Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110020 articles
Browse latest View live

USAJILI WA KWANZA KWA YANGA NI HUU, YAANZA NA BEKI WA KATI KUTOKA ZANZIBAR

$
0
0
Meneja wa timu ya Yanga Hafidh Saleh akimkabidhi jezi ya Yanga mchezaji mpya wa timu hiyo Abdallah Haji Shaibu "Ninja" aliyesajiliwa kutoka timu ya Taifa ya Jang"ombe akiingia kandarasi ya miaka miwili.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MABINGWA wa ligi kuu Vodacom  Tanzania klabu ya Yanga wamefanikiwa kupata saini ya beki wa timu ya Taifa ya Jang"ombe Abdallah Haji Shaibu "Ninja" ambaye walionyesha nia hiyo toka michuano ya Mapinduzi mwezi Januari Visiwani Zanzibar.

Kufanikisha kupata saini ya beki huyo kutoka visiwani Zanzibar, Yanga wanakuwa wamefanya usajili wao wa kwanza toka kumalizika kwa ligi msimu wa 2016/17.

Shaibu amepewa kandarasi ya miaka miwili akitarajiw akurithi mikoa ya Mzanzibar Nadir Haroub ' Canavaro' ambaye ameweza kuitumia klabu ya Yanga kwa takribani miaka 11 toka alivyojiunga.
Beki wa kati Abdallah Haji Shaibu "Ninja"  akiwa anasaini kandarasi ya kuitumika klabu ya Yanga akitokea timu ya Taifa ya Jang'ombe, kushoto ni Katibu Mkuu wa Yanga Charles Boniface Mkwasa.



MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AKABIDHIWA VIFAA TIBA VYA UZAZI ZAIDI YA 200 NA BALOZI WA KUWAIT HAPA NCHINI

$
0
0
Balozi wa Kuwait hapa nchini Jasem Al- Najem amemkabidhi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan vifaa tiba vya uzazi zaidi ya 200 ambavyo vitasambazwa katika hospitali mbalimbali kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

Makabidhiano ya vifaa hivyo vya uzazi yamefanyika leo Ikulu ya Dar es Salaam ambapo Balozi wa Kuwait hapa Nchini Jasem Al- Najem amesema Serikali ya nchi hiyo imetoa vifaa hivyo kama hatua ya kuendelea kudumisha na kuendeleza mahusiano mazuri kati ya nchi hiyo na Tanzania.

Amesema kuwa Serikali ya Kuwait imetoa vifaa hivyo ikiwa ni awamu ya kwanza na lengo ni kutoa vifaa hivyo zaidi ya 1000 vyenye thamani ya shilingi milioni 40 kwa wanawake wajawazito na waliojifungua katika hospitali mbalimbali nchini.

Mara baada ya kupokea msaada huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameishukuru Serikali ya Kuwait kwa msaada huo ambao utasambazwa katika hospitali mbalimbali kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea beseni lenye vifaa vya uzazi kutoka kwa Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem.Kuwait imetoa mabeseni 200 ya vifaa vya uzazi kwa hatua ya awali ambapo watatoa zaidi ya mabeseni 1000 yenye vifaa vya uzazi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).
Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan akitazama moja ya Dawa,mara baada ya kukabidhiwa mapema leo Ikulu jijini Dar,vifaa tiba vya uzazi zaidi ya 200 na Balozi wa Kuwait hapa nchini,Mhe,Jasem Al-Najem,vifaa hivyo vitasambazwa katika hospitali mbalimbali kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

Hatimae 'Pedeshee Ndama' huru kwa dhamana.

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii

Baada ya kufanikiwa kulipa faini ya milioni 200 hatimae leo mfanyabiashara , Ndama Shabani Hussein, maarufu kama Pedeshee Ndama mtoto ya Ng'ombe amepata dhamana.

Ndama amepata dhamana baada ya kuwa na wadhamink wawili na kuwasilisha hati ya mali isiyohamishika yenye thamani zaidi ya shilingi milioni 600.

Wiki iliyopita Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimtia hatiani Ndama na kumuhukumu kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya milioni 200 baada ya kukiri shtaka la kutakatisha USD 540,000.

Aidha mahakama hiyo iliyoketi chini ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa ilimsomea masharti ya dhamana mshtakiwa huyo iwapo angefanikiwa kulipa kiasi hicho cha milioni 200 ili awe huru katika mashtaka matano yanayoendelea kumkabili mahakamani hapo ambayo upelelezi wake bado haujakamilika.

