Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110017 articles
Browse latest View live

Makamu wa Rais Mgeni Rasmi Kongamano la Kimataifa la Jinsia

$
0
0

Na Husna Saidi-MAELEZO

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano la Kimataifa la Jinsia na Usawa Katika Jamii lililoandaliwa na Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Aprili 27 mpaka 28 mwaka huu chuoni hapo.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Afisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Chuo hicho Lila Mandu alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu lengo la kongamano hilo.

Mandu alisema lengo kuu la kongamano hilo ni kuchunguza kwa kina masuala mbalimbali ya kijinsia pamoja na kubaini mbinu bora za kuondoa ukosefu wa usawa wa jinsia katika muktadha wa Taasisi za Elimu ya Juu.

“Tutatathmini sababu na changamoto zinazosababisha ukosefu wa usawa wa kijinsia katika Taasisi za Elimu ya Juu kwa kutumia mifano mizuri kutoka Taasisi zingine ambazo zinajitahidi kuhamasisha usawa na haki za wanawake na wanaume pia,” alisema Mandu.

Aliendelea kwa kusema kuwa kongamano hilo litabainisha fursa za kimkakati katika kuwahusisha wadau wa masuala ya jinsia katika kuhamasisha usawa na haki za watu wote ambapo litakuwa na washiriki 140.

Aliwataja washiriki hao kuwa ni wasomi kutoka DUCE, Taasisi na vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi, wanafunzi wa shahada za uzamili na uzamivu katika masuala ya jinsia, wawakilishi wa mashirika ya haki za binadamu, watunga sera pamoja na wasomi wanaotambulika Kimataifa katika masuala ya jinsia.

Kwa upande wake, Mratibu Kitengo cha Jinsia DUCE Fatma Hamad alisema licha ya maovu wanayotendewa wanawake kuendelea kujitokeza hapa nchini, kongamano hilo litasaidia kutoa elimu ya jinsia na usawa ili kusaidia Serikali na wananchi kwa ujumla kuondokana na hadha hiyo.

Chuo cha DUCE pamoja na waandaaji wa kongamano hilo wamealika wadau mbalimbali wa masuala ya jinsia, wasomi, waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla kushiriki katika kongamano hilo.

MSAJILI VYAMA VYA SIASA ALAANI VURUGU ZILIZOTOKEA KATIKA MKUTANO WA CUF NA WAANDISHI WA HABARI

ELIMU YA KODI NI MUHIMU KWA KILA MMOJA WETU - MHE. SAMIA SULUHU HASSAN

YANGA YAWAPA KONGOLE WACHEZAJI, YAZINDUA MCHAKATO WA WANACHAMA KUCHANGIA TIMU

$
0
0


Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa akizungumza na waandishi wa habari.

Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii

UONGOZI wa klabu ya Yanga umetoa pongezi kwa wachezaji wa timu hiyo kwa kuweza kutinga hatua ya nusu fainali kombe la ASFC baada ya kuibanjua Tanzania Prisons goli 3-0 mchezo uliopigwa jumamosi katika dimba la Taifa. 

Yanga imefanikiwa kuingia hatua hiyo na tayari amegusia maandalizi ya timu kuelekea mchezo wa nusu fainali ASFC tarehe 30 April dhidi ya Mbao FC jijini Mwanza . 

Droo ya nusu fainali ASFC ilifanyika jana jioni . Mabingwa hawa watetezi Yanga SC watawavaa Mbao FC na Simba SC watakwaana na Azam FC uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam tarehe 29 April 2017.

Katibu Mkuu Charles Boniface Mkwasa amesema kuwa wanaheshimu uwezo wa Mbao na wao wanajipanga vyema kupata ushindi katika uwanja wa Kirumba . Benchi la ufundi baada ya droo ya jana na kujua mpinzani wetu ni nani , tayari wameanza mazoezi kujiandaa na mchezo huo .

Katika mkutano huo na waandishi wa habari, Mkwasa ametumia mkutano huo kueleza hatua ambayo klabu imechukua katika kuongeza mapato ya klabu hiyo kutokana na kulegalega kwa hali ya uchumi klabuni hapo . 

Hatua iliyochukuliwa ni kufungua akaunti maalumu ambayo itawapa fursa wapenzi , wanachama, mashabiki na wadau wa timu hiyo kuichangia fedha klabu yao ili kuipa nguvu ya misuli ya kiuchumi. 

"ni ombi la wanachama wenyewe kujitolewa kuichangia timu yao na sisi kama uongozi tumeona ni jambo lenye tija . Hii haina tafsiri ya kwamba klabu haina fedha na imekwama kabisa kujiendesha bali tumelipitisha ili kukidhi matakwa ya wengi," alisema Mkwasa. 

Mkwasa alisema kuwa anafahamu wote wanaokuja uwanjani au kulipia kadi kama sehemu ya kuongeza mapato ya klabu lakini kwa mfumo huu ambao tunaenda kuuzindua utatoa fursa kwa kila mdau popote alipo kuichangia klabu kama sehemu ya kujivunia timu hii na kusimama kama nguzo muhimu ya maendeleo ya klabu.


UJUMBE WA KAMPUNI YA “ENGINEERING CUNSULTANTS GROUPS”-ECG

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akisalimiana na mgeni wake Mwenyekiti wa Kampuni ya “Engineering Consultants Groups”-ECG Bw.Amr Hassan Allouba alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo na ujumbe wake .
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akizungumza na mgeni wake Mwenyekiti wa Kampuni ya “Engineering Consultants Groups”-ECG Bw.Amr Hassan Allouba yaliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akifuatana na Mwenyekiti wa Kampuni ya “Engineering Consultants Groups”-ECG Bw.Amr Hassan Allouba (katikati) baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo,(kushoto) Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Misri Balozi Mohamed Haji Hamza.
Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abdulyahaya Mzee (kushoto) alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari wa Vyombo mbali mbali kuhusu Ripoti ya mkaguzi na Mdhibiti wa fedha za Serikali iliyozungumzia upotevu wa fedha katika Mawizara mbali mbali ambazo zimekuwa zikilipwa kwa makosa,katika ukumbi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.]24/04/2017.

Rais Magufuli amteua Prof. Chibunda kuwa Makamu Mkuu wa Chuo SUA, Awasili Dodoma

WATATU WASHIKILIWA KWA KOSA LA UVAMIZI WA MKUTANO WA CUF JUZI.

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii. 

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu watano kwa tuhuma za kushiriki tukio la uvamizi wa Mkutano wa wanachama wa CUF uliofanyika Vinna Hotel Mabibo, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 

Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam Simon Sirro amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa Habari jijini hapa. Amesema kuwa. Aprili 22 mwaka huu majira ya mchana, walipokea taarifa ya kuwa watu wasiofahamika wakiwa na silaha walivamia mkutano huo na kujeruhi baadhi ya watu. 

Kamanda Sirro ameongeza kuwa, mpaka sasa watuhumiwa watatu waliokamatwa wanaendelea kuhojiwa na upelelezi utakapokamilika hatua za kisheria zitafuatwa juu yao na amewasihi watu kutii sheria bila shuruti kwani hakuna mtu au kikundi chochote cha watu wanaoweza kuwa na mamlaka ya kushambulia wengine. 

"Kama unamalalamiko pitia polisi, au mahakamani siyo kuvamia kundi la watu wengine kama wako juu ya sheria, tunafuatilia wale wote waliohusika katika kufanya shambulio hilo na mtu mmoja aliyejeruhiwa sana anataja watu walioshambulia" amesema Sirro. 

Kamanda Sirro, amesema jeshi la polisi linaamini kuwa watu waliofanya uvamizi huo walifanya kwa utashi wao wenyewe na kwamba pindi upelelezi ukikamilika watachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kupelekwa mahakamani. 

Aidha amewaonya baadhi ya viongozi wa CUF waliotangaza kuwafuata watu fulani na kuwawajibisha ni vema wakumbuke kuwa hakuna mtu aliyeko juu ya sheria kwani hakuna mtu aliyeko juu ya mamlaka. 

Mapema wiki iliyopita, watu wasiojulikana wakiwa na bastola walivamia mkutano wa wanachama wa CUF ambao wanamuunga mkono, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad na kuwapiga wanachama wa CUF pamoja na waandishi wa habari ambao walikuwepo eneo hilo. 

Mkutano huo ambao ulikuwa na lengo la kumtambulisha Katibu Mkuu wa CUF , ulivurugika baada ya vurugu kubwa zinazodaiwa kufanywa na wanachama wa CUf ambao wanamuunga mkono Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba. 

katika vurugu hizo, Mtu mmoja ambaye bado hajafahamika jina lake miongoni mwa waliovamia mkutano wa wanachama wa CUF ameshambuliwa na wananchi wakati akijaribu kutoroka.
Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio la uvamizi wa Mkutano wa wanachama wa CUF uliotokea mwishoni mwa wiki hii. 

KIGAMBONI YAONGEZA WIKI MOJA YA UUZAJI WA VIWANJA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 

 MKURUGENZI Mtendaji wa Manispaa ya Kigamboni,Stephen Katemba amesema kuwa mji wa kigamboni utajengwa kwa kisasa na kuwataka wananchi kwenda kup[ata viwanja vilivyopimwa.

 Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake, Katemba amesema kuwa walitangaza utoaji wa fomu za wananchi wanaotaka viwanja katika mji wa Kigamboni kuanzia ni Aprili 18 hadi 25 mwaka huu na utoaji wa fomu hizo unaendelea hadi Mei 2 pamoja na siku zote huduma zitatolewa bila kujali mapumziko na siku kuu. 

 Katemba amesema wameanza katika viwanja 6000 kwa awamu ya kwanza na wataendelea na awamu zingime lengo ni kutaka mji huo kuwa wa kisasa kuliko mji mingine iliyoo katika jiji la Dar es Salaam. 

 Amesema viwanja hivyo viko katika maeneo ya Kisarawe, Somangila, Ukooni ambapo wananchi watakao kuwa na viwanja hivyo watapata hati na malipo yake yanatakiwa ndani ya miezi miwili baada ya kurudisha fomu hizo. Aidha amesema wale wote watakaorudisha fomu hizo na kulipa ni uhakika kupata viwanja hivyo hakuna utapeli katika viwanja vya Kigamboni. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Kigamboni, Stephen Katemba akizungumza na waandishi habari (hawapo pichani)juu ya Uuzaji wa viwanja katika Mji wa Kigamboni leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Kigamboni, Stephen Katemba akionyesha Ramani kwa waandishi habari maeneo ambayo viwanja vinauzwa katika awamu ya kwanza leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Kigamboni, Stephen Katemba akitoa maelekezo kwa wananchi waliofika katika kupata huduma za viwanja leo jijini Dar es Salaam.

SADC ORGAN TROIKA MINISTERIAL ASSESSMENT FOLLOW UP MISSION 19 TH -22 ND APRIL 2017KINSHASA, DRC

$
0
0
The Chairperson of the Organ on Politics, Defence and Security Cooperation, H.E. Dr. John Pombe Joseph Magufuli, President of the United Republic of Tanzania, deployed a follow-up Mission of the Ministerial Committee of the Organ Troika (MCO-T) to the Democratic Republic of Congo (DRC) from the 19thto 22ndApril 2017, to assess the current political and security situation in the country, including the implementation of the 31 December 2016 Episcopal Council of Catholic Bishops (CENCO) mediated Agreement.

The mission was within the mandate received from the Extraordinary Summit held in Lozitha, Swaziland on 17 April 2017, whereby Summit had “mandated the Organ Ministerial Troika to immediately conduct a follow-up mission to the DRC, on a date to be agreed upon in consultation with the Chairperson of the Organ and Government of the DRC”.  The Summit directive is also in line with the Organ Ministerial Troika’s (OMT) recommendation arising from its previous mission to the DRC undertaken from 10-13 October 2016, which underscored the need to carry out “follow up assessment missions and to lend support to the political, security and the electoral processes in the DRC”. 

Hon. Dr. Augustine P. Mahiga, Minister of Foreign Affairs and East African Cooperation of the United Republic of Tanzania and Chairperson of the Ministerial Committee of the Organ (MCO), led the mission, accompanied by Hon. Manuel Augusto, Deputy Minister of External Relations of the Republic of Angola and Deputy Chairperson of the MCO, and Hon. Nyeleti Mondlane, Deputy Minister of Foreign Affairs and International Cooperation of the Republic of Mozambique, supported by the SADC Secretariat led by Mr. Jorge Cardoso, Director of the Organ on Politics, Defence and Security Affairs, representing the Executive Secretary of SADC. SADCAmbassadors accredited to the DRC were also part of the mission.

The Missionconsulted with various stakeholders, including Hon. Leonard She Okitundu, Vice Prime Minister and Minister for Foreign Affairs and Regional Integration of DRC; the CENCO; representatives of other Religious Groups; the representatives of the Presidential Majority and opposition political partiesincluding the three splinter groups of the Rassemblement; representatives of the Civil Society; the National Independent Electoral Commission (CENI); and MONUSCO. The mission further engaged with the EU Ambassador to the DRC, accompanied by representatives from EU countries.
The mission paid courtesy calls on Prime Minister SamyBadibanga and Prime Minister designate Bruno Tshibala, respectively, and concluded its visit with a meeting and briefing with H.E. Joseph Kabila Kabange, President of the DRC.
Following consultations and exchange of views with the various stakeholders, the Organ Troika Ministerial Mission: 

1.welcomed the efforts of the President of the DRC to push forward the political process, inspite of the obstacles encountered in the implementation of the Political Agreement and, in particular, the Special Arrangements;
2.noted with concern that the demise of the leader of the Opposition, Etienne Tshisekediwa Mulumba, has complicated the implementation of the Special Arrangements and resulted into a political procrastination in the appointment of the Chairperson of the National Monitoring Committee (NMC) and, to some extent, the appointment of the Prime Minister;
3.urged all political stakeholders to support the establishment of a government of national unity, which will encompass inclusiveness,national unity and reconciliation; 
4.encouraged the Government of the DRC to prioritize socio-economic programmes in order to improve the livelihood conditions of the Congolese people; 
5.condemned the escalation of violence and insecurity in the Kasai Provinces perpetrated bythe KamwinaNsapu militia group, and encouraged the Government to strengthen the capacity and presence of local state institutions and urged all stakeholders to refrain from actions that would undermine the political and security stability;

6.noted that there is ample consensus on the need for the conduct of peaceful, credible and transparent elections in order for the country to enter into a new political and democratic dispensation;

7.commended the efforts by CENI in registering close to 23 millionvoters out of an estimated 45 million, andurged all relevant stakeholders to continue supporting the CENI in the preparation of the electoral process;
8.re-affirmed SADC’s support to the ongoing implementation process of the December 31st 2016 Political Agreements and called upon all stakeholders to finalize the implementation of the Special Arrangements, in line with the Constitutional Provisions; and,

9.called upon the international community and all relevant stakeholders to continue supporting the implementation of the 31 December 2016 Agreement and respecting the wishes of the Congolese people with a view to ensure the sustainable peace, security and stability of the DRC.


Done in Kinshasa, Democratic Republic of Congo
23rdApril 2017

MICHUZI TV: POLISI KANDA MAALUM YAZUNGUMZIA TUKIO LILILOTOKEA KATIKA MKUTANO WA CUF NA WAANDISHI WA HABARI JIJINI DAR

WAZIRI SIMBACHAWENE AZINDUA TAWI LA DCB MKOA WA DODOMA LEO

$
0
0
Waziri wa Nchi ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. George Simbachawene (MB) ameipongeza benki ya DCB kwa hatua kubwa waliyofikia ya  kwa kuwa miongoni mwa benki zilizoanzisha huduma zinazoendana na teknolojia ya kisasa kama ilivyo kwa huduma za kibenki kwa njia ya mawakala (DCB Jirani) na huduma za kibenki kwa njia ya simu za mkononi (DCB Pesa).

Simbachawene amesema kufunguliwa kwa tawi hili zitasogeza huduma za kibenki karibu na wafanyabishara na wakazi wa mji wa Dodoma na haya ndiyo maendeleo tunayotaka katika sekta ya kibenki ili huduma za benki zipatikane kwa urahisi zaidi kwa wananchi na nina hakika wananchi wengi watapata huduma bora kupitia tawi hili. 

Hivyo nawaasa wafanyabiashara, wafanyakazi na wakazi wote wa mkoani Dodoma watumie fursa hii kwa kufungua akaunti mbalimbali za DCB kupitia tawi hili, ni imani yangu kwamba huduma zitakozotolewa na tawi hili zitakuwa bora na zenye kumjali mteja.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB Edmund Mkwawa ametoa shukrani za dhati kwa Mhe. George Simbachawene, Waziri wa TAMISEMI kwa kukubali kuwa Mgeni rasmi katika hafla hii ikiwa ni mara yako ya pili kukubali wito kuwa mgeni rasmi. Mara ya kwanza ilikuwa ni kuzindua rasmi tawi la Benjamini Mkapa lililopo maeneo ya Samora karibu na ofisi za Halmshauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Mkwawa amesema kwa upande wa Dodoma wamefanikiwa kupata mawakala 38 ambao muda si mrefu wataanza kutoa huduma za DCB mitaa ya Dodoma karibu zaidi na wananchi. Mbali na hapa Dodoma, pia wana mpango wa kupeleka huduma za DCB mikoa mingine kupitia DCB Jirani kama vile mikoa ya Pwani, Morogoro, Tanga, Mwanza, Geita, Shinyanga, Kahama, Mtwara, Arusha, Iringa na Mbeya lengo ni kuwa na mawakala 1,500 nchi nzima kufikia Disemba mwaka huu. 

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya DCB Prof . Lucian Msambichaka  ametoa wito kwa wakazi wote wa Dodoma na vitongoji jirani wazipokee huduma za DCB na wawe mstari wa mbele kutumia huduma za benki tawini hapo ili kukuza tawi hili na kuwa na uwezo mkubwa wa kuwahudumia wananchi wengi zaidi katika suala zima la kupiga vita umasikini. 
Prof Msambichaka ameongezea na kusema wana imani wengi watanufaika na benki hii kwa kujenga utamaduni wa kujiwekea akiba mara kwa mara, kuimarisha usalama wa fedha zenu na kujenga uwezo wa kupanua biashara kwa kutegemea. Huduma hizi zina lengo la kusogeza huduma za kibenki karibu zaidi na wananchi na kuongeza amana za benki ambazo ndio uti wa mgongo wa benki zote duniani.
Mgeni rasmi Waziri wa Nchi ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. George Simbachawene (MB) akizundua tawi la Benki ya DCB mkoa wa Dodoma akishuhudiwa na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania John Malecela(Kulia) Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB Edmund Mkwawa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya DCB Prof . Lucian Msambichaka .

Mgeni rasmi Waziri wa Nchi ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. George Simbachawene (MB) akizungumza kabla ya uzinduzi wa tawi jipya la Benki ya DCB mkoa Dodoma na kuwapongeza kwa hatia kubwa waliyofikia ya kuendelea kutanua huduma zao nje ya Mkoa wa Dar es salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB Edmund Mkwawa (kushoto) akisalimiana na Mgeni rasmi Waziri wa Nchi ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. George Simbachawene (MB) wakati akiwasili jengo la LAPF Mkoa wa Dodoma wakati wa uzinduzi wa tawi la DCB mkoani humo. Katikati ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya DCB Prof . Lucian Msambichaka

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Balozi Asha Rose Migiro ampongeza Mwanariadha Alphonse Simbu

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha - Rose Migiro leo aliandaa hafla fupi katika makazi ya Balozi kumpongeza kijana mtanzania Alphonse Simbu alieshika nafasi ya tano katika mbio za "London Marathon" zilizofanyika tarehe 23 Aprili 2017 jijini London.

Katika salamu zake, Balozi Migiro alimpongeza Bw. Simbu kwa heshima aliyoipa Tanzania jijini London na Duniani  kupitia mbio za London. alimsihi atumie matokeo hayo kama hamasa ya  kufanya bidii zaidi kwa ajili ya mashindano ya mbio ndefu anayotarajiwa kushiriki baadae mwakani.

Simbu alimshukuru Balozi Migiro Kwa ushirikiano mkubwa wa kibalozi alioupata akiwa jijini London.Alimkabidhi Balozi Fulana ya kumbukumbu ya ushiriki wake kwenye mbio hizo.
Pichani Balozi Asha Rose Migiro akipokea Fulana hiyo.

MICHUZI TV: WAZIRI MKUU AFUNGUA KONGAMANO KUHUSU MMONYOKO WA MAADILI, AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUHIMIZA NIDHAMU KWA WAUMINI WAO

$
0
0



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya, Nchini, Rogers Siyanga akizungumza katika Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na kufunguliwa na Waziri Mkuu, kassim Majliwa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017.
Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Alhaji Abubakary Zuberi akizungumza katika Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na kufunguliwa na Waziri Mkuu, kassim Majliwa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017.
Naibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Selemani Jafo akizungumza katika Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na kufunguliwa na Waziri Mkuu, kassim Majliwa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya, Nchini, Rogers Siyanga baada ya Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), na kufanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Alhaji Abubakary Zuberi baada ya Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), na kufanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017.

RAIS DKT. MAGUFULI AWASILI MKOANI DODOMA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRIL 25,2016


WABUNGE WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WATINGA UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON, DC

$
0
0

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo siku ya Jumatatu April 24, 2017 wametembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na kukutana na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Wilson Masilingi. Katika picha toka kushoto ni Mkuu wa Utawala na Fedha Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Bi. Swahiba Mdeme,Mwambata wa Jeshi Ubalozi wa Tanzania na Canada Col. Adolph Mutta, Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Bajeti Mhe. Hawa A. Ghasia, Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Wilson Masilingi, Mbunge Mhe. Janeth Z. Mbene, Mhe. Josephat S. Kandege, Afisa wa Ubalozi Bwn. Dismas Assenga na Afisa wa Bunge Bwn. Godfrey Godwin. Wabunge hao wa Bunge la Jamhuri ya Muungano waTanzania walikuja Washington, DC kuhudhuria mikutano ya kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Wilson Masilingi. Katika picha toka kushoto ni Afisa wa Bunge Bwn. Godfrey Godwin, Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Bajeti Mhe. Hawa A. Ghasia, Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Wilson Masilingi, Mbunge Mhe. Janeth Z. Mbene, na Mhe. Josephat S. Kandege

TAKUKURU MKOA WA RUVUMA WAOKOA FEDHA ZA MIRADI MBALIMBALI

$
0
0
Ofisi ya kupambana na rushwa mkoa wa Ruvuma TAKUKURU kwa kipindi cha miezi tisa toka julai 2016 hadi marchi mwaka huu imeokoa fedha kiasi cha shilingi 91,811,768.91 zilizokuwa zimetolewa katika miradi mbalimbali,iliyokuwa inaviashiria vya ubadhirifu habari kamili hiyo hapa chini

JARIDA LA MTANDAONI LA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI (NIT) APRILI-JUNI 2017.

MAHAKAMA KUU TANGA YAJIPANGA KUMALIZA KESI

$
0
0
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga
Mhe. Imani Abood Muonekano wa majengo ya Mahakama Kuu
kanda ya Tanga baada ya kukamilika kwa ukarabati
Na Lydia Churi- Mahakama

Mahakama ya Tanzania kupitia Mpango Mkakati wake wa miaka mitano (2015/16-2019/2020) pamoja na Mradi wa Maboresho ya huduma za Mahakama, imepania kuhakikisha kuwa kesi zote za zamani pamoja na zile zinazosajiliwa zinamalizika ili wananchi waweze kuwa na kujenga imani zaidi na chombo hicho muhimu cha utoaji wa haki nchini. Katika kulitekeleza hili, ipo mikakati iliyowekwa na Mahakama kwa ujumla na ile inayowekwa na kila Kanda ya Mahakama Kuu nchini.

Mikakati ya Mahakama ni pamoja na Majaji na Mahakimu kupangiwa idadi ya kesi watakazotakiwa kuzisikiliza na kuzimaliza katika kipindi cha mwaka mmoja. Kila Jaji amepangiwa kumaliza kesi 220 kwa mwaka na kila hakimu anatakiwa kusikiliza kesi 250 kwa mwaka. Mkakati mwingine wa jumla ni kiwango cha muda kilichopangwa kwa kesi kukaa Mahakamani, mathalani, Mahakama ya Tanzania imepanga kuwa kesi zote zilizosajiliwa Mahakama Kuu zisikae Mahakama kwa muda unaozidi miaka miwili wakati katika Mahakama za Hakimu Mkazi pamoja na zile za wilaya imeamuliwa kesi isizidi miezi 12 Mahakamani. Kesi katika Mahakama za Mwanzo inatakiwa kumalizika katika kipindi cha miezi sita.

Aidha, Mahakama imeanzisha utaratibu wa kufanya vikao na wadau wake ili kujadili namna ya kumaliza kesi kwa wakati kama moja ya mikakati yake ya kuhakikisha kesi zote za zamani zinamalizika Mahakama na pia kesi zinazosajiliwa zinamalizika kwa wakati ili kutimiza wajibu wake wa kikatiba wa kuwapatia wananchi wa Tanzania Haki sawa na kwa wakati.

Pamoja na kuwepo kwa mikakati ya Mahakama ya kumaliza kesi zilizoko Mahakamani, Mahakama Kuu kanda ya Tanga nayo imejiwekea mikakati yake ili kuhakikisha inaenda sambamba na kasi ya Mhimili huo ya  kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa wakati kwa kumaliza kesi zao kwa wakati.

Akizungumzia suala la kumalizika kwa kesi kwa wakati, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu kanda ya Tanga Mheshimiwa Imani Abood alisema kanda yake imepanga kuwanunulia Mahakimu wake wote (68) kompyuta Mpakato (Laptops) zitakazowasaidia katika kurahisisha kazi zao na kuondosha mashauri kwa wakati katika Mahakama mbambali za mkoa wa Tanga. Alisema lengo ni kuhakikisha Mlundikano wa kesi zilizopo Mahakamani unaisha na pia kesi zinazosajiliwa zinamalizika kwa wakati.

Jaji Mfawidhi alifafanua kuwa kompyuta hizo zitawasaidia waheshimiwa Mahakimu katika kuandika hukumu ili wananchi waweze kupati haki kwa wakati. Aliongeza kuwa hivi sasa Mahakimu wa mahakama za Mwanzo huandika hukumu kwa kalamu na baadaye hukumu hizo hupelekwa kwenye mahakama za wilaya ambapo kuna umeme kwa ajili ya kuchapwa na baadaye hurudishwa kwenye kwenye Mahakama za Mwanzo.

Alisema pia kanda yake inakabiliwa na uhaba wa watumishi hasa Makatibu Muhtasi pamoja na vitendea kazi jambo ambalo limekuwa likichelewesha utolewaji wa hukumu pamoja na upatikanaji wa nakala za hukumu kwa wakati. Aliongeza kuwa kwa Mahakimu kupatiwa kompyuta hizo kutarahisisha upatikanaji wa haki.
Pamoja na kuwapatia Mahakimu Kompyuta, Jaji Abood alisema Mahakama Kuu Kanda ya Tanga inao mpango wa kuhakikisha inazipatia umeme baadhi ya Mahakama za Mwanzo kupitia Mradi wa Umeme vijijini (REA) ili kurahisisha upatikanaji wa nakala za hukumu kwa wakati. Na hivi sasa tayari Mahakama za Mwanzo tano zimeshapatiwa umeme.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

SIMBA YAIFUATA DAWA YA KUIA AZAM JUMAMOSI KOMBE LA FA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

KIKOSI cha timu ya Simba kimeendelea kujifua kwa nguvu wakijiandaa na mchezo wa nusu fainali dhidi ya Azam utakaofanyika mwishini mwa wiki hii.

Jumamosi ya April 29, ni nusu fainali ya kwanza ya kombe la Shirikisho la Azam HD baina ya Simba na Azam itakaopigwa katika dimba la Uwanja wa Taifa.

Kwa sasa Simba wapo Morogoro wakijiandaa na mchezo huo ambapo chini ya Kocha Joseph Omog na Jackson Mayanja kimeamua kujichimbia huko kwa ajili ya kuwapa muda wa kupumzika wachezaji wake na kuwapa mbinu mpya mbalimbali.

Hii inakuwa ni mechi ya ushindani mkubwa sana kwa timu hizi mbili zikikutana kwa mara ya tatu ndani ya msimu mmoja ambapo katika michezo miwili ya awali ila mmoja akishinda mchezo mmoja.

Kwa mujibu wa Kiongozi wa Simba, Abbas Ally amesema kuwa wachezaji wana ari kubwa sana na wako vizuri na wanaamini watapigana mpaka mwisho ili kupata ushindi kwenye mchezo huo.

"Huu ni mchezo muhimu sana kwetu, ni muhimu kupata ushindi  ili tuweze kuingia fainali ya kombe la Shirikisho na wachezaji wana ari kubwa sana ya ushindi na wameahidi kupambana mpaka mwisho,"amesema Ally.

Mpaka sasa Kikosi cha Simba kinakabiliwa na majeruhi wawili ambao wanatarajiwa kuukosa mcheoz huo ambao ni Hamad Juma na Jamal Mnyate.
Wachezaji wa Simba wakiwa katika mazoezi ya pamoja kulekekea mchezo wao wa nusu fainali ya kombe la Shirikisho la Azam HD siku ya Jumamosi dhidi ya Azam.



 Golikipa Peter Manyika akiwa katika mazoezi  kulekekea mchezo wao wa nusu fainali ya kombe la Shirikisho la Azam HD siku ya Jumamosi dhidi ya Azam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 110017 articles
Browse latest View live




Latest Images