Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109611 articles
Browse latest View live

HAFLA YA UZINDUZI WA MRADI WA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI AWAMU YA TATU (REA III) KATIKA MKOA WA IRINGA.

0
0

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Dkt Gideon Kaunda akizungumza na Wananchi wakati wa Hafla ya uzinduzi wa mradi wa usambazaji umeme vijijini Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Iringa uliofanyika katika kijiji cha Image wilayani Kilolo. Kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Gissima Nyamo-hanga (wa kwanza kulia), Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kulia), Mbunge wa Kilolo, Mhe.Venance Mwamoto (wa tatu kulia) wakisoma maombi ya wananchi ya kuunganishiwa umeme katika Mradi wa usambazaji umeme vijijini Awamu ya Tatu, wakati wa Hafla ya uzinduzi wa mradi wa usambazaji umeme vijijini Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Iringa uliofanyika katika kijiji cha Image wilayani Kilolo.
Wanafunzi wa Sekondari ya Wasichana wa Jamii ya Kimasai wilayani Kilolo wakitumbuiza wakati wa Hafla ya uzinduzi wa mradi wa usambazaji umeme vijijini Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Iringa uliofanyika katika kijiji cha Image wilayani Kilolo.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa tatu kuli mstari wa nyuma) pamoja na viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuzindua mradi wa usambazaji umeme vijijini Awamu ya Tatu (REA III) katika mkoa wa Iringa. Wa nne kulia ni Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Gissima Nyamo-hanga na wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Dkt Gideon Kaunda. Waliosimama mbele ni Wanafunzi wa Sekondari ya Wasichana wa Jamii ya Kimasai wilayani Kilolo.

UZINDUZI WA MAONYESHO YA KWANZA YA TAMTHILIYA YA KICHINA INAYOITWA “MFALME KIMA” KWA LUGHA YA KISWAHILI YAFANYIKA LEO

0
0
Na Shamimu Nyaki.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel amewaomba Wataalamu wa lugha ya Kichina hapa nchini kutafsiri Filamu za Kiswahili kwa lugha ya kichina ili zipate soko nchini China.
Prof. Elisante Ole Gabriel ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa anazindua Maonyesho ya kwanza ya Tamthiliya ya kichina inayoitwa “Mfalme Kima” iliyotafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili ambapo amesema kuwa njia nzuri ya kufikisha ujumbe kwa watanzania katika filamu za kichina ni kutumia lugha ya Kiswahili.

“Njia rahisi ya kufikisha ujumbe kwa watu wote ni kutumia lugha mtambuka katika tamthiliya zetu hii itasaidia sana kukuza uhusiano wetu na Jamhuri ya Watu wa China”,Alisema Prof.Ole Gabriel.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi vya Luninga Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Bibi Suzan Mungy ameelza kuwa ushirikiano wa shirika hilo na Kampuni ya Star Times ambayo ndio waandaji wa Tamthiliya hiyo umeleta mafanikio makubwa ikiwemo kuongezeka kwa watazamaji wanaopenda tamthiliya za kichina zenye tafsiri ya lugha ya Kiswahili zinazooneshwa katika luninga hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel akizungumza na hadhira (haipo katika  picha) katika hafla ya Uzinduzi wa maonyesho ya kwanza ya Tamthiliya ya kichina inayoitwa “Mfalme Kima” kwa lugha ya Kiswahili uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Makampuni ya StarTimes, Bi. Guo Ziqi akizungumza katika hafla ya Uzinduzi wa maonyesho ya kwanza ya Tamthiliya ya kichina inayoitwa “Mfalme Kima” kwa lugha ya Kiswahili uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa uzalishaji wa vipindi vya Luninga  Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Bibi Suzan Mungy akizungumza na hadhira (haipo katika picha) akitoa maelezo mafupi kuhusu Shirika hilo linavyoshirikiana na Serikali ya China  katika  hafla ya  Uzinduzi wa maonyesho ya kwanza ya Tamthiliya ya kichina inayoitwa  “Mfalme Kima” kwa lugha ya Kiswahili uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Kimataifa nchini China, Bi. Ma Li akizungumza katika hafla ya Uzinduzi wa maonyesho ya kwanza ya Tamthiliya ya kichina inayoitwa “Mfalme Kima” kwa lugha ya Kiswahili uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wakifuatilia kinachoendelea kwenye uzinduzi wa tamthiliya.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI MWIGULU AIONGOZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE YA ULINZI NA USALAMA KUKAGUA MRADI WA UJENZI KITUO CHA POLISI OYSTERBAY JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu (kushoto), akiongozana na wajumbe wengine wa kamati hiyo wakati wakiwasili katika eneo la mradi wa ujenzi wa kituo cha polisi, Oysterbay, leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu (katikati), akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu baada ya kuwasili katika eneo la mradi unaoendelea wa Ujenzi wa Kituo cha Polisi, Oysterbay,leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba.
Mtaalamu wa Majengo kutoka kampuni inayojenga Kituo cha Polisi Oysterbay, Mhandisi Fanuel Malekela, akitoa maelezo ya mchoro wa ujenzi wa kituo hicho kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu (wapili kushoto),wakati kamati hiyo ilipotembelea ujenzi wa mradi huo.Wengine ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba(watatu kushoto) na Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu. Ziara hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Fedha wa Jeshi la Polisi, Albert Nyamhanga, akitoa maelezo ya mradi wa Ujenzi wa kituo cha Polisi,Oysterbay kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu(watatu kulia), wapili kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba(kulia), akiwaongoza kutoka ndani ya jengo wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama baada ya kumaliza kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa kituo cha polisi,Oysterbay leo jijini Dar es Salaam.Huku sehemu kubwa ya mradi huo ikiwa imekamilika. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

