande zote mbili, ile ya mashtaka na ya utetezi Septemba 18, kuwasilisha hoja zao kama mshtakiwa ana kesi ya kujibu au la.

Katika kesi hiyo, Lissu anakabiliwa na kesi ya uchochezi ambapo mapema mwaka huu, akiwa katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alitoa kauli za uchochezi kuwa, “Mamlaka ya Serikali mbovu ni ya kidikteta uchwara inahitaji kupingwa na kila Mtanzania kwa nguvu zote, “huyu diktekta uchwara lazima apingwe kila sehemu”. Kama uongozi utafanywa na utawala wa kijinga nchi inaingia ndani ya giza nene.’’

Kwa simu Kutoka London: Mwito kwa Watanzania Kuchacharuka London - Na Freddy Macha

POLISI WAREJEA NA MEDALI MICHEZO YA MAJESHI

0
0
Wanamichezo wa Polisi walioshiriki michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za Afrika Mashariki (EAPCCO Games) Kampala Uganda wamerejea nchini ambapo wamefanikiwa kujinyakujilia jumla ya medali 6, 1 ya dhahabu, 2 za fedha na 3 za Shaba na hivyo kuibuka mshindi wa tatu kwa ujumla katika michezo hiyo iliyoshirikisha majeshi ya Polisi kutoka nchi saba.

Wanamichezo hao wamepokelewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro ambapo alisema Jeshi hilo litaendelea kushiriki michezo mbalimbali ili kujenga afya na ukakamavu kwa Askari pamoja na kuboresha mahusiano ya utendaji kazi katika kubadilishana uzoefu na kuiletea sifa nchi.

IGP Sirro alisema wanamichezo hao wamefanya kazi kubwa ambapo pamoja na uchache wao wameonyesha kuwa wako vizuri katika michezo jambo ambalo ni hazina kubwa kwa Jeshi la Polisi Tanzania.

Kwa upande wake Kamishna wa Polisi Jamii Mussa Ali Mussa alisema michezo hiyo imeliletea sifa taifa la Tanzania na Jeshi la Polisi kwa ujumla hivyo kuna haja ya kuhakikisha kuwa wanamichezo hao wanakaa kambini muda mrefu pindi itakapojitokeza michezo mingine ili waweze kufanya vizuri zaidi.

Naye mshindi wa medali ya Dhahabu katika riadha mita 800 PC Basil John amesema Michezo hiyo ilikuwa na ushindani mkubwa lakini walijitahidi kupambana ili kuhakikisha wanarejea na medali licha ya kuwa  wachache katika michezo hiyo ya majeshi ya Polisi.

Michezo hiyo ilifanyika Agosti 25 mpaka 30 mwaka huu ambapo nchi zilizoshiriki ni pamoja na mwenyeji Uganda, Tanzania, Kenya, Rwanda, Sudan, Burundi pamoja na Sudani Kusini ambapo Uganda ilichukua ushindi wa kwanza, Kenya wa pili na watatu Tanzania.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akipokea kombe la ushindi wa tatu kutoka kwa Inspekta Hashim Abdallah wakati wa mapokezi ya wanamichezo wa Polisi waliokuwa wakishiriki Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za Afrika Mashariki (EAPCCO Games) nchini Uganda.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akimpongeza Mwanariadha wa Polisi PC Basili John baada ya kushinda medali ya Dhahabu katika Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za Afrika Mashariki (EAPCCO Games) nchini Uganda hivi karibuni ambapo Polisi Tanzania ilishika nafasi ya Tatu kati ya nchi saba zilizoshiriki michezo hiyo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akimpongeza Mwanamichezo wa Polisi Koplo Gaston Komba baada ya kushinda medali ya shaba kwa upande wa Taikondo katika Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za Afrika Mashariki (EAPCCO Games) nchini Uganda hivi karibuni ambapo Polisi Tanzania ilishika nafasi ya Tatu kati ya nchi saba zilizoshiriki michezo hiyo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro na Viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na Wanamichezo wa Polisi walioshiriki katika michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za Afrika Mashariki (EAPCCO Games) nchini Uganda hivi karibuni ambapo Polisi Tanzania ilishika nafasi ya Tatu kati ya nchi saba zilizoshiriki michezo hiyo.(Picha na Jeshi la Polisi).
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live




Latest Images