Katika masharti hayo, Ndama alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika na atoe fedha taslimu kiasi cha USD 270,200 ambacho ni sawa na zaidi ya milioni 600 mahakamani hapo ama mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha

Licha ya kupata dhamana, Ndama amerudishwa gerezani kukamilisha taratibu kabla ya kuachiwa huru. 

Hukumu hiyo ya shtaka la sita la kutakatisha fedha ilitolewa baada ya Wakili wa Serikali, Christopher Msigwa kumsomea maelezo ya awali (PH) Ndama na kuyakubali maelezo ya awali na maelezo yote yanayounda shtaka hilo la kutakatisha fedha, akapatikana na hatiani na kupewa adhabu hiyo.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Wakili Msigwa aliiambia mahakama kuwa mshtakiwa amekubali shtaka la sita la kutakatisha fedha na maelezo yanayounda shtaka hilo, hawana kumbukumbu za nyuma za makosa dhidi ya Ndama ila ni rai ya upande wa mashtaka kuwa wakati mahakama ikitoa adhabu izingatie matakwa ya kifungu cha 13(a) cha sheria ya kuzuia utakatishaji fedha.

TANZANIA GOVERNMENT, BARRICK GOLD FOR AMICABLE TALKS ON ACACIA COMPANY'S WOES

$
0
0
By Sultani Kipingo

Tanzania’s President Dr. John Pombe Joseph Magufuli today met with the Executive Chairman of Barrick Gold Corporation Prof. John Lawson Thornton, and  both have agreed to start a dialogue to put to bed the sizzling Acacia company’s gold concentrate export ban.

President Magufuli hosted Prof Thornton at the State House in Dar es Salaam a few hours after the non-Independent executive chairman of Barrick jetted into the East African country by private jet in efforts to pull out of the quagmire.

“We just had extensive and very productive discussions about the situation here on Acacia, and I have come here in order to help resolve the problem,  and I have assured the President that we are very interested in sitting down and reaching a resolution which is a win-win – a win for Tanzania and a win for Barrick and our subsidiary company Acacia…

“And after having this extensive conversation I feel very optimistic that we will reach a resolution that is a win-win for all parties and will be sitting down soon by the team designated by the President and our team to go through the details and I feel very good about the progress today”, Prof. Thornton remarked after the meeting.

Barrick owns some 63.9% of shares in the Acacia Company, which has been accused of underpaying the Tanzania government tens of billions of dollars over the 20 years it has been operating in the country.

The government of Tanzania in March banned exports of unprocessed copper and gold, which Acacia says is costing it $1m a day.

Shares in Acacia Mining reportedly fell sharply on Monday after Tanzania accused the London-listed company of operating illegally, and indicated it wanted to take part ownership of the miner.

Barrick Gold Corporation is the largest gold mining company in the world, with its headquarters in Toronto, Ontario, Canada. It is also currently undertaking mining projects in Argentina, Australia, Canada, Chile, the Dominican Republic, Papua New Guinea, Peru, Saudi Arabia, the United States and Zambia. For 2013, it produced 7.2 million ounces of gold at all-in sustaining costs of US $915/ounce and 539 million pounds of copper at C1 cash costs of $1.92/pound. As of December 31, 2013, its proven and probable mineral reserves were 104.1 million ounces (3250 U.S. tons) of gold, 888 million ounces of silver contained within gold reserves, and 14.0 billion pounds of copper. 


On January 20, 2006, Barrick acquired a majority share of Placer Dome. The production of the combined organization moved Barrick to its current position as the largest gold producer, ahead of Newmont Mining Corporation.
Tanzania’s President Dr. John Pombe Joseph Magufuli today met with the Executive Chairman of Barrick Gold Corporation Prof. John Lawson Thornton after their meeting at the State House in Dar es salaam. Right is the Canadian High Commissioner to Tanzania Mr. Ian Myels

