Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110114 articles
Browse latest View live

INTRODUCING "KAA KIJANJA" BY FEZA FT. NIKKI WA PILI


BBC DIRA YA DUNIA JUMANNE 11.07.2017

JOB VACANCY: THE DIRECTOR - CENTRE FOR FOREIGN RELATIONS DAR ES SALAAM

MSAFIRI KAFIRI.....

MTANZANIA ABUNI EXTENSHENI ZA UMEME ZA MBAO

Mjadala baada ya Mbunge wa Sengerema Mhe. William Ngeleja kurudisha Fedha za Mgao wa Escrow

LABOR DAY COLUMBUS, OHIO PATAKUA HAPATOSHI

$
0
0

HOTELS IN COLUMBUS

Hampton Inn Columbus I-70 E/Hamilton Road

2093 S Hamilton Rd, Columbus, OH 43232
hamptoninn3.hilton.com
(614) 552-2400

Holiday Inn Express & Suites Columbus Southeast
4041 Hamilton Square, Groveport, OH 43125
ihg.com
(614) 920-2400

Hawthorn Suites by Wyndham Airport Columbus East
2084 S Hamilton Rd, Columbus, OH 43232
wyndhamhotels.com
(614) 864-8844

La Quinta Inn Columbus Airport Area
2447 Brice Rd, Reynoldsburg, OH 43068
laquintacolumbusairport.com
(614) 866-6456

Comfort Suites Columbus
5944 Scarborough Blvd, Columbus, OH 43232
choicehotels.com
(614) 552-2525

Days Inn & Suites Columbus East Airport
2100 Brice Rd, Reynoldsburg, OH 43068
wyndhamhotels.com
(614) 864-1280

Courtyard by Marriott Columbus Airport
2901 Airport Dr, Columbus, OH 43219
marriott.com
(614) 475-8530

DKT. PHILIP MPANGO ATATUA CHANGAMOTO YA MSONGAMANO WA WALIPAKODI TRA VINGUNGUTI DAR ES SALAAM

$
0
0

Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, eneo la Vingunguti Jijini Dar es Salaam na kuagiza kuongezwa kwa wafanyakazi na vitendea kazi katika ofisi hiyo baada ya kukuta msongamano mkubwa wa watu waliojitokeza kulipa kodi ya majengo.

Dkt. Mpango ambaye alitumia muda wake mwingi kusikiliza kero za baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwa wingi kulipa kodi hiyo, ameiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania kuongeza wafanyakazi kumi pamoja na mashine za kieletroniki za kukusanyia kodi pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa kuwahudumia wazee na watu wenye ulemavu.

“Nimeagiza wafanyakazi waongezwe, viti 50 kwa ajili ya kutumiwa na wazee pamoja na akina mama wenye watoto vitaletwa, pamoja na kuongeza mashine za kielektroniki 5 kutoka 3 zilizokuwepo ambapo sasa zitakuwa mashine 8, hatua hii itaondoa changamoto hii” alifafanua Dkt. Mpango

Amerejea pongezi zake kwa Watanzania kwa kujitokeza kwa wingi kila mahali nchini kote kulipa kodi ya majengo akikielezea kitendo hicho kuwa ni cha kizalendo na kitaisaidia nchi kuondokana na umasikini kwa kuwa itakuwa na uwezo wa kuwahudumia wananchi wake kikamilifu.

Dkt. Mpango amewahakikishia Wazee waliotimiza umri wa kuanzia miaka 60 na kuendelea kwamba Serikali imewaondolea kodi ya majengo kwenye nyumba zao wanazoishi kutokana na kutambua mchango wao mkubwa katika kulitumikia Taifa wakati wa ujana wao.

Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kulipa kodi katika Ofisi hiyo ya TRA, Vingunguti, wamepongeza utaratibu wa Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philip Mpango wa kuwajibika na kutumia muda wake kuwatembelea na kuwahudumia wananchi na pia wamemmwagia sifa kem kem Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa hamasa kubwa aliyowapa na kwamba wako tayari kumuunga mkono kwa hali na mali ili nchi ipate maendeleo kwa haraka
Matukio mbalimbali ya picha zikionyesha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango akifanya ziara za kushitukiza katika maeneo muhimu kwa lengo la kuangalia utaratibu wa ulipaji kodi mbalimbali hususan ya majengo na vituo vya mafuta ili kubaini kasoro mbalimbali na kutoa maelekezo masuala muhimu anayoyabaini ambapo jana alikuwa Kigamboni, Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kulipa kodi katika Ofisi hiyo ya TRA, Vingunguti wakimsikiliza Dkt Mpango.

