Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

TFF YATANGAZA MAKUNDI LIGI DARAJA LA KWANZA MSIMU 2017/18

$
0
0
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetangaza makundi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa timu 24 zitakazochuana msimu huu wa 2017/18 kuwania nafasi tatu muhimu za kupanda daraja kucheza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu wa 2018/19.

Kwa mujibu wa makundi hayo yaliyoratibiwa na Bodi ya Ligi ya TFF, kundi ‘A’ litakuwa na timu za African Lyon, Ashati United, Friends Rangers za Dar es Salaam, JKT Ruvu na Kiluvya United za Pwani, Mgambo JKT ya Tanga, Mvuvumwa ya Kigoma na Polisi Moro ya Morogoro.

Kundi ‘B’ zitakuwa timu za itakuwa na timu za Coastal Union ya Tanga; JKT Mlale ya Ruvuma; KMC ya Dar es Salam, Mawezi Market ya Morogoro, Mbeya Kwanza ya Mbeya, Mufundi United ya Iringa, Mshikamano na Polisi Dar za Dar es Salaam.

Kundi ‘C’ ina timu za Alliance School, Pamba na Toto African za Mwanza, Rihno Rangers ya  Tabora, Polisi Mara ya Mara, Polisi Dodoma ya Dodoma, Transit Camp ya Shinyanga na JKT Oljoro ya Arusha.

Kadhalika, TFF imeagiza timu za Ashanti United, Friends Rangers, KMC na Polisi Dar ya Dar es Salaam kuwasilisha majina ya viwanja vitakavyotumiwa na timu zao wakati wa ligi hiyo inayotarajiwa kuanza baadaye mwezi ujao.

Kutaja viwanja hivyo ni matakwa ya Kanuni ya 6 (1) za kanuni Mama ya VPL inayozungumzia Viwanja kadhalika kusomwa pamoja na Kanuni ya 11 inayozungumzia Leseni za Klabu kwamba kila timu haina budi kuwa na viwanja vya mcehi za nyumbani ikiwa ni masharti ya kupata leseni ya klabu.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AFUNGUA MAONYESHO YA VYUO VIKUU, ATAKA PROGRAMU ZA ELIMU YA JUU ZIWEZESHE WAHITIMU KUJIAJIRI

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) kuhakikisha kwamba programu zote zinazotolewa na taasisi za elimu ya juu zinawawezesha wahitimu kujiajiri na kuwa na sifa za ushindani katika soko la ajira kimataifa.

Amesema wakati umefika sasa kwa wasomi katika vyuo vyetu vikuu tujiridhisha kuwa mitaala inayotolewa kama inawaandaa wahitimu kupata taaluma na stadi za kuweza kujiajiri na kupambana na changamoto za kimaisha.

Ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Julai 26, 2017) wakati wa ufunguzi wa maonesho ya 12 ya Elimu ya Juu, jijini Dar es Salaam.  Amesema taasisi za elimu ya juu nchini ziangalie mitaala yake na kuimarisha mfumo wa ithibati na udhibiti wa ubora wa elimu na mafunzo ili kwenda sambamba na dunia ya kazi inayoendana na agenda ya maendeleo ya Taifa.

Waziri Mkuu amesema maonesho hayo ni jukwaa la kipekee ambalo litaibua mjadala sahihi kuhusu uhalali wa kozi zinazotolewa na vyuo husika vya elimu ya juu. “Hivyo mnayo nafasi ya kuonesha kwa vitendo uwezo wenu katika utafiti, ubunifu na matumizi ya sayansi na teknolojia zinazotumika katika maendeleo ya viwanda.”

Amesema ni vema mfumo wa ithibati na udhibiti wa ubora wa elimu na mafunzo ukaimarishwa ili kuhakikisha asilimia 60 ya wanafunzi wanahitimu shahada kwenye sekta ambazo zinachangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi.

Amesema taasisi za elimu ya juu ziweke mikakati ya kuinua na kuboresha taaluma  wanayoitoa ili ilete tija kwa maendeleo ya Taifa na Dunia. Pia kuanzisha program za mafunzo zenye kukidhi mahitaji na kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kuzingatia mahitaji ya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amezitaka taasisi hizo kuendelea kuimarisha mfumo wa udahili na kujipanga kutumia fursa za elimu na mafunzo ndani na nje ya nchi kwa makundi yote ya jamii kwa usawa katika ngazi zote hususan ufundi, hisabati, sayansi na teknolojia.

Pia Waziri Mkuu amesema ni wakati muafaka kwa taasisi za elimu ya juu nchini kuandaa mikakati ya kuongeza udahili kwa kuzingatia mahitaji ya rasilimali watu na ujuzi unaohitajika katika sketa zinazokua haraka mfano mafuta, gesi na madini.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu mtambo wa kuamia ndege waharibifu wa mazao kutoka kwa Mkuu wa Taasisi ya Tekinolojia ya Dar es salaam (Dar es salaam Insititute of Technology), Profesa Preksedis Ndomba (kulia) wakati alipotembelea banda la Taasisi hiyo katika Maonyesho ya Vyuo Vikuu yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnanzi Mmoja jijini Dar es salaam Julai 26, 2017. Kulia kwake ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea mabanda kabla ya kufungua Maonyesho ya Vyuo Vikuu kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Julai 26, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage (kulia kwake) pamoja na Viongozi wa TCU wakiimba wimbo wa taifa kabla ya Waziri Mkuu kufungua Maonyesho ya Vyuo Vikuu kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Julai 26, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na wawakilishi wa taasisi mbalimbali zilizoshiriki katika Maonyesho ya Vyuo Vikuu yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dr es salaam Julai 26, 2017.

