Introducing Njenje Official Video by Nillan
↧
↧
PROFESA MWANDOSYA AENDELEA KUTANGAZA KIVUTIO CHA UTALII CHA MATEMA BEACH WILAYANI KYELA MKOA WA MBEYA
Waziri mstaafu Profesa Mark Mwandosya akiwa ameamka alfajiri na mapema ili kufanya mazoezi na kuzunguka katika ziwa Nyasa hususan kwenye fukwe maarufu na mwanana za Matema wilayani Kyela mkoani Mbeya. Fukwe hizo ni mojawapo ya vivutio vikubwa vya utalii kwa kuwa na mandhari ya kupendeza, samaki wa kila aina pamoja na utengenezaji wa vyungu, magudulia na mitungi vya udongo. Profesa Mwandosya ameiambia Globu ya Jamii kwa njia ya mtandao kwamba Matema Beach pia ni location nzuri sana kwa watengeneza filamu za muziki, tamthiliya na kadhalika.
Waziri mstaafu Profesa Mark Mwandosya akiwa anafurahia Matema Beach
Waziri mstaafu Profesa Mark Mwandosya akiwa anafurahia Matema Beach ndani ya mtumbwi unaoteleza juu ya maji tulivu na masafi ya Ziwa Nyasa.
↧
MAKABURI 22 YA WATU WENYE UALBINO YAFUKULIWA TANZANIA...TAS YAMUOMBA JPM KUFANYA KAMA DAWA ZA KULEVYA NA VIROBA
Na Kareny Masasy- Malunde1 blog
Inaelezwa kuwa tangu kuibuka kwa mauaji ya watu wenye ualbino mwaka 2007 takribani makaburi 22 nchini Tanzania yamefukuliwa na watu wasiojulikana.
Chama hicho kimeiomba serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na rais John Pombe Magufuli kuweka mkazo katika mapambano dhidi ya ukatili wa watu wenye ulemavu wa ngozi kama ilivyoonesha nguvu za kutosha katika vita ya dawa za kulevya na pombe aina ya viroba.
Akizungumza juzi kwenye kikao cha viongozi wa chama watu wenye ualbino kutoka mikoa ya kanda ya Ziwa ambayo ni Mara,Mwanza na Shinyanga na wanachama wengine Afisa mahusiano na habari TAS taifa Josephat Torner vitendo vya kufua makaburi ya watu wenye ualbino yanatishia amani yao
Torner alisema wanaiomba serikali kuelekeza nguvu katika masuala ya mauaji na ufukuaji wa makaburi ili kuwafanya watu wenye ualbino waishi kwa amani ndani ya nchi yao.
Katikati ni Afisa mahusiano na habari wa chama cha watu wenye ualbino nchini Tanzania (TAS )Josephat Torner akizungumza wakati wa kikao cha viongozi na wanachama wa chama hicho ambapo walilaani vitendo vya ufukuaji wa makaburi ya watu wenye ualbino.Kulia ni Mwenyekiti TAS mkoa wa Mara Joseph Sinda,kushoto ni mwenyekiti TAS mkoa wa MwanzaAlfred Kapole
Baadhi ya wanachama wa chama cha watu wenye ualbino nchini Tanzania wakiwa katika kikao hicho. Picha na Suzy Butondo-Malunde1 blog.
↧
KAMATI YA BUNGE ARDHI MALIASILI NA MAZINGIRA YAKAGUA MRADI WA KUWEZESHA UMILIKISHAJI WA ARDHI (LTSP)
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh Angelina Mabulla Akifafanua namna Fomu ya Umiliki Ardhi inavyo tumika ili kupata taarifa za awali za Mwananchi anaye andaliwa Hati ya Kumiliki Ardhi mbele ya Wajumbe wa kamati ya Bunge Ardhi Maliasili na Mazingira na Wananchikatika kijiji cha Mikoleko Wilaya ya Kilombero- Morogoro
Mratibu wa Mradi wa Kuwezesha Umilikishaji wa Ardhi Godfrey Machabe akisoma Ripoti ya maendeleo ya mradi huo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Mazingira wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya Mradi huo Wilayani Kilombero-Morogoro
Mwenyekiti wa kijiji cha Mikoleko Wilaya ya kilombero akielezea ushiriki wa Wanakijiji katika zoezi la kumilikisha ardhi ndani ya kijiji hicho Mbele ya Wajumbe wa kamati ya Bunge Ardhi, Maliasili na Mazingira.
↧
ZIWA JIPE NA BWAWA LA NYUMBA YA MUNGU HATARINI KUTOWEKA
Na Lulu Mussa
Mwanga - Kilimanjaro
Imebainika kuwa Ziwa Jipe liko hatarini kutoweka endapo hatua za haraka hazitachukuliwa katika kulinusuru. Hayo yamesemwa na Waziri mwenye dhamana ya usimamizi wa Mazingira Mh. January Makamba alipofanya ziara ya kukagua ziwa hilo ambalo sehemu kubwa imezungukwa na magugu maji.
Waziri Makamba amesema kuwa ziwa hilo ni rasilimali muhimu na hivyo ni lazima kuwe na mpango wa muda mfupi na ule wa muda mrefu. Kupitia Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamiza wa Mazingira (NEMC) ameazimia kutangaza kupita Tangazo la Serikali kuwa eneo hilo ni eneo nyeti kimazingira."Tutatanga eneo hili kuwa eneo nyeti kimazingira na tutaweka masharti ya matumizi katika eneo hili" Alisisitiza Makamba
Azimio hilo la kutangaza kuwa eneo mahsusi ama nyeti kimazingira itasaidi katika kuandika maandiko mbalimbali ya miradi na kupata fedha kutoka kwa wadau na washirika wa maendeleo. Pia litawekwa chini ya uangalizi maalumu na kuweka masharti ya matumizi bora ya eneo hilo. " Tutaweka masharti makali na magumu zaidi ili watakao kiuka wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria" Aliongezea Waziri Makamba.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akizungumza na Mtendaji wa Kijiji cha Butu, Kata ya Jipe Wilayani Mwanga Bw. Nassor Abdul wakati Waziri Makamba alipotembelea Ziwa Jipe ambalo limeathiriwa kwa kiasi kikubwa na magugu maji ambayo yanasababisha kupungua kwa shughuli za uvuvi ambazo ndio chanzo kikubwa cha mapato kwa wakazi wa eneo hilo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bw. Aron Mbogho.
Mifano kwa vitendo: Pichani Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akiwa amembeba mtoto Meshack Ombeni katika Kijiji cha Butu pembezoni mwa Ziwa Jipe. Waziri Makamba amewaasa wananchi hao kulinda Ziwa hilo ili liweze kunifaisha vizazi vijavyo na kuwatahadharisha kuwa uharibifu wa mazingira utahatarisha uhai wa ziwa hilo. .
Upungufu mkubwa maji katika bwawa la nyumba ya Mungu. Inasemekana kupungua kwa kina cha maji kunatokana na ukame wa muda mrefu na uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na shughuli za binadamu katika vyanzo vya maji vinavyopeleka maji katika bwawa hilo ukiwemo Mto Kikuletwa. Kwa tarifa kamili BOFYA HAPA
↧
↧
JUST IN: Maafisa sita wa Uhamiaji wapandishwa cheo kuwa Makamishna wa Uhamiaji, wateuliwa kushika nyadhifa mbalimbali
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dr. John Pombe Joseph Magufuli amewapandisha cheo Maafisa sita wa Uhamiaji kuwa Makamishna wa Uhamiaji kuanzia tarehe 28 mwezi Februari mwaka 2017, Wakati huo huo amewateua kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi la Uhamiaji.
Walioteuliwa kushika nyadhifa hizo ni Mrakibu wa Uhamiaji (SI) Edward Peter Chogero kuwa Kamishna wa Divisheni ya Fedha na Utawala, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Samwel Rhobby Magweiga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Udhibiti na Uongozi wa Mipaka, Mrakibu Mwandamizi (SSI) wa Uhamiaji Gerald John Kihinga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Pasipoti na Uraia, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Musanga Mbusuro Etimba kuwa Kamishna wa Divisheni ya Hati za Ukaazi na Pasi, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Hannerole Morgan Manyanga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Sheria.
Aidha Mh.Rais amemteua pia Naibu Kamishna wa Uhamiaji Mourice David Kitinusa kuwa Kamishna Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA). Uteuzi huo unaanzia tarehe 28 mwezi Februari mwaka 2017.
Imetolewa na
Meja Jenerali Projest Rwegasira
Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
26 Machi 2017
↧
NEWS ALERT: RAIS DKT. MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA KATIBU MKUU NISHATI NA MADINI
↧
MAKALA YA SHERIA: MWANAMKE ALIYETELEKEZWA NA MUMEWE AFANYE NINI KISHERIA.
Na Bashir Yakub
Kutelekezwa ni pamoja na kunyimwa huduma za muhimu ambazo kama mke alistahili kupata. Huduma muhimu ni kama chakula, mavazi , makazi, matibabu, hela ya kujikimu kwa matumizi ya kawaida ya mwanamke, pamoja na kila hitaji ambalo kama mwanamke alitakiwa kulipata.
Ifahamike kuwa habari ya kutelekeza inawahusu wote mke na mme kwa maana ya kuwa mme anaweza kumtelekeza mke halikadhalika mke anaweza kumtelekeza mme. Hata hivyo makala yatazungumzia mme kumtelekeza mke ambapo sura ya 29 , Sheria ya ndoa iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 itarejewa.
1.AINA ZA KUTELEKEZA.
( a ) Aina ya kwanza ni kutelekeza ambako mume anaondoka kabisa ndani ya nyumba ambayo alikuwa akiishi na mke wake kama wanandoa na kwenda kuishi kwingine. Haijalishi huko alikoenda panajulikana ni wapi au hapajulikani suala la msingi ni kwamba hayupo katika makazi yake ya kawaida ya familia.
Aidha ikiwa hayupo nyumbani lakini kwa sababu za msingi na za kisheria huko sio kutelekeza. Sababu hizo ni kama kuwa jela, kuwa hospitali, kuwa amehamishiwa sehemu nyingine kwasababu ya matibabu kwa mfano wengine huamishiwa mikoani, na pia kuwa vitani labda baadae mkapoteza mawasiliano na mazingira mengine ya dharula za kibinadamu na ambayo siyo ya makusudi hayawezi kuitwa kutelekeza.
( b ) Aina nyngine ya kutelekeza ni hatua ya kuwa mme na mke wanaishi wote katika nyumba moja au chini ya paa moja lakini mume huyo hajishughulishi na kutoa matumizi au matunzo kwa mke huyo kwa namna yoyote ile. Hajui anakula nini, hajui anavaa nini, hajui anapata vipi matibabu, kwa ufupi hajui lolote zaidi ya kumuona tu kama binadamu wengine ambao anawaona mitaani na hana uhusiano nao.
Pia kuishi chini ya paa moja lakini vyumba tofauti nako ni kutelekeza hata kama mke anapewa matumizi yote yanayostahili. Zaidi, hata kulala chumba kimoja lakini vitanda tofauti kwa muda mrefu tena kwa makusudi kwasababu ya mgogoro wowote nako ni kutelekeza. Lakini pia kulala kitanda kimoja bila kushiriki tendo la ndoa kwa makusudi kwa muda mrefu bila sababu za msingi za kiafya au vinginevyo nako ni kutelekeza.
↧
SPIKA JOB NDUGAI NA WAJUMBE WA KAMATI ZA BUNGE ZA BAJETI NA NISHATI NA MADINI WATEMBELEA BANDARI YA DAR ES SALAAM
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akimpa muhtasari Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai ambaye ameongoza wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge za Nishati na Madini pamoja na Kamati ya Bajeti bandari ya Dar es salaam kujionea makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini iliyokuwa imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali leo Machi 26, 2017
Sehemu ya makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini ambayo imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali
Sehemu ya wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge za Nishati na Madini pamoja na Kamati ya Bajeti wakitembelea bandari ya Dar es salaam kujionea makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini ambayo imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali leo Machi 26, 2017
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akimpa maelezo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai na wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge za Nishati na Madini pamoja na Kamati ya Bajeti bandari ya Dar es salaam juu ya makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini iliyokuwa imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali leo Machi 26, 2017
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiwa na wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge za Nishati na Madini pamoja na Kamati ya Bajeti akiongea na wanahabari katika bandari ya Dar es salaam baada ya kujionea makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini ambayo imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali leo Machi 26, 2017
↧
↧
RAIS DKT MAGUFULI ATAKA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUKAGUA SEKTA YA MADINI
6
↧
PROFESA MUHONGO ASAINI LESENI ZA MADINI
Na Veronica Simba – Dodoma
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesaini leseni za madini kutoka kwa wawekezaji mbalimbali waliowasilisha maombi na kutimiza taratibu zote zinazotakiwa kwa mujibu wa sheria.
Leseni ya kwanza iliyosainiwa ni ya uchimbaji wa kati wa dhahabu katika eneo la Masagalu, Handeni yenye namba ML 570/2016. Leseni hiyo imehamishwa kutoka kwa mmiliki wake wa awali ambaye ni Najim & Company Ltd kwenda kwa Shale Investments Tanzania Ltd.
Aidha, Waziri Muhongo alisaini leseni namba ML 572/2017 ya Sisti Mganga. Leseni hiyo ni ya uchimbaji wa kati wa madini ya ujenzi katika eneo la Itiso, Chamwino mkoani Dodoma.
Leseni nyingine iliyosainiwa na Waziri Muhongo ni ya uchimbaji wa kati wa madini ya ujenzi aina ya kokoto, ambayo mmiliki wake ni Said Abdallah. Leseni hiyo namba ML 573/2017 ipo eneo la Chipite, Masasi.
Profesa Muhongo aliwataka waombaji na wamiliki wote wa leseni za madini nchini, kuhakikisha wanatekeleza ipasavyo taratibu zote kama zilivyobainishwa katika Sheria ya Madini ikiwemo ulipaji wa mrabaha na kodi mbalimbali, kujenga mahusiano mema na jamii zinazowazunguka pamoja na kuzingatia utunzaji na uhifadhi wa mazingira.
Zoezi hilo la utiaji saini lilifanyika hivi karibuni, Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma na kushuhudiwa na wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati na Madini.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akisaini leseni za madini za wawekezaji mbalimbali waliowasilisha maombi na kukamilisha taratibu zote zinazotakiwa. Anayeshuhudia ni Mwanasheria wa Wizara, Khadija Ramadhan.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kutoka kulia), akikabidhi leseni iliyohamishwa kutoka kwa mmiliki wake wa awali Najim & Company Ltd kwenda kwa Shale Investment Tanzania Ltd.
↧
Kiongozi Mkuu wa Madhebu ya Bohora Duniani akamilisha ahadi ya kuleta madaktari wa Moyo nchini katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Madaktari bingwa wa upasuaji wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Saifee ya nchini India wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa moyo . Katika ziara aliyoifanya nchini mwishoni mwaka jana kiongozi Mkuu wa Madheebu ya Bohora Duniani Mtakatifu Dkt. Syedna Aliqadr Mufaddal Saifuddin alimuahidi Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuleta madaktari wa Moyo nchini ambao watashirikiana na Madaktari wa JKCI kufanya upasuaji kwa wagonjwa. Timu ya wataalam hao ambao idadi yao ni sita imeshawasili nchini na tayari wameanza kufanya upasuaji ambao utachukuwa siku tano na wanatarajia kufanya upasuaji wa kuvuna mishipa ya damu mguuni na kuipandikiza katika mishipa ya moyo iliyoziba ( CABG-Coronary Artery Bypass Graft) na upasuaji wa milango miwili hadi mitatu ya moyo ambayo inamatatizo na inahitaji kubadilishwa kwa wagonjwa 15.
Daktari bingwa wa upasuaji wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Evarist Nyawawa (kushoto) kwa kushirikiana na mwenzake wa Hospitali ya Saifee ya nchini India Ali Oscar Behranwala wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa moyo . Katika ziara aliyoifanya nchini mwishoni mwa mwaka jana kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtakatifu Dkt. Syedna Aliqadr Mufaddal Saifuddin alimuahidi Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuleta madaktari wa Moyo nchini ambao watashirikiana na Madaktari wa JKCI kufanya upasuaji kwa wagonjwa. Timu ya wataalam hao ambao idadi yao ni sita imeshawasili nchini na tayari wameanza kufanya upasuaji ambao utachukuwa siku tano na wanatarajia kufanya upasuaji wa kuvuna mishipa ya damu mguuni na kuipandikiza katika mishipa ya moyo iliyoziba ( CABG-Coronary Artery Bypass Graft) na upasuaji wa milango miwili hadi mitatu ya moyo ambayo inamatatizo na inahitaji kubadilishwa kwa wagonjwa 15.
Madaktari bingwa wa upasuaji wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Saifee ya nchini India wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa milango ya moyo ambayo inamatatizo na kuweka milango mingine. Picha na Anna Nkinda – JKCI
↧
NAY WA MITEGO AACHIWA HURU
Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Emmanuel Elibariki maarufu kama Nay wa Mitego, ambaye alikuwa amekamatwa na kushikiliwa na maafisa wa polisi nchini, kuhusiana na wimbo wake wenye jina la "Wapo", ameachiliwa huru mchana wa leo.
Nay wa Mitego ameachiliwa huru kufuatia uamuzi wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe baada ya kupokea ushauri wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Hata hivyo Waziri Mwakyembe alimtaka Nay wa Mitego auboreshe zaidi wimbo wake.
Wimbo huo mpya wa Ney wa Mitego, ulianza kusambaa katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei alikuwa amesema mwanamuziki huyo alikamatwa kwa kosa la kutoa wimbo wenye maneno ya kashfa dhidi ya serikali.
↧
↧
STARS KUSHUKA DIMBANI KESHO KUUMANA NA BURUNDI
Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii
Timu ya Tanzania "Taifa Stars" inatarajiwa kushuka tena kesho Machi 28 katika mchezo wa pili wa kirafiki unaotarajiwa kuanza majira ya saa 10:00 jioni kumenyana na timu ya taifa ya Burundi.
Stars inaingia tena Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kucheza na Intamba Murugamba ya Burundi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa, kwa mujibu wa kalenda ya wiki ya mechi za kimataifa ya FIFA.
Huu ni mchezo wa pili kwa Taifa Stars kucheza ndani ya wiki moja baada ya ule wa awali dhidi ya The Zebras ‘Pundamilia’ wa Botswana uliofanyika Uwanja huo wa Taifa, jijini Dar es Salaam Jumamosi iliyopita.
Katika mchezo huo wa Jumamosi, Taifa Stars ambayo kwa sasa inanolewa na Salum Mayanga akisaidiwa na Patrick Mwangata ambao ni makocha wapya wa kikosi hicho, walishinda kwa mabao 2-0.
Tayari Intamba Murugamba wametua nchini tangu jana Jumapili saa 4.30 asubuhi na kufikia Hoteli ya De Mag iliyoko, Kinondoni, Dar es Salaam na jioni yake walifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Karume, Ilala jijini. Leo Jumatatu, inafanya mazoezi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa upande wake, Mayanga alifurahishwa na ushindi wa Jumamosi iliyopita dhidi ya The Zebras ya Botswana na hivyo amehimiza Watanzania kujitokeza kwa wingi katika mchezo wa kesho.
Katika kuunga mkono wito wa Kocha Mayanga, TFF imebakiza viingilio vya mchezo huo kuwa sawa na vile vya Jumamosi iliyopita kwani katika mzunguko ambao unachukua mashabiki wengi kiingilio kitakuwa ni Sh 3,000.
Kwa upande wa VIP “A” Kiingilio kitakuwa ni Sh 15,000 wakati VIP “B” na VIP “C” kiingilio kitakuwa ni Sh 10,000. Viingilio hivyo vimelenga kuwaalika Watanzania wengine kwenda uwanjani.
↧
Askari wanaodaiwa kuiba mafuta ya ndege na wenzao wapandishwa kizimbani
Askari wawili wanaodaiwa kuiba mafuta ya ndege ya serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na raia wengine wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo kujibu tuhuma za kula njama na kuhujumu nchi.
Mwendesha Mashtaka wakili wa serikali mwandamizi Nassoro Katuga akisaidiana na wakili Leornad Chalo waliwataja askari hao kuwa ni F. 8419 Koplo Bahati Nyerema Msilimani (33), mkazi wa Ukonga Kota za Airwing na F.9901 PC Benaus (34), anayeishi Ukonga Madafu.
Wengine ni Iddy Juma Nyangas (42), mlinzi wa Moko mkazi wa Vingunguti kwa Mnyamani na Ramadhani Bakari Mwinshehe (52), fundi wa ndege mkazi wa Yombo Buza.
Mbele ya Hakimu Voctoria Nongwa imedaiwa kuwa, kati ya Machi 1 hadi 17 mwaka huu, katika uwanja wa ndege wa mwalimu Julius Nyerere washtakiwa wote kwa pamoja walikula njama ya kutenda kosa la kuhujumu.
Iliendelea kudaiwa kuwa, siku na mahali hapo washtakiwa hao kwa ajali ya kuhujumu manufaa ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, bila kuwa na uhalali kisheria walitoboa ndege kukinga lita 280.6 kutoka kwenye ndege ya ATCL namba 5-HMWF-DASH 8 Q 300.
Iliendelea kudaiwa kuwa kitendo hicho kilikuwa ni kuingilia utoaji wa huduma maalumu kwa jamii ya ndege.
Watuhumiwa wa Uhujumu uchumi wa mafuta ya ndege ya serikali (ATCL) wakiwa kizimbani.
Hata hivyo, washtakiwa hao hawakutakiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mashtaka yao yako chini ya sheria ya uhujumu uchumi na DPP hajatoa kibali cha kuipa mamlaka Mahakama ya Kisutu Kusikiliza kesi hiyo.
Hata hivyo, Mahakama imewaachia washtakiwa hao kwa dhamana kwa vila hakuna kibali cha DPP kinachopinga dhamana na pia mahakama ya kisutu inayomamlaka ya kutoa dhamana kwa kesi isiyozidi shilingi milioni kumi na katika mashtaka yanayowakabili washtakiwa haionyeshi garama za mafuta washtakiwa wanazodaiwa kuhujumu.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi April 27,mwaka huu,.
Wakili Katuga ameiarifu mahakama kuwa, upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na washtakiwa wako nje kwa dhamana ya wadhamini wawili kila mmoja walioweka dhamana ya shilingi milioni moja.
Aidha mahakama imewataka washtakiwa kutosogelea maeneo yao ya kazi na vilevile kutyosafiri nje ya Dar esSalaam bila kibai cha mahakama.
↧
TIC YAINGIA MAKUBALIANO YA MRADI EAST AFRICA AND INVESTIMENT HUB
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC) kimesaini makubaliano ya Mradi wa East Africa and Investiment Hub kwa ajili ya uchocheaji wa uwekezaji nchini.
Akizungumza wakati wa makubaliano hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari amesema kuwa makubaliano hayo yatachochea uwekezaji pamoja na upatikanaji wa masoko nje ya nchi.
Tandari amesema katika kufanya kazi ya mradi huo utasaidia Tanzania kupata wawekezaji kutokana na wigo uliopo katika mradi unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID).
Aidha amesema mradi huo ni wa miaka mitano ambao TIC inaingia katika makubaliano, tayari miaka mitatu umefanya kazi katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Aliongeza kuwa mpaka kumalizika kwa mradi huo nchi itanufaika na kodi pamoja na kuongezeka kwa ajira kwa vijana.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Cliford Tandari akizungumza na Mkurugenzi wa Mradi wa East Africa and Investiment Hub, Kanini Mutooni baada ya kusaini makubaliano ya mradi huo leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari akibadilishana hati na Mkurugenzi wa Mradi wa East Africa and Investiment Hub, Kanini Mutooni leo Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Watendaji wakuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini, wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Cliford Tandari akiwa katika picha ya pamoja na watu wanaotekeleza mradi East Africa and Investiment Hub pamoja na watendaji wa TIC leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massak,Globu ya jamii.
↧
MAHAKAMA KUU TANGA YAWEKA MIKAKATI KUONDOSHA MASHAURI KWA WAKATI
Na Lydia Churi- Mahakama, Tanga.
Mahakama Kuu Kanda ya Tanga inakusudia kuwanunulia Mahakimu wake 67 kompyuta Mpakato (Laptops) ili kurahisisha kazi zao na kuondosha mashauri kwa wakati katika Mahakama mbambali za mkoa wa Tanga.
Akizungumza kwa niaba ya Mtendaji wa Mahakama Kuu kanda ya Tanga, Afisa Utumishi wa Kanda hiyo, Bwana Farid Mnyamike amesema kompyuta hizo zitawasaidia waheshimiwa Mahakimu katika kuandika hukumu ili wananchi waweze kupati haki kwa wakati.
Alisema katika kanda yake, baadhi ya Mahakama zina uhaba wa watumishi hasa Makatibu Muhtasi pamoja na vitendea kazi jambo ambalo limekuwa likichelewesha utolewaji wa hukumu pamoja na upatikanaji wa nakala za hukumu kwa wakati. Aliongeza kuwa kwa Mahakimu kupatiwa kompyuta hizo kutarahisisha upatikanaji wa haki.
Aidha, Afisa Utumishi huyo alisema hivi sasa Mahakama Kuu kanda ya Tanga inao mpango wa kuhakikisha inazipatia umeme baadhi ya Mahakama za Mwanzo kupitia Mradi wa Umeme vijijini (REA) ili kurahisisha upatikanaji wa nakala za hukumu kwa wakati.
Mahakama ya Tanzania ilimwekea malengo kila Hakimu nchini ya kuhakikisha anasikiliza kesi zaidi ya 250 kwa mwaka ili kuondosha mrundikano wa mashauri yaliyoko kwenye Mahakama mbalimbali nchini.
Bwana Mnyamike aliitaja mipango mingine iliyowekwa na Kanda yake katika kuitekeleza nguzo ya pili ya Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa Mahakama ya Tanzania kuwa ni kuwapeleka Mahakimu wenye mashauri machache kwenye Mahakama zenye mashauri mengi ili kuhakikisha mashauri yote ya muda mrefu yanaondoshwa na yaliyofunguliwa yanamalizika kwa wakati.
Ili kuleta mabadiliko ndani ya Mahakama, Mahakama ya Tanzania iliandaa Mpango Mkakati wa Miaka mitano 2015-2020 unaotekelezwa kupitia nguzo tatu ambazo ni Utawala bora, Upatikanaji wa Haki kwa Wakati na pamoja na kurudisha na kujenga imani ya wananchi kwa Mahakama.
↧
↧
MUUNGANO DAY SATURDAY APRIL 29TH, 2017 - SEATTLE, WA
↧
MWANAHABARI GEORGE BINAGI WA LAKE FM MWANZA AUAGA UKAPERA
Jana March 26,2017 ilikuwa siku muhimu kwa mwanahabari wa 102.5 Lake Fm Mwanza na mwanablogu wa BMG, George Binagi wa Tarime Mara pamoja na Miss Upendo Kisaka wa Moshi Kilimanjaro baada ya kuuaga ukapera.
Wapendanao hao walifunga pingu za maisha katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza na baadaye hafla kufanyika Ukumbi wa Sun City Hotel, Ghana Green View Jijini Mwanza.
"Ahsanteni nyote mliotusaidia kutimiza ndoto yetu kubwa katika maishani yetu. Familia yangu, ndugu, jamaa na marafiki zangu. Waumini wote wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza chini ya Mchungaji Daniel Kulola na kila mmoja kwa nafasi yake, Mungu awabariki.
Mmenionesha upendo wa ajabu mno.
Wazazi wangu hususani mama mpendwa, nimetimiza deni mliloniachia duniani. Hakika sasa mtapumzika kwa amani, pahali pema, peponi, Amina. Ndoa na iheshimiwe na watu wote. Mungu atuongoze vyema". Mr & Mrs George Binagi.
Shukurani za pekee pia ziwaendelee best man na Best Lady, Mr and Mrs. Joel Maduka kutoka Storm FM Geita na Maduka Online kwa kufanikisha shughuli hiyo kwenda vyema.
BMG inakusihi uendelee kutazama picha za awali za shughuli hiyo wakati wataalamu wetu wakiendelea kukuandalia picha nyingine ikiwemo picha za kanisani. BOFYA HAPA
↧
ZAO LA KOROSHO LINDI NA MTWARA LAKUMBWA NA UGONJWA WA MNYAUKO
Zao la korosho nchini lipo hatarini kuporomoka kufuatia kugundulika kwa ugonjwa mpya wa mnyauko wa mikorosho ambao umeua mikorosho zaidi ya elfu 40 hadi sasa katika mikoa ya LINDI na MTWARA. Fungua video kupata taarifa kamili
↧
More Pages to Explore .....