Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live

MBUNGE WA TANGA MUSSA MBARUKU ATEMBELEA KITUO CHA TV CHA TANGA

0
0
 Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku akisaini kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika kituo cha Television cha Jiji la Tanga (Tanga TV) akiwa na wajumbe wa kamati ya Mfuko wa Jimbo kuangalia fedha za mfuko wa Jimbo zilivyotumika kulia ni Meneja wa kituo hicho,Mussa Labani
 Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku kulia akimsikiliza Afisa Mipango na Uchumi wa Jiji la Tanga ambaye pia ni Katibu wa Mfuko wa Jimbo,Ramadhani Possi mara baada ya kusaini kitabu hicho
 Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku akiwa na wajumbe wa kamati hiyo wakiorodhesha baadhi ya vitu wakati wa ziara hiyo
 Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku katika akimsikiliza Meneja wa kituo hicho,Mussa Labani kushoto
 Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku wa pili kutoka kushoro akipewa maelekezo na Meneja wa Kituo cha Tanga TV Mussa Labani
 Afisa Mipango na Uchumi wa Jiji la Tanga ambaye pia ni Katibu wa Mfuko wa Jimbo,Ramadhani Possi wa pili kutoka kushoto akimuonesha jambo  Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku

DC IKUNGI AONGOZA UZINDUZI WA ALBAMU YA INJILI YA MWIMBAJI ELINEHEMA BABU

0
0
Katika uzinduzi huo, Mhe.Mtaturu ameendesha zoezi la uuzaji wa albamu hiyo iitwayo TARATIBU NITAFIKA na kusaidia upatikanaji wa zaidi ya shilingi Milioni Tatu ikiwa ni fedha taslimu pamoja na ahadi.

Mhe.Mtaturu amewahimiza waimbaji wa nyimbo za injili wilayani humo kutumia vyema fursa waliyonayo kwa kuimba nyimbo zenye kuhamasisha amani na upendo nchini, akitolea mfano kwaya ya AIC Makongoro ya Jijini Mwanza iliyoimba wimbo uitwao AMANI kwa ajili ya kuhamasisha amani nchini.

Mwimbaji Elineema Babu ameachia albabu ya tatu iitwayo "Taratibu Nitafika" yenye nyimbo nane ambapo amewasihi wadau wengine kumsaidia kwa kununua albamu hiyo (Audio) ili aweze kupata shilingi Milioni Sita zinazohitaji ili aweze kurekodi video ya albamu hiyo. Taratibu Nitafika ni albamu ya tatu baada ya kutanguliwa na albamu mbili ambazo ni Nitumie pamoja na Fanya Kazi ya Bwana.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Mhe.Miraji Mtaturu (wa tatu waliokaa), leo Agosti 20,2017 ameongoza uzinduzi wa albamu ya injili ya mwimbaji Elineeema Babu (wa tatu kushoto) uliofanyika kwenye uwanja wa Stendi Mpya ya Ikungi.
Mwimbaji Elirehema Babu akitumbuiza kwenye uzinduzi huo hii leo
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida Mhe.Miraji Mtaturu akizungumza kwenye uzinduzi huo ambapo alikuwa mgeni rasmi

