Na Robert Hokororo, Kishapu
Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 umepokelewa kimkoa kijiji cha Kinampanda kata ya Shagihilu katika wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga kutoka Simiyu na kuzindua miradi ya maendeleo yenye thamani ya sh. bilioni 3.7.
Katika mapokezi hayo Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini alimkabidhi mwenzake wa Shinyanga, Albert Msovela ambaye alimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kishapu.
Katika mbio hizo jumla ya miradi 12 ilizinduliwa ikiwemo ya kituo cha mafuta wenye thamani ya sh. milioni 337 kutoka kwa mjasiliamali Kija Ng’wani na mashine ya kusindika mafuta ya alizeti na unga wa mahindi sh. 244.
Mingine ni mashine ya kukoboa mpunga na kuweka katika madaraja sh. milioni 535.8 na ufugaji ng’ombe sh. milioni 400 ya mjasiliamli Mabela Masolwa pamoja na eneo la viwanda lenye ekari 278 ambao thamani yake ni sh. bilioni 1.1.
Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa wa Shinyanga, Albert Msovela (kushoto) akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa mwenzake wa Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini tayari kwa mbio hizo mkoani Shinyanga.
Mwenge wa Uhuru ukikimbizwa eneo la Maganzo wilayani Kishapu wakati ukiendelea kizindua miradi ya maendeleo. Kulia mbele ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga akitoa hamasa kwa wananchi.
Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Amour Hamad Amour akiweka nafaka ya mahindi katika mashine ya kusaga unga wakati wa uzinduzi wa mradi wa kiwanda kidogo cha kusindika alizeti na kusaga unga wakati wa mbio za Mwenge zilipopita kata ya Mwamalasa wilayani Kishapu mkoani Shinyanga jana.
Mwenyekiti wa halmashauari ya Kishapu, Boniphace Butondo akicheza ngoma wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru kijiji cha Kinampanda.
Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Amour Hamad Amour akikagua bidhaa katika banda la wanawake wajasiliamali wilayani Kishapu eneo la mkesha Maganzo. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA