Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110109 articles
Browse latest View live

Mkazi Tabata aibuka na mkwanja wa Biko

$
0
0
DROO ya nane iliyochezeshwa leo jijini Dar es Salaam na waendeshaji wa Bahati Nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’ imefanyika huku mkazi wa Tabata, jijini Dar es Salaam, Daniel Dancan Mwakaboko akifanikiwa kuibuka na mkwanja wa Sh Milioni 10. 

Hiyo ni siku chache baada ya wakazi wa Ubungo, Sospeter Muchunguzi na Stanley Kapondo, mfanyakazi wa TANESCO nao kuibuka na mamilioni ya Biko kwa siku tofauti ndani ya wiki moja.

Akizungumza katika droo hiyo, Balozi wa Biko, Kajala Masanja alisema kwamba siri kubwa ya ushindi ni kucheza Biko mara nyingi zaidi, akiamini kuwa kila anayecheza ana nafasi kubwa ya kuibuka kidedea na ushindi huo.
Picha tofauti tofauti Balozi wa Biko Kajala Masanja akimkaribisha mgeni wake mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Chiku Salehe katika droo ya nane ya Sh Milioni inayoondeshwa na Biko Tanzania ambapo mkazi wa Tabata, jijini Dar es Salaam, Daniel Dancan Mwakaboko alifanikiwa kutangazwa mshindi katika droo iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Picha na Mpigapicha wetu. 
Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Chiku Salehe kushoto akiwa na Balozi wa Biko, Kajala Masanja wakati wanamtafuta mshindi wa droo ya nane wa Biko ambaye mkazi wa Tabata, Daniel Mwakaboko alitangazwa mshindi na kuzoa jumla ya Sh Milioni 10 atakazokabidhiwa jijini Dar es Salaam.

Alisema mchezo wa Biko ni mzuri na rahisi kucheza kwake, hivyo ni jukumu la kila Mtanzania kutumia nafasi yake vizuri kwa kucheza bahati nasibu hiyo iliyojizolea umaarufu katika kipindi kifupi baada ya kuanzishwa kwake.

“Hakuna njia ya mkato ya kuweza kushinda donge nono la Biko badala yake dawa ni kucheza kwa wingi kwa kufanya miamala kwenye simu za Tigo, Vodacom na Airtel kwa kuingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu ni 2456,” Alisema Kajala.

Naye Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, aliwataka Watanzania kuingia kwa wingi katika mchezo wa Biko hususan wakazi wa mikoa mbalimbali ya Tanzania nao wakiwa kwenye nafasi kubwa ya ushindi.

“Tumetoa zawadi kwa washindi zaidi ya 30,000 nchi nzima kwa zawadi kuanzia Sh 5000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja nchini kote, hivyo tunawaomba watu wa mikoani nao kuongeza mwendo kuwania mamilioni ya Biko yanatotoka kila siku, huku droo kubwa ya Sh Milioni 10 ikifanyika siku mbili kwa wiki, yani Jumatano na Jumapili,” Alisema Heaven. 

Naye Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Chiku Salehe, alisema anajisikia faraja kuwa mwangalizi katika droo iliyompa ushindi mkazi wa Tabata, Mwakaboko, akiamini kuwa kila Mtanzania anaweza kuzoa mamilioni ya Biko.

“Mchezo wa Biko ni rahisi kucheza, ni salama na tunaangalia kwa kina ili kila Mtanzania aweze kushinda kihalali na kuongeza kipato chake kama walivyokusudia, ukizingatia kuwa endapo mtu anaibuka na mamilioni ya Biko anaweza kufika mbali kiuchumi,” Alisema Chiku. 

Mshindi wa droo hiyo, Mwakaboko hakusita kuonyesha furaha yake kwa kutangazwa mshindi, huku akisema licha ya kuchelewa kushinda, lakini hakuvunjika moyo akiamini kuwa siku moja bahati inaweza kuwa yake.

“Nashukuru sana kwa kutangazwa mshindi wa Biko wa Sh Milioni 10, sasa nitaipata lini,” Alihoji Mwakaboko kwa kupitia simu wakati anahojiana na balozi wa Biko, Kajala.

Kwa ushindi huo, Mwakaboko anatarajiwa kukabidhiwa fedha zake mapema ili aweze kuziingiza katika matumizi yake ya kimaisha hususan ya kumkwamua kiuchumi kwa kupitia mchezo wa Biko uliojizolea umaarufu mkubwa ukitambulika kama nguvu ya Buku.

‘MABODI’ NI MAARUFUKU KUCHAGUA VIONGOZI WASALITI NDANI YA CCM

$
0
0


NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR. 

WAFUASI wa CCM wameshauriwa kutowachagua baadhi ya wanachama wenye kashfa na tabia za usaliti kuwa viongozi wa ngazi mbali mbali zinazowaniwa ndani ya chama na jumuiya zake hicho kupitia uchaguzi unaoendelea hivi sasa. 

Ushauri huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadala “ Mabodi” katika mwendelezo wa mafunzo elekezi ya kuwajengea uwezo watendaji na viongozi wa majimbo ya Mkoa wa Magharibi Unguja, ili waelewe kwa kina Mabadiliko ya Katiba ya CCM na kanuni mbali mbali yaliyofanyika hivi karibuni mjini Dodoma. 

Dkt. Mabodi alisema chama hicho ili kiendelee kuimarika ni lazima wanachama wake ambao ni waaminifu wafanye maamuzi magumu ya kuwaweka kando kwa njia ya Kidemokrasia baadhi ya wanachama wenye dalili na sifa za usaliti sambamba na kamati za maadili kuanzia ngazi za chini kuwafanyia vikao vya kikanuni kuwajadili na kuwapatia fursa za kujitetea endapo watakutwa na makosa wachukuliwe hatua kwa mujibu wa maelekezo ya Katiba na kanuzi za maadili. 

Pia Dkt. Mabodi alieleza kwamba lengo la kuchukua maamuzi hayo sio kuwaonea watu hao bali ni kukisafisha chama ili kibaki na wanachama waadilifu watakaokilinda na kukipigania katika mazingira yoyote hasa wakati wa chaguzi za chama na dola pamoja na vipindi mbali mbali vya misukosuko ya kisiasa nchini. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadala” Mabodi” akitoa ufafanuzi wa mabadiliko ya Katiba ya CCM yaliyofanyika mwaka 2017, kwa washiriki wa mafunzo elekezi ya kuwajengea uwezo ili waweze kuzikabili changamoto za uchaguzi wa chama na jumuiya zake. 
Mwasilishaji ambaye pia ni Afisa kutoka Makao Makuu ya CCM Dodoma, Nd.Alhaji Rajab Kundya akiwasilisha mada za Mabadiliko ya katiba ya CCM ya mwaka 2017, pamoja na maboresho ya kanuzi ya uchaguzi ya chama hicho. 
Ni baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa makini mada zinazowasilishwa wakiwemo makatibu, wenyeviti , wajumbe wa kamati za siasa za ngazi za matawi hadi majimbo kwa chama na jumuiya zake, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mkoa wa Mjini Amani Unguja.(PICHA NA AFISI KUU CCM ZANZIBAR). 

SPIKA MHE. JOB NDUGAI ATEMBELEA BUNGE LA KENYA

$
0
0
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job akipokea zawadi kutoka Spika wa Bunge la Kenya Mhe Justin Muturi.

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai  (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kuhusu Bunge la Kenya linavyofanya kazi kutoka kwa Spika wa Bunge hilo Mhe Justin Muturi.Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la Kenya ambapo amembatana na wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge, Mhe Mary Chatanda, Mhe Salim Turky na Mhe Mch.Peter Msigwa.

(Picha na Ofisi ya Bunge)

TUTAIFUNGIA MIGODI YOTE INAYOPATA AJALI ZA KIZEMBE: KAMISHNA WA MADINI

$
0
0
Na Veronica Simba.

Serikali imesema itaifungia migodi yote ya madini ambayo itapata ajali kutokana na uzembe na haitafunguliwa hadi hapo Mkaguzi Mkuu wa Migodi atakapojiridhisha kuwa hali ya usalama imeboreshwa na hatua stahiki za kisheria zimechukuliwa kwa Meneja wa Mgodi au Msimamizi aliyehusika na uzembe huo.



Hayo yalisemwa hivi karibuni na Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka wakati akifungua mafunzo maalum kwa wachimbaji wadogo wa madini nchini, kwa lengo la kuwakumbusha kuzingatia kanuni zote za usalama mahali pa kazi ili kuepusha ajali za mara kwa mara zinazotokea na kusababisha vifo.



Mafunzo hayo ambayo yameandaliwa na Wizara ya Nishati na Madini, kupitia Idara yake ya Madini, yalifunguliwa rasmi Mererani, wilayani Simanjiro, Mkoa wa Manyara, ambapo Kamishna Mchwampaka aliwaambia wachimbaji wadogo wa madini wa eneo hilo kuwa, kwa sasa uchimbaji mdogo wa madini nchini umegubikwa na ajali nyingi ambazo zinaweza kuepukika endapo tahadhari za kiusalama zitachukuliwa.



“Ajali zinazotokea katika Migodi mingi ya wachimbaji wadogo hapa nchini, zimesababisha vifo, vilema vya maisha na pia gharama kubwa wakati wa shughuli za uokoaji.”



Kamishna Mchwampaka alisema kuwa, Serikali imelazimika kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha kuwa uchimbaji madini nchini, unafanyika kwa mujibu wa Sheria ya Madini kwa kuzingatia usalama na pia utunzaji wa mazingira.
 Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (wa pili kutoka kulia), akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa wachimbaji wadogo wa madini wa eneo la Mererani, wakati wa mafunzo maalum kuhusu usalama migodini yaliyofanyika hivi karibuni. Wengine pichani (kutoka kulia) ni Mkaguzi Mkuu wa Migodi Tanzania, Mhandisi Ally Samaje, Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kaskazini, Adam Juma na Fundi Sanifu Migodi kutoka Ofisi ya Madini Dar es Salaam, Stanslaus Basheka.
 Mkaguzi Mkuu wa Migodi Tanzania, Mhandisi Ally Samaje, akiwasilisha mada kuhusu Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira katika Migodi ya Wachimbaji Wadogo wa Madini, wakati wa mafunzo maalum kwa wachimbaji wadogo wa eneo la Mererani yaliyozinduliwa rasmi hivi karibuni.
 Fundi Sanifu Migodi kutoka Ofisi ya Madini Dar es Salaam, Stanslaus Basheka, akiwasilisha mada kuhusu Matumizi salama na utunzaji wa baruti migodini, wakati wa mafunzo maalum kwa wachimbaji wadogo wa madini wa eneo la Mererani hivi karibuni.
 Ofisa wa Sheria kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Hadija Ramadhan, akiwasilisha mada kuhusu Ufafanuzi wa Sera ya Madini ya Mwaka 2009, Ufafanuzi wa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na Kanuni zake za Mwaka 2010, wakati wa mafunzo maalum kwa wachimbaji wadogo wa madini wa eneo la Mererani hivi karibuni.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

JARIDA LA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU - APRILI, 2017.

PROFESA MBARAWA AZINDUA BODI YA DMI

$
0
0
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa akiwasili chuo cha cha Bahari Dar es Salaam(DMI) kuzindua bodi ya Ushauri ya Chuo hicho kushoto ni Mkuu wa Chuo hicho Dk. Erick Massami na kulia ni Mwenyekiti wa wa Bodi hiyo Nahodha Ernest Mihayo Bupamba Uzinduzi huo ulifanyika jana Chuoni hapo Jijini Dar es Salaam 
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa akizungumza wakati akizindua bodi ya Ushauri ya Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kushoto Mwenyekiti wa wa Bodi hiyo Nahodha Ernest Mihayo Bupamba na kulia ni Mkuu wa Chuo hicho Dk. Erick Massami.Uzinduzi huo ulifanyika jana Chuoni hapo Jijini Dar es Salaam.
Dk. Tumaini Gurumo, Naibu Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) Mipango, Fedha na Utawala akitoa ufafanuzi wa jambo kwa Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa (kushoto) jana wakati Waziri huyo akizindua bodi ya Ushauri ya Chuo hicho wa pili kushoto ni Mkuu wa Chuo hicho Dk. Erick Massami na wa tatu kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma,Utafiti na Ushauri.
Mhasibu Mkuu wa Chuo Cha Bahari Dar es Salaam(DMI) Haika Kessy akijitambulisha kwa Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa wakati Waziri huyo kuzindua bodi ya Ushauri ya Chuo hicho wengine pichani Maofisa wa Chuo hicho.

MRADI WA KUWA MFANO WAZINDULIWA JIJINI DAR, WANAFUNZI KUKUTANA KWA MIDAHALO

$
0
0
Baadhi ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari za Zanaki na Msimbazi, wakiwa katika picha ya pamoja na Wasimamizi wa Mdahalo uliozikutanisha shule hizo mbili pamoja na Walimu wao baada ya uzinduzi rasmi wa Mradi wa Kuwa Mfano, ulioratibiwa na Taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na Taasisi ya Friedrich Naumann, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Zanaki, Jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. Katika Mdahalo huo, Shule ya Sekondari ya Zanaki ndiyo iliibuka na ushindi. 
Afisa Mipango wa Taasisi ya Friedrich Naumann, Veni Swai akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Shule za Sekondari Zanaki na Msimbazi katika Mdahalo uliozikutanisha shule hizo mbili, ulioambatana na uzinduzi rasmi wa Mradi wa Kuwa Mfano, ulioratibiwa na Taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na Taasisi ya Friedrich Naumann, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Zanaki, Jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
Mmoja wa wasimamizi wa Mdahalo huo, Dorothy Kipeja akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Shule za Sekondari Zanaki na Msimbazi katika Mdahalo uliozikutanisha shule hizo mbili, ulioambatana na uzinduzi rasmi wa Mradi wa Kuwa Mfano, ulioratibiwa na Taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na Taasisi ya Friedrich Naumann, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Zanaki, Jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.   
Mkuu wa Kitengo cha Elimu wa Taasisi ya Doris Mollel, Erick Kajahurwa akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Shule za Sekondari Zanaki na Msimbazi katika Mdahalo uliozikutanisha shule hizo mbili, ulioambatana na uzinduzi rasmi wa Mradi wa Kuwa Mfano, ulioratibiwa na Taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na Taasisi ya Friedrich Naumann, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Zanaki, Jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
Afisa Mipango wa Taasisi ya Friedrich Naumann, Vena Swai akikabidhi zawadi ya mpira kwa Mwanafunzi Mwanahamisi Ally wa Shule ya Sekondari ya Zanaki, baada ya kuwa mmoja wa washindi katika Mdahalo uliozikutanisha shule mbili za Zanaki na Msimbazi, ulioambatana na uzinduzi rasmi wa Mradi wa Kuwa Mfano, ulioratibiwa na Taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na Taasisi ya Friedrich Naumann, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Zanaki, Jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.

MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 33, MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO MAY 24, 2017.

$
0
0
 Mwenyekiti   wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Azzan Zungu akiongoza kikao cha thelasini na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 24, 2017.
 Naibu Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha thelasini na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 24, 2017.
  Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama  akizungumza jambo  na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura  katika kikao cha thelasini na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 24, 2017.
 Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM) Mhe.Ally Keissy akiuliza swali katika  kikao cha thelasini na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 24, 2017.
 Mbunge wa Viti Maalum(CCM) Mhe.Kiteto Koshuma akiuliza swali katika  kikao cha thelasini na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 24, 2017.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Mchezo wa m-Bet wamwaga shilingi milioni 826

$
0
0
Ofisa wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, Kabora Mboya(kushoto) Msemaji wa M bet,Godluck Wambura wakimsikiliza kwa makini mshindi wa shilingi milioni 109/- Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa,Raymond Bintabara(26)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi mshindi huyo hundi yake aliyojishindia kupitia mchezo wa kubahatisha wa Supper 12 unaoendeshwa na M-bet.
Ofisa wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, Kabora Mboya(kushoto)akimkabidhi hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 109/- Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa,Raymond Bintabara,aliyejishindia kupitia mchezo wa kubahatisha wa Supper 12 unaoendeshwa na M-bet,hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es salaam,Wanaoshuhudia wapili kushoto ni Msemaji wa M bet,Godluck Wambura na Meneja wa huduma kwa wateja wa kampuni hiyo, Jaykishan Kaba.
Meneja huduma kwa wateja wa M bet, Jaykishan Kaba na Msemaji mkuu wa kampuni hiyo,Godluck Wambura wakimwelekeza mshindi wa shilingi milioni 109/- ambaye ni Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa,Raymond Bintabara jinsi ya kujaza fomu za kuwekewa fedha zake kwenye akaunti yake wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi mshindi huyo hundi yake aliyojishindia kupitia mchezo wa kubahatisha wa Supper 12 unaoendeshwa na M-bet.
Watanzania elfu 22 wamefanikiwa kujishindia jumla ya shingi milioni 826 kupitia mchezo wa kubashiri matokeo ya mechi za ligi za Ulaya m-Bet.

Akiongea na waandishi wa habari wakati wa kumkabidhi hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 109,388,350/- Mwanafunzi wa Chuo Kikuu Iringa  Raymond Bintabara (26) aliyeibuka mshindi wa kitita hicho, Msemaji wa M bet,Godluck Wambura  aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuwa, kampuni yake itaendeleo kutoa zawadi kwa washiriki wanaofanya vizuri katika utabiri wa motokeo ya mechi.

Mpaka kufikia leo hii tumeshatoa zaidi ya shilingi milioni 826 na tuataendelea kutoa zaidi. Tunawashauri Watanzania kuchangamkia fursa  kwa kubashiri zaidi,” alisema 

Raymond Bintabara (26)  aliibuka mshindi baada ya kufanikiwa kubashiri kwa usahihi matokeo ya mechi 12 kupitia perfect 12 ya m-Bet

Akiwa mwenye furaha, Bintabara alikabidhiwa kitita hicho cha fedha katika hafla fupi iyofanyika katika ofisi za m-Bet zilizopo jijini Dar es Salaam.

“Leo tunayofuraha kubwa kumkabidhi Bintabara kitita hiki cha Sh milioni 109,388,350/- kwa kuwa mshindi wetu wa m-Bet. Tunaamini fedha alizoshinda zitamsaidia katika elimu yake lakini pia kwenye mambo mengine kwa ajili ya maendeleo yake”,  alisema mkurugenzi wa m-Bet.

Wambura aliwataka Watanzania kuchangamkia fursa kwa kutumia mtandao wa intaneti kuonyesha ushabiki halisi wa soka akisema kuwa Perfect 12 ni mchezo wa ziada unaoruhusu kutabiri mechi 12 kwa Tsh 1,000 tu ambapo ukipatia zote  unaondoka na kitita chako mchana kweupe na ndicho Bintabara alichofanya.

Kwa upande wake msindi wa siku aliwashauri watanzania wote pamoja na wanafunzi wenye umri unaoruhusiwa kisheria kujitokeza kubashiri matokeo ya mechi mbalimbali kupitia Kampuni ya m-Bet ili kujishindia mamilioni.

"Nashukuru sana m-Bet, nitatumia fedha hizi kutimiza ndoto zangu za kielimu pamoja na za kimaisha kwa ujumla", alisema.

m-Bet, ni Kampuni iliyosajiliwa chini ya Sheria za Tanzania na kupewa leseni na Bodi ya Michezo ya kubahatisha tanzania kwa lengo la kufanya upatikanaji rahisi na mwingiliano wa huduma ya mchezo wa kubahatisha (Sim Betting) nchi nzima

“Kushiriki, ingia www.m-bet.co.tz, chagua kucheza kawaida au Perfect 12 ambapo kwa Shilingi 1000, unachagua matokeo 12. Ukipata yote sawa, unanyakua kikapu cha m-Bet,” alisema Kabba.

TIB YAANZA KAZI BANDARINI KWA MUDA WA SAA 24

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii

Katika kuendana na kasi ya Rais John Pombe Magufuli benki ya biashara ya TIB imeanzisha huduma za kibenki kwa masaa 24 katika tawi dogo la benki hiyo lililopo katika eneo la Bandari ya Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkurugenzi wa Benki ya Biashara ya TIB Frank Nyabundege amesema huduma hiyo inawawezesha wananchi wote kulipia kodi za aina mbali mbali pamoja na tozo zote za bandari.

Amesema hivi karibuni TIB benki na TRA ziliingia mkataba kwa kuunganisha mfumo wa malipo ya kodi ambapo mtu akilipa kodi kupitia mfumo huo katika tawi lolote la benki hiyo, taarifa zake zitaonekana moja kwa moja kwenye mtandao wa TRA.

Amesema kuwa, benki hiyo ya biashara (TIB), ndiyo benki pekee yenye dhamana ya kusimamia sehemu kubwa ya akaunti za TPA hivyo mwananchi atakapolipia tozo yoyote bandarini taarifa zake huonekana mara moja katika mtandao wake hivyo kurahisisha na kuwezesha kuendelea na taratibu zingine za utoaji mizigo kwa haraka zaidi.

“TIB bank inatoa huduma mbali mbali kutokana na mahitaji ya mteja, zikiwemo za akaunti za aina mbalimbali kwa makampuni na watu binafsi, mikopo ya muda mfupi na muda wa kati dhamana za kibenki uuzaji na ununuaji wa fedha za kigeni na shughuli zote za kibenki”, amesema Nyabundege.

Aidha amesema, benki hiyo ya kibiashara yenye matawi 6 nchini, Dar esSalaam matatu, Mwanza, Arusha na Mbeya inamilikiwa na serikali kwa asilimia 100 na pia inatoa huduma kwa watu binafsi taasisi binafsi na serikali.


Mkurugenzi wa Benki ya Biashara ya TIB Frank Nyabundege, akizungumza na Waandishi wa habari juu ya benki hiyo kufanya kazi saa 24 Bandari ya Dar es Salaam
Mkurugenzi mkuu wa Habari na Mawasiliano wa Benki ya Biashara ya TIB Frank Nyabundege , Theresia Soka akizungumzia ubora wa huduma hizo.
Watendaji wa Benki ya Biashara ya TIB
Sehemu ya Waandishi wa Habari walifika katika mkutano huo

HOTUBA YA RAIS DKT MAGUFULI BAADA YA KUPOKEA TAARIFA YA UCHUNGUZI WA MCHANGA WA DHAHABU

UBALOZI WA RWANDA NCHINI WAADHIMISHA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MAUAJI YA KIMBARI

$
0
0
Babalozi kutoka nchi mbali mbali wakiwasha mishumaa wakiongozwa na Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Mhe. Eugene Kayihura kwenye maaadhimisho ya Kumbukumbu ya Mauaji ya Kimbari dhidi ya Watusi iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Saalam.
 Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, Eugene Kayihura akiongozana na Waziri Mkuu mstaafu, Dkt. Salim Ahmed Salim wakati wakiwasili kwenye Ukumbi wa Mlimani city Jijini Dar es salaam, kulikofanyika Maadhimisho ya  Kumbukumbu ya Mauaji wa Kimbari dhidi ya Watusi yaliyotokea miaka 23 iliyopita huko nchini Rwanda.

Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania, Mhe Edzai Chimonyo akizungumza kwenye maadhimisho ya Mauaji ya Kimbari yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, Eugene Kayihura akizungumza kuhusu mauaji ya Kimbari yaliyotokea nchini Rwanda wakati wa maadhimisho ya miaka 23 yaliyofanyika leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu mstaafu, Dkt. Salim Ahmed Salim  akizungumza kwenye maadhimisho ya miaka 13 ya mauaji ya kimbari ya nchini Rwanda yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Nyimbo za mataifa mawili Tanzania na Rwanda zikiimbwa wakati wa maadhimisho ya miaka 23 ya Kimbali nchini Rwanda yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam
Sheikh Hamis Mtonga akiomba dua wakati wa kuanza maadhimisho ya miaka 23 ya Kimbari ya nchini Rwanda leo.

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo

MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SARPCCO WAFUNGULIWA JIJINI ARUSHA

$
0
0
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe. Hamad Masauni akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu wakati anawasili katika ukumbi wa mikutano wa AICC kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO). Kulia ni Mkuu wa INTERPOL kanda ya Kusini Mubita Nawa.
 Katibu Mtendaji wa SADC, Dk. Stegnomena Tax akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu kabla ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) unaofanyika mkoani Arusha. IGP Mangu ndiye Mwenyekiti wa shirikisho hilo kwa kipindi hiki.
 Baadhi ya Wakuu wa majeshi ya Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika SADC wakitoa heshima wakati wimbo wa taifa unapigwa wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) uliofanyika Mkoani Arusha. IGP wa Tanzania, Ernest Mangu ndiye Mwenyekiti wa shirikisho hilo kwa kipindi hiki. 
 Katibu Mtendaji wa SADC, Dk.Stegnomena Taxi, akitoa hotuba wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) Mkutano huo ulifunguliwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe.Hamad Masauni Mkoani Arusha. IGP wa Tanzania Mangu ndiye Mwenyekiti wa shirikisho hilo kwa kipindi hiki.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

SERIKALI YATOLEA UFAFANUZI UTARATIBU MPYA WA KUUZA HATI


MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI WATOA ELIMU KATIKA MIKOA YA DODOMA, MOROGORO, KILIMANJARO NA ARUSHA

$
0
0

Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), umeendesha semina ya siku moja kwa waajiri nchini katika mikoa minne, ili kutoa elimu juu ya shughuli za Mfuko na wajibu wa waajiri kwa wafanyakazi wao katika kujisajili na kuwalipa michango kwa niaba ya waajiriwa wao.

Akizungumza katika semina hiyo mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko Dkt. Francis Michael .



Amesema kuanzishwa kwa mfuko huo kumekuja wakati muafaka ambapo Tanzania inaelekea katika uchumi wa viwanda hivyo kupelekea ongezeko la wafanyakazi ambapo chombo hicho ndio mkombozi wa majanga yatokanayo na kazi.                


“Ni muda muafaka kwa waajiri kutambua wajibu wenu katika Mfuko huu na pia kutambua madhara ya kutotekeleza wajibu wenu” Alisema Dkt. Michael.


Katika hotuba yake, Dkt. Michael alieleza umuhimu wa waajiri kuwalipia michango wafanyakazi wake kama sheria inavyotaka, ili kuwawekea akiba pindi wapatapo na majanga wakiwa kazini.


Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi ni Taasisi ya Serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na umeundwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa wafanyakazi Sura ya 263 iliyorejewa Desemba, Mwaka 2015.


Dkt. Michael amesema, Mfuko umeamua kuandaa semina hiyo ili kutoa elimu zaidi kwa waajiri  kwa kutambua kuwa waajiri ndio wadau wakuu wa Mfuko huo na semina hiyo itawasaidia kujua kazi za Mfuko lakini pia wajibu wa waajiri kwa wafanyakazi katika kutoa michango ya kila mwezi.

 Mjumbe wa Bodi wa  Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. Francis Michael akifungua Semina ya uelimishaji kwa Waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Morogoro leo (jana), kulia ni Mwanasheria Mwandamizi Bi. Irine Mungu.
 Mwanasheria Mwandamizi Bi. Irine Mungu kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) akitoa mada kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Morogoro leo.
 Afisa Uhusuano Mwandamizi kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) akitoa mada katika semina ya uelimishaji kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi mkoani morogoro leo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MKURUGENZI MKUU TIC GEOFFREY MWAMBE AWATAHADHARISHA WAWEKEZAJI WENYE NIA MBAYA

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC) Geoffrey Idelphonce Mwambe ametoa tahadhari kwa wawekezaji wote wa nje na ndani ambao hawana nia njema na maendeleo ya taifa kuwa hawana nafasi nchini na kwamba hawatapata fursa yoyote Tanzania.

Mwambe ametoa tahadhari hiyo jana jioni katika kikao kifupi kilichoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dokta Rehema Nchimbi kwa ajili ya kumuaga rasmi Mkurugenzi huyo mara baada ya uteuzi wake ambapo hapo awali alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Manyoni.

Amesema kituo cha uwekezaji kitashirikiana na wawekezaji wenye nia njema tu ila wale ambao wanataka kujinuafiasha wao na kuliacha taifa bila faida yoyote hawatapewa fursa yoyote ya kuwekeza nchini.

Mwambe ameongeza kuwa atahakikisha kuwa wawekezaji wenye ubora na ambao uwekezaji wao unamgusa mtanzania moja kwa moja wanapatikana hasa wale ambao watasaidia kutoa ajira kwa wananchi na kukuza uchumi.

“Nina imani na wawekezaji wadogo ambao nitajitahidi kuwaunganisha na wawekezaji wakubwa ili wakue na wajenge uchumi wa taifa itawasaidia pia hao wawekezaji wadogo watapata uzoefu na hivyo kuwa wawekezaji wakubwa”, amesema.
 Mkurugenzi wa TIC Geoffrey Mwambe (wa kwanza kushoto) akipokea zawadi ya saa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (wa kwanza Kulia) katika kikao cha kumuaga, Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo na Mkuu wa Wilaya Mkalama JacksoN Masaka.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Nchini Geoffrey Mwambe akiwashukuru viongozi wa Mkoa wa Singida kwa ushirikiano katika kikao kifupi cha kumuaga.
 Mkurugenzi wa TIC Geoffrey Mwambe (wa kwanza kushoto) akipokea zawadi ya saa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (wa kwanza Kulia) katika kikao cha kumuaga, Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo na Mkuu wa Wilaya Mkalama JacksoN Masaka.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

SERIKALI YATOA UTARATIBU MAALUM BAADA YA KUVUNJWA CDA DODOMA

Msajili Wa Vyama Vya Siasa Apongezwa Kwa Kusimamia Sheria Na Kanuni.

$
0
0
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imepongezwa kwa kusimamia vyema Sheria na Kanuni zinazoongoza vyama vya Siasa hapa nchini hali inayochochea kukua kwa demokrasia.

Akizungumza katika mkutano wa kawaida wa siku moja iliyoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa, Katibu Mkuu wa Chama cha UDP Dkt. Goodluck Ole Medeye amesema utaratibu wa kuvisimamia vyama na kuvikagua ili kuhakikisha kuwa vinazingatia Sheria na Kanuni ni mzuri na ni wa kupongezwa.

“Napongeza kwa kazi nzuri ya kukagua hesabu za vyama inayofanywa na mkaguzi na mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa vyama vinavyopata ruzuku na visivyopata ruzuku hali ambayo inachochea uwajibikaji katika vyama ” alisisitiza Ole Medeye.

Akifafanua Ole Medeye amesema kuwa Serikali kupitia Msajili wa vyama vya Siasa anafanya kazi nzuri ya kuhakikisha kuwa kila chama kinafuata taratibu na kuomba ofisi hiyo kuendeleza utaratibu wa kukutana na viongozi wa vyama na wale wanaosimamia rasilimali za vyama kwa lengola kuhakikisha kila kimoja kinatimiza na kufuata sheria na kanuni zilizowekwa.

Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi akizungumza na Viongozi wa Vyama vya Siasa na watendaji wao wakati wa mkutano wa siku moja uliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam kujadili na kuweka mikakati ya kuondoa mapungufu yanayojitokeza katika kutekeleza Sheria na Kanuni za usajili wa vyama vya Siasa hapa nchini. Kushoto ni Msajili Msaidizi Bw. Sisty Nyahoza na kulia ni Msajili Msaidizi Bi. Piencia Kiure.
Msajili wa vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi akisisitiza jambo kwa viongozi wa vyama vya Siasa (hawapo pichani),wakati wa mkutano wa siku moja na viongozi hao leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Msajili Msaidizi Bw. Sisty Nyahoza.

Msajili Msaidizi Bw. Sisty Nyahoza akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayovihusu vyama vya siasa ikiwemo utekelzaji wa Sheria namba 5 ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992.

Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Chama cha CCK Bw. Renatus Muhabi mara baada ya kumaliza mkutano wa siku moja uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam ikiwa ni utaratibu ulioanzishwa na Msajili wa vyama vya siasa kukutana na viongozi wa vyama hivyo na watendaji wao.

Katibu Mkuu wa Chama cha UDP Goodluck Ole Medeye akipongeza utaratibu wa Msajili wa Vyama vya Siasa kusimamia sheria na kanuni zinazosimamia vyama vya siasa ikiwemo kufanyika kwa ukaguzi wa mahesabu katika vyama vyao.(Picha na Frank Mvungi-Maelezo).


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MKUU WA WILAYA YA UBUNGO AAGIZA KUANZA UJENZI WA MADARASA MANNE NA VYOO VYA SHULE YA SEKONDARI MBURAHATI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori Leo Jumatano, Mei 24, 2017 ameiagiza Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo inayoongozwa na Ndg John Lipesi Kayombo kuanza mchakato wa ukamilisho wa ujenzi wa Madarasa manne katika shule ya Sekondari Mburahati iliyopo Katika Mtaa wa Barafu, Kata ya Mburahati Jijini Dar es salaam.

Sambamba na Agizo hilo pia ameagiza kujengwa vyoo vya wanafunzi kutokana na uchache wa vyoo vilivyopo ili kukabiliana na wingi wa wanafunzi.

Mkuu wa Wilaya ametoa agizo hilo wakati wa kikao Cha pamoja kilichofanyika Shuleni hapo kwa kuhudhuriwa na Uongozi wa Shule hiyo, Kamati ya Shule, Uongozi wa serikali ya Mtaa na Afisa Mtendaji wa Kata ya Mburahati.

Mhe Makori alisema kuwa kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaojiunga na kidato Cha kwanza Kila mwaka kumekuwa na upungufu mkubwa wa madawati Jambo ambalo linachangia wanafunzi shuleni hapo kuanza kusoma kwa kupokezana hivyo mpango mahususi kukabiliana na changamoto hiyo ni pamoja na kuanza kujenga miundombinu ya kutosha itakayowasaidia wanafunzi kupata elimu bora.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akizungumza wakati wa ziara yake ya kikazi katika shule ya Sekondari Mburahati iliyopo Katika Mtaa wa Barafu, Kata ya Mburahati Jijini Dar es salaam.Leo Jumatano, Mei 24, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akisikiliza maelezo kuhusu shule ya Sekondari Mburahati mara baada ya kuzuru shuleni hapo.Leo Jumatano, Mei 24, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori (Kulia) akimsikiliza Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mburahati Ndg Bagaya Kashato akitoa maelezo kuhusu  kukwama kwa ujenzi wa madara ya shule ya Sekondari Mburahati mara baada ya kuzuru shuleni hapo, Mwingine ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg James mkubo.Leo Jumatano, Mei 24, 2017.

Viewing all 110109 articles
Browse latest View live




Latest Images