Dkt Mpango akipata maelezo mafupi kutoka kwa Maofisa hao.
Dkt Mpango akisikiliza kero mbalimbali kutoka Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kulipa kodi katika Ofisi hiyo ya TRA, Vingunguti


DARAJA LA MTO KALAMBO LAKAMILIKA

$
0
0
Serikali kupitia Wakala wa barabara nchini TANROADS mkoa wa Rukwa imekamilisha ahadi yake kwa wananchi ya kuwapunguzia changamoto ya usafirishaji wa abiria na mzigio kwa kukamilisha ujenzi wa Daraja la mto Kalambo pamoja na barabara ya Sumbawanga Matai hadi Kasanga port (112km) ambapo Kilomita 71.4 zimeshawekwa lami.

Akizungumza mara baada ya kukagua daraja na barabara hiyo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani amesema kukamilika kwa barabara hiyo kutafungua fursa za kiuchumi kwa wananchi wa mkoa Rukwa na nchi nyingine za jirani ikiwemo Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Burundi.

“Tuliwaahidi wananchi kujenga darala na barabara hii ili wafanyabiashara na wakulima waweze kusafirisha bidhaa na mazao yao kwenda katika masoko kwa wakati na hivyo kukuza uchumi wao binafsi na taifa kwa ujumla,” ameaema Eng. Ngonyani.

Ameongeza kuwa chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli Serikali itahakikisha ndani ya kipindi cha miaka mitano inakamilisha ahadi zote walizoahidi kwa wananchi ili wananchi wanufaike na Serikali yao.

“Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli ipo kwa ajili ya wananchi wote, na sisi kama wasimamizi tuliopewa dhamana kwenye Wizara tutahakikisha kile tulichokiahidi kwa wananchi tunakitekeleza kwa wakati ili wananchi wanufaike na uchumi wa nchi ukue,” amesisitiza Eng. Ngonyani.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Wa pili kushoto) akitoa maelekezo kwa Mkandarasi anayejenga Kituo cha Mzani cha Singiwe Kilichopo katika barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga Port (112KM) Mkoani Rukwa wakati alipokagua ujenzi huo Mkoani Rukwa.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Katikati) akipanda katika Daraja la Mto Kalambo Mkoani Rukwa wakati alipokagua daraja hilo ambalo ujenzi wake umekamilika.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Wa pili kulia) akikagua Daraja la Mto Kalambo Mkoani Rukwa wakati alipokagua daraja hilo ambalo ujenzi wake umekamilika.Wa kwanza ni Meneja wa Wakala wa barabara (TANROADS) Rukwa Eng. Msuka Mkina.

WAZIRI MPANGO AKIFUNGIA KITUO CHA MAFUTA CHA GBP ENEO LA UWANJA WA NDEGE DAR ES SALAAM

$
0
0

Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam 

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika eneo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na kuamuru kituo cha Mafuta cha GBP kifungwe hadi hapo kitakapo funga mashine maalumu za kutolea risiti baada ya kubainika hakitumii ipasanyo mashine za kieletroniki za kukusanyia kodi (EFD) 

Dkt. Mpango amechukua hatua hiyo baada ya kujionea kituo hicho kikiwa na  pampu nne za mafuta lakini kuna mashine moja pekee ya mkononi ya kutolea  risiti jambo linasababisha wateja wao wengi kutopewa risiti na hivyo kuikosesha Serikali mapato yake na ni kinyume cha sheria za nchi. 