Taasisi ya SUKOS yakabidhi Vifaa vya Zimamoto Hospitali ya Muhimbili Leo

$
0
0
Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji -SUKOS, leo ameikabidhi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) vifaa vya zimamoto ili kusaidia uokozi mara yanapotokea majanga ya moto.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Suleiman Kova amesema wameamua kutoa msaada huo katika hospitali hiyo kwa kuwa imekuwa ikitoa huduma nzuri za afya.

“Tulifanya utafiti tukavutiwa na huduma nzuri zinazotolewa Muhimbili hivyo tumeanza na Muhimbili na baadaye tutaenda kutoa msaada kwenye taasisi nyingine. Kama mnavyojua tunafanya kazi ya kijitolea,” amesema Kova.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru ameshukuru Muhimbili kupatiwa msaada huo na kwamba vimetolewa wakati muhafaka.

Mkurugenzi wa Ufundi, Gaudence Aksante amesema vifaa hivyo vitatunzwa ili viweze kutoa huduma iliyokusudiwa.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji -SUKOS, Suleiman Kova (kulia) akimkabidhi vifaa vya zima moto Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru kwa ajili ya kutoa huduma ya uokoaji endapo itatokea majanga ya moto katika maeneo ya kazi au majumbani. Kulia ni Mkurugenzi wa Ufundi, Gaudence Aksante.
Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru akishukuru baada ya kupokea msaada huo Leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Suleiman Kova na Mkurugenzi wa Ufundi, Gaudence Aksante akifuatilia tukio hilo.
Meneja wa Masoko na Mauzo wa Kampuni ya Astrade Tanzania, Abdallah Massawe akielezea matumizi ya kifaa maalumu cha kutoa taarifa mara gesi inapokuwa ikivuja kwenye mtungi. Kifaa hicho kinasaidia watumiaji wa gesi kuchukua taadhari mara gesi inapoanza kuvuja.
Mmoja wa wafanyakazi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji –SUKOS, Ramadhani KHamisi akionyesha jinsi ya kuzima moto baada ya kutokea mlipuko sehemu za kazi au majumbani.

MAHAKAMA KUU YATUPILIA MBALI SHAURI LA PST, TPBO DHIDI YA TPBC

$
0
0

Rais wa Shirikisho Ngumi za Kulipwa TPBC,  Chaurembo Palasa.



Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.



KESI iliyokuwa imefunguliwa katika Mahakama kuu na Kampuni Tatu za kuendesha biashara ya Ngumi Tanzania imetupiliwa mbali baada ya kushindwa kukidhi Vigezo.

Kampuni hizo za Puglist Syndicate of Tanzania (PST), Tanzania Professional (TPBO) na Tanzania Proffesional boxing Limmited zilifunguwa kesi ya kupinga kusajiliwa kwa Tanzania Proffesiona Boxing Commision na Baraza la michezo la Taifa.

Katika Kesi hiyo Kampuni hizi ziliungana ili kutaka "BMT" ieleze kwanini walikipa usajili chama cha kusimamia Ngumi za kulipwa wakati hawana uwezo wa kusajili michezo ya kulipwa.

Akizungumza kwa Simu kutoka Dar es salaam Rais wa Shirikisho lililoshtakiwa Chaurembo Palasa alisema Kesi hiyo iliyokuwa ikisikilizwa na Jaji Kihiyo imetupwa baada ya kutokidhi vigezo kisheria.

Alisema kesi hiyo ilifunguliwa na Emanuel Mrundwa Katika Mahakama  ya Temeke lakini ilishindwa kusikiliza shauri hilo kutokana na kukosa nguvu kisheria. Kesi hiyo ilielekezwa na kupelekwa Mahakama kuu ndipo Kampuni zilipoungana na kuomba kusikilizwa huku wakiishtakiwa wakiongezeka kuwa TPBC na BMT.

BMT na TPBC ililazimika kutoa vielelezo vya kupinga kushtakiwa na Kampuni hizo kutokana na Baraza hilo kuwepo kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Bunge.

Kutokana na ombi lao kukosa vigezo vya Kisheria Mahakama Kuu imeamuwa kuliondowa Shauli hilo na kuwataka walalamikaji kulipa Gharama za kesi. Gharama za kesi hazikuweza kujulikana mara moja kutokana kuandaliwa ofisi ya Mwanasheria mkuu wa Serikali. Kutokana na kushindwa kwa kesi hiyo TPBC itabaki kuwa Kamisheni ya Ngumi za kulipwa Tanzania na sasa inapaswa kuendelea na mchakato wa kuwa na vyama vya Mikoa.

