Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110152 articles
Browse latest View live

Rais Mpya wa Ufaransa kuapishwa leo

$
0
0
Rais mteule wa Ufaransa, Emmanuel Macron anataraji kuapishwa leo Jumapili kuongoza nchi hiyo, akiwa ni rais wa kwanza mwenye umri mdogo kuwahi kuongoza taifa hilo.

Kuapishwa kwa Macron kunakuja huku akiwa anakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kufufua uchumi na kuleta pumzi mpya ya uhai ndani ya umoja wa Ulaya

Macron anaapishwa kuchukua nafasi ya rais anayemaliza muda wake, Fancois Hollande ambaye miaka yake mitano madarakani ilikumbwa na ukosefu mkubwa wa ajira na mashambulizi ya kigaidi.

Baada ya kupita katika zulia jekundu katika Ikulu ya Elyzee katikati mwa jiji la Paris, Macon na Hollande watakuwa na mazungumzo ya faragha katika ofisi ya rais ambako Macron atakabidhiwa namba za kufungua silaha za Nuclear za Ufaransa.

NEC yaanza maandalizi uboreshaji wa daftari la wapiga kura

$
0
0
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani (kulia) akifafanua jambo wakati akitoa elimu ya mpiga kura kwenye kituo cha redio Dodoma FM cha mjini Dodoma.Kulia kwake ni Afisa wa Tume Bw. Mawazo Bikenye na mbeye ni watangazaji .Picha na Hussein Makame, NEC-Dodoma.

Hussein Makame-NEC, Dodoma

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeanza maandalizi ya kufanya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 baada ya Serikali kutenga Shilingi Bilioni 10 kwa ajili ya kazi hiyo katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Tume hiyo Bw. Kailima Ramadhani kwa nyakati tofauti wakati akitoa elimu ya mpiga kura katika vituo vya redio vilivyoko mkoani Dodoma.

Alisema kuwa maandalizi ya uboreshaji huo ni pamoja na kutoa elimu ya mpiga kura kupitia vituo vya redio nchi nzima mpango ambao umeanza kutekelezwa kwa baadhi ya mikoa nchini.

“Tume imeanza maandalizi ya kufanya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, Serikali imeshatenga Shilingi Bilioni 10 kwa ajili ya kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura mwaka 2017/2018”alisema Bw. Kailima.

Aliongeza kuwa kwa kipindi hicho Tume itatoa kadi mpya ya mpiga kura kwa watakaoandikishwa upya, waliopoteza kadi na kadi zilizoharribika, kwa wanaohamisha taarifa zao ikiwemo waliohamia Dodoma, na kufuta wapiga kura waliopoteza sifa za kuwa wapiga kura.

Bw. Kailima aliwataka wananchi wafuatilie elimu ya mpiga kura inayotolewa kupitia redio ya mikoani kuelewa mambo mbalimbali yanayohusu mchakato wa uchaguzi ili fikapo mwaka 2020 kila mwananchi awe ameelimika na asiweze kupotoshwa.

Alisema kwamba kwa muda mrefu elimu ya mpiga kura imekuwa haitolewa kwa mujibu wa matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria ya Taifa ya Uchaguzi.

Alifafanua kuwa Ibara 74 (6) (e) ya Katiba inaitaka Tume kutekeleza majukumu kwa mujibu wa Sheria nyingine yiyite iliyotungwa na Bunge na Ibara ya 18 inampa kila mwananchi haki ya kupata taarifa muhimu zinazohusu nchi yake

KMTC YAJIPANGA KUJENGA JIKO LA KUYEYUSHIA CHUMA

$
0
0

Na. Benedict Liwenga-WHUSM, Moshi.

Kiwanda cha Utengenezaji Vipuri vya Mashine Kilimanjaro (KMTC) iko mbioni kujenga mtambo utakaotumika katika kuyeyusha chuma kwa ajili ya kuendeleza shughuli zake za utenegenezaji wa dhana mbalimbali za mashine ikiwemo kukarabati mifumo ya umeme ya kiwanda hicho ambaye ilikua haijatumika kwa muda mrefu,

Kauli hiyo imetolewa jana na Meneja Mkuu wa Kiwanda hicho, Mhandisi Adriano Nyaluke wakati alipokutanana Waandishi wa habari na kueleza mikakati ya kukiendeleza kiwanda hicho ikiwemo shughuli mbalimbali zinazofanyika kiwandani hapo ili baadaye kiweze kutoa ajira rasmi kwa Watanzania.

MhandIsi Nyaluke amesema kwamba, kwa sasa katika amamu ya kwanza wana mahitaji ambayo yanahitajika kukamilika ikiwemo mpango wa kutafuta fedha toka katika Mifuko ya Jamii ili kuweza kujenga mtambo huo pamoja na fedha za mtaji wa kutengeneza zana mbalimbali kiwandani hapo.

“Mpaka sasa tuna bajeti ya shilingi bilioni 1.6 na tuna mpango wa kuendelea kutafuta fedha zaidi toka katika Mifuko ya Kijamii na tunaamini fedha hizo tutazipata ili tuweze kuendelea na mpango wa kujenga mtambo huo pamoja na utengenezaji wa zana za kiwanda”, alisema Nyaluke. 
Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Uzalishaji Vipuri vya Mashine Kilimanjaro (KMTC), Mhandisi Adriano Nyaluke akiwaonyesha Waandishi wa habari (hawapo pichani) baadhi ya mitambo itumikayo kutengeneza vipuri mbalimbali vya mashine 13 Mei, 2017 Moshi, Kilimanjaro. 
Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Uzalishaji Vipuri vya Mashine Kilimanjaro (KMTC), Mhandisi Adriano Nyaluke (kushoto) akiwaonyesha Waandishi wa habari mashine ya kutengeneza randa zitumikazo katika kazi za useremala, 13 Mei, 2017 Moshi, Kilimanjaro. 
Wafanyakazi wa Kiwanda cha Uzalishaji Vipuri vya Mashine Kilimanjaro (KMTC), wakiwa kazini Moshi, Kilimanjaro 13 Mei, 2017. 
Afisa Mawasiliano wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Bw. Abel Ngapemba akiangalia moja ya mashine itumikayo kuchonga chuma wakati alipotembelea katika Kiwanda cha Uzalishaji Vipuri vya Mashine Kilimanjaro (KMTC), kilichopo Moshi, Kilimanjaro 13 Mei, 2017. 

WAZAZI WATAKIWA KUWAEPUSHA WATOTO NA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI.

$
0
0
Na Hassan Silayo-MAELEZO 

Wazazi nchini wametakiwa kutekeleza wajibu wao kwa watoto kwa kuhakikisha wanawaendeleza na kuwawezesha wafanikishe ndoto zao kwa kuwaepusha na ndoa pamoja na mimba za utotoni. 

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi.Sihaba Nkinga katika Mahafali ya 5 ya kidato cha sita ya shule ya sekondari Mwendakulima iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama. 

Bi.Sihaba amesema kuwa wazazi wanajukumu la kuhakikisha wanawalea na kuwalinda kwani wazazi wanahaki ya kisheria ya kuwalinda watoto dhidi ya viashiria vyote vinavyoweza kuwaweka katika mazingira hatarishi. 

Bi.Sihaba aliongeza kuwa wazazi na walezi wana haja ya kushirkiana na serikali katika kuwalinda watoto wakike kwani watoto wa kike ni nyenzo muhimu hasa kwenye mpango wa serikali katika kuelekea uchumi wa kati kupitia viwanda. 

Aidha,Bi.Sihaba kuwa Serikali imefanya marekebisho ya Sheria ya Elimu sura namba 33 inayotoa katazo kumpa ujauzito motto wa shule chini ya miaka 18 hivyo wazazi wahakikishe wanalisimamia kwa pamoja ili kuweza kufanikisha sheria. 
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi.Sihaba Nkinga akikata utepe kuashiria kuanza kwa mahafali ya 5 ya kidato cha sita katika shule ya Sekondari Mwendakulima iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama. 
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi.Deodatha Makani akiongea jambo na Mkurugenzi wa Ubora na Maendeleo wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Save the Children Amy Schmiot mahafali ya 5 ya kidato cha sita katika shule ya Sekondari Mwendakulima iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama. 
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi.Sihaba Nkinga akitoa vyeti pamoja na zawadi kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Mwendakulima iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama alipohudhuria mahafali ya 5 ya kidato cha sita ya shule hiyo. 

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MAY 14,2017

RAIS DKT MAGUFULI AKIZUNGUMZA NA JUMUIA YA WAFANYABIASHARA WA TANZANIA NA AFRIKA KUSINI MEI 11,2017

Dua Maalum ya kuliombea Taifa Amani na Utulivu pamoja na kujiandaa kuukaribishwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

$
0
0
Na Othman Khamks Ame, OMPR
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Mkusanyiko wa Waumini wa Dini ya Kiislamu katika mfumo wa kushikamana bila ya kufarakana daima huzaa baraka zinazootesha neema na kheir miongoni mwa Umma huo mtukufu mbele ya Muumba wao Mwenyezi Mungu.
Alisema Vitabu vya Dini na  Miongozo yote iliyotolewa katika Vitabu hivyo imekuwa ikielekeza na kusisitiza umuhimu wa Binaadamu hasa Wale walioamini Vitabu hivyo kushikamana pamoja ili lile lengo lao la kumuabudu Mwenyezi Muungu likamilike bila ya kutetereka kwa kitu chochote kile.
Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati wa Dua Maalum ya kuliombea Taifa Amani na Utulivu pamoja na kujiandaa kuukaribishwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaokaribia kuingia wiki chache zijazo dua iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Malindi Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na Mamia ya Waumini wa Dini ya Kiislamu, Wananchi pamoja na baadhi ya Viongozi wa Serikali na Kisiasa.
Alisema Waumini na Wananchi wote wanapaswa kuzingatia  umuhimu wa suala la Amani iliyopo Nchini kwani kwa kufanya hivyo kutatoa fursa kwa Waumini hao kutekeleza kwa utulivu Ibada zao sambamba na Wananchi kuendelea na harakati zao za Kimaisha za kila siku.
Akizungumzia ujio la Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuingia wiki chache zijazo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alitoa wito kwa Wafanyabiashara wote hapa Nchini kuacha tabia ya kupandisha bei za bidhaa muhimu zinazotumiwa kwa wingi na waumini wa Dini ya Kiislamu katika kipindi hicho cha saumu.
Alisema tabia hiyo mbaya ni dhambi kubwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haitakuwa na huruma katika kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wowote watakaopandisha bei bidhaa zao bila ya sababu za msingi zitakazokubalika.
Mapema Mufti Mkuu wa Tanzania  Bara Sheikh Abubakar  Zubeir Ali alisema Dua ni fursa kubwa inayompa fursa Mwanaadamu kumuomba Mungu amuelekeze katika njia ya Amani.
Sheikh Zubeir alisema Mwenyezi Muungu muda wote hutarajia kuombwa na waumini wake vyenginevyo anaondosha baraka zake na kutowajaalia kheir na hatma njema waombaji hao anayoisisitiza kila siku kufanywa  na waja wake.
Hata hivyo Mufti Mkuu huyo wa Tanzania alitahadharisha wazi kwamba zipo ishara zinazoanza  kujichomoza za mmong’onyoko wa Maadili unaotishia kutetereka kwa Amani jambo ambalo kila Muumini na Mwananchi anapaswa kuliondoa au kulikemea lisije kuleta athari hapo baadae.
 Waumini wa Dini ya Kiislamu wakisoma Dua maalum ya kuliombea Taifa Amani na Utulivu pamoja na kujiandaa kuukaribishwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani iliyofanyika katika Msiki wa Ijumaa Malindi Mjini Zanzibar.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akijumuika pamoja na Waumini mbali mbali wa dini ya Kiislamu Nchini katika Dua maalum ya kuliombea Taifa Amani na Utulivu pamoja na kujiandaa kuukaribishwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Kulia ya Balozi  Seif ni Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Ka’abi pamoja na Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam  Sheikha Alhad Mussa Salum.
 Mufti Mkuu wa Tanzania Bara Sheikh Abubakar Zubeir Ali  wa kwanza kutoka Kushoto,  Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji pamoja na Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Mh. Ayoub Mohamed Mahmoud walikuwa miongoni wa  Viongozi walioshiriki Dua hiyo.
 Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Madhehebu ya Shia Kutoka Nchni Iran waliojumuipa pamoja na Waumini wa Zanzibar katika Dua ya kuliombea Taifa  Aman.
 Maulamaa na wahadhiri kutoka Nchini Misri nao walikuwa miongoni mwa washiriki wa Dua hiyo iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Malindi.
 Baadhi ya Maimamu wa Misikiti mbali mbali ya Mkoa wa Mjini Magharibi wakisoma Dua hiyo maalum ya kuliombea Taifa Amani na Utulivu pamoja na kujiandaa kuukaribishwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitoa nasaha ya kuwataka waumini na Wananchi kuendelea kudumisha Amani kwenye Dua ya Kuliombea Taifa amani. Picha na – OMPR – ZNZ.

VIJANA WATAKIWA KUUFAHAMU UMUHIMU WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0
Mabalozi wa vijana wanaoiwakilisha Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Yohana Lambo Mayenga pamoja na Suzane William Mollel wamekutana na Wafunzi wa Chuo cha Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara, kwa lengo la kutoa mafunzo na kuwahamasisha Wanafunzi wa vyuo vikuu (Vijana) nchini kote, kuufahamu umuhimu wa Ushirikiano wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuuimarisha katika Mchakato wa Jumuiya hiyo Kikanda, katika Warsha ya siku moja iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo, Mei 12, 2017. Jumla ya Wanafunzi 230 walihudhulia Warsha hiyo.
Mabalozi wa vijana wanaoiwakilisha Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Yohana Lambo Mayenga pamoja na Suzane William Mollel (wa tatu na nne kushoto) wakiwa wameshika Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na baadhi ya Wafunzi wa Chuo cha Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara, wakati wa Warsha ya siku moja iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo, Mei 12, 2017.
Naibu Balozi wa vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Suzane William Mollel (aliyesimama) akiwasilisha mada katika Warsha ya siku moja kwa Wafunzi wa Chuo cha Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara, juu ya umuhimu wa Ushirikiano wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuuimarisha Mchakato wa Jumuiya hiyo Kikanda, iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo, Mei 12, 2017. 
 Wanafunzi wa Chuo cha Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara, wakimsikiliza kwa makini Balozi wa vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Yohana Lambo Mayenga.
Sehemu ya wanafunzi hao wakiwa kwenye Warsha hiyo.
Balozi wa vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Yohana Lambo Mayenga akikabidhi Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara akikabidhi Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mmoja wa Viongozi wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho.


BREAKING NYUZZZZ......: ZACHARIA HANS POPPE ABWAGA MANYANGA SIMBA

$
0
0
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Simba, Zacharia Hans Poppe ameachia ngazi.

Habari za uhakika zimeeleza kuwa Hans Poppe ameandika barua ya kuachia ngazi kwa madai kuwa anaona mambo yanaendeshwa ndivyo sivyo.

Chanzo chetu cha kuaminika kinaeleza kuwa "Hans Poppe ameachia ngazi kwa kuwa hakufurahishwa na mlolongo ulivyokuwa hadi Simba kuingia mkataba wa SportPesa,” kilieleza chanzo.

"Hans Poppe ameandika barua kujiuzulu kwenye kamati ya utendaji, maana yake anaondoka moja kwa moja katika nafasi ya mwenyekiti wa kamati ya usajili.

"Kilichomchukiza, anasema kuna kundi lililoongozwa na Rais Evans Aveva na makamu Geofrey Nyange Kaburu, lilifanya mambo kimya kimya na Hans Poppe amesema hata Mo Dewji aliyeisaidia Simba mishahara naye hakushirikishwa hata kiungwana tu, hivyo amepinga hilo."

SHINDANO LA MISS USTAWI KUFANYIKA MEI 19 UKUMBI WA KING SOLOMON JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
  Mashindano ya Miss Ustawi wa Jamii 2017 yanatarajia kufanyika siku ya ijumaa, Mei 19 katika Ukumbi wa King Solomon jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwalimu wa Warembo hao, Clara Nyaki amesema maandalizi yafanyika kwa ustadi kutokana jinsi walivyowachuja. Amesema kuwa mshindi atakayepatikana atakuwa ameonyesha uwezo wake binafsi ikilinganishwa wengine wataofuata.

Clara amesema siku hiyo itakuwa ya kipekee kutokana na maandalizi watapopata mshindi wa kuwakilisha warembo wenzake. Pia, Clara amewakaribisha Watanzania wote kwa ujumla kuja kushuduhia tukio hilo.
Kwa upande wao hao Walimbwende hao wamesema wamejinada kila mmoja kuondoka na ushindi kulingana na maandalizi waliyoyafanya katika kipindi chote walichokuwa na mwalimu wao. Warembo watakaojimwaga siku hiyo ni Ruth Deouratius ,Melody Thomas, Elizabeth Julius, Careen Kileo, Loyce Jeck ,Diana Wambura , Angela Milanzi pamoja na Elice Mwakajila .
 Warembo wakiwa katika picha ya pamoja kwa pozi mbalimbali watavyokwenda katika kinyanganyilo hicho kitachofanyika Mei 19 katika ukumbi wa King Solomon jijini Dar es Salaam. 

MBUNGE WA LUSHOTO ATEMBELEA BARABARA YA MOMBO-SONI KUJIONEA ATHARI ZA BARABARA

$
0
0


Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia akikagua athari za mafuriko kwenye barabara ya Soni hadi Mombo ambapo imefungwa kutokana na vifusi,mawe kudondoka barabarani na hivyo kusababisha adha hiyo
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia kulia akisalimiana na wananchi
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia kulia akiteta jambo na wataalamu wanaosimamia zoezi la kuondosha kifusi na mawe

Creda likiendelea na kazi yake kama kawaida .

Naibu Meya Ilala Awaomba Vijana Temeke kuchangamkia fursa ya mikopo inayotelewa

$
0
0

Na Humphrey Shao ,Globu ya Jamii

Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto amewaomba Vijana wa Temeke kuchangamkia fursa ya Mikopo ya Vijana inayotolewa na Halmashauri hiyo.

Kumbilamoto ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaama alipokuwa akizindua Tamasha la Miaka tisa ya mbio za pole (Jogging) kwa vijana wa Dovya.

"Nawashukuru sana vijana wa Dovya Jogging ya Temeke leo kwa kunialika katika tamasha hili kubwa la kutimiza miaka 9 ya jogging yenu pia kwa upekee nimshukuru Mbunge wa Temeke mh Mtolea kwa kunikaribisha katika jimbo lake nishiriki michezo kwani Muchezo ni ajira hivyo nawaomba mtumie fursa hii kuwaambia mchangamkie fursa za mikopo ya halmashauri ya Temeke inayotolewa kwa Vijana"amesema Kumbilamoto.

Amesema kuwa mikopo hiyo ambayo inatokana na 10% ya mapato ya Halmashauri itawasaidia kujikwamua kiuchumi kama watabuni miradi na kujikusanya katika vikundi .

Amesisitiza hakuna mtu wakuwafata vijana na kuwajaza mapesa mfukoni bila ya wao kujishughulisha katika ujasiliamali na kujiajiri kupitia fursa zinazo patikana .
 Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala ,Omary Kumbilamoto akiongoza Mazoezi ya pamoja katika Tamasha la Michezo la Dovya Joging Wilayani Temeke
 Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto  akizungumza na Vijana Yombo Dovya wakati wa Tamasha la Michezo la Jonging ya Dovya

Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akiwa na Mbunge wa Temeke Abdalah Mtolea wakati wa sherehe za klabu ya Mbio za pole ya Dovya Jogging 

Mkazi wa Bunju James Peter azoa milioni za Biko

$
0
0
MKAZI wa Bunju jijini Dar es Salaam, James Peter amefanikiwa kuibuka kidedea katika droo ya tano ya wiki ya kuwania Sh Milioni 10 baada ya kutangazwa mshindi kwenye kinyang’anyiro hicho.

Droo hiyo ya tano ya wiki imechezeshwa leo jijini Dar es Salaam na Balozi wa Biko, Kajala Masanja kwa kushirikiana na Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Emmanuel Ndaki.

Akizungumza katika droo hiyo ya tano, Kajala Masanja alisema mshindi wa Milioni 10 wa wiki hii alibahatika kutangazwa mshindi baada ya kupigiwa simu mara tatu, huku mara mbili akishindwa kupokea simu kwa haraka.

Alisema hata hivyo baadaye alipokea simu hali inayoonyesha kwamba alikuwa na bahati kubwa kwa kunyakua fedha hizo zinazotolewa kwa mshindi mmoja kila mwisho wa wiki, huku washindi wengine zaidi ya 20,000 wa zawadi za papo kwa hapo wakijishindia zawadi kem kem.

“Tumefanikiwa kumpata mshindi wa Sh Milioni 10 ambaye anatokea jijini Dar es Salaam, akiongeza idadi ya washindi wanne kutokea jijini hapa, huku mmoja pekee akitokea jijini Mwanza,” alisema Kajala.

Naye Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven aliwataka Watanzania hususan wakazi na wananchi wa mikoa mbalimbali ya Tanzania kujitokeza kwa wingi kucheza biko ili waibuke washindi kwa kufanya miamala kwenye simu zao za Tigo, Vodacom na Airtel ambapo katika kipengele cha lipa bili wataingiza namba ya kampuni ambayo ni 505050 na namba ya kumbukumbu 2456.

“Kucheza biko ni rahisi kwa saabubu baada ya kuweka kiasi kuanzia Sh 1000 ambayo inatoa ushindi wa papo kwa hapo pia humpa fursa mtu kuingia kwenye droo kubwa ya wiki ya kuwania Sh Milioni 10, huku zawadi za papo kwa hapo zinatolewa na Biko ikianzia sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja, huku hadi sasa washindi zaidi ya 20,000 wakiwa wamenyakua zawadi mbalimbali za fedha kutoka kwetu Biko,” Alisema.

Balozi wa Biko Kajala Masanja kulia akiagana na Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Emmanuel Ndaki baada ya kumaliza kuchezesha droo ya tano ya Sh Milioni 10 ambapo mkazi wa Bunju, jijini Dar es Salaam, James Peter kutangazwa mshindi wa droo hiyo ambapo amejishindia jumla ya Sh Milioni 10.
Balozi wa Biko Tanzania Kajala Masanja akifurahia namba ya ushindi ambapo mkazi wa Bunju, jijini Dar es Salaam, James Peter amejinyakulia jumla ya Sh Milioni 10 katika droo iliyochezeshwa jana jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Emmanuel Ndaki. 


TFDA: DAWA ZILIZOPO SOKO ZINA UBORA WA ASILIMIA 98

$
0
0
Frank Mvungi-Maelezo

Serikali imewahakikishia wananchi kuwa dawa zilizopo katika soko zina ubora kwa asilimia 98 na itahakiksha zinaendelea kukidhi vigezo vya ubora kama zilivyokuwa wakati zinasajiliwa kwa mujibu wa sheria, kanuni,miongozo na taratibu za udhibiti.

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya chakula na Dawa (TFDA) Bw. Hiiti Sillo wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliolenga kueleza mikakati ya Mamlaka hiyo katika kudhibiti ubora na usalama wa chakula,dawa,vipodozi na vifaa tiba ili kulinda afya za wananchi.

“Katika maabara ya TFDA inayokidhi ithibati ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kati ya sampuli za dawa 199 za Binadamu zilizochunguzwa,sampuli 184 sawa na asilimia 92.5 zilikidhi vigezo vya ubora na sampuli za dawa 10 aina ya Ergometrine ya sindano ambayo ni sampuli 5 sawa na asilimia 2.5 hazikufikia ubora kwa kuwa na kiasi cha kiambata hai chini ya kiwango kinachokubalika.”Alisisitiza Sillo

Akifafanua Sillo amesema kabla ya dawa kusajiliwa na TFDA na hatimaye kuruhusiwa kuingia katika Soko,zinafanyiwa tathmini ya Ubora,Usalama na ufanisi sanjari na ukaguzi wa mifumo ya utengenezaji bora Kiwandani na hizo ni hatua za awali za mifumo ya udhibiti wa dawa duniani.

Pia Sillo aliongeza kuwa dawa zinapokuwa katika soko zinafuatiliwa na TFDA kuona kama zinaendelea kukidhi vigezo vya ubora hadi tarehe ya mwisho ya matumizi (expiry date) ambapo utaratibu huu hujulikana kama Post- Marketing Surveillance au Market Control kwa mujibu wa mwongozo wa shirika la Afya Duniani (WHO) na ulianza kuwekwa na TFDA tangu mwaka 2007.

Katika utaratibu huo kila mwaka sampuli za dawa za aina tofauti zinachukuliwa na wakaguzi kutoka katika soko Zahanati,Vituo vya Afya, Hospitali,maduka ya dawa na maghala ya kuhifadhia dawa ya umma na binafsi na kufanyiwa uchunguzi wa kimaabara.

Vigezo vinavyotumika kuchagua dawa zinazofanyiwa ufuatiliaji ni pamoja na dawa zenye matumizi makubwa,dawa za kutibu magonjwa ya makundi maalum kama watoto na akina mama wajawazito,dawa zenye historia ya kushindwa kustahili mazingira mbalimbali ya usafirishaji na utunzaji (unstable products)

Kwa kipindi cha mwaka 2012/2015 Sillo alibainisha kuwa dawa zilizofanyiwa ufuatiliaji ili kuona ubora wake ni pamoja na dawa za kutibu malaria,dawa aina ya vijiua sumu (Antibiotics) Dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi,dawa za kupunguza maumivu,dawa za kutibu kisukari,dawa za kutibu magonjwa ya moyo,dawa za kuzuia kutoka damu nyingi wakati wa kujifungua aina ya misoprostol.

Katika kipindi cha mwaka 2016/2017 hadi machi 2017, TFDA ilifuatilia katika soko,ubora wa dawa za binadamu aina ya Albendazole vidonge,mchnaganyiko wa dawa ya vidonge aina ya Diclofenac na paracetamol,dawa ya macho yenye mchanganyiko wa Dexamethazone na Neomycin,dawa za mifugo aina ya Oxytetracycline 10% na 20 ambazo uchunguzi wake uko katika hatua za mwisho na matokeo yatatolewa mara yatakapokuwa tayari.

Aidha Sillo amesema kuwa mfumo wa kufuatilia usalama wa dawa katika soko unafanya kazi vizuri hapa nchini tangu mwaka 1989 na umeendelea kuboreshwa ambapo oktoba 2016 tulianzisha mfumo wa utoaji taarifa za madhara ya dawa kielekroniki kwa kutumia simu ya kiganjani.

Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania(TFDA) kwa mujibu wa Sheria ya Chakula,Dawa na Vipodozi,sura ya 219 ina jukumu la kudhibiti ubora na usalama wa chakula,dawa, vipodozi na vifaa tiba ili kulinda Afya za wananchi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Taasisi yake leo Jijini Dar es Salaam.
: Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Taasisi yake leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Majaribio ya Dawa na Ufuatiliaji kutoka Mamlaka hiyo Bi. Kissa Mwamwitwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Hiiti Sillo (katikati) akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari wakati wa mkutano wake na waandishi wahabari( hawapo pichani) kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Taasisi yake leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Meneja wa Kanda ya Mashariki wa TFDA, Emmanuel Alphonce na Meneja Majaribio ya Dawa na Ufuatiliaji kutoka Mamlaka hiyo Bi. Kissa Mwamwitwa.Picha zote na: Frank Mvungi – MAELEZO.

Ziara ya Rais wa Zanzibar Dk.Shein kukagua Maeneo yaliyokumbwa na Mafuriko leo

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa tatu kushoto) alipokuwa akiangalia maji ya Mvua yaliyofurika katika bonde la Mwanakwerekwe nyumba mbili leo kutokana na ujenzi holela wa Nyumba za Wananchi zilizojengwa na kupelekea kutopitisha maji katika njia inayoelekea Ziwa Maboga, kutokana na mvua kubwa za Masika zinazoendelea kunyesha.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) alipokuwa akiangalia maji yanayopita katika barabara ya Mwera gudini – Fuoni meli saba leo wakati alipokuwa katika ziara ya kutembelea maoneo mbali mbali yaliyopatwa na maafa ya Mvua za masika zinazoendelea kunyesha (katikati) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe,Ayoub Mohamed Mahmoud.
Pichani ni maji ya Mvua yakiwa yamefurika na kupelekea kufunga njia ambapo wananchi na magari hupita kwa taabu kubwa katika barabara ya Bonde la Kibonde Mzungu,wakati leo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ( hayupo pichani) alitembelea eneo hilo akiwa na ujumbe wake katika ziara maalum
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akitoa maelekezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji Nd,Mustafa Aboud Jumbe (kulia) alipotembelea barabara ya Mwera gudini – Fuoni meli saba leo wakati alipokuwa katika ziara ya kutembelea maoneo mbali mbali yaliyopatwa na maafa ya Mvua za masika zinazoendelea kunyesha (kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe,Ayoub Mohamed Mahmoud.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati)alipokuwa akiangalia ramani inayoonesha utaratibu wa Ujenzi wa Mitaro kutoka kwa Mkuu ya Idara ya Mipango Miji,Kazi na Ujenzi katika Baraza la Manispaa ya Zanzibar Nd,Mzee Khamis Juma (kulia) wakati alipotembelea Bonde la Maji mwanakwerekwe leo akiwa katika ziara maalum ya kutembelea maoneo mbali mbali yaliyopatwa na maafa ya Mvua za masika zinazoendelea kunyesha (kushoto) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe,Mohamed Aboud Mohammed. Picha na Ikulu. 14/05/2017.

NEWS ALERT: KATIBI WA CCM KATA YA BUNGU WILAYANI KIBITI AUWAWA KWA RISASI

$
0
0
Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Bungu wilayani Kibiti, Alife Mtulia ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amethibitisha.
Kamanda Lyanga amesema mauaji hayo yamefanyika usiku wa kuamkia leo (Jumapili) katika Kijiji cha Nyambunda. Amesema Mtulia aliuawa na watu hao alipokuwa anakwenda kuoga.
Kamanda amesema mwili wa marehemu umepelekwa kituo cha afya cha Kibiti kwa uchunguzi.
Mauaji ya askari Polisi, viongozi wa Serikali za Mitaa na raia yamekuwa yakifanyika mara kwa mara katika wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani.
Jumanne wiki hii akiwasilisha bungeni bajeti ya wizara yake, 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba aliliambia Bunge kuwa Serikali itaanzisha mkoa mpya wa kipolisi katika wilaya za Kibiti, Rufiji, Mkuranga na Mafia ili kuimarisha ulinzi.

LG 2017 System Air Conditioning Tech Seminar held in Dar es salaam

$
0
0
Green Technology embedded products are gaining fast traction in response to the increased regulations for energy efficient products locally and globally

In response to the growing demand for eco-friendly & energy efficient air conditioning solutions in East and Central Africa, LG Electronics East and Central Africa engaged with industry stakeholders to discuss the impact and opportunity for sustainable solutions. The seminar served as a platform for over 100 attendees, including leading consultants, property developers, architects and interior designers to envision the future of Tanzania with environment-friendly technology. 
At the event, LG showcased the prowess of its inverter technology platform with green refrigerants, which is designed to facilitate continuous optimum cooling in East and Central Africa, and thereby contributing toward a greener environment. 
Speaking at the event, Mr. Janghoon Chung, Managing Director of LG Electronics Africa Logistics FZE said, “The East and Central Africa region has established a strong understanding of the importance of using and developing environment friendly products. 
With the rise of trends like smart cities and green buildings in the Middle East and Africa, the Heating, Ventilation and Air Conditioning (HVAC) products and equipment’s market is all set to find high usage across different residential, commercial and industrial applications. Companies are investing in R&D and designing new products that have better energy ratings and result in lower emissions and utility bills. With such a proactive approach by industry players including LG, the Heating, Ventilation and Air Conditioning (HVAC) industry looks set to experience robust growth in the coming years in response to increasing demand”. We are proud to showcase these solutions today in Tanzania and are certain it will create a strong business impact in the community.” 
 Acting Director of Research, Tanzania Building Agency, TBA, Eng. Mtapuri Juma, who was the chief guest on the LG 2017 System Air Conditioning Tech Seminar  and the Launch of  the new eco-friendly & energy efficient air conditioning solutions products for Tanzania,  visiting the AC exhibitions which LG showcased the prowess of its inverter technology platform with green refrigerants, which is designed to facilitate continuous optimum cooling . She is accompanied by Mr. Janghoon Chung, Managing Director of LG Electronics Africa Logistics FZE and LG Technical Director Hebert Wamalwa.
 Acting Director of Research, Tanzania Building Agency, TBA, Eng. Mtapuri Juma, who was the chief guest on the LG 2017 System Air Conditioning Tech Seminar  and the Launch of  the new eco-friendly & energy efficient air conditioning solutions products for Tanzania,  visiting the AC exhibitions which LG showcased the prowess of its inverter technology platform with green refrigerants, which is designed to facilitate continuous optimum cooling . She is accompanied by Mr. Janghoon Chung, Managing Director of LG Electronics Africa Logistics FZE and LG Technical Director Hebert Wamalwa.
 A Dar es Salaam lady, who was  a guest guest at the LG 2017 System Air Conditioning Tech Seminar  and the Launch of  the new eco-friendly & energy efficient air conditioning solutions products for Tanzania, found her self a winner of LG Ultra Modern Microwave, as she receives it from LG Technical Director Hebert Wamalwa. Looking on is Mr. Janghoon Chung, Managing Director of LG Electronics Africa Logistics FZE. The event took place in Dar es Salaam over the weekend.
 Acting Director of Research, Tanzania Building Agency, TBA, Eng. Mtapuri Juma, who was the chief guest on the LG 2017 System Air Conditioning Tech Seminar  and the Launch of  the new eco-friendly & energy efficient air conditioning solutions products for Tanzania,  visiting the AC exhibitions which LG showcased the prowess of its inverter technology platform with green refrigerants, which is designed to facilitate continuous optimum cooling . She is accompanied by Mr. Janghoon Chung, Managing Director of LG Electronics Africa Logistics FZE and LG Technical Director Hebert Wamalwa.
Mr. Rama Esteem from Dar es Salaam, who was a guest at the LG 2017 System Air Conditioning Tech Seminar  and the Launch of  the new eco-friendly & energy efficient air conditioning solutions products for Tanzania, receives the 43in, LG Flat Screen Smart TV from LG Technical Director Hebert Wamalwa. Looking on is Mr. Janghoon Chung, Managing Director of LG Electronics Africa Logistics FZE. The event took place in Dar es Salaam over the weekend. For more CLICK HERE

PROF. MUKANDALA AWAASA VIJANA WASIKUBALI KUSUKUMWA NA MAWIMBI

$
0
0

*Asema utu, maendeleo na maisha bora havipatikani kwa fedha

MAKAMU MKUU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Prof. Rwekaza Mukandala amewataka vijana wanaohitimu kidato cha sita nchini wawe makini na wasikubali kusombwa na mawimbi ya dunia.

Ametoa wito huo jana (Jumamosi, Mei 14, 2017) wakati akizungumza na wahitimu 237 wa kidato cha sita wa shule ya sekondari ya St. Joseph Cathedral kwenye mahafali ya sita ya shule hiyo yaliyofanyika shuleni hapo, jijini Dar es Salaam.

Prof. Mukandala alisema: “Kwa hatua mliyofikia kila mmoja anapaswa atafakari kwa kina wito wake kimaisha. Kuweni makini, msisukumwe na mawimbi ya dunia na kujikuta mmepoteza ndoto zenu,” alisisitiza.

“Kuhitimu kidato cha sita si jambo dogo. Ni hatua ya kuwaongiza kujiandaa na utu uzima ikiwemo kujiunga na elimu ya vyuo vya juu na kuingia kwenye ndoa. Ni muda wa kutathmini yale uliyopitia na kutafakari maisha yako ya baadaye. Ni fursa ya kutoa shukrani kwa Mungu, kwa wazazi na walimu ambao walifanya kazi kwa umakini na kujitoa ili mfikie hatua nzuri mliyopo sasa,” alisema.

Alisema kuanzia sasa kila mmoja wao anapaswa kujiamini, kujituma zaidi na kujiona kuwa ana wajibu wa kujiletea maendeleo binafsi. “Mnapaswa kuepuka mwenendo wa kujiona mnyonge, au mtu asiyeweza kutimiza ndoto zake. Jenga tabia ya kuwa makini na maisha yako, jali mazingira yako na maendeleo yako,” alisisitiza.

Aliwataka wahakikishe wanakuchukua hatua mahsusi na kupata taarifa sahihi kuhusu taaluma wanazozitaka. Aliwataka wawe waadilifu na wenye heshima kwa watu wote lakini pia akawaasa juu ya maisha ya kutaka kupata fedha kwa haraka na kujilimbikizia mali.

“Epukeni rushwa na ufisadi. Mnatakiwa kujua kuwa utu, maendeleo na maisha bora havipatikani kwa fedha ingawa nayo ni muhimu katika maisha. Msitegemee kuishi kwa kuzingatia mambo makubwa yanayopimika kwa fedha,” alisema.
Mkuu wa Shule ya St. Joseph Cathedral, Sista Theodora Faustine akimkabidhi zawadi na cheti, Prof. Rwekaza Mukandala ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya sita ya kidato cha sita, ili ampatie mhitimu. Mahafali hayo yalifanyika Jumamosi, Mei 13, 2017 shuleni hapo. (Picha na Irene Bwire)
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Prof. Rwekaza Mukandala ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya sita ya kidato cha sita ya Shule ya St. Joseph Cathedral, akizungumza na wahitimu (hawapo pichani). Mahafali hayo yalifanyika Jumamosi, Mei 13, 2017 shuleni hapo. (Picha na Irene Bwire).  
Viranja wa darasa la PCM, Martin na Nsobya Musona wakipokea zawadi ya keki kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Prof. Rwekaza Mukandala ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya sita ya kidato cha sita ya Shule ya St. Joseph Cathedral, yaliyofanyika Jumamosi, Mei 13,2017) shuleni hapo. 
Baadhi ya wazazi, walezi na ndugu walioshiriki mahafali ya sita ya kidato cha sita ya shule ya sekondari ya St. Joseph Cathedral yaliyofanyika Jumamosi, Mei 13, 2017 shuleni hapo.

Announcement of Zuriels Annual DUSUSU Awards to African First Lady for 2017 Next Week

$
0
0
It is possible you have heard or read about Zuriels annual DUSUSU Awards, which she presents to an African First Lady, whose work in the area of Girls Education in their countries exemplifies Zuriels belief in the need for not just political office holders, but non office holders to fight for, on the African continent.

She began this initiative in 2014, after her maiden First Lady's colloquy she convened in Lagos in April 2014. That year, the DUSUSU First Lady Award went to Salma Kikwete of Tanzania, in 2015 to Margaret Kenyatta of Kenya (Top), and in 2016 to Monica Geingos of Namibia (below right).
What makes this award very personal to the First Ladies who receive it is that there is nothing 'political. or 'economically driven' about it, rather, it is being presented by a Girl, who is not just passionate about Girls Education and globally recognized for it, but she herself recognizes the singular efforts of those on the African continent - First Ladies, who are quietly but measurably making a difference in this fight. So as it were, more than any other Award these First Ladies receive, this one is very dear to them as well.

It is also unique, because they cannot campaign for it, and are not privy in any way to the selection criteria, otherwise, they could position themselves for it.

Announcement Next Week

Zuriels committee would be announcing the recipient for the Awards next week, and she would be making the travel to the recipients country to personally present the Award, as she has done in the past, in the State House, Presidential Palace, or Prime Ministers Residence - as applicable.

RC WA ARUSHA AONGOZA WANANCHI KUWAAGA WANAFUNZI KWENDA MAREKANI KWA MATIBABU

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akifurahia jambo na mmoja wa marubani wa kampuni ya Samaritan's Purse kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro kabla ya wanafunzi watatu hawajaelekea Marekani kwa matibabu kufuatia ajali iliyotokea wilayani Karatu wiki iliyopita.

Mbunge wa jimbo la Singida Kaskazini,Lazaro Nyalandu akizungumza jambo kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro.

Mbunge wa jimbo la Singida Kaskazini,Lazaro Nyalandu na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo wamjulia hali Doreen Elibarick

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akimsalimia Doreen Elibarick kabla ya kupanda ndege kwenda Marekani kwa matibabu.

Utaratibu wa kuwaingiza kwenye gari kisha kwenye ndege ukiendelea na maafisa wa uwanja wa ndege wa KIA.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akifurahia Kadi zilizoandaliwa na wanafunzi wa shule ya ISM kwa ajili ya wanafunzi wenzao.
Imeandaliwa na www.rweyemamuinfo.blogspot.com
Viewing all 110152 articles
Browse latest View live




Latest Images