WANANCHI NAWAOMBA MYAKUBALI MAAMUZI YALIYOFANYWA NA RAIS WETU-NAPE NNAUYE.

0
0

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na mbunge wa Mtama Nape Mosses Nnauye amewataka Watanzania kukubaliana na suala la kusitishwa kwake uteuzi wa cheo hicho baada Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli amemteua Dk Harrison Mwakyembe kuchukua nafasi hiyo ya Nape.

Akizungumza na waandishi nje ya Hoteli ya Protea leo, Nape amesema wanatakiwa kukubaliana na hali halisi kwani uteuzi uliofanywa huwezi kuukosoa na anashikuru kwa kuweza kupata muda wa kufanya kazi na Rais Magufuli.

“Wanachi mnatakiwa kukubaliana na maamuzi yaliyofanywa na Rais wetu kwani tukumbuke kuwa Tanzania ni kubwa kuliko Nape na maamuzi yaliyofanywa yana tija kubwa sana kwa tasnia ya habari, michezo na wasanii na hampaswi kuanzisha matatizo, Tanzania ni nchi yetu sisi na tujue Nape hawezi kuwa mkubwa kuliko Tanzania,"

Nape amesema kuwa anawashauri watanzania wote kuwa watulivu na zaidi amefurahi kufanya kazi kama Waziri wa habari na amewaomba wana tasnia ya habari ya habari kushirikiana na Waziri Mteule Harrison Mwakyembe kwani ni mwanahabari na pia ni mwanasheria mzuri.

“Nina amini nilitumia akili zangu zote na kwa akili nawashukuru wasanii, waandishi, wanamichezo kwa ushirikiano wenu. Nilipenda kuendelea kufanya kazi nanyi lakini muda wa aliyeniteua umefika, nitawakumbuka sana, ninawapenda sana ila ninawaomba mumuunge mkono Waziri Mwakyembe na kuendelea kumwamini Rais wetu John Pombe Magufuli kwani ndiye tuliyepewa na mungu, ndiye rais tuliyemchagua,” amesema Nape.
Aliyekuwa Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari nje ya hoteli ya Protea jijini Dar es Salaam leo
 
 Aliyekuwa Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye akifafanua jambo kwa msisito alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nje ya hoteli ya Protea jijini Dar es Salaam leo
Waandishi wa habari wakimsikiliza Aliyekuwa Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye alipokuwa akizungumza nao

MICHUZI TV: ALICHOONGEA NAPE NNAUYE BAADA YA KUVULIWA UWAZIRI LEO

WAZIRI MBARAWA AITAKA BODI YA WABUNIFU MAJENGO NA WAKADILIAJI MAJENZI KUJITANUA ZAIDI

0
0
Judith Ferdinand, BMG

Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiliaji Majenzi, nchini, imehimizwa kushirikiana na wataalamu kutoka nchi jirani katika kutoa mafunzo kwa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi ili kuendane na teknolojia ya kisasa.

Wito huo umetolewa leo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, katika mafunzo endelevu ya 27 ya Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi yanayofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa Rocky City Mall Jijini Mwanza.

