Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110153 articles
Browse latest View live

Bagumako: Mamilioni ya Biko nimeyavulia kofia

$
0
0
MSHINDI wa Sh Milioni 20 kutoka Bahati Nasibu ya Biko, Leonard Bagumako, amesema ameyavulia kofia mamilioni ya Biko, baada ya kukabidhiwa huku akiwa hakufahamu lolote kwamba yeye angeweza kuyatwaa.

Bagumako aliyasema hayo jana wakati anakabidhiwa fedha zake jumla ya Sh Milioni 20, katika benki ya NMB, jijini Dar es Salaam, huku akiwa kijana mwenye umri wa miaka 21 tu anayefanya shughuli za uuzaji wa duka Kigamboni.

Akizungumzia fedha hizo, Bagumako alisema awali aliamini kuwa mchezo wa Biko unahusu watu matajiri, lakini baada ya kukabidhiwa fedha hizo, ameamini kila Mtanzania bila kuangalia wapi anaishi na uchumi wake anaweza kuibuka kidedea kwa kupata ushindi.

“Biko nimewavulia kofia kwa sababu kumbe hata sisi mafukara tunaweza kushinda zawadi mbalimbali za biko kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja za papo kwa hapo, bila kusahau ushindi mnono wa Sh Milioni 20 kama niliyoupata mimi,” Alisema.

Naye Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko, Hassan Melles, alisema baada ya kumkabidhi Bagumako fedha zake, wanashauku kubwa ya kumkabidhi mtu mwingine Milioni 20 atakayetokana na droo ya 27 itakayofanyika Jumapili, jijini Dar es Salaam.

“Bagumako ameshapata fedha zake na mwingine atapokea kutoka droo kubwa ya Jumapili, ambapo Biko tunaamini yoyote anaweza kuibuka na ushindi huo mnono kwa kucheza biko kwa mitandao ya simu Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money kwa kufanya miamala kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo namba yetu ya kampuni ni 505050 na kumbukumbu ni 2456.

“Namna ya kucheza ni rahisi kwa sababu mshiriki atafanya muamala kulingana na matakwa ya mtandao wake, huku kiasi cha Sh 1,000 kikiwa na nafasi mbili, ushindi wa papo kwa hapo pamoja na kuingia kwenye droo kubwa ya kuwania Sh Milioni 20 inayofanyika Jumapili na Jumatano,” Alisema.

Kwa kipindi cha miezi miwili ya Mei na Juni, tayari bahati nasibu ya Biko, wameshatoa zaidi ya Sh Bilioni moja kwa washindi wa papo kwa hapo na donge nono la Sh Milioni 20 linalotoka kila Jumatano na Jumapili.
Mratibu wa Matukio na Mawasiliano, Hassan Melles kulia akimkabidhi jumla ya Sh Milioni 20 mshindi wao wa droo ya 26 ya Biko, Leonard Bagumako wa pili kutoka kulia. Wengine pichani ni baba mlezi wa Bagumako, Gerlad Madaraka kushoto pamoja na mtumishi wa NMB, Tawi la Bank House, jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa Matukio na Mawasiliano, Hassan Melles kulia akimkabidhi jumla ya Sh Milioni 20 mshindi wao wa droo ya 26 ya Biko, Leonard Bagumako katikati. Kushoto ni baba mlezi wa Bagumako, Gerlad Madaraka. Picha na Mpigapicha wetu.


Wajumbe wa Kamati ya Maadili Malawi watembelea Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

$
0
0
 

 

WajumbewaKamatiyaMaadiliyanchini Malawi watembelea Tanzania kujifunzautendajikaziwamaeneombalimbalinchini, ikiwanipamojanautendajikatikaWizarayaArdhi, NyumbanaMaendeleoyaMakazi, hususankatikaeneo la utoajihudumakwaUmmakatikakupambananaRushwanauadilifuwaUtumishi. 

MratibuwaKituo cha hudumakwamteja; Johnson Sangaakionyeshaelectronic queing machineyakuhudumiawatejasawasawanaanayewahikufika, ambayohutumikakatikaKituo cha HudumakwaMteja; KwaWajumbewaKamatiyaMaadilikutoka Malawi.

KamatiyaMaadilikutokanchiniMalawi ikiwakwenyepichayapamojanaKamatiyauadilifuyaWizarayaArdhi.

Na Kitengo cha MawasilianoSerikaliniWizarayaArdhi, NyumbanaMaendeleoyaMakazi.

Benki M yasherehekea miaka 10 ya mafanikio

$
0
0
Benki M, nchini Tanzania inayokua kwa kasi imetimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 2007.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Mkurugenzi mkuu wa benki hiyo, Jacqueline Woiso amesema kuwa benki hiyo imeendelea kukua kwa kasi katika kipindi cha miaka 10 ya uwepo wake na rasilimali zake zimefikia Trilioni moja ndani ya miaka kumi tu ilihali benki inayokaribia katika rekodi hiyo ilifikisha rasilimali zenye thamani ya Trilioni moja katika kipindi cha miaka 17. 

 “Wakati tunatimiza miaka 10 katika soko, tunachosherehekea sio idadi tu ya miaka tuliyotimiza, bali ni mafanikio makubwa tuliyofikia ambayo kila mtu amejionea. Tumeleta mapinduzi katika teknolojia ya kibenki, huduma kwa wateja, faida na kusaidia jamii” alisema.

Benki hii changa iliyoko katika benki kumi bora nchini imekuwa ikikua kwa kasi “Tumekuwa tukifanya vizuri katika masoko kwa muda mrefu na tulifanikiwa kuanza kupata faida ndani ya miaka miwili (2) tu toka kuanzishwa kwa benki yetu. Tumekuwa ni benki ambayo imefanikiwa kuwa na rekodi ya juu sana katika ukuaji kwa upande wa rasilimali na pia faida” aliongeza Bi. Woiso

Kwa upande wa huduma kwa wateja, Bi woiso alisema kuwa Benki M imekuwa ni benki ya kwanza kutoa huduma masaa 12 kila siku kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa mbili usiku, siku 7 za wiki yaani Jumapili hadi Jumapili.

Benki M ilianza kutoa huduma tarehe 27 Julai 2007 ikiwa na tawi moja lililoko barabara ya Nyerere, na baadae iliongeza matawi mengine jijini Dar es salaam, Arusha na Mwanza.
Mkurugenzi mkuu wa Benki M Bi. Jacqueline Woiso akiongea katika mkutano na wandishi wa habari hapo jana jijini Dsm ambapo Benki M imetimiza miaka 10 na kupata mafanikio makubwa. Kulia ni mkuu wa idara ya mawasiliano wa Benki hiyo Bw. Allan Msalilwa.
Benki hiyo pia imekuwa ikishiriki kwa kiasi kikubwa katika kusaidia jamii ikiwa ni moja ya sera kubwa za benki hiyo ambayo huiita Money@heart, “tunashirikiana na taasisi mbalimbali katika kufanikisha miradi mingi kwenye jamii katika sekta ya Afya, Elimu, Maji Utunzaji wa mazingira na pia kuwainua wajasiriamali na wasanii wa michoro ya asili nchini”. 

Pia alisema kuwa wamefanikiwa kupata tuzo mbalimbali za kimataifa ikiwemo tuzo ya benki bora ya biashara kwa mwaka 2015 iliyotolewa katika soko la hisa la London, Benki bora katika sekta ya biashara za makampuni Afrika Mashariki, Benki bora inayoshiriki katika maendeleo ya jamii Afrika Mashariki na hivi karibuni Benki bora katika sekta ya biashara za makampuni Tanzania na Benki bora katika utoaji wa huduma kwa wateja zilitolewa na Banker Africa” alisema Woiso.

Bi Jacqueline aliongeza Benki M imeendelea kujivunia uwiano wa kijinsia kwa wafanyakazi walioajiriwa na Benki hiyo ambapo wamekuwa na uwiano wa asilimia 50 kwa 50 kati ya wanaume na wanawake mpaka sasa.

“Kwa niaba ya wafanyakazi na uongozi wa Benki M, tunapenda kuwashukuru wateja wetu kwa kuendelea kutuamini na kutufanya kuwa chaguo bora katika benki zinazotoa huduma kwa makampuni nchini, toka tulipoanza mwaka 2007. Tunayo furaha kuendelea kuwahudumia tutaendelea kuwapa huduma bora mnayostahili. Mafanikio yote tuliyoyapata yanatokana na wateja kama ninyi.” Alimalizia Bi. Woiso.

WANAHABARI WAHAMASISHWA KUANDIKA HABARI ZA KUUTANGAZA UTALII WETU NCHINI

$
0
0
Mkurugenzi Idara ya Habari MAELEZO Dkt.Hassan Abbas akiwasilisha mada katika Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana  kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. .

Akiwasilisha mada ya Wajibu wa Wanahabari katika kutangaza Utalii nchini,Dkt Abbas alisema kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) wana wajibu wa kuwashirikisha Wanahabari kwa kuwapatia taarifa sahihi,Ili jamii nayo ielimishwe habari zenye usahihi katika nyanja mbalimbali za Utalii.

"Tuwafadhili Waandishi wa habari kufanya stadi muhimu kama habari za Takwimu (data Journalism) na za uchunguzi (investigative journalism) kwa habari zenye maslahi kwa Taifa kama vile kufichua mitandao ya Waharifu wa mazingira au Majangili",alisema Dkt Abbas.

Dkt.Abbas amewataka Wanahabari kuandika habari za Utalii kwa wingi katika suala zima la kuutangaza Utalii wa nchi yetu,ambao ukitangazwa vizuri itasaidia kukuza uchumi wetu na hatimae kuongeza pato la Taifa,akaongeza kuwa pia na jamii inayozunguka katika suala zima la utalii itanufaika kwa namna moja ama nyingine.
Pichani kati ni Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Utangazaji Tanzania (TBC),Dkt Ayub Rioba akiwa sambamba na Meneja Mahusiano wa TANAPA,Pascal Shelutete na wadau wengine wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Dkt.Hassan Abbas alipokuwa akiwasilisha mada katika Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana  kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. 
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri ,Theophil  Makunga  akiwa na Wajumbe wengine katika Mkutano wa Wahariri na Waandishi waandamizi  ulioandaliwa na Tanapa
Wahariri na Waandishi waandamizi wa Habari walioshiriki katika Mkutano Maalum wa Mwaka ulioandaliwa TANAPA juu ya Utalii na Tanzania ya Viwanda 
Mwandishi wa gazeti la Mwananchi Mkoa wa Morogoro Lilian Lucas  akipitia jarida la Mamlaka ya Hifadhi ya  Ngorongoro wakati wakati somo la umuhimu wa kuhifadhi na kutangaza utalii wa eneo hilo.
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006)Ltd, Absalom Kibanda  akichangia jambo kwenye mada iliyohusu Wajibu wa Wanahabari katika kutangaza Utalii nchini, wakati wa mkutano wa Wahariri na Waandishi wa Habari Waandamizi juu ya Utalii na Tanzania ya Viwanda.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri ,Theophil  Makunga  akiuliza moja ya swali kwenye mada iliyohusu Wajibu wa Wanahabari katika kutangaza Utalii nchini,katika mkutano wa Wahariri na Waandishi wa Habari Waandamizi juu ya Utalii na Tanzania ya Viwanda.

ZIMAMOTO WAKUTANA NA WADAU WA VIFAA VYA USALAMA DHIDI YA MAJANGA YA MOTO (TAFEDA) JIJINI DAR

$
0
0
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (Katikati), akizungumza na Wadau wa Vifaa vya Usalama dhidi ya majanga ya moto (TAFEDA), walipokutana na kufanya kikao katika ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Jeshi hilo, leo jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Wadau wa Vifaa vya Usalama dhidi ya majanga ya moto (TAFEDA), Mohamed Kaumbwa akitoa utambulisho wa wajumbe aliombatana nao, walipokutana na kufanya kikao katika ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, leo jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye, akiwa kwenye picha ya pamoja na Wadau wa Vifaa vya Usalama dhidi ya majanga ya moto, leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji)

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA-JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

BAADA YA KUTAMBIANA, NUSU FAINALI YA PILI YA SPRITE BBALL KINGS KUENDELEA KESHO DON BOSCO OYSTERBAY

$
0
0
Manahodha wakiwa katika picha ya pamoja.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Michuano ya mpira wa kikapu ya Sprite Bball Kings 2017 imezidi kupamba moto baada ya timu zilizofanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali kutambiana.

Michuano hiyo inayoendelea wikiendi hii katika Viwanja vya Don Bosco imekuwa ya ushindani mkubwa ikiwa ni mchezo wa raundi ya pili ya nusu fainali.

