More Channels
Showcase
Articles on this Page
(showing articles 36321 to 36340 of 65431)
- 07/19/17--11:42: _Kiwanja Kinauzwa Bu...
- 07/19/17--12:09: _BBC DIRA YA DUNIA J...
- 07/19/17--12:19: _Introducing "HAPA W...
- 07/19/17--12:24: _SPORTPESA YATOA SHU...
- 07/19/17--20:00: _ Mapacha walioungan...
- 07/19/17--15:37: _ BALOZI SEIF AKITAK...
- 07/19/17--16:07: _Utalii wa Ndani : I...
- 07/19/17--16:46: _NAIBU WAZIRI MANYAN...
- 07/19/17--16:50: _INTRODUCING "NADOND...
- 07/19/17--16:59: _MWANASHERIA MKUU WA...
- 07/19/17--20:30: _MAKALA YA SHERIA: K...
- 07/20/17--00:00: _MISS TANGA TALK SHO...
- 07/20/17--02:00: _MAGAZETI YA ALHAMIS...
- 07/19/17--22:07: _MAKILAGI: WATAKAOTU...
- 07/20/17--00:22: _TANZIA: MAMA WA MZA...
- 07/20/17--00:29: _HABARI NJEMA KWA WA...
- 07/20/17--01:49: _RAIS DKT MAGUFULI A...
- 07/20/17--01:57: _VIJANA WA ZAMANI CO...
- 07/20/17--02:03: _WAZIRI MWAKYEMBE AW...
- 07/20/17--02:08: _SITAVUMILIA HATI CH...
(showing articles 36321 to 36340 of 65431)
Channel Description:
Most read Swahili blog on earth
Kipo Mita 800 kutoka Barabara kubwa iendayo Bagamoyo. Kiwanja kimepimwa, kina hati na kipo katika eneo lililopangwa na kuendelezwa vizuri.
Bei: Tshs. 40m/- (maelewano yapo) na malipo yanaweza kufanywa kwa awamu
mbili.
Mawasiliano: +255 713 576464 au +1 832 734 3292
(ikiwa haipatikani acha sms whatsapp)
Email: roseodessa@yahoo.com
0 |
|
0 |
|
Habari na Picha na Richard Mwaikenda
Akizungumza wakati wa mkutano huo, Tarimba alisema kuwa ziara ya Everton nchini imekuwa ni ya mafanikio makubwa kimichezo, kiuchumi, kijamii na hasa kuutangaza vilivyo utalii wa Tanzania Duniani.
Tarimba hakusita pia kuishukuru Ikulu kwa kuwapa sapoti kubwa kufanikisha ziara ya Everton hasa katika masuala ya kumpata mgeni rasmi, Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan pamoja na kuruhusu vyombo vya dola kwa ajili ya usalama wa timu hiyo.
"Kwa niaba ya SportPesa ambao ndiyo wadhamini wakuu wa timu hiyo, tutakuwa wachoyo wa fadhila kama tutashindwa kuwashukuru wadau wote ambao kwa namna moja ama nyingine walituunga mkono katika kuhakikisha kuwa maandalizi ya ziara hii yanafanikiwa." Alisema Tarimba na kuongeza kuwa...
Napenda Kumshukuru Rais John Magufuli kwa kutoa baraka zake, lakini pia nipende kumshukuru Makamu wake Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa utayari wa kuwapokea wageni wetu ."
Alimshukuru pia Waziri wa Habari, Utamadjuni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe kwa niaba ya wizara hiyo kwa kuwa bega kwabega katika jukumu hilo hizo. Pia hakusita kutoa pole kwa waziri huyo kwa kufiwa na mkewe.
Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa Kampuni ya Sportpesa, Tarimba Abbas akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, ambapo alitoa shukrani kwa wanahabari, vyombo vya dola, serikali na watanzania kwa kufanikisha ziara ya timu ya Everton ya Uingereza hapa nchini.
Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa Kampuni ya Sportpesa, Tarimba Abbas akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, ambapo alitoa shukrani kwa wanahabari, vyombo vya dola, serikali na watanzania kwa kufanikisha ziara ya timu ya Everton ya Uingereza hapa nchini.
0 |
|
0 |
|
Na Francis Godwin, Iringa
SERIKALI ya wilaya ya Kilolo na mbunge wa kilolo Mhe. Venance Mwamoto wamewapongeza kwa zawadi za maandalizi ya chuo kikuu mapacha Maria na Consolata Mwakikuti (19) waliofanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kidato cha sita mwaka huu.
Wakikabidhi zawadi hizo kwa mapacha hao jana mbele ya walezi wao wa kituo cha Nyota ya asubuhi ambako wanaishi Maria na Consolata, Mkuu wa wilaya ya Kilolo Mhe. Asia Abdallah, Mhe.Mwamoto ambao waliongozana na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Kilolo Bw. Alloyce Kwezi na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilolo Seth Moto walisema wamevutiwa na ufaulu wa mapata ambao ni yatima hivyo wamelazimika kuwaanzishia maandalizi ya chuo mapema zaidi kwa lengo la kuwawezesha kuanza chuo kwa wakati.
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kilolo Kwezi alisema kwa kufanya kwao vizuri kumeongeza heshima kubwa kwa wilaya ya Kilolo ambayo ndio iliyoongoza kwa matokeo ya kidato cha sita kwa mkoa wa Iringa wenye shule 25 huku wilaya hiyo ikiongoza kimkoa kwa kuwa na shule Pomerini ndio iliibuka ya kwanza kwa shule zote 25.
Hivyo alisema moja kati ya mkakati wa Halmashauri ya Kilolo ni kuendelea kufanya vizuri zaidi katika mitihani mbali mbali pamoja na mambo mengine ya kimaendeleo ili kuifanya wilaya hiyo kuwa mbele kwa kila jambo .
Mkuu wa wilaya ya Kilolo alisema kuwa pamoja na wilaya kutoa msaada huo kwa watoto hao mapacha kama sehemu yao ya maandalizi ya chuo bado milango ipo wazi kwa wadau wengine walioguswa na watoto hao kuzidi kuwasaidia kwani wao wenyewe wameonyesha nia ya kuendelea na masomo na kuwa mfano kwa baadhi ya jamii ambayo imekuwa ikiwaficha watoto wenye ulemavu kwenda shule .
“ Wametuowezesha wilaya yetu kufanya vizuri kweli! Tunawapongeza wao ,walimu na wadau wote wa elimu zaidi wanafunzi ambao wamefanya vizuri katika mitihani hiyo.
"Kilolo ilikuwa ikitazamwa sana kuona nini matokeo ya Maria na Consolata ila bila viongozi na wadau wengine wa elimu kujitoa kwa ajili yao yawezekana wasingefanya vizuri …..tupo pamoja nao na tutaendelea kuwa pamoja zaidi hadi chuo “ Mkuu huyo wa wilaya alisema.
Aliongezea kuwa moja kati ya mahitaji yao makubwa kwa sasa ni nyumba yao maalum kwa ajili ya kuishi pindi watakapokuwa chuo kwani wao wanahitaji nyumba maalum ambayo ni rafiki zaidi na aina ya ulemavu waliokuwa nao .
Mbunge wa Kilolo Mwamoto mbali ya kuwapongeza mapacha hao bado alitaka wananchi wote wenye watoto wenye ulemavu kuiga mfano wa mapacha hao na hatapendezwa kuona watoto wenye ulemavu wa aina yeyote ile wanafichwa majumbani .
Pia alisema moja kati ya mkakati wake kuona mazingira ya shule mbali mbali katika wilaya ya Kilolo yanakuwa rafiki na kuwataka wananchi kuendelea na ujenzi wa vyumba vya madarasa ,maabara ili kuepukana na changamoto ya miundo mbinu ya elimu pamoja na kwenda sawa na serikali ya Rais Dkt John Magufuli ya uboreshaji wa elimu .