“Sasa nawachukulia hatua ili liwe fundisho kwa wengine wote wanaouza mafuta nchini bila kufuata taratibu, na nitaanza na wewe, biashara yako isimame mpaka mashine zifungwe kwenye kituo chote na utekeleze mara moja” alisistiza Dkt. Mpango 

Katika ukaguzi wa Kituo cha Mafuta cha Puma, Dkt. Mpango amesifu utaratibu mzuri uliowekwa na kituo hicho kwa kufunga mashine maalumu za kutolea risiti zilizounganishwa na kila pampu za mafuta kitu ambacho ndicho Serikali inavitaka vituo vyote vya mafuta vitumie mfumo huo 

“Kituo hiki kimezingatia sheria sheria kwa kufunga mashine kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali na hapa tunauhakika wa kupata fedha za kuwatumikia wananchi, kinyume kabisa na kituo cha mafuta nilichokifungia, hapa ndio ningeomba Watanzania wanunue mafuta” aliongeza Dkt. Mpango. 




Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (aliyevaa tai) akimhoji mmoja wa wahudumu wa Kituo cha mafuta cha GBP kilichopo karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kabla ya kukifunga kwa kosa la kutotumia Mashine za kierektroniki za EFDs. 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akitoa agizo kwa msimamizi wa Kituo cha Mafuta cha GBP kilichopo karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nerere kukifunga maramoja kwa kutofuata maagizo ya Serikali ya kutumia Mashine za EFDs kwenye vituo vya Mafuta. 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akizungumza na baadhi ya wakazi wa maeneo ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere pamoja na wamiliki wa vyombo vya moto kuhusu umuhimu wa kudai risiti wanaponunua mafuta kwenye vituo vya mafuta, wakati alipokifunga Kituo cha Mafuta cha GBP, baada ya mmiliki wake kubainika kukiuka masharti kwa kutotoa risiti za kielektroniki (EFD)kwa wateja wake. 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwa katika mitaa ya maeneo ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, akizungumza na baadhi ya wakazi wa maeneo hayo kuhusu umuhimu wa kudai risiti wanaponunua mafuta kwenye vituo vya mafuta na kuitaarifu Serikali wanapobaini wamiliki wa vituo hivyo hawatoi risiti za EFD. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

INTRODUCING "THAMANI" BY SAMPAMBA

Kagera yote kupata umeme wa uhakika 2021, Bilioni 45.43 kutumika sehemu ya kwanza ya mradi

$
0
0

Na Greyson Mwase, Kagera 

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani amesema vijiji na vitongoji vyote vya mkoa wa Kagera vinatarajiwa kupata umeme wa uhakika ifikapo mwaka 2021 kama sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) 

Dkt. Kalemani aliyasema hayo mapema Julai 11, 2017 kwenye hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) utakaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) iliyofanyika katika kijiji cha Rwabigaga wilayani Kyerwa mkoani Kagera pamoja na kumtambulisha mkandarasi atakayefanya ujenzi wa sehemu ya kwanza ya mradi katika mkoa huo. 

Alisema utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika mkoa wa Kagera utahusisha vipengele vitatu ambavyo ni pamoja na kusambaza umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa kabisa na miundombinu ya umeme na kuongeza wigo wa usambazaji umeme katika vijiji ambavyo vimefikiwa na miundombinu ya umeme lakini baadhi ya maeneo na vitongoji havikuungwa. 

Waziri Kalemani alisema kipengele cha tatu kinahusisha usambazaji wa umeme utokanao na vyanzo vya nishati jadidifu kwenye maeneo yaliyo mbali na gridi hususan visiwani. 

Aliendelea kusema kuwa utekelezaji wa mradi huu utatekelezwa kwa vipindi viwili tofauti ambapo sehemu ya awali itahusisha upelekaji umeme katika vijiji 141 kwa gharama ya shilingi bilioni 45.43 na kuongeza kuwa utekelezaji wa sehemu ya kwanza ulianza tangu mwezi Februari mwaka huu ambapo inatarajiwa kukamilika mapema Aprili, 2019 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akikata  utepe kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Kagera uliofanyika katika kijiji cha Rwabigaga wilayani Kyerwa. Kulia kabisa ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Kagera uliofanyika katika kijiji cha Rwabigaga wilayani Kyerwa. Kulia kabisa ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga na kushoto ni Mbunge wa Kyerwa, Innocent Bilakwate. 
Waliosimama ( kuanzia wa pili kutoka kulia mbele), Mbunge wa Kyerwa, Innocent Bilakwate, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Dkt. Gideon Kaunda wakiwa katika picha ya pamoja na wanakijiji wa Rwabigaga wilayani Kyerwa mkoani Kagera mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi wa Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Kagera uliofanyika kijijini hapo mapema Julai 11, 2017

WATANZANIA WASHAURIWA KUUNGA MKONO MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA.

$
0
0
Na Sixmund J. Begashe  wa Makumbusho ya Taifa

Watanzania wameshauriwa kuunga mkono jitihada mbali mbali zinazofanywa na Serikali, Mashirika ya Umma na Wadau mbali mbali katika mapambano dhidi ya rushwa  ili kutokomeza kabisa tatizo hili hapa nchini. 
Hayo yamesema na Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam Bwana Achiles Bufure kwenye usahili uliofanywa na Makumbusho hiyo ili kuchaguwa wasanii watakao unda kikundi kimoja kwa lengo la kutoa elimu ya Mapambano dhidi ya Rushwa hapa nchini.

 

Bw Bufure ameongeza kuwa Makumbusho imeona itumie wasanii wa fani mbali mbali kupitia program ya sanaa na Utamaduni ijulikanayo MUSEUM ART EXPLOSION ili kufikisha ujumbe kwa haraka zaidi na ambao utakaokaa akilini mwa watu kwa muda mrefu kupitia sanaa za ufundi na zile za jukwaani. 
Wakizungumza baada ya Usahili huo, msanii Bi Yame Muhamedi wa Kikundi cha sanaa cha UKOO na Salum Mbaya wa St Kamilius Wameipongeza Makumbusho ya Taifa kwa kuwashirikisha wasanii katika program ya MUSEUM ART EXPLOSION AGAINST CORRUPTION kwani  imewapa nguvu na hari ya kuendelea kufanya kazi za sanaa katika kuleta matokeo chanya ya kimaendeleo ndani ya nchi na kuahidi kufanya vyema kazi iliyopo mbele yao ya kufikisha ujumbe kwa jamii juu ya madhara ya Rushwa nchini. 
Program ya MUSEUM ART EXPLOSION AGAINST COTTUPTION ni moja kati ya program tano nchini zilizopata ufadhili wa Ubalozi wa Uswiss wenye lengo la kutoa elimu kwa watanzania juu ya Madhara na namna ya kupambana na Rushwa nchini.
 Wasanii kutoka vikundi mbali mbali wakifanya usajili kabla ya usahili.

 Wasani wakiwajibika katika usahili uliofanyika Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam ili kupata nafasi ya kushiriki mapambano dhidi ya rushwa kupitia sanaa.
 Usaili ukiendelea jukwaani
Kushoto ni Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Bw. Achiles Bufure akifuatilia kwa karibu zoezi la usahili kwa wasanii  lililofanywa na Makumbusho hiyo. Kulia ni Msanii Nguli wa sanaa za Jukwaani Bw Aloyce Makonde akitoa maelezo kwa wasanii  wakati wa usahili huo.

INTRODUCING "KISELA" BY VANESSA MDEE Ft. MR P (P-SQUARE)

$
0
0
Queen Vanessa Mdee Collaborates with Nigerian Royalty!

Benki ya NBC yashinda Tuzo ya Superbrand Afrika Mashariki

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kushoto),akipokea tuzo ya ubora ya Superbrand Afrika Mashariki kwa mwaka 2017-18 kutoka kwa Mkurugenzi wa Miradi wa Superbrands Afrika Mashariki, Jawad Jaffer katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Hii ni mara ya pili kwa NBC kupokea tuzo hiyo mara ya kwanza ikiwa ni mwaka 2015-16.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (​wa tatu kushoto), akipozi kwa picha pamoja na baadhi ya wawakilishi wa makampuni yaliyoshinda tuzo za Superbrand Afrika Mashariki katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo jijini Dar es Salaam jana. Hii ni mara ya pili kwa NBC kupokea tuzo hiyo mara ya kwanza ikiwa ni mwaka 2015-16

DKT NCHIMBI APOKEA MADAWATI ZAIDI YA 2000 KUTOKA BUNGENI KWA NIABA YA MIKOA YA KASKAZINI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi leo ampokea madawati 2579 kutoka kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa niaba ya mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro.

