Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110167 articles
Browse latest View live

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YATEMBELEA MAPANGO YA AMBONI JIJINI TANGA LEO

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (wa tatu kulia) akiongoza wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, kutembelea Mapango ya Amboni Jijini Tanga leo. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Atashasta Ndetiye (wa pili kushoto), Wajumbe wa kamati hiyo, Nape Nnauye (kushoto) na Shaban Shekilindi (kulia). 
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakiangalia sehemu ya barabara iliyomeguka ndani ya eneo la Mapango ya Amboni.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakisikiliza maelezo kuhusu mapango hayo kutoka kwa Mhifadhi wa Mambo ya Kale, Jumanne Gekora.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati) akizungumza na wajumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii muda mfupi kabla ya kuanza ziara ya kuingia ndani ya mapango ya Amboni. Mhandisi Makani alisema mipango ya Serikali ni kutambua vivutio vya aina mbalimbali ikiwemo vya mambo ya kale kama yalivyo mapango ya Amboni kuviboresha na kuvitangza ili vichangie zaidi katika pato ta taifa.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani na baadhi ya wajumbe wa msafara huo wakiwa ndani ya mapango ya Amboni.
Picha na; Hamza Temba-Wizara ya Maliasili na Utalii

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

kumbukumbu ya mama joyce mkamsuri marealle

$
0
0
Mama. unafikisha miaka saba tangu ulipotutoka Septemba 2, 2010. Mama tunakukumbuka. 
Pumzika kwa amani mama yetu mpenzi. 
 - Emmy marealle

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

BURIAN ANATOLIA NSEKA, KAPUMZIKE KWA AMANI MAMA YETU

$
0
0
Mama Anatolia Nseka enzi za uhai wake
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Mama Anatolia Nseka kuingiza nyumbani kwake Tabata Barakuda jijini Dar es Salaam jana baada ya kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ulikokuwa umehifadhiwa baada ya kufariki dunia Tarehe 30-8-2017 katika hospitali hiyo alikokuwa amelazwa kwa matibabu. Mama Nseka mazishi yake yanatarajiwa kufanyika leo Makaburi ya Kinyerezi.
 Baadhi ya ndugu zake mama Nseka wakilia baada ya mwili huo kuwasili nyumbani kwake. Hakika ni huzuni kubwa kumpoteza mpendwa wetu.

 Mwili ukiingizwa ndani.
 Ni huzuni kubwa.
Jeneza likiingizwa nyumbani kwake.
Picha na DottoMwaibale

Article 3

MAGAZETI YA JUMAMOSI LEO SEPT 2, 2017

MADIWANI JIJINI TANGA WATAKIWA KUHESHIMU TARATIBU ZA VIKAO

$
0
0
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga (CCM) Alhaji Mustapha Selebosi ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nguvumali akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji akipitia kabrasha kushoto ni Naibu Meya wa Jiji hilo,Mohamed Haniu ambapo Meya huyo aliwataka madiwani kuheshimu taratibu za vikao. 
Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Daudi Mayeji akizungumza wakati wa kikao hicho kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji hilo,Alhaj Mustapha Selebosi na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa .
Naibu Meya wa Jiji la Tanga,Mohamed Haniu akizungumza wakati wa kikao hicho kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji hilo(CCM) Alhaj Mustapha Selebosi kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaji Mussa Mbaruku .
Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa kikao hicho. 

WANANCHI WAHIMIZWA KUJIUNGA NA MFUKO WA AFYA YA JAMII

$
0
0

Na Stella Kalinga, Simiyu

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka ametoa wito kwa wananchi Wilayani Bariadi mkoani humo kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii(CHF).

Mtaka ametoa wito huo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Ngulyati wilayani Bariadi wakati wa ziara yake yenye lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Amesema azma ya Serikali ni kuwa ifikapo mwaka 2020 Watanzania wote wawe wamejiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii(CHF) au Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), hivyo akawahamasisha wananchi ambao bado hawajajiunga na CHF kujiunga kwa kuwa gharama yake ni nafuu.

“Watu wa Ngulyati ni wafanyabiashara wazuri, wafanyakazi wazuri, wakulima wazuri ningetamani kuwaona wote hapa mnakuwa na kadi za Mfuko wa Afya ya Jamii ambazo zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000, hii ni sawa na kuku mmoja tu mnapata matibabu watu sita kwa maana ya baba, mama na watoto wa nne” amesema.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizugumza na wananchi wa Kata ya Ngulyati wilayani Bariadi katika Mkutano wa hadhara wakati wa ziara yake yenye lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.
Mchungaji Nicholuos Chimbu mkazi wa Kijiji cha Ngulyati(kulia) wilayani Bariadi akiwasilisha kero yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(hayupo pichani) alipofanya ziara wilayani humo kwa lengo la kuzikiliza kero za wananchi na kuzitafuatia ufumbuzi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga wakiteta jambo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa katika Kata ya Ngulyati aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Minza Maduhu mkazi wa Kijiji cha Ngulyati wilayani Bariadi akiwasilisha kero yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(hayupo pichani) alipofanya ziara wilayani humo kwa lengo la kuzikiliza kero za wananchi na kuzitafuatia ufumbuzi.


Z Anto amng'ang'ania Diamond na Alikiba, asema 'wote nawaweza vizuri'

$
0
0
Msanii wa muziki aliyewahi kufanya vizuri na wimbo Malavidavi, Mpenzi Jini na nyingine nyingi, Z Anto, amefunguka kwa kusema kuwa wiki hii ataachia kazi yake mpya huku akidai haamini kama kazi yake hiyo itashindwa kufanya vizuri kwa kuwa Diamond na Alikiba wameachia kazi zao mpya ambazo zinashindanishwa mitandaoni.

Akiongea na waandishi wa habari Jumamosi hii jijini Dar es salaam, Z Anto amedai yeye atapita katikati ya Diamond na Alikiba kwa kuwa muziki wake unapendwa na watu wa rika zote na pia hauna makundi kama ulivyo wa wawili wao.

 "Wote nawaweza sana, muziki wangu ni mtamu na hauna makundi kwahiyo kila mtu anaweza kuusikiliza hata hao bila shaka ni mashabiki wa muziki wangu ndio maana nikasema kuogopa kuachia ngoma sasa hivi kwaajili ya Diamond na Alikiba utakuwa ni ujinga," alisema Z Anto.

 Aliongeza "Binafsi najiamini sana kwa sababu muziki wangu ni mzuri na tayari kuna platfom ambayo niliiweka toka kipindi cha nyumba sema tu ukimya wangu ndio umewapa nafasi hawa ndugu zangu lakini sioni kama nitatizo kwasababu bado nafasi yangu naiona," Muimbaji huyo amesema anajua muziki umebadilika sana ndio maana na yeye amejipanga kivingine ili kukabiliana na watu ambao wanashindana kwa sasa kwenye muziki.

 "Kila mtu anatakua kuwa juu zaidi ya mwenzake na ukimya wangu umewapa nafasi wasanii wengi sana na lengo langu ni kufanya vizuri zaidi ndio maana nikasema sishindani na Diamond wala Alikiba mimi nitapita katikati yao na mashabiki ndio wenye maamuzi ya mwisho katika hili kwahiyo mimi ningesema tusubiri kazi mpya waisapport halafu ndio tuanze kupima," alisema Z Anto. 

 "Mimi naamini msanii yoyete anaweza kufanya vizuri zaidi ya hata wakongwe kama akijipanga vizuri muziki una sifa hiyo, kwahiyo mimi naweza kusema lolote linaweza kutokea kwenye muziki lisiwe leo au kesho muda ukifika hauwezi kushindana nao, wakati ni ukuta," alifafanua zaidi. Katika ujio wake muimbaji huyo amesema tayari ameandaa audio na video ambayo itaanza kutoka na kuleta picha mpya katika muziki wake. "Kazi zipo tayari kwa sababu ni nyingi na naanza na moja moja, siku yoyote kuanzia leo nitaachia kazi moja na baada ya upepo wa hapo nitaendelea kasi hiyo hiyo kadri mambo yanavyokwenda," alisema Z.

INTRODUCING LE MUTUZ ONLINE TV

TANZIA: DC wa zamani Muhingo Rweyemamu amefariki dunia

$
0
0
Mwandishi wa habari mkongwe na aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya katika Serikali ya awamu ya nne, Muhingo Rweyemamu amefariki dunia asubuhi ya leo baada ya kusumbuliwa na maradhi ya tumbo na mapafu kwa muda mrefu.

Taarifa zaidi zitafuata baadaye kadri zitakavyotufikia

WANAFUNZI 8 WA SHULE ZA SEKONDARI NA 7 WA SHULE ZA MSINGI WAJAZWA MIMBA RUFIJI

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Rufiji

Jumla ya wanafunzi wa kike nane wa shule za sekondari na saba na shule za msingi wilayani Rufiji mkoani Pwani ,wamebainika kuwa wana mimba, mwaka huu. Kutokana na taarifa hiyo, mkuu wa wilaya ya Rufiji, Juma Njwayo, amewaasa wanafunzi wa kike kuacha kukimbilia mambo ya ovyo badala yake wajidhatiti katika elimu ili kupata maarifa na ufahamu.

Akizungumza baada ya kukamilisha ziara yake ya mwezi mmoja ya kutembelea shule 43, kuzungumza na wazazi na walezi, alisema mimba za utotoni zinakwamisha jitihada za kumkomboa mtoto wa kike kitaaluma. Njwayo alieleza, kati ya mimba zilizobainika mwanafunzi mmoja ni wa shule ya sekondari Ngorongo, Nambunju na wengine saba ni wa shule za msingi.

Alifafanua, zipo hatua za kisheria zinazochukuliwa kwa waliohusishwa kuwatia mimba wanafunzi hao, ambapo watendaji wa kata wameshawashtaki kwenye vyombo vya sheria. Alisema, pia wanatengeneza mazingira mazuri kwa watoto mashuleni kwa kuwataka walimu wakae nao mara kwa mara kuwaelimisha wajiepushe na wanaume wadanganyifu .

Kwa mujibu wa Njwayo, kilichomsukuma kufanya ziara hiyo ilikuwa baada ya kupata taarifa kuwa kuna wanafunzi watoro wa kudumu 190 kati ya wanafunzi 2,442 wanaotarajiwa kufanya mtihani wa darasa la saba mwaka huu. Aidha katika ziara hiyo amefanikiwa kuwarejesha shule wanafunzi hao 54 wa shule ya Ikwiriri, shule ya msingi Utete tisa na shule ya msingi Mapinduzi tisa.

Njwayo alielezea, alichogundua ipo changamoto ya wazazi kutokuwa na ushirikiano na walimu na kutofuatilia mwenendo wa watoto wao kila siku.

"Elimu ni muhimu, ni nguzo na msingi wa maisha yetu, na kwa watoto wetu, itaweza kuwasaidia kupata ufahamu wa kujiajiri na kuwa mwanakilimo bora wa kisasa na kuwa na upeo kuliko kukosa elimu " alisisitiza Njwayo.

Njwayo ,alisema kwasasa kuna watendaji wa vijiji na kata wamefukuzwa kutokana na kukatwa kwani hawakuwa na cheti cha kidato cha nne hivyo wanaajiriwa wapya kuziba mapengo .

"Hapo ndipo inapoonekana thamani ya elimu ,hivyo wanafunzi waache michezo na vishawishi ,;wasome kwa bidii " alisema Njwayo.

TAIFA STARS YAIKALISHA BOTSWANA UWANJA WA UHURU JIJINI DAR, YAICHAPA BAO 2-0

$
0
0
Nahodha wa Timu ya Taifa (Taifa Stars), Mbwana Samatta akiondoka na mpira mbele ya mabeki wa timu ya Taifa ya Botswana, katika mchezo wa kirafiki wa kimamataifa, uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Taifa Stars imeshinda 2-0.
 Mchezaji Gadiel Michael wa Taifa Stars akichuana na Beki wa Botswana, Mosha Gaolaole, katika mchezo wa kirafiki wa kimamataifa, uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Taifa Stars imeshinda 2-0.
Mshambuliaji wa Taifa Stars, Simon Msuva akiachia shuti kali lililomshinda mlinda mlango wa Botswana na kuingia wavuni, katika mchezo wa kirafiki wa kimamataifa, uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Taifa Stars imeshinda 2-0.
 Simom Msuva, Mzamiru Yassin na Shizza Kichuya wakishangilia baada ya ushindi walioupata dhidhi ya Botswana, mchezo uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaam. Taifa Stars imeshinda 2-0.

RAIS DKT. MAGUFULI NA MKEWE MAMA JANETH WASHIRIKI IBADA KWENYE KANISA LA WASABATO MAGOMENI

EFM NJE NDANI , SINGELI MICHANO ZAPAGAWISHA WAKAZI WA TABATA

$
0
0
 Msanii Chipukizi wa Muziki wa Singeli nchini akionyesha umahiri wake wa kuimba katika jukwaa la Singeli michano linaloendeshwa na programu ya Mziki mnene na Nje ndani  ya Efm Radio
 Mashabiki wa Muziki wa Singeli wakiwa wanashangilia ndani ya Uwanja wa Toto Tundu Tabata Jijini Dar es Salaam leo.
 Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva Harmorapa akiongoza kundi la Efm Joging Tabata katika mazoezi ya mbio za pole yaliyofanyika asubuhi ya leo jijini Dar es Salaam
 Baadhi ya Wanachama wa Efm Jogging  wakiwa katika mazoezi ya mbio za pole Tabata jijini Dar es Salaam leo
 Mkurugenzi wa Radio ya Efm na Tv E Sebo akiwania mpira mbele ya beki wa Tabata Veterans katika mchezo wa kirafiki uliochezwa katika uwanja wa Tabata Sigara Jijini Dar es Salaam
 Benchi la Ufundi la timu ya Soka ya Efm na Tv E likiongozwa na Sudi Mkumba
 Wacheaji wa Efm wakifanya mazoezi kabla ya mchezo huo kuanza mapema leo

SHAKA AWAONYA WATAKAOJIHUSISHA NA RUSHWA KWENYE CHAGUZI ZA UVCCM

$
0
0
 Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka akizungumza na Waandishi wa Habari wakati akitoa taarifa ya mwenendo wa mchakato wa uchaguzi wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) na kusema kuwa yoyote atakaye jihusisha na vitendo vya Rushwa asitegemee nafasi ndani ya jumuiya hiyo au chama
 Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka, akisisitiza jambo kwa Waandishi wa habari juu ya mwenendo wa Jumuiya hiyo nchini na mafanikio waliyoyapata ndani ya miaka mitatu
 Waandishi wa  Habari walioshiriki mkutano huo wakifuatilia hotuba ya Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shakha Hamdu Shakha.


Ndugu Waandishi wa habari;

Kwa mara nyingine tena tunawakaribisha kwa mikono miwili katika mkutano huu muhimu. Karibuni sana huku nikiwaomba  mjione mko huru na mko nyumbani .

Dhana ya Demokrasia ni jambo muhimu linalohitaji kuheshimiwa na kuenziwa ndani ya Chama na  Jumuiya zake. Kiongozi wa UVCCM mahali popote pale huchaguliwa kwa kufanyika uchaguzi huru na wa  haki unaozingatia Kanuni na Taratibu za Uchaguzi kama zilivyoagizwa na vikao husika bila ya kukiuka, kupuuzwa au kuvunjwa.

Nia ya UVCCM ni kujenga na kudumisha haiba  njema ya kuendelea kuheshimu misingi ya demorasia ya kweli , yenye kuchunga  adabu na kufuata nidhamu, miiko na maadili kwa kila mwanachama anayetaka kutumia haki ya kuchagua au kuchaguliwa.

April Mwaka 2017 Chama Cha Mapinduzi kilianza mchakato wa Uchaguzi ndani ya Chama na Jumuiya zake. Kufuatia mabadiliko ya Kanuni ya UVCCM yaliyofanyika mwezi Machi, 2017 tulianza Uchaguzi katika ngazi za Matawi ambapo hadi leo jumla ya Matawi 23,529  sawa na Asilimia 99.4% kati ya Matawi  23,670 sawa na Asilimia 0.59% yamekamilisha uchaguzi.
Ngazi za   Kata  3,913 sawa na Asilimia 96.59% kati ya Kata 4,051 sawa na asilimia 3.4% zimekamilisha uchaguzi .Kwa upande wa majimbo ya  Zanzibar majimbo 54 sawa na Asilimia 100%, wamekamilisha uchaguzi.  

Ngazi ya Wilaya na Mkoa  mchakato wa uchujaji wa  majina kwa Vijana waliomba nafasi mbali mbali ndani ya Jumuiya yetu , umeanza na  unaendelea vizuri huku jumla ya Vijana 7,606 wamejitokeza kuchuka fomu za kugombea nafasi mbali mbali katka Jumuiya yetu, hali inayoonyesha kumekupo kwa mabadiliko  na msisimko wa kisiasa ukilinganisha na chaguzi zilizopita.

Kwa upande wa ngazi ya Taifa Vijana 350 wamejitokeza kuomba nafasi za uongozi ndani ya UVCCM kama ifuatavyo:-

(i)Nafasi ya Mwenyekiti113Walioomba
(ii)Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Taifa24Walioomba
(iii)Nafasi 5 za Wajumbe wa H/Kuu103Walioomba
(iv)Nafasi  5 za Wajumbe wa B/Kuu Taifa81Walioomba
(v)Nafasi 1 Wawakilishi UWT14Walioomba
(vi)Nafasi 1 Wawakilishi Wazazi15Walioomba

HATIMAYE MDAU WA GLOBU YA JAMII NDG. ALLY NYAMBI AMVIKA PETE MCHUMBA WAKE BI.EUNICE MWAKANG’ATA

$
0
0
 Mdau wa Globu ya Jamii Ndugu Ally Nyambi  akifurahia  baada ya kumvika Pete mchumba wake Bi.Eunice John Mwakang’ata huko maeneo ya Jacaranda jijini Mbeya.

  Mdau wa Globu ya Jamii Ndugu Ally Nyambi akila pozi na mchumba wake Bi.Eunice John Mwakang’ata baada ya hafla hiyo ya kumvisha pete
  Mdau wa Globu ya Jamii Ndugu Ally Nyambi akila pozi na mchumba wake Bi.Eunice John Mwakang’ata baada ya hafla hiyo ya kumvisha pete.
 Mdau wa Globu ya Jamii Ndugu Ally Nyambi akila pozi na mchumba wake Bi.Eunice John Mwakang’ata na mzaa chema baada ya hafla hiyo ya kumvisha pete. Uongozi wa Michuzi Blog unawatakia wapendanao hawa maandalizi mema ya siku yao ya kumeremeta.

BALOZI WA KUWAIT NCHINI, MHE JASEEM AL NAJEM AKABIDHI MABESENI 300 ZANZIBAR

$
0
0
Makamu wa pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Idd akipokea zawadi ya kumbumbu kutoka kwa Balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem.
Balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Zanzibar.
Balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem akimkabidhi mabeseni 300 ya vifaa tiba vya mama mjamzito Waziri wa Afya wa Zanzibar , Mahmoud Thabit Kombo(wapili kulia) katika hafla ilifanyika katika Hospitali ya mnazi mmoja.

WADAU WAZIDI KUMUUNGA MKONO RC MAKONDA UJENZI OFISI ZA WALIMU.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda leo amekutana na kufanya mazungumzo na chama cha Wamiliki wa Malori ya Usafirishaji wa Mchanga ambao wamemuunga mkono kwenye kampeni ya ujenzi wa ofisi za walimu kwa kujitolea kusafirisha mchanga wote utakaohitajika. 

Wamiliki hao kwa kauli moja wamemwambia Makonda kuwa suala la kusafirisha mchanga wa kujenga ofisi zote 402 watalibeba hao hivyo yeye aendelee na majukumu mengine. 

Makonda ameshukuru chama hicho kwa kutambua thamani na mchango wa mwalimu. 

Amesema Walimu wakiboreshewa Mazingira ya kufanyia kazi itawawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi na kuwapatia Wanafunzi Elimu bora itakayosaidia Taifa kuwa na wataalamu wa kutosha na kupunguza utegemezi wa wataalamu kutoka nje ya nchi. 

Ametoa wito kwa Jamii kuendelea kuchangia Kampeni ya ujenzi wa Ofisi za Walimu ili Walimu wasifanyekazi kwenye mazingira Magumu. 

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa chama cha wamiliki wa Malori ya Kusafirisha Mchanga Bwana Emmanuel Moshi amesema kuwa wameamua kuunga mkono kutokana na juhudi za Makonda na kutambua thamani ya Mwalimu huku akieleza kuwa wataendelea kumuunga mkono.

chama cha Wamiliki wa Malori ya Usafirishaji wa Mchanga wamuunga mkono RC Makonda

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo amekutana na kufanya mazungumzo na chama cha Wamiliki wa Malori ya Usafirishaji wa Mchanga ambao wamemuunga mkono kwenye kampeni ya ujenzi wa offisi za walimu kwa kujitolea kusafirisha mchanga wote utakaohitajika.
Wamiliki hao kwa kauli moja wamemwambia Makonda kuwa suala la kusafirisha mchanga wa kujenga ofisi zote 402 watalibeba hao hivyo yeye aendelee na majukumu mengine.
Makonda ameshukuru chama hicho kwa kutambua thamani na mchango wa mwalimu.
Amesema Walimu wakiboreshewa Mazingira ya kufanyia kazi itawawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi na kuwapatia Wanafunzi Elimu bora itakayosaidia Taifa kuwa na wataalamu wa kutosha na kupunguza utegemezi wa wataalamu kutoka nje ya nchi.
Ametoa wito kwa Jamii kuendelea kuchangia Kampeni ya ujenzi wa Ofisi za Walimu ili Walimu wasifanyekazi kwenye mazingira Magumu.
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa chama cha wamiliki wa Malori ya Kusafirisha Mchanga Bwana Emmanuel Moshi amesema kuwa wameamua kuunga mkono kutokana na juhudi za Makonda na kutambua thamani ya Mwalimu huku akieleza kuwa wataendelea kumuunga mkono.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda  akiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa  chama cha Wamiliki wa Malori ya Usafirishaji wa Mchanga ambao wamemuunga mkono kwenye kampeni yake ya ujenzi wa offisi za walimu kwa kujitolea kusafirisha mchanga wote utakaohitajika. Picha na Emmanuel Massaka
Viewing all 110167 articles
Browse latest View live




Latest Images