Ujenzi wa Tazara Flyover Wakamilika kwa Asilimia 53

0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa. Makame Mbarawa akimuelezea jambo Rais wa Shirika la Maendeleo Kimataifa la Japan (JICA) Dkt. Shinichi Kitaoka (kushoto) alipotembelea kukagua maendeleo ujenzi wa Barabara ya Juu (Tazara Flyover) inayoendelea kujengwa katika eneo la Tazara Jijini Dar es Salaam leo.
Rais wa Shirika la Maendeleo Kimataifa la Japan (JICA) Dkt. Shinichi Kitaoka akimuelezea jambo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia) alipotembelea kukagua maendeleo ujenzi wa Barabara ya Juu (Tazara Flyover) inayoendelea kujengwa katika eneo la Tazara Jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa. Makame Mbarawa akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa wataalamu wa Kampuni ya Ujenzi ya Sumitomo Mitsui wakati wa ziara ya Rais wa Shirika la Maendeleo Kimataifa la Japan (JICA) Dkt. Shinichi Kitaoka (watatu kushoto) alipotembelea kukagua maendeleo ujenzi wa Barabara ya Juu (Tazara Flyover) inayoendelea kujengwa katika eneo la Tazara Jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa. Makame Mbarawa akitazama mchoro wa mradi wa ujenzi wa Barabara ya Juu (Tazara Flyover) wakati wa ziara ya Rais wa Shirika la Maendeleo Kimataifa la Japan (JICA) Dkt. Shinichi Kitaoka (kushoto kwake) alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni mmoja wa wataalamu wa Kampuni ya Ujenzi ya Sumitomo Mitsui ambayo ndiyo mkandarasi wa mradi huo
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa na Rais wa Shirika la Maendeleo Kimataifa la Japan (JICA) Dkt. Shinichi Kitaoka wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa TANROADS, na wataalamu wa Ujenzi mara baada ya kumaliza ziara ya kukagua maendeleo ujenzi wa Barabara ya Juu (Tazara Flyover) inayoendelea kujengwa katika eneo la Tazara Jijini Dar es Salaam leo.
Muonekano wa Juu na Pembeni mwa bararaba ya Juu (Tazara Flyover) ambao ujenzi wake umekamiklika kwa asilimia 53 na unatarajiwa kukamilika mapema mwezi wa kumi mwakani.

Picha na: Idara ya Habari – MAELEZO

WANACHAMA wa Coastal Union ya Tanga waazimia kurudisha umoja kwenye klabu ili kuhakikisha timu hiyo inarejea Ligi Kuu Tanzania Bara.

0
0
WANACHAMA wa Coastal Union ya Tanga wameazimia kurudisha umoja kwenye klabu ili kuhakikisha timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza inarejea Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Akzungumza na mwandishi wetu baada ya kuisha mkutano wa wanachama kutoka Tanga, msemaji wa klabu hiyo maarufu Wagosi wa Kaya, Hafidh Kido alisema kwa mipango iliyokuwepo hakuna sababu ya kuifanya timu hiyo kongwe nchini kushindwa kurejea ligi kuu msimu ujao.

“Mkutano ulikuwa na ajenda nyingi lakini kubwa ilikuwa ni kuleta umoja na kubainisha mikakati ya kushiriki vema ligi daraja la kwanza msimu huu.
“Tumefanya usajili wa nguvu, wachezaji wengi waliokuwa wakishiriki ligi kuu msimu uliopita tumewanaka na tayari wamesharipoti kambini,” alisema Hafidh Kido na kuongeza:

“Hii ni Coastal Union mpya, wapenzi na wanachama wote uliokuwa ukiwajua wamerejea kwa ajili ya kuongeza nguvu. Sasa hivi Coastal Union ni wali ng’ombe hakuna njaa.”

Kwa upande wake Mwenyekiti Kamati ya Usajili na Mashindano, Hemed Hilal ‘Aurora’ alisema; “Makundi ndiyo yaliyoidhoofisha Coastal Union lakini leo nathibitisha wazi makund yamekufa na Coastal Union ni moja.”
Alisisitiza kuwa kila mmoja atimize wajibu wake ili msimu huu mambo yanyooke na Coastal Union irudi mahali panapostahili kwa sababu kushiriki ligi daraja la kwanza si hadhi yao.

MKUTANO WA 37 WA SADC WAMALIZIKA MJINI PRETORIA

0
0
Mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC umemalizika leo tarehe 20 Agosti 2017 katika mji wa Pretoria Afrika Kusini ambapo Wakuu wa nchi na Serikali wa SADC kwa kauli moja wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti aliyemaliza muda wake katika Asasi ya Ushirikiano wa siasa , Ulinzi na Usalama Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kazi nzuri aliyoifanya katika kipindi cha uongozi wake akiwa Mwenyekiti wa Asasi hiyo. 

Tanzania imemaliza kipindi chake cha Uenyekiti wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama tarehe 19 Agosti, 2017 wakati wa Mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa nchi wanachama wa SADC ambao umefanyikia hapa Pretoria, Afrika Kusini kuanzia tarehe 19 na 20 Agosti, 2017. 

Akizungumzia mambo muhimu yaliyojadiliwa katika mkutano huo wa 37 wa SADC, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema pamoja na mambo mengine SADC imetambua na kuthamini mchango wa Tanzania katika kipindi cha Uongozi wa Asasi ya Saisa , Ulinzi na Usalama iliyokuwa chini ya Rais Dkt. John Pombe magufuli. 
Makamau wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka saini moja ya makubaliano katika mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Kusini mwa Afrika wakati wa kuhitimishwa kwa mkutano huo mjini Pretoria. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Dkt. Stergomena Tax akila kiapo mara baada ya kuteuliwa kuwa Katibu Mtendaji wa SADC .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais 
Makamau wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka saini moja ya makubaliano katika mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Kusini mwa Afrika wakati wa kuhitimishwa kwa mkutano huo mjini Pretoria. 
Dkt. Stergomena Tax mara baada ya kuteuliwa na kula kiapo kuwa Katibu Mtendaji wa SADC .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais 
.



UTAFITI WA KUGEMA UTOMVU WA KUTENGENEZEA BAZOKA (CHEWING GUM) PAMOJA NA GEL WAANZA KATIKA SHAMBA LA MITI LA SAO HILL

0
0

Shamba la miti la Sao Hill likishirikiana na Kampuni ya Art International limeanza utafiti wa kugema utomvu wa miti ya msindano kama njia ya kujiongezea kipato.

Akizungumza na Kamati ya Bunge ya Maliasili na Mabadiliko ya tabia ya nchi ya nchini Malawi iliyotembelea Shamba la Miti la Sao Hill, Meneja wa Shamba hilo Salehe Beleko amesema katika kuongeza vyanzo vya mapato wameingia mkataba na kampuni hiyo kufanya utafiti na ikibainika kwamba haitaathiri ukuaji wala ubora wa miti wataidhinisha kuwa chanzo kipya cha mapato.

Akifafanua Salehe Baleko amesema wanatarajia kuuza kila kilo moja ya utomvu kwas h. 750. Beleko amesema kwa kuwa ni utafiti wameanza kwanza na miti iliyokuwa tayari kuvunwa wakiona hakuna madhara wataendelea kwenye miti michache yenye umri mdogo na matokeo ya utafiti huo yatapelekea ama kukuza ama kukataza kabisa zoezi hilo.

Naye mtaalamu wa kampuni ya uchina, Yhoung Zhoung amesema taasisi yake imefuata taratibu zote za ugemaji na usafirishaji wa utomvu huo na amefafanua kwamba kampuni yake inahitaji miti millioni mbili kwa mwaka ilikupata ujazo wa utomvu wanauhitaji

Akijibu swali la mke wa Rais wa zamani wa Malawi, Patricia Muluzi ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo ambaye alitaka kujua matumizi ya utomvu huo mtaalamu huyo amesema baada ya kuchakatwa na kuchanganywa na kemikali mbalimbali utomvu huo hutumika kutengenezea dawa mbalimbali bazoka (chewing gum) pamoja na gel