Manahodha kutoka timu hizo wametambiana kwa kila mmoja kumuambia mpinzani wake kuwa ajipange katika mchezo huo wa raundi ya pili ambapo matokeo hayo yanaweza kutoa majibu ya kuelekea fainali.

Kwa upande wa timu ya mpira wa kikapu ya Mchenga Bball Stars, nahodha wao Mohamed Yusuph amesema kuwa watahakikisha mchezo wa pili dhidi ya wapinzani wao Flying Dribblers unamalizika kwa siku hiyo kwani hawatakubali kuona wanaenda raundi ya tatu.

Nahodha wa Flying Dribblers Geofly lea ametamba na kuwatahadharisha Mchenga kuwa hawatakubali kuona wanarudia makosa ya mchezo uliopita kwani katika raundi hii watahakikisha ushindi utakuwa upande wao.

Kwa upande wa wapinzani wengine Timu ya Kurasini na TMT, Nahodha wa Kurasini Rajab Hamis amewatahadharisha TMT kuwa raundi hii wamejipanga sana na wataumaliza mchezo siku hiyo huku nahodha wa TMT Isihaka Masoud akiweka wazi kuwa alama walizofungwa ni chache sana lazima wapindue matokeo.

Hatua hiyo ya nusu fainali ilianza kupigwa mwishoni mwa wiki iliyopita na tayari Flying Dribllers walikubali kipigo cha vikapu 119 dhidi ya 70 kutoka kwa Mchenga All Stars na Kurasini waliibuka na ushindi wa vikapu 87 kwa 80 vya TMT.

Nusu fainali ya pili itaendelea wikiendi hii.

Mashindano ya Kigwangalla Cup 2017 yazinduliwa jimbo la Nzega vijijini

$
0
0
Mashindano ya mpira wa miguu kwa timu za Kata zilizo ndani ya Jimbo la Nzega Vijijini maalufu kama ‘Kigwangalla Cup’ yamezinduliwa rasmi jioni ya Julai 27, 2017 huku miamba 20 ikitarajiwa kuumana kumpata bingwa wa Jimbo hilo kwa mwaka huu.

Awali akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mbunge wa  Nzega Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla aliwataka wachezaji wote wanaoshiriki michuano hiyo kuwa na nidhamu iliwaitumie michuano hiyo kama kipimo cha wao cha kuonesha vipaji vyao ili waonekane ngazi za juu.

“Mpambane kweli kweli. Kila mmoja wenu aoneshe uwezo wake wa kusakata kabumbu. Pia muzingatie nidhamu ya hali ya juu kwani michezo inaleta umoja na amani, inaimalisha afya ya miili yetu” alieleza Dk. Kigwangalla wakati akuzungumza na wachezaji katika ufunguzi wa michuano hiyo.

Dk. Kigwangalla pia alipata wasaha wa kukagua timu zilizofungua rasmi michuano hiyo kati ya Mizibaziba dhidi ya Nkiniziwa ambazo hadi kipyenga cha mwisho ziliweza kutoka droo ya bao 1-1. Dk. Kigwangalla alieleza kuwa, jumla ya Kata 19 za jimbo lake hilo zimeweza kutoa timu ilikushiriki michuano hiyo huku timu maalum ikiingizwa ambayo itajumuisha Madiwani wote kutoka Kata hizo ili kufanya jumla ya timu 20.
Mbunge wa  Nzega Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na wachezaji wa Kata ya Nkiniziwa wakati wa ufunguzi rasmi wa michuano ya Kigwangalla Cup 2017, iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Msingizi Nkiniziwa, timu hizo zilitoka droo ya bao 1-1.
 Mbunge wa  Nzega Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na timu ya Kata ya Mzibaziba wakati wa ufunguzi rasmi wa michuano ya Kigwangalla Cup 2017, iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Msingizi Nkiniziwa, timu hizo zilitoka droo ya bao 1-1.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LEO TAREHE 28.07.2017


MAHAKAMA YAIAMURU MAGEREZA KUMPELEKA HOSPITALI KWA MATIBABU MSHTAKIWA HARBINDER SINGH

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii. 

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewaamuru Magereza kumpeleka mshitakiwa Harbinder Singh Sethi katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu. 

Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi amesema hayo leo, baada ya mshtakiwa Sethi kuieleza mahakama kuwa, anaumwa.

