Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live

WAVAMIZI WA MAENEO YA HIFADHI ZA RELI WAPEWA MIEZI SITA

0
0
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani akitoa maelekezo kwa Meneja wa Kampuni ya Simu (TTCL) mkoa wa Rukwa na Katavi Bw. Peter Kuguru wakati alipokagua eneo ambalo Mkongo wa Taifa umeharibika kwa kuliwa na panya Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa.

 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani (Katikati) akiangalia ramani ya Mkongo wa Taifa wakati alipokagua eneo ambalo Mkongo wa Taifa umeharibika kwa kuliwa na panya Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa.

 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani (Kulia) akitoa maelekezo kwa Mkandarasi anayejenga barabara ya Kanazi-Kizi-Kibaoni (76.6KM) Wakati alipokagua ujenzi wa barabara hiyo kwa  kiwango cha lami. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Tehama yaongeza ufanisi wa Utoaji wa huduma kwa wakazi wa mkoa wa Dodoma

Queen Vanessa Mdee Collaborates with Nigerian Royalty!

0
0
Fresh off of her acting debut on MTV SHUGA, East Africa's leading female artist Vanessa Mdee releases her brand new single Kisela. The single features Nigerian King of Pop Mr P (Peter Okoye) of PSquare. 
This horn heavy stadium anthem tells a story of a heartbroken woman who discovers what she thought was a relationship is actually a mere hook up. This captivating break up song produced by Nigeria's smash hit making producer EKelly (produced VeeMoney’s Cash Madame) is another indication of Vanessa's versatility. 
The heart wrenching lyrics play on a tale as old as time. The Clarence Peters directed visuals are an absolute delight and show off both Peter and Vanessa's ability to play a role. 
These two will have you hooked displaying their star quality in this passionate story. Vanessa was heard stating that Peter Okoye is the definition of a music icon and this dream come true not only gave her an added lesson in music and entertainment but also a class in humility and professionalism.

BENJAMIN FERNANDES: MTANZANIA WA MFANO ALIYEKATAA MSHAHARA WA MILIONI 450 KUJA KUTUMIKIA TAIFA

0
0
Kwa hisani ya Clouds 360
 Benjamin Fernandes akipeperusha bendera ya Taifa nchini Brazil
 Benjamin Fernades akipeperusha bendera ya Taifa kazini kwake Seattle, Marekani
Benjamin Fernades akipeperusha bendera ya Taifa wakati wa kubeba nondozzzz yake ya MBA katika chuo Kikuu cha Stanford School of Business huko Marekani

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 10.07.2017

MAREHEMU SETH KATENDE KUAGWA JUMATANO VIWANJA VYA LEADERS CLUB JIJINI DAR ES SALAAM

DC KIBAHA ASUMPTA MSHAMA KUWANYANG'ANYA ARDHI WAMILIKI WASIOZIENDELEZA ILI KUDHIBITI VICHAKA VYA UHALIFU

0
0


MKUU wa Wilaya  ya  Kibaha Mhe. Asumpta Mshama  (pichani)  ametoa onyo  kali kwa  wamiliki wote wa ardhi ambao wanazimiliki kwa muda mrefu bila kuziendeleza hali inayopelekea kuzalisha mapori yanayoficha vitendo vya  kihalifu Kibaha Mkoani Pwani.
Bi Mshama amesema hayo leo akiwa katika  mkutano wa hadhara uliofanyika maeneo ya Visiga , Kibaha Mkoani Pwani ambapo aliweza kupokea changamoto mbalimbali kutoka kwa wananchi wa eneo hilo  ikiwa ni pamoja na tishio la kuzungukwa na mapori yenye wanyama wakali pamoja na kuwa  maeneo ya yanayofanyika vitendo viovu.


"Wamiliki wote wenye maeneo makubwa  ya  ardhi  ambazo haziendelezwi serikali itawapokonya ifikapo Septemba Mosi mwaka huu" amesema Mhe. Mshama.

Akiwa kwenye muendelezo wa ziara yake Wilaya ya Kibaha  alisema  wamiliki wenye maeneo makubwa wamekuwa wakizalisha  mapori ambayo yamekuwa  vichaka vya kufanyia vitendo viovu ndani ya Mkoa wa Pwani huku akitolea mifano ya mapori yaliyopo Wilaya ya Kibiti.
Ameongeza kwa kusema kuwa yuko tayari kwenda Mahakamani kwa kuwang'anya ardhi wamiliki wasioendelwza maeneo hayo huku akisema kuwa hati zimeandikwa mwisho wa kuendeleza eneo ni miaka mitatu huku akiongeza kwa kusema kuwa  baada ya kuzichukua ardhi hizo fomu zitatolewa kwa wananchi ili wazijaze nankugaiwa maeneo.

INTRODUCING Diamond Platnumz's new single "ENEKA"


WAZIRI UMMY MWALIMU ATEMBELEA KITUO CHA AFYA CHA KATORO MKOANI GEITA

0
0
 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisalimiana na watumishi wa kitupo cha afya cha mji mdogo wa Katoro, mkoani Geita.Waziri huyo amefika katika  kituo hicho ili kujionea hali ya kituo hicho ambacho kinahudumia idadi kubwa ya wakazi wa mji huo pamoja na jirani zake licha ya kuwa na changamoto ya watumishi pamoja na miundombinu.
 Waziri Ummy akimsalimia mtoto aliyefika kituoni hapo pamoja na mama yake kupata huduma ya afya,kulia ni Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho Dkt. Peter Janga
 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akimfafanulia jambo mmoja wa wagonjwa waliofika kupata huduma kwenye kituo cha afya cha Katoro

 Waziri Ummy akitoa maelekezo kwenye matangazo yaliyobandikwa kwenye kuta za kituo hicho,kushoto ni Mkurugenzi wa HALMASHAURI YA Geita Lawrence Kalabezile.Waziri huyo amewataka watumishi wa kituo hicho kujituma na kutimiza wajibu wao katika kuwahudumia wananchi hususan katika kuokoa maisha ya wagonjwa.
Katika ziara hivyo Waziri Ummy alikagua ujenzi wa jengo la upasuaji wa dharura unaojengwa kwenye kituo hicho.Waziri wa Afya yupo  katika ziara ya kikazi ya  siku tatu Mkoani Geita (PICHA ZOTE NA WIZARA YA AFYA)

KARIBU JUMAMOSI KWENYE MAOMBI YA SHUKRANI KITAIFA UWANJA WA UHURU JIJINI DAR ES SALAAM

ASKOFU JOSEPHAT GWAJIMA MAREKANI

Masauni aliagiza Jeshi la Polisi kufungua kituo makazi ya kabila la Wahazabe

0
0
 Na Felix Mwagara (MOHA)
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amelitaka Jeshi la Polisi mkoani Manyara kufungua Kituo cha Polisi katika Makazi ya Kabila la Wahazabe wanaoishi katika Bonde la Yueda Chini, wilayani Mbulu. 
Masauni alisema hayo jana wakati akizungumza na mamia ya wananchi wa kabila  hilo mara baada ya kukagua jengo la mifugo katika eneo la bonde hilo ambalo jamii hiyo ilijitenga kwa kuweka makazi pembezoni mwa Mji wa Mbulu. 
“Hivi karibuni Kituo cha Polisi kitafunguliwa hapa ili kulinda usalama wenu katika eneo hili ambalo lilikua halina kituo cha Polisi kwa miaka mingi. Serikali ya Rais Magufuli ni sikivu ndio mana nimekuja hapa kuwasikiliza matatizo yenu na kuwatekelezea.” Alisema Masauni huku akishangiliwa na wananchi hao. 
Aliongeza kuwa, mchakato wa kujenga kituo hicho umeanza na tayari ametoa maelekezo kwa Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa huo, kwa kushirikiana na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Wabunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini na Mbulu Mjini. 

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watatu kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Flatei Massay (wapili kulia) wakicheza ngoma ya Wabarbaig/Watatoga kabla ya Masauni kuzungumza na mamia ya wananchi wa Kabila maarufu la Wahazabe na makabila mengine yaliyopo katika Bonde la Yueda Chini, Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara. Masauni aliiagiza Jeshi la Polisi mkoani humo, kujenga Kituo cha Polisi kwa uharaka ili jamii hiyo ambayo inaishi pembezoni mwa mji wa Mbulu.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na mamia ya wananchi wa Kabila maarufu la Wahazabe na makabila mengine yaliyopo katika Bonde la Yueda Chini, Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara. Masauni aliiagiza Jeshi la Polisi mkoani humo, kujenga Kituo cha Polisi kwa uharaka ili jamii hiyo iweze kupata ulinzi wa kutosha katika eneo hilo.
 Wananchi wakimshangilia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) wakati alipowatangazia kufunguliwa Kituo cha Polisi hivi karibuni katika Kijiji cha Bonde la Yueda Chini, lililopo wilayani Mbulu, Mkoa wa Manyara. 
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akijadiliana na maafisa wa halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, mkoani Manyara pamoja na watendaji mbalimbali wa wilaya hiyo, ndani ya jengo la mifugo lililopo Yaeda Chini katika makazi ya Wahazabe, ambalo linatarajiwa kufunguliwa Kituo cha Polisi. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi mkoani Manyara (RPC), Francis Massawe, na kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Flatei Massay.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akimsikiliza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Francis Massawe alipokuwa akijibu maswali mbalimbali ya uhalifu ambayo yaliulizwa na wananchi (hawapo pichani) wa Kijiji cha Yueda Chini Wilaya ya Mbulu mkoani humo, ambalo kuna makazi ya jamii ya Kabila la Wahazabe.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Umoja International Outreach Church: A NIGHT WITH MASANJA MKANDAMIZAJI

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WAKABIDHIWA GARI IRINGA

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza ambaye ni Mgeni rasmi akikata utepe ikiwa ni ishara ya kukabidhi rasmi gari la kuzimia moto kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, tukio ambalo limeshuhudiwa na Kamaishna Jenerali wa Jeshi hilo, Viongozi mbalimbali wa kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoani humo, Mdau aliyetoa msaada huo Ndugu, Zacharia Hanspoppe, Maafisa na Askari wa Jeshi hilo pamoja na wananchi. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji akionesha funguo ya gari hilo mara baada ya tukio la kukata utepe na kukabidhiwa rasmi na Mkuu wa Mkoa Bi. Amina Masenza ambaye alikuwa ni Mgeni rasmi katika makabidhiano hayo. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza mwenye kitambaa cheupe katikati, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye wa kwanza mbele, Mdau ndugu Zachalia Hanspope wa pili kutoka kushoto, pamoja na Viongozi wa kamati ya vyombo vya ulinzi na usalama Mkoani Iringa wakifurahi tukio la makabidhiano. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)
Gari lililokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoro na Uokoaji Thobias Andengenye. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza (kushoto) akiagana na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (kulia) mara baada ya kuhitimisha shughuli ya makabidhiano ya gari la kuzimia moto lililotolewa msaada na mdau Ndugu Zacharia Hanspoppe. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji).

SUMMER BBQ SATURDAY JULY 15, 2017 NEW JERSEY, NEW YORK.

0
0
Nahodha msaidizi wa timu ya New York, Elisante Shayo akikabidhiwa uzi na Malkia wa Nyuki wa timu ya New York tayari kwa mchezo wao wa Jumamosi hii dhidi ya D.C. 
Timu ya New York Tanzania Community a.k.a NYATI  wapo tayari kwa mchezo wao dhidi ya timu ya Watanzania kutoka Washington D.C Jumamosi hii ya Julai 15, 2017  kuanzia saa nane mchana katika viunga vya Lincoln Park, Nj.
Mchezo huu ni wa kukata na Mundu na siyo wa kukosa maana historia ya machungu ya timu New york siyo ya kubeza kutokana na kupokea kipigo cha nusu dozen miaka miwili iliyopita vijana wamesema labda itokee tu safari hii D.C watatafutana na kama siyo kutafuta njia ya kutokea uwanjani baada ya  kupata kipigo na vijana wa New York watakae ongozwa na vijana wenye damu mchanganyiko kutoka vyuo  vya mafunzo.  
Vijana wamejitolea kuwafuta machozi wapenzi wao watakaokuwa wakiwachagiza  kwenye uwanja wanyumbani siku hiyo. Kabla ya Mchezo mwamuzi ataanza kukagua (Identity Card ) ya kila mchezaji ilikuondowa utata wa kupata watalii wasiokuwa na tija ya kizalendo, kwani Uzalendo wa Kitanzania kwanza.
Address ni hii: 

Introducing Dewish The Matrix "M A R U F U K U"

NEWS ALERT: PROFESA FLORENS D.A.M LUOGA ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA BODI TRA

MSTAAFU ATOA WITO WANANCHI KUJIUNGA NA PSPF KUPITIA UCHANGIAJI WA HIARI PSS, ASEMA AMEONA FAIDA ZAKE IKIWEMO BIMA YA AFYA

0
0

MSTAAFU wa utumishi wa umma, Bi. Marcella Isidori Chanda, amewahimiza wananchi na wastaafu wenzake, kujiunga na Mfuko wa Pensehni wa PSPF, kupitia mpango wake wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), kwani kuna faida nyingi mwanachama atazipata.

Bi. Chanda, ameyasema hayo muda mfupi baada ya kujiunga na Mpango huo wa PSS, leo Julai 10, 2017, baada ya kupatiwa elimu ya huduma zitolewazo na PSPF kwa wanachama wake.

“Mimi nilikuwa mtumishi wa benki na nimestafu mwaka 2013, ni meona iko haja ya kujiunga na mpango huu ambao hatimaye moja ya mambo yaliyonivutia ni kupatiwa bima ya afya, kwani nimeelzwakuwa ukiwa mwanachama wa PSS, basi unapata sifa za kujiunga na bima ya Afya, tofauti na ukiwa mtu binafsi gharama zinakuwa kubwa mno na zinafikia hadi shilingi 1,500,000nkwa mwaka.” Alisema Bi. Chanda.

Akieleza zaidi, Bi. Chanda alisema, amefikia uamuzi wa kujiunga naPSPF, baada ya kupata taarifa nyingi kupitia vyombo vya habari kuwa, lakini pia majirani na jamaa zngu kuwa wamekuwa wakifaidika na huduma ya afya kupitia bima ya afya.

Mstaafu huyo alsiema, leo amejiunga na PSS na pia atamueleza mumewe naye pia ajiunge. “Natoa wito wka wastaafu wenzangu na wananchi kwa ujumla kujiunga na PSPF ili kujihami na gharama za matibabu. Kwa upande wake, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi alisema, karibu asilimia 60 ya wananchi wanaofika kwenye banda hilo, wamekuwa wakijunga na Mpango wa PSS na moja ya sababu kubwa ni kupatiwa bima ya Afya.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani, (kulia), akizungumza jambo mbele ya Afsia Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi alipotembelea banda la Mfuko huo leo Julai 10, 2017.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Elimu kwa Umma, wa Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi Hifadhi ya Jamii, (SSRA), Bi. Sarah Kibonde Msika, (kushoto) akimsikiliza Bw. Njaidi kwenye banda la PSPF, Julai 10, 2017. SSRA imeweka maafisa wake katika kila banda la Mifuko ya Hifadhio ya Jamii, ili kufuatilia utoaji huduma wa Mifuko hiyo kwa wananchi kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.


Afasia Msaidizi wa Uenddshaji wa PSPF, Bw. Win-God Simon, (kushoto), akiwahudumia maafisa hawa wa polisi ambao ni wanachama wa Mfuko.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 11, 2017

Tamthilia Mpya ya UZIKWASA Wilayani Pangani kuanza hivi karibuni

0
0
 Kwa mara nyingine tena shirika la UZIKWASA lililopo wilayani Pangani limekuja na mambo mapya. Safari hii ni tamthilia ya mchezo wa redio unaofahamika kama Tamapendo. Lengo la tamthilia hii ni  kuonesha changamoto za vijana wawili kujiendeleza katika maisha yao katika jamii ambapo kanuni za unyanyasaji wa kijinsia za kijamii bado zinashinda.

Tamapendo inakuwa tamthilia ya pili ya redio kutengenezwa na shirika la UZIKWASA baada ya mchezo wa redio wa Penye Nia…..uliopatwa kusikilizwa na jamii nzima ya Pangani kupitia kituo cha redio cha Pangani FM, ambacho pia kinamilikiwa na shirika la UZIKWASA wilayani Pangani.

Shirika hili pia limekuwa na utaratibu kutengeneza filamu mbali mbali hasa kuhusu maswala ya haki na ukatili wa kijinsia.  Kutokana na utafiti wa ndani kabisa filamu za UZIKWASA zinasimulia story halisi  za jamii ya Pangani na zilifanikiwa kugusa watamazaji kwa sababu filamu hizi ni kama kioo cha changamoto zao.

Filamu hizo ni  Fimbo ya Baba ambayo ilitengenezwa mwaka 2006, Chukua Pipi iliyotoka 2012 na  filamu maarufu ya  AISHA ya mwaka 2015.  AISHA ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa, siyo Pangani tu, lakini Tanzania nzima na nchi nyingi za kimataifa. Imepata tuzo mbalimbali kimataifa kutoka tamasha za filamu maarufu USA  na Africa.
Pamoja na hayo yote, sasa shirika la UZIKWASA limekuja tena na tamthilia la redio inayoitwa Tamapendo. Kama kawaidi ya filamu na tamthilia ya redio za UZIKWASA karibu waigizaji wote hutokea Pangani. Na ndivyo ilivyotokea kwa Tamapendo ambayo imeongozwa kwa ushirikiano na wagurugenzi wa mchezo Chande Omar na Irene Sanga. Story ya tamthilia hii inatokana na tafiti iliofanika na UZIKWASA pamoja na mchango wa wanajamii wa Pangani.  

Tamthilia imetengenezwa na kuhaririwa kwenye studio ya redio Pangani FM –Sauti ya Jamii.

Tamapendo ni kuhusu nini?

Ni story ya vijana wawili Fatuma na Chaballa wanaokutana na dhuruba kubwa ya maisha.  Wanajiona kuelemewa na mambo mazito kuhusiana na ukatili mbalimbali na dharau kuhusiana na haki za wanawake na wasichana.

Wakati wakijinusuru kutetea upendo wao wa dhati na kufuatilia ndoto zao katika maisha, wanajikuta kunaswa na mtego wa tamaa unaotawala kijijini kwao.  Je, unajua ni mtego gani waliokutana nao Fatuma na Chaballa?

Ni matumaini ya UZIKWASA kuwa  Tamapendo baada ya kuzinduliwa Pangani itazunguka nchi nzima ili kuwafikia wasikilizaji wengi na kuibua mijadala.
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live




Latest Images