SHUKRANI NA IBADA

$
0
0
Mzee Matthew Gordon Kayuza

Familia ya Marehemu Mzee Matthew Gordon  Kayuza ya Ada Estate Kinondoni Dar Es Salaam inapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa niaba ya koo za Kayuza, Daudi Kolawa, Samatta, Mbiza, Poyo, Sentimea, Chienela na Nshunju kwa kuwafariji kwa hali na mali kipindi chote cha kumuuguza na hatimaye kifo na mazishi ya baba yao mpenzi Mzee Matthew Gordon Kayuza aliyefariki tarehe 21/06/2017 katika hospitali ya Aga Khan na kuzikwa tarehe 24/06/2017 kwenye makaburi ya Kinondoni Dar Es Salaam

Shukrani za pekee ziwafikie wafuatao: Waheshimiwa Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Hamisi Juma, Jaji Kiongozi Ferdinand Wambali, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, na Mama Salma Kikwete.

Uongozi na wafanyakazi wa NSSF, Indian School, Dar Es Salaam, na Bank M

Madaktari na manesi wa Aga Khan Hospitali DSM, Dr. Jerusalem Makotore, Dr Gabriel Ndunga na manesi Esther, Joyce na Neema ambao walikuwa wakimhudumia Mzee nyumbani
Wachungaji, wahudumu na kwaya ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Albano,Rev.Canon Albano Mbulinyingi, Jumuiya ya Mtakatifu Theresia ya Kanisa la Kristo Mfalme Kinondoni, majirani, ndugu na marafiki  

Kutakuwa na mkesha wa kumaliza msiba Ijumaa tarehe 28/06/2017 kuamkia Jumamosi tarehe 29/07/2017 nyumbani kwa Marehemu Ada Estate, Kinondoni ikifuatiwa na ibada ya shukrani siku hiyo ya Jumamosi saa 2 asubuhi katika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Albano Posta Dar Es Salaam. Nyote mnakaribishwa.

“BABA MZEE MATTHEW KAYUZA TULIKUPENDA SANA ILA MUNGU AMEKUPENDA ZAIDI, PUMZIKA KWA AMANI, DAIMA UTAENDELEA KUISHI NDANI YA MIOYO YETU”.

TANZANIA YASHIRIKI KIKAO CHA 71 CHA BODI YA UKAGUZI YA UMOJA WA MATAIFA (UNBOA)

$
0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG )wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Prof Mussa J Assad wa pili kutoka kushoto akiwa na wajumbe wa Bodi ya Umoja wa Mataifa baada kikao cha 71 kinachoendelea mjini New York Marekani, kikao hicho kinafanyika kwa muda wa siku mbili.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu (CAG) za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Profesa Mussa Assad ambaye ni mjumbe wa Bodi ya Ukaguzi ya Umoja wa Mataifa (UNBoA), jana tarehe 25 Julai, 2017 ameshiriki kuidhinisha ripoti za kaguzi za shughuli za Umoja wa Mataifa kwa mwaka ulioishia tarehe 31 Desemba 2016, kwenye kikao cha 71 cha Bodi ya Ukaguzi ya wanachama wa Umoja wa Mataifa kinachoendelea Mjini New York, nchini Marekani.

Katika kikao hicho, wajumbe wa bodi hiyo walipitia na kusaini ripoti ishirini na nane (28) za ukaguzi wa shughuli za Umoja wa Mataifa. Kati ya ripoti zilizoidhinishwa na wajumbe wa Bodi hiyo, ripoti kumi na moja (11) zilitokana na kaguzi zilizofanywa na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (NAOT) na kuwasilishwa na CAG, Prof. Mussa Assad kwenye kikao hicho cha Bodi. Aidha, ripoti kumi na saba (17) zilizosalia zilitokana na ukaguzi uliofanywa na Ofisi za Ukaguzi wa Hesabu za Serikali za India na Ujerumani.
Katibu Mkuu umoja wa Mataifa Bwana Antonic Guterres akizunguza na wajumbe wa Bodi ya Ukaguzi wa Umoja wa Taifa katika kikao cha Bodi kilichofanyika mjini New York Marekani hivi karibuni.

Ripoti kumi na moja zilizowasilishwa na Prof. Assad ni kaguzi za Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Shirika la Idadi ya Watu Duniani la Umoja wa Mataifa (UNFPA), Shirika la Ujenzi na Misaada la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wakimbizi wa Palestina na Mashariki (UNRWA), Mfuko wa Akiba kwa Watumishi wa UNRWA Wakazi (UNRWA – SPF), Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN – Women), Mfuko wa Ukuzaji Mitaji la Umoja wa Mataifa (UNCDF), Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Makazi (UN Habitat), Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP), Mahakama ya Umoja wa Mataifa inayoshughulika na Mauaji yaliyotokea Rwanda (ICTR), Mahakama ya Umoja wa Mataifa inayoshughulika na Mauaji yaliyotokea Yugoslavia ya zamani (ICTY), Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kupunguza shughuli za mahakama za kimataifa (IRMCT).

NEWS ALERT: WANACHAMA NANE WA CUF WALIOFUKUZWA WAKOSA UBUNGE

$
0
0
Kufuatia barua aliyopokea Spika wa Bunge Mhe. Job Yustino Ndugai kutoka kwa Mwenyekiti Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Kaimu Katibu Mkuu Mhe. Magdalena Hamisi Sakaya (Mb) wa Chama cha Wananchi (CUF), Mheshimiwa Spika angependa kuwaarifu Watanzania wote kwamba amejiridhisha kuwa Wabunge hao wamefukuzwa Uanachama kulingana na taratibu za Chama hicho na hivyo wamekosa sifa za kuendelea na Ubunge. Wabunge hao ni: - 

1. Mhe. Severina Silvanus Mwijage, (MB);

2. Mhe. Saumu Heri Sakala, (MB);

3. Mhe. Salma Mohamed Mwassa, (MB);

4. Mhe. Riziki Shahari Mngwali, (MB);

5. Mhe. Raisa Abdallah Mussa, (MB);

6. Mhe. Miza Bakari Haji, (MB);

7. Mhe. Hadija Salum Ally Al-Qassmy, (MB); na

8. Mhe. Halima Ali Mohamed, (MB).

Hivyo, kwa mamlaka aliyonayo kwa kuzingatia kifungu cha 67(1)(b) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 kikisomwa pamoja na kifungu 37(3) cha Sheria ya Uchaguzi Sura 343 kama ilivyojadidiwa Mwaka 2015, Mheshimiwa Spika ametangaza nafasi hizo kuwa wazi na pia kumuandikia Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili aendelee na hatua zinazostahili kujaza nafasi hizo kwa Mujibu wa Sheria na Taratibu zilizopo.

Imetolewa na: 
Ofisi ya Spika,
S. L. P. 941,
DODOMA.
26 Julai, 2017

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA MAADHIMISHO YA MIAKA 100 YA SKAUTI, AWAVISHA NISHANI VIONGOZI WASTAAFU

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akihutubia wakati wa ufunguzi wa sherehe za miaka 100 ya Skauti Tanzania kwenye ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimvisha nishani Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Ali Hassan Mwinyi ambaye alikuwa mlezi wa pili wa chama cha Skauti Tanzania kuanzia mwaka 1985 mpaka 1995 wakati wa sherehe za miaka 100 ya Skauti nchini.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimvisha nishani Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alikuwa mlezi wa pili wa chama cha Skauti Tanzania kuanzia mwaka 2005 mpaka 2015 wakati wa sherehe za miaka 100 ya Skauti nchini zilizofanyika kwenye ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimvisha nishani Bi. Fatma Karume kwa niaba ya Hayati Mhe. Abeid Amani Karume ambaye alikuwa Rais wa kwanza wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambaye alikuwa mstari wa mbele katika kuhimiza shughuli za Vijana wa skauti katika visiwa vya Unguja na Pemba kwenye  sherehe za miaka 100 ya Skauti nchini zilizofanyika kwenye ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimvisha nishani Rais Mstaafu wa Awamu wa Sita wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Amani Abeid Karume ambaye alikuwa mlezi wa pili wa chama cha Skauti Tanzania kuanzia mwaka 2000 mpaka 2010 wakati wa sherehe za miaka 100 ya Skauti nchini zilizofanyika kwenye ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimvisha nishani Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim ambaye alikuwa skauti tangia shuleni na alipokuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika ambapo mwaka 2001 alipendekeza kuwe na siku ya SKAUTI AFRIKA itakayokuwa inaadhimishwa kila tarehe 13 mwezi Machi . 

CHUO CHA MUSLIM MOROGORO WATOA FURSA YA WATANZANIA KUSOMA LUGHA YA KICHINA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MAONESHO ya Elimu ya Juu yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja yamefunguliwa rasmi leo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Kassim Majaliwa Kassim huku yameonesha mwitikio mzuri kwa vyuo mbalimbali vilivyojitokeza kudahili wanafunzi wanaotaka kujiunga na kozi  tofauti kwenye vyuo vyao.

Ili kutoa fursa ya elimu kwa wanafunzi wanaojiunga na vyuo hivyo, Chuo cha Muslim Morogoro kimewataka wanafunzi wachangamkie fursa ya elimu ya lugha ya Kichina inayopatikana katika chuo chao kwani kimeweza kuwasaidia wanafunzi wengine kufahamu lugha hiyo pamoja na kupata nafasi za kusoma nchini China bure.

Akizungumza na Globu ya Jamii, Afisa Habari wa Chuo cha Muslim Morogoro Ngaja Mussa amesema kuwa wanatoa kozi ya elimu hiyo ya lugha ya kichina kwa wanafunzi wote wanaotaka kuifahamu na pia utakaposoma kwa mwaka mmoja na kuifahamu vizuri lugha hiyo unapata nafasi ya kusoma nchini China.

Ngaja amesema kwa sasa kuna walimu takribani saba wanatoa mafunzo ya elimu hiyo katika chuo chao, mbali na kozi hiyo ya lugha ya Kichina wanatoa pia kozi mbalimbali katika ngazi ya astashahada, stashahada na shahada.

Kwa ngazi ya shahada kwa mwaka 2017/18  wana kozi za Bachelor of Arts with Education pamoja na Bachelor of law with Shariah huku ngazi ya Astashahada na Stashahada wana kozi za  Procurement and Logistics Management, Journalism, Medical Labaratory Technology, Science and Laboratory Technology, Laws with Shariah pamoja na Islamic Bankinga and Finance.
 Afisa Habari wa Chuo cha Muslim Morogoro Ngaja Mussa akitoa maelezo wa wageni waliotembelea banda la Chuo hicho na kuwaelezea namna wanavyofanya udahili wa wanafunzi kwa mwaka 2017/18 pamoja na elimu ya lugha ya Kichina inayopatikana katika chuo chao kwenye Maonesho ya Elimu ya Juu yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.
Mkufunzi wa Chuo cha Muslim Morogoro, Faraji Tamim akitoa maelezo wa wageni waliotembelea banda la Chuo hicho na kuwaelezea namna wanavyofanya udahili wa wanafunzi kwa mwaka 2017/18 pamoja na elimu ya lugha ya Kichina inayopatikana katika chuo chao kwenye Maonesho ya Elimu ya Juu yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.
 Wanafunzi akitoa maelezo wakati walipotembelea banda la Chuo hicho na kuwaelezea namna wanavyofanya udahili wa wanafunzi kwa mwaka 2017/18 pamoja na elimu ya lugha ya Kichina inayopatikana katika chuo chao kwenye Maonesho ya Elimu ya Juu yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.
Mkufunzi wa Lugha ya Kichina Sun Fei akielezea jambo kwa mwanafunzi aliyefika katika banda la Chuo cha Muslim Morogoro namba ya kujiunga na Chuo chao na kusoma elimu ya lugha ya Kichina. Picha na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA YANAWEZA KUEPUKIKA KWA KULA VYAKULA VYA ASILI PAMOJA NA KUFANYA MAZOEZI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Magonjwa yasiyoambukizwa yanaweza  kuepukika kwa kutumia vyakula vya asili pamoja na kufanya mazoezi ambapo hakuna gharama inaweza kufanya mtu kuchangia. Magonjwa hayo ambayo ni Kisukari, shinikizo la Damu, pamoja na Unene wa kupindukia.

 Hayo aliyasema Mwenyekiti wa Kikundi cha Mtambani  kilichopo Mlandizi wilayani Kibaha, mkoani Pwani, Mohamed Pongwe wakati akizungumza na Michuzi Blog, amesema kuwa magonjwa yasiyombukizwa yanaweza kuepukika kwa kula vyakula visivyo na mafuta pamoja na kufanya mazoezi katika mazingira wanayoishi.

Amesema walipata elimu baada ya Shirika la Help Age International  kupitia mradi wa Afya kwa Rika Zote  ambapo  waliweza kuanza ufugaji wa kuku pamoja na kilimo cha mboga mboga.

Pongwe amesema kuwa wanafanya kilimo cha mboga mboga  na ufugaji wa kuku  ambapo wanauza na fedha zinazopatika zinaingia katika kikundi pamoja na wao wenyewe kula mboga mboga na mayai na nyama za kuku hali ambayo imeweza kuboresha afya zao.

Aidha amesema katika miradi hiyo wameza kupata laki tano ambapo uzalishaji unaendelea katika maeneo yote ikiwa ni pamoja na kubadilika kiuchumi katika kikundi.
 Mwenyekiti wa Kikundi Cha Mtambani, Mohaamed Pongwe akizungumza  katika sehemu wanayofanya kilimo cha mboga mboga.
 Mwanakikundi, Mwajuma Fanuel akizungumza na katika sehemu ya kilimo cha mbogamboga .
 Baadhi ya wanakikundi wakiweka mbolea ya kinyesi cha kuku katika shamba la mbogamboga.
Wanakikundi wa Mtambani Mlandizi wakiwa katika picha ya pamoja 

TAKUKURU MWANZA YATHIBITISHA KUWAHOJI WANAFAMILIA WA SOKA NA KUWAACHILIA KWA DHAMANA

$
0
0




Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoani Mwanza Mhandisi Ernest Makale.


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoani Mwanza (TAKUKURU) imethibitisha kuwahoji wanafamilia wa soka wakiwemo Mjumbe Chama cha Soka Wilaya ya Ubungo (UFA) Shaffih Dauda na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es salaam (DRFA) Almas Kasongo.


Mbali na hao TAKUKURU wamethibitisha pia kuwahoji Elias Mwanjali, Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo, Mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Mbeya Bw. Elias Mwanjaa , Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Mguu mkoa wa Shinyanga Benasta Lugola na wajumbe wa mikoa ya jirani kwasababu ya kuwepo kwa viashiria vya rushwa na kampeni.

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoani Mwanza Mhandisi Ernest Makale amethibitisha kuwahoji kwa wanafamilia hao wa mpira ambapo waliwashikilia tokea jana saa 3 usiku na wameachiwa kwa dhamana huku uchunguzi ukiendelea na watakapojiridhisha wanaweza kuwakamata tena.