Hakimu Shaidi amesema,suala la afya ya mshitakiwa ni la msingi hivyo mamlaka zinazohusika zihakikishe mshitakiwa anapata matibabu na tarehe ijayo watoe taarifa kama amri imetekelezwa au la.

Kabla ya kutolewa kwa amri hiyo, mshtakia Seth amedai kuwa hali yake ni mbaya kwani aliongea  na magereza ili aweze kupata matibabu toka kwa daktari wake lakini alipelekwa Hospitali ya Amana.

Sethi amedi kutokana na maradhi yake ya uvimbe tumboni kuhitaji mtaalamu, alishindwa kupata matibabu katika hospitali ya Amana.

Mwendesha Mashitaka kutoka  Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Vital Peter alidai suala la ugonjwa ni la kitaalamu ambalo linahitaji kuthibitishwa ili kujiridhisha licha ya mshitakiwa kujieleza, hakuna nyaraka zinazounga mkono hoja zake kutoka kwa mtaalamu zinazoelezea hali yake.

Alidai kutibiwa ni haki ya mshitakiwa kwa kuwa wapo wataalamu katika hospitali  ya Muhimbili na magereza.

Hata hivyo, alidai upelelezi wa shairi hilo haujakamilika na kuomba tarehe kwa ajili ya kutajwa.

Sethi ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Power African Power (T) Limited (PAP), anashtakiwa na mwenzake,  James Rugemarila ambaye ni Mkurugenzi wa VIP Engineering na mmiliki mwenza wa zamani wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL).

Wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka  12 ya  uhujumu uchumi  kwa kuisababishia serikali hasara ya dola za Marekani milioni 22. 1 na Sh bilioni 309.

Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 3 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na kuangalia upelelezi umefikia wapi.

CHANELI YA UTALII YA TBC KUZINDULIWA DESEMBA 20 MWAKA HUU

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt. Ayub Rioba amesema mchakato wa uanzishwaji wa Chaneli ya Habari za Utalii kuzinduliwa Desemba 20 mwaka huu.

akizungumza wakati wa uwasilishaji wa mada ya Chanel ya Utalii kwa Wahariri na Waandishi wa Habari wakati wa mkutano wa Utalii na Tanzania ya Viwanda ulioandaliwa na TANAPA Jijini Tanga..

"Chanel hii ni moja ya vitu ambavyo vitasaidia katika kukuza utalii wetu hivyo sasa tupo katika mchakato na wabia wetu TANAPA, NGORONGORO na wadau wengien wa masuala ya habari" amesema Dr Rioba .

Amesema kuwa kikubwa wanachokiangalia sasa ni aiana gani ya uwekezaji unatakiwa kufanywa hili kufanya chombo hicho kuwa bora zaidi hili kuweza kumvutia kila mtu .

aidha Dk Rioba ametoa fursa kwa wadau na wanahabari kutoa maoni yao juu ya namna gani Chanel hiyo inapaswa kuwa hili kuvutia.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt. Ayub Rioba akitoa ufafanuzi kuhusu mchakato wa kuanzisha chaneli ya Utalii ndani ya televisheni y Taifa (TBC),mbele ya Wahariri na Waandishi waandamizi mapema jioni ya leo katika katika Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana  kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. 

KAMATI YA KUZUIA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU WAKUTANA NA WADAU KUJADILI NAMNA YA KUPAMBANA NA BIASHARA HIYO

$
0
0
Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu , Seperatus Fella, akizungumza na wadau kutoka taasisi zinazojihusisha na kupambana na biashara hiyo waliokutana katika jijini Dar es Salaam leo, ili kujadili mikakati ya kutokomeza biashaara hiyo nchini. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Afisa uchunguzi Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu, Ahmed Mwendadi, akifafanua jambo kwa wadau kutoka Taasisi zinazopambana na biashara hiyo waliokutana jijini Dar es Salaam, ili kujadili mikakati ya kutokomeza biashaara hiyo. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkurugenzi Mtendaji wa ANPPCAN Tanzania, Wilbert Muchunguzi, akieleza jambo juu ya shughuli wanazofanya katika kupambana na Biashara Haramu ya Kuzuia Usafirishaji Binadamu nchini. Kushoto ni Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Seperatus Fella. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

KAMPUNI YA GOOD ONE YATOA MSAADA WA VIFAA HOSPITALI YA MBAGALA RANGI TATU

Serikali Haitavumilia Kuona Taasisi Zinajiendesha kwa Hasara

$
0
0


Msajili wa Hazina Dkt. Oswaid J. Mashindano akifafanua jambo katika kikao kazi cha uhamasishaji wa sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu mbele ya Wenyeviti wa Bodi, Watendaji Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Mihale Mwakabinga na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Umma wa OMH, Bw. Maftah Bunini. 
Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti wa Ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Mihale Mwakabinga akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya Msajili wa Hazina, Bodi na Wizara Mama katika usimamzi wa Mashirika na Taasisi za Umma katika kikao kazi kikao kazi cha uhamasishaji wa sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu kilichowakutanisha na Wenyeviti wa Bodi za Wakurugenzi,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Umma kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina akielezea jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu maana ya Mashirika ya Umma katika kikao kazi kikao kazi cha uhamasishaji wa sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu kilichowakutanisha Wenyeviti wa Bodi za Wakurugenzi, Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Msajili wa Hazina Dkt. Oswaid J. Mashindano na Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti wa Ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Mihale Mwakabinga. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Samwel Mwita Nyantahe akichangia hoja wakati wa kikao kazi baina ya Ofisi ya Msajili wa Hazina na Wenyeviti wa Bodi za Wakurugenzi, Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kuhamasisha sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu yao. 

TEF YALAANI WAANDISHI WA HABARI WA TBC KUFUKUZWA KWENYE MKUTANO WA CHADEMA

WATOTO WA KIKE WAASWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI NA HISABATI

$
0
0

Na. Paschal Dotto- MAELEZO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano Mhe. Janauary Makamba amewaasa watoto wa kike kusoma masomo ya sayansi ambayo yatawawezesha kupata utaalamu katika fani ya uhandisi.

Akizungumza kwa niaba ya Makamu wa Rais katika Tamasha la Wahandisi wanawake(TAWECE) lililofanyika katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es salamu Mhe. Makamba amesema kuwa katika juhudi za kujenga taifa la viwanda fani ya uhandisi ni muhimu hivyo watoto wakike hawana budi kuweka kipaumbele katika masomo ya sayansi.

“katika hali ya kawaida wahandisi wa kike ni wachache kulinganisha na wahandisi wa kiume hii ni kutoka na kuwepo kwa imani kuwa masomo katika kada hii ni ya wanaume na si wanawake kama watoto wengi wanavyojua,watoto wa kike onyesheni tofauti someni masomo ya sayansi muweze kutoa mchango kwa taifa “ Alisema Waziri Makamba.

Pia Waziri Mhe. Makamba ameishukuru Serikali ya Norway kwa kutoa nafasi kwa masomo kwa watoto wa kike kusomea uhandisi kwani hali hii imesaidia kuongeza idadi ya wahandisi wa kike kutoka 96 kwa mwaka 2010 hadi kufikia wahandisi 379 kwa mwaka huu.
Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulukia Muungano na Mazingira January Makamba (kulia) akimsikiliza Msajili wa Bodi ya Wahandisi nchini Tanzania(ERB) Mhandisi Patrick Balozi (kushoto) akitoa neno la utangulizi wakati wa uzinduzi wa kongamano la tatu la wahandisi wanawake nchini mapema hii leo jijini Dar es Salaam.

Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulukia Muungano na Mazingira January Makamba (kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa Chama cha Wahandisi Wanawake nchini Mhandisi Alice Isibike akielezea changamoto wanazokutana nazo wahandisi wanawake mapema hii leo wakati wa uzinduzi wa kongamano la tatu la wahandisi wanawake nchini mapema hii leo jijini Dar es Salaam.

Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulukia Muungano na Mazingira January Makamba akizungumza na wahandisi wanawake nchini wakati akizindua kongamano la tatu la wahandisi wanawake nchini mapema hii leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wahandisi wanawake wakimsikiliza Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulukia Muungano na Mazingira January Makamba wakati akizindua kongamano la tatu la wahandisi wanawake nchini mapema hii leo jijini Dar es Salaam.Picha na Eliphace Marwa – Maelezo 



KIWANDA CHA NONDO CHA UNIQUE STEEL CHAJIPANGA KATIKA UWEKEZAJI KUHUDUMIA BOMBA LA MAFUTA

$
0
0


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Kiwanda cha uzalishaji wa nondo cha Unique Steel Rolling Mills kilichopo Tanga kimesema kimejipanga kufanya uwekezaji mkubwa,Ili kutumia fursa ya uwepo wa ujenzi wa Bomba la gesi kutoka Tanga mpaka Uganda kutumia malighafi kutoka kiwandani hapo.

Hayo yamebainishwa na Mhasibu Mkuu wa kiwanda hicho, Sikander Omar alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari waliotembelea kiwanda hicho Jijini Tanga.Omar amesema kuwa Wakati Serikali ikipambana kuhakikisha viwanda vinakua nchini, baadhi ya viwanda vilivyopo vimekuwa vikikumbana na changamoto mbalimbali zinazozuia uzalishaji kwa wakati."Moja ya changamoto hizo ni kukatika katika kwa umeme bila taarifa jambo linalotia hasara wakati wa uzalishaji.

Mbali na hilo upatikanaji wa mikopo kwa ajili ya kuwekeza zaidi imekuwa ni changamoto kwao,anapambana kukiboresha kiwanda hicho lakini umeme kutokuwa wa uhakika imekuwa changamoto".Amesema Omar.Amesema kwa sasa wanazalisha hadi tani 60 za nondo ambazo nyingi huuzwa mkoa wa Arusha.

Akizungumzia changamoto zilizopo msimamizi wa kiwanda hicho, Jagjeet Singh alisema umeme unapokatika wakati wa uzalishaji inakuwa ni hasara kwao kwa kuwa mtambo wa kuyeyusha chuma hupoa na vyuma vilivyokuwa vinayeyuka ili kutoa nondo huganda.

Kiwanda hicho ambacho kilikuwa cha Serikali na kuzinduliwa Julai 21, 1971 kilisimama na kuanza uzalishaji tena hivi karibuni baada ya kuchukuliwa na mwekezaji huyo. Omar amesema hivi sasa wako katika mchakato wa kutafuta mkopo ili kukiongezea nguvu kiweze kuzalisha zaidi na kutoa huduma katika mikoa zaidi ya Tanga na Arusha ambalo ndilo soko kubwa lao lilipo kwa sasa.
Mhasibu Mkuu wa kiwanda cha Nondo cha Unique Steel Rolling Mills kilichopo Tanga, Sikander Omar akizungumza na Wandishi wa Habari waliotembelea kiwanda chake kungalia hali ya uzalishaji
Watendaji wa kiwanda cha Unique Steel Rolling Mills kilichopo Tanga wakiwaonesha waaandishi wa habari sehemu ya kuzalishia Nondo ambayo imesimama kutokana na matatizo ya Umeme
Mwandishi wa habari wa Gazeti la Mwananchi Boniface Meena akiangalia moja ya Nondo zinazozalishwa na Kiwanda cha Unique Steel Rolling Mills kilichopo Tanga

CHANJO YA HOMA YA INI KUPATIKANA KWA WANANCHI WOTE MPAKA KUFIKIA 2020

$
0
0

NA WAMJW –DAR ES SALAAM.

CHANJO ya homa ya Ini inatarajiwa kupatikana kwa wananchi wote bila kujali kigezo cha umri wala uwezo wa kifedha kwa wananchi wenye hatari au ugonjwa wa ini kwa bei nafuu mpaka kufikia mwaka 2020 kutoka mwaka wa fedha 2018/2019.

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu maadhimisho ya ugonjwa wa homa ya ini duniani.

“Katika kuadhimisha siku ya ugonjwa wa homa ya ini duniani tumedhamiria kuhakikisha chanjo ya ugonjwa huu inapatikana kwa watu wote nchini ambao wana hatari ya kupata maambukizi ya homa ya ini au tayari wamepata ugonjwa huo kwa bei nafuu kwa mswaka wa bajeti 2018/2019” alisema Waziri Ummy. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiwahutubia waandishi nwa habari (Hawapo kwenye picha) katika kilele cha maazimisho ya siku ya Homa ya Ini Duniani yaliyofanyika leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mganga mkuu wa Serikali Pro Muhamad Bakari kambi na Kulia ni Afisa kutoka kitengo cha magonjwa ya Mlipuko Dkt. Azma Simba. 
Waandishi wa habari kutoka vyombo tofauti wakifuatilia kwa ukaribu tamko la kilele cha maadhimisho ya Homa ya Ini Duniani lililotolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (Hayupo kwenye picha) leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam 