Mjumbe wa Kmaati hiyo, Rashid Pemba Msusa, amesema kwa mara ya kwanza wameshuhudia matumizi mapya kabisa ya zao la mti teknolojia ambayo hawajawahi kuiona nchini kwao Malawi. Hata hivyo ameahidi kufuatilia matokeo ya utafiti huo ili ukifaa wauhamishie Malawi.
Mti aina ya msindano ambao umegemwa utomvu katika Shamba la miti la Sao Hill lililoko Mufindi mkoani Iringa ikiwa ni utafiti unaofanywa na Kampuni ya Art International kwa kushirikiana na shamba hilo ikiwa ni njia ya kujiongezea kipato.
Meneja wa Shamba la miti la Sao Hill, Salehe Baleko akikinga utomvu unaotoka katika mti wa msindano ambao baada ya kugemwa huchakatwa na kuchanganywa na kemikali mbalimbali ambao hutumika kutengenezea dawa mbalimbali ikiwemo bazoka (chewing gum) pamoja na gel. (Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii) 
Mtaalamu wa Kampuni ya Art International, Zhoung Yhoung akitoa maelezo kuhusu zoezi la ugemaji wa utomvu kwa ujumla unaofanywa na kampuni yake (Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii) 

Daily News-Habari leo: Simba SC: Mabadiliko ya Muundo 20/08/2017

MAKONDA ALIONGEZEA NGUVU SHIRIKA LA UTANGAZAJI TBC

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo ametoa msaada wa Gari aina ya Noah, Pikipiki Tatu, Computer Tano na Camera Mbili za kisasa kwa Shirika la Utangazaji Tanzania TBC ili kuongeza nguvu katika kuwafikia Wananchi.

Mbali na Vifaa hivyo vya kisasa pia Makonda amefanikiwa kumpata mfadhili atakaepaka Rangi Jengo lote la TBC kuanzia siku ya kesho ili liwe na mwonekano wa kisasa.

Akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo MAKONDA amesema lengo ni kuwawezesha Wananchi ambao hawana uwezo wa kuita vyombo vya habari na kueleza matatizo yao waweze kufikiwa.

Makonda ametoa msaada huo baada ya kufika Ofisi za TBC na kubaini uwepo wa changamoto za vifaa ikiwemo Usafiri, Camera na Computer ambapo kwa sasa Gari na Pikipiki hizo zitawawezesha Waandishi kufika kwenye matukio kwa uharaka huku*Compute* zikimuwezesha  Mhariri kutekeleza majukumu yake.

Vifaa hivyo vitatumika kuongeza nguvu kwenye kipindi cha Hadubini ambacho kimekuwa kikisaidia Wananchi wanyonge kupaza sauti zao.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa TBC  Bi. MARTHA SWAI amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwapatia msaada huo kuku Zaitun Mkwama ambae ni mtayarishaji wa kipindi cha Hadubini akieleza kuwa vifaa hivyo vitawaongezea ufanisi katika kazi yao.
NOA1
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akikabidhi msaada wa Gari aina ya Noah, Pikipiki Tatu, Computer Tano na Camera Mbili za kisasa kwa Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania  TBC  Bi. MARTHA SWAI . 
NOA2
Hizi ni Pikipiki tatu zilizokabidhiwa kwa TBC ikiwa ni miongozi mwa vifaa vilivyotolewa na Mkuu wa Mkoa huyo kwa Shirika hilo.

MAGAZETI YA JUMATATU LEO AGOSTI 21,2017

Standard Chartered Bank to pay 50bn/- for IPTL’s case

0
0
By our Correspondent

THE Independent Power Tanzania Limited (IPTL) and Pan African Power Solutions (T) Limited (PAP) have moved the High Court (Commercial Division) to order Standard Chartered Bank Hong Kong Limited and Standard Chartered Bank Malaysia Berhard to pay about 50bn/-as security for costs.
 
In an application lodged before the Dar es Salaam Court recently, the two local companies are seeking such orders for payments of 22,880,006 US dollars, pending determination of proceedings challenging enforcement a foreign judgment for payments of about 400bn/- in favour of the two banks.

Judge Barke Sahel will hear the application that has been filed under certificate of urgency on October 10th this year. The application has been supported by seasoned Advocate Joseph Makandege, who is also the Company Secretary and Chief Counsel of IPTL and PAP.

In the affidavit to support the application, Mr. Makandege, currently the Acting Executive Chairman and Managing Director of IPTL and PAP, states that the two banks, who are respondents, are corporate citizens of and domiciled in Hong Kong in the Peoples’ Republic of China and Malaysia, respectively.

“None of them is registered in the country or own any property, let alone an immovable property, or asset or has a known registered establishment in Tanzania, within the local limits of the jurisdiction of this court,” reads part of the affidavit.

He stated that as of to date none of principal officers of the respondent banks has signed or verified any document or pleading, be it in proceedings for enforcement of the impugned judgment or counter affidavits filed in opposition to the applicants proceedings to set aside registration of such judgment.

UVCCM MKOANI SINGIDA WAMPONGEZA DC IKUNGI

0
0
Umoja wa Chama cha Mapinduzi UVCCM mkoani Singida umempongeza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mkoani humo Mhe.Miraji Mtaturu kwa kuanzisha michuano ya Ikungi Elimu Cup 2017 ili kuhamasisha wananchi na wadau mbalimbali kuchangia utatuzi wa changamoto za elimu kupitia Mfuko wa Elimu Ikungi.

Mwenyekiti wa UVCCM mkoani Singida, Jimson Mhagama (pichani) alitoa pongezi hizo jana Agosti 19,2017 kwenye uzinduzi wa michuano hiyo uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya sekondari Ikungi mkoani Singida ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Tawala mkoani Singida, Dkt.Angeline Lutambi aliyemwakilisha Mkuu wa mkoa huo Dkt.Rehema Nchimbi.

Uzinduzi wa michuano hiyo, ulikwenda sambamba na uzinduzi wa zoezi la ufyatuaji wa matofali kwa ajili ya ujenzi wa maabara uliokwama tangu mwaka 2009 katika shule ya sekondari Ikungi hii ikiwa ni uzinduzi rasmi wa zoezi kama hilo kwenye kata zote wilayani Ikungi ambapo kila Kata imepewa jukumu la kufyatua matofali elfu kumi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na nyumba za waalimu.

Katika zoezi hilo, walijitokeza wadau pamoja na viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani, wenyeviti wa halmashauri, jeshi la polisi, Tanesco na wanachi ambao walimuunga mkono Mkuu wa wilaya ya Ikungi, Mhe.Mtaturu aliyekabidhi mifuko 100 ya simenti na wao wakachangia fedha taslimu zaidi ya shilingi 800,000 na ahadi zaidi ya shilingi 1,900,000, ahadi za simenti mifuko 194 na mchanga wa moramu malori matano kutoka kwa mdau wa maendeleo wilayani Ikungi Hussein Sungita.

HAKIMU MAKETE: ACHENI KUWALAUMU POLISI WANAPOTOA DHAMANA KWA WATUHUMIWA

0
0
Na Edwin Moshi

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Makete Mjini ameitaka jamii kuacha kutupa lawama kwa polisi ama Mahakama pale Mtuhumiwa anapoachiwa kwa dhamana

Ameyasema hayo hivi karibuni katia kikao Maalum cha timu ya ulinzi na usalama wa Mtoto kilichoketi katika Ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete kujadili mambo mbalimbali Kuhusu Watoto

"Kama kuna mahali unapoona huridhiki na kupewa dhamana mtuhumiwa, nenda polisi ukaulize, na kama ni mahakamani nenda mahakamani ukaulize na sio kuwalaumu polisi au mahakama mitaani" amesema hakimu huyo

Zaidi Tazama video hii hapa chini:-

CHAMA CHA ADC CHASHEREHEKEA KUTIMIZA MIAKA MITANO TANGU KUANZISHWA KWAKE

0
0

Siku ya jana Chama Cha Alliance for Democratic Change (ADC) chenye kaulimbiu ya Dira ya Mabadiliko kimetimiza miaka mitano tangu kupata usajili rasmi 22 Agosti 2012.
Akizungumza katika maadhimisho ya Chama hicho Mwenyekiti wa chama hicho Hamad Rashid ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, ametoa wito kwa vyama vya siasa kuiga mfano wa ADC ambao wamekuwa wakimaliza migogoro yao kwa njia ya mazungumzo kwa kipindi hicho cha miaka mitano tofauti na vifanyavyo vyama vingine.

Mwenyekiti Hamad Rashid ameuzungumzia mgogoro unaoendelea ndani ya Chama cha CUF na kueleza kuwa hatua waliyofikia ya kupelekana mahakami siyo sahihi kwani itazidi kuchochea mgogoro huo.
"Mahakama kazi yake ni kuhukumu mmoja lazima akose na mwingine lazima apate kutokana na hukumu, ni vyema viongozi wawili wanaoonekana kutajwa katika mgogoro huo Profesa Lipumba na Maalim Seif kukaa katika meza moja ya majadiliano na kuutatua mgogoro huo" Alisema Hamad Rashid.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RC TABORA KUWAKABA KOO VIONGOZI WA SACCOS WANAOKULA FEDHA ZA WANACHAMA.

0
0
Na Tiganya Vincent-RS –TABORA

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imeiagiza Maafiza kuhakikisha wafanya ukaguzi katika Vyama vya Ushirika Vya Kuweka na Kukopa (SACCOS) ili kuridhisha kama fedha walizoweka wanachama zipo au hazipo iweze kuwachukulia hatua kali.

Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri katika nyakati tofauti alipokuwa akiongea na wajumbe Jukwaa la Ushirika na wakati wa Sherehe ya kuwaaga walimu walistaafu kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma.

Alisema kuwa amelazimika kuchukua hatua hiyo baada ya kupata malalamiko kutoka kwa watumishi wakiwemo walimu kuwa wamekuwa wakiweka fedha katika SACCOS kama sehemu ya kujiwekea akiba lakini wanapohitaji kukopa wanaambiwa fedha hazipo.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora alisisitiza Mtu atakayebainika kula fedha za wanachama wa SACCOS hajiandae kufikishwa katika vyombo vya Sheria ili kujibu masharti.

“Niwaagiza Maafisa Ushirika waende wakakague SACCOS zote…haiwezekani Serikali ifikishwe hapo na ibaki kimya”alisisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

“Ukaguzi huo ni pamoja na kuangalia Viongozi waliopo katika SACCOS wamekopa kiasi gani na wanalipa kwa mfumo gani isije ikiwa wanaonufaika ni viongozi tu” aliongeza Mwanri.

Aliongeza kuwa baada ya ukaguzi huo Ofisi yake itayafanyia kazi ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua mbalimbali wale wote watakaonekana kutumia vibaya madaraka yao katika SACCOS.

Naye Kaimu Afisa Ushirika wa Wilaya ya Urambo Hilda Boniface akisoma risala ya wanaushirika alisema kuwa baadhi ya SACCOS zimekufa kwa sababu ya viongozi wake ikiwemo Wakurugenzi Watendaji kushindwa kupeleka makato ya fedha za wanaushirika katika sehemu husika.

Alisema kuwa hali hiyo imewakatisha baadhi ya wanaushirika na kuwafanya wasione umuhimu wa kujiunga na SACCOS katika maeneo yao.

Article 4


SIHABA NKINGA AWATAKA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII KUUNDA KAMATI ZA ULINZI WA WATOTO KUANZIA NGAZI YA MTAA

0
0


Na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WAMJW.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia wazee na watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya jamii) Bibi Sihaba amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii katika halmashauri zote nchini kutekeleza wajibu wa uundaji wa Kamati za Ulinzi na Usalama wa mtoto kuanzia ngazi ya mtaa mahali walipo wananchi ili kuwa na mfumo thabiti wa kuzuia na kutoa huduma kwa watoto wanaofanyiwa ukatili.

Ameyasema hayo mapema wiki hii wakati wa kikao cha majumuhisho kwenye kilele cha safari yake ya kikazi katika kijiji cha Tanangozi, kata ya Mseke, tarafa ya Mlolo, wilaaya ya Iringa vijijini mkoani Iringa na kupokea taarifa za utetezi wa haki za watoto kutoka kwa Baraza la Watoto la Kata ya Mseke, Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto, na Timu ya malezi ya watoto wa Kata ya Mseke.

Ameongeza kuwa mabaraza ya watoto yakianzishwa na kuimarishwa katika ngazi za vijiji na kata yatasaidia kutoa raghiba ya watoto kujitambua, kujithamini na kujilinda dhidi ya vitendo vya ukatili na pia kujiepusha na vishawishi vya mahusiano na wanaume katika umri mdogo.

Aidha, Katibu Mkuu aliwapongeza wajumbe wa vyombo hivyo vilivyoundwa na watoto na wazazi kuendeleza wajibu wao wa kuzuia na kutokomeza ukatili na nyanyasaji wa watoto katika ngazi ya familia, jamii na shuleni ili kuongeza ubora wa jamii zetu katika utoaji wa haki za msingi za watoto wote katika jamii zetu.

Alisema Serikali imekamilisha mwongozo wa utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa kutokomeza dhidi ya wanawake na watoto hapanchioni amabo utasambazwa kwa wadau ili kutoa maelekezo fasaha ya utendaji katika maeneo ya utekelezaji wa Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Katibu Mkuu Bibi Sihaba Nkinga amesisitiza kutumia vikundi vya malezi ya watoto na sanaa katika Kata ya Msewe, Wilaya ya Iringa Vijijini kwa kujiunga pamoja na kutumia stadi na mbinu walizonazo katika kuelimu jamii kuacha vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ili kuimarisha mazingira upatikanaji wa haki na usawa kwa wototo wote.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto anayeshughulikia Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bibi Sihaba Nkinga(kushoto) akisalimiana na mjumbe wa Kamati Kuu ya Baraza la Watoto Taifa Lulu Nziku mara baada ya kumaliza mkutano na Baraza la kata ya mseke iringa Vijijini hivi karibuni.Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW.

KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO B IBI SIHABA NKINGA AKUTANA NA KAMATI YA ULIZI NA USALA WA MTOTO WILAYA YA MUFINDI.

MICROSOFT PROJECT TRAINING

TUSUA MAPENE NA PROMOSHENI YA VODACOM

0
0
* Niwakati mwingine tena Vodacom Tanzania imewaletea wateja wake na watanzania wote kwa ujumla  promosheni mpya kabambe kabisa inayojulikana kama Tusua Mapene. Promosheni hii itawawezesha wateja wetu na wananchi wote kwa wale ambao watajiunga na mtandao wetu kushiriki katika bahati nasibu na kujishindia vitita mbalimbali  mpaka kiasi cha shilingi milioni 150 ndani ya siku 150. 
Promosheni hii inampa mteja wa vodacom fursa ya kushiriki kupitia ujumbe mfupi wa maneno, huduma ya M-pesa au mitandao ya kijamii. 
*Vodacom itatoa mshindi mmoja wa Sh. 100M/-, washindi watano wa Sh. 20M/- na mshindi moja wa Sh. 15M/- KILA SIKU na mshindi wa mwisho wa promosheni(Grand draw) atajishindia kitita cha shilingi Million 150/- 
*Jinsi yakushiriki katika promosheni hii ni rahisi sana mteja anachotakiwa kufanya ni kutuma neno  “CHECK” au “VODA” kupitia ujumbe mfupi wa maneno kwenda namba 15544, kwa gharama ya shilingi 300 tu ikijumuisha kodi kwa kila ujumbe.

 Meneja huduma za Ziada na Tehama wa Vodacom Tanzania,Mathew Kampambe(kushoto) na Msimamizi wa michezo  ya kubahatisha nchini,Abdallah Hemed(kulia)wakimsikiliza Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC, Matina Nkurlu(katikati)alipokuwa akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa Uzinduzi wa Promosheni mpya ya Tusua Mapene inayoendeshwa na kampuni hiyo uliofanyika jijini Dar es salaam leo ambapo mkazi wa mkoa wa singida Munira Jumanne alijishindia Tsh. Laki 5/- Ili Mteja wa Vodacom aweze kushiriki kwenye promosheni hii anatakiwa kutuma neno  “CHECK” au “VODA” kwenda namba 15544, kwa gharama ya shilingi 300 tu.

Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC, Matina Nkurlu(kulia)akiongea kwa njia ya simu ya mkononi na mshindi  aliejishindia Tsh. Laki 5/- Munira Jumanne Mkazi wa mkoa wa Singida wakati wa Uzinduzi wa Promosheni mpya ya Tusua Mapene inayoendeshwa na kampuni hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo,Ili Mteja wa Vodacom aweze kushiriki kwenye promosheni hii anatakiwa kutuma neno  “CHECK” au “VODA” kwenda namba 15544, kwa gharama ya shilingi 300 tu.Anaeshuhudia kushoto ni Meneja huduma za Ziada na Tehama wa Vodacom Tanzania,Mathew Kampambe.
Meneja huduma za Ziada na Tehama wa Vodacom Tanzania,Mathew Kampambe(kushoto) na Msimamizi wa michezo  ya kubahatisha nchini,Abdallah Hemed(kulia)wakionyeshwa na  Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC, Matina Nkurlu(katikati) namba ya simu ya mshindi  aliejishindia Tsh. Laki 5/- Munira Jumanne Mkazi wa Singida wakati wa Uzinduzi wa Promosheni mpya ya Tusua Mapene inayoendeshwa na kampuni hiyo uliofanyika jijini Dar es salaam leo. Ili Mteja wa Vodacom aweze kushiriki kwenye promosheni hii anatakiwa kutuma neno  “CHECK” au “VODA” kwenda namba 15544, kwa gharama ya shilingi 300 tu.



DREAMS initiatives Provides safe space for adolescent girls in Shinyanga aiming at prevention of risky HIV behaviors

0
0
 Richard Minyako, a Data Manager at Shinyanga-based civil society organization called Rafiki SDO orienting an out of school adolescent girl, Zubeda Said, on how to use a special computer with tailored programs on prevention of risky HIV behaviors as part of the DREAMS Initiative safe space activities rolled out by Jhpiego's Sauti Project.  The DREAMS Initiative in Tanzania is funded by the US Government through PEPFAR and aims to create determined, resilient, empowered, AIDS-free, mentored and safe young women to live healthier lives and achieve their dreams.
 Out-of-school adolescent girls Swaum Mohamed (19) (left) and Rachael Charles (19) (right) using computers with tailored programs on prevention of risky HIV behaviors at a safe space run by Shinyanga-based civil society organization called Rafiki SDO  as part of the DREAMS Initiative package rolled out by Jhpiego's Sauti Project.  The DREAMS Initiative in Tanzania is funded by the US Government through PEPFAR and aims to create determined, resilient, empowered, AIDS-free, mentored and safe young women to live healthier lives and achieve their dreams. 
 Out-of-school adolescent girls  using computers with tailored programs on prevention of risky HIV behaviors at a safe space run by Shinyanga-based civil society organization called Rafiki SDO  as part of the DREAMS Initiative package rolled out by Jhpiego's Sauti Project.  The DREAMS Initiative in Tanzania is funded by the US Government through PEPFAR and aims to create determined, resilient, empowered, AIDS-free, mentored and safe young women to live healthier lives and achieve their dreams.
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live




Latest Images