Taarifa inasema kuwa wanafamilia hao walitumia mgongo wa Ndondo Cup kufanya jambo lao usiku wa saa 3 jana na ndipo walipotiliwa shaka na kufuatiliwa na kutiwa mikononi mwa Takukuru ambao wamethibitisha kuwashikilia tokea jana usiku na kuwaachia kwa dhamana

WANAFUNZI WAJITOKEZA KWA WINGI KATIKA MAONESHO YA ELIMU YA JUU VIWANJA VYA MNAZI MMOJA

$
0
0
Wanafunzi na watu mbalimbali wakiwa katika banda la Chuo Kikuu Dar es salaam wakifuatilia namna ya kudahili kozi mbalimbali za Chuo hicho kwenye maonesho ya elimu ya Juu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Wanafunzi na watu mbalimbali wakiwa katika Global Education Likn wakifuatilia namna ya kudahili nje ya nchi katika vyou  mbalimbal kwenye ikiwa ni maonesho ya elimu ya Juu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Wanafunzi na watu mbalimbali wakiwa katika banda la Chuo cha Ardhi wakifuatilia namna ya kudahili  kozi mbalimbali za Chuo hicho kwenye maonesho ya elimu ya Juu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Wanafunzi na watu mbalimbali wakiwa katika banda la Dar es salaam Institute of Technology wakipata maelezo mbalimbali ya namna ya wanafunzi wa chuo hicho wanavyotengeneza vifaa kazi mbalimbali pamoja kutoa nafasi kwa wanafunzi kudahili  kozi mbalimbali za Chuo hicho kwenye maonesho ya elimu ya Juu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Wanafunzi na watu mbalimbali wakiwa katika banda la Chuo cha Mzumbe wakifuatilia namna ya kudahili  kozi mbalimbali za Chuo hicho kwenye maonesho ya elimu ya Juu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Wanafunzi na watu mbalimbali wakiwa katika banda la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) wakipata maelezo ya  namna ya kudahili  kozi za Chuo hicho kwenye maonesho ya elimu ya Juu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. Picha na Zaynab Nyamka wa Globu ya Jamii

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

MAHAKAMA YA PILI YA WATOTO NCHINI YAZINDULIWA MBEYA

$
0
0

Na Lydia Churi-Mahakama, Mbeya

Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma leo amezindua rasmi Mahakama ya watoto katika jiji la Mbeya na kufanya idadi ya Mahakama hizo nchini kufikia mbili. Mahakama ya kwanza ya watoto iko Kisutu jijini Dar es salaam.

Mahakama hii ya Watoto iliyoanza kufanya kazi rasmi Aprili 18 mwaka huu jijini Mbeya pamoja na ile ya Kisutu zina kazi kubwa ya kuamua kesi za watoto wanaojikuta wana ukinzani na Sheria zinazohusu watoto nchini pamoja na kutafsiri sheria hizo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania alisema maendeleo endelevu ya Tanzania yatajengwa kwa misingi ya haki za watoto huku akinukuu andiko la shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na watoto (UNICEF) lisemalo maendeleo ya taifa lolote yatakamilika baada ya watoto kuwa na afya njema, salama pamoja na kupata elimu.

Alisema uzinduzi wa jengo la Mahakama hiyo ya watoto unaashiria safari ndefu iliyonayo Tanzania ya kuhakikisha haki za watoto zinalindwa kwa kuwa pia bado kuna mikoa mingi ambayo inahitaji huduma hii muhimu.

Prof. Juma alisema kazi kubwa ya Mahakama ya Tanzania ni kutoa tafsiri pana ya sheria zinazohusu haki za watoto ili kupanua wigo wa ulinzi kwa watoto huku akiwataka Majaji na Mahakimu nchini kutafsiri sheria hizo ili zitekeleze wajibu wao kisheria.

Akitolea mfano wa Sheria ya Watoto namba 21 ya mwaka 2009, Kaimu Jaji Mkuu alisema sheria hii inashirikisha mihimili yote mitatu hivyo haki zote zinazotajwa na sheria hii ni lazima zipatikane inavyostahili. Prof. Juma pia amewataka Mahakimu wanaosikiliza kesi za watoto kuainisha mapungufu ya sheria hii na kuyawasilisha kwenye kamati ya Jaji Mkuu inayohusu masuala ya Sheria. 


Kaimu Jaji Mkuu Wa Tanznaia Mhe. Prof. Ibrahim Juma Akifungua Pazia Kuashiria Uzinduzi Wa Mahakama Ya Watoto Leoi Jijini Mbeya. Katikati Ni Mwakilishi Wa Unicef Nchini, Stephanie Shanler Na Kushoto Ni Jaji Kiongozi Wa Mahakama Kuu Ya Tanzania Mhe. Ferdinand Wambali. 
Kaimu Hjaji Mkuiu Wa Tanznaia Mhe. Porof. Ibrahim Juma Akikata Utepe Kuzindua Jengo La Mahakama Ya Watoto Leo Jijini Mbeya. 
Kaimu Jaji Mkuu Wa Tanznaia Akizungumza Wakati Wa Hafla Hiyo 
Kaimu Jaji Mkuu Wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma Akiwa Katika Picha Ya Pamoja Na Viongozi Wa Mahakama Ya Tanzania Mara Baada Ya Kuzindua Mahakama Ya Watoto Leo Jijini Mbeya 


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Audio Release: Mrisho Mpoto kuachia 'Kitendawili' baada ya 'Sizonje' kubaki njia panda

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki wa asili nchini Tanzania, Mrisho Mpoto baada ya kufanya vizuri na wimbo ‘Sizonje’ ambao ulipendwa na watu wa rika zote ndani ya nchi na kimataifa, hatimaye Jumatatu hii (tarehe 1 August 2017) anatarajia kuachia wimbo wake mpya ‘Kitendawili’ akiwa amemshirikisha mkali wa nyimbo za mahaba, Kassim Mganga.

Wimbo uliopita ‘Sizonje’ wa muimbaji huyo uliacha maswali mengi kwa wapenzi wa muziki wake kutokana namna maishiri ya wimbo huo yalivyokuwa magumu huku wengi wakidai huwenda wimbo huo alimuimbia Rais John Pombe Magufuli kitu ambacho hakuwahi kukiweka wazi licha ya Rais huyo kutamka mara kadhaa katika mikutano yake kwamba wimbo huo alikuwa kwaajili yake.

Sasa mshairi huyo ametangaza ujio wake mpya na wimbo ‘Kitendawili’ akiwa Kassim Mganga ikiwa ni wimbo wa kwanza ambao unawakutanisha wawili hao ambao kila mmoja ni mkali kwa upande wake.
Mpoto amesema amerekodi wimbo wake huo mpya katika studio za Combination Sound chini ya producer mahiri, Man Walter ili kupata ladha tofauti ya muziki wake.

“Mimi naamini muziki ni ladha, nyimbo zangu nyingi nimefanya ndani ya studio yangu chini ya producer Alan Mapigo na zilifanya vizuri. Lakini katika project hii mpya nikaona sio mbaya kama nikibadili dhala ya beat na kupata kitu tofauti na kweli Man Walter amefanya kitu kizuri sana, menejimenti pamoja na watu wangu wa karibu wamefurahishwa na kile ambacho amefanya ,” alisema Mpoto.

Aliongeza, “Pia katika wimbo huu utamsikia Kassim Mganga, huyo ni mtu mpya kabisa katika nyimbo zangu, amefanya kitu kikubwa sana ambacho bila shaka kitawashangaza mashabiki wengi wa muziki. Kwahiyo napenda kuwaambia mashabiki wakae mkao wa kula, Mpoto nimerudi upya na kazi ni nzuri.”
Mjomba amewataka mashabiki wake wa muziki kuusubiria kwa hamu wimbo huo ambao utaachiwa siku ya Jumatatu (tarehe 1 mwezi August) kupitia mitandao ya kijamii (blogs) pamoja na redio.
Pia mshairi huyo amesema siku hiyo ataachia kwanza audio na baada ya siku kadhaa atatoka video ambayo amedai ndani yake kuna mambo mengi mapya ambayo hayajazoeleka kwenye muziki wake.
Kwa upande wa muimbaji Kassim Mganga ambaye ameshiriki ndani project ya namna hiyo kwa mara ya kwanza na Mrisho Mpoto, amesema amefurahishwa na namna wimbo huo ulivyoandaliwa huku akiwataka mashabiki kusubiria muziki mzuri.
“Kusema kweli hii ni mara yangu ya kwanza kufanya kazi ya namna hii na Mrisho Mpoto ambaye hata mimi ni shabiki wa muziki wake. Nimefurahishwa sana na kile tulichokifanya, binafsi nafarijika kuona ushirikiano wetu jinsi ulivyozalisha kitu kikubwa katika muziki, natamani ngoma itoke hata kesho ili mashabiki waone kitu ambacho nakizungumzia. Kwahiyo mashabiki wa muziki kwa umoja wetu tusubirie muziki mzuri ambao utateka fikra na kutoa burudani kwa mashakibiki,” alisema Kassim Mganga.

LADIES WHO INSPIRE – BEATRICE NDUNG’U

$
0
0

BEATRICE NDUNG’U is not just a GOAL getter but also a pride of Africa who has successfully impacted sister nations she had the opportunity of reaching out to. There is no particular age for one’s vision to be discovered, which also helped Beatrice in Nurturing her dreams and plans for the future from the bright age of 19. EM’S DAMILOLA SHOTE shares this bit in the interview with co-founder Wolfpack agency.


PLEASE INTRODUCE YOURSELF BRIEFLY TO EM... Beatrice Ndung’u is a Kenyan, but a brand in Africa. A motivational speaker, Public relations, media and creative marketing guru. I am a Jill of all trades. I co-own a Public relations agency in Tanzania known as Wolfpack www.wolfpacktz.com which manages some of the biggest names in East Africa, from companies, to celebrities to people in Government. I also co-own an importing and logistics company in Kenya and Tanzania known as Afrochina where we bring in anything you want from China to Africa at an affordable wholesale price. 

Article 13

Dkt. Mwakyembe atoa shukrani kwa Watanzania

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo, Sanaa na Burudani, Dkt. Harrison Mwakyembe amewashukuru Watanzania kwa ushirikiano mkubwa waliompa katika kuombeleza kifo cha mkewe Linah Mwakyembe kilichotokea usiku wa Julai 15 mwaka huu kwenye Hospitali ya Aga Khan ya Jijini Dar es salaam.
Dkt. Mwakyembe pia amemshukuru Rais John Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa mchango mkubwa walioutoa katika kumuuguza mkewe.
Dkt. Mwakyembe ametoa shukrani hizo  Julai 26 wakati akizungumza na wanahabari nyumbani kwake Kunduchi wilayani Kinondoni.
Mbali na hao, Dkt. Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Kyela Mkoani Mbeya, amewashukuru viongozi wote wa dini akiwamo Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zuberi na maaskofu.
"Wanafamilia tutakumbuka moyo adhimu na upendo na ushirikiano tulioupata kutoka Katibu Mkuu wa wizara hii Profesa Elisante Ole Gabriel na viongozi wengine waandamizi wa Serikali. Mwisho kabisa Wanakyela kwa uvumilivu wao katika kipindi hiki kigumu," amesema Dkt. Mwakyembe.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari (hawapo katika picha) leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa neno la shukrani kwa wote walioshiriki katika kumfariji kipindi cha msiba wa mke wake mpendwa Bi. Linah George Mwakyembe.