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Mhe. Asia Abdallah, mbunge wa Kilolo Mhe. Venance Mwamoto mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilolo Seth Moto wakiongea na watoto hao
mbunge wa Kilolo Mhe. Venance Mwamoto akiwapongeza mapacha walioungana mapacha Maria na Consolata Mwakikuti
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Mhe. Asia Abdallah akiwapongeza mapacha walioungana mapacha Maria na Consolata Mwakikuti
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Mhe. Asia Abdallah akiwapa zawadi ya laptop mapacha walioungana mapacha Maria na Consolata Mwakikuti
Mapacha walioungana Maria na Consolata Mwakikuti wakipokea mito
Mapacha walioungana Maria na Consolata Mwakikuti wakipokea mablanketi
0 |
|
0 |
|
Na Othman Khamis Ame
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema wakati umefika kwa Chama cha Skauti Nchini kuongeza nguvu za kuwaelimisha Vijana wenzao hasa walioko Vijijini ili wajikomboe kupenda kujishughulisha na kazi au miradi ya ujasiri amali.
Alisema Vijana wengi wamekuwa na tabia ya kujihusisha na vigenge vya kihuni mitaani vinavyopelekea kujiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya wizi pamoja na vitendo vya kudhalilisha watoto wanawake na watu wenye mahitaji Maalum.
Balozi Seif Ali Iddi alitoa Kauli hiyo wakati akizungumza na Vijana wa Chama cha Skauti Zanzibar wanaojiandaa kuelekea Mkoani Dodoma kushiriki Tamasha la Wiki Moja la Maadhimisho ya Miaka 100 ya Skauti Tanzania hapo katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Alisema zipo fursa nyingi za ajira zinazopatikana katika Sekta ya Utalii ambazo Vijana endapo wataamua kuzichangamkia zinaweza zikawapatia kipato kwa kutumia soko la bidhaa zinazotokana na kilimo cha mboga mboga na mazao ya Baharini.
Balozi alifahamisha kwamba Uskauti kwa vile hauna mafungamano ya itikadi ya Kisiasa wala Dini unalengo la kuwaunganisha Vijana katika harakati zao za kimaisha kupitia misingi ya kujenga Utaifa wao.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisisitiza umuhimu wa vijana wa Skauti kufundishwa mbinu na mafunzo ya kuogelea na kuzamia kutokana na majukumu yao yaliyowazuunguka ya kuwa wao ni miongoni mwa Taasisi zinazotoa huduma wakati yanapotokea maafa au majanga.
Balozi Seif alielezea kuridhika kwake na Kanuni 10 za Skauti zinazoelekeza uzalendo unaojenga Taifa lenye Wananchi wanaopendana na kuwa na nguvu za kukabiliana na changamoto zinazowazunguuka katika misingi ya nidhamu na uwajibikaji.
Mapema Kamishna Mkuu Msaidizi wa Chama cha Skauti Zanzibar Maalim Suleiman Takadir alisema Skauti iliasisiwa Zanzibar mnamo mwaka 1912 na Mwaka 1917 ikaanzishwa upande wa Tanzania na kufifia katika miaka ya 60.
Maalim Takadir alisema Chama hicho kilianzishwa tena Mwaka 1992 chini ya Rais wa Awamu ya Tano Dr. Salmin Amour ili kufufua ari ya kuwajenga Vijana katika uzalendo.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknologia, Mhandisi Stella Manyanya wa pili kutoka kulia akitembelea shule ya Msingi Bagamoyo wakati wa ziara yake wilayani Korogwe kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert Gabriel na anayefuatia ni Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM) Marry Chatanda
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknologia, Mhandisi Stella Manyanya akiwa ameshika mtoto wakati wa ziara yake kulia ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert Gabriel kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe,Jumanne Shauri
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknologia, Mhandisi Stella Manyanya akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Bagamoyo iliyopo wilayani Korogwe ambapo aliwataka kusoma kwa bidii ili waweze kupata mafanikio
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe,Jumanne Shauri akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Matondoo wakati wa ziara hiyo ambapo aliwataka kutilia mkazo masomo ya sayansi.
0 |
|
0 |
|
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju ametoa wito kwa Asasi zisizo za kiserikali ( NGO) kushirikiana na kufanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili kupitia ushirikiano huo kukomesha na hatimaye kumaliza kabisa changamoto zinazowakabili watanzania wenye albinism.
Mwanasheria Mkuu ametoa wito huo leo ( Jumatano)wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Bi Ikponwosa Ero, Mtaalamu Huru wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kuhusu watu wenye albinism
“ Ningependa kutoa shukrani zako kwa kuamua kuja Tanzania na kukutana na viongozi mbalimbali wa Serikali, hii ni fursa muhimu kwako ya kupata taarifa sahihi na rasmi kuhusu jitihada , juhudi na mikakati mbalimbali inayofanywa na serikali na taasisi zake katika kukabili vitendo vya jinai dhidi ya watanzania wenzetu wenye albinism” akasema Mhe. Mwanasheria Mkuu
Na Kuongeza “ kupitia kwako nikuombe basi uwahimize viongozi wa asasi zisizo za kiserikali hususani zile zinazojihusisha na watanzania wenye albinism kushirikiana na kufanya kazi kwa karibu na Ofisi yangu na Taasisi nyingine za serikali kwa sababu wote tuna nia na lengo moja la kuwasaidia watanzania wenzetu”..
Akasema Serikali inachukulia kwa uzito wa hali ya juu makosa ya kijinai dhidi ya watu wenye albinism na kwamba, watuhumiwa wote ambao wamepatikana na hatia wamefikishwa mbele ya vyombo vya sheria na sheria kuchukua mkondo wake.
Akasisitiza kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano imesisitiza sana juu ya haki ya mtu kuishi na kwamba haki hiyo ni kwa watanzania wote bila ya kubagua wakiwamo watu wenye albinism au ulemavu wa aina yoyote.
“ Haki ya mtu kuishi imefafanuliwa na kuelezwa kwa kina kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na haki hiyo haimbagui mtu mwenye albinisim au mtanzania yoyote ile na ndio maana makosa ya jinai dhidi ya haki ya mtu kuishi awaye yeyote yule yanachukuliwa kwa uzito ule ule”.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju akifafanua kuhusu namna Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupitia Divisheni ya Mashtaka inavyoshughulikia kwa kupeleleza na kuendesha kesi za jinai dhidi ya watu wenye albnism. katika maelezo yake Mwanasheria Mkuu amesema Serikali inachukulia kwa uzito wa hali ya kipekee matatizo yanayowakabili watanzania wenye ualbino na kwamba juhudi hizo zimesaidia sana katika kupunguza kwa kiasi kikubwa matukio ya jinadi dhidi ya watanzania hao ingawa bado kunachangamoto.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. George Masaju akimsikiliza Bi. Ikponwosa Ero, Mataalam Huru wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kuhusu watu wenye albnism. Mhe. Mwanasheria Mkuu na Bi. Ero walikutana leo Jijini Dar es Salaam, ambapo walibadishana mawazo kuhusu namna Ofisi ya Mwanasheria Mkuu inavyoshughulikia matukio ya kijinai dhidi ya watanzania wenye albnism.
0 |
|
0 |
|
Na Bashir Yakub
1.UKOMO WA HAKI.
Hakuna haki isiyo na ukomo wa muda unapokuwa unaidai. Huwezi kudai haki muda wowote unaotaka wewe. Ni lazima udai haki ndani ya muda.Na ni ule muda tu uliowekwa na sheria. Ipo sheria rasmi inayoeleza muda wa kudai haki mbalimbali. Inaitwa Sheria ya Ukomo wa Muda , Sura ya 89. Katika sheria hiyo hapajaelezwa tu ukomo wa kudai haki katika masuala ya ardhi bali pia katika masuala mengine yote ya haki unazoweza kudai.
Ndani ya Sheria ya Ukomo wa Muda kumeelezwa ukomo wa kudai haki iliyotokana na masuala ya mikataba na makubaliano, ukomo wa kudai haki katika masuala ya udhalilishaji, ukomo wa rufaa, ukomo wa haki katika masuala ya bima, madai ya fedha, rehani za mikopo, na mambo mengine mengi.
2. HUJAPITWA NA MDA BADO UNAWEZA KUIDAI ARDHI YAKO.
Wako watu huko nyuma walidhulumiwa ardhi muda mrefu na sasa wamekata tamaa. Wamekata tamaa kutokana na kuona ni mda mrefu umepita tangu haki hiyo iporwe na sasa wanadhani kuwa hawawezi tena kudai haki hiyo.
Wako watu wamedhulumiwa ardhi katika masuala ya mirathi, katika masuala ya mikopo, katika masuala ya mikataba na makubaliano, katika masuala ya ndoa na machumo ya mali za ndoa, katika masuala ya uvamizi, katika masuala ya kuharibu mipaka n.k. Na ardhi hapa tunazungumzia mashamba, viwanja na nyumba. Hivi kwa pamoja ndivyo huitwa ardhi.
Basi yafaa ujue kuwa kama wewe ni kati ya waathirika wa jambo hili basi bado unayo haki ya kudai ardhi yako madhali muda huo haujakupita. Haki yako inaishi mpaka miaka 12 na itakufa baada ya muda huo. Kama imepita miaka sita, mitano, nane, kumi, n.k. bado muda wako wa kudai na kurudishiwa ardhi upo.

Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) imeapa kuwa ya mfano katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa wagombea wa nafasi mbalimbali katika Jumuia hiyo watakaobainika kutumia rushwa au kufanya vitendo vyovyote vinavyokiuka kanuni za Uchaguzi.
Kiapo hicho kimetolewa jana jijini Dar es Salaam, na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Amina Makilagi wakati akitangaza maazimio ya Kikao Cha Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UWT kilichofanyika juzi Makao Makuu ya Jumuiya hiyo, jiijini.
"Tunashukuru kwamba baada ya Mwenyekiti wetu wa CCM, Rais Dk. John Magufuli kuonyesha anapambana na rushwa kufa na kupona na kwa dhati kabisa, kila mtu amemuelewa na sisi UWT tunaahidi kumuunga mkono kwa kuhakikisha katika uchaguzi huu hatutakuwa na mzaha, yeyoyote atakayebainika kutumia rushwa hatutamuonea aibu hata awe nani", alisema Makilagi.
Alisema, uchaguzi kwa ngazi ya Matawi umefanyika kwa asilimia 95, ngazi ya Kata vikao vya uchujaji vinaendelea na kwa ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa uchaguzi unaendelea.
Mama mzazi wa Zarina Hassan maarufu kama ‘Zari The Boss Lady’ ambaye ni mzazi mwenza wa Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz, Halima Hassan (kulia) amefariki dunia asubuhi hii, baada ya kuugua kwa wiki kadhaa na kulazwa katika Hospitali ya Nakasero iliyopo nchini Uganda akidaiwa kusumbuliwa na maradhi ya moyo na figo.
Zari amethibitisha kifo cha mama yake kupitia ukurasa wake wa Instagram.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI..
AMEN.
0 |
|
0 |
|
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe magufuli akiwa ameambatana na mgeni wake Rais wa Burundi,Pierre Nkurunziza aliewasili mapema leo katka uwanja wa mpira wa Lemela mjini Ngara,Rais Dkt Magufuli amempokea Rais Nkurunziza akiwa kwenye ziara yake kikazi mkoani Kagera.
Aidha Rais Nkurunziza baada ya kupokelewa na Mwenyeji wake Rais Dkt Magufuli,alipata wasaa wa kuwasalimia wananchi mbalimbali waliofika kumpokea katika uwanja huo wa mpira mjini Ngara.
0 |
|
0 |
|

Siku ya kwanza walivyojitokeza kujifua hii ilikua siku ya Jumanne July 18, 2017 Columbus, Ohio.

Mazoezi yakiendelea siku ya pili Jumatano July 19, 2017 Cloumbus, Ohio
0 |
|
0 |
|
Na Shamimu Nyaki-WHUSM
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe amewashukuru viongozi wote wa Serikali, Sekta binafsi, Taasisi za Kidini vyombo vya habari na watanzania wote waliomfariji katika msiba wa mke wake Bibi Linah Mwakyembe uliotokea Julai 15 mwaka huu.
Akizungumza wakati wa Misa ya mazishi ya mke wake huyo iliyofanyika jana nyumbani kwake Kyela Mhe. Mwakyembe ameeleza kuwa amefarijika sana kwa upendo ulioonyeshwa na kila mtu kwa nafasi yake katika kipindi hiki kigumu na kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika kila jambo.
“Mimi na wanangu tumefarijika sana kwa kuona jinsi ambavyo Watanzania na wana Kyela mlivvyokuwa na upendo kwetu mmetupa faraja na mmetutia nguvu na mmetuoshesha ushirikiano mkubwa katika jambo hili tunaomba mwenyezi Mungu awabariki sana na asanteni sana”Alisema Mhe Waziri Mwakyembe.
Kwa Upande wake Mhe.Amos Makala Mkuu wa Mkoa wa Mbeya wakati akitoa salamu za pole kwa niaba ya wanachi wa mkoa wake amesema wananchi wa Mbeya watamkumbuka marehemu mama Linah Mwakyembe kwa moyo wake wa kujitolea kusaidia jamii katika mambo mbalimbali ikiwemo kufundisha jamii kumcha Mungu pamoja na Ujasiriliamali uliosaidia wanawake wa Kyela kujiajiri.
“Wananchi wa Mbeya tunakupa pole sana Mhe. Mwakyembe pamoja na familia yako lakini pia tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa maisha ya mama Linah hapa duniani ambayo yameleta faida kwa jamii tunamuomba mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi amina lakini na wewe pia tunakuombea Mungu aendelee kukupa uvumilivu na uamini kuwa hili nalo litapita”.Alisema Mhe Makala.
Marehemu Bibi Linah Mwakyembe ameagwa na kuzikwa jana nyumbani kwake Kyela na ameacha watoto watatu.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe
Mkuu wa Mkoa wa Singia Dkt Rehema Nchimbi amesema hatavumilia kuona halmashauri inafanya uzembe na kupata hati chafu ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Fedha za Serikali kwakuwa itamchafua yeye na taswira ya uongozi wote wa Mkoa wa Singida.
Dkt Nchimbi ametoa kauli hiyo mapema jana wakati wa baraza maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za serikali ambazo amesema hoja nyingi zimetokana na uzembe.
Amesema licha ya kuipongeza Manispaa ya Singida kwa kupata hati safi, uwepo wa hoja umedhihirisha kuwa kuna baadhi ya watendaji wanafanya kazi kwa uzembe na kutofuata taratibu na sheria hivyo wajirekebishe haraka.
Dkt Nchimbi ameongeza kuwa hoja nyingi zinajitokeza kwa kukosa umakini na watendaji kufanya kazi kwa mazoea hali ambayo ikiendelea inaweza kuipelekea manispaa kupata hati isiyoridhisha hivyo kupata hati safi kuwaongezee nguzu ya kuboresha utendaji kazi wao.
Aidha amewashauri wakuu wa idara na watumishi wengine kuitendea haki manispaa yao kwa kuchapa kazi kuwa wadilifu na kufuata sheria kwani wakifanya hivyo wataepuka hoja zisizo za lazima na kuharakisha maendeleo.
Mkuu wa Mkoa wa Singia Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na Meya wa Manispaa ya Singida Gwae Chima Mbua kabla ya kuanza kwa baraza Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Bravo Kizito Lyampembile akifungua baraza Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
Baadhi ya Viongozi wa Manispaa ya Singida wakifuatilia baraza Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA