Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110031 articles
Browse latest View live

Tamasha la E-FM Redio la Komaa Concert lilivyozizima jiji la Mwanza

$
0
0
Tamasha la E-FM Redio ya Jijini Dar es salaam, liitwalo Komaa Concert lililokuwa mahususi kwa ajili ya redio hiyo kuwashukuru wasikilizaji wake wa 91.3 lilifunika jiji la Mwanza kwa mapokezi yao makubwa.Katika tamasha hilo, wanamuziki mbalimbali akiwemo Dulla Makabila, Ney Wa Mitego, Darassa, Stamina, Rich Mavoko, Aga Star, Chemichal, Ben Pol na wengine wengi walidondosha burudani kali katika uwanja wa CCM Kirumba

Darassa akitumbuiza  kwenye tamasha la KOMAA CONCERT uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza

Dulla Makabila akifanya yake kwenye tamasha la KOMAA CONCERT uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza

Ney Wa Mitengo akiwapa raha mashabiki  kwenye tamasha la KOMAA CONCERT uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. Picha na BMG



MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA DSM AMTEMBELEA KARDINAL POLYCARP PENGO LEO

$
0
0
MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amtembelea Askofu wa Jimbo kuu Katoliki la Dar es salaam Mwadhama Kardinal Polycarp Pengo Ofisini kwake leo ,Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini leo.baada ya kutoka nje kwa matibabu. 
Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akisalimiana na Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Kardinal Polycarp Pengo alipomtembelea ofisini kwake mapema leo.
Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Kardinal Polycarp Pengo akizungumza na Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita kuhusu hali ya afya yake alipomtembelea leo Ofisini kwake ,kanisa la Mtakatifu. Joseph.
Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akimsikiliza Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Kardinal Polycarp Pengo alipomtembelea ofisini kwake leo ,Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini hapa.
Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akipata Baraka kutoka kwa Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Kardinal Polycarp Pengo alipomtembelea ofisini kwake leo, katika kanisa la Mtakatifu Joseph leo alipomtembelea kumjilia hali yake.
Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kumjulia hali Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama KardinalPolycarp Pengo alipomtembelea ofisini kwake leo, katika kanisa la Mtakatifu Joseph leo alipomtembelea kumjilia hali yake.

Serikali Kuimarisha Uwanja wa Ndege wa Mpanda

$
0
0

Serikali imemuagiza Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda kuwasiliana na Kampuni ya Uendelezaji Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro (KADCO) ili kupata gari la Zimamoto ili ndege za Shirika la ndege Tanzania (ATCL) ziweze kuanzisha safari zake katika Mkoa wa Katavi.

Akizungumza mara baada ya kukagua uwanja huo Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani amesema kwa muda sasa kiwanja hicho kimekuwa kikitumiwa na ndege chache za Shirika la kuhudumia wakimbizi (UNHCR), hivyo ni wakati sasa kutumika na ndege zetu ili kuboresha huduma za usafiri wa anga Mkoani hapa.

“Kamilisheni mazungumzo na KADCO ili kupata gari la Zimamoto lenye ujazo wa Lita 4,000 litakalokuwa na uwezo wa kukabiliana na majanga ya moto endapo yatatokea, kutakapokuwa na gari hilo uwanjani hapa tutaanzisha safari za ndege za Shirika letu wakati ndege yetu ta tatu itakapowasili,” amesema Eng. Ngonyani.

Aidha, amemtaka meneja wa Uwanja huo wa ndege kuhakikisha anaingiza uwanja huo katika mpango maalum kwa ajili ya ujenzi wa taa kiwanjani hapo ili uwanja huo uweze kutumika kwa mchana na usiku.

Eng. Ngonyani ameongeza kuwa azima ya Serikali ni kuhakikisha usafiri wa anga nchini unaimarika kwa kutumia ATCL na mashirika mengine yalipo nchini hivyo kama Serikali imejipanga kuendelea kuboresha miundombinu ya viwanja ili viwe katika viwango vinavyokubalika.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (katikati) akitoa maelekezo kwa Meneja wa Kiwanja cha ndege cha Mpanda Seth Lyatuu (kushoto) wakati alipokagua huduma za uwanja huo Mkoani Katavi.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani(Kulia) akikagua Mfumo wa ukatishaji tiketi kwa njia ya kielekroniki katika Stesheni ya Mpanda Mkoani Katavi. Katikati ni Meneja Mradi wa kampuni ya Makgroup Ltd Bw. Joseph Mrosso.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Kampuni ya Reli Tanzania, Kanda ya Tabora Bw. Frederick Masangwa(Katikati), wakati alipokagua huduma za usafiri wa Reli Mkoani Katavi.
Meneja wa Msimamizi wa Bandari ya Kigoma Bw. Morris Mchindiuza (aliyenyoosha mkono) akimwonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Wa pili kulia) eneo itakapojengwa bandari ya Kalema iliyopo Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Wa pili) akitoka kukagua kingo za bandari ya Kalema iliyopo Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi

AFYA YA MTOTO MWENGE YAIMARIKA; RC NCHIMBI AWAASA WAZAZI JUU YA KUWAPA WATOTO WAO MAJINA

$
0
0

Afya ya mtoto Mwenge aliyenusurika kifo baada ya kutumbukizwa chooni na kukaa humo kwa zaidi ya saa 14 kabla ya kuokolewa akiwa hai, inaendelea kuimarika huku akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Kiomboi Wilayani Iramba.

Mtoto Mwenge alitupwa chooni na mama yake mzazi Winfrida Lori (23) mwanafunzi katika Chuo cha Uuguzi cha Kiomboi Wilayani Iramba ambapo mama huyo amekiri kujifungua mtoto huyo wa kiume katika Kijiji cha Luono Julai 3, saa mbili usiku kisha kumfunga vitambaa mdomoni na kumtumbukiza chooni.

Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Kiomboi Regina Alex amesema afya ya Mtoto Mwenge inaendelea kuimarika pamoja na hali ya mama mzazi wa mtoto huyo pia inaimarika tofauti na hapo awali ambapo alikuwa dhaifu na kushindwa kumnyonyesha mtoto.

“Winifrida alikuwa hawezi kumyonyesha mtoto Mwenge hapo mwanzoni lakini sasa hivi anamnyonyesha vizuri na maziwa yanatoka ya kutosha, Mtoto mwenge ana hali nzuri na sasa amefikisha uzito wa kilogramu 2.9 hali ambayo inaridhisha kwakweli”, ameeleza muuguzi huyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi (picha ya maktaba).


Mngereza kuwa mgeni rasmi tamasha la SHIWATA.

$
0
0
KATIBU Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Geofrey Mngereza amekubali kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Wasanii litakalofanyika Ijumaa jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Cassim Taalib alisema Mngereza atashuhudia michezo mbalimbali itakayofanywa na wasanii na wanamichezo.

Alisema tamasha hilo ambalo awali lilikuwa lifanyike kijiji cha Wasanii Mkuranga limehamishiwa jijini Dar es Salaam sababu kubwa ya kuhamisha tamasha hilo ni kutokana na mvua ya msimu uliopita kuharibu barabara ya kwenda kijijini.

Taalib alisema tamasha hilo sasa litafanyika kwa siku mbili kuanzia Ijumaa Julai 14.7.2017 na kuhitimishwa Jumamosi Julai 15 mwaka huu katika viwanja vya Chuo cha Uhazili, splendid Ilala Bungoni.Alisema mpaka sasa wanatarajia kupokea wanamichezo kutoka sehemu mbalimbali kama vile Mkuranga, Kibiti, Zanzibar na Morogoro ambako zaidi ya wanamichezo 600 wamethibitisha kushiriki.

Baadhi ya michezo ambayo itafanyika ni sarakasi, Tae kwon-do, muziki wa dansi, ngumi, soka,rede,muziki wa asili,wu shuu,ngoma,singeli na michezo mingine.Alisema kampuni ya SBC wanaotengeneza soda za Pepsi imekubali kuwa wadhamini wakuu wa tamasha hilo na kuongeza kuwa milango iko wazi kwa wadhamini wengine kujitokeza.

Akizungumzia ujenzi wa nyumba zao kijijini alisema mgawo na makabidhiano ya nyumba 14 ndogo,kubwa tatu na viwanja 35 vilivyopimwa utafanyika Julai 16 siku moja baada ya kumalizika tamasha hilo.

Alisema kuanzia sasa wanachama wanaotaka kujenga nyumba zao wenyewe wawasiliane na Shiwata ili wapewe maelekezo na utaratibu wa kufanya usafi kwenye makazi yao.Mwenyekiti alisema utaratibu wa kulipia umeme kupitia mpango wa umeme vijiijini (REA)unaendelea na mikakati ya kukarabati barabara ya kufika kijijini unafanyika.

DKT. MPANGO ATEMBELEA BANDA LA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA KATIKA MAONYESHO YA SABASABA, AKIPONGEZA KWA UTENDAJI WAKE

$
0
0

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango. (kushoto), akikaribishwa na Afisa Udahili wa Chuo Cha Uhasibu Arusha, (IAA), Bw. Gerald Malisa, alipofika kutembeela banda la chuo hicho lililoko jengo la Wizara ya Fedha na Mipango, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, maarufu Sabasaba,barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanaendelea kwenye viwanja hivyo na yatafikia kilele Julai 13, baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, kuomba Tan Trade waongeze siku tano zaidi ili kutoa fursa pana kwa wanachi kutembelea maonesho hayo na kupata faida mbalimbali.





WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango ametembelea banda la Chuo Cha Uhasibu Arusha, (IAA), lililoko kwenye jengo la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam kunakofanyika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.


Waziri alikipongeza chuo hicho kwa maendeleo kilichofikia na kusaidia kutoa wataalamu katika Nyanja za uhasibu na utunzaji wa hesabu ambapo sasa kinaendelea kupanua huduma zake kwenye maeneo mengine nje ya makao makuu yake jijini Arusha.



Akimpatia maelzo waziri mpango, Afisa Uhusiano na Masoko wa chuo hicho, Sarah Goroi, alimueleza Waziri Mpango kuwa chuo hicho kwa sasa ukiacha makao makuu yake jijini Arusha pia kina matawi jijini Dar es Salaam, jijini Mwanza na wilayani Babati mkoa wa Manyara.


Sarah  alisema, chuo kinatoa elimu ya uhasibu ngazi ya Astashahada(certificate), Stashahada(Diploma), Shahada ya Kwanza(Bachelor degree), Post Graduate diploma, na Shahada ya Uzamili (Masters Degree).

“Mheshimiwa waziri huduma tunazozitoa kwenye banda letu ni pamoja na kufanya udahili hapa hapa kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na programu mbalimbali zinazotolewa na chuo cheti kwa ngazi nilizozitaja.” Alifafanua Sarah

Alisema Mtu anayehitaji kujiunga na chuo hicho, afike kwenye banda la chuo akiwa na picha moja ya passport size ya rangi, na vivuli vya vyeti vya kidato cha nne, (Form Four), na Kidato cha Sita,(Form Six), kwa wale wanaoomba kujiunga na programu za Shahada ya Kwanza, au Cheti cha kuhitimu elimu ya Chuo Kikuu kwa wale wanaotaka kujiunga na programu za Masters.

Akieleza zaidi Sarah alisema, kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na programu za Astashahada (Cheti) wanapaswa wafike na vivuli vya vyeti vya kumaliza elimu ya sekondari (Kidato cha nne) 

Chuo cha Uhasibu Arusha, ni taasisi ya kielimu iliyoanzishwa na sheria ya taasisi za elimu ya uhasibu Arusha ya mwaka 1990 (Act of 1990), udhibiti wa jumla na uongozi wa taasisi uko chini ya Baraza la Uongozi la chuo, (Governing Council), alifafanuaSarah..

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, (NEC), anayeshughulikia masuala ya Siasa na Uhusinao wa Kimataifa, Kanali (mstaafu), Nelubinga, (kulia), akizungumza jambo wakati alipotembelea banda hilo, huku Afisa Uhusiano na Masoko wa chuo hicho, Sarah Goroi(kushoto), akimsikiliza. Katikati ni Kanali Mstaafu, F.L Kakiziba.
Waziri Dkt. Mpango, akifurahia jambo wakati akipatiwa maeelzo kuhusu huduma za kielimu zitolewazo na Chuo hicho. Kulia ni Afisa Uhusiano na Masoko wa chuo hicho Sarah  Goroi.


Dkt. Mpango, (kushoto), akisaini kitabu cha wageni kwenye banda hilo, wanaoshuhudia kutoka kulia ni Afisa Utawala wa chuo Bi. Sekunde Titus, Afisa Uadahili, Bw.Gerald Malisa, na Afisa Uhusiano na Masoko, Sarah Goroi.

Afisa Uhusiano na Masoko wa chuo cha Uhasibu Arusha Sarah Goroi akitoa maelezo kwa wateja waliofika katika banda lao kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam kunakofanyika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.

WAZAZI WASHAURIWA KUTUMIA AKAUNTI YA MTOTO NA CHIPUKIZI YA NMB

$
0
0
BENKI ya NMB imewashauri wazazi na walezi kuwafungulia watoto wao akaunti mbili mpya ambazo zimeanzishwa na benki hiyo ya Mtoto Akaunti na Chipukizi Akaunti kwa ajili ya kutumia kuwawekea fedha watoto wao.

Hayo yamesemwa na Mratibu wa Elimu ya Fedha wa benki ya NMB, Ryoba Mkono baada ya kutoa elimu ya fedha kwa wazazi na watoto kwenye maonesho ya 41 ya Saba Saba yanayofanyika jijini  Dar es Salaam. Mkono alisema mzazi atakuwa na nafasi ya kuchagua akaunti gani inamfaa mtoto kulingana na umri wake na kwa kila akaunti mtoto atakuwa anapata riba ya asilimia tano kila mwisho wa mwaka kulingana na kiasi cha fedha alichonacho kwenye akaunti.

“Mtoto Akaunti inahusisha watoto wenye umri kuanzia miaka 0 hadi 17 gharama yake ya kufungua ni 5,000. Ni akaunti ya kuweka akiba na mzazi ndiyo anaweza kuweka na kutoa na mara nyingi tunashauri mzazi asitoe ili itumike kwa mtoto baadae.”

“Kwa upande wa NMB Chipukizi Akaunti hii inahusisha watoto wenye umri wa miaka 13 hadi 17 ni akaunti ambayo ina ATM Card na mtoto anaruhusiwa kutoa pesa hadi 50,000 kupitia ATM zetu au NMB Wakala kwa siku moja na kila akitoa pesa mzazi anapata ujumbe kuwa mtoto katoa pesa,” alisema Mkono.

Pia Mkono alizungumza kuhusu faida za akaunti hizo mbili tofauti na akaunti zingine ambazo zinapatikana kwenye benki ya NMB, ”Faida yake ni hazina makato ya mwezi kwa ajili ya uendeshaji, pia mtoto anapata riba ya asilimia tano ya kiasi alichonacho kwenye akaunti yake ya NMB.”

Aidha Mkono aliwashauri wazazi kuwafungulia watoto akaunti hizo ili wapate huduma boa kutoka NMB lakini pia hata katika kipindi cha maonesho ya Saba Saba watoto wataweza kutumia kadi zao kununua vitu mbalimbali ambavyo wanahitaji.

“Wazazi wamekuwa wakiwapa watoto pesa mkononi wanapoenda kwenye Saba Saba lakini kama mtoto ana miaka 13 anaweza kuwa na ATM Card ni vyema wakawafungulia akaunti ili wazoee kutumia pesa kwa uadilifu na hata mwakani wakija kwenye Saba Saba wanakuwa wanaweza kutumia kadi zao kutoa pesa ili kufanya matumizi yao,” alisema Mkono.

Mahojiano ya Mubelwa Bandio, Viola na Dj D - Ommy ndani ya Kilimanjaro Studios U.S.A

$
0
0
Machi 16 2017, Mubelwa Bandio na Viola walipata nafasi ya kufanya mazungumzo na Dj D-Ommy katika studio za Kilimanjaro Studios.
Dj D-Ommy ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi nchini Marekani amezungumza mengi kuhusu maisha, kazi na tasnia nzima ya muziki.
Pia akapata fursa kuzindua rasmi kifaa kipya cha kazi kwa studio yetu, Pioneer DDJ SZ2 - Karibu utazame ukisikiliza

SHULE YA KWANZA KIMKOA MTIHANI WA MOCK 2017 DAR ES SALAAM

MASAUNI AFANYA ZIARA YA KIKAZI WILAYA ZA KONDOA, CHEMBA MKOANI DODOMA LEO

$
0
0
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimsalimia Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, mkoani Dodoma, Sezaria Makota, mara baada ya kuwasili wilayani humo kwa ajili ya ziara ya kikazi. Wapili kulia ni Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Winnie Kitazi, na kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi wilayani humo, SSP Mohamed Kitia.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akiwasalimia Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Wilaya ya Kondoa na Chemba mara baada ya kuwasili mjini Mkondoa kwa ajili ya ziara ya kikazi. 

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, mkoani Dodoma, Sezaria Makota wakati alipokua akitoa taarifa yake ya Wilaya kwa kiongozi huyo ambaye yupo ziarani katika Wilaya ya Kondoa na Chemba. 
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Chemba, mkoani Dodoma, Simon Odunga,wakati alipokua akitoa taarifa yake ya Wilaya kwa kiongozi huyo ambaye yupo ziarani katika Wilaya ya Kondoa na Chemba. 
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akimsikiliza Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kondoa, SSP Mohamed Kitia wakati alipokua akitoa taarifa yake ya Ulinzi na Usalama wilayani humo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Sezaria Makota, na Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga. Masauni yupo ziara ya kikazi katika Wilaya hizo ambapo alizitembelea Taasisi zilizopo ndani ya Wizara yake. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

KAMISHNA WA VIBALI NA PASI AONGOZA WAFANYAKAZI WA IDARA YA UHAMIAJI KUTOA HUDUMA KWA WANANCHI KATIKA MAONESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA YA SABASABA

$
0
0
 Kamishna wa Vibali na Pasi nchini, Musanga Etimba akitoa maelezo kwa mwananchi Oliver Gabriel, aliyetembelea Banda la Idara ya Uhamiaji katika Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa,jijini Dar es Salaam.
 Mwananchi aliyetembelea Banda la Idara ya Uhamiaji, Oliver Albert akiuliza maswali kwa Kamishna wa Vibali na Pasi nchini, Musanga Etimba baada ya kutembelea Banda la Idara hiyo katika Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa,jijini Dar es Salaam.Katikati ni Mdhibiti wa Pasipoti nchini, Mrakibu Mwandamizi Peter Mwitwa.
 Mkaguzi wa Idara ya Uhamiaji nchini, Mustafa Kipingu (kushoto), akitoa huduma kwa mwananchi aliyetembeleaBanda la Idara hiyo katika Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa,jijini Dar es Salaam.
zi wa Idara ya Uhamiaji, Kitengo cha Uhusiano, Aziz Kirondomara (kushoto), akitoa huduma kwa mwananchi aliyetembeleaBanda la Idara hiyo katika Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa,jijini Dar es Salaam.
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

WATEMI WA KISUKUMA, VIONGOZI WA TAS WATEMBELEA KITUO CHA WATOTO WENYE UALBINO SHINYANGA

$
0
0
Watemi wa Kisukuma Kanda ya Ziwa Victoria na viongozi wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania( Tanzania Albinism Society -TAS) wamefanya usafi wa mazingira kisha kula chakula cha pamoja na watoto wenye ualbino wanaolelewa katika kituo cha Buhangija katika manispaa ya Shinyanga.

