Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109935 articles
Browse latest View live

prof dos santos kuwasilisha mada ya uhifadhi wa misitu na mpango mkakati wa utalii nchini

$
0
0
Mtendaji Mkuu Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania, Ibrahim Mussa (kushoto) alipokuwa akimueleza mambo mbalimbali ya uhifadhi na changomoto zake inapokuja suala la kushirikisha vyombo vya habari kabla ya kufungua mkutano wa sita wa wahariri na wanahabari waandamizi unaohusu sekta ya utalii nchini ambao umeandaliwa na Hifadhi za Taifa (TANAPA) unaofanyika jijini Tanga 27 - 29, Julai 2017. Pichani kati ni Mkurugenzi Mkuu wa Shrika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA),Allan Kijazi 
 
Katika mkutano huo Prof  Silayo atawasilisha mada "uhifadhi wa misitu ya hifadhi ya asili na mpango mkakati wa utalii Kesho Ijumaa ya tarehe 28 Julai 2017 saa 05:45 asubuhi na kurushwa moja kwa moja kupitia ukurasa wa facebook wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (www.facebook.com/foresttz). 
 

usikose kuungana naye na atajibu maswali yatakayoibuka kutokana na mada atakayoiwakilisha!

Mratibu wa Mradi wa Misitu ya Hifadhi ya Mazingira Asilia Tanzania, Gerald Kamwenda (Kushoto) akijadiliana jambo na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof Dos Santos Silayo mara baada ya kupokea taarifa za wajumbe wa Mkuno Mkuu wa Mwaka wa Wahariri na Wanahabari Waandamizi ulioandaliwa na Hifadhi za Taifa Tanzania kutembelea Hifadhi ya Misitu Asilia ya Amani Siku ya Jumamosi (Julai 29,2017).



LISSU AACHIWA KWA DHAMANA

$
0
0
Na Mwene Said wa Globu ya Jamii, Dar es Salaam.

Mahakama ya Hakimu Mkazi kisutu, jijini Dar es Salaam, imemwachia kwa dhamana Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, baada ya kutupilia mbali pingamizi la dhamana lililotolewa na upande wa Jamhuri.

Uamuzi huo ulitolewa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri aliyepangiwa kusikiliza kesi hiyo. Alisema mahakama yake baada ya kupitia hoja za upande wa Jamhuri za pingamizi hilo haukuithibitishia mahakama kama kuna kesi kati ya hizo anazotuhumiwa aliwahi kuruka dhamana.

Alisema hoja ya mshtakiwa kuzuiwa dhamana kwa sababu ya usalama wake, haina mashiko na haijitoshelezi kuweza kumweka Lissu mahabusu.

Kuhusu jopo la mawakili 18 wa utetezi, hakimu alisema ni ishara wazi kwamba  inaonesha anaishi vizuri na watu na wanaupendo dhidi yake.

Hakimu alisema mashtakiwa atakuwa nje kwa kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaotoka serikalini au taasisi zinazotambulika, watakaosaini hati ya dhamana ya Sh. milioni 10 milioni kila mmoja.

Pia, alisema mshtakiwa asitoke nje ya jiji la  Dar es Salaam bila kibali cha mahakama hiyo. Lissu alitimiza masharti hayo na yuko nje kwa dhamana.

Wakili wa Serikali Simon Wankyo alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika aliomba mahakama kupanga tarehe ya kusikiliza maelezo ya awali.

Hakimu Mashauri alisema kesi hiyo itasikilizwa maelezo ya awali Agosti 24, mwaka huu.

Mapema Julai 24, mwaka huu Lissu alirudishwa rumande baada ya upande wa Jamhuri kuwasilisha pingamizi la dhamana kwa madai kuwa kwa maslahi ya usalama wake.

Hata hivyo, upande wa Utetezi uliongozwa na jopo la mawakili 18, akiwamo Fatuma Karume, Peter Kibatala, Samaa Salah, Dickson Matata, Faraji Mangula, Nashon Nkungu, Konda Johaness, Alex Masaba, Deus Mteja, Matojo Kosata, Novatus Muhangwa, John Mhozwa, Hassan Kihangyo, Jamhuri Johnson, Daim Halfan, Elisha Magabe (mke wa Lissu) na Boniface Mahela ulipinga pingamizi hilo.
Katika kesi ya msingi, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi alidai kuwa Julai 17, mwaka huu mtaa wa Ufipa uliopo Kinondoni, jijini Dar es Salaam, alitoa maneno na lugha ya uchochezi dhidi ya Rais.

Alinukuu maneno hayo kuwa" Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ni ya kibaguzi wa kifamilia, kikabila, kikanda na kidini. Vibali vya kazi |(work permit) vinatolewa kwa wamishenari wa kikatoliki tu huku madhehebu mengine yakielezwa kupanga foleni uhamiaji.

