Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

MWENGE WA UHURU WAKAGUA MIRADI MANISPAA YA KIGAMBONI YA SH.BILIONI 229.4

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
 MWENGE wa Uhuru umezunguka katika Wilaya ya Kigamboni na kugagua miradi ya maendeleo saba yenye thamani ya Sh bilioni 229.4
Akizungumza wakati wa kuitimisha Kata ya Kimbiji wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam, Mkuu wa  Wilaya hiyo, Hashimu Mgandilwa,  aliitaja miradi hiyo ikiwa ni pamoja na Barabara inayounganisha daraja la Mwalimu Nyerere na barabara ya Ferry kwa thamani ya Sh.bilioni 21.
Mwenge huo umezindua Chama Cha Kuweka na kukopa cha Tulemune  chenye  mtaji wa Shilingi milioni 25, Mradi wa Ufugaji wa Samaki katika kata ya Kibada wenye thamani ya Shilingi milioni 400.
 Mgandilwa amesema Mwenge wa uhuru umewezesha kuzinduliwa kwa miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuzindua Jengo la kutolea huduma ya mama na mtoto pamoja na vifaa vya zahanati ya Kisarawe II.
 Kiongozi wa Mbio za Mwenge, Amour Hamad Amour, aliwataka wananchi kuendelea kuanzisha viwanda ili kufanikisha kampeni ya serikali ya kufikia uchumi wa kati tutakapofikia mwaka 2020.
Amesema kuwa watu hawapaswi kusubiri kupata mitaji mikubwa ndio waanzishe viwanda na kwamba wanapaswa kuanzia katika viwanda vidogo kwani hata nchi zilizoendelea zilianza hivyo.
Makamu wa Rais wa Kiwanda cha Lake  kinachozalisha saruji ya Nyati, Afroz Ansary aliiomba Serikali kukarabati miundombinu ya barabara ya kuelekea kiwandani hapo kwani imekuwa changamoto kwa biashara ya kampuni hiyo.
Amesema  kutoka na barabara kutokuwa muzuri kiwanda hicho kimekuwa kikisitisha uzalishaji wa saruji kutokana na kuwa na shehena kubwa kwenye maghala yao.
"Kwa muda sasa tuna shida ya barabara ya kuingia kiwandani huku jambo ambalo limekuwa likikwamisha usafirishaji hususani katika kipindi cha Mvua.
"Mzigo hautoki wala hatuingizi baadhi ya vitu muhimu katika kuendesha kuwanda kama vile makaa ya mawe hivyo kusababisha kodi ya serikali isipatikane ya kutosha, pia kuathiri wafanyakazi kwa kuchelewesha mishahara yao,"
Mwenge wa Uhuru ukiwa katika kiwanda cha Lake Cement kilichopo Kimbiji Manispaa ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam .
Kiongozi wa Mbio za Mwenge, Amour Hamad Amour akipanda mti katika kiwanda cha Lake Cement kilichopo Kimbiji Manispaa ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge, Amour Hamad Amour akizungumza katika kiwanda lake Cement mara baada ya mwenge wa Uhuru kupita katika kiwanda hicho.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashimu Mgandilwa akizungumza katika Kiwanda cha Lake Cement wakati Mwenge wa Uhuru ulipopita katika kiwanda hicho .

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 36, MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO MAY 29, 2017

$
0
0
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Mhe. Job Ndugai akiingia Bungeni kwa ajili ya kuongoza kikao cha 36 cha Mkutano wa Saba Bunge la 11 Mei 29, 2017.
  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha 36 cha Mkutano wa Saba Bunge la 11 Mei 29, 2017. 
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe akijibu maswali mbalimbali kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria katika kikao cha 36 cha Mkutano wa Saba Bunge la 11 Mei 29, 2017. 
 Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Ritha Kabati akiuliza swali katika kikao cha 36 cha Mkutano wa Saba Bunge la 11 Mei 29, 2017.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt Agustine Maige pamoja na Naibu wake Mhe. Susan Kolimba wakijiandaa kuwasilisha Bajeti ya Wizara yao kwa mwaka wa fedha 2017/2018 katika kikao cha 36 cha Mkutano wa Saba Bunge la 11 Mei 29, 2017.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

“MRADI WA BOMBA LA MAFUTA KUTOKA HOIMA NCHINI UGANDA HADI BANDARI YA TANGA WAIVA”

$
0
0
MRADI wa Bomba la Mafuta Mkoani Tanga umefikia kwenye hatua ya wataalamu kukagua njia itakayopitisha miundombinu ya bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Hatua hiyo imekuja baada ya serikali ya Tanzania na Uganda kutiliana saini ya mkataba baina ya nchi na nchi (Iga) kukamilika.

Hayo yalisemwa leo na Mwanasheria Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini Tanzania (TPDC), Kelvin Gadi wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda lao ambalo lipo eneo la mwahako jijini Tanga kunakofanyika maonyesho ya tano ya biashara kimataifa.

Alisema tayari wameshafanya maamuzi yameshakamilika wataalamu wanafanya tathimi ya udongo katika njia ambayo bomba hilo litapita kwa taarifa ya awali njia iliyopatikana upana mita 200 na baadae watalaamu wataipunguza mpaka 100.

Awali akizungumza kuhusiana na mradi huo, Afisa Uhusiano wa Shirika hilo, Augustino Kasale alisema mradi huo utapita katika mikoa nane ya Tanzania na kuzalisha ajira 10000 za kudumu na muda mfupi.

Alizitaja fursa ambazo zitakuwa moja kwa moja ni hutoaji huduma wakati wa ujenzi, ajira za muda mfupi na moja kwa moja, fursa za usafirishaji ikiwemo kuufungua mkoa wa Tanga kiuchumi.

“Hivyo hivi sasa wananchi wa mkoa wa Tanga wanapaswa kujiandaa na ujio wa Bomba la Mafura ghafi kutoka hoima nchini Uganda hadi Mkoani Tanga “Alisema.

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.


 Afisa Uhusiano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Augustino Kasale kulia akimueleza jambo  Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage kushoto wakati alipofungua maonyesho ya tano ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga.
 Mwanasheria Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini Tanzania (TPDC), Kelvin Gadi wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda lao ambalo lipo eneo la mwahako jijini Tanga kunakofanyika maonyesho ya tano ya biashara kimataifa.
 Afisa Uhusiano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Augustino Kasale akizungumza na waandishi wa habari leo

JAFO APONGEZA USHIRIKIANO ULIOPO KISARAWE KATIKA UJENZI WA ZAHANATI

$
0
0


Naibu Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo amewapongeza viongozi wote pamoja na wananchi wa wilaya ya kisarawe katika ujenzi wa zahanati Mpya 11 pamoja na wodi 2 za wazazi.

Jafo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisarawe alitoa pongezi hizo alipokuwa akifanya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni Kisarawe.

Ujenzi huo unafanyika kupitia fedha za mfuko wa jimbo ambazo zimetumika kununua saruji na mabati na pia  fedha kutoka Halmashauri ya wilaya ya kisarawe na michango ya wananchi.

Akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa zahanati ya visiga, Jafo alipongeza wananchi wa visiga kwa kuunga mkono juhudi ya serikali ya awamu ya tano katika kujileta maendeleo.Aliwaomba viongozi wote waendelee na moyo huo huo wa mshikamano ili kufanikisha utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2015.

Katika hatua nyingine, Wananchi wa Tarafa ya Chole wilayani Kisarawe wameishukuru serikali ya awamu ya tano baada ya Mbunge wa jimbo la Kisarawe na Naibu Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais Tamisemi kukabidhi gari la wagonjwa aina ya Toyota Landcruiser kwa Kituo cha Afya chole.
FO1
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Chole katika kituo cha Afya Chole. 
FO2
Gari la wagonjwa lilokabidhiwa katika Kituo cha Afya cha Chole
FO3
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Kituo cha Afya Chole pamoja na viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe mara baada ya Kukabidhi gari la wagonjwa.
FO4
Jengo la Zahanati ya Visiga.

FEMINA HIP YAJA NAKAMPENI MPYA YA NGUVU YA BINTI

$
0
0
Na  Ashraf Said, Globu ya jamii.

Tasisi ya Femina Hip imeanzisha kampeni yake mpya inayokwenda kwa jina la Nguvu ya Binti ili kumsaidia msichana anapokuwa katika siku zake .

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo, Lydia Charles amesema kuwa Femina Hip imezindua kampeni ya Nguvu ya Binti ambayo itawakilishwa na wasichana wenye historia,Tabia, na uzoefu tofauti .


“ timu mpya ya nguvu ya binti itakuwa na sauti ya wasichana wote nchini Tanzania , wakichimbua , Kujadili na kujaribu kutatua changamoto na vikwazo mbalimbali kwa pamoja” amesema.


Amesema kuwa wasichana hao watakuwa mawakili kwa mambo ya kijamii, Kiuchumi na kisiasa.


Ameliza kwa kusema kuwa Femina Hip pamoja na wasichana wa kundi hilo wanamini kwamba ni lazima kufanya kazi pamoja , kufunguka na kuzungumza kuhusiana na hedhi ,maumivu wakati wa hedhi , Usafi wa miiko inayousishwa na hedhi kwa kushirikisha walimu , wazazi, walezi na Wanaume pia .
 Mratibuwa programu ya Nguvu ya Binti , Lydia Charles akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya mpango wao wa kuwawezesha wanawake wanapokuwa katika siku zao leo katika ofisi zao  katika eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi wa Kays Hygien, Sauda Simba akizungumzia kuhusu kampuni  ya Femina  iliyodhamini programu hiyo
Sehemu ya Waandishi wa wakufuatilia mkutano 

BULEMBO AUNGURUMA TABORA MJINI LEO, AZITAKA HALMASHAURI KUPELEKA FEDHA ZA MIKOPO KWA VIJANA NA KINAMAMA

$
0
0


Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Alhaj Abdalla Bulembo akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wa Wilaya za Uyui na Tabora mjini, Viongozi wa CCM na watendaji wa Serikali, katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, akiwa katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Tabora, leo.

 Pamoja na kuzungumzia taratibu za uchaguzi ndani ya unaoendelea katika ngazi za mashina, Bulembo amewataka wana CCM, kutambua kuwa sare za CCM zina thamani kubwa kwa kuwa ni za Chama tawala hivyo wazivae hata wanapokuwa wanakwenda kutafuta huduma katika maeneo muhimu, Amewataka pia madiwani kuhakikisha Halmashauri za wilaya zao zinatoa mgawo wa asilimia kumi fedha kutoka mapato yao, kwa ajili ya kuwapatika vijana na kina mama kwa ajili ya mikopo kwa kuwa utaratibu huo upo kisheria.
" Ndugu Bulembo Kazi hii ya Ukuu wa mkoa naipenda sana, hasa kwa sababu nasimamia ilani ya Chama changu, kwa niaba ya Wananchi wa mkoa huu, mpelekee Salaam, Mwenyetiki wetu, Rais Dk Magufuli, kwamba Tabora tunampongeza kwa kazi nzuri anazofanya, mwambie tuna imani naye na tutazidi kumuunga mkono", akisema, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggry Mwanri alipotambulishwa kwenye kikao hicho
Wajumbe wakionyesha bashasha na furaha kwenye kikao hicho
Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggry Mwanri akimtambulisha Mkuu wa Wilaya ya Tabora mjini, Mwalimu Queen Mwanshinga Mlozi, wakati wa mkutano huo.

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 29.05.2017

USIKOSE OFA KABAMBE KUTEMBELEA MBUGA ZA WANYAMA BURE WIKIENDI HII!!


MAGAZETI YA LEO JUMANNE MAY 30,2017

AFRICA REGIONAL MEETING OF LABOUR STATISTICIANS IN PREPARATION FOR THE 20TH ICLS OPENS IN DAR ES SALAAM

$
0
0
BY K-VIS BLOG/KHALFAN SAID.

REPRESENTATIVES from more than 35 African Countries converge in Tanzanian commercial capital Dar es Salaam in capacity-building workshop on labour statistics and Africa Regional meeting of labour statisticians in preparation for the 20th ICLS, to be held in Geneva, Switzerland in October, 2018.The regional workshop started Monday May 29, 2017 at Ramada Hotel in Dar es Salaam.
ILO’s Assistant Director General and Regional Director for Africa, Mr. Aeneas Chuma, makes his welcoming remarks. With him is Madam Mary Kawar, Director, ILO Country Office for Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda and Burundi.
Speaking on behalf of the ILO, The ILO’s Assistant Director General and Regional Director for Africa, Mr. Aeneas Chuma, (above), said, quality statistics are increasingly needed as the basis for sound policy advice and support to countries at a time when the economy are changing fast.

“This regional meeting consists of two activities of capacity-bilding workshop on labour statistics highlighting the 19th ICLS resolution on work statistics and regional consultation of labour statistics in preparation for the 20th ICLS.” He explained.Mr.Chuma also said, The 19th ICLS resolution, which was the latest labour statistics standard adopted in October 2013, is a core subject of the first activity.

“I would like to recall that, ILO, we follow a learning approach which is a participatory and hands-on methodology emphasizing knowledge, experience and good practice sharing. I understand such will be the approach to be used in this meeting.” He insisted.
Mr.Anthony Mavunde, (pictured above), is Tanzanian Deputy Minister of State in The Prime Minister’s Office (Labour,Youth, Employment and Persons with Disability), who was the Chief guest at the opening session.

In his remarks, the Deputy Minister said, “We all understand that labour statistics play an essential role in the efforts of our countries to achieve decent work for all and for the ILO’s support to these efforts.” Said Deputy Minister. 

“These statistics are needed for development and evaluation of policies towards this goal and assessing progress towards decent work. They are also an important tool for information and analysis, helping to increase understanding of common problems, explains actions and mobilizes interest.” He said.

Mr. Mavunde further said, improving the collection and availability of labour statistics is an important factor in not only promoting employment creation and improved livelihoods but also in achieving the 17 SDGs, especially Goal 8. “Promoting sustained, inclusive and sustainable economic growth, full and productive employment and decent work for all.” He stated.

The deputy minister also said, at the national level, labour market information is particularly important to the governments and all stakeholders, for policy formulation, planning and for monitoring and evaluation, increasingly , government requires labour market information to monitor the implementation of programmes and legislation and to monitor and evaluate economic and labor market performance.
Some of the participants attend the workshop.

WAZIRI MKUU KASIM MAJALIWA AMETIZA AHADI YAKE KWA WANANCHI WA MADABA KWA KUWALETEA GARI LA WAGONJWA

$
0
0
Hatimaye waziri mkuu KASIMU MAJALIWA ametimiza ahadi yake aliyotoa januari 5 mwaka huu, kwa wakazi wa halimashauri ya wilaya ya madaba mkoani ruvuma ya kuwaletea gari la wagonjwa ili iweze kusaidia katika EO matatizo.HABARI KAMILI HII HAPA

RC GAMBO AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUACHA DHANA YA KUOGOPA KUSTAAFU

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa arusha Mrisho Gambo amewataka Watumishi katika sekta za umma kuacha dhana ya kuogopa kustaafu kazi pindi wanapofikia muda wa kustaafu badala yake wanatakiwa kujipanga kabla muda haujafika.

Aidha watumishi wanaogopa kustaafu kwa kuwa wanaanza kujiandaa miaka miwili kabla hali ambayo inawapa uoga mkubwa wastaafu watarajiwa.

Mrisho Gambo ameyasema hayo jana wakati akifunga mkutano wa mfuko wa mafao ya kustaafu (GEPF) uliokuwa ukiendelea jijini Arusha.

Gambo alisema kuwa kwa sasa wastaafu wanapata magonjwa ya moyo kwa kuwa hawajajiandaa na kubuni miradi ambayo inaweza kuwaletea vipato kama mishahara yao ilivyokuwa.

Alisema maandalizi ni muimu sana kwa wafanyakazi hata kama bado hawajafikia muda wa kustaafu kwani kustaafu sio ajali bali ni kitu ambacho kipo na kimeshawekewa utaratibu na mifuko ya hifadhi jamii hapa nchini pamoja na Serikali.

"Wastaafu wengi wanakufa pindi wanapoacha kazi hiyo sio sawa ni lazima kila mtu ajiandae na abuni njia mojawapo ya kujiongezea kipato kwani hata kama ukijiajiri mwenyewe ni lazima utapata kipato kama kile ulicho kuwa unalipwa kama sehemu ya ujira wako "aliongeza Gambo.

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza katika mkutano wa nane wa wadau wa mfuko wa mafao ya kustaafu wa GEPF jijini Arusha juzi ,wakati akifunga mkutano huo ambapo aliwataka wastaafu watarajiwa kujiandaa kustaafu kwa kubuni miradi mbalimbali ya kuongeza kipato hali itakayosaidia wao kujiendeleza kimaisha(Habari Picha na Pamela Mollel Arusha)
Katibu Mkuu katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Eric Shitindi akizungumza katika mkutano huo ambapo alisema ni vyema watumishi wakajianda mapema wakiwemo wa umma na sekta binafsi .
Mkurugenzi wa mfuko wa GEPF Daudi Msangi alisema kuwa tayari kuna mikakati mbalimbali ambayo imeletwa kwenye mkutano huo na itaanza kufanyiwa kazi kwa malengo ya kuboresha maslai ya wanachama na nchi kwa ujumla.

Wadau wa mkutano wakiwa wamesimama kuashiria kumalizika kwa mkutano huo.


MATUKIO MBALIMBALI KWENYE MAONYESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA JIJINI TANGA

$
0
0

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akitoa elimu kuhusu umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko huo kwa wakazi wa Jiji la Tanga kwenye banda lao lililopo katika eneo la Mwahako Jijini Tanga kunakofanyika maonyesho ya tano ya biashara ya kimataifa
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akiptia kwenye banda la Hifadhi za Taifa Tanzania (Tanapa) wakati alipofungua maonyesho ya kimataifa ya  biashara ya tano yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akisalimiana na mmoja wa watumishi Tanapa wakati wakati alipotembelea banda lao kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akiendelea na shughuli ya kukagua mabanda ya Maonyesho.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

UNESCO KWA KUSHIRIKIANA NA GPF TANZANIA WAENDESHA SEMINA YA KUWAJENGEA UWEZO VIJANA ,CHUO KIKUU CHA MWALIMU NYERERE

$
0
0
Picha zote na Fredy Njeje

"Kiongozi bora ni pamoja na yule ambaye anahakikisha kuwa kuna amani katika eneo la kazi na watu anaowaongoza" hayo yalisemwa na bwana Nelson aliyekuwa mwakilishi wa Asasi ya Kiraia ya Global Peace Foundation(GPF) Nchini Tanzania wakati wa semina ya vijana katika kushiriki programu mbalimbali za Umoja wa Mataifa iliyoandaliwa na UNESCO kwa kushirikiana na Global Peace Foundation Tanzania. 

Alisema kuwa kiongozi makini ni yule anayehakikisha kuwa kuna amani katika eneo la kazi na kuwafanya wafanyakazi wake waishi kama familia moja ili kuondoa migogoro mbalimbali ambayo inaweza ikazuirika.

"Amani inatakiwa kudumishwa kuanzia ngazi ya familia, jamii na taifa kwa ujumla" alisema Nelson na kuongeza kukosekana kwa amani kunaweza kusababisha maafa kama vifo kwa sababu ya vita pia uchumi kuyumba kutokana na watu kuhofia kufanya shughuli za kimaendeleo kwa sababu ya machafuko.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UNESCO Youth Forum Bw. Frank Joash alisema vijana wengi hawana uwelewa wa program mbali mbali za umoja wa mataifa hivyo waliamua kuwakutanisha ili kuwapa uelewa ili wapate kujiunga.

Nae Bw. Jackson Oganga ambao walishawahi kusoma nje ya nchi kupitia ufadhili ‘Scholarship” walielezea kwa kina namna walivyo fika huko, changamoto na jinsi zinavyotokea na kuwasihi vijana hao kutokata tamaa na kuendelea kuomba nafasi hizo mpaka pale watakapo fanikiwa nao kutimiza ndoto zao za kwenda kusoma nje.
Muandaaji wa Semina hiyo iliyofanyika Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere na Mwenyekiti wa UNESCO Youth Forum Bw. Frank Joash akieleza namna ambavyo vijana wanaweza kujiunga katika programu mbalimbali za Umoja wa Mataifa.
Vijana kutoka Maeneo mbalimbali wakiwa wanasikiliza kwa makini mambo mbalimbali yaliyokuwa yanazungumziwa wakati wa semina hiyo iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere Kigamboni .
Mwakilishi wa Asasi ya Kiraia ya Global Peace Foundation(GPF) Bw. Nelson akieleza namna viongozi katika sekta mbalimbali wanavyoweza kusaidia kudumisha amani katika Jamii.
Mshauri wa mambo mbalimbali ya Kijamii na uchumi Bw. Anthony Luvanda akitoa masomo mbalimbali ya namna vijana wanavyoweza kujikwamua na kujitegemea kwa kufanya shughuli mbalimbali.

BALOZI SEIF ALL IDD AVUTIWA NA UTENDAJI KAZI WA TASAF

$
0
0

NA Estom Sanga- Zanzibar 

Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Balozi Seif Ali Iddi amesema mchango unaotolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika kuhamasisha wananchi kupambana na umasikini unapaswa kuungwa mkono kwani unakwenda sambamba na dhamira ya serikali zote mbili za kuwaondolea wananchi kero ya umasikini. 

Balozi Iddi ametoa kauli hiyo alipokutana na baadhi ya wadau wa Maendeleo na Maafisa wa TASAF ofisini kwake mjini Unguja baada ya viongozi na wadau hao wa maendeleo kuhitimisha ziara ya kuwatembelea Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya masikini kisiwani humo. 

Amesema mafanikio makubwa yanayojitokeza katika nyanja za elimu, afya na ongezeko la shughuli za kiuchumi miongoni mwa walengwa wa Mpango huo ni ushahidi tosha kuwa wananchi hususani wale ambao wamekuwa wakikabiliwa na umasikini , wanahitaji kwa kiwango kikubwa utekelezaji wa shughuli za Mpango huo ambao umekuja kwa wakati hasa kutokana na ukubwa wa tatizo la umasikini nchini. 

Balozi Iddi amesema kwa kutambua hilo serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuunga mkono utekelezaji wa shughuli za TASAF kisiwani humo na kuwataka wananchi hususani wale walioko kwenye Mpango wa kunusuru kaya masikini kutumia fursa hiyo vizuri ili hatimaye waweze kuboresha maisha yao. 

Picha ya juu na chini ,Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akizungumza na Wadau wa Maendeleo na viongozi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF ofisini kwake mjini Unguja.
Balozi Seif Ali Idd akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Ladislaus Mwamanga baada ya kupata maelezo ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko huo kisiwani Zanzibar,anayewaangalia ni Msimamizi wa shughuli za TASAF katika Benki ya Dunia ,Bwana Muderis Mohamed.
Mmoja wa wanafunzi wa shule ya Msingi Kizimbani,Unguja ambaye anatoka kwenye Kaya ya Mlengwa Wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini akikokotoa hesabu, anayemwangalia ni Msimamizi wa shughuli za TASAF katika Benki ya Dunia Bwana Muderis Mohamed.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bwana Ladislaus Mwamanga(aliyesimama)akizungumza na baadhi ya wananfunzi wanaotoka katika Kaya za Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika shule ya msingi Kizimbani kisiwani Zanzibar.


TAARIFA YA KIFO CHA MZEE FRANCIS MAIGE KANYASU

MSAMA ANG'AKA HABARI ZA KUCHAFULIWA YEYE NA FAMILIA YAKE

$
0
0




Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mtaa wa Mkwepu Posta jijini Dar es salaam wakati akielezea habari ya gazeti moja la wiki lililoandika habari za kwamba amefilisika na anatafutwa na mahakama,ikiwemo na kudaiwa kuwakimbia Wafanyakazi wake.

Akizugumza hayo jijini Dar Es Salaam,Alex Msana amesema yeye ana kampuni nyingi tu,ambazo zote ni zina Wakuregenzi wake na Mameneja wake,ambao wanakwenda kwenye shughuli zao za kiofisi kila siku, na Wafanyakazi wapo na wanaendelea na shughuli zao za kila siku .

"Sijaona mtu yeyote kutoka Mahakamani akileta ujumbe wa yeye kuitwa mahakamani, lakini pia hakuna hata taarifa ya yeye kuitwa polisi kwa tuhuma yoyote kama ilivyodaiwa kwenye hilo gazeti,hivyo habari hizo ni za uzushi na zinalenga kumpaka matope, lakini baya zaidi zinaihusisha familia yake" alisema Msama .

Msama amesema kuwa ni kweli amepungunza Wafanyakazi,hasa katika kitengo cha uchapishaji wa Magazeti,ili kukidhi hali halisi ya sasa,na kwamba kampuni yake si ya Kwanza kupunguza Wafanyakazi,anasema kufuatia hatua hiyo amekuwa akisikia maneno na mengine yakisambazwa kwenye mitandao ya kijamii yenye lengo la kumchafua yeye pamoja na familia yake.

Amesema kwa sasa ameamua kuchukua hatau,anajadiliana na wanasheria wake ili kuchukua hatua za kisheria kuwafikisha mahakamani wahusika, kwa sababu wamelenga kumvunjia heshima yeye, kampuni zake na familia yake mbele ya jamii ya Watanzania.

Amesema kuwa mara baada ya kuandaa utaratibu wa kisheria, watapeleka mashtaka mahakamani ili kudai haki yake ya msingi ya udhalilishaji uliofanywa na wahusika hao. 
Msama amewaasa Waandishi wa Habari kutumia kalamu zao vizuri sambamba na weredi wao katika majukumu makubwa ya kuielemisha jamii,katika masuala muhimu,ikiwemo na kujenga Nchi kwa kila nyanja husika,na si kukaa na kutunga ama kuzusha habari zisizokuwa na ukweli wowote.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari jana  kuhusiana na Madai yake kuchafuliwa yeye na Familia yake kupitia gazeti moja litakalo kwa wiki.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akionesha kukerwa na habari hizo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye moja ya ofisi zake jijini Dar es salaam jana 

Taarifa ya Waziri wa Afya kuhusu ugongwa wa ebola

Barclays Bank Tanzania hosted its customers for a live viewing FA cup

$
0
0
Barclays Bank Tanzania hosted its customers for a live match viewing of the FA Cup at the ‘Karambezi by Barclays’ restaurant. After the match, customers who were able to correctly predict the winner of the match received signed jerseys and footballs from Premier League. The match ended with Arsenal lifting the trophy for a record 13th time. Go Goooners! All Barclays Premier customers who pay their bill with a Barclays Visa card qualify to receive up to 20% off food and drinks. More details in pictures;
Barclays Bank Tanzania Retail and Business Banking Director, Kumaran Pather (left) posing for a memento photograph with some of banks valued customers. 
Barclays Bank Tanzania Retail and Business Banking Director, Kumaran Pather (left) and banks Marketing Manager, Joe Bendera (second left), with some premier customers; Africa Practice Country Manager, Charles Washoma (right) and ENGEN Petroleum Tanzania Managing Director, Paul Muhato.
Barclays Bank Tanzania Premier Centre Manager, Sophia Mang’enya (left) and BBT Retail and Business Banking Director, Kumaran Pather (second left) greets customers.  
Barclays Bank Tanzania Retail and Business Banking Director, Kumaran Pather (centre), handing over a ball to a customer who correctly predicted the winning team. Left is BBT Marketing Manager, Joe Bendera. 

KIFAA CHA DIJITALI KUWAWEZESHA WAKULIMA WADOGO TANZANIA KUPATA FEDHA, PEMBEJEO NA MAFUNZO

$
0
0
 Wakulima wadogo nchini Tanzania hivi karibuni wataweza kupata taarifa mbalimbali za kijiditali kuhusu masuala ya pembejeo, ukiwemo ushauri utakaosaidia kutatua matatizo yanayowakabili kama vile upatikanaji wa fedha, pembejeo na mafunzo. 

Mradi huo umezinduliwa na taasisi tatu za Alliance for a Green Revolution in Africa (AGRA), Positive International Limited (PIL), na Grameen Foundation katika sherehe zilizohudhuriwa na maofisa wa serikali, wawakilishi wa vyama vya wakulima, taasisi za fedha, kampuni za mbegu, wafanyabiashara wa nyenzo za kilimo na wale wanaojishughulisha na biashara za mazao ya sekta ya kilimo. 

Kifaa hicho cha dijitali kitawawezesha wakulima kulipia mapema pembejeo wanazohitaji kupitia simu za mkononi kwa bei nafuu. Pia kifaa hicho kitawapa wakulima pembejeo kulingana na mazao na malengo yao ya uzalishaji na pia kupata taarifa za ushauri kuhusu matumizi bora ya pembejeo hizo. 

“Moja ya changamoto kubwa zinazowakabili wakulima ni kwamba hukosa fedha mwanzoni mwa msimu wa upandaji mazao, jambo ambalo huwalazimisha kutafuta fedha hizo kwa ajili ya ununuzi wa pembejeo na hivyo kuwaongezea mzigo,” alisema Hedwig Siewertsen, kiongozi anayeshughulikia masuala ya fedha wa shirika la Alliance for a Green Revolution in Africa (AGRA). 

“Kifaa hicho cha dijitali kwa ajili kusaidia upatikanaji pembejeo za kilimo ni ufumbuzi wa kipekee. Kitawaimarisha na kuwasaidia wakulima kutenga fedha kwenye akaunti zao za simu ili waweze kununua pembejeo bora kwa muda muafaka na kwa bei nafuu ya asilimia 30.” 

Wakulima wadogo nchini Tanzania huzalisha asimia 70 ya chakula ingawa karibu nusu yao hawazalishi chakula cha kutosha kwa ajili ya mauzo. Wanakabiliwa na ukosefu wa teknolojia ya kilimo cha kisasa, hawana uwezo wa kujipatia pembejeo bora na wanakosa huduma za kiufundi za ughani zinazoweza kuwasidia kukuza kilimo pamoja na ukosefu wa mafunzo. Mwakilishi wa AGRA nchini, Bw. Vianey Rweyendela akifafanua jambo wakati wa uzinduzi huo.

Badala yake wakulima hawa wanategemea zaidi kilimo cha mvua, zana duni za kilimo na mbegu hafifu ambazo ubora wake hupungua kila msimu wa kilimo. 

Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images