Katibu Mtendaji wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino nchini Tanzania -TAS Taifa Bw. Mussa Mussa akizungumza katika kituo/Shule ya Msingi Buhangija katika manispaa ya Shinyanga.Kulia ni Katibu wa Umoja wa Watemi wa Kisukuma kanda ya Ziwa, ambaye ni chifu/mtemi wa Bujashi wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza Charles Dotto Balele.Kushoto ni Mwalimu Mlezi wa Shule ya Msingi Buhangija, Frola Kakutebe.

Watoto na maafisa kutoka TAS wakiwa eneo la tukio
Katibu wa Umoja wa Watemi wa Kisukuma kanda ya Ziwa, ambaye ni chifu/mtemi wa Bujashi wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza Charles Dotto Balele Itale akila chakula na watoto wanaolelewa katika kituo cha Buhangija katika manispaa ya Shinyanga. 

SAJOREC-CAS to reinforce partnership with SUZA

$
0
0
A delegation of Sino-Africa Joint Research Center-Chinese Academy of Sciences (SAJOREC-CAS), University of Science and Technology of China (USTC) has on 6th July, 2017 paid their second visit at the State University of Zanzibar (SUZA) seeking to sustain collaborative relationship which has been established between the parties. The delegation was led by Prof. Xue Yan, the Deputy Director, SAJOREC-CAS while SUZA was represented by Prof. Idris Rai, the Vice Chancellor. 
The visitors have agreed to partner with SUZA in research and staff capacity development in areas of environmental studies, fisheries, remote sensing and water resource management. Under this partnership SUZA staff and students can benefit from various scholarships (MSc and PhD) and fellowship programs.
 

The Chinese Academy of Science (CAS), the largest scientific organization in China which is mandated to undertake research and innovation for the Chinese government is a major driving force behind a wide range advance of research areas.
 
Through support and guidance from CAS, China is focused on building "big science" infrastructure, as well as on developing a talent pool of top notch scientists for the country. This talent pool is being built through programs to retain and cultivate the best Chinese scientists. CAS is encouraged to travel globally for training and to develop collaborations, as well as numerous incentive programs for international scientists to visit and work in China; this is the reason behind their second visit at SUZA within a year period.
A delegation of Sino-Africa Joint Research Center-Chinese Academy of Sciences (SAJOREC-CAS), University of Science and Technology of China (USTC) pose for a group photo with the officials of the State University of Zanzibar (SUZA) at Serena Hotel in the Isles.

Raila Odinga hospitalised after rallies in Kilifi, Mombasa

INTRODUCING "UR BEATIFUL" BY EMMA GUITAR


SIMULIZI: KITANDA CHA SOKWE MTU na Dokta Mungwa Kabili

$
0
0

Ni simulizi la ukweli linalo husu maisha ya kijana Lugwisha kutoka kitongoji cha Goweko, wilayani Uyui mkoani Tabora ambaye baada ya kumaliza shule ya msingi mnamo mwaka 1994 huko kijijini kwao, alifunga safari hadi jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kutafuta maisha. 


 Miaka kumi baadae kijana Lugwisha akawa amepata mafanikio makubwa yaliyobadilisha maisha yake. Mafanikio katika maisha ya Lugwisha yanasababisha kuinuka kwa maadui ambao hawapendezwi na kufanikiwa kwake. Maadui hawa wanapanga njama mbalimbali za kupambana dhidi ya mafanikio ya Lugwisha. 

Kati ya maadui wa Lugwisha, ni maadui wawili tu ndio wanaonekana kuwa na nia thabiti na ya dhati katika mapambano dhidi ya Lugwisha. Maadui hao ni Beka Msangi pamoja na Bundala. 
Beka Msangi alikuwa mmiliki wa bar iliyo kuwa jirani na bar iliyo milikiwa na Lugwisha. Bar hii ya Lugwisha ilikuwa ni moja kati ya makumi ya vitega uchumi vyake vilivyo muingizia fedha nyingi. Bar ya Lugwisha ilikuwa maarufu sana jijini Dar es Salaam na ilikuwa ikifurika wateja kuanzia Jumatatu hadi Jumapili. 
Bar hii ya Lugwisha ilikuwa katika eneo lenye bar nyingi. Uwepo wa bar ya Lugwisha katika eneo hilo uliua biashara ya karibu bar zote zilizo kuwepo katika eneo ikiwemo bar ya Beka Msangi. Beka Msangi hakutaka kukubaliana na hali hiyo na hivyo kufikia uamuzi wa kusafiri hadi katika kijiji cha Mchukwi wilayani Rufiji mkoani Pwani, kwa ajili ya kumroga Lugwisha. Baada ya kupiga ramli, wachawi wa Rufiji wanaona njia pekee ya kupambana na Lugwisha ni kumuhamisha kichawi yeye na bar yake kwa kutumia uchawi wa Kizigua, ujulikanao kama “Sunkwa”. 

MKUTANO MKUU WA JUMUIYA YA WAISLAM WA AHMADIYYA KANDA YA ZIWA WAFANYIKA SHINYANGA

$
0
0
Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Tanzania Maulana Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry (wa tatu kutoka kushoto) akimpokea mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack (wa pili kushoto) kwa ajili ya kushiriki mkutano mkuu waJumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya kanda ya ziwa mwaka 2017 uliofanyika katika Kijiji cha Sungamile kata ya Mwalugulu wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Tanzania Maulana Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry akimkaribisha mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack na wageni mbalimbali waliohudhuria mkutano huo.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akitoa hotuba yake wakati wa kutano mkuu waJumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya kanda ya ziwa mwaka 2017.
Viongozi mbalimbali wa serikali wakiwa eneo la tukio. Kushoto ni Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akifuatiwa na Afisa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Maria Yondani.
Waumini na wananchi wakiwa eneo la tukio.


BENKI YA CRDB YASAIDIA UJENZI WA NYUMBA YA WALIMU KATIKA SHULE YA SEKONDARI LAIKALA KONGWA DODOMA

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai, ambaye pia ni mbunge wa Kongwa, akipokea mfano wa hundi  ya Sh. Milion 15 kutoka kwa Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Tawi laDodoma, Rehema Hamisi kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa nyumba ya walimu katika Shule ya Sekondari Laikala iliyopo wilayani Kongwa. Kulia ni Diwani wa Kata ya Sagala, Simon Kamando, akishuhudia.
Spika wa Bunge, Job Ndugai (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB Tawi la Dodoma pamoja na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo.
 Wanafunzi wakifurahia mfano wa hundi iliyotolewa na Benki ya CRDB. 
  Sehemu ya mifuko ya sarui iliyokabidhiwa na Benki ya CRDB kwa Shule ya Sekondari Laikala. 

TANZANIA YABADILI MSIMAMO WA UNESCO WA KUITAKA KUSITISHA UJENZI WA MRADI WA STIEGLER'S GORGE KATIKA PORI LA AKIBA LA SELOUS

$
0
0
Tanzania imesisitiza uamuzi wake wa kuendelea na mpango wa kujenga mradi mkubwa wa kuzalisha umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge Hydro Power Project) yaliyopo ndani ya Pori la Akiba la Selous mbele ya wajumbe wa Kamati ya Urithi wa Dunia kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya Watanzania.

Akizungumza mwishoni mwa wiki katika mkutano wa 41 wa wajumbe wa Kamati ya Urithi wa Dunia unaoendeshwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) ambao unaendelea katika Jiji la Krakov nchini Poland, Kiongozi wa msafara huo ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi aliwaeleza wajumbe wa mkutano huo kuwa mpango huo ulikuwepo katika ajenda ya Serikali ya Tanzania tangu miaka ya 1960's na kwamba ukubwa wa eneo litakalotumika kutekeleza mradi huo ni asilimia tatu tu ya eneo lote la pori hilo ambalo lina ukubwa wa kilometa za mraba 50,000.

Aliongeza kuwa, “Itakumbukwa kuwa mnamo mwaka 1982 wakati pori hili (Selous) limewekwa katika orodha ya maeneo ya urithi wa dunia, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhifadhi wa Asili (IUCN) liliutambua mradi huo wa Stiegler's Gorge kutokuwa na madhara makubwa katika uharibifu wa mazingira ukizingatia ukubwa wa pori hilo na eneo litakalotumika kujenga mradi huo”.

Aliwaeleza wajumbe hao kuwa, Serikali ya Tanzania inatekeleza sera ya kujenga uchumi wa viwanda hali inayopelekea kuwa na mahitaji makubwa ya nishati ya umeme hivyo kwa kuzingatia vyanzo vilivyopo imekuwa ni muhimu sasa kufikiria tena ujenzi wa mradi huo kama chanzo kingine muhimu cha nishati kuwezesha kufikia azma hiyo.

Alisema mradi huo utaongeza uzalishaji wa umeme nchini kufikia asilimia 144.8 hivyo kuondoa upungufu wa nishati uliopo kwa sasa na pindi utakapokamilika utawanufaisha watanzania wengi wanaoishi bila umeme ikiwa ni pamoja na kukidhi mahitaji yake ya kuendesha viwanda.

Muonekano wa mto Rufiji kutokea angani ambao maporomoko yake yatatumika kuzalisha umeme katika mradi unaotarajiwa kujengwa na Serikali wa Stiegler's Gorge.
Sehemu ya mto Rufiji unakatiza katika Pori la Akiba la Selous.

WAKUU WA SHULE BINAFSI WALIPE BIMA ZA AFYA KWA WANAFUNZI –SPIKA MSTAAFU MAKINDA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 

Spika Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, ,Anne Makinda amesema wakuu wa shule binafsi wanachukua fedha za huduma ya matibabu ya afya kwa wanafunzi lakini wanafunzi hao wamekuwa hawapati huduma wanazostahili na kulingana na kiasi walicholipia. 

Wakuu wa Shule binafsi wamekuwa wakilipisha wanafunzi fedha za huduma ya matibabu ikiwa ni njia moja ya maelezo kujiunga (joining instruction) ila inapotokea mtoto anaumwa humrudisha kwa wazazi wake. 

Mwenyekiti huyo ameyasema hayo wakati alipotembelea banda la NHIF katika Maonesho ya biashara ya Kimataifa katika Viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam, amesema mwanafunzi akilipia bima ya afya lazima atumie na sio kubaki mzigo kwa mzazi wakati alishalipia fedha ya matibabu hiyo. 

Amesema kuwa wakuu wa shule wanatakiwa kujiunga na mfuko wa taifa ya wa bima ya Afya NHIF ili kuweza kuwahudumia wanafunzi katika kupata matibabu.Anne Makinda amesema kuwa katika maonesho ya sabasaba wamesajili bima za afya kwa watoto 1600 na kuongeza kuwa wananchi wamekuwa na mwitikio mkubwa katika kupata bima za afya. 

Amesema kuwa wameboresha bima ya afya katika mfuko wa afya ya jamii katika halmashari kwa kila aliyepata bima kutibiwa mkoa mzima tofauti na hapo nyuma kutibiwa katika Wilaya husika. Aidha amesema kuwa wataendelea kutoa huduma za bima za afya ikiwa ni pamoja na serikali kuweka mpango wa kila mtu kuwa na bima ya afya.
.Spika Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, Anne Makinda akikabidhi kadi za bima ya afya kwa watoto chini ya miaka 18 kwa wanachama wapya katika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam. 
.Spika Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, , Anne Makinda akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea banda la NHIF katika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Spika Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, Anne Makinda akipata maelezo kutoka Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti , Angela Mziray katika banda la NHIF katika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Sheik Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum akipata maelezo kutoka kwa Meneja Wanachama wa NHIF, Ellentruda Mbogoro katika banda la NHIF katika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.

Viewing all 110031 articles
Browse latest View live




Latest Images