Viongozi wakuu wa serikali wanachaguliwa kutoka kwenye familima, kabila na ukanda...acheni woga pazeni sauti... kila mmoja wetu...tukawaambie wale ambao bado wanampa msaada wa pesa Magufuli na serikali yake kama tulivyowaambia wakati wa serikali ya makaburu, hii serikali isusiwe na jumuiya ya kimataifa isusiwe  kisiasa, kiuchumi na kidiplomasia kwa sababu ya utawala huu wa kibaguzi... yeye ni dikteta uchwara" mwisho wa kunukuu.

Upande huo wa Jamhuri ulidai kuwa maneno hayo ni ya uchochezi yenye lngo la kuvuruga amani.

TUME YA UCHAGUZI YATEUA WABUNGE 8 WA VITI MAALUM KUPITIA CHAMA CHA ANANCHI CUF

DK. KIGWANGALLA AKABIDHI GARI LA WAGONJWA JIMBONI KWAKE

$
0
0
 
Mkuu wa Wilaya ya Nzega, mkoani Tabora, Mh. Geofrey Ngupula akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa gari jipya na la kisasa la kubebea wagonjwa lililokabidhiwa katika kituo cha Afya Busondo, Tarafa ya Puge, lililotolewa na Mbunge wa Nzega Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla.


Mbunge wa jimbo la Nzega Vijijini ambaye pia ni Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla amekabidhi gari maalum la kubebea wagonjwa (Ambulance) mpya na la kisasa katika Kituo cha Afya Busondo kilichopo Tarafa ya Puge ambalo litakuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa Nzega Vijijini. 

Tukio hilo la kukabidhi gari hilo limefanywa na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, mkoani Tabora, Mh. Geofrey Ngupula mapema Julai 26,2017, aliyekuwa mgeni rasmi ambaye alitoa agizo kali kwa Mganga Mkuu wa Kituo hicho kuhakikisha gari hilo linatumika kwa shughuli zilizokusudiwa ikiwemo za kubebea wagonjwa na akina mama wajawazito kuwawaisha sehemu muhimu za kutolea huduma stahiki. 

Mkuu wa Wilaya huyo alimpongeza Mbunge wa Jimbo hilo Dk. Kigwangalla kwa kuweza kuwasaidia wananchi wa Jimbo hilo kwa kuweza kuwasaidia gari hilo la Wagonjwa kwani litasaidia kuokoa maisha ya wananchi hao ambao wapo maeneo ya mbali na kituo cha Afya huku pia likitarajiwa kuwa msaada kwa kuwapeleka wateja katika ngazi za juu za huduma hiyo ikiwemo Hospitali za Wilaya, Mkoa, Kanda na Taifa.

Aidha, alisema ni marufuku wagonjwa kuombwa kuchangia mafuta ya ambulance hiyo au gharama yoyote ile, gari hili wagonjwa walitumie bure kwani limetolewa bure na pia huduma zote zikiwemo za mafuta zinalipwa na Halmashahuri hiyo. 
Gari hilo la kubebea wagonjwa linavyoonekana.

“Gari hilo lipatikane kituoni wakati wote pamoja na dereva. Tumeshahakikishiwa hapa Halmshauri imesema ina mafuta ya kutosha litakuwa linajazwa lita 90, kila yatakapokuwa yametumika hivyo kusiwe na kisingizio kingine cha kuweza kudai mafuta ama kuwatoza wananchi gharama na atakayefanya hivyo Serikali hii si ya mchezo hatua kali zitafuata , tutakutumbua tu” alieleza Mh. Ngupula. 

Ameongeza kuwa gari hilo ambalo ni la kisasa, litunzwe na kulindwa ili liweze kutumika kwa miaka mingi ijayo na kuwa msaada kwa Tarafa hiyo na wananchi wote watakaopata msaada wakiwemo wale wa maeneo mengine ya jirani. Kwa upande wake, Dk. Kigwangalla amewaomba wananchi waendelee kumuombea kwa kazi anayofanya ikiwemo jukumu la kulitumikia Taifa katika nafasi yake ya Unaibu Uwaziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Dk. Kigwangalla ameishukuru serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli kwa kuweza kuwa karibu na Wananchi ikiwemo kushughulikia suala la maji kutoka Ziwa Victoria na kuja Mkoa wa Tabora ikiwemo kuanzia katika Wilaya hiyo ya Nzega na kisha kwenda maeneeo mengine. 
 
“Tunampongeza Rais wetru Dk. Magufuli kwa kuwa karibu na wananchi wake. Tulikuwa nae Mkoani kwetu hapa Tabora na amezindua miradi mbalimbali ikiwemo ya barabara na ule wa maji safi yatakayotoka Ziwa Vitoria. Shida ya maji kwa wananchi wa Nzega inaenda kuwa historia kwani Maji hayo yatakuja hapa na kisha kwenda maeneo mengine. 

SERIKALI YATOA SIKU 30 KWA WAAJIRI KOTE NCHINI KUJISAJILI NA MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI, (WCF), VINGINEVYO HATUA ZA ADHABU ZA VIFUNGO NA FAINI KUTEKELEZWA

$
0
0
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, ametoa siku 30 kwa waajiri wote nchini ambao hawajasajili, kujisajili katika Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi (WCF), na kutoa michango kwa wakati, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Waziri Mhagama alitoa agizo hilo jijini Mbeya Julai 27, 2017 wakati wa zoezi la ukaguzi wa kushtukiza jijini humo kuwabaini waajiri ambao bado hawajatekeleza Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Sura 263 Marejeo ya Mwaka 2015 kifungu cha 5, ambayo inawataka waajiri wote kutoka sekta ya Umma na Binafsi, Tanzania Bara kujisajili kwenye Mfuko huo.

“Mwajiri ambaye hajajisajili kwenye Mfuko, anaweza kufikishwa mahakamani na adhabu ni pamoja na kutozwa faini ya kiasi cha fedha kisichozidi shilingi milioni 50 au kifungo kisichozidi miaka 5 jela au vyote kwa pamoja, hivyo nawasihi waajiri kutoka sekta binafsi na umma Tanzania Bara ambao hawajasajili kutekeleza sheria hiyo inayowataka kujisajili WCF katika muda huo nilioutoa.” Alisisitiza Mhe. Waziri Jenista Mhagama.

Katika ziara hiyo ya ukaguzi wa kushtukiza Mhe. Waziri alifuatana na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omar, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano cha Mfuko huo, Bi. Laura Kunenge na Afisa Kazi wa Mkoa wa Mbeya, Bi. Mary Patrick Mwansisya ambapo taasisi ya kwanza ambayo Mhe. Mhagama aliikagua ni Hospitali ya K’s iliyoko eneo la Mafyati na St. Aggrey iliyoko Uyole na kubaini kuwa taasisi hizo hazijajisajili katika Mfuko.

Aidha Waziri alitoa siku saba kwa waajiri wote Mkoani Mbeya wapatao 107 ambao bado hawajajisajili ikiwemo Hospitali ya K’s na Shule ya sekondari St. Aggrey kujisajili ndani ya muda huo.

“Mkishindwa kutekeleza agizo hilo maana yake mnatuelekeza kutumia kifungu cha 71(4), cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi kinachotamka adhabu ya faini ya kiasi cha fedha kisichopungua shilingi milioni 50, kifungo cha miaka 5 jela au vyote kwa pamoja.” Alisema.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama, (kulia), akizungumza leo Julai 27, 2017 wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa kushtukiza kwenye Hospitali ya K’s iliyoko eneo la Mafyati jijini Mbeya ili kubaini kama mwajiri kwenye hospitali hiyo amejisajili katika  Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF). Waziri ametoa siku 30 kwa waajiri kutoka sekta ya umma na binafsi Tanzania Bara, kujisajili na Mfuko huo, vinginevyo watakabiliwa na adhabu mbalimbali ikiwemo faini ya shilingi milioni 50, kifungo cha miaka 5 jela au vyote kwa pamoja. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Afya na Tathmini wa Mfuko huo, Dkt. Abdusalaam Omar.

 Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano cha Mfuko huo, Bi. Laura Kunenge. (kushoto), na Afisa Kazi Mkoa wa Mbeya, Bi.Mary Patrick Mwansisya, (kulia), wakiuliza alipo mkurugenzi wa Hospitali ya K's mara baada ya kuwasili na waziri Mhagama katika ziara ya ukaguzi wa kushtukiza leo Julai 27, 2017.
 Waziri Mhagama, (wakwanza kulia), Bi. Laura na Dkt. Omar, wakimsubiri Mfanyakazi huyu wa K's Hospital akiwasiliana kwa simu na mwajiri wake ili kumjulisha uwepo wa Waziri na ujumbe wake kwenye hospitali hiyo.
 Maafisa wa polisi wakiwa tayari kuhakikisha usalama unazingatiwa wakati wa zoezi hilo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

6 of 38 Print all In new window WADAU MBALI MBALI WA MAFUTA WAKUTANA KUJADILI ZABUNI YA UINGIZAJI WA MAFUTA KWA MWEZI WA TISA

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Serikali wa Uagizaji Mafuta ya pamoja(PBPA), Modestus Lumato akizungumza na Michuzi TV kuhusu Tenda ya Uagizaji Mafuta kwa Makampuni mbalimbali kwa Mwezi wa Tisa. Lumato amesema kuwa Uagizaji wa Mafuta hayo hufanyika mapema, kama inavyofanyika sasa mwezi wa Saba kwa Mafuta ya Mwezi wa Tisa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Zabuni ya kuagiza Mafuta kwa pamoja, Ali Saeed akifungua Sanduku la Zabuni tayari kwa kujadili Makampuni yaliyoandaa Uagizaji wa Mafuta, katika Kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Zabuni ya kuingiza Mafuta kwa pamoja, Ali Saeed akiwa na bahasha za maombi tayari kwa kujadiliwa.
Baadhi ya Wawakilishi wa Makampuni yaliyoomba Zabuni ya kununua Mafuta wakiwa katika Kikao cha kupata washindi wa Zabuni hizo.

MAVUNDE AWADUWAZA WANAKIJIJI WA MATUMBULU KWA KUKAMILISHA AHADI YAKE.

$
0
0


Mbunge wa Jimbo la Dodoma Anthony Mavunde ameendelea kutekeleza ahadi zake alizoahidi wakati wa kampeni ya uchaguzi Mkuu wa 2015 ambapo leo amekamilisha ahadi yake ya kutatua kero ya maji katika kijiji cha Matumbulu.

Mavunde amekamilisha ahadi yake ya kutatua kero hiyo kwa kutoa mabomba ya kusambazia maji kijiji kizima yenye urefu wa Kilomita 1 yenye thamani ya zaidi ya Sh.Milioni 8.

Kufuatia utekelezaji huo wa ahadi hiyo, wananchi hao walishikwa na butwaa kwa uharaka wa utekelezaji wa ahadi hiyo kwakuwa tatizo hilo la upatikanaji wa maji katika eneo ilikuwa ya muda mrefu hali iliyosababisha wananchi kutumia maji yasiyo safi na salama.

Wananchi walikuwa wanakosa fursa ya kupata maji kwa urahisi na hivyo kuwalazimu kutembea umbali mrefu kutafuta maji na muda mwingine kutumia maji ambayo si safi na salama kutoka na umbali wa kufuata maji.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji cha Matumbulu Alfred Malogo, amefurahishwa na utekelezaji wa ahadi hiyo na kwamba alichokifanya Mavunde kuwapatia wakazi wa kijiji hicho mabomba kwa ajili ya kusambazia maji kitatatua kero yao ya muda mrefu ya upatikanaji wa maji.

Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akikabidhi mabomba ya kusambazia maji katika kijiji cha Matumbulu.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akikabidhi mabomba ya kusambazia maji katika kijiji cha Matumbulu kwa wananchi.

.Mabomba ya kusambazia maji katika kijiji cha Matumbulu

Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza na Diwani wa Kata ya Matumbulu Emmanuel Chibago.


WAZIRI MAKAMBA AFANYA ZIARA KATIKA MTO MSIMBAZI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia Mazingira na Muungano Januari Makamba akikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa kingo katika mto Msimbazi eneo la Ilala Bungoni wakati wa ziara yake ya kikazi kukagua ujenzi wa kingo za Mto Msimbazi, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni na barabara ya Barack Obama mapema hii leo.
Baadhi ya mafundi wakiendelea na kazi ya ujenzi wa kingo za mto Msimbazi katika eneo la Ilala Bungoni wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia Mazingira na Muungano Januari Makamba ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa kingo za Mto Msimbazi, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni barabara ya Barack Obama mapema hii leo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia Mazingira na Muungano Januari Makamba akimsikiliza mfanyabiashara ya chakula (Mama Lishe) katika eneo la Ilala Bungoni alipokuwa katika ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa kingo za Mto Msimbazi, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni na barabara ya Barack Obama mapema hii leo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia Mazingira na Muungano Januari Makamba (kulia) akimsikiliza Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Profesa, Shadrack Mwakalila wakati wa ziara ya Waziri huyo ya kukagua ujenzi wa kingo za Mto Msimbazi, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni na barabara ya Barack Obama mapema hii leo.

Eneo la mradi wa ujenzi wa kingo katika Mto Msimbazi eneo la Ilala Bungoni jijini Dar es Salaam.


RC MAKONDA AGAWA KOMPYUTA KATIKA HALMASHAURI ZA JIJI LA DAR ES SALAAM

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh.Paul Makonda leo amekabidhi kompyuta za kisasa 50 zenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 170 kwa Manispaa tano za Mkoa wa Dar es salaam pamoja na Watu wa Jiji na Mkoa kwa ajili ya kurahisisha utoaji wa vibali vya ujenzi.

Katika mgawanyo huo kila Manispaa imepatiwa kompyuta nane (8) huku Ofisi ya Jiji wakipatiwa kompyuta tano (5) na Ofisi ya Mkoa wakipatiwa kompyuta tano (5) ikiwa ni ufadhili wa kampuni ya ulinzi ya TAMOBA Company Ltd iliyomuunga Mkono RC Makonda kutokana na kuhamasika na utendaji kazi wake mzuri.

Makonda amesema Kompyuta hizo zitawekewa Mfumo wa kisasa ujulikanao kama Dar Ardhi E.System utakaoziunganisha idara zote zinazohusika na utoaji wa vibali vya ujenzi (One stop Center) ili kurahisisha Mwananchi kupata kibali cha ujenzi ndani ya muda mfupi, ambapo mwananchi atakuwa na uwezo wa kutuma maombi ya kibali cha ujenzi kwa kutumia simu ya mkononi mwake au Computer hata akiwa nyumbani na akapewa majibu yake kwa haraka.

“Kazi yangu kubwa ni kupunguza mateso,malalamiko na kero za Wananchi dhidi ya maswala ya Ardhi, na namna mbili za kupunguza ni pamoja na kuwawezesha watendaji kuwa na nyenzo na vifaa vitakavyorahisisha kufanya kazi zao kisasa zaidi kuendana na kasi ya Rais wetu Dr.John Magufuli, na pili ni kusimamia uwajibikaji kwamba kila mmoja anatekeleza majukumu yake ili Mwananchi wa Mkoa wa Dar es salaam asipate adha na mateso aliyokuwa akiyapata kwenye Sekta ya Ardhi.

Umuhimu wa kutoa vibali vya ujenzi ni jambo lisilopingika hasa katika mji huu unaokuwa kwa kasi barani Afrika” Alisema Makonda. Aidha kompyuta hizo zitawekewa Mfumo maalumu utakao kuwa ukikusanya Maoni na mapendekezo ya wananchi ambapo wananchi watakuwa na fursa ya kutuma maoni yao na kero mbalimbali zinazowakabili kwenye sekta ya Ardhi.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Mkaonda akipanga kompyuta mara baada ya kupokea kuoka Kampuni ya TAMOBA Company Ltd ya jijini Dar es salaam. 

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akiangalia kompyuta mara baada ya kupokea kopmyuta hizo zilizotolewa na Kampuni ya TAMOBA Company Ltd ya jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Paul Makonda (kushoto)akikabidhi Mkurugenzi wa Manispaa ya Ialala,Msongela Palela Computer za kisasa 50 zenye thamani ya zaidi ya Shilling Million 170 kwa Manispaa tano za Mkoa wa Dar es salaam pamoja leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa ,Paul Makonda akiteta jambo na watendaji wa kampun ya ulinzi ya TAMOBA Company Ltd iliyomuunga Mkono Mheshimiwa Makonda kutokana na kuhamasika na utendaji kazi wake mzuri.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

WATUHUMIWA WA MAKOSAMBALIMBALI MBARONI TEMEKE

$
0
0
Na Agness Francis wa Globu ya Jamii

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto amewatia mbaroni wahalifu wa makundi ya ukabaji na uporaji  nyakati za usiku na sehemu za fukwe wilayani Temeke, pamoja wanafunzi watoro wakiwemo na wazazi wao.

Vibaka hao wanaoshikiliwa na jeshi la polisi hadi sasa  umri wao ni kati ya miaka 12-25, opresheni hiyo ilikamata wahalifu 8 kutoka Mbande na wengine 8 kutoka Chamazi wilayani humo.

Hata hivyo wahalifu hao walikiri kuwa makundi na vishawishi ndio huwasababishia kufanya matukio hayo kwa kutumia visu na mapanga kwa kupora pochi za kina mama  kuchukua simu pamoja na fedha.Vile vile alikemea utoro wa wanafunzi   na kutaka wazazi kurejeshe watoto mashuleni na kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kila mtoto anapata haki yake ya msingi katika kupata elimu.

Nae mzazi Zuhura Hamza alizungumza` kwa kusema watoto wenyewe ndio hawasikii hawataki kusoma wamejitahidi kadri ya uwezo wao lakini hawajapata suluhu la tatizo hilo hivyo akiomba msaada kwa wakuu wa shule.

Kamanda Muruto  alitoa wito kwa wazazi wawahimize watoto kwenda shule, kwani watoto wamezagaa mitaani na kujiingiza katika makundi mabovu  kama ya madawa ya kuevya, uporaji, uvuataji bangi na sigara.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto akizungumza na waaandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kuwashikilia watuhumiwa wa makundi ya ukabaji na uporaji nyakati za usiku na sehemu za fukwe wilayani Temeke, pamoja na  wanafunzi watoro wakiwemo na wazazi wao.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto akiwaonesha wanahabari watuhumiwa wa makosa mbalimbali leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii

HATUA ZILIZOFIKIWA KATIKA MAFUNZO YA MFUMO MPYA WA KUANDAA MIPANGO NA BAJETI ZA SERIKALI ZA MITA

SERIKALI YAWATAKA VIONGOZI WA CHAMA CHA WAFUGAJI NCHINI KUONDOA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

$
0
0


Na Pamela Mollel,Arusha

Serikali imewataka viongozi wa chama cha wafugaji Tanzania pamoja na watetezi wa haki za wafugaji kuhakikisha wanaondoa migogoro ya wafugaji na wakulima, ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara Nchini hali ambayo imekuwa ikirUdisha maendeleo nyuma

Akizungumza jijini hapa katika ufunguzi wa warsha ya siku tatu iliyowakutanisha watetezi wa haki za wafugaji nchini ,Katibu Tawala Wilaya ya Arusha David Mwakiposa alisema kuwa lengo la mafunzo hayo nikuwajengea uwezo hao watetezi ili waweze kuondoa migogoro inayojitokeza katika jamii

“Serikali tunaomba sana watetetezi wa haki za wafugaji kuangalia kwa uzito wa kipekee kuondoa migogoro ya wafugaji na wakulima na wahamasishe uwanzishwaji wa viwanda vya kuchakata bidhaa za mifugo ili kumuunga mkono Raisi Magufuli katika sera ya viwanda”Alisema Mwakiposa

Aidha alisema kuwa sekta ya wafugaji na kilimo inaajiri watanzania walio wengi zaidia asilimia 70 na ndio sekta pekee ambayo haiitaji elimu kubwa tofauti na ajira za viwandani na sehemu nyingine hivyo ni muhimu kujengwa uwezo ili kutimiza sera ya viwanda hapa nchini

Katibu Tawala Wilaya ya Arusha David Mwakiposa akizungumza leo katika warsha ya siku tatu jijini Arusha iliyowakutanisha watetezi wa haki za wafugaji nchini , mafunzo hayo yanalengo la kuwajengea uwezo watetezi hao ili waweze kuondoa migogoro inayojitokeza katika jamii(Habari Picha na Pamela Mollel Arusha).Washiriki wa semina hiyo wakiwa katika picha ya pamoja leo jijini Arusha kwa semina ya siku tatu.

SERIKALI YAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO NA VYOMBO VYA HABARI NCHINI

$
0
0
Na Lorietha Laurence-WHUSM.

Serikali imeeleza kuwa inathamini na kutambua mchango mkubwa unaotolewa na Vyombo vya Habari nchini katika kuhakikisha kuwa jamii inapata taarifa sahihi na kwa wakati.

Akizungumza katika ziari yake alipotembelea vyombo vya habari vya Radio EFM na Radio One/ ITV leo Jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema kuwa lengo kubwa la Serikali ni kuwepo kwa ushirikiano mzuri na sekta ya habari nchini.

“Lengo la ziara hii ni kuimarisha uhusiano baina ya Serikali na vyombo vya habari pamoja na kufahamu utendaji wenu wa kazi na namna mnavyosimamia maudhui ya vipindi vyenu mnavyoviandaa” amesema Prof. Gabriel.

Aidha aliongeza kuwa ni jambo jema linalofanywa na watanzania wazawa kuwekeza katika sekta ya habari kwa kuwa dunia ya sasa imetawaliwa na utandawazi kupitia taarifa mbalimbali zinazotolewa zenye lengo la kuhabarisha na kujenga taifa letu. 

Kwa upande mwingine Prof. Gabriel amewataka watumishi wa vyombo hivyo vya habari kufanya kazi kwa kuzingatia maadili, weledi na uzalendo ili kufikia malengo waliyojiwekea.Pia amewataka watumishi wa vyombo hivyo vya habari kujenga utamaduni wa kufanya kazi kwa kujituma ili kupata matokeo chanya katika soko la ushindani na kuifikia jamii kubwa zaidi katika kutoa habari za uhakikia na zenye usahihi.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiongea na watumishi wa Radio ya Efm (hawapo katika picha) alipofanya ziara ya kutembelea chombo hicho cha habari leo Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Radio ya Efm wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (hayupo katika picha) alipotembelea chombo hicho cha habari leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Radio ya Efm pamoja na watendaji wa Wizara ya Habari wakati wa ziara yake leo Jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akiongea na Viongozi wa Radio One na ITV alipofanya ziara yake IPP Media leo Jijini Dar es Salaam kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji Radio One na ITV Bi. Joyce Mhaville.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyekaa) pamoja na watendaji wa Wizara ya Habari wakiangalia namna mfumo wa urushwaji wa habari unavyofanya kazi katika studio za ITV wakati wa ziara yake leo Jijini Dar es Salaam.


MNADA WA HADHARA: MALI ZA UBALOZI DAR ES SALAAM

$
0
0
UNIVERSAL AUCTION CENTRE Kwa idhini waliyopewa na  OFISI YA UBALOZI watauza kwa mnada wa hadhara  Funicha za nyumbani na Generator  tarehe 29 Julai, 2017Jumamosi saa 4:00 asubuhi. Mnada utafanyika Golden Resort Sinza,  Lion Street.


Fanicha na Computer zitaanza kuuzwa kuanzia saa 4:00 asubuhi: 
Sofa sets, Recliner, Sofa Bed, Wing chairs, Chest drawers,  Dressers, Mirror, Credenza, Entertainment Centre, Coffee table, Book case, Meza za chakula / Viti, Meza za ofisi, Carpet, Vitanda ,Magodoro, Fridge, Freezer, Music system, TV, Jiko la umeme, Washer, Dryer,  Heavy duty Tread mill, Computer set, Photocopy m/c, File cabinet, safe,  A/c Split unit, Refrigerant Reclaim System  na vingine vingi.


Generator Zitaanza kuuzwa saa 6.00 mchana:

Idadi

Aina

Model

Mwaka

Ushuru

3

Generator 40 & 60 KVA

Perkins Diesel   Engine

2001/ 2004

Bado


Mali zote zinaweza kukaguliwa Golden Resort Sinza,Lion Street tarehe 26  hadi 28 Julai, 2017 kuanzia saa 4:00. asubuhi mpaka saa 11:00 jioni.


MASHARTI YA MNADA:

  1. Mnunuzi  wa Fanicha atatakiwa kulipa malipo yote kwa keshia (cashier). Na mnunuzi wa Generator  atatakiwa kulipa 25% pale pale na salio lilipwe ndani ya siku 4 za kazi  mwisho wa kulipa tarehe 3 August 2017, saa 10:00 jioni. Ukishindwa kulipa kwa muda huo generator litauzwa  kwa mshindi mwingine aliyefata  na dhamana haitarudishwa. 
  1. Mali zote zitauzwa kama zilivyo bila dhamana.


  1. Mnunuzi atawajibika kulipa ushuru na kodi zingine zote.


  1. Mali yote iliyouzwa itatakiwa kuondolewa baada ya kulipa malipo yote pamoja na kodi 


  1. Kila mtu atatakiwa kuwa na bid namba itakayo patikana getini,


Kwa maelezo zaidi waone:

UNIVERSAL AUCTION CENTRE

PLOT NO. 5 “E” LION STREET SINZA

CELL NO:  0754 284 926, 0757 284 926                       
E-mail: universalauction@hotmail.com


DAR ES SALAAM.

SPIKA NDUGAI APONGEZWA BAADA YA KUSHINDA NAFASI YA MWENYEKITI WA MASPIKA KATIKA MABUNGE YA JUMUIYA YA MADOLA BARANI AFRIKA

$
0
0
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akipongezwa na Naibu Spika wa Cameroon, Mhe. Monjowa Lifaka baada ya kushinda nafasi ya Mwenyekiti wa Maspika na Viongozi wa Bunge katika Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika. Uchaguzi huo umefanyika leo katika Mkutano wa Maspika wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika uliomalizika leo Mjini Abuja.
Ofisi ya Bunge inapenda kuuarifu umma kuwa Spika wa Bunge Mhe. Job Yustino Ndugai (Mb), leo amechaguliwa kuwa Mwenyekiti  wa Maspika na Viongozi wa Bunge katika Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika. Uchaguzi huo umefanyika  katika Mkutano wa Maspika wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika uliomalizika leo Mjini Abuja.

Kwa wadhifa huo, Mhe Ndugai ataongoza Maspika wenzake toka Mabunge na Mabaraza ya kutunga Sheria  63 yaliyoko katika nchi 18 za Jumuiya ya Madola kwenye Bara la Afrika. Wadhifa huo ni wa miaka miwili kuanzia sasa hadi mwaka 2019 kutakapofanyika uchaguzi mwingine.

Nchi wanachama wa Umoja wa Mabunge Barani Afrika ni pamoja na Afrika  ya Kusini, Botwana, Cameroon ,Ghana, Kenya, Lesotho,   Msumbiji, Mauritius, Malawi, Nigeria, Namibia, Rwanda, Seychelles, Sierra Leone, Swaziland, Tanzania, Uganda na Zambia.

Akizungumzia uchaguzi huo,  Mhe Ndugai amesema "Kwa hakika nawashukuru Maspika wenzangu kwa kunipa dhamana hii ya kuwa Mwenyekiti wao, ni heshima kwangu binafsi lakini zaidi Kwa Tanzania. Ni matumaini yangu kwamba Bunge letu litaendelea kung'ara kitaifa na kimataifa tukiwa Bunge moja lenye Upendo na mshikamano".

Huu ni wadhifa wa nne kwa Mhe. Ndugai katika masuala ya Bunge kwenye medani ya Kimataifa. Amewahi kuwa Mwakilishi wa Nchi za Afrika Mashariki katika Kamati ya Utendaji ya Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Duniani mwaka 2008-2011, Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii ya Umoja wa Mabunge ya Afrika, Pacific na Carribbean na Jumuiya ya Ulaya  mwaka 2011-2014 na Rais wa Baraza la Mabunge ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC – PF)
Imetolewa na: 
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano 
Ofisi ya Bunge 
DODOMA 
 27 Julai 2017.

WANAHABARI WAJADILI UMUHIMU WA UHIFADHI NA UJIRANI MWEMA JIJINI TANGA

$
0
0
--
 Mkurugenzi wa Utalii na Masoko  kutoka Hifadhi za Taifa Tanzania, Ibrahim  Mussa akizungumza wakati wa Mjadala juu ya uhifadhi katika Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika leo  kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga, ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. 
 Mtaalam na Mtafiti wa Tembo,Dk Alfred Kikoti  akizungumza na Wahariri na Waandishi Waandamizi wa Vyombo  mbalimbali vya habari nchini  kuhusu Ikolojia ya tembo katika hifadhi nchini katika Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika leo  kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga, ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. 
 Mwenyekiti wa MisaTan , Salome Kitomari  akichangia jambo katika moja ya mada katika Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika leo  kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga, ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. 
 Ofisa anaeshughulikia masuala ya Ujirani mwema kutoka TANAPA, Ibrahim Ninga akitoa somo kwa Wanahabari nini Mamlaka yake imefanya katika kuakikisha hakuna migogoro baina ya hifadhi na Majirani
 Sehemu ya Wahariri na Waandishi Waandishi waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari  ambao wameshiriki Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika leo  kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga, ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. 

SERIKALI KUUNDA KAMATI YA KUKAGUA VIWANDA VYOTE NCHINI

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage ameunda kamati itakayo shirikisha wakuu wa mikoa yote Tanzania,  kwa Viwanda vyote vilivyobinafsishwa kuvitembelea na kuvikagua na kutoa taarifa ya maamuzi kwa viwanda vitakavyokuwa havifanyi kazi kwa kutokutii agizo la Rais Dkt. John Pombe Magufuli alilolitoa mkoani Pwani katika ziara yake ya kutembelea na kuzindua viwanda.
Waziri Mwijage ameyasema hayo leo ofisini kwake alipo kukutana na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali ambapo alisema adhma ya serikali ni kuhakikisha viwanda vinalindwa na kuongeza uzalishaji lakini pia serikali imejikita zaidi katika kuwasaidia wananchi kupata ajira katika viwanda.
Aliongeza kuwa, wengi walipenda kuanzisha viwanda kwa bei rahisi sana lakini wameshindwa kuviendeleza na wengine kufanya shughuli tofauti na iliyokusudiwa, Waziri amesema kamati hii itakaa Dar es salaam ambapo itashirikisha wataalamu kutoka idara mbalimbali za serikali na kupitia Viwanda vyote ili kuvikagua na kujiridhisha kabla ya kutoa maamuzi.

Pamoja na hilo la ubinafsishaji, Mwijage amezungumzia swala la Mchele wa bandia ambapo taarifa zimekuwa zikizagaa katika mitandao ya kijamii kuwa Tanzania tunazalisha mchele bandia,  na kusema kuwa Tanzania hakuna mchele bandia na taarifa hizi ambazo zimekuwa zikisambaa zinaharibu jina la nchi yetu kwani sisi ni wazalishaji na wasambaji wakubwa wa mchele kwa nchini mbalimbali.
Waziri ameahidi kufanya ufuatiliaji muda wote na atakapopatiwa taarifa zozote kuhusiana na upatikanaji wa mchele bandia kwa kuomba kupigiwa simu kupitia no. 0800110827.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam leo.
Wanahabari wakimsikiliza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

WADAU WA MAFUTA WAKUTANA KUJADILI UINGIZAJI WA NISHATI HIYO

SHUKRANI NA IBADA YA MAREHEMU MZEE MATTHEW GORDON KAYUZA

$
0
0
Marehemu Mzee Matthew Gordon Kayuza

Familia ya Marehemu Mzee Matthew Gordon  Kayuza ya Ada Estate Kinondoni Dar Es Salaam inapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa niaba ya koo za Kayuza, Daudi Kolawa, Samatta, Mbiza, Poyo, Sentimea, Chienela na Nshunju kwa kuwafariji kwa hali na mali kipindi chote cha kumuuguza na hatimaye kifo na mazishi ya baba yao mpenzi Mzee Matthew Gordon Kayuza aliyefariki tarehe 21/06/2017 katika hospitali ya Aga Khan na kuzikwa tarehe 24/06/2017 kwenye makaburi ya Kinondoni Dar Es Salaam

Shukrani za pekee ziwafikie wafuatao: Waheshimiwa Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Hamisi Juma, Jaji Kiongozi Ferdinand Wambali, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, na Mama Salma Kikwete. Uongozi na wafanyakazi wa NSSF, Indian School, Dar Es Salaam, na Bank M, Madaktari na manesi wa Aga Khan Hospitali DSM, Dr. Jerusalem Makotore, Dr Gabriel Ndunga na manesi Esther, Joyce na Neema ambao walikuwa wakimhudumia Mzee nyumbani, Wachungaji, wahudumu na kwaya ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Albano,Rev.Canon Albano Mbulinyingi, Jumuiya ya Mtakatifu Theresia ya Kanisa la Kristo Mfalme Kinondoni, majirani, ndugu na marafiki.  

Kutakuwa na mkesha wa kumaliza msiba leo Ijumaa tarehe 28/07/2017 kuamkia Jumamosi tarehe 29/07/2017 nyumbani kwa Marehemu Ada Estate, Kinondoni. Itafuatiwa na ibada ya shukrani siku hiyo hiyo ya Jumamosi saa mbili  asubuhi katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Posta Dar Es Salaam. Nyote mnakaribishwa.

“BABA MZEE MATTHEW KAYUZA TULIKUPENDA SANA ILA MUNGU AMEKUPENDA ZAIDI, PUMZIKA KWA AMANI, DAIMA UTAENDELEA KUISHI NDANI YA MIOYO YETU”.

MICHUZI TV: RAIS MAGUFULI AWATAKA WALIOBINAFSISHIWA VIWANDA NA HAVIFANYI KAZI WAVIRUDISHE

Viewing all 109935 articles
Browse latest View live




Latest Images