Akipokea madawati hayo yaliyosafirishwa katika magari 19 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Dkt Nchimbi amelipongeza jeshi hilo kwa uzalendo huo wa kuhakikisha mali za umma zinafika Singida kwa ajili ya kuanza kusambazwa katika halmashauri husika zikiwa salama na katika hali nzuri.

Dkt Nchimbi amelipongeza Bunge kwa uzalendo wa kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli katika kuhakikisha sekta ya elimu inaboreka nchini  ili kutimiza azma ya kufikia uchumi wa kati na wa viwanda. 

Amesema madawati hayo yataongeza motisha kwa wanafunzi kujisomea kwakuwa mazingira yatawawezesha kuandika na kusoma kwa ufanisi zaidi.
Aidha Dkt Nchimbi amezitaka halmashauri zitakazopokea madawati hayo kuhakikisha wanayatunza ili yadumu na kuwanufaisha wanafunzi kwa muda unaostahili.

“Madawati na yenyewe yanahitaji ukarabati, sio kwakuwa mmepewa basi muyaache tu, hapana, ukiona ubao unalegea kidogo basi hakikisha unarekebisha na sio kuanza kusubiri waliotupatia ndo waturekebishie”, amesema na kuongeza kuwa.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akipokea kwa furaha moja ya magari ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) yaliyokuwa yamebeba Madawati hayo 2579 yanapelekwa katika mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro. Madawati hayo yametolewa na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akimpongeza kwa furaha mmoja wa mwanajeshi aliyehusika kusafirisha Madawati 2579 yaliyotolewa na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro. Madawati hayo yamefikishwa Singida kwa ajili ya urahisi wa kuyasambaza katika mikoa hiyo.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akishirikiana na wanajeshi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Askari wa Magereza kushusha madawati yalitolewa na Bunge. Madawati hayo 2579 yanapelekwa katika mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KUFUNGWA KWA AWAMU YA PILI YA UREJESHAJI HALI YA MIUNDO MBINU YA UMMA MKOANI KAGERA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa afungua Zahanati katika kijiji cha Nandaka Wilayani Ruangwa

$
0
0


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akifungua Zahanati katika kijiji cha Nandaka Wilayani Ruangwa, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku nne Mkoani Lindi, Julai 11, 2017.

Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Wananchi wa Nandanga mara baada ya kufungua Zahanati katika kijiji cha Nandaka Wilayani Ruangwa, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku nne Mkoani Lindi,
Julai 11, 2017.
Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Wananchi wa Nandanga mara baada ya kufungua Zahanati katika kijiji cha Nandaka Wilayani Ruangwa, akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku nne Mkoani Lindi,
Julai 11, 2017.

WATEJA WAFURAHIA TECNO DUDE

$
0
0
Baada ya mzigo mpya kutoka Tecno kuingizwa mtaani kwaajili ya Watanzania wiki moja iliyopita baadhi ya watumiaji wa bidhaa hiyo warudisha majibu mazuri kwa angle tofauti tofauti kuhusiana na simu hiyo #TecnoDude kwa uzoefu waliyoupata katika kipindi hiki kifupi toka wainunue.
Hawa ni baadhi ya wateja wanafamilia wa #TecnoDude #TecnoWashaDude wakijidaiya mambo waliyoyakuta ndani ya simu hiyo kupitia mitandao yao ya kijamii hususan Instagram na  Facebook. 
Wateja mbali mbali wakifurahia sim mpya kutoka Tecno Toleo liitwalo " Wx3Lte" yenye uwezo mkubwa wa 4g, camera na memory ya kutosha. Maarufu kwa jina la "TecnoDude" simu hii inapatikana maduka yote ya  Vodacom nchini @sanchosong @jrjunior5 @eric_mkomoye #tecnodude #tecnowashadude

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JULAI 12, 2017

Viewing all 110114 articles
Browse latest View live




Latest Images