Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110135 articles
Browse latest View live

APOLOGISE, PLEASE


TEMBO MBUGANI NA HOTELINI

SALAAM KUTOKA COMORO

$
0
0
Na Profesa Mark Mwandosya
Nimeona niandike waraka huu kutoka ughaibuni, ingawa si ugenini sana, nikiwa Jamhuri ya Comoro. Nimebahatika kusafiri sana kikazi duniani kote, kuanzia Japan mpaka Brazil, kuanzia Guyana mpaka Australia. Nimeiwakilisha nchi kikazi katika mabara yote isipokuwa Aktiki na Antaktika. 
Namshukuru Rabuka kwa kuniwezesha kulitumikia Taifa langu kwa zaidi ya miaka arobaini. Nimetembelea nchi zote jirani isipokuwa Jamhuri ya Comoro. Mara nyingi tumezoea kusema Tanzania inapakana na nchi nane; Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Watu ya Congo, Zambia, Malawi, na Msumbiji. Tunasahau kwamba watu wa Visiwa vya Comoro ni jirani zetu. 
Badala ya mpaka wa ardhi tunatenganishwa na Bahari ya Hindi. Inawezekana hii ikawa ndio sababu ya nchi zetu kutokuwa na ushirikiano wa karibu kiuchumi na kiutawala, pamoja na kwamba kijamii na kiutamaduni sisi, na hasa watu wa mwambao wa pwani na Zanzibar, Wacomoro wamekuwa ni sehemu yetu. Mara nyingi utasikia fulani na fulani wametutangulia mbele za haki na wamezikwa katika makaburi ya waComoro. 
 Nakiri kwamba pamoja na kusafiri sana nje ya nchi, sikuwahi kubahatika kufika nchi ya jirani ya Comoro. Hivyo basi nikiwa mstaafu, na ilhali Mwenyezi Mungu amenijalia siha njema, moja ya nchi ambazo nimeamua kutembelea ni nchi jirani, Comoro. 
 Nikiongozana na mke wangu Lucy, kijana wetu Emmanuel, tuliondoka Dar es Salaam kuelekea Moroni, mji mkuu wa Comoro, jumanne kwa njia ya anga kupitia ndege aina ya Bombadier, De Havilland Dash 200, Q400, ndege ya Shirika la ATC ambayo iliondoka kama ilivyopangwa, asubuhi saa 2 barabara. 
Muda mfupi baada ya ndege kufika usawa wa anga uliopangwa kwa safari hii, wahudumu wakatupatia, soda, kahawa au chai kwa jinsi kila msafiri alivyohitaji, vinywaji hivi vikiambatana na karanga na korosho. Hakika ndege ilijaa. Wasafiri wengi walikuwa ni wafanyabiashara wa Comoro wakitoka Dar es Salaam wakiwa na bidhaa mbali mbali. 
Hicho ni kielelezo cha jinsi ATC ilivyohodhi soko. Na kama itashindwa kuhudumia soko hili basi itakuwa ni kutokana na makosa yake na si vinginevyo.
Jengo la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Prince Said Ibrahim, Hahaya, Moroni 
Ofisini kwa Mheshimiwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro
Msikiti wa Shiounda, Bangoi-Kouni, Ngazija.

Ndani ya Msikiti wa Shiounda, Bangoi-Kouni, Ngazija.

Mtaa wa Medina, Badjanani, Moroni, Ngazija.
Picha zote na Emmanuel Mwandosya.
Kupata chanzo na kusoma
 makala kamili BOFYA HAPA


CHANGIA USHIRIKI WA JAMAFEST JIJINI KAMPALA MWEZI UJAO

TaGEDO YAPATA UGENI KUTOKA UJERUMANI, WAFANYA SHUGHULI MBALIMBALI IKIWEMO USAFI WA MAZINGIRA

$
0
0
KIGAMBONI, DAR ES SALAAM.

Vijana kutoka Chuo Cha Munister nchini Ujerumani, leo wametembelea Kituo cha Taasisi ya Kijamii ya kuelendeleza Vijana na Kinamama katika Ujasiriamali hapa nchini (TaGEDO) kilichopo Kigamboni Dar es Salaam, na kushiriki katika shughuli mbalimbali ikiwemo kusafisha mazingira.

Vijana hao zaidi ya 20 walishirikiana na vijana wenzao kutoka TaGEDO na kufanya usafi kwenye eneo la Ofisi ya Mtaa wa Kisiwani na baadaye kushiriki katika mafunzo ya ushonaji nguo kwenye mradi wa ushonaji nguo wa kituo hicho na baadaye ulifanyika mjadala wa kubadilishana uzoefu katika mafanikio na changamoto zinazokabili vijana na kinamama.

Kituo hicho cha Taasisi ya TaDEDO hadi sasa kina vijana 83 ambao kwa namna mojawapo walikosa fursa ikiwemo ya kutoendelea na masomo ambao sasa wanapatiwa mafunzo ya ujasiriamali wa kubuni na kushona nguo ambapo baadhi yao tayari ni mafundi.
Vijana wa Kituo cha ubunivu na ushonaji nguo cha Taasisi ya Kijamii ya TaGEDO, wakimwelekeza jinsi ya kutumia cherehani, kijana Astrid Naundorf kutoka Chuo Kikuu Cha Munister, wakati vijana wa Chuo hicho walipotembelea Kituo hicho, Kigamboni Dar es Salaam, leo.
Taasisi ya Kijamii ya kuelendeleza Vijana na Kinamama katika Ujasiriamali hapa nchini (TaGEDO) Venance Kalumanga akichoma taka, wakati yeye na wenzake wa Taasisi hiyo, walipoungana na Vijana kutoka Chuo Cha Munister nchini Ujerumani, kufanya usafi kwenye eneo la Ofisi ya Mtaa wa Kisiwani, Kigamboni, dar es Salaam, leo
Vijana wa TaGEDO wakishirikiana na Vijana hao kutoka Ujerumani kukusanya taka wakati wakifanya usafi kwenye ofisi ya Mtaa wa Kisiwani, Kigamboni Dar es Salaam, leo.

MBUNGE WA BUSANDA AKABIDHI VIFAA VYA OFISI KWENYE OFISI ZA CCM MKOA WA GEITA

$
0
0

Mbunge wa Jimbo la Busanda Mkoani Geita,Lolesia Bukwimba akikabidhi komputa kwenye idara ya vijana na wanawake kwenye ofisi za chama cha mapinduzi “(CCM)Mkoani Geita. 
Mbunge wa Jimbo la Busanda akikabidhi komputa kwa Katibu wa chama cha mapinduzi Wilaya ya Geita. 
Mbunge wa Busanda Lolesia Bukwimba ameeleza kuwa vifaa ambavyo amekabidhi kwenye ofisi ya CCM ni kutokana na hali ngumu ambayo walikuwa wakikutana nayo ya upungufu wa vitendea kazi kwenye Ofisi za CCM. 
Nje ya ofisi za CCM Mkoa wa Geita. 
PICHA ZOTE NA JOEL MADUKA WA MADUKA ONLINE

PROF. BRIAN VAN ARKADIE ATOA SOMO MAPINDUZI YA KILIMO MHADHARA WA ESRF

$
0
0
TAASISI ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) imefanya mhadhara mkubwa ulioshirikisha wanazuoni mbalimbali kujadili historia na nafasi ya kilimo na sera zake katika kufanikisha safari ya viwanda ya Tanzania, kwa kuangalia mazao ya chakula kama mazao ya biashara. 

 Katika mhadhara huo msemaji Mkuu alikuwa Prof. Brian Van Arkadie, majadiliano yalitanguliwa Prof Samuel Wangwe na Aloyce Hepelwa Akiwasilisha mada yake aliwataka wataalamu kubadilika katika namna ya kusaidia kuongeza tija katika kilimo na kuachana na dhana za zamani kwamba wakulima wameshindwa kubadilika na kukwamisha maendeleo. 

 Amesema katika mjadala huo wa hadhara kuhusu maendeleo ya kilimo kutoka wakati wa uhuru hadi sasa katika jengo la mikutano la ESRF mjini hapa alisema kwamba tafiti nyingi zimekuwa zikishutumu wakulima kwa kuwa na muono mdogo na kubisha mabadiliko yanayohitaji kuongeza uzalishaji. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho kwa washiriki wa mhadhara mkubwa ulioshirikisha wanazuoni mbalimbali kujadili historia na nafasi ya kilimo na sera zake katika kufanikisha safari ya viwanda ya Tanzania, kwa kuangalia mazao ya chakula kama mazao ya biashara uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Prof. Brain Van Arkadie ambaye ni msemaji mkuu wa mhadhara mkubwa ulishirikisha wanazuoni mbalimbali kujadili historia na nafasi ya kilimo na sera zake katika kufanikisha safari ya viwanda ya Tanzania, kwa kuangalia mazao ya chakula kama mazao ya biashara akiwasilisha utafiti wake katika mkutano huo ulioandaliwa na ESRF na kufanyika jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja ya washiriki wa mhadhara mkubwa ulioshirikisha wanazuoni mbalimbali kujadili historia na nafasi ya kilimo na sera zake katika kufanikisha safari ya viwanda ya Tanzania, kwa kuangalia mazao ya chakula kama mazao ya biashara ambao uliandaliwa na ESRF na kufanyika jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida akibadilishana mawazo na wageni waalikwa baada ya kumalizika kwa mhadhara huo ulioandaliwa na ESRF na kufanyika jijini Dar es Salaam.

AFISA MTENDAJI MKUU WA STANDARD CHARTERED BANK-TANZANIA, ABADILISHANA UZOEFU WA KAZI NA WAFAYAKAZI WA AIRTEL LEO

$
0
0
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel-Tanzania, Bw. Sunil Colaso, (kushoto), akibadilishana mawazo na Kaimu Mkurugenzi wa Mtandao (Network), Bw. Emmanuel Luanda, Mkurugenzi wa IT, Bw. Frank Filman, na Mkurugenzi wa Masoko, Bw.Isack Nchunda. kampuni ya Airtel ilitembelewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Standard Charted bank ili kubadilishana uzoefu katika kuhudumia wateja wao.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel-Tanzania, Bw. Sunil Colaso, (kulia), na Afisa Mtendaji Mkuu, wa Standard Chartered Bank-Tanzania, Bw. Anjay Rughani, wakizunhuzma kabla ya kuanza kwa semina hiyo. 
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel-Tanzania, Bw. Sunil Colaso, akizungumza na wafanyakazi wa kampuni hiyo wakati akimkaribisha Afisa Mtendaji Mkuu wa Standard Chartered Bank-Tanzania, Bw. Sanjay Rughani, kutoa semina ya kuhamasisha (motivation), makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam. kampuni ya Airtel ilitembelewa na Afisa Mtendaji Mkuu huyo kutoka Standard Charted Bank ili kubadilishana uzoefu katika kuhudumia wateja wao.
Afisa Mtendaji Mkuu, wa Standard Chartered Bank-Tanzania, Bw. Anjay Rughani, ambaye ni mmoja kati wa watanzania wachache wanaoshikilia nafasi hiyo ya juu kwenye taasisi za kimataifa, akizungumza wakati wa semina ya kuwahamasisha (motivation), wafanyakazi wa kampuni ya simu za mikononi, Airtel, makao makuu, jijini Dar es Salaam. 

MAGAZETI YA ALHAMIS LEO AGOSTI 24,2017

IGP SIRRO ATEUA KAIMU KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR NA KAMANDA WA KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM

$
0
0


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Nyakoro Sirro amemteua Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Juma Yusuf Ally kuwa Kaimu Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Uteuzi huo unafuatia kustaafu kwa aliyekuwa kamishna wa Polisi Zanzibar Kamishna Hamdani Omari Makame kwa mujibu wa sheria baada ya kutimiza umri wa miaka sitini (60).

Kabla ya uteuzi huo DCP Juma alikuwa ni Mkuu wa Utawala na Fedha Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.

IGP Sirro pia amemteua Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  (SACP) Lazaro Mambosasa kuwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam. Kabla ya uteuzi huo, SACP Mambosasa alikuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.

Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Kaimu Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa MtwaraKamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  (SACP) Neema Mwalimu Mwanga anakwenda Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.

IGP Sirro pia amemteua aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Gilles Bilabaye Mroto kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma na  Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Emmanuel Lukula kwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke.

Kabla ya uteuzi huo, ACP Lukula alikuwa Afisa Mnadhimu wa Polisi mkoa wa Mbeya.

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wote kuendela kushirikiana na Jeshi hilo kwa kufichua taarifa za uhalifu na wahalifu ili kwa pamoja tuendelee kuiweka Tanzania salama.


Imetolewa na:
Barnabas David Mwakalukwa - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi.
S.L.P 9141
Dar es Salaam



WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ATEMBELEA TAASISI YA MAFUNZO YA UANASHERIA KWA VITENDO TANZANIA (LAW SCHOOL OF TANZANIA

$
0
0


Na Scholastica Njozi – Law School of Tanzania


Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi amewataka watumishi wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School) kutambua kuwa wamebeba dhamana kubwa kwa Taifa. 


Waziri Kabudi ametoa wito huo leo alipotembelea Taasisi hiyo wakati akiwa katika ziara ya kutembela taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo ili kujionea  namna Taasisi hiyo inavyotoa mafunzo.


“Nataka niwahakikishie kuwa mmebeba jukumu kubwa sana kwa Taifa hivyo mnapotekeleza majukumu yenu zingatieni sana kuhakikisha wahitimu wanakuwa na maadili, wasiopenda rushwa na kubwa zaidi watambue wanakwenda kuwatumikia watanzania maskini”, alisema Mhe. Waziri.”  Prof. Kabudi aliongozana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Amon Mpanju.


Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Taasisi Dkt. Zakayo Lukumay, amesema watahakikisha wahitimu wote wanakuwa na uzalendo kwa nchi yao kwa kupitia mafunzo wanayoyapata. 

Prof. Palamagamba Kabudi mwenye tai nyekundu akiwa na viongozi wa Taasisi alipotembelea majengo.
Prof. Palamagamba Kabudi, akimsaidia mwanafunzi  Bi. Jesca Mbawala namna ya kutafuta vitabu kupitia mtandao, alipotembelea maktaba ya Taasisi.

Waziri wa Katiba na Sheria, Prof.Palamagamba Kabudi akitia saini kitabu cha wageni


Mpangokazi wa kitaifa wa Haki za Binadamu katika biashara mbioni kukamilishwa

$
0
0
Na MbarakaKambona,

Wadau wa haki za binadamu kutoka taasisi mbalimbali zikiwemo za serikali, taasisi binafsi na wafanyabiashara wamekuta na kupitia rasimu ya kwanza ya mapendekezo ya Mpangokazi wa kitaifa wa Haki za Binadamu katika biashara.

Wadau hao walikutana Agosti 23, 2017 katika kikao kilichofanyika katika ofisi zaTume ya Haki za Binadamu jijini Dar es Salaam kujadili rasimu hiyo kufuatia utafiti uliofanywa na wataalamu na maoni yaliyokusanywa kutoka katika maeneo mbalimbali ya biashara.

Akizungumza wakati wa kufungua mkutano huo, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora,Mhe.Iddi Ramadhani Mapuri alisema kuwa kuanzishwa kwa mpango huo kumelenga katika kuhakikisha kuwa mifumo yote ya kitaifa na kimataifa ya sera na sheria inazingatia na ulinzi na utetezi haki za binadamu wakati wote wa utekelezaji wa majukumu ya kibiashara na kuweka mifumo ya utatuzi wa migogoro ya waathirika pale itakapojitokeza.

Utafiti huo ambao ulifanyika Mei, 2017 ulihusisha wadau mbalimbali wakiongozwa na Tume, zikiwemo taasisi za serikali, taasisi binafsi, wafanyabiashara na wananchi ulifanyika katika maeneo maalum yaliyochaguliwa ikiwemo maeneo ya kilimo katika Mkoa wa Mbeya- Mbarali, Maeneo ya viwanda Mkoani Dodoma na Singida na maeneo yaUtalii upande wa Zanzibar uliofanyika.

Utafiti huo unafuatia tamko la Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lilitolewa mwaka 2011 linalotaka nchi wanachama kuanzisha Mpangokazi wa kitaifa wa Haki za Binadamu katika maeneo ya biashara ili kutoa muongozo wa kulinda uvunjifu wa haki za binadamu katika maeneo hayo.

 Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mhe.Iddi Ramadhani Mapuri akiongea na washiriki wa kikao cha wadau wa haki za binadamu wakati akifungua mkutano huo uliofanyika katika ofisi za Tume zilizopo  jijini Dar es Salaam Agosti 23, 2017. Kulia kwake ni Kamishna Mkaazi wa Tume Zanzibar, Mhe. Mohamed Hassan na Kushoto kwake ni  Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Bwn. Francis Nzuki
 Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Bwn. Francis Nzuki akiongea katika kikao cha wadau wa haki za binadamu mara baada ya Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mhe.Iddi Ramadhani Mapuri (katikati) kufungua rasmi mkutano huo.
 Mmoja wa watoa mada ya haki za binadamu na biashara, Bi. Nora Gotzmann akiwasilisha mada yake iliyohusu masuala ya Biashara na Haki za Binadamu, jinsi ya kulinda, kuheshimu na namna ya kupata utatuzi wa migogoro inapojitokeza.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

Taarifa Kwa Umma Matokeo Ya Uchaguzi Wa Wanafunzi Wa Kidato Cha Tano Awamu Ya Pili

MAKAMBA AFUNGUA KONGAMANO LA NNE LA DIASPORA ZANZIBAR

$
0
0
Na Mathias Canal, Zanzibar

Kongamano la nne la Watanzania waishio ughaibuni (4th Tanzania Diaspora Conference) limefunguliwa jana tarehe 4 Agosti 2017 kwa kuwashirikisha washiriki wapatao 350, ambapo miongoni mwao wanadiaspora wamehudhuria zaidi ya 200 na watendaji kutoka taasisi za Serikali zote mbili wakiwa ni 150.

Diaspora wametakiwa kutumia fursa mbalimbali za uwekezaji nchini katika sekta ya kuimarisha na kuanzisha viwanda ili kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa dhamira yake ya kuifanyaTanzania kuwa nchi ya viwanda.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania anayeshughulikia Mazingira Mhe Januari Makamba (MB)  alipomuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia suluhu Hassan akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano la nne la watanzania waishio nje ya nchi litakalodumu kwa siku mbili Agosti 23 na 24, 2017 katika ukumbi wa Sea Cliff Hotel uliopo katika kijiji cha Kama Wilaya ya Magharibi A.

Mhe Makamba alisema kuwa kwa sasa Demokrasia imeimarika nchini kutokana na serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama kukubaliana kwa kauli moja kuimarisha usalama wa wananchi ili kurahisisha uimara wa uwajibikaji wa ujenzi wa Taifa.

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania anayeshughulikia Mazingira Mhe Januari Makamba MB) akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano la nne la watanzania waishio nje ya nchi lililofanyika jana Agosti 23, 2017 Sea Cliff Hotel Mjini zanzibar.

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania anayeshughulikia Mazingira Mhe Januari Makamba MB) akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano la nne la watanzania waishio nje ya nchi lililofanyika jana Agosti 23, 2017 Sea Cliff Hotel Mjini zanzibar
Baadhi Washiriki wa Kongamano la nne la Watanzania waishio ughaibuni (4th Tanzania Diaspora Conference) wakifatilia Mjadala wa ufunguzi wa kongamano hilo
Mkurugenzi Mpya wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Ndg Geofrey Mwambe akizungumza wakati wa Kongamano la nne la watanzania waishio ughaibuni linalofanyika Sea Cleaf Hotel Mjini Zanzibar

Washiriki wa Kongamano la nne la watanzania waishio Ughaibuni (Diaspora) wakitembelea shamba la BIG BODY SPICE kujionea kilimo cha mazao ya viuongo
Washiriki wa Kongamano la nne la watanzania waishio Ughaibuni (Diaspora) wakisikiliza kwa makini maelezo kuhusu kilimo cha mazao ya viuongo mara baada ya kutembelea shamba la BIG BODY SPICE

Washiriki wa Kongamano la nne la watanzania waishio Ughaibuni (Diaspora) wakisikiliza kwa makini maelezo kuhusu kilimo cha mazao ya viuongo mara baada ya kutembelea shamba la BIG BODY SPICE


WIZARA YA AFYA NA MSD WASAINI MKATABA NA KAMPUNI YA ZIPLINE KWAAJILI YA KUSAMBAZA DAWA KWA DRONE

$
0
0
WIZARA  ya afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto na Bohari ya Dawa Tanzania(MSD) wamesaini mkataba wa makubaliano na kampuni ya Zipline jijini Dar es Salaam leo kwaajili ya kuanza kujenga vituo vya kurushia Drone za kusafirishia dawa kataka maeneo mbalimbali hapa nchini wakianzia na Mkoa wa Dodoma na Mwanza.

 akizungumza wakati wa kusaini na kubadilishana mikataba ya makubaliano, Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa  mradi huo umekuja wakati muafaka kutokana na ukuaji wa Teknolojia Bohari ya Dawa Tazania itapata urahisi wa kusambaza zawa katika vituo mbalimbali vya Afya.

Amesema kuwa  kwa kuanza mradi huo utaanza kwa kusambaza dawa ambazo zinaubaridi kama Damu katika vituo 200 vya mkoa wa Dodoma ambapo baada ya hapo watandelea na mikoa ya Kanda ya ziwa na baadae nchi nzima.

 Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zipline, Keller Rinaudo,amesema kuwa Mradi huo umefanikiwa kwa kiasi kikubwa nchini Rwanda na hapa nchini utaenda vyema zaidi pia amesema kuwa utatoa ajira nyingi kwa vijana wa kitanzania ambao watakuwa na mawazo mazuri ya ubunifu kwaajili ya kuendeleza kuenea mradi huo hapa nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt. Mpoki Ulisubisya, Mkurugenzi Mkuu Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zipline, Keller Rinaudo wakisaini mkataba wa kuanza kujenga vituo vya kurushia Drone zitakazo kuwa zikisafirisha dawa kwenye maeneo ambayo hayafikiki kwa urahisi. Kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Bakari Kambi.
Mkurugenzi Mkuu Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu wakibadilishana mkataba wa makubaliano na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zipline, Keller Rinaudo wakibadilishana kwaajili ya kuanza kujenga vituo vya kurushia drone zitakazo kuwa zikisafirisha dawa katika maeneo mbalimbali ya nchi. Ktikati ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya akisuhudia wanavyobadilishana mikataba hiyo jijini Dar es Salaam leo.

.
  
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya akizungumza wakati wa kusaini Mkataba kati ya wizara ya Afya, Bohari ya Dawa Taznania(MSD) na Kampuni ya Zipline kwaajili ya kuanza kufanya utafiti wa maeneo yatakayojengwa kwaajili ya sehemu ambapo Kampuni ya Zipline itakuwa ikirushia vifaa maalum ambazo ni Drone zitatumika kusambaza dawa katika mikoa maeneo ambayo ni ngumu kufikika kwa urahisi kutokana na umbali wake.
 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zipline, Keller Rinaudo, akizungumza wakati wa kusaini Mkataba wa Makubaliano kuanza kujenga vituo kwaajili ya kurushia Drone ambazo zitakuwa zikisafirisa dawa kwenye maeneo ambayo hayafikiki kwa urahisi ikiwa mradi huo utaanza katika mikoa ya Dodoma na Mwanza. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu na Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya.

MKAZI WA LINDI ALAMBA KITITA CHA ZAIDI YA MIL 118/- M-BET

$
0
0
 Mshindi wa kitita cha zaidi ya shilingi milioni wa zaidi 118/- Erick Matey ambaye ni mkazi wa mkoa wa Lindi,akiwa ameshikilia hundi yake mara baada ya kukabidhiwa rasmi leo wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi mshindi hiyo aliyojishindia  kupitia mchezo wa kubahatisha Supper 12 unaoendeshwa na M-bet.

 Kaimu Mkurugenzi wa  Uendeshaji na Sheria wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, James Mbalwe(kulia) na Afisa habari wa M-BET,David Malley(katikati)wakimsikiliza mshindi waM-BET aliyejishindia zaidi ya shilingi milioni  118/- Erick Matey,Ambaye ni mkazi wa mkoa wa Lindi,Wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi mshindi huyo hundi yake aliyojishindia  kupitia mchezo wa kubahatisha Supper 12 unaoendeshwa na M-bet.
 Mshindi wa kitita cha zaidi ya shilingi milioni wa zaidi 118/- Erick Matey ambaye ni mkazi wa mkoa wa Lindi(kushoto)akiwaonesha hundi yake waandishi wa habari(hawapo pichani) Wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi mshindi hiyo aliyojishindia  kupitia mchezo wa kubahatisha Supper 12 unaoendeshwa na M-bet,Wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa  Uendeshaji na Sheria wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, James Mbalwe na Afisa habari wa M-BET,David Malley.
Na Mwandishi wetu
MKAZI wa mkoa wa Lindi Mjini, Erick Matey mwenye umri wa miaka 26 ameibuka mshindi baada ya kubashiri vyema matokeo ya mechi kupitia Kampuni ya m-Bet na kujishindia zaidi ya Shilingi Milioni 118/-.

Matey amekabidhiwa fedha zake leo katika hafla  fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana

Kwa upande wake, Afisa habari wa  M-Bet, David Malley alisema kuwa Matey alifanikiwa kuzoa kitita hicho baada ya kufanikiwa kutabiri matokeo ya mechi 12 za ligi ya Ulaya kwa mtindo wa kucheza kawaida yaani super 12.

“Tunafarijika kumkabidhi Matey kitita hicho cha aidi ya Sh milioni 118/- akiwa ndiye mshindi wa m-Bet ambapo atapata Sh milioni 97/- baada ya makato ya kodi,” alisema Malley.

Aliwataka watanzania kuchangamkia kutumia mtandao wa intaneti kuonyesha ushabiki halisi wa soka akisema kuwa Perfect 12 ni mchezo wa ziada unaoruhusu kutabiri mechi 12 kwa Tsh 1,000 tu ambapo ukipatia zote  unaondoka na kitita chako mchana kweupe.

PROF. ELISANTE OLE-GABRIEL AFUNGUA MKUTANO WA MASUALA YA UTAMADUNI-UDSM.

$
0
0
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Elisante Ole-Gabriel akiongea na wadau wa masuala ya utamaduni toka baadhi ya nchi za Afrika Mashariki wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa siku tatu unaohusu kujadili mambo ya utamaduni baina ya nchi hizo unaofanyika katika Ukumbi wa Nkrumah uliopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Cuthbert Kimambo akiongea na wadau wa masuala ya utamaduni toka baadhi ya nchi za Afrika Mashariki wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa siku tatu unaohusu kujadili mambo ya utamaduni baina ya nchi hizo unaofanyika katika Ukumbi wa Nkrumah uliopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

 Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa masuala ya Utamaduni unaofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) katika Ukumbi wa Nkrumah wakifuatilia hotuba toka kwa mgeni rasmi pamoja na Viongozi wengine wa Chuoni hapo wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa siku tatu unaohusu kujadili mambo ya utamaduni baina ya nchi za Afrika Mashariki.

 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Elisante Ole-Gabriel akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa siku tatu unaohusu kujadili mambo ya Utamaduni baina ya nchi za Afrika Mashariki unaofanyika katika Ukumbi wa Nkrumah uliopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 

(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM)

WAZIRI KAIRUKI AZINDUA MPANGO WA ELIMU YA RUSHWA KUTUMIA MABASI YA UDART LEO.

$
0
0
Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais MeneJementi ya Utumishi wa Umma na Uongozi Bora, Angelah Kairuki akikata utepe kuashiria uznduzi wa mpango elimu ya ruswa utakaornezwa na mabasi takribani 60 ya UDART. Pmoja naye ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando na viongozi mbalimbali. 
Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menegementi ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angelah Kairuki akimshukuru Msanii Mrisho Mpoto kwa kazi nzuri ya kufikisha ujumbe kwa jamii katika hafla ya uzinduzi huo. 
Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menegementi ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angelah Kairuki akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa meza kuu pamoja na viongozi mbalimbali.
(Imeandaliwa na Robert Okanda Blogspot)

IGP SIRRO AWASILI MKOANI TANGA KWA ZIARA YA KIKAZI

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro, akipokea salamu ya heshima ya kijeshi baada ya kuwasili mkoani Tanga, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo, IGP Sirro amewataka askari kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia sheria na taratibu za nchi.

 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro, akikagua kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) baada ya kuwasili mkoani Tanga, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo na kuwataka kufanyakazi kwa weledi na kwa kuzingatia sheria na taratibu za nchi.

 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro (kushoto), akipokea taarifa kutoka kwa kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, SACP Benedict Wakulyamba (aliyesimama), mara alipowasili katika mkoa huo kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo ili kujua changamoto wanazokutananazo wakati wakitekeleza majukumu yao ya kazi za Kipolisi
Picha na Jeshi la Polisi.
Viewing all 110135 articles
Browse latest View live




Latest Images