Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

kashangae feri

$
0
0
Wakati Dar es salaam unaambiwa nenda kashangae feri ambapo shilingi inazama ila meli inaelea, kwa upande wa jiji la Singapore ni tofauti kidoooogooo.... Hapo unaambiwa nenda Marina Bay kashangae meli iko juu ya vikwangua anga...Hii ni mojawapo ya hoteli za kitalii maarufu san
a jijini Singapore yenye bonge moja la Casino. Kiingilio kwa wageni ni bure... kwa wenyeji dola mia za Singapore...


uzi mpya wa bwawa la maini wa kuchezea ugenini... mtatutaka msimu huu...

RAIS KIKWETE AHITIMISHA ZIARA YAKE NCHINI SINGAPORE KWA KUTEMBELEA MAENEO MBALIMBALI

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji Upya wa Miji Upya ya Singapore leo Juni 6, 2013 ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembelea Taasisi ya Elimu ya ufundi (Institute of Technical education) iliyo sawa na VETA kwa Tanzania leo Juni 6, 2013.ambapo pamoja na mambo mengine walijionea jinsi wanafunzi wake wanavyofundishwa kuunda vipuli vya aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na vya ndege.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji mijini ya Singapore leo Juni 6, 2013.ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu.
Baadhi ya wafanyabiashara walioongozana na Rais Jakaya Kikwete katika ziara ya kikazi nchini Singapore wakiwa katika picha ya kumbukumbu na mawaziri walio katika msafara huoleo Juni 6, 2013. . Wa pili kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe akifuatiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Abdallah Kigoda na Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe (wa tatu) kulia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika picha ya pamoja na viongozi wa Mamlaka ya Ustawishaji Upya ya Miji ya Singapore leo Juni 6, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika picha ya pamoja na viongozi wa Taasisi ya Elimu ya Ufundi ya Singapore baada ya kutembelea kampasi yao jijini Singapore leo Juni 6, 2013. PICHA NA IKULU

BARCLAYS Step Ahead Walk 2013 kufanyika tarehe 08 June, 2013 Jijini Dar

HOJA YA HAJA: MAONI NA ANGALIZO JUU YA RASIMU YA KATIBA

$
0
0
Dear Ankal
Kwa kweli wajumbe wa tume ya katiba wameyatendea  haki maoni ya watanzania  juu ya katiba  mpya. Ingawa  sijapata  muda  wa kusoma  kifungu hata kifungu kwa  utulivu, lakini kwa muonekano wa  awali  rasimu ni  nzuri  na itahitaji marekebisho machache  ya kimsingi.  Rasimu ya  katiba  imependekeza kuwepo kwa  serikali tatu, yaani ya  Muungano, ya Tanzania zanzibar(ambayo ipo kwa sasa) na ya Tanzania Bara( ambayo katika  katiba ya zamani imo ndani ya serikali ya Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania). Kwa  utaratibu wa tume rasimu ya katiba itajadiliwa katika mabaraza mbalimbali yalioundwa katika ngazi tofauti na baadae kwenye  bunge la katiba  na mwishowe itapigiwa kura ya maoni na itakuwa tayari mwaka 2014. Serikali , inataka   katiba hii ianze  kutumika katika uchaguzi wa mwaka 2015.
 
Angalizo langu:
Iwapo  katiba hii  itapita katika mchakato mzima na ikakubalika kwa wananchi kwamba  tuwe na serikali tatu. Serikali  ya Muungano itakuwa na katiba, Serikali ya Tanzania Zanzibar  wanayo katiba yao, Serikaliya  Tanzania bara itakuwa haina katiba yake, hivyo basi  tutabidi  tuanze  mchakato mpya  wa kupata  katiba ya serikali ya Tanzania bara mwaka 2014. Hili linaweza  kuchukua muda mrefu na pengine kuchelewesha au  kuhairisha  uchaguzi wa mwaka  2015.
 
Sijui serikali na wanasiasa wanaliangaliaje  hili.
Wadau wa Globu ya Jamii je mna mawazo gani  kuhusu angalizo hili?


Mdau wa KATIBA

KUTANA NA ALVIN KIJANA WA KITANZANIA AISHIYE SINGAPORE ANAYEFANYA MAKUBWA NA KAMPUNI YA NOKIA

$
0
0
Alvin Walter Makundi ni kijana mdogo wa Kitanzania anayeishi na wazazi wake nchini Singapore. Akiwa na umri wa miaka 14 na mwanafunzi wa kidato  cha pili  huko Singapore, tayari ameshatumbukiza jina lake katika orodha ya wataalamu wa application katika moja ya makampuni makubwa duniani ya kutengeneza simu za mkononi ya NOKIA, ambapo anatengeneza applications ambazo  anazituma katika kampuni hiyo ambayo nayo bila hiana huitumia. Kwa idhini ya mama yake Globu ya Jamii ilipata fursa ya kuongea naye kuhusu hayo maajabu anayoyafanya. Msikilize. hapo chini...

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Bw. Walter P. Makundi, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio Singapore siku alipokutana na kuzungumza nao. Bw. Makundi, ambaye ni Meneja mradi wa kampuni kubwa ya ujenzi ya APCO PTE LTD ya hapo Singapore, ndiye baba mzazi wa Alvin. Kulia kwake ni mkewe, Mama Alvin.
Chini Rais Kikwete akisalimiana na Alvin ambaye aliongozana na mama yake pamoja na dada kuja kumuaga wakati Rais akiondoka Singapore usiku huu.

The Best Thing Africa Has To Offer

BIG BROTHER: THE CHASE,HEARTS TRUMP HEADS IN THIS WEEK’S NOMINATIONS

$
0
0
The housemates on Big Brother: The Chase may have struggled to nominate each other for eviction after just 24 hours in the game last Monday, but this week DStv audiences saw how alliances, relationships and grudges fuelled a tense nomination day in the houses. 

When the dust had settled and the Heads of House had had their say during Monday night’s first nomination show, Ruby housemates Koketso & LK4 and Diamonds Feza, Hakeem & Dillish found themselves up for eviction this week but the final decision is now all up to the viewers!

Following a shocking first set of evictions, which saw Huddah and Denzel leave on Sunday, it was time for housemates to sharpen their minds on who they will be nominating. The Diamonds’ nominations saw Bolt lead the pack with 5, followed by Hakeem and Dillish with 4 each.

 The bulk of the housemates cited Bolt’s perceived laziness as a motivating factor for their nominations, while Hakeem was put in the firing line because the housemates felt he was clearly not happy to find himself in the Diamond house. Bimp and Fatima avoided nomination altogether.

Diamond Head of House Betty was only ever going to save one housemate as part of her ‘save & replace’ decision – and didn’t disappoint by saving love interest Bolt from the block and putting Feza up for eviction in his place. Relations between Betty and Feza have been rocky since day one, with the Tanzanian nominating the Ethiopian last week and also putting her up for eviction in Elikem’s place.

Once the Rubies had spoken, Biguesas had picked up 5 nominations while LK4 got 4. 

The housemates predominantly cited Biguesas’ lack of participation in life in the house as their reason for nominating him, while many seem to be seeing LK4 as being particularly manipulative. Neyll has received a frosty reception since being swapped over during the Airtel Arena Showdown last week, reflected in the nominations he received.

Selly, in her role as Ruby Head of House, also let her heart lead her ‘save & replace’ decision, sparing Biguesas and replacing him with Koketso.

So, there are three ways to vote to keep your favourite housemate in Big Brother: The Chase - via web, SMS or mobile site – and you can win amazing prizes in the process, like DStv HD PVR’s and DStv Walkas. Voting opened immediately after Monday night’s nomination show and closes at 07:00 on Sunday morning

To vote via web or mobile site, go to the official Big Brother website, www.bigbrotherafrica.com , log in, click ‘Vote’ and then click the appropriate button for the housemate you’d like to keep in the house. You may vote once per hour.

To vote via SMS, send the word VOTE, followed by the name of the housemate you’d like to keep in the game, to the number for your country below. SMS’s are charged at specified network tariffs in the various countries. VAS rates apply.

 Free minutes do not apply. Please note that you can vote 100 times by SMS per telephone number during each voting period.

Tanzania

Vodacom 15456 TZS 600
Tigo 15456 TZS 600
Zantel 15456 TZS 600
Airtel 15456 TZS 600

Big Brother: The Chase fans can catch all the latest news, video, and all-important voting information at www.bigbrotherafrica.com.

Stay tuned to DStv channels 197 and 198 for all the Big Brother: The Chase action 24/7 for the next three months, or catch the daily shows on AfricaMagic Entertainment at 21:00, Tuesday-Friday with highlights of the week on Saturday at 21:00.

Miondoko kwa KUMEREMETA KWENYE MNUSO

MKATAA KWAO MTUMWA

Rasimali zote zilizopo nchini ni kwa manufaa ya Watanzania wote-Kinana.!

