Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110020 articles
Browse latest View live

MAVUNDE AFUNGUA MPANGO WA UFUNDI WA KISASA WA KUTENGENEZA BIDHAA ZA NGOZI JIJINI MWANZA

$
0
0
 Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe Anthony Mavunde amefungua mpango wa mafunzo ya ufundi wa kisasa wa kutengeneza viatu kwa njia za kisasa kwa vijana 1000 wanaotaka mikoa zaidi ya kumi nchini.

Akizundua mpango huo katika karakana ya viatu na bidhaa za ngozi ya Taasisi ya Teknlojia ya Dar es salaam (DIT) tawi la  Mwanza, Mhe Mavunde, amesema mpango huo unalenga kuwajengea uwezo wa kujiajiri vijana na pia kutumia bidhaa zitokanazo na mazao ya mifugo kwa ajili ya kuzalisha viatu na bidhaa za ngozi nchini.

Amesema, serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli imejipanga kuhakikisha inatekeleza azma ya ujenzi wa viwanda kwa kuwajengea uwezo vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa katika kujiandaa na mfumo wa mapinduzi ya viwanda ambavyo vimeshaanza kujengwa nchini.
Aidha amewataka vijana kutochagua kazi au kubweteka kuwa kazi rasmi ni zile za ajira ya moja kwa moja serikali au sekta binafsi, amewataka vijana kubadilisha mtazamo wa maaana ya Ajira kwa kutokukaa na kusubiri nafasi za ajira.Amesema mpango huu wa miaka mitano unalenga kuwafikia vijana zaidi ya milioni 4 nchini katika kuwajengea uwezo ambao utawafanya kujiajiri au kuajiriwa katika Tanzania ya viwanda.

 Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe Anthony Mavunde akikagua ngozi zinazotumika kwenye mafunzo hayo katika Taasisi ya Teknlojia ya Dar es salaam (DIT) tawi la  Mwanza
 Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe Anthony Mavunde akitembelea karakana ya Taasisi ya Teknlojia ya Dar es salaam (DIT) tawi la  Mwanza
 Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe Anthony Mavunde akishuhudia sehemu ya vijana hao 1000 kutoka mikoa zaidi ya kumi wakijifunza namna ya kutengeneza viatu
Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe Anthony Mavunde katika picha ya pamoja na vijana hao pamoja na wakufunzi wao. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

INTRODUCING NEW HIT SINGLE "WAPI" by Peter Msechu produced by Armyz

MBUNGE WA MUFINDI MJINI ATOA MSAADA WA VITANDA SHULE YA SEKONDARI YA ISALAVANU

$
0
0
 Hii ndio hali ilivyokuwa kwa Wanafunzi  wa shule ya Sekondari ya Isalavanu wilayani Mufindi mkoa wa mkoani Iringa ambao walikuwa wanalala kwa kutandika magodoro sakafuni. Zishukuriwe jitihada za Mbunge wa Mufindi mjini Mhe. Cosato Chumi ambaye kwa kushirikiana na  wadau wake wa maendeleo amekabidhi vitanda 35 aina ya double decker kuondoa adha hiyo.
 Wanafunzi  wa shule ya Sekondari ya Isalavanu wilayani Mufindi mkoa wa mkoani Iringa wakimshangilia Mbunge wa Mufindi mjini Mhe. Cosato Chumi wakati anashusha vitanda vyao
Vitanda 35 aina ya double decker vikiwa vimewasilishwa shuleni hapo na Mbunge wa Mufindi mjini Mhe. Cosato Chumi.

SPEECH BY HIS EXCELLENCY MBELWA KAIRUKI, AMBASSADOR OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA TO THE PEOPLE’S REPUBLIC OF CHINA, AT THE OPENING OF WOMEN EMPOWERMENT CONFERENCE ON 3 June 2017, BEIJING

$
0
0
Our Host, Madam Angelina Makoye,

Invited guests,

Ladies and Gentlemen,


Welcoming remarks

I thank the organizers for inviting me to join you this afternoon at the opening of the Women Empowerment and Mentorship Seminar. In particular I commend Ms Angelina Makoye for this wonderful and innovative idea to convene this meeting that provides an opportunity to bring women’s perspective to One Belt, One Road Initiative.

I keenly listened to Ms. Makoye’s welcoming statement and asked myself, what else I can talk about, because, she said it all.  If it was my decision, I would have said that we should straight go to important items of the meeting – which is to listen to our guest speakers who will give us inspirational talk relevant to today’s subject.

But since, I have this opportunity to speak let me say few words about One Belt, One Road initiative,  and its potential contribution to women empowerment.

Ladies and Gentlemen,

Our event today is taking place few weeks after the historical high-level forum on the Belt and Road Initiative that took place here in Beijing.  May I seize this moment to commend His Excellency President Xi Jinping for the visionary and innovative idea of One Belt and One Road.  The Revival of the Silk Road Economic Belt and the 21st Century Maritime Silk Road has won wide support from the international community, and there is now a broad international consensus on quickening its implementation.   Our gathering here is a clear testimony that One Belt, One Road Initiative is not a solo performance or an empty slogan, but a series of concrete discussions and actions taking place at local, regional and global stage to bolster up the global and regional economy. 
To read more CLICK HERE

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNE 4,2017

KATIBU MKUU MAENDELEO YA JAMII AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA DC WA MISUNGWI

$
0
0

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akifafanua jambo kwa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Juma Samwel Sweda ( wa pili kulia) wakati alipomtembelea Ofisini kwake hivi karibuni.
Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Juma Samwel Sweda akizungumza na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga(kulia) alipomtembelea Ofisini kwake hivi karibuni.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw.Elliurd Mwaitekele(kushoto) akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga(hayupo Pichani) wakati Katibu Mkuu huyo alipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi hivi karibuni kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Bi Deodata Makani na Kaimu Mkurugenzi wa Manunuzi kutoka Wizara hiyo Bi. Martha Chuma.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto(Maendeleo yaJamii) Bi. Sihaba Nkinga(kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw.Elliurd Mwaitekele(kulia) wakati wakijadiliana jambo mara baada ya Katibu Mkuu huyo kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi hivi karibuni.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga(kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe.Juma Samwel Sweda(kulia) wakati wakijadiliana jambo mara baada ya Katibu Mkuu huyo kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya huyo hivi karibuni.Picha zote na Raymond Mushumbusi MAELEZO Misungwi Mwanza.


WASTAAFU PSPF MWAKA 2017/18 "KULAMBA" SHILINGI TRILIONI 1.3 ZA MAFAO

$
0
0

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said 

Katika hotuba yake aliyotoa Kati wa ufunguzi rasmi wa semina hiyo, Bw. Mayingu alisema, PSPF inatarajia kulipa wastaafu kiasi cha shilingi Trilioni 1.3 kwa mwaka huu tu wa 2017/18."Kwa mwaka 2017/18 pekee, Mfuko unatarajia kuwalipa wastaafu 9,552 jumla ya mafao yanayofikia shilinginTrilioni 1.3.

Kisai hiki cha Mafao ni kikubwa, hivyo kupitia semina hii Wastaafu watarajiwa wa PSPF wamejifunza namna ya kupanga maisha yao baada ya kustaafu ikiwa ni pamoja na fursa za uwekezaji wa mafao yao ili mafao haya yaweze kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya uchumi na kuongeza fursa za ajira." Alisema Bw. Mayingu katika hotuba yake. 

Miongozi mwa mambo waliojifunza wastaafu hao wanaokadiriwa kufika 450, ni pamoja na uanzoshwaji wa viwanda vidogo vidogo, namna bora ya utunzaji fedha kwenye taasisi za fedha, (mabenki), lakini pia mbinu mbalimbali za ujasiriamali. 

Kuhusu mafunzo yaliyotolewa na SIDO, Bw. Mayingu alisema Mfuko ulikutana na Shirika la Kuhudumia Viwanda vidogo vidogo (SIDO) na kujadiliana namna ambavyo taasisi hizi mbili zinaweza kushirikiana na kuwafanya wastaafu wa PSPF wapate ujuzi wa kuwekeza na kuweza kutengeneza ajira kwa vijana. 

"Lengo likiwa SIDO iwajengee uwezo kitaalamu na kuwapatia vifaa ili wastaafu wa PSPF waweze kuanzisha viwanda vidogo vidogo na shughuli nyingine za uzalishaji." Alisema Bw. Mayingu. Alisema wameamua kufanya hivyo kwa kzuingatia ukweli kuwa, katika kufuatilia wastaafu wa Mfuko wamegundua kuwa baadhi yao hujiingiza katika biashara mbalimbali ambazo hawakujiandaa vema na matokeo yake kupoteza mafao yao.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, aliongozana na Mkurugenzi wa Uendeshaji Bi. Neema Muro na Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji Bw. Gabriel Silayo, baada ya kufungwa kwa semina kwa wastaafu watarajiwa wa wilaya zote za mkoa wa Mwanza iliyofanyika ukumbi wa chuo cha watumishi wa Benki Kuu ya Tanzania, huko Capri-point jijini Mwanza. 

Bw. Mayingu, (kushoto), akijadiliana jambo na Bwana Dominic Haule, Mkurugenzi IMADS, (wakwanza kulia), wengine wanaosikiliza kutoka kushoto ni Bi. Neema Muro, Bw. Gabriel Silayo, Bw.Bw.Luseshelo Njeje na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi, baada ya kufungwa kwa semina hiyo
Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, (kushoto), Mkurugezni wa Uendeshaji, Bi.Neema Muro, (katikati) na Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji, Bw. Gabriel Silayo, wakifurahia michango ya mawazo kutoka kwa washiriki wa semina.
Washiriki wakijadiliana.

KATIBU MKUU MAENDELEO YA JAMII ATEMBELEA CHUO CHA MAENDELEO YA JAMII (UFUNDI) MISUNGWI.

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto(Maendeleo yaJamii) Bi. Sihaba Nkinga( wa pili kulia) akiongozana na watendaji kutoka Wizarani pamoja na viongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Misungwi alipotembelea katika Chuo hicho kwa ziara ya kikazi hivi karibuni.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto (Maendeleo yaJamii) Bi. Sihaba Nkinga(wa tatu kulia) akimsikiliza Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Misungwi Mhandisi Harold Jackson Mtyana (kulia) alipokuwa akimuelezea kuhusu chumba cha Kompyuta cha Chuo hicho wakati wa ziara yake ya kikazi hivi karibuni.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto (Maendeleo yaJamii) Bi. Sihaba Nkinga akitumia moja ya Kompyuta zilizopo katika Chumba cha Kompyuta cha Chuo cha Maendeleo ya Jamii Misungwi ikiwa ni mradi uliwezeshwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Korea ya Kusini.
Muonekano Chumba cha Kompyuta cha Chuo cha Maendeleo ya Jamii Misungwi ikiwa ni mradi uliwezeshwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanznia na Serikali ya Korea ya Kusini.Picha zote na Raymond Mushumbusi MAELEZO Misungwi Mwanza.


VIONGOZI WAMIMINIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU NDESAMBURO KUTOA POLE KWA FAMILIA

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson akitoa mkono wa pole kwa mama Mjane wa Marehemu Dkt Philemoni Ndesamburo ,Ndehorio Ndesamburo alipotembelea nyumbani kwa marehemu kuifariji familia. 
Mwenyekiti wa Chadema Taifa na Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni ,Freeman Mbowe akitoa mkono wa Pole kwa mjane wa marehemu Dkt Ndesamburo ,Ndehorio Ndesamburo nyumbani kwake KDC mjini Moshi.
Waziri wa Malisili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akitoa pole kwa mama mjane wa marehemu Ndesamburo nyumbani kwake KDC mjini Moshi.
Mbunge wa jimbo la Same Magharibi ,David Mathayo David akitia saini katika kitabu cha waombolezaji nyumbani kwa marehemu Dkt Philemoni Ndesamburo.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro,Idd Juma akitia saini katika kitabu cha waombolezaji nyumbani kwa marehemu Ndesamburo KDC Mjini Moshi.
Mkuu wa mkoa wa Arusha ,Mrisho Gambo akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Rombo Joseph Selasini walipokutana nyumbani kwa marehemu Ndesamburo.

TPDC YAIBUKA MSHINDI WA TUZO YA BANDA BORA SEKTA YA NISHATI NA MAZINGIRA

$
0
0
Waziri wa Malisili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe kushoto akimkabidhi  Afisa Uhusiano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Augustino Kasale tuzo ya mshindi wa banda bora la sekta ya nishati na mazingira katika maonyesho ya Kimataifa ya Biashara wakati alipokwenda kuyafunga kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella.
 Waziri wa Malisili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe kushoto akifurahia jambo na  Afisa Uhusiano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Augustino Kasale mara baada ya kumkabidhi tuzo ya mshindi wa banda bora la sekta ya nishati na mazingira katika maonyesho ya Kimataifa ya Biashara wakati alipokwenda kuyafunga kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella.
 Watumishi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wakiongozwa na Afisa Uhusiano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Augustino Kasale kulia na katikati ni Mwanasheria wa TPDC Kelvin Gadi wakiwa na tuzo yao walioipata.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

TEMBO 110 WAVAMIA MASHAMBA, WAUA MWANAKIJIJI MMOJA TUNDURU

$
0
0
Tembo 110 wamevamia mashamba ya wananchi na kufanya uharibifu wa mazao katika kata za Mbati,Kalulu,Namwinyu na Jakika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma na kuua mk azi mmoja wa Mbwembwele aliyejulikana kwa jina moja la Kalengo mwenye umri wa miaka 70, Taarifa zaidi hii hapa video yake.

CUF YA MAALIM SEIF YAZINDUA OFISI MAGOMENI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

Suleiman Msuya


IKIWA ni takribani miezi 10 sasa kwa Chama cha Wananchi (CUF), upande wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad kuvamiwa katika Ofisi Kuu za Bugurunina kundi la Profesa Ibrahim Lipumba chama hicho kimezindua ofisi mpya za chama hicho katika eneo la Mtaa wa Idrisa, Kata ya Mzimuni, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Aidha, Seif amesisitiza kuwa hatarajii kukutana na  Profesa Lipumba kwa kile alichodai kuwa hatambuliki katika chama na hana  sifa hizo kwa sasa.


Akizindua ofisi hiyo ambayo lengo kubwa ni kwa ajili ya wabunge 40 wa CUF, Seif alisema  uamuzi wa wabunge hao kumpatia ofisi ya kufanyia kazi hapo ni cha kiungwana na kinahitajika kuungwa mkono na wanachama wote.


Alisema kwa muda wa miezi 10 sasa wamekuwa wakishindwa kufanya kazi hasa upande wa Tanzania Bara jambo ambalo limewaathiri sana hivyo kupatiwa ofisi kutamsaidia kutimiza majukumu yake vilivyo bila hofu yoyote.


Maalim Seif alisema kukosa ofisi kumewaathiri sana katika baadhi ya mambo hivyo anaamini kwa sasa akifikia Dar es Salaam anamahali pa kukutana na wakurugenzi wake.


“Nimekuwa ni kija hapa nakosa sehemu ya kukutana na wakurugenzi, viongozi mbalimbali wanachama ila hiki ambacho wabunge wamefanya ni cha kuungwa mkono sijawahi kufanya kazi na wabunge wanao kipenda chama kama kipindi hiki,” alisema.


Katibu huyo alisema atahakikisha kuwa anaanza kazi haraka iwezekanavyo kwa kukutana na wakurugenzi wake ili waweze kutekeleza majukumu ya chama.


“Hakuna shaka kuwa hu u unaoitwa mgogoro umeturudisha nyuma sana hivyo naamini wakati wa kufanyakazi umerejea na hawa wabaya wetu hawata ambulia kitu kwani CUF ni  chama imara hakitikisiki,” alisema.


WAZIRI WA MALISILI NA UTALII AZINDUA MAONESHO YA KIMATAIFA YA UTALII NA VIWANDA MKOANI KILIMANJARO.

$
0
0
Waziri wa Malisili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho ya tatu ya kimataifa ya Utalii yanayofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu Ushirika mjini Moshi.
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Devota Mdachi akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa maonesho makubwa Afrika Mashariki ya Utalii na Viwanda yanayofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu Cha Ushirika mjini Moshi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTB,Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akisalimia wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akitoa neno kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho ya Kili Fair yanayojumuisha zaidi ya washiriki 300 kutoka nchi tisa.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akimsadia Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii,TTB Bi Devota Mdachi kufika katika eneo la mfano wa Kilele cha Uhuru ,Mlima Kilimanjaro.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe ,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi (TTB) Jaji Mstaafu ,Thomas Mihayo,Mkuu wa wilaya ya Moshi Kippi Warioba na viongozi wengine wakiwa katika kilele cha Uhuru cha Mfano kilichopo katika maonesho yanayoendelea katika uwanja wa chuo kikuu cha ushirika mjini Moshi.

RC TABORA ASISITIZA VITAMBULISHO KWA WATU WOTE WALIOPO KATIKA ENEO LA MACHIMBO YA KITUNDA.

$
0
0
Na Tiganya Vincent-RS-Tabora

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri amuagiza Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge kushirikana na Kampuni zenye leseni ya uchimbaji madini ya dhahabu kuhakikisha wachimbaji wadogo wadogo na wafanyabiashara waliopo eneo la machimbo ya dhahabu ya Kitunda wanapatiwa vitambulisho kwa ajili ya kuimarisha usalama na utambuzi wao wakati wakifanya shughuli hiyo.

Bw. Mwanri alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na Watendaji wa Halmashauri ya Sikonge na viongozi wa Kampuni zote zilizopewa leseni ya uchimbaji madini ya dhahabu katika eneo la Kitunda.

Alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuwatambua wachimbaji wadogo wadogo na wafanyabiashara  wote walioajiriwa na wale waliojiajiri  ili kuepuka mgongano ambayo umekuwa ukijitokeza kwa baadhi ya wachimbaji wadogo wadogo kuvamia machimbo ya wenzao wanaposikia yana dhahabu na hivyo kusababisha mrundikano wa watu wengi katika shimo moja na kuhatarisha usalama wao.

Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kuwa vitambulisho hivyo pia vitasaidia kuwatambua wachimbaji wadogo wadogo wa Kampuni moja na nyingine  ili kuepuka vurugu.

Alisema kuwa kabla ya zoezi hilo kufanyika ni vema uongozi wa Halmashauri na Kampuni zote uwe na taarifa sahihi za mhusika ikiwa ni pamoja na mahali alipozaliwa na uraia wake ili kuepuka kutoa ajira kwa wageni badala wachimbaji wadogo wadogo wa Kitanzania.

Bw. Mwanri alisema mtu asianze kazi za uchimbaji kabla ya kusajiliwa katika daftari kubwa na lile na mitaa ili Serikali ijue ni nani waliopo hapo na wanatoka wapi katika nchi hii ya Tanzania.

DKT ANSIGAR STUFFE OSB AFUNGUA MRADI WA MAJI WENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 60 KATIKA KIJIJI CHA LIGANGA

$
0
0
Asilimia kubwa ya mwili wa binadamu unategemea maji lakini maji yamekuwa tatizo kubwa kwa jamii yetu ya Tanzania ,Ni miaka 29 sasa imepita tangu mkurugenzi wa hospitali ya peramiho ambaye pia ni daktari bruda ANSAGAR STUFFE OSB kuhakikisha jamii ya taarafa ya ruvuma inaondokana na huba wa maji.

mambo ya Gado

Sheikh Shariff amaliza Ziara yake jijini Arusha,kuelekea Tanga

$
0
0
 Sheikh Shariff Majini kutoka Dar es salaam leo Jumapili amemaliza ziara yake Jiji Arusha kwa kufanya mkutano mkubwa katika stendi ya Hiace jirani na Soko la Kilombero.

Ikumbukwe Sheikh alianza ziara Arusha siku ya Jumapili tarehe 28 May ambapo aliendesha Dua katika ukumbi wa C.C.M Mkoa.

Aliendeleabnq mkutano wa nje siku ya Jumamosi tarehe 03 Juni na amemaliza mikutano yake Jumapili tarehe 04 Juni kati viwanja vya stendi yaa Hiace jirani na soko lq Kilombero Jijini Arusha.

Jumatatu tarehe 05-06-2017 Sheikh ataanza ziara Mkoa wa Tanga ambapo Junamosi tarehe 10 Juni na Jumapili Juni atafanya mkutano mkubwa pamoja na mambo mengine atafanya Dua kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa saba mchana ili kuwahi kuandaa futru kwa akina mama.
 Sehemu ya umati wa wakazi wa Arusha waliojitokeza kwenye mkutano wa Sheikh Shariff Majini.
 Sehemu ya umati wa wakazi wa Arusha waliojitokeza kwenye mkutano wa Sheikh Shariff Majini.
Sheikh akiongoza dua pamoja na kuombea watoto waliofika mkutanoni.

TAIFA STARS IKIJIFUA JIJINI ALEXANDRIA, MISRI

$
0
0
 Kipa Aishi Manula, akichupa kudaka mpira wakati wa mazoezi yanayosimamiwa na Kocha wa Makipa wa Taifa Stars, Patrick Mwangata aliyepiga magoti katika mazoezi yanayofanyika Kituo cha michezo cha Tolip (Tolip Sports City) hapa Alexandria, Misri. Taifa Stars  inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti inayozalishwa na Kampuni ya Bia ya SBL, inajiandaa kucheza na Lesotho Juni 10, 2017 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataiafa ya Afrika (AFCON) za mwaka 2019 zitakazofanyika Cameroon. 
 Kipa Said Mohammed Nduda , akichupa kuzuia mpira wakati wa mazoezi yanayosimamiwa na Kocha wa Makipa wa Taifa Stars, Patrick Mwangata aliyepiga magoti katika mazoezi yanayofanyika Kituo cha michezo cha Tolip (Tolip Sports City) hapa Alexandria, Misri. 
 Kipa Benno Kakolanya, akidaka mpira wakati wa mazoezi yanayosimamiwa na Kocha wa Makipa wa Taifa Stars, Patrick Mwangata aliyepiga magoti katika mazoezi yanayofanyika Kituo cha michezo cha Tolip (Tolip Sports City) hapa Alexandria, Misri. 
 Kiungo wa pembeni wa Taifa Stars, Simon Msuva akiwa kwenye kasi kuwahi mpira wakati wa mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika Kituo cha michezo cha Tolip (Tolip Sports City) hapa Alexandria, Misri. 
Libero wa Taifa Stars, Erasto Nyoni (katikati) akijitahidi kudhibiti mpira mbele ya washambuliaji wenye njaa ya kufunga, Ibrahim Ajib (kulia) na Abderheman Mussa kabla ya kipa Said Mohammed hajatokea kusaidia wakati wa mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika Kituo cha michezo cha Tolip (Tolip Sports City) hapa Alexandria, Misri.  Picha na Alfred Lucas wa TFF.

RAIS MSTAAFU MWINYI NA WASHINDI WA FAINALI YA MASHINDANO YA KITAIFA YA KUHIFADHI QURAN LEO

$
0
0
Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi (waliosimama katikati) akiwa na wageni waalikwa na baadhi ya vijana walioibuka washindi kwenye fainali ya mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi Quran Tukufu kutoka Tanzania Bara na Visiwani yaliyofanyika ndani ya viwanja vya Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam jana, chini ya uratibu wa Taasisi ya Al-Manahilul Irfan Islamic Centre. Wa pili kulia waliosimama ni Makamu wa Rais mstaafu Dk Gharib Bilal

SAKA SAKA YAKITA UKONGA, MAJUMBA SITA – ILALA

$
0
0
Kituo cha Efm redio kimekabidhiwa kiasi cha shilligi Milioni moja na laki tano (1,500,000/=) pesa taslimu kwa washindi mbali mbali walioshiriki katika mchezo wa saka saka (treasure hunt) leo tarehe 04/06/2017 kwa wakazi wa wilaya ya Ilala – Ukonga (Majumaba sita) katika kiwanja cha Gonga. Huu ni msimu wa tatu wa Saka saka tokea mchezo huu umeanzishwa na mwaka huu itafanyika katika wilaya tano, Kigamboni, Ilala, Ubungo, Temeke kwa Dar es salaam na Bagamoyo kwa wilaya ya Pwani.
 Denis Rupia( kulia ) mtagazaji wa E-fm radio akiwaanamuhoji moja ya mshiriki wa Saka saka (katikati)  na Aneth Mrindoko- Afisa matukio, uhusiano na mwasiliano (kushoto) akiwa anakagua kitu kilichotolewa na mshiriki kama ndicho kilichofichwa na Efm.
 Baadhi wa wananchi wa Ukonga wakishuhudia zoezi zima lililokuwa linaendelea.
 Baadhi ya washiriki wa Saka saka wakiwa wako tayari kwa ajili ya uhakiki wa kile walichokiokota ni kitu kilichokuwa kimefichwa na Efm redio.
 Lulu Riziki Magala ambae ni mshindi wa kwanza aliye ibuka na shilingi 1,000,000 pesa tasilimu za kitanzania.
 Moja ya washindi Mohamed Madiga akikabidhiwa kiasi cha shilingi elfu hamsini na Jesca Mwanyika - Afisa matukio, uhusiano na mawasiliano.
Viewing all 110020 articles
Browse latest View live




Latest Images