 Tanzania’s President Dr. John Pombe Joseph Magufuli  assures the Executive Chairman of Barrick Gold Corporation Prof. John Lawson Thornton  a fair deal after their meeting at the State House in Dar es salaam.
 Executive Chairman of Barrick Gold Corporation Prof. John Lawson Thornton speaks to the press after the meeting at the State House in Dar es salaam.
 Tanzania’s President Dr. John Pombe Joseph Magufuli speaks to the press after his meeting with the Executive Chairman of Barrick Gold Corporation Prof. John Lawson Thornton  at the State House in Dar es salaam.Right is the Canadian High Commissioner to Tanzania Mr. Ian Myels, second right is Tanzani's Minister for Justice and Constitutional Affairs Prof. Palamagamba Kabudi.
  Executive Chairman of Barrick Gold Corporation Prof. John Lawson Thornton speaks to the press after the meeting at the State House in Dar es salaam. Photo Courtesy of the State House



KIPINDI MAALUM: RAIS DKT MAGUFULI ALIPOKUTANA NA MWENYEKITI WA BARRICK GOLD CORPORATION PROFESA JOHN THORNTON

SERIKALI YAIONGEZEA BAJETI TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA NCHINI

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM-Dodoma

Serikali imeiongezea Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini kiasi cha shilingi bilioni 2.6 katika Bajeti yake ya mwaka 2017/2018 kwa kutambua na kuthamini majukumu yake katika Taifa.

Kauli hiyo imetolewa Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango (MB),Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maaluum (CCM), Mhe. Mwantumu Dau Haji aliyetaka kujua mpango wa Serikali kuiwezesha Tume hiyo kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Mhe. Mwantumu Haji amesema kuwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imekuwa ikitengewa fedha kidogo sana katika bajeti kwa zaidi ya miaka mitatu mfululizo hali inayosababisha Tume hiyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Akijibu swali hilo, Dkt. Kijaji alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2017/18, Serikali imetenga bajeti ya Sh. 6,166,978,000 kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 42.31 ya bajeti ya mwaka 2016/17 ambayo ilikuwa Sh. 3,557,589,200.

Alisema kuwa viwango vya ukomo wa bajeti kwa mafungu, hutegemea vipaumbele vya Taifa na maoteo ya mapato katika kipindi husika hivyo ongezeko la ukomo wa bajeti ya Tume hiyo kwa mwaka 2017/18 linaonesha dhahiri kuwa Serikali inatambua umuhimu wa Tume hiyo pamoja na majukumu yake.

Dkt. Kijaji aliongeza kuwa Serikali inaendelea kuimarisha mikakati ya ukusanyaji wa mapato ya ndani il kuhakikisha mafungu yote ya kibajeti ikiwemo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yanaendelea kupata fedha za kutosha ili kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

“Napenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, tarehe 01/06/2017 Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alizindua mfumo wa ukusanyaji mapato ya ndani ujulikanao kama ‘Revenue Gateway System’ ikiwa ni moja ya mikakati ya Serikali kuimarisha ukusanyaji mapato yake yatakayowezesha upatikanaji wa fedha za kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi”, alifafanua Dkt. Kijaji.

RAIS DKT MAGUFULI ATEUA MWENYEKITI WA BODI YA KITUO CHA UWEKEZAJI TANZANIA (TIC).

KOCHA MKUU WA STARS MAYANGA ATANGAZA KIKOSI CHA COSAFA

$
0
0


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Shabani Mayanga, leo Jumatano Juni 14, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 22 watakaounda kikosi kinachokwenda kushindana kuwania Kombe la Castle Cosafa nchini Afrika Kusini.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti, inatarajiwa kuanza kambi rasmi kesho Jumapili Juni 18, mwaka huu. Kambi hiyo itakuwa kwenye Hoteli ya Urban Rose, iliyoko Mtaa wa Jamhuri katikati ya jiji la Dar es Salaam.

 Afisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Alfred Lucas amesema kuwa kikosi hicho ambacho kimechaguliwa kimeweza kuongeza baadhi ya wachezaji wengine ikiwa pia ni katika kukiandaa kikosi hicho kwa ajili ya Michuano ya Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN).

Lucas amesema Taifa Stars inajiandaa na michuano ya Cosafa inayotarajiwa kuanza  Juni 25, mwaka huu. Michuano hiyo, inaandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika ambako Tanzania - mwanachama wa Cecafa, imepata mwaliko kushiriki.

Tanzania imepangwa kundi A ambako wapinzani wake ni Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B ni Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe. Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali.



Afisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Alfred Lucas 




HATI MILIKI ZA ARDHI ZA KIMILA ZINAKUBALIKA KATIKA TAASISI ZA KIFEDHA KUPATA MIKOPO

WAKAZI WA MJI WA SONGEA WAJITOKEZA KWA WINGI KUCHANGIA DAMU

$
0
0
Kila ifikapo juni 14 ya kila mwaka ni siku ya kuchangia damu kwa hiari ,katika mkoa wa ruvuma Wakazi wa manispaa ya songea wamejitokeza kwa wingi kuchangia damu Lakini licha ya wananchi kujitokeza kwa wingi manispaa ya MANISPAA YA SONGEA yakabiliwa na uhaba wa damu katika hospitali ya RUFAA YA MKOA WA SONGEA,KITUO CHA AFYA MJIMWEMA kama anavobainisha msimamizi wa shughuli za mahabara MAGRETHI NGONYANI. HABARI KAMILI HII HAPA VIDEO YAKE.

MAKONDA KUBADILI JESHI LA POLISI KWENDA KISASA KATIKA KUKABILIANA NA UHALIFU

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema jeshi la Polisi katika Mkoa huo linatakiwa  kuwa la mfano wa kuigwa katika kukabiliana na kila wimbi la uhalifu, ili wananchi waishi kwa amani kutokana na umuhimu wa biashara.

Makonda ameyasema hayo leo wakati wa kupeleka magari  26 ya polisi  kwenye ukarabati katika gereji  iliyoko  maeneo ya Utalii mkoani Kilimanjaro, kwa ajili ya matengenzo pamoja na ufungaji wa Kamera katika magari  hayo alipokuwa anazungumza na jeshi la polisi leo  Osterbay  jijini Dar es Salaam.

Amesema katika kukabiliana na rushwa na jeshi hilo, watafunga kamera katika kila kituo ndani ya jiji la Dar es Salaam,  ambapo OCD , kanda maalumu, pamoja  na Mkuu wa Jeshi la Polisi  wataweza kuona kile ambacho kinafanyika. 

Makonda amesema jeshi la Polisi Mkoa wa Dar es Salaam linatakiwa kuwa la kisasa zaidi katika kukabiliana na uhalifu wa kila namna ikiwa ni pamoja na kuwa na vifaa vya kisasa.

Amesema katika maboresho hayo wataweka Kompyuta kila kituo ili  kuachana na kuandika maelezo katika karatasi na mtu yeyote,  baada ya kuwekwa kompyuta hizo asikubali kuandikiwa maelezo katika karatasi.
Aidha amesema kuna baiskeli ziko njiani ambazo zitagawiwa kwa polisi ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na uhalifu katika mazingira ambayo kifaa hicho kinaweza kupita.

 Nae Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya  amesema Jeshi la Polisi kanda maalumu inakabiliwa na changamoto ya magari pamoja na mafuta na kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi katika kukabiliana na wahalifu wa kila namna .

Amesema kuwa kutokana maboresho hayo yataweza kubadilisha hata takwimu zilizo katika kipindi hiki zisirudie kutokana na maboresho hayo.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na watendaji  mkoa  na polisi katika hafla ya upelekaji wa gari 26 ya jeshi la polisi katika matengenezo mkoani Kilimanjaro leo jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya (wa pili kutoka kulia) akitoa ufafanuzi kuhusu magari yaliyoharibika  kwa ajili ya kwenda katika matengenezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda  (kulia) na watatu kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni , Ally Hapi leo katika Kituo cha Polisi Osterbay jijini Dar es Salaam.
 Moja ya gari mbovu ya Polisi ikiwa tayari kwa kusafirishwa kwa ajili matengenezo mkoani Kilimanjaro katika hafla iliyofanyika katika Kituo cha Polisi cha Osterbay jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na Wanajeshi wataopeleka magari kwa ajili ya matengenezo mkoani Kilimanjaro katika hafla iliyofanyika leo katika kituo cha Osterbay jijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS APOKEA TAARIFA YA KIKOSI KAZI KUTOKA MBEYA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewaagiza Wakuu wa wilaya nchini kuchukua hatua stahiki katika kulinda na kuhifadhi mazingira katika wilaya zao ili kukabiliana uharibifu mkubwa wa mazingira kwenye misitu na vyanzo vya maji ili visikauke na kuleta athari kwa binadamu na viumbe wengine.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo mara baada ya kukabidhiwa Taarifa ya Kikosi Kazi cha Mkoa wa Mbeya na Mkuu wa mkoa wa huo Amos Makalla kuhusu Mapendekezo ya Marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji katika wilaya za Mbarari na Chunya - Ikulu, Jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema tatizo la uharibifu wa mazingira katika baadhi ya wilaya nchini ni kubwa hivyo kuna umuhimu mkubwa kwa Wakuu wa wilaya kwa ushirikiano na watendaji wengine katika kukabiliana na hali hiyo kwenye maeneo yao.