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII INJINIA RAMO MAKANI AFUNGA RASMI MKUTANO WA SITA WA TANAPA KWA WAHARIRI NA WANAHABARI WAANDAMIZI MKOANI TANGA

$
0
0
Naibu Waziri Maliasili na Utalii Injinia  Ramo Makani akimkabidhi Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006)Ltd, Absalom Kibanda cheti cha ushiriki wa Mkutano wa Mwaka na Wahariri na Wanahabari Waandamizi nchini uliohitimishwa jioni ya leo jijini Tanga.Katika hatua hiyo ya kukabidhiwa vyeti,washiriki wote walikabidhiwa vyeti vya ushiriki wao kwa ukamilifu katika mkutano huo.

Mgeni rasmi,Naibu Waziri Maliasili na Utalii Injinia  Ramo Makani(wanne kulia) akiwa katika picha ya pmoja na washiriki wa Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Wanahabri waandamizi ulioanza kufanyika jana kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. 

Naibu Waziri Maliasili na Utalii Injinia Ramo Makani leo akizungumza jambo wakati akifunga rasmi Mkutano wa Mwaka na Wahariri na Wanahabari Waandamizi nchini jijini Tanga.

Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa TANAPA,Bwa.Ibrahim Mussa akiwashukuru washiriki wa Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,na kuhitimishwa rasmi jioni ya leo na Naibu Waziri Maliasili na Utalii Mhe. Ramo Makani .

 Meneja Mahusiano wa TANAPA,Pascal Shelutete akizungumza jambo kabla ya mgeni rasmi kufunga Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga.
Sehemu ya Meza kuu,kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF),Theophil Makunga,Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO),Dkt.Hassan Abbas,Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa TANAPA,Bwa.Ibrahim Mussa ,Mgeni rasmi-Naibu Waziri Maliasili na Utalii Mhe. Ramo Makani,Mkuu wa Wilaya ya Tanga,Mhe.Thobis Mwilapwa.


Baadhii ya washiriki wa mkutano huo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo kabla ya kufungwa rasmi jioni ya leo.

RAIS DKT MAGUFULI AAGIZA KUSIMAMISHWA KAZI KWA NAIBU KAMISHNA WA UHAMIAJI *Ni baada ya kutoa vibali vya uraia kwa Wasomali 50

$
0
0
RAIS Dkt. John Magufuli amemuagiza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kumsimamisha kazi Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Bi. Grace Hokororo (pichani chini)  asimamishwe kazi kwa tuhuma za kuingiza nchini raia 50 wa Somalia na kuwapa vibali vya kuishi kinyume cha taratibu.
Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa Julai 28, 2017), na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kumaliza kikao na Makamishna wa uhamiaji  Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
Pia Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba kuunda tume ya uchunguzi kuhusu utoaji wa vibali uraia nchini. 
Amesema haiwezekani raia wa kigeni wanaingizwa nchini na wanapewa vibali vya kuishi bila ya kufanyiwa uchunguzi wa kina. “Idara ya Uhamiaji tunaitegemea kusimamia mipaka yetu na kuziba mianya ya watu kuingia bila ya kufuata taratibu lakini kwa mapenzi yake Ofisa huyu ameruhusu Wasomali kuingia bila kufuata taratibu.”

Waziri Mkuu amesema ni lazima uchunguzi ufanyike ili kubaini  ukweli: “Tulidhani ni kitu gani kilimsukuma kutoa vibali kwa Wasomali hao ambao hawakuwepo nchini wameingia na kupewa vibali moja kwa moja kwa mapenzi yake tu sasa hii ni dosari hatuwezi kuivumilia.”
Amesema Serikali inaitegemea Idara ya Uhamiaji kwa kuzuia mianya ya uingiaji raia mbalimbali kutoka nje ya nchi bila ya kufuata taratibu, hivyo Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ameagiza Ofisa huyo asimamishwe kazi na uchunguzi ufanyike ili kubaini malengo yake.

RAIS MAGUFULI NA RAIS MUSEVENI WA UGANDA KUWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAFUTA GHAFI TOKA HOIMA NCHINI UGANDA HADI TANGA KUFANYIKA AGOSTI 5, 2017

Viewing all 110153 articles
Browse latest View live




Latest Images