Profesa Mbarawa amesema,kwa kutumia wataalamu kutoka nje ya nchi, itasaidia na kuwawezesha wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi, kubadilishana uzoefu pamoja na kuendana na soko la ushindani.

Pia amewaomba wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi,wanapopata fursa katika miradi ya ujenzi watumie elimu walionayo, kwa ajili ya maslahi ya taifa sambamba na uadilifu.
Mwenyekiti wa Bodi Dr Ambwene Mwakyusa (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) vifaa vya maabara.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema vifaa hivyo atavipeleka katika shule moja ya wasichana ya sayansi, sambamba ameishukuru bodi hiyo kupitia wataalamu wa ujenzi kwa kutoa vifaa hivyo ambavyo vitakua chachu kwa wanafunzi kusoma masuala ya ubunifu majengo na ukadiriaji majenzi.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akizungumza kwenye Mkutano wa mashauriano baina ya Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiliaji Majenzi unaofanyika kwa siku mbili kuanzia jana, katika Ukumbi wa Rock City Mall Jijini Mwanza.
Kaimu Msajili wa Bodi, Albert Munuo, akizungumza kwenye mkutano huo.
Wajumbe waliohudhuria mkutano huo.

VIJANA WA SERENGETI BOYS WAKABIDHIWA KADI ZA BIMA YA AFYA NA NHIF

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umetoa kadi za bima kwa wachezaji wote 23 wa timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 'Serengeti boys' kwa ajili ya masuala ya matibabu.

Kaimu Mkurugenzi na Masoko Mfuko huo Angela Mziray alisema wamekuwa washirikiana na Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) katika shughuli mbalimbali ikiwemo kuwa sehemu ya udhamini wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Angela alisema kwa sababu ugonjwa unakuja bila taarifa na wachezaji wapo kwenye hatari ya kuumia na kuugua pia kwahiyo imekuwa vizuri kwa TFF kuliona hilo nakuwapatia kadi za bima ya afya.

"Namshukuru Rais Jamal Malinzi kwa kusimamia suala hili mpaka leo tumefikia hatua hii na ninaahidi kwa niada ya NHIF tutaendelea kushirikiana na TFF katika masuala mbalimbali," alisema Mziray.

Kwa upande wake Katibu mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa alisema bima hizo zitakuwa msaada mkubwa kwa wachezaji hao kwakua wataweza kutibiwa mahali popote nchini hata wasipokuwa kambini.

NHIF imefika asilimia 90 nchi nzima wakiwa na zaidi ya vituo 6000 kwa ajili ya kutoa huduma ya afya.

Serengeti ambayo inaendelea na kambi jijini Dar es Salaam inataondoka wiki ijayo kuelekea mkoani Kagera kwa kambi ya wiki moja kabla ya kuelekea nchini Morocco kwa kambi ya mwezi mzima.
Kaimu Mkurugenzi na Masoko Mfuko wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Angela Mziray akizungumza na vijana wa Serengeti Boys pamoja na waandishi wakati wa makabidhiano ya kadi za Afya za Bima kwa ajili ya matibabu leo Jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa kamati ya soka la Vijana Ayubu Nyenzi na Meneja wa Uanachama wa NHIF Eletruda Mbogoro.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Selestine Mwesigwa akizungumza na vijana wa Serengeti Boys pamoja na waandishi wakati wa makabidhiano ya kadi za Afya za Bima kwa ajili ya matibabu leo Jijini Dar es salaam. 

Kaimu Mkurugenzi na Masoko Mfuko wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Angela Mziray akikabidhi kadi za Bima kwa ajili ya matibabu kwa vijna wa Serengeti Boys leo Jijini Dar es salaam.
Viongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wakiwa pamoja na viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) na vijana wa Serengeti Boys mara baada ya kukabidhiwa kadi za Bima ya Afya leo Jijini Dar es salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE MAMBO NJE, ULINZI NA USALAMA YASISITIZA SERIKALI KUANZA MATUMIZI YA VITAMBULISHO VYA TAIFA

0
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo Nje, Ulinzi na Usalama leo imefanya ziara ya kukagua mradi wa Vitambulisho vya Taifa; ambapo mbali na kupokea taarifa ya utekelezaji pia walitembelea na kukagua kituo kikuu cha Kuhifadhi, kuchakata na kuzalisha Vitambulisho vya Taifa -Data Centre.

Akizungumza wakati wa kukaribisha Kamati hiyo; Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) amesema mpaka sasa NIDA imefanikiwa kutekeleza majukumu yake kwa kiwango kikubwa pamoja na changamoto kubwa ya fedha iliyopo.

Akizungumza kwa niaba ya Kamati hiyo; Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Adad Rajab (Mb) amepongeza jitihada kubwa zinazofanywa na NIDA na kwamba Kamati imeridhishwa na kazi kubwa na nzuri inayofanywa na NIDA na kwamba Kamati yake itaendelea kuishauri Serikali kuongeza bajeti ya fedha kwa NIDA ili kuwezesha kukamilisha zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa, kwani manufaa ya kuwa na mradi huu kwa Taifa ni makubwa katika Nyanja zote.

Wakitoa maoni yao wajumbe wa Kamati hiyo wameitaka Wizara kuiwezesha NIDA na kuharakisha matumizi ya Vitambulisho vya Taifa kielektroniki kwani tayari idadi kubwa ya wananchi wameshatambuliwa na taarifa zao kuingizwa kwenye mfumo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba akiwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo Nje, Ulinzi na Usalama walipowasili NIDA kutembelea na kukagua maendelea ya mradi wa Vitambulisho vya Taifa.

Nje, Ulinzi na Usalama Mh. Adad Rajab (Mb), akiongea jambo wakati wa kikao na Menejimenti ya NIDA baada ya kupokea taarifa ya Utekelezaji toka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Bw. Andrew W. Massawe. Kulia ni Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo Mh. Kanali Mstaafu Ramadhani Issa Abdallah(Mb).Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bw. Andrew W. Massawe, akisoma ripoti ya Utekelezaji Mradi wa Vitambulisho vya Taifa kwa kamati ya ulinzi na Usalama ya Bunge. Kushoto ni Mh Sophia H. Mwakagenda(Mb) na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nchi Mh. Balozi Simba Yahya.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba pamoja na baadhi ya wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge wakisikiliza jambo wakati walipotembelea kituo cha uchakataji taarifa cha NIDA (NIDA DATA CENTER). Katikati ni Mh. Adad Rajab(Mb) mwenyekiti wa kamati na kulia ni Mh. Sophia H. Mwakagenda(Mb) Mjumbe wa kamati


HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Kamati ya Bunge Yaipongeza Muhimbili kwa Kuboresha Huduma za Afya

0
0

Na John Stephen, MNH

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii imeipongeza Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kutokana na ubunifu wa kufanya mageuzi makubwa ya kuboresha huduma za afya.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Njombe, Mheshimiwa Lucia Mlowe wakati akichangia taarifa ya utendaji iliyowasilishwa kwa kamati hiyo na Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru.

“Napenda kuwapongeza viongozi na wafanyakazi wa MNH kutokana na ubunifu wenu mkubwa mnaofanya katika kuleta maendeleo ambayo yamelenga kutoa huduma bora. Kutokana na juhudi hizi Serikali inapaswa kutoa fedha ilizoziahidi kwa MNH.

“Nchi nzima inaitegemea MNH, Serikali ione huruma kwa MNH iwapelekee fedha, isiwaache pekee yao,” amesema Mlowe.

Mjumbe wa kamati hiyo msheshimiwa Faustin Mdugulile ameipongeza MNH kutokana na mageuzi makubwa ya kuboresha huduma za afya na ameahidi kuisema MNH bungeni ili serikali kushughulikia changamoto zinazoikabili hospitali hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akitoa taarifa fupi ya utendaji kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.ambayo imeitembelea hospitali hiyo leo. Kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kingwangallah na Mwenyekiti wa kamati hiyo Peter Serukamba.
Baadhi ya Wajumbe wa kamati hiyo wakifuatilia ripoti ya utendaji iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Profesa Museru.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kingwangallah (kushoto), Mwenyekiti wa kamati hiyo, Peter Serukamba na Mkurugemzi Mtendaji wa MNH, Profesa Museru wakisiliza maoni ya wajumbe wa kamati hiyo leo.
Mjumbe wa Kamati hiyo, Dk Faustin Ndugulile akitoa maoni yake baada ya mkurugenzi wa hospitali hiyo kuwasilisha taarifa ya utendaji ya hospitali hiyo kwa wajumbe.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATEMBELEA KIWANDA CHA NGUO MAURITIUS

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha Compagnie Mauricienne De Textile Ltee kinachotengeneza nguo kwa kutumia teknolojia ya kisasa nchini Mauritius chenye uwezo wa kutengeneza tani milioni 40 hadi 50 kwa mwaka.
Aidha, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji hao kuja nchini Tanzania na kuwekeza katika viwanda vya kutengeneza nyuzi pamoja na nguo kwa kuwa kuna malighafi za kutosha kwa ajili ya uzalishaji huo.
Waziri Mkuu alitembelea kiwanda hicho kilichoko katika mji wa Latour Koenig jana (Jumatano, Machi 22, 2017) na kujionea namna wanavyotengeneza nguo kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kuamua kuwakaribisha waje kuwekeza nchini.
“Tumefarijika na uwekezaji wenu na tumejionea namna ambavyo mnavyoendesha kiwanda chenu kuanzia utengenezaji wa nyuzi hadi nguo, hivyo tunahitaji viwanda kama hivi nchini Tanzania kwa sababu sisi tunazalisha pamba nvingi na yenye ubora unaokubalika kimataifa,” alisema.

Waziri Mkuu alisema madhumuni  ya kuwakaribisha wawekezaji hao kuja Tanzania na kuwekeza katika  viwanda vya kutengeneza nyuzi yanalenga kuboresha kilimo cha pamba na kuwawezesha wakulima kupata tija.

“Tunalima pamba nzuri na hawa hawalimi wananunua kutoka nje ya nchi yao, hivyo wakija kuwekeza Tanzania itawarahisishia kupata malighafi ya uhakika na kwa urahisi ”  alisema.
Alisema viwanda hivyo vitasaidia maendeleo ya kilimo cha pamba kwa sababu vitatoa ajira kwa wananchi wengi hivyo kuwawezesha kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini wa kipato.
Mbali na kuwakaribisha wawekezaji hao, pia Waziri Mkuu alitoa wito kwa wananchi wenye uwezo kuhakikisha wanajenga viwanda vya nyuzi kwenye mikoa yote inayozalisha pamba ili waweze kuiongezea thamani kabla ya kuiuza.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fedha wa kiwanda hicho Bw. David Too Sai Voon alisema wamefurahishwa na mualiko wa kuja Tanzania kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji wa viwanda vya nyuzi na nguo.

Bw. David alisema kiwanda chao kilianzishwa mwaka 1986 na kwa sasa kimeajiri wafanyakazi 18,000 ambapo mauzo yao kwa ni dola milioni 200. “Nguo tunazotengeza ni za kiwango cha kimataifa na tunauza katika maduka makubwa barani Ulaya,”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, MACHI 23, 2017.
 Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akitazama mitambo ya kiwanda cha kuengeneza nyuzi za pamba wakati alipotembelea kiwanda cha nguo cha Compagne Mauricienne De Textile Ltee kilichopo nje kidogo ya mji wa Port  Louis nchini Mauritious. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama nguo zilizoshonwa  kwa vitambaa vilivyotengenezwa na kwanda cha nguo cha Compagne Mauricienne De Textile Ltee cha Mauritius wakati alipotembelea kiwanda hicho, nje kidogo ya mji wa Port Louis nchini Mauritius, Machi 22, 2017.


Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akizungumza viongozi wa kiwanda cha  nguo cha Mauritius cha Compagnie Mauricienne De Textile Ltee baada ya kutembelea kiwanda hicho kilichopo nje kidogo ya mji wa Port Louis Machi 22, 2017.

COCA - COLA KWANZA YAENDELEA KUTAMBULISHA UJIO WAKE MPYA WA MKANDA MWEKUNDU KWENYE CHUPA KWA SHULE ZA MBEYA, YATINGA AIR PORT SEKONDARI YAMWAGA ZAWADI NA SODA KWA WANAFUNZI

0
0

Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Airport iliyopo jijini mbeya wakiwa wamekamatia soda mkononi kutoka katika kampuni ya Coca-Cola ikiwa ni muendelezo wa  kuamsha shangwe na Coca-cola na ujio mpya wa mkanda mwekundu katika chupa za soda ya Coca-Cola.

Mmoja kati ya wanafunzi wa shule hiyo ya Airport iliyopo Jijini Mbeya akijaribu kushiriki shindano la kupiga danadana kwa kutumia Mpira na hatimae kujinyakulia Mpira huo kutoka Coca-Cola.

Mwanafunzi wa shule ya Air Port Sekondari akionesha moja ya zawadi aliyoipokea kutoka Coca-Cola kwanza walipotembelewa shuleni hapo.

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Airport wakiwa katika uwanja wa shule yao uliopo katika eneo la jakalanda jijini mbeya kuuonja msisimko na Coca-Cola yenye muonekano wa kuvutia uliozinduliwa hivi karibuni mkoani Mbeya na kuingizwa mtaani ili wanaMbeya waendelee kuamsha shangwe zao na Coca-Cola ya nguvu yenye muonekano mpya wa mkanda mwekundu kwenyechupa za Coca-Cola.
PICHA ZOTE NA FADHIRI ATICK MR.PENGO MBEYA.

ALPHAYO KIDATA ATEULIWA KUWA KATIBU MKUU IKULU

RAIS DKT MAGUFULI APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO TOKA KWA MABALOZI SITA WA NCHI MBALIMBALI IKULU DAR ES SALAAM LEO

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho kutoka kwa Mhe. Laszlo Eduard Mathe Balozi wa Hungary nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi Kenya leo Machi 23, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho kutoka kwa Mhe. Sidibe Fatoumata Kama, Balozi wa Guinea  nchini mwenye makazi yake jijini Addis Ababa, Ethiopia, leo Machi 23, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho kutoka kwa Mhe. Lebonaamang Thanda Mokalake, Balozi wa Botswana nchini mwenye makazi yake jijini Lusaka, Zambia, leo Machi 23, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho kutoka kwa Mhe. Adam Maiga Zakariaou Balozi wa Niger  nchini mwenye makazi yake jijini Addis Ababa, Ethiopia, leo Machi 23, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho kutoka kwa  Mhe. Jean Pierre Jhumun, Balozi wa Belarus  nchini mwenye makazi yake jijini Addis Ababa Ethiopia  leo Machi 23, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho kutoka kwa Dmitry Kuptel Balozi wa Mauritius  nchini mwenye makazi yake jijini Maputo nchini Msumbiji leo Machi 23, 2017 Ikulu jijini Dar es salaam.

PICHA NA IKULU

RAIS SHEIN AKUTANA NA UJUMBE WA CHAMA CHA KIKOMONISTI CHA CHINA LEO

0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na mgeni wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomonisti cha China(CPC) Bw. Guo Jinlong alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo akiwa na Ujumbe aliofuatana nao.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akifuatana na mgeni wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomonisti cha China(CPC) Bw. Guo Jinlong alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo akiwa na Ujumbe aliofuatana nao.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na  mgeni wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomonisti cha China(CPC) Bw. Guo Jinlong alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo akiwa na Ujumbe aliofuatana nao.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na  mgeni wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomonisti cha China(CPC) Bw.Guo Jinlong (wa tatu kulia) alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo akiwa na Ujumbe aliofuatana nao (Picha na Ikulu).

BBC DIRA YA DUNIA ALHAMISI 23.03.2017


TUTASAIDIA JUHUDI ZA TTB - MABALOZI

0
0
Mabalozi walioteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kuiwakilisha Tanzania katika nchi  mbalimbali duniani wameihakikishia Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kuwa wamejizatiti kikamilifu kwenda kusaidia juhudi kubwa za Bodi hiyo katika kuitangaza Tanzania kama eneo bora la Utalii duniani katika nchi wanazokwenda kufanyakazi sambamba na kuhamasisha wafanyabiashara kutoka mataifa hayo kuwekeza nchini katika sekta ya utalii ikiwa ni utekelezaji wa jukumu lao kubwa la kukuza diplomasia ya uchumi.

Wamepongeza juhudi zinazofanywa na TTB katika kuvitangaza vivutio vyetu vya utalii lakini wakaomba iangalie namna gani inaweza kusaidia katika kuboresha huduma zitolewazo na wadau wa utalii kwa watalii wanaotembelea Tanzania kama vile mahotelini kwani bado hatufanyi vema katika suala la huduma bora na nzuri kwa watalii. Aidha wameiomba TTB kushauri mamlaka na watoa huduma wengine katika sekta ya utalii kupunguza gharama wanazotoza kwani ni kubwa sana kiasi cha kuifanya Tanzania kulalamikiwa na wageni wengi kuwa ni eneo la utalii ghali sana ukilinganisha na nchi nyingine ambazo ni washindani wetu katika sekta ya Utalii.

Hayo yamesemwa leo  na mabalozi hao wakiongozwa na Balozi Omari Yusuph Mzee walipotembelea makao makuu ya Bodi ya Utalii Tanzania kwa lengo la kuzungumza na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi hiyo Bi Devota Mdachi na kupanga mikakati ya namna balozi hizo zinavyoweza kushirikiana na TTB katika kuitangaza Tanzania na kuhamashisha wawekezaji kutoka nchi wanazokwenda kufanyakazi kuja nchini kuwekeza katika sekta ya utalii.

Mapema  Mkurugenzi Mwendeshaji wa TTB Bi Devota Mdachi aliwaelezea waheshimiwa mabalozi mikakati mbalimbali ambayo Bodi yake imekuwa ikitekeleza katika kuitangaza Tanzania nje ya nchi kwa lengo kuvutia watalii wengi zaidi na kukuza utalii kwa ujumla. Alitaja baadhi ya mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuweka matangazo katika maeneo na vyombo mbalimbali vya habari nje ya nchi, kualika na kuleta nchini watu maarufu ili kuja kutembelea vivutio vyetu vya utalii, kuteua mabalozi wa hiari wa utalii na kutumia mitandao mbalimbali ya kijamii.

Mkurugenzi Mwendeshaji Bibi Devota Mdachi aliwakabishi mabalozi hao vielelezo mbalimbali vya utalii wa Tanzania na kuahidi kuwa bodi yake itakuwa ikiwatumia vielelezo mbalimbali vya utalii vitakavyo wasaidia katika kutekeleza jukumu la kusaidia utangazaji utalii katika nchi walizopangiwa. Mabalozi hao watano na nchi wanazo kwenda ni Omari Yusuph Mzee (Algeria), Matilda Masuka (Korea Kusini), Dkt. Pindi Chana (Kenya), Grace Mgovano (Uganda), Fatma Rajab (Qatar) na Balozi Abdallah Kilima (Oman).  

 Mkurugenzi Mwendeshaji wa TTB Bi devota Mdachi akizungumza na Mabalozi waliomtembelea ofisini kwake jana.Kushoto ni Balozi Omari Yusuph Mzee na kulia ni Balozi Abdallah Kilima.

 Balozi wa Tanzania nchini Kenya Dkt Pindi Chana akisisitiza jambao wakati wa mazungumzo baina yao na Mkurugenzi Mwendshaji wa TTB walipomtembelea ofisini kwake Dar es salaam.

 Mkurugenzi Mwendshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania Bi Devota Mdachi (kulia) akimkabidhi Balozi Abdallah Kilima moja ya majarida ya TTB yanayozungumzia utalii wa Tanzania wakati timu ya mabalozi sita walioteuliwa hivi karibuni walipomtembela Mkurugenzi huyo ofisini kwake jijini Dar es salaam. 

Mabalozi wanaowakilisha Tanzania katika baadhi ya nchi duniani wakiwai katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa TTB Bi Devota Mdachi (wa nne kushoto) na baadhi ya Maafisa waandamizi wa TTB . Kutoka kushoto ni Bw. Geofrey Meena Meneja Masoko wa TTB, Mh. Balozi dkt Pindi Chana , Mh. Balozi Omari Yusuph Mzee, Mh. Balozi Fatma Rajab  (wa tano), Mh. Balozi Grace Mgovano (wa sita), Mh. Balozi Matilda Masuka (wa saba) na Bw. Philip Chitaunga Meneja Huduma kwa watalii wa TTB. 

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddiatembelea kampuni ya Mahindra jijini New Delhi, India

0
0
Kampuni ya Kimataifa ya Uhandisi katika utengenezaji wa vyombo vya Moto ya Mahindra yenye Makao Makuu yake Mjini New Delhi Nchini India imeamua kuiunga Mkono Zanzibar katika muelekeo wake wa kuimarisha miradi ya maendelelo.
Mkuu wa shughuli za Kimataifa wa Kampuni hiyo Bwana Arvind Mathew alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha pamoja kati ya Uongozi wa Kampuni yake na Ujumbe wa Zanzibar unaoongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kilichofanyika Makao Makuu ya Kampuni hiyo yaliyopo Mjini New Delhi. 
Bwana Arvind Mathew alisema kutokana na kukuwa kwa Teknolojia ndani ya Kamupuni ya Mahindra, Uongozi wa Taasisi hiyo ya Uhandisi Nchini India hivi sasa umekusudia kuelekeza nguvu zake katika Mataifa rafiki kwa nia thabiti ya kuona Mataifa hayo hasa yale ya Bara la Afrika yanakuwa Kiuchumi. 
Alisema Mahindra imejipanga kuangalia njia za kusaidia uimarishaji wa Sekta ya Kilimo kupitia miundombinu imara na vifaa vya Kisasa vitakavyoongeza nguvu za uzalishaji kwa kundi kubwa la Wakulima katika mazao ya viungo yenye tija kubwa katika soko la Kitaifa na Kimataifa. Alisema Wataalamu wa Kampuni ya Mahindra wamekuwa shahidi katika safari zao za kawaida kwenye Mataifa mbali mbali waliyowekeza miradi yao ya Kiuchumi kuwaona Wakulima wa maeneo hayo wakiendesha shughuli zao katika mazingira magumu.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wa ili kutoka Kushoto akizungumza na Wafanyabiashara na Wawekezaji wa Mji wa New Delhi Nchini India kwenye Makamo Makuu wa Shirikisho la Viwanda Mjini New Delhi. Wa kwanza kutoka Kulia ni Mkuu wa shughuli za Kimataifa za Kampuni ya Mahindra Bwana  Arvind Mathew, wa kwanza kutoka Kushoto ni Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi Dr. Sira Ubwa Mamboya na Kushoto ya Balozi Seif ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili Mh. Mihayo Juma N’hunga.
 Mkuu wa shughuli za Kimataifa za Kampuni ya Mahindra Bwana  Arvind Mathew Kushoto akibadilishana mawazo na Balozi Seif mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
 Balozi Seif  akizungumza katika kikao cha pamoja mkati ya Ujumbe wake na Wawekezaji na Wafanyabiashara wa Mji wa New Delhi na Majimbo jirani yanayouzunguuka Mji huo makamo Makuu ya Shirikisho la Viwanda la India Mjini New Delhi. Kushoto ya Balozi Seif ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirikisho hilo ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Ushauri wa Kimataifa wa CII Bwana K.K Kapila na Kulia yake ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya Bibi Asha Ali Abdulla.
 Balozi Seif akimzawadia mlango Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirikisho hilo ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Ushauri wa Kimataifa wa CII Bwana K.K Kapila mara baada ya kumaliza mazungumzo yao 
Picha na – OMPR – ZNZ. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

UFAFANUZI KUTOKA MAHAKAMA YA TANZANIA KUHUSU HABARI YA "UTATA WA JAJI MKUU"

Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete Akutana na Rais Dennis Sassou Nguesso wa Congo Brazaville

0
0
Rais Mstaafu na Kamishna wa Kamisheni ya Kupendekeza Namna Bora ya Kugharamia Fursa ya  Elimu  Duniani  ( Education Commission on Financing Global Education Opportunity) juzi tarehe 21 Machi, 2017, amekutana na Rais wa Jamhuri ya Congo Mhe. Dennis Sassou Nguesso alipomtembelea Ikulu yake jijini Brazaville.
Katika nafasi yake ya Mjumbe Maalum wa Kamisheni hiyo, Rais Mstaafu amemkabidhi  Rais Sassou Nguesso Ripoti ya Kamisheni hiyo yenye mapendekezo ya namna Dunia inavyoweza kukabili janga la Elimu kwa kuwekeza katika Mpango wa Kizazi cha Elimu (A Learning Generation). Mpango huo unalenga kuleta mapinduzi makubwa ya Elimu katika nchi zinazoendelea ndani ya Kizazi Kimoja  (miaka 30). 
Azma kuu ya Mpango huo ni kuwezesha ifikapo mwaka 2040, watoto wote kote duniani wawe wanapata elimu iliyo sawa, na kwa kiwango cha ubora unaolingana dunia nzima.
 Rais Mstaafu na Kamishna wa Kamisheni ya Kupendekeza Namna Bora ya Kugharamia Fursa ya  Elimu  Duniani  ( Education Commission on Financing Global Education Opportunity) akilakiwa na  Rais wa Jamhuri ya Congo Mhe. Dennis Sassou Nguesso alipomtembelea Ikulu yake jijini Brazaville.
  Rais Mstaafu na Kamishna wa Kamisheni ya Kupendekeza Namna Bora ya Kugharamia Fursa ya  Elimu  Duniani  ( Education Commission on Financing Global Education Opportunity) akimkabidhi ripoti hiyo  Rais wa Jamhuri ya Congo Mhe. Dennis Sassou Nguesso alipomtembelea Ikulu yake jijini Brazaville.
 Rais Mstaafu na Kamishna wa Kamisheni ya Kupendekeza Namna Bora ya Kugharamia Fursa ya  Elimu  Duniani  ( Education Commission on Financing Global Education Opportunity)akiongea na wanahabari  jijini Brazaville. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

Viewing all 109611 articles
Browse latest View live




Latest Images