Amesema kabla ya hatua kuchukuliwa ni vizuri wananchi wakaelimishwa kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira kabla ya kuondolewa kwenye maeneo waliyovamia ikiwemo maeneo ya vyanzo vya maji.

Makamu wa Rais pia amepongeza timu ya wataalamu wa kikosi kazi cha Mkoa wa Mbeya kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya inayolenga kuokoa mfumo wa ikolojia katika Bonde la Mto Ruaha Mkuu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa mkoa wa Mbeya Ndugu Amos Makala ya kikosi kazi cha mkoa wa Mbeya kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji kati ya Wilaya ya Mbarali na Chunya (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Mbeya Ndugu Amos Makala wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya kikosi kazi cha mkoa wa Mbeya kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji kati ya Wilaya ya Mbarali na Chunya (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza mbele Mkuu wa mkoa wa Mbeya Ndugu Amos Makala pamoja na kikosi kazi chake wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya kikosi kazi cha mkoa wa Mbeya kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya mpaka kati ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na Vijiji kati ya Wilaya ya Mbarali na Chunya (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

SERIKALI YAJIDHATITI KUTOKOMEZA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE KUFIKIA 2020.

$
0
0

NA WAMJW  DAR ES SALAAM

 SERIKALI imejidhatiti kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ili kutimiza malengo ya kujenga uchumi wa viwanda na afya bora mpaka kufikia 2020.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka unaolenga kupitia shughuli za mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

“Tunataka mpaka kufikia 2020 tuwe tumetokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi  kipaumbele  kama mabusha na matende ili kuweza kuinusuru nchi katika aina hii ya magonjwa yanayojitokeza katika nchi zinazoendelea hususan Tanzania” alisema Prof. Kambi.

Aidha Prof. Kambi amesema kuwa licha ya kudhibiti mabusha na matende pia wamejidhatiti kuzuia ugonjwa wa usubi na kichocho kabla ya kufikia 2025 ili kuendana na mpango wa dunia wa kudhibiti magonjwa hayo.
Kwa upande wake Mratibu wa Mpango wa Taifa Wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt. Upendo Mwingira amesema kuwa wananchi wanatakiwa wajitokeze kupata dawa na tiba za magonjwa hayo kwan hazina madhara kwa binadamu.

Mkutano huo uliokutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya afya  kutoka duniani kote umelenga kupata mpango kazi wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa mwaka 2017 na 2018 ili kuweza kupata njia za kudhibiti magonjwa hayo kama vile mabusha na matende, kichocho na usubi.
Mganga Mkuu wa Serikali Prof Bakar Kambi akiwasirisha mchango wake mbele ya wadau wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (Hawako kwenye picha) katika  mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za mpango wa Taifa wa wa udhibiti wa magonjwa hayo uliyofanyika Kunduchi jijini Dar Es salaam.
Mratibu wa Mpango wa taifa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt Upendo Mwingira akifuatilia kwa ukaribu mjadala uliokuwa ukiwasilishwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof Bakar kambi (hayupo kwenye picha) katika mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, anaefuatia ni Mkurugenzi wa Idara ya Afya TAMISEMI Dkt. Ntuli  Kapologwe na mkurugenzi wa kinga  Dkt Neema Ruzibamayila.
Wadau kutoka nchi mbali mbali wakifuatilia mjadala kwa ukaribu katika mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele uliofunguliwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof Bakar Kambi (Hayupo kwenye Picha) uliyofanyika Kunduchi jijini Dar Es salaam.
Wadau wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele wakiwa kwenye picha ya pamoja ikiongozwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof Bakar Kambi katika mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za mpango wa Taifa wa magonjwa hayo uliyofanyika Kunduchi jijini Dar Es salaam.

MAONESHO YA 41 YA SABASABA KUANZA JUNI 28 MWAKA HUU

$
0
0
Na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

Watanzania wameaswa kujitokeza katika maonesho ya 41 ya Biashara ya kimatifa jijini Dar es salaam yanayotarajia kuaanza June 28 mwaka huu katika kuangalia fursa mbalimbali za kibiashara zinazotokana na sekta ya Kilimo ilikuweza kufikia uchumi wakati unaolenga maendeleo ya viwanda.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Mamlaka ya Biashara Tanzania (Tantrade) , Theresa Chilambo wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya maandalizi yanayoendelea katika Viwanja Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa maaonesho ya mwaka huu yanatarajiwa kuwa nafursa nyingi za kilimo biashara kutokana makapuni mengi ya kimataifa kutaka kushiriki na kukuza ushiriki wao ilikuweza kutoa hamasa kwa mkampuni ya ndani.

‘’Mwaka huu kutakwa na banda maalum litakalohamasisha watanzania na wadau wa nje ya nchi kuweza kuhamasika kuweza kununua bidhaa za ndani ilikuhamasisha mchakato mzima wa made in Tanzania’’amesema Thesia chilambo.
Sehemu ya mafundi wakiwa katika ukarabati katika mabanda mbalimbali katika vwanja vya sabasaba.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Mamlaka ya Biashara Tanzania (Tantrade) , Theresia Chilambo akizungumza na waandishi habari juu ya maonesho ya 41 yatayoanza Juni 28 katika viwanja vya Sabasaba leo jijini Dar es Salaam.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU D9 CLUB


Viongozi wa Dini Watangaza Siku Saba za Kumwombea Rais Magufuli

$
0
0
Na Jonas Kamaleki- MAELEZO
Viongozi wa dini wametangaza maombi ya siku saba nchi nzima kumwombea Rais John Pombe Magufuli ili aendelee na juhudi zake za kulinda raslimali za watanzania kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam katika mahojiano maalum na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii ya dini zote, Askofu William Mwamalanga kwa niaba ya viongozi wa dini.

“Tumeamua kufanya maombi ya siku saba kwa kumtaka kila mtanzania popote alipo kutembea hatua saba kila siku akimwombea Mhe. Rais Magufuli ili Mungu amlinde pamoja na anaofanyanao kazi kwa usahihi (uaminifu)”, alisema Askofu Mwamalanga.

Ndani ya siku hizo saba kila mtanzania atakuwa ametembea jumla ya hatua 49 akimwombea Rais Magufuli na wezalendo wenzake.


Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Dini, maombi hayo yataanza kesho Alhamisi Juni 15(leo) nchi nzima na yatajumuisha watu wa dini zote nchini, yaani madhehebu ya Kiislam, Kikristo, Kihindu, Budha na madhehebu mengine.

Maombi haya yanafanyika baada ya kuona kuwa Mhe. Rais Magufuli kuchukua hatua madhubuti za kutaka waliohusika kwa namna yoyote kuiba raslimali za Taifa hususani madini, wanachukuliwa hatua na kuitaka kampuni ya ACCASIA kulipa kile ambacho walichukua kinyume cha sheria.

Askofu Mwamalanga amesema kuwa Kamati yake inamwomba Rais Magufuli achukue hatua za haraka kudhibiti raslimali za nchi kwa upande wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambako mali nyingi zinatoroshwa na wajanja wachache.

Kamati hiyo ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii ya dini zote imemwomba Mhe. Rais aziunganishe Wizara za Nishati na Madini na Maliasili na Utalii na kuunda wizara moja ambayo itasimamia kwa karibu raslimali za watanzania.

“Tunamwomba Rais Magufuli amchague mtu makini na mzalendo mwenye uchungu na nchi hii ili asimamie wizara hiyo, na nina hakika wizara hiyo ikisimamiwa vizuri, ndoto ya Rais ya kuifanya Tanzania kuwa nchi mhisani itatimia kwa kuwa hapa Mungu ametujalia kila kitu”,alisema Askofu Mwamalanga.

Viongozi hao wamempongeza Rais Magufuli kwa Uzalendo na Ujasri alionao katika kulinda raslimali za Taifa na kupambana na maovu. Wamesema ni kiongozi wa kuigwa na Marais au viongozi Duniani kote.

Kuhusu suala la walioachishwa kazi kutokana na kuwa na vyeti feki, Askofu Mwamalanga amesema kuwa Kamati inamwomba Mhe Rais kuwasamehe wale ambao wameitumikia nchi hii kati ya miaka mitano na 30 ili walau wapatiwe kifuta jasho licha ya kwamba walitumika bila kuwa na vyeti halali vya Kidato cha nne.

“Msamaha tunaoomba si wa kuwarudisha kazini bali tunaomba kwa ajili ya kupata kiinua mgongo kwani wengine walitumika kwa uaminifu na hata kupewa tuzo za ufanyakazi hodari (bora) hasa katika sekta za Afya,wauguzi, Elimu na maeneo mengine”, alisema Askofu Mwamalanga.


Mapema wiki hii, Rais Magufuli alipokea ripoti ya pili ya uchunguzi wa makinikia ambayo iliwajumuisha wanasheria na wachumi. Katika ripoti hiyo ilibainika kuwa kiasi kikubwa cha madini kilichukuliwa bila watanzania kupata chochote. Takriban madini yenye thamani ya shilingi trilioni 108 yalisafirishwa nje ya nchi bila Tanzania kupata faida kutokana na madini hayo.

MICHUZI BEAT: BODA BODA SINZA MAKABURINI

Ngoma azipendazo ankal

$
0
0

Bokelo Isenge - tambola na mokili.

Kampuni ya Wazawa, yakamilisha hatua za Msingi kuuza hisa zake kwa watanzania - Maxmalipo

$
0
0

Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr.Donalth Ulomi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza hati iliyopewa kampuni hiyona ambayo inaiwezesha Kampuni kumilikiwa na Umma wa watanzania.

Akiongea na Wanahabari Dr. Ulomi amesema kwamba Kuanzia Sasa Kampuni ya Maxcom Africa itatambulika kwa Jina la Maxcom Africa Public Limited Company (Maxcom Africa PLC) . Kampuni hii maarufu kwa jina la Maxmalipo ni Moja ya Kampuni zilizoanzishwa na kuendeshwa na wazawa watanzania ambayo imeifikia hatua za Mwisho katika mchakato wa kuanza kuuza hisa zake kwenye soko la hisa. Dr. Olumi amewaambia wanahabari kwamba wanasubiri kibali cha wasimamizi wa Soko la Hisa ili waweze Kuorodhesha Kampuni yao katika Soko hilo

Kampuni hii ilianzishwa mwaka 2008 na mpaka leo imefika nchi zaidi ya 5 barani Africa.Hafla hiyo ya uzinduzi wa uuzaji wa hisa ulifanyika mapema leo katika makao makuu ya Maxcom Africa Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam.

Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr. Donalth Ulomi (kulia ) akikata utepe wa kuzindua rasmi Jina Lipya la Kampuni ya Maxcom Africa PLC anayeshuhudia ni Mkurungezi wa Uendeshaji wa Maxcom Africa Bw.Ahmed Lusasi mapema leo katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika makao makuu ya Maxcom Africa PLC Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam.
Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr,Donalth Ulomi (kulia ) akionesha nembo ya jina jipya Maxcom Africa PLC na kushoto kwake ni Mkurungezi wa Uendeshaji wa Maxcom Africa Bw.Ahmed Lusasi mapema leo katika hafla ya uzinduzi wa Jina jipya la Kampuni hiyo iliyofanyika makao makuu ya Maxcom Africa PLC Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam
Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr. Donalth Ulomi akifanya mahojiano na mwandishi wa habari mara baada ya uzinduzi rasmi wa Jina Jipya la Kampuni ya Maxcom Africa PLC.

Mjumbe wa Bodi ya kampuni ya Maxcom Africa Dr. Donalth Ulomi akifanya mahojiano na mwandishi wa habari mara baada ya uzinduzi rasmi wa Jina Jipya la Kampuni ya Maxcom Africa PLC. 

FILAMU YA KISOGO YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
  Msanii wa Filamu nchini Salim Ahmed maarufu Gabo Zigamba (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa filamu yake fupi ya Kisogo mapema jana jijini Dar es Salaam, kulia ni Afisa Mawasiliano wa Kampuni ya Sarafu Media Bw. Myovela Mfwaisa. 
 Afisa Habari wa Kampuni ya Sarafu Media Bw. Myovela Mfwaisa (katikati) kushoto akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa filamu fupi ya Kisogo mapema jana jijini Dar es Salaam, kushoto Msanii wa filamu hiyo Bw. Salim Ahmed maarufu Gabo Zigamba na kulia ni Mtaalam wa TEHAMA toka Kampuni ya Uhondo Bw. Amon John. 
 Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia filamu fupi ya Kisogo wakati ikizinduliwa na msanii wa filamu hiyo Salim Ahmed maarufu Gabo Zigamba.

Picha zote na Eliphace Marwa - Maelezo
Viewing all 110020 articles
Browse latest View live




Latest Images