Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

SERIKALI YATOLEA UFAFANUZI SUALA LA VYETI FEKI


MAONYESHO YA SITA YA MADINI YA VITO YAANZA RASMI LEO JIJIJI ARUSHA

$
0
0
Na Woinde shizza, Arusha
Maonesho ya sita ya madini na vito maarufua kama Arusha Gem fair yameanza rasmi jijini Arusha leo huku ikielezwa kwamba Wananchi wengi wanaoishi karibu na migodi inayochimbwa madini ya aina mbalimbali wamekuwa hawanufaiki kutokana na viongozi wa maeneo husika kutokuwa na mahusiano mazuri na wamiliki wa migodi hiyo.
Hayo yamebainishwa na Mbunge wa jimbo la Simanjiro Mhe. James Ole Milya wakati akiongea katika uzinduzi wa maonesho hayo. 

“Asilimia kubwa ya wananchi ambako madini hayo yanachimbwa ukifuatilia maisha yao ni duni na hawana maendeleo yoyote. Kwa ufupi hawanufaiki na madini ambayo yanatoka katika maeneo yao. Hivyo ni wajibu wa Serikali kuangalia upya sera ya madini.

"Mfano mwananchi wa Mererani madini yanachimbwa kwao, lakini ukiangalia maisha wanaoyoishi huwezi kusema wanakaa sehemu inayotoka Tanzanite ambako ni hapo pekee duniani,”alisema Milya
Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini katika Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe amesema kuwa sera ipo na sheria zipo za kuhakikisha wananchi ambao wanazunguka maeneo ya migodi wananufaika na migodi hiyo, lakini ukifuatilia kwa kiasi kikubwa wale wananchi ambao hawanufaiki ni wale ambao unakuta viongozi wao wa mtaa au kijiji hawana ushirikiano mzuri na viongozi au wawekezaji waliowekeza katika maeneo yao.
"Hivyo ni wajibu wa wananchi pamoja na viongozi kushirikiana kwa pamoja na kuungana ili kuweza kusaidia", alisema.
Bw. Mdoe aliongezea kuwa haya ni maonyesho ya sita kufanyika na yanafanyika kwa muda wa siku tatu, lengo ikiwa ni kutimiza dira iliopo katika sera ya madini ya mwaka 2009 inayosisitiza kuwa Tanzania iwe kitovu cha madini.
"Sekta ndogo ya vito inachangia katika uchumi wa maendeleo ya jamii hivyo maonyesho haya ni fursa kwa wachimbaji na wafanyabiashara wa hapa nchini kuweza kupata fursa ya kujitangaza zaidi.
“Wageni wengi kutoka nchi mbalimbali wanahudhuria katika maonyesho haya, wengine wanakuja kununua madini wengine wameleta madini yao ili yauzwe> kwa hiyo hii ni fursa ya pekee ya wachimbaji wetu wa ndani kujitangaza na kupanua soko la zaidi kikubwa zaidi waangalie ni namna gani watayafanya madini yao yawe na dhamani zaidi”alisema Bw. Mdoe.
baadhi ya madini yaliyoletwa katika maonyesho
Mkuu wa mkoa wa Manyara Dk Joel Bendera akifuatilia jambo wakati alipokuwa anazindua rasmi maonyesho ya sita ya vito na madini yanayofanyika katika hotel ya Mounti Meru ilipo jijini Arusha.
Meya wa jiji la Arusha Mstahiki Calist Lazaro pamoja na wabunge kadhaa aalihudhuria katika uzinduzi wa maonyesho hayo ya vito na madini.
Habari picha na Woinde Shizza, Arusha.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MAY 4,2017

Mshindi wa mashindano ya 'Bball Kings' kujinyakulia kitita cha shilingi milioni 10

$
0
0

Kituo cha East Africa Television (EATV) na East Africa Radio kwa udhamini wa Kinywaji cha Sprite, kiimeandaa mashindano ya mpira wa kikapu yanayojulikana kama ‘Bball Kings’.

Akizungumza na Waandishi wa habari mapema jana jijini Dar,Mwakilishi wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania - Tanzania Basketball Federation (TBF),  Mwenze Kabinda alisema kuwa 
yanatarajia kufanyika katika viwanja tofauti ndani ya Jiji la Dar es Salaam kuanzia mwezi huu wa Mei na kufikia tamati mwezi Julai mwaka huu.

Kabinda alisema kuwa mashindano hayo yatashirikisha timu mbalimbali za mpira wa kikapu kutoka pande mbalimbali za Tanzania.

" Dhumuni kuu la mashindano haya ni kuutangaza na kuibua vipaji vipya katika mchezo wa kikapu hapa nchini.Mashindano haya yamepatiwa kibali kuendeshwa hapa nchini kwa kuzingatia sheria za Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania - Tanzania Basketball Federation (TBF),na kwamba mashindano haya yatakuwa na hatua kuu saba",alisema Mwenze Kabinda.
 Meneja Mauzo na Masoko (EATV),Ronald Mbowe  akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari mapema jana jijini Dar kuhusiana na zawadi mbalimbali zitakazotolewa katika Mashindano hayo,na pia vigezo vitakavyotumika katika ushiriki wake.
 Afisa Masoko wa Sprite-Tanzania,Pamela Lugenge. (kulia),ambao ndio wadhamini wa Mashindano hayo,akizungumza mbele ya Waandishi wa habari,mapema jana jijini Dar,naona ya kuyaboresha mashindano hayo ambayo yamekuwa yakiwavutia mashabiki wengi wa mchezo huo
Pichani kushoto ni Mwakilishi wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania - Tanzania Basketball Federation (TBF),  Mwenze Kabinda akitoa ufafanuzi kuhusiana na mashindano ya mpira wa kikapu yanayojulikana kama ‘Bball Kings’.,mbele ya Waandishi wa habari mapema jana,ambapo mashindano hayo yanatarajiwa kuanza kurindima ndani ya mwezi huu wa Mei na kufikia  tamati mwezi Julai,mwaka huu.Pichani kati ni Meneja Mauzo na Masoko (EATV),Ronald Mbowe na kulia ni Afisa Masoko wa Sprite-Tanzania,Pamela Lugenge. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RAS TANGA ATAKA WAANDISHI WA HABARI KUPEWA USHIRIKIANO

$
0
0
KATIBU Tawala Mkoa Tanga Mhandisi Zena Said ameziagiza taasisi za Serikali na mashirika ya umma kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari pindi wanapohitaji taarifa kutoka kwenye taasisi hizo kwa ajili ya kuhabarisha umma.

Ameyazungumza hayo leo wakati wa kuadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari Duniani ambapo Mkoa Tanga maazimisho hayo yalifanyika katika ukumbi wa klabu ya waandishi wa habari na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali na zisizo za kiserikali.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya waandishi wa habari kutoa malalamiko yao mbele ya Katibu Tawala huyo wa Mkoa ambae alikua mgeni rasmi katika maazimisho hayo ya kuwa zipo baadhi ya taasisi za Serikali kushindwa kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari pindi wanapohitaji kutekeleza majuku yao ya kazi.

Burhan Yakubu ambae ni mjumbe na mwaandishi wa habari alisema kumekuwepo na utaratibu usioendana na maadili ya kiuwandishi katika Hospitali kuu ya Rufaa ya Bombo kwa kutengeneza urasimu wa kupatikana kibali kutoka kwa katibu tawala Mkoa wakati mwandishi anapohitaji kupatiwa tariifa zozote kutoka katika Hospitali hiyo
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi akifungua maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari Duniani kimkoa yaliyofanyika kwenye ukumbi wa klabu ya waandishi wa habari mkoani Tanga (Tanga Press Club) leo kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga,Hassan Hashim kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga,Lulu George 
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga,Hassan Hashim akizungumza katika maadhimisho hayo leo 
Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga,Lulu George akizungumza katika maadhimisho hayo kushoto ni Katibu Msaidizi Alex Abraham .

MAKALA YA SHERIA: MKE ANARUHUSIWA KUUZA MALI YA MUMEWE BILA RIDHAA YA MUME ILI KUJIPATIA MAHITAJI

$
0
0
Na  Bashir  Yakub.

Matunzo  ya  mke  kutoka  kwa  mme  ni  jambo  la  lazima.  Kwa  maana  kuwa  ni  lazima  mme  kutoa  mahitaji  kwa  mke  wake  .Hakuna  uhiari  katika  hili. Ni  lazima  na  neno  lazima  maana  yake inajulikana. Ifahamike  kuwa  matunzo  anayotoa  mme   kwa  mke  wake  si  msaada,  si  hisani, si  upendeleo,  si  zawadi  bali  ni  wajibu.  

Matunzo  yenyewe  ni  kama   chakula ,  sehemu  ya  kulala  na  kuishi, mavazi,  matibabu  na  kila  kitu  ambacho  ni  muhimu  kwa  mahitaji  ya  mke  husika. Kifungu  cha  63(a)  cha  Sheria  ya  ndoa  kinasema  kuwa  ni  wajibu    na  lazima  kwa  mume  kumtolea  matunzo  mke  wake. 

1.VIPI  MUME  AKISHINDWA  KUTOA  MATUMIZI.

Yapo  mambo  ambayo  mke  anaweza  kuyafanya  ikiwa  mme  wake  atashindwa  kumtolea  matumizi .  Mojawapo  ni  hili  la  kuruhusiwa  kuuza  mali  ya  mme  wake  bila  ridhaa  ya  mme huyo. 

Tutaona  likoje  hili  baadae.  Mengine  ambayo  anaweza  kufanya  mke  ikiwa  amenyimwa  matumizi  ni  pamoja  na  kufungua  shauri  mahakamani  kudai  matumizi, na  hata  kudai   talaka  ikiwa  hali  hiyo  imekuwa sugu.

2.  KUUZWA  KWA  MALI  YA   MME.
Kwa  ujumla  kifungu  cha 64( 1 ) cha  Sheria  ya ndoa  kinasema  kuwa  mke  ataruhusiwa  kuuza  mali  ambayo  kimsingi  inamilikiwa  na  mme  wake  kwa  ajili  ya  kujipatia  matunzo  au  mahitaji  muhimu  ya  kwake  na/au   ya  watoto/mtoto  wake. 

Kuhusu  ni  kipi  kinaweza  kuuzwa,  wakati  gani  kiuzwe,  kwa masharti  yapi  tutaona  hapa  chini.
3.  MASHARTI   KABLA  MKE  HAJAUZA.

( a ) Kwanza  ambaye  anaruhusiwa  kuuza  ni  lazima  awe  mke  halali wa  mme  huyo.  Kimada( concubine) hawezi  kuuza  mali  ya  mwenzake.  Ni  mke  wa  ndoa  tu  ndiye  anayeruhusiwa. Yaweza  kuwa  ndoa  ya  kidini, ya  kimila, ya  serikali  au  ile  inayotokana  na kuishi  wote  miaka  miwili.
( b ) Ni  lazima  iwe  mke  amenyimwa  matumizi  muhimu. Ikiwa  hajanyimwa  matumizi  hawezi  kuwa  na  mamlaka  ya  kuuza  mali  ya  mme  wake. 

( c ) Pia  ikiwa  ana  watoto/mtoto  na  hawana  matumizi  basi  napo  anaweza  kuuza  mali  ya  mme  wake.
( d ) Huwezi  kuuza  mali  ya mme  wako   kwa  ajili  ya  kujipatia  matumizi  ya  anasa.  Matumizi  yatakayokupelekea  kuuza  mali  ya  mme  ni  yale  ya  lazima. 

Mahakama yawaachia huru wabunge watatu wa Ukawa na Makada wao

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru wabunge watatu wa Ukawa na Makada wao baada ya kuonekana hawana kesi ya kujibu. Wabunge hao na wenzao walikuwa wakikabiliwa na tuhuma za kumjeruhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresa Mmbando.
Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya kiridhika kwamba ushahidi ulioletwa mahakamani hapo haukuwa unatosha kuwakuta washtakiwa na kesi ya kujibu.
Amesema kuwa katika ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashtaka  umeshindwa kuthibisha kwani, hata  mlalamikaji Mmbando hakumbuki ni nani alimjeruhi. Ameongeza kuwa, ushahidi wake ulielezea tu Jinsi washtakiwa walivyojishughulisha na nyaraka siku ya tukio na siyo kumjeruhi.
Kuhusu kushikwa matiti, Hakimu Shaidi alisema kitendo hicho kingeweza kupelekea mlalamikaji kufungua kesi nyingine lakini siyo kujeruhi.

Katika kesi hiyo upande wa mashtaka uliita mashahidi watatu kutoa ushahidi ambapo hakuna ushahidi ulioweza kuwatia hatiani watuhumiwa hao na kukutwa na kesi ya kujibu.
Wabunge wa Chadema, na makada wao pamoja na Wakili Wao Peter Kibatala wakifurahi nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kiachiwa huru kwa kuonekana hawana kesi ya kujibu dhidi ya tuhuma iliyokuwa inawakabili ya kumjeruhi Katibu Tarafa Mkoa wa Dar es Salaam Theresia Mmbando. Habari kamili BOFYA HAPA

RC NDIKILO AWATAKA WAKULIMA WA MATUNDA KULIMA KISASA ILI KUPATA SOKO NDANI NA NJE YA NCHI

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo 

WAKULIMA wa matunda wametakiwa kulima kwa kutumia mbegu bora na kilimo cha kisasa ili kupata soko kwenye viwanda vinavyosindika zao hilo, ndani na nje ya nchi. Aidha wananchi wameshauriwa kulima kilimo kinachostahimili ukame ikiwemo mahindi, mihogo, viazi vitamu na mikunde ili kujihadhali na baa la njaa baadae

Hata hivyo wametakiwa kuhifadhi chakula wakati wa mavuno utakapofika kwani kwa kufanya hivyo itawasaidia kuwa na akiba ya kutosha. Rai hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo, alipotembelea kiwanda cha Elven Agri company ltd kilichopo Mapinga na kiwanda cha Sayona kinachomilikiwa na kampuni MAMA ya MMI steel, kilichopo kata ya Mboga wilayani Bagamoyo.

Alieleza, wakulima wengi wanahitaji kulima kwa tija badala ya kupata hasara kwa kukosa masoko. Mhandisi Ndikilo alisema, kwa kutambua hilo, kuna kila sababu ya kubadilika kwa kuona umuhimu wa kulima matunda yaliyo na rutuba bora na yanayojiuza. 

"Wataalamu wa kilimo, watendaji wa halmashauri katika idara hii, mtoke maofisini muende kuwapa elimu wakulima hawa ili waweze kujifunza kulima kwa kutumia mbegu za msimu mfupi, kuweka pembejeo na kupalilia, Kwa kutoa elimu za mara kwa mara kwa kufuata teknolojia za kisasa, lazima waende na wakati ili waweze kunufaika kwa jasho lao "alisema mhandisi Ndikilo. 
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo, aliyeshika ndizi, akionyeshwa hatua za uzalishaji katika usindikaji wa matunda kwenye kiwanda cha kusindika matunda cha Elven Agri co. Ltd kilichopo Mapinga, Bagamoyo.
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto) akionyeshwa namna bidhaa mbalimbali kama pilipili zinavyofungashwa katika kiwanda cha kusindika matunda cha Elven Agri co. Ltd kilichopo Mapinga Bagamoyo.

EFM RADIO YATUA KANDA YA ZIWA

$
0
0
KATIKA kuhakikisha watanzania wengi wanapata matangazo yake, Kituo cha Utangazaji cha Efm kimetanua matangazo yake kwa kuongeza masafa ya 91.3 fm Mkoani Mwanza huku Uongozi ukibainisha kuwa, matarajio ni kuhakikisha Matangazo hayo yanafika katika mikoa mingine kumi, ikifuatiwa na Mkoa wa Mbeya.

Mikoa mingine ni pamoja na, Singida, Kilimanjaro, Manyara, Mtwara, Tanga , Kigoma na  Dodoma.

Kwa mujibu wa Meneja Mkuu wa EFM Radio, Denis Ssebo amesema lengo la kuanza na Mkoa wa Mwanza, wameangalia idadi ya watu ambao wanapatikana kupitia Kanda ya Ziwa Victoria lakini pia ukubwa wa jiji baada ya jiji la Dar es salaam.

Lengo la Efm Radio ni kuhakikisha inahabarisha, kuburudisha, kuwawezesha pamoja na kuwapa elimu wasikilizaji wake wote katika kila mkoa itakaposikika.  Hivyo mikoa mingine ikae mkao wakula, “tutawafuata mlipo… Denis Ssebo”.
EFM NI KWIKWI

VIDEO: HUSSEIN MACHOZI AACHIA VIDEO NA WIMBO MPYA ‘NIPE SIKUACHI’

$
0
0
Baada ya kukaa kimya kwa miezi kibao bila kuachia wimbo, Hussein Machozi ameachia wimbo mpya uitwao, Nipe Sikuachi. Wimbo huo umetayarishwa na mshindi wa tuzo ya mtayarishaji bora wa Bongo Flava katika miaka tofauti, Man Walter kupitia studio zake za Combination Sound.

“Combination yangu ya mimi na Man Walter, sidhani kama kuna kitu cha mchezo hapo,” anasema Machozi kuhusiana na wimbo huo. “Man Walter ni mshkaji kitambo, tumekutana tukakubaliana kufanya kazi na tukaona kabisa kwamba sisi tukifanya kazi wawili itakuwa kazi na ndicho kilichofanyika,” ameongeza.

Anaeleza, “Video pia imefanyika Italy, Gressoney Italy. Kuna mabadiliko makubwa ukiangalia location ambazo tumezizoea, ukiangalia video ambazo kila siku tunaziona Tanzania za magari na majumba.”

Machozi ambaye anafahamika kwa vibao vingi vilivyowahi kufanya vizuri kwenye vituo vya redio na runinga ndani na nje ya Tanzania vikiwemo ‘Utaipenda’, ‘Kwaajili Yako’, ‘Addicted’ na zingine, amedai kuwa ukimya wake ulitokana na majukumu mengine ya kimaisha.

“Kama unavyojua, hakuna mtu anapenda kuwa kimya, na ukifuatilia vizuri kuna kazi kadhaa nilishawahi kuziachia lakini hazikufika nilikotarajia nadhani kwasababu ya ukosefu wa management.

Kwa sasa Hussein anaishi nchini Italia baada ya kuwa ameenda kusoma, lakini hiyo haimaanishi kuwa ameupa kisogo muziki, kitu anachoamini alizaliwa kukifanya. “Kinachokuja kuonekana sasa hivi, hakijawahi kuonekana katika macho ya watu na nimejaribu kufanya hivyo kwasababu mimi mwenyewe nahitaji mabadiliko, nifanye kitu ambacho ni kipya zaidi hata kwenye macho yangu mimi, kwahiyo nimekikubali kwamba ni kipya, video ni mpya, audio ni mpya kabisa.”

Video ya wimbo huo ipo Youtube tayari na audio itapatikana mtandaoni

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA PALESTINA DR.RIYAD MALIKI,AKARIBISHA KURA YA UNESCO, AKISEMA DUNIA IMEAMUA KUSIMAMIA HAKI

$
0
0
Ramallah, Mei 2, 2017 (Wafa) – Waziri wa Mambo ya Nje wa Palestina Dr. Riyad Maliki,Jumanne ya wiki hii amekaribisha matokeo ya kura ya Bodi ya Utendaji ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO),kwa kupitisha maazimio mawili yanayohusu Palestina,ambayo ni: Palestina inayokaliwa kimabavu na Taasisi za kiutamadui na kielimu. Nchi zipatazo ishirini (20) zimepitisha maazimio hayo,huku nyingine kumi (10) zikipinga na ishirini na tatu (23) hazikupiga kura.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Maliki amezishukuru nchi hizo zilizopitisha maazimio hayo mawili na kujua wajibu wake katika kuhifadhi maeneo matakatifu nchini Palestina. Alisisitiza kuwa "licha ya jitihada zinazotolewa na serikali kutokana na tamaa ya serikali ya Israeli katika kudhoofisha maazimio ya Palestina ndani ya UNESCO, hata hivyo dunia imepitisha maazimio yetu kwa kuchagua haki iko wapi mbele ya usawa,kazi na sera zake haramu .

Ameongeza kusema kwamba, hilo limethibitisha kushindwa kwa kampeni nyingi za Israeli dhidi ya maazimio yahusuyo Palestina, Jerusalemu na UNESCO, huku wakishindwa pia wale wote waliounga mkono hatua ya kudhoofisha maazimio hayo, miongoni mwa nchi mbalimbali,vikundi,taasisi na hata watu binafsi.

Amesema maazimio yameonesha nyanja za kihistoria, kiutamaduni na urithi wa mji wa Jerusalemu,jambo linalosisitiza umuhimu wa kupeleka mwakilishi wa kudumu wa UNESCO mjini Jerusalemu,ili kufuatilia ukiukwaji na kuondoa vitendo vya uharibifu vinavyofanywa na Israeli,ambayo inafanya juhudi kufuta urithi wa kihistoria,kidini na wa kiutamaduni wa mji huo,hatimae kubadilisha kabisa hadhi yake.

Waziri huyo wa Mambo ya Nje wa Palestina, kwa upande mwingine ameelezea kutoridhika kwake na msimamo wa nchi zilizokataa kupitisha maazimio hayo mawili,kwa mtazamo wa kushajihisha kuendelea kwa utawala wa kivamizi na vitendo vyake haramu mjini Jerusalemu inayokaliwa kwa mabavu. Pia kushuka kwa misimamo na misingi ya nchi hizi, ambazo baadhi yake zinadai kutetea misingi ya sheria za kimataifa na haki za binadamu.

Ametilia mkazo kwa kusema, "Sisi tutaendelea kutetea urithi wetu, utamaduni wetu na uwepo wetu,huku tukikabili kampeni zote za kuvuruga hilo na kuziharibu, zinazoongozwa na mamlaka ya kivamizi ya Israeli. Vilevile mapambano ya silaha kwa mujibu wa sheria za kimataifa na matakwa ya taifa la Palestina lenye uwezo wa kujipangia mustakabali wake uliepukana na uvamizi”.

Aidha, ametoa wito kwa mataifa yote duniani kubeba majukumu yao na si kuingilia kazi za UNESCO, wala kuihamasisha Israeli kama ndio taifa la kivamizi kuendelea kufanya maovu yake. Pia Ametoa wito kwa mashirika ya Umoja wa Mataifa, hasa UNESCO, kuulinda urithi wa Jerusalemu, utamaduni na historia yake, Jerusalemu ambayo ndio mji mkuu wa Palestina, kutokana hatua zote za kuvuruga ustaarabu wa mji huo.

WAGOMBEA URAIS NCHINI UFARANSA WAPIGANA VIJEMBE KATIKA MDAHALO

$
0
0
Mdahalo wa televisheni wa baada ya duru ya kwanza na kabla ya duru ya pili ya uchaguzi wa urais nchini Ufaransa ulifanyika Jumatano, Mei 3, mjini Paris. Wagombea urais wawili Emmanuel Macron na Marine Le Pen ndio walishiriki mdahalo huo.

Wagombea hao, kila mmoja alitoa sera zake kwa kuwashawishi wale ambao bado hawajaonyesha msimamo wao wa kupiga kura. Emmanuel Macron na Marine Le Pen walishambliana kwa maneno makali.

Wagombea katika duru ya pili ya uchaguzi wa urais nchini Ufaransa walikabiliana vikali katika mdahalo wa televisheni uliofanyika Jumatano Mei 3. Emmanuel Macron na Le Pen walipambana kwa muda wa zaidi ya saa 2 na dakika 30 katika mdahalo wa baada ya duru ya kwanza na kabla ya duru ya pili ya uchaguzi wa urais. Marine Le Pen mgombea kwa tiketi ya chama cha FN, ambaye alichukua nafasi ya pili baada ya kushindwa na Emmanuel Macron alionekana kumshambulia mpinzani wake kuanzia mwanzo wa mdahalo huo.

Bi Le Pen alisema Emmanuel Macron ni "mgombea wa utandawazi wa kikatili, wa ukatili wa kijamii, wa vita vya wote dhidi ya wote". "Mkakati wako ni kusema tu uongo, lakini haupendekezi chochote," alijibu Emmanuel Macron, akijitetea.

Mdahalo huo uligeuka na kuchuku sura nyingine ambapo wagombea hao wawili walijibizana vikali, kila mmoja akimshambulia mwenginei. Bii Le Pen alimstumu mpinzani wake kuhusu masuala makubwa ya viwanda kama sera ya kiuchumi na kijamii. "Wewe unatii mahitaji ya Umoja wa Ulaya, ushindani usio wa haki za kimataifa (...) huna ujasiri wa kitaifa, haufikirii maslahi ya taifa," Marine Le pen amesema.

Ziara ya kiwanda cha Whirlpool katika mji wa Amiens tarehe 26 Aprili ilirejelewa katika mdahalo huo na kuzua mvutano mkubwa. Emmanuel Macron amemtuhumu mpinzani wake kuwa "alichukulia maisha ya dhiki yanayo wakabili wafanyakazi wa kiwanda hicho kwa kutetea maslahi yake.""Mimi sijajificha" katika mkutano na shirikisho la wafanyakazi, alijibu Bi Le Pen. "

Katika mdahalo huo wagombea waligusia maswala ya usalama na ugaidi. bi Le pen amesema " inabidi kurejesha mipaka yetu, kufukuza wageni kukwama katika nchi yetu, kuwanyima wageni uraia" alisema Marine Le Pen, kabla kumshutumu Emmanuel Macron kuwa anarahisisha ugaidi wa Kiislamu ".

Emmanuel Macon alijitetea kwa kuhakikisha kuwa tishio la kigaidi ni "kipaumbele" kwake. "Kama amiri jeshi mkuu, kama mkuu wa usalama, nitafanya mapambano kwa pande zote dhidi ya ugaidi wa Kiislamu, " amesema Bw Macron.chanzo RFI 

MASHINDANO YA KUMBUKUMBU YA HABIBU MNDEME MAARUFU KAMA HABIBU CUP YAMALIZIKA WILAYANI MWANGA

$
0
0


Mgeni rasmi katika mashindano ya kumbukumbu ya Habibu Mndeme ,Thabiti Mndeme akimkabidhi kikombe cha umalkia wa mchezo wa netiboli wa timu ya Green Bird Collage .
Mgeni rasmi katika mchezo wa fainali za Mashindano ya Habibu Cup ,Thabit Mndeme akisalimiana na wachezaji wa timu ya Nyerere.
Mgeni rasmi katika mchezo wa fainali za Mashindano ya Habibu Cup ,Thabit Mndeme akisalimiana na wachezaji wa timu ya Kifaru.
Mgeni rasmi katika mchezo wa fainali kati ya timu za sekondari za Nyerere na sekondari ya Kifaru,Thabit Mndeme akizungumza kabla ya kuanza kwa mchezo wa fainali baina ya timu hizo mbili.
Kikundi cha ushangiliaji cha timu ya Nyerere .

TADB, SUA INK AGREEMENT ON RESEARCH AND DEVELOPMENT COOPERATION

$
0
0
TADB’s Acting Managing Director, Mr. Francis Assenga (centre) chairs an agreement meeting on research and development cooperation when SUA’s Principal of College of Agriculture, Prof. Susan Nchimbi-Msolla (second right) and her assistant Prof. Benard Chove (right) paid a visit at TADB premises. Looking on are some of TADB’s management members.
TADB’s Acting Managing Director, Mr. Francis Assenga (second left) exchanges partnership agreement with SUA’s Principal of College of Agriculture, Prof. Susan Nchimbi-Msolla. Witnessing are TADB’s Head of Legal Services, Neema-Christina John (Left) and SUA’s Deputy Principal of College of Agriculture, Prof. Benard Chove (right). The eve took place at TADB’s premises in Dar es Salaam.
TADB’s Acting Managing Director, Mr. Francis Assenga (second left) and SUA’s Principal of College of Agriculture, Prof. Susan Nchimbi-Msolla display their exchanges partnership agreement. The agreement that aims at facilitating collaboration in the development and implementation of capacity building programs for smallholder farmers, medium and large scale farmers and agro-processors in Tanzania and SUA Graduates for practical training and employment at TADB and its partner institutions.Witnessing are TADB’s Head of Legal Services, Neema-Christina John (Left) and SUA’s Deputy Principal of College of Agriculture, Prof. Benard Chove. The eve took place at TADB’s premises in Dar es Salaam.
TADB’s Acting Managing Director, Mr. Francis Assenga (second left) and SUA’s Principal of College of Agriculture, Prof. Susan Nchimbi-Msolla display their exchanges partnership agreement. The agreement that aims at facilitating collaboration in the development and implementation of capacity building programs for smallholder farmers, medium and large scale farmers and agro-processors in Tanzania and SUA Graduates for practical training and employment at TADB and its partner institutions. Others in the photo are management members of TADB and SUA’s Deputy Principal of College of Agriculture, Prof. Benard Chove (right). The eve took place at TADB’s premises in Dar es Salaam.

NEWZ ALERT:RAIS DKT MAGUFULI AMTEUA PROF.EGID BEAUTUS MUBOFU KUWA MKURUGENZI MKUU WA TBS


Wakandarasi 3,000 nchini wafutiwa usajili kwa kukiuka sheria.

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameagiza kuwa miradi yote yenye thamani isiyozidi bilioni 10 wapewe Wakandarasi wa ndani hasa kwa miradi inayotekelezwa kwa fedha za ndani kwani wakandarasi hao watasaidia kuongeza ajira kwa vijana wa Kitanzania na kuongeza uwekezaji ndani ya nchi.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo mjini DODOMA wakati anafungua mkutano wa siku Mbili wa mashauriano wa Bodi ya Usajili wa Wakandarasi mwa mwaka 2017.

Makamu wa Rais amesisitiza wakandarasi hao kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili na sheria pamoja na kumaliza kazi wanazopewa ndani ya muda uliopangwa kwa kuzingatia ubora wa kazi na gharama zilizokubalika kwenye mikataba na sio vinginenevyo.

Makamu wa Rais amewataka wakandarasi kote nchini kuacha mara moja tabia ya kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi wanayopewa.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kuwapa kipaumbele wakandarasi wazawa ili wathubuti kujitosa na kumudu zabuni za ujenzi kwani kwa kufanya hivyo kutaleta faida mbalimbali ikiwemo fedha watakazopata watawekeza ndani ya nchi na kutoa ajira za kutosha kwa vijana wa Kitanzania.

“Hatuwezi kuwa na Tanzania ya Viwanda huku tukiwanufaisha Makandarasi wa nje pekee ni lazima Makandarasi wa ndani wanufaike pia.”

Kuhusu madeni ya wakandarasi, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewahakikishia wakandarasi kuwa Serikali haijawasahau na bajeti ya Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano ambayo imepitishwa na bunge imezingatia kilio hicho cha wakandarasi.

Ameahidi kuwa Serikali itaendelea kulipa madeni inayodaiwa na wakandarasi ili kujenga mahusiano mazuri ya wakandarasi hao.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Mashauriano Wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi kwa Mwaka 2017 kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Kikwete mkoani Dodoma.
 Wajumbe  wa Mkutano wakimsikiliza kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Mashauriano Wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi kwa Mwaka 2017 kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Kikwete mkoani Dodoma.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Makandarasi Mhandisi Consolata Ngimbwa akihutubia wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Mashauriano Wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi kwa Mwaka 2017 kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Kikwete mkoani Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa,Viongozi wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi  na Wajumbe waliohudhuria mkutano wa Mashauriano Wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi kwa Mwaka 2017 nje ya  ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Kikwete mkoani Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Wakandarasi Wanawake mara baada ya kufungua Mkutano wa siku mbili wa Mashauriano Wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi kwa Mwaka 2017 kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Kikwete mkoani Dodoma. 

SERIKALI YA AWAMU YA TANO YAPONGEZWA KWA KUENDELEA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA

$
0
0
Spika Mstaafu wa Bunge na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Mama Anna Makinda akiwasili katika ukumbi wa Ledger Hotel Jijini Dar es Salaam kufungua Kongamano la Kwanza la Bima ya Afya na Kinga ya Jamii.
Frank Mvungi-Maelezo

Serikali  ya Awamu ya Tano imepongezwa kwa kuimarisha na kuendeleza miundo mbinu ya Afya,uboreshaji huduma kupitia teknolojia  na Usambazaji wa madawa  hadi kwenye vituo vya kutolea huduma.

Kauli hiyo imetolewa Leo Jijini Dar  es Salaam na Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Bi Anna Makinda wakati akifungua Kongomano  la kwanza la bima ya afya na kinga ya jamii .

“’Lazima tuangalie na kuwatambua wale ambao hawawezi kulipia huduma za afya na tuangalie namna gani tutahakikisha wanapata huduma na isitokee wakati wowote wengine wakpoteza maisha kwa kukosa fedha za kujiunga na Bima ya Afya.’’ Alisisitiza Makinda.

Akifafanua Makinda amesema kuwa kuna umuhimu wa kuangalia namna huduma zinavyotolewa katika vituo vya kutolea huduma,upataikanaji wa vifaa tiba na dawa,hali inayochochea upatikanaji wa huduma bora kwakuwa ndiyo dhamira ya Serikali kupitia mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Kuhusu Afya bora kwa wote Makinda alibainisha kuwa azma hiyo itafikiwa kupitia utaratibu wa Bima ya Afya na na mpango wa CHF iliyoboreshwa katika Halmashauri 50 hapa nchini.

Akizungumzia mkakati wa kutoa huduma bora Makinda amesema kuwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umejipanga kuhakikisha kuwa huduma zinazotolewa na watoa huduma zinaendana na dhamira ya Serikali kuhakikisha kuwa kila mtanzania anapata huduma bora za afya .

Aliongeza kuwa watoa huduma watakao toa lugha zisizofaa kwa wagonjwa,kuwanyanyapaa, kuonyesha tabia ya ukatili watafungiwa kutoa huduma kama kituo hicho kimesajiliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Kwa Upande wake Kamishna wa Mamlaka ya Udhibiti wa Bima nchini Dkt.Baghayo Saqware  amesema kuwa kuna umuhimu wa kuwa na Sera ya Taifa ya Bima itakayowezesha wananchi huduma bora za Afya.

“Sera ya Taifa ya Bima tasaidiakuondoa tatizo la watoa huduma za Bima wasio waaminifu “ alisisitiza Dkt.Saqware.

Tanzania kama nchi imekuwa na historia ndefu ya kutoa huduma bora za matibabu kupitia bima ya Afya,Kuanzishwa kwa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na Bima Binafsi zikiwa ni juhudi za kuboresha huduma hizo hapa nchini.

Kongamano la Bima ya Afya na Kinga limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Bima Nchini (TIRA) na shirika la Pharm Access International.

SERIKALI KUBORESHA BARABARA ZA MAJIJI: WAZIRI MKUU

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ina mkakati wa kufanya yote nchini yawe na barabara za viwango vya kimataifa na zinazopitika kwa urahisi.

“Tumeanza kujenga barabara za kisasa katika jiji la Arusha ambalo ni jiji la utalii, tutakwenda Mwanza na Dar es Salaam kwa kujenga barabara zenue njia za juu (flyovers) zikiwemo za magari na za waenda kwa miguu,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo mchana (Alhamisi, Mei 4, 2017) wakati akizumngumza na wananchi wa Tengeru, wilayani Arumeru, mkoani Arusha mara baada ya kukagua barabara ya Sakina-Tengeru yenye urefu wa km. 14.1 ambayo itakuwa na njia nne za magari.

“Nimekuja kukagua ujenzi wa barabara hii ya Sakina hadi Tengeru lakini mkandarasi akimaliza anajenga barabara nyingine ya kilometa 42.1 na hivyo hapa Arusha tutakuwa na kilometa 56.5 za awamu ya kwanza,” alisema.

Alisema maboresho ya barabara za Jiji la Arusha yanafanyika ili kuwezesha wafanyabiashara kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi na viwanda vitakapoanza kujengwa, itakuwa hawana shida ya mawasiliano.

Akizungumzia tatizo la uhaba wa ardhi aambalo lililibuliwa na mbunge wa Arumeru Mashariki, Bw. Joshua Nassari, Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw, Mrisho Gambo aendelee na zoezi la kuuzungukia mkoa wake ili kubaini maeneo yenye matatizo sugu.

Mapema, akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara hiyo kwa Waziri Mkuu, Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Arusha, Eng. Mgeni Mwanga alisema ujenzi wa barabara hiyo ambao ulianza Juni 2015, unatarajia kukamilika Juni 2018.

“Ujenzi wa barara ya Sakina –Tengeru ni wa awamu ya kwanza ya ujenzi wa barabara yenye urefu wa km. 230 ya kutoka Arusha –Holili- Taveta –Voi ambayo ujenzi wake unatarajiwa kugharimu sh. bilioni 139.34. Ujenzi huo unagharimiwa na Serikali ya Tanzania pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).

Sambamba na barabara hiyo, Eng. Mwanga alisema mkandarasi wa barabara hiyo ataanza kujenga barabara nyingine ya km. 42.1 inayoanzaia Usa River hadi Kisongo kwa kiwango cha lami ambayo itakuwa na madaraja saba wakati ile ya Sakina hadi Tengeru ina madaraja makubwa mawili.

Naye mbunge wa Arumeru Mashariki, Bw. Joshua Nassari alisems uhaba wa ardhi bado ni tatizo kubwa kwenye wilaya hiyo kiasi kwamba hawana hata eneo la kujenga shule au zahanati.

“Maeneo yote yameuzwa na wenyeviti wa vijiji na madiwani, hivi sasa ukitaka kujenga shule au zahanati hakuna eneo hata moja. Mheshimiwa Waziri Mkuu tunaomba utusaidie kufuatilia suala hilo licha ya kuwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi alishakuja na kuelezwa hali halisi ilivyo,” alisema.

DASANI MARATHON KUFANYIKA MEI 14,2017 JIJINI DAR

$
0
0
 Kampuni ya Coco- Cola Kwanza kupitia Maji ya Dasani imedhamini mashindano ya riadha marathon ‘Dasani Marathon’ itakayofanyika Mei 14 jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Coca –Cola Kwanza , Nalaka Hattiachchi , amesema kampuni imedhamini mbio hizo ili kuweza kuchochea riadhaa nchini.

Amesema kuwa wanariadhaa wanaotakiwa kushiriki mbio za Kilomita 10 na 21 na tayari usajili umeanza kufanyika kwa kuwa washiriki 1000.
Rais wa Dar Running Club, Goodluck Elvis amesema mbio hizo zilianza miaka mitatu iliyopita na zimeendelea kwa kuibua wanariadha wengi ambao baadaye wanaweza kuleta historia ya nchi kama ilivyokuwa.

Mshindi wa Dasani Maradho wa kwanza atapata sh. Milioni mbili na wa pili atapata sh.700000 na zawadi mbalimbali zitatolewa na washiriki wanatakiwa kujisajili kwa sh.30000 kulipa kwa M-pesa 243388.
Vituo vya kujiandikisha Colosseum Gym, Masaki,Shoppers Supermarket , Mikocheni na Mlimani City.

Mwanariadha Mkongwe Juma Ikangaa amesema kuwa watu wakiwa tayari kwa kujitoa katika kushiriki riadhaa wanaweza kuwa na rekodi katika dunia.Amesema kinachotakiwa katika ushiriki ni kujiandaa na kuwa na tamaa ya kupata ushindi bila kufanya hivyo riadha itakuwa jina kwa Tanzania.
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Coca Cola Kwanza , Nalaka Hattiachchi akizungumza na waandishi habari juu ya udhamini kampuni hiyo katika Dasani maradhoni, kushoto ni Rais Dar Running Club , Goodluck Elvis Kulia Mwanariadha Mkongwe , Jumaa Ikangaa.
 
 

MAVUNDE:VIJANA MILIONI 4 KUNUFAIKA NA MAFUNZO YA VITENDO

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde amesema Vijana zaidi ya Milioni Nne nchini watafikiwa na programu ya mafunzo kwa Vitendo ili waweze kuhimili ushindani pindi wanapohitimu vyuo.

Mavunde amesema hayo leo alipokuwa akizindua programu ya mafunzo kwa vitendo iliyoandaliwa na Chama cha Waajiri nchini (ATE) kwa kushirikiana na Shirika la kazi Duniani (ILO) Kanda ya Afrika Mashariki.

“Kwenye program hii ya miaka mitano tunakwenda kuwafikia vijana Milioni Nne nchini ambapo katika mwaka huu wa fedha 2017/2018 vijana 27,000 watapewa mafunzo kwa vitendo” amesema Mavunde.

Waziri Mavunde amewashukuru ATE kwa kuungana na serikali katika kusaidia vijana wa kitanzania kuingia katika mpango huo ambao unaondoa pingamizi la kuwataka vijana kuwa na uzoefu hili waajiriwe katika taasisi mbalimbali.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa ATE , Almas Maige amesema mpango huo utawasaidia waajiri kupata wafanyakazi ambao wataweza kuwasaidia kwa uzalishaji bila ya kuchukua muda mrefu kujifunza.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Anthony Mavunde akizungumza katika uzinduzi wa mpango wa mafunzo kwa vitendo kutoka Kwa Chama Cha Waajiri nchini ATE kwa kushulikiana na Shirika la Kazi Duniani ILO leojijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Anthony Mavunde akionyesha Vitabu vya programu vya mafunzo kwa vitendo mara baada ya kuzindua programu hiyo katika ukumbi wa Hyatt Kempiski leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Anthony Mavunde akikata utepe kuashiria uzinduzi wa programu ya mafunzo kwa vitendo kutoka kwa Chama cha Waajiri nchini ATE, Kulia kwake ni Mwenyekiti wa ATE nchini , Almas Maige(MB) akishuhudia uzinduzi huo leo jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Anthony Mavunde akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa uzinduzi wa programu ya mafunzo kwa Vitendo kwa Vijana .

Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images