MNUSO MKONGWE KULIKO YOTE WA OLD SCHOOL REUNION COLUMBUS, OHIO - USIPIME ZIMEBAKI WIKI 5 TU

$
0
0

Kutokana na maombi ya wachezaji wa soka wanaokuja Columbus kutoka Ulaya kucheza gemu la Simba na Yanga, mtanange wa Simba na Yanga utachezwa baada ya mpira wa kikapu siku  ya Jumamosi Sept 2, 2017. ANDAA KIBUBU!

HOTELS IN COLUMBUS

Hampton Inn Columbus I-70 E/Hamilton Road

2093 S Hamilton Rd, Columbus, OH 43232
hamptoninn3.hilton.com
(614) 552-2400

Holiday Inn Express & Suites Columbus Southeast
4041 Hamilton Square, Groveport, OH 43125
ihg.com
(614) 920-2400

Hawthorn Suites by Wyndham Airport Columbus East
2084 S Hamilton Rd, Columbus, OH 43232
wyndhamhotels.com
(614) 864-8844

La Quinta Inn Columbus Airport Area
2447 Brice Rd, Reynoldsburg, OH 43068
laquintacolumbusairport.com
(614) 866-6456

Comfort Suites Columbus
5944 Scarborough Blvd, Columbus, OH 43232
choicehotels.com
(614) 552-2525

Days Inn & Suites Columbus East Airport
2100 Brice Rd, Reynoldsburg, OH 43068
wyndhamhotels.com
(614) 864-1280

Courtyard by Marriott Columbus Airport
2901 Airport Dr, Columbus, OH 43219
marriott.com
(614) 475-8530

TANZANIA: WOLRD MUST WORK TOGETHER TO CREATE MULTILATERAL, DEMOCRATIC AND TRANSPARENT INTERNET GORVERNACE SYSTEM

$
0
0
Deputy Minister for Information, Culture, Arts and Sports Hon.. Annastazia James Wambura (MP) speaking during the closing session of the New Media Round table meeting held yesterday at JNICC in Dar es Salaam.

By Tanzania Information Service-MAELEZO

Tanzania has urged international community to enhance dialogue and cooperation in order to promote transformations leading to multilateral, democratic and transparent global internet governance system.

Speaking at the closing of the one day New Media Round Table held at Mwalimu Nyerere Convention Centre in Dar Es Salaam, Deputy Minister for Information, Culture, Arts and Sports Ms Anastazia Wambura said the world has to take a collective action to guarantee a peaceful, secure, open and cooperative cyberspace.

“A secure, stable and prosperous cyberspace is of great significance to all countries and the world” She said and insisted that cyberspace should neither become a battle field for countries to wrestle with one another nor a hotbed for crimes.

In this respect, the Deputy Minister called for countries to work together in addressing cyberspace criminal activities among other terrorism, phonography, drug trafficking, money laundering and gambling.

“All cybercrimes, either commercial cyber theft or hacker attacks against government networks should be firmly combated in accordance with relevant laws and international conventions” she said and cautioned on double standards in dealing with such crimes.

The Deputy Minister noted that “cyberspace is not a place beyond the rule of law” hence countries must build a good order in cyberspace in accordance with the law to protect the legitimate rights and interest of all internet users.

“Cyberspace is virtual but players are real. Everyone should abide by the law with the rights and obligations of parties concerned clearly defined”, she said and added that cyberspace must be governed, operated and used in accordance with law, so that the internet could enjoy sound development under the rule of law.

The Deputy Minister asserted that global community should hold the future of the cyberspace therefore the members of international community should step up communication, broaden consensus and deepen cooperation to build a community of shared future in cyberspace. She reminded the participants which included media, government officials and private sector that maintaining cyber security was a shared responsibility of the whole international community because no one was invulnerable from it.

“All countries should work together to contain the abuse of information technology, oppose cyber surveillance and cyber-attacks and reject arms race in cyberspace” The Deputy Minister told Round Table participants.

The Media Round was opened by Minister for Works, Transport and Communication Professor Makame Mbarawa who reiterated government resolve to continue with its efforts to implement National ICT Broadband Backbone project and its measures to ensure cyber environment was free from crimes.

The Round Table was also attended by Chinese Vice Minister for National Cyberspace Administration Mr. Ren Xianling who urged China and Tanzania to use social media to strengthen relations between the two countries.

Also in attendance was Chinese ambassador to Tanzania Dr. LU Youking who told participants that media was very important tool in strengthening excellent relations existing between the two countries and the cyber media round table demonstrated how closer media of the two countries were.
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images