Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110105 articles
Browse latest View live

MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL 26,2017


NAIBU WAZIRI MHE ANASTAZIA WAMBURA AKIFAFANUA KUHUSU UKARABATI WA VIWANJA VYA MPIRA WA MIGUU NCHINI.

HALI YA USALAMA KIBITI SASA NI SHWARI, VYOMBO VYA DOLA VYAENDELEA NA KAZI - RC NDIKILO

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani

MWENYEKITI wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo, amewahakikishia wananchi kuwa hali ya usalama wilaya ya Kibiti na Rufiji ipo shwari. Aidha amesema jeshi la polisi linaendelea na oparesheni mbalimbali za kuwasaka wahalifu wanaochafua mkoa na taifa.

Aliyasema hayo, kufuatia habari zinazoendelea kusemwa na kuandikwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuhusu mambo yanayoendelea kwenye wilaya hizo. Mhandisi Ndikilo, aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa polisi waliopo kwenye oparesheni hiyo na kuacha kukimbia miji yao kama wanajiamini sio wahalifu.

"Kumekua na taarifa zinazoendelea kuandikwa suala ambalo mkoa haujawahi kutoa taarifa zaidi ya tukio la mauaji ya vifo nane iliyotokea april 13 na kukemea usafiri wa pikipiki ifikapo saa 12 jioni " alisema. Alibainisha kwamba, endapo kutakuwa na tukio ama jambo litakalojitokeza serikali ya mkoa, wilaya, jeshi la polisi litatolea ufafanuzi.

Mwenyekiti huyo wa kamati ya ulinzi na usalama ambae pia ni mkuu wa mkoa huo, alieleza, kuwa sasa vyombo vya dola vinawasaka watu waliojihusisha na mauaji ya wenyeviti wa vijiji, vitongoji na polisi . "Jeshi la polisi ama serikali haiwezi kumwonea mtu yoyote kwani inafanywa kwa kuzingatia sheria"alisema.

Mhandisi Ndikilo alisema jeshi la polisi linafanya kazi yake kwa weledi na kazi yake kubwa ni kulinda amani ya wananchi na mali zao. “Nawaombeni wananchi msiwe na hofu juu ya operesheni hiyo na hakuna haja ya kukimbia makazi yao kwani kuna taarifa kuwa kuna watu wamehama kwenye nyumba zao na kukimbia,” alisema Ndikilo.

Alisema kuwa watu wanaokimbia wanatia mashaka, hawana sababu ya kukimbia nyumba zao na familia zao kwani wanaotafutwa ni wahalifu na si raia wema. Mhandisi Ndikilo, alisema wananchi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola ili viweze kufanya kazi zake ipasavyo.

Aliwatoa hofu watu wote wanaofanya shughuli zao kwenye wilaya hizo kutokuwa na wasiwasi kwani ulinzi umeimarishwa .

FATILIA HAPA MOJA KWA MOJA SHEREHE YA MIAKA 53 YA MUUNGANO MJINI DODOMA LEO

MSAMAHA WA RAIS KWA WAFUNGWA KATIKA KUADHIMISHA MIAKA 53 YA MUUNGANO WA TANZANIA

$
0
0
Katika kuadhimisha Miaka 53 ya Muungano wa Tanzania tarehe 26 Aprili, 2017 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa msamaha kwa wafungwa wafuatao:-

Wafungwa wote ambao baada ya punguzo la kawaida la moja ya tatu (1/3) linalotolewa chini ya Kifungu 49(1) cha Sheria ya Magereza Sura ya 58, wawe wametumikia nusu (½) ya vifungo vyao vilivyobaki, isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika Ibara ya 2(i – xxi).

Wafungwa wagonjwa wenye magonjwa kama UKIMWI, Kifua kikuu (TB) na Saratani (Cancer) ambao wako kwenye “terminal stage”. Wafungwa hawa wathibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.

Wafungwa wazee wenye umri wa miaka sabini (70) au zaidi. Umri huo uthibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.

Wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani, pamoja na wale walioingia na watoto wanaonyonya na wasionyonya.

Wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili (Physical disability and mental disability). Ulemavu huo uthibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Msamaha huu wa Mheshimiwa Rais hautawahusu wafungwa wafuatao:-

Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa.
Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa na adhabu hiyo kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au kifungo gerezani.

MACHIMBO YA KITUNDA YASIMAMISHWA KWA MUDA MKUU WA MKOA WA TABORA ILI KUEPUKA MAAFA ZAIDI

$
0
0
Na Tiganya Vincent, RS-Tabora

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo amesimamisha kwa muda uchimbaji wa madini aina ya dhahabu katika machimbo ya Kitunda wilayani Sikonge ili kuepusha maafa zaidi yasije yakatokea.

Hatua hiyo inafuatia maafa yaliyokea hivi karibuni ambapo wachimbaji wadogo wadogo sita walifariki baada ya kufukiwa na kifusi na mmoja kufariki kwa kukosa hewa wakati wa uchimbaji wa dhahabu katika eneo la Kitunda wilayani Sikonge.

Uamuzi huo umetolewa jana wilayani Sikonge na Mkuu wa Mkoa wa Tabaora Bw, Mwanri baada ya yeye na kwa kushirikiana na Kamati na Ulinzi na Usalama mkoani humo kutembelea machimbo yalisababisha maafa hayo kwa ajili ya kujionea na kasha kuwapa pole wafiwa.

Alisema kuwa yeye na Kamati yake wameona ni vema wasimamishe kwa muda ili taratibu zote za kuhakikisha usalama na zile Baraza la Taifa la Mazingira za mpango wa ulinzi wa mazingira(Environmental Protection Plan) zinafuatwa kabla ya kendelea na shughuli za uchimbaji.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa lengo ni kutaka Wachimbaji hao waendele kuchimba katika hali ya usalama bila kuharatisha maisha yao na nguvu kazi ya Taifa.

Kufuatia hatua hiyo , Bw. Mwanri aliwaagiza Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kati na Magharibi Salim Salim na Afisa Madini Mkazi wa Tabora Laurent Mayala kuhakisha kuwa umbali kutoka shimo moja la uchimbaji hadi jingine unazingati matakwa ya Sheria na Kanuni kuliko ilivyo sasa ambapo kutoka shimo hadi shimo ni mita 3 hali ambayo ni hatari.

DC GONDWE AZINDUA CHANJO YA POLIO WILAYANI HANDENI,AWATAKA WANANCHI KUTILIA MKAZO

$
0
0
Wananchi Wilayani Handeni wametakiwa kutilia mkazo suala la kuwapeleka watoto kupata chanjo mara zinapotangazwa ili kuendana na msemo wa kinga ni bora kuliko tiba.

Rai hiyo ilitolewa wakati wa uzinduzi wa wiki ya chanjo ya polio wenye kauli mbiu ya “jamii iliyochanjwa ni jamii yenye afya” uliofanyika katika Zahanati ya Mumbwi iliyopo Katika Kijiji cha Mumbwi kata ya Komkonga.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe mbaye pia alikuwa mgeni rasmi alieleza kuwa Serikali inajitahidi kutoa chanjo bure hivyo wananchi pia wanao wajibu wa kuhakikisha wanapeleka watoto wao kupata chanjo hizo kwaajili ya ustawi wa afya za watoto.

“Halmashauri ya Wilaya ya Handeni inazo chanjo za kutosha, chanjo mkoba na chanjo tembezi zitafika kwenye maeneo ambayo bado hayana zahanati ili kuhakikisha watoto wote Wilayani Handeni wanachanjwa” alisema Mh. Gondwe.

Aidha , aliwataka Maafisa Tarafa, Watendaji Kata na Vijiji kuweka agenda ya usafi na mazingira, afya na bima kuwa ndelevu katika viko vyao vya Vijiji.Akizungumzia suala la malaria kwenye siku ya maadhimisho ya siku ya malaria duniani Mh. Gondwe alisema kila mwanachi anawajibu wa kutunza mazingira na kutokomeza mazalia ya mbu ili kutokomeza kabisa ugonjwa huo.

“Chanjo zinatolewa bure,vipimo vya malaria vinatolewa bure na baadhi ya dawa za malaria bure lakini ni vyema kila mwananchi kuwa na bima ya afya ili kuepuka gharama za matibabu na kuhakikisha kuwa suala la afya haliwi tatizo kwenye Wilaya ya Handeni”alisema Mh.Gondwe.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh Godwin Gondwe akizindua zoezi la utoaji chanjo Kwa watoto kwa kumpatia mtoto matone ya chanjo ya polio.

Mh Godwin Gondwe akiwa kwenye picha ya pamoja na walezi wahakikishe watoto aliowapatia chanjo huku akiwa amembeba mtoto ikramu mbarouk Mara baada ya kutoa chanjo Kwa watoto wao.
Viongozi mbalalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wakiongozwa na mkuu wa Wilaya Mh Godwin Gondwe wakiwa wamebeba watoto waliopatiwa chanjo
Baadhi ya wazazi waliojitokeza kuleta watoto wao kupatiwa chanjo.

DC KISHAPU AWATAKA MAOFISA UGANI KUHAKIKISHA WANAFIKA KWA WAKULIMA NA KUWAFUNDISHA MBINU BORA ZA KILIMO.

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Nyabaganga Taraba amewaagiza maofisa ugani wa kata zote kuhakikisha wanawafikia wakulima na kuwafundisha mbinu bora za kilimo chenye tija.

Ameagiza pia wananchi kulima mazao yanayostahimili ukame hususan mtama na uwele badala ya kuwa na kasumba ya kung’ang’ania kilimo cha mahindi ambacho katika sehemu kubwa ya wilaya hakifanyi vizuri.

Taraba alitoa agizo hilo wakati wa ziara yake kwenye mashamba ya mtama katika kata za Uchunga, Mwaweja na Ukenyenge kujionea na kufanya tathmini ya kilimo wilayani humo.

Aliwataka maofisa hao kujiwekea utamaduni wa kutembelea mashamba ili kuwafundisha namna ya matumizi ya mbegu bora kwani wengi wao hupanda bila utaalamu.

Aliwataka kusimamia Sheria ndogo ya mwaka 2008 ya Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu inasisitiza kuwa kila kaya wilayani humo iweze kulima ekari mbili za mazao yanayostahili ukame ambayo ni mtama.

Mkuu wa wilaya hiyo alisema kuwa hata hivyo wakulima wengi wilayani humo wameweza kutekeleza sheria ndogo hiyo lakini wamepata changamoto mbalimbali zikiwemo ukosefu wa maarifa ya matumizi ya aina sahihi za mbegu.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba akionesha masuke ya zao la mtama wakati akikagua mojawapo ya mashamba ya wakulima wa Kata ya Mwaweja wakati wa ziara yake.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba (wa pili kulia) akibadilishana mawazo na mkulima, Sendama Luhende, Ofisa Kilimo, Sarai Pura na mkulima Mariam Nkinga wakati wakikagua shamba.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu akiendelea kukagua shamba la mtama katika Kata ya Mwaweja..


BALOZI WA KUWAIT NCHINI MHE.JASEM AL-NAJEM AENDELIEA KUUNGA MKONO SHULE YA SEKONDARI YA TOLIDO

$
0
0
Ubalozi wa Kuwait unaendelea kuiunga mkono Shule ya Sekondari ya Tolido iliyopo Tanga kwa kuipatia idara ya shule hiyo mashine ya kutoa kopi(photocopy machine) iliyopokelewa na msimamizi wa Shule Bi, Basilisa Soka.

Mashine hiyo inatarajiwa kuisaidia Shule na kurahisisha kazi za idara kwa ajili ya kuinua kiwango cha elimu.

Itakumbukwa kuwa Balozi wa Kuwait nchini Mhe.Jasem Al-Najem alizindua kisima cha maji katika shule hiyo mwishoni mwa mwaka jana 2016 ambapo mradi wa ujenzi wake ulifadhiliwa na Msamaria mwema raia wa Kuwait na kutekelezwa na Asasi ya Direct Aid-ofisi ya Tanga, kisima hicho ndio cha kwanza kuzinduliwa tangu ubalozi wa Kuwait kuzindua mpango wake wa 'Kisima cha maji kwa kila Shule'.

Idadi ya visima ambavyo tayari vimezinduliwa ndani ya mpango huo vimefikia visima 27 katika shule mbalimbali katika kipindi cha miezi minne tu.

Ubalozi wa Kuwait utaendela kuisaidia Shule ya Tolido ya Sekondari mjini Tanga na shule nyingine Tanzania ili kuunga mkono mchakato wa elimu nchini.

KIKOSI KAZI CHA KUNUSURU MTO RUAHA CHATEMBELEA SKIMU YA MWENDAMTITU- MBALARI.

$
0
0
Kikosi cha Kitaifa cha kunusuru Ikolojia ya Mto Ruaha kilichoundwa na Makamu wa Rais wa Tanzania kilichoko Mkoani Mbeya, kimeeendelea na ziara yake kwa kutembelea skimu ya Mwendamtitu iliyopo wilayani Mbarali. Katika ziara hiyo Kikosi kazi kiligundua jinsi ambavyo miundombinu ya skimu hiyo inavyopoteza maji ambayo yalitakiwa kuingia Mto Ruaha. 

Aidha pia kimegundua kuwa skimu hiyo imeanzishwa pasipo kufuata sheria za umwagiliaji kwani haina kibali cha umwagiliaji wala kibali cha matumizi ya maji yanayoingia katika mfereji wa skimu hiyo.

Wakiongea katika ziara hiyo Wajumbe wamesikitishwa an kitendo cha skimu hiyo cha kutumia maji mengi pasipo kuwa na kibali chochote wala pasipo kuwa na miundombinu ya mifereji inayowezesha maji kurudi mto Ruaha mKuu.” Katika skimu hii Maji yanatitririka bure na kwa aina hii ya umwagiliaji kamwe mto Ruaha Mkuu hautapata maji, ila tutachukua hatua stahiki” aliongea Mjumbe Injinia Seth Luswema.

Kwa upande wa wananchi wa eneo hilo wameiomba Serikali iwasaidie kuwapatia elimu jinsi ya kuendesha skimu hiyo na pia kuelekezwa jinsi ya kuweka miundombinu rafiki kwa ajili ya kuokoa kiasi cha maji kinachopotea. Wamesema wao hawana elimu yoyote na hawajui kama wanakosea kwa jinsi wanavyoendesha skimu hiyo.

Kikosi hiko bado kipo Mkoani Mbeaya katika wilaya ya Mbalari kwa ajili y akuzungukia na kukagua maeneo mbalimbali amabayo yanachangia maji kutokwenda Mto Ruaha Mkuu.
Mjumbe wa Kikosi kazi Injinia Seth Luswema (wa kwanza kushoto), akiwa meza kuu pamoja na Viongozi wa Chama kwa wilaya ya Mbalari, Kuanzia kushoto ni Mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi, uchumi na maliasili, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, Katibu wa CCM wilaya na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Mbalari.
Wajumbe wa Kikosi kazi cha Kitaifa cha kunusuru ikolojia ya mto Ruaha, wakipata maelekezo toka kwa Katibu wa skimu ya umwagiliaji ya Mwendomtitu akielekeza juu ya wanavyotumia maji ya umwagiliaji ya Mto Ruaha kumwagilizia mashamba ya mpunga.
shamba la vitunguu lililoko karibu na kianziao cha maji cha askimu cha mwendamtitu wilayani Mbalari likionekana kushamiri kwa sabau ya maji ya kusukuma na pampu wanayotoa mto Ruaha.
Wajumbe wa Kikosi kazi wakisikiliza maoni ya Wananchi wa kata ya Mwendamtitu walipotembelea skimu yao ya umwagiliaji.


RC NCHIMBI ABAINISHA KUSHINDWA KUMPATIA CHANJO MTOTO NI UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU

$
0
0
Wazazi wanaoshindwa kuwapeleka watoto kupata huduma za chanjo wanakiuka haki za binadamu hasa haki ya kuishi na pia wanaenda kinyume na juhudi za serikali za kupambana na maradhi, umaskini na ujinga.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amesea hayo katika hotuba yake iliyosomwa na Mwakilishi wake Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo wakati wa uzinduzi wa wiki ya chanjo uliofanyika mapema leo katika hospitali ya Sokoine Manispaa ya Singida.

Dkt. Nchimbi amesema watoto wote wenye umri wa chini ya miaka mitano wanapaswa kupata chanjo zote ili kuwakinga na magonjwa ya homa ya ini, surua, nimonia, kuhara, kifua kikuu, na pepopunda ambayo yanazuilika kwa chanjo na motto akiugua kupona ni nadra

“Mtoto akiumwa magonjwa hayo kwa kukosa chanjo kupona ni majaliwa na akipona anaweza kupata ulemavu wa kudumu, hivyo nawasisitiza msipuuze mzingatie kukamilisha chanjo zote” amesisita

Ameongeza kuwa serikali imekamilisha wajibu wake kwa kuhakikisha chanjo zote zinapatikana na hivyo umebaki wajibu wa kila mzazi na mlezi kuhakikisha motto anapata chanjo pamoja na kuwaelimisha na kuwafichua wale wasiowapeleka watoto kupata chanjo.
Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo akitoa chanjo kwa mtoto wa umri wa siku nne ikiwa ni uzinduzi wa wiki ya chanjo Mkoani Singida mapema leo katika hospitali ya Sokoine manispaa ya Singida.
Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo akifurahi mara baada ya kutoa chanjo kwa mtoto wa umri wa siku nne ikiwa ni uzinduzi wa wiki ya chanjo Mkoani Singida mapema leo katika hospitali ya Sokoine manispaa ya Singida.
Baadhi ya wazazi wakiwa na watoto wao waliojitokeza katika hospitali ya Sokoine Manispaa ya Singida wakishiriki uzinduzi wa wiki ya chanjo Mkoani Singida.

RAS –TABORA AWATAKA WACHIMBAJI MADINI WA KITUNDA KUJIKINGA NA VVU

$
0
0
Na Tiganya Vincent, RS-Tabora

Katibu Tawala Mkoa wa Tabora(RAS) Dkt. Thea Ntara amewataka Wachimbaji Wadogo wadogo waliopo eneo la Kitunda wilayani Sikonge kuzingatia matumizi mipira ya kufanyia mapenzi(condom) wanapoamua kufanya hivyo ili kujikinga na maambukizi yanayowekusababishia kupata Virusi vya UKIMWI.

Hatua hiyo itasaidia waweze kuendelea kuwa na afya nzuri itakayowasaidia kuishi maisha mengi na kukatiza ndogo zao.
Dkt. Ntara alitoa kauli hiyo jana wilayani Sikonge wakati akitoa pole kuifuatia Maafa ya wachimbaji Saba wa madini katika eneo la Kitunda ambapo sita walikufa kwa kufukiwa na kifusi na mmoja alikufa kwa kukosa hewa.

Alisema kuwa umati wa wachimbaji ulipo katika eneoi hilo ni zaidi ya elfu kumi, hivyo ni vema wakatumia mipira kujikinga na UKIMWI wakati wakifanya mapenzi ili uwepo dhahabu hapo usije ukasababisha tatizo lingine katika jamii hiyo na ile inayowazunguka.

Dkt. Ntara alisema kuwa wachimbaji wengi katika eneo hilo bado wanaumri mdogo hivyo ni vema wakalinda afya zaidi ili wasiweze kutumbukia katika matatizo yatakayokazi maisha yao na kupoteza nguvu kazi ya Taifa ambayo bado inahitajika sana kwa maendeleo ya nchi hii.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MAONESHO YA WIKI YA USALAMA NA AFYA KAZINI 2017 MKOANI KILIMANJARO

$
0
0
Maonesho ya wiki ya usalama na afya kazini yameanza leo siku ya Jumatano tarehe 26/04/2017 katika viwanja vya Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo taasisi mbalimbali za serikali na binafsi zimepata fursa ya kuonyesha namna zinavyozingatia masuala ya usalama na afya kazini kwa wafanyakazi wao. 

Miongoni mwa taasisi zilizopata fursa ya kushiriki maonyesho hayo kwa mwaka huu ni pamoja na kampuni za uchimbaji wa madini za Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara ambazo zinamilikiwa na kampuni ya uchimbaji ya Acacia.

Ambapo katika maonesho hayo migodi hiyo ya imekuwa ikionesha vifaa mbalimbali vya uokozi pamoja pamoja na mbinu zitumikazo kuhakikisha mazingira ya usalama kwa wafanyakazi wao wawapo kazini.

Maadhimisho ya mwaka huu ya siku ya afya na usalama mahali pa kazi yameandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) yakiwa na kauli mbiu ya “ Ongeza wigo wa ukusanyaji na utumiaji wa takwimu za usalama na afya” .Maadhimisho hayo yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 28,2017.
Mkaguzi wa Mitambo Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kanda ya Kaskazini Boysafi Sabato akifurahia jambo baada ya kufika katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Afisa Mazingira mgodi wa Bulyanhulu Florence Nyuki akimwelezea Mkaguzi wa Mitambo Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kanda ya Kaskazini Boysafi Sabato namna mgodi huo unavyotunza mazingira na kuhakikisha usalama unakuwepo katika maeneo yao ya kazi
Afisa viwango vya usalama mgodi wa Bulyanhulu Setieli Kimaro akitoa elimu kuhusu mambo ya usalama mgodini kwa wananchi waliotembelea banda la la mgodi wa Bulyanhulu.

SPIKA WA BUNGE AKAGUA VIKOSI VYA TIMU YA BUNGE LA JMT NA TIMU YA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR

$
0
0

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (wa pili kulia) wakati akikagua kikosi cha timu ya netball ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya timu ya netball ya Bunge la Wawakilishi Zanzibar, katika mchezo uliochezwa leo katika uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma. 
Mchezaji wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwenye jezi ya rangi ya bluu bahari, akifunga goli dhidi ya timu ya Bunge la Wawakilishi Zanzibar, katika mchezo wa netball uliochezwa leo katika uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma. 
Wachezaji wa timu ya netball ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (jezi ya rangi ya bluu bahari), wakipambana na wachezaji wa Bunge la Wawakilishi Zanzibar (jezi orange), katika mchezo wa netball uliochezwa leo katika uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma. 

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 26.04.2017


MAGAZETI YA LEO ALHAMIS APRIL 27,2017

RC GAMBO AZINDUA BARABARA ARUSHA,AKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO , SAMBAMBA NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI KUSIKILIZA KERO ZAO

$
0
0

Na.Vero Ignatus ,Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amtembelea na kujionea mradi wa darasa la watoto wenye ulemavu katika shule ya msingi Meru iliyopo Jijini hapa. 

Akiwa katika shule hiyo yenye jumla ya wanafunzi 68 miongoni mwao wasichana wakiwa 34 na wavulana 28 huku walimu viziwi wakiwa wawili na mtaalam mmoja wa kitengo cha I. C. T, Gambo alijionea mwenyewe jinsi wanafunzi hao wanavyofanya kazi kwa kutumia teknolojia hiyo. 

Akisoma risala mbele ya Mkuu huyo wa mkoa mwalimu Musa Lwambano alisema shule hiyo unajumla ya walimu 42 ambapo walimu 15 ni wa kitengo na 27 wa shule ya kawaida huku idadi ya wanafunzi ikiwa ni 1,384 wavulana wakiwa ni 709 na wasichana wakiwa ni 675

Amesema shule hiyo inawafadhili kutoka nchi ya Finland walioshirikiana na Halmashauri ya Jiji la Arusha lililotoa Sh, milioni 20 na wafadhili wakichangia zaidi ya sh, milioni 180 huku fedha hiyo ikisaidia kujenga jengo bora la ICT na kununua vifaa kama kompyuta mpakato (laptop) 184,deskitopu 5,Projekta 6,Sola 14,Scana Kamera 4,Ipad 22, Mashine ya Laminationi na printa 4.

Pia vijana viziwi wanne wamepata ajira katika kitengo hicho hukuwakimshukuru Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia kwa kuwawezesha kupata maendeleo hayo shuleni hapo

Gambo alimpongeza walimu na wanafunzi wa shule hiyo kwa kutoa elimu kwa wanafunzi wenye ulemavu na kuwasihi walimu kuongeza juhudi za kutoa elimu kwa wanafunzi hao ili waweze kupata ajira na kujikwamua kiuchumi 

Awali Rc Gambo alijionea jinsi wanafunzi hao viziwi wakiimba wimbo wa Taifa kwa kutumia alama zao wakiongozwa na walimu wao ambao ni Veola Wilson na Neema Lema 
Gambo anaendelea na ziara yake ya siku tano Jiji hapa kwa kuzindua miradi mbalimbali ikiwemo uzinduzi wa barabara ya Mahakama na St, James uliogharimu Sh milioni 586. pamoja na kuzungumza na wananchi ili kutatua kero zao

Gambo amewaagiza watumishi wa jiji la Arusha wakiwemo wataalam wa vitengo mbalimbali kuhakikisha wanatatua kero za wananchi haraka iwezekanavyo ili kuondokana na kero zinazowakabili.

Miradi iliyokaguliwa ni pamoja na Visima viwili vya maji vilivyoko magereza vilivyogharimu milioni 372, madarasa 6 Shule ya msingi Olasity,madarasa 4 ya Shule ya msingi Burka Estate ambayo yamegaharimu jumla ya shilingi 218 milioni .
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gamboa akiwa ameshika mkasi ishara ya kukata utepe katika uzunduzi wa barabara ya St.James na Mahakamani jana Jijini Arusha,Kulia kwake ni mkuu wa wilaya ya Arusha mjini Gabriel Daqarro.Picha na Vero Ignatus Blog.
Watoto wenye ulemavu kutoka shule ya msingi Meru wakiimba wimbo wa Taifa kama picha hapo juu inavyoonekana wakiongozwa na mwalimu Neema Lema ,na hii inayofuata hapa chini wakiongozwa na mtafsiri na mwalimu Viola Wilson .Picha na Vero Ignatus Blog
Mkuu wa Mkoa wa Arusha akiangalia kwa makini kile ambacho mtoto mwenye ulemavu Amina kutoka shule ya msingi Meru akitumia kompyuta katika kuhariri video aliyoichagua,aliyeshika kipazasauti ni mtaalam wa masomo ya Tehama katika kitengo cha walemavu bi.Betha Denis.Picha na Vero Ignatus Blog.

WAZIRI WA SHERIA PROFESA KABUDI AZIDI KUMWAGA CHECHE BUNGENI

JPM:KILA MTANZANIA ALINDE NA KUIMARISHA MUUNGANO

$
0
0

Kila mtanzania ametakiwa kuhakikisha anafanya jitihada za kuimarisha na kulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa miaka 53 iliyopita.

Akizungumza leo wakati akihutubia wananchi katika sherehe za Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano katika uwanja wa Jamhuri uliopo mjini Dodoma, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alisema kuwa ni muhimu watanzania wakalinda Muungano kwa vile una manufaa kwa nchi zote mbili.

“Kila mtanzania ahakikishe anafanya jitihada za kuimarisha na kulinda Muungano wetu, kwa vile Muungano na amani iliyopo nchini ndio chachu ya maendeleo yetu” alisema Rais Magufuli.

Rais Magufuli alisisitiza kuwa “Muungano ndio silaha yetu, ni nguvu yetu, mimi na mwenzangu Dkt. Shein tutaulinda Muungano kwa nguvu zote na yeyote atakayejaribu kuuvunja atavunjika yeye” alisema Rais Magufuli

Akitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika miaka 53 ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar ni pamoja na kuunganisha mataifa mawili na kuunda taifa moja lenye nguvu.

Rais Magufuli alitaja mafanikio mengine ni pamoja na kuwa ni kuimarisha miundombinu ya usafiri wa anga, majini, nchi kavu na reli, kukabiliana na matatizo ya umaskini, ukosefu wa ajira na kukua kwa uhusiano wa diplomasia kati ya Tanzania na mataifa mbalimbali ambapo yamepelekea mafanikio katika nyanja za kiuchumi, kisiasa, na jamii.

Aidha, hii ni mara ya kwanza kwa sherehe za Maadhimisho ya Muungano kufanyika mkoani Dodoma ambapo, Rais Magufuli alisema kuwa Serikali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali za kujenga miundombinu ili kufikia azma yake ya kuhamishia makao yake makuu mjini Dodoma ifikapo mwaka 2020.

“Niwahakikishie wana Dodoma na Watanzania kwa ujumla kwamba Serikali sasa tumefika Dodoma na hatutarudi nyuma tena,ambapo awamu ya kwanza ya watumishi wa Serikali takribani 3,000 kwa ngazi za Mawaziri,Naibu Waziri,Makatibu wakuu na Manaibu Katibu wakuu wameshahamia Dodoma, kama tulivyoahidi kufikia mwaka 2020, Serikali yote itakuwa imehamia hapa”, alisisitiza Rais Magufuli.

Sherehe za Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano zenye kauli mbiu isemayo “Miaka 53 ya Muungano, tuulinde na kuimarisha, tupige vita dawa za kulevya na kufanyakazi kwa bidii”, zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wajane wa viongozi waasisi wa Muungano ambapo ni Mama Maria Nyerere na Mama Shadya Karume.

APPRECIATION

$
0
0
 BELOVED MAMA EUPHRACIA HIPOLITE MATAFU
12/09/1940 – 17/04/2017


We lost a Wonderful woman, mother, sister, aunt, grandmother and a friend who can never be replaced.  During these days and weeks following Her passing away, we have been blessed with the loving embrace of our Family and Friends.  

It is during these difficult times that we see how lucky we are to have been blessed with a loving family, wonderful and caring friends - there are no words that seem adequate enough to say thank you to every one of you.  

We offer our prayers and GOD’s Blessings to each one of you.  Special thanks go to Dr. Fatma of Aga Khan Hospital in Dar es Salaam; Dr. Urassa in Arusha; Doctors and Nurses of Mount Meru Hospital, Arusha; Dr. Mary of St Laurent Diabetic Clinic; Dar es Salaam; Father Temu of Holy Spirit Parish Ngarenaro, Arusha; Jumuiya ya Mt. Yohani Mtume Ngarenaro, High Court of Tanzania; Christian Social Services Commission (CSSC); Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation (EGPAF), QUEENS VICOBA Group; T80 UDSM Group of Engineers; Jumuiya ya Mt. Maximillian Kolbe of Mikocheni; City Trust Real Estate and Debt Collectors Ltd of Arusha; Jitegemee Group Class of 1999, Neighbors and Friends.

Thank you very much for all your sympathy, it is greatly appreciated.

GOD BLESS YOU ALL

Viewing all 110105 articles
Browse latest View live




Latest Images