Dereva mzembe ahukumiwa kwenda jela miezi 12 na kufungiwa Leseni yake Maisha

$
0
0
Na Bazil Makungu Ludewa

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ludewa katika Mkoa wa Njombe imemhukumu kwenda jela miezi kumi na mbili na kunywang’anywa leseni ya udereva na kisha kufungiwa kutoendesha gari lolote katika maisha yake Edward Mliwa kwa kusababisha majeraha kwa watu watano baada ya kupata ajali kwa uzembe. 

 Akisoma hukumu hiyo iliyochukua takribani masaa mawili hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Ludewa Fredrick Lukuna alisema kuwa mahakama yake imeridhika na ushahidi ulioletwa mbele yake na upande wa mashtaka na kwamba mshtakiwa atatumikia kifungo cha miezi kumi na mbili jela au kulipa faini ya sh hamsini elfu (50,000) kwa kila kosa.

Lukuna mshtakiwa Edward Mliwa anashtakiwa kwa makosa matano ikiwemo kuendesha chombo cha moto kwenye barabara ya umma kwa uzembe na kusababisha ajali iliyowajeruhi watu watano kinyume na sheria chini ya kifungu 41, 50 na 63(2) cha sheria barabarani sura ya 168.

Hakimu mkazi mfawidhi akaendelea kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Novemba 12 mwaka 2012 katika kijiji cha Masasi barabara ya Ludewa Manda wilayani Ludewa ambapo alikuwa akiendesha gari aina ya center yenye namba za usajiri T 715 AZU akiwa amebeba abiria kupita kiasi.

Awali mshtakiwa alikiri kosa moja tu ambalo ni kusababisha majeraha kwa abiria watano lakini akakana kuhusika na kosa na uzembe akiwa na chombo cha moto hata hivyo mahakama hiyo imeiamuru mamlaka ya mapato nchini TRA kuifungia leseni ya mshtakiwa maisha kutokana na makosa hayo.

Akiomboleza mahakani hapo Edward Mliwa akaiomba mahakama kumwonea huruma na kumpunguzia adhabu kwa sababu anayofamilia inayomtegemea, hata hivyo alilipa faini na kupona kwenda jela.

watoto watukutu wakipewa mafunzo wanabadilika na kuwa watoto wema - MAMA SALMA KIKWETE

$
0
0
Na Anna Nkinda – Singapore

Watoto waliotengwa na jamii kutokana na tabia ya kutokuwa na maadili mazuri (watukutu) kama watapewa nafasi ya kupata mafunzo ya kutosha ya dini, elimu ya darasani na kuonyeshwa msingi mzuri wa maisha wanaweza kubadilika na kuwa watoto wema.

Hayo yamesemwa leo na Mama Sahnim Sokaimi ambaye ni mkuu wa kituo cha kurekebisha tabia za watoto wa kike watukutu cha PERTAPIS kilichoko nchini Singapore wakati akiongea na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alipotembelea kituo hicho.

Alisema kuwa chuo hicho kinawapokea watoto wa kike kuanzia umri wa miaka 12 hadi 21 ambao mahakama imewakuta na makosa mbalimbali ikiwa ni pamoja na uvutaji wa sigara chini ya miaka 18, utumiaji wa madawa ya kulevya na kufanya biashara ya kuuza mwili (sexual activities).

Wadau wakiwa katika mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi unaoendelea mjini Bonn Ujerumani.

$
0
0
kushoto Bw Sheha Mjaja Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Zanzibar, na Kulia ni Bw. Emmauel Tutuba kutoka wizara ya fedha, wakifuatilia jambo katika mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi unaoendelea mjini Bonn Ujerumani.picha na Evelyn Mkokoi

NANI WA KUIBUKA NA TAJI LA REDD'S MISS SINZA LEO?

$
0
0
Warembo 11 kati ya 12 wanaopanda jukwaani leo kuwania Taji lenye Sifa Kuu mbili ya Redd's Miss Sinza 2013, lakini pia linaloshikiliwa na Redd's Miss Tanzania 2012-2013, Brigit Alfred, leo katika Ukumbi wa Meeda Club uliopo Sinza Mori. Katika shindano hilo litakalosindikizwa na burudani kabambe kutoka kwa Bendi mahiri ya African Stars, 'Twanga Pepeta', viingilii vitakuwa ni Sh. 20,000/= kwa VIP na Sh. 10,000/= kwa viti vya kawaida. Shindano hili limedhaminiwa na Redds Original, Mtandao wa Sufianimafoto Blog, Dodoma Wine, Chilly Willy Energy Drink, Fredito Entertainment, CXC Africa, Clouds Media Group na Salut5.com.
Hapa wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mazoezi yao....ya maandalizi.... Picha na www.sufianimafoto.com

SOMKI - FURSA YA UDHAMINI KWA AJILI YA WANAFUNZI WA KIKE WENYE VIPAJI LAKINI HAWAJIWEZI

$
0
0

Tunayo furaha kuwafahamisha kuwa kuna nafasi za udhamini kwa ajili ya wanafunzi wa kike wenye vipaji lakini wasiojiweza, chini ya Mradi wa Somesha Mtoto wa Kike (SOMKI). Mradi wa SOMKI unaleta utofauti katika maisha ya wanafunzi wa kike wa Tanzania wanaoishi katika mazingira magumu na wasiojiweza na ambao wameonyesha vipaji maalum au imeonekana kuwa na uwezo wa kufanya vizuri katika masomo yao na kufikia viwango vya juu au daraja la kwanza katika mitihani yao.


Udhamini huu ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba hawaathiriki na hali yao ya kimaisha ya sasa na kwamba wanaweza kupata fursa ya kubadilisha maisha na kuwa na maisha bora. Baada ya mchakato wa uhakiki na tathmini ya uhitaji itawapa walengwa fursa ya kupata elimu na kuwapunguzia mazingira magumu wanayoishi na kujisomea.


Tunaelewa kuwa katika shule yenu au utakuwa na taarifa kuwa kuna wanafunzi wanaostahili kupata nafasi hii. Kwa barua hii tunaomba uweze kusambaza taarifa hii na kuhamasisha wale wanaostahili kutuma maombi yao. Tafadhali nafasi hizi hutolewa mara moja tu kwa mwaka. Maombi haya yako wazi hadi kufikia tarehe 30 Desemba 2013, kwa ajili ya wanafunzi watakaodhaminiwa kitaaluma na Mradi wa SOMKI kwa mwaka 2014.


Maombi yatumwe kwenye anuani iliyopo hapo chini. Na kwa maelezo zaidi msisite kututafuta kwa anuani iliyopo hapo chini na namba ya simu.


Mlalakuwa,  Mikocheni,  
Plot No: 36 B,  
P.O. Box 71821, 
 Dar es Salaam, Tanzania 
Email: sophiamkana@yahoo.com
Tel: +255-0656 647 280


Wenu mtiifu,


 Jane M

Mratibu wa Mradi 

WAZIRI WA HABARI UTAMADUNI UTALII NA MICHEZO ZANZIBAR ATEMBELEA KITUO CHA KURUSHIA MATANGAZO YA RADIO BUNGI

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk (wakatikati)akisikiliza maelezo kutoka kwa Fundi Mkuu wa Zbc Radio Ali Aboud alievaa kanzu kushoto kutokana na kuunguwa kwa Kifaa cha Waya wa Cable na kusababisha Radio kutokusema kwa siku kadhaa kwa kutumia masafa ya Kati (Midium Wave) hapo katika kituo cha kurushia matangazo Bungi Wilaya ya Kati Unguja.
Mhandisi wa Kichina Zhao Wei Min akitoa ufafanuzi wa Kifaa cha Waya wa Cable kilichoungua na kusababisha Radio kutokusema kwa siku kadhaa kwa kutumia masafa ya Kati (Midium Wave)mbele ya Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk alipofanya ziara makusudi ya kuangalia matatizo hapo katika kituo cha kurushia matangazo Bungi Wilaya ya Kati Unguja.
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk wakwanza kulia akitoa maelekezo kwa wafanyakazi kuhusu namna ya kutatua tatizo la kuungua kwa Kifaa cha waya wa Cable ambacho kimesababisha Radio kutokusema kwa siku kadhaa kwa kutumia masafa ya Kati (Midium Wave) hapo katika kituo cha kurushia matangazo Bungi Wilaya ya Kati Unguja. PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.

Airtel yaongeza muda vifurushi vya Airtel Yatosha, sasa huduma masaa 25 kwa siku

$
0
0
  Airtel Tanzania imeendelea kutimiza dhamira yao ya kuwapatia wateja wake unafuu zaidi kupitia huduma yake ya AIRTEL YATOSHA nchini ambapo sasa wateja watafurahia Vifurushi vya Airtel Yatosha kwa masaa 25 kwa siku,   hii itawawezesha watanzania kufurahia kupiga simu mtandao wowote kwa gharama nafuu kwa muda mrefu zaidi.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa Airtel yatosha masaa 25 Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alisema” kuanzia sasa, huduma ya Airtel yatosha kwa siku itakua kwa masaaa 25 kuanzia pale mteja anapojiunga na huduma, yaani masaa 24 ya kuongea na kama vile haitoshi Airtel yatosha inakuongezea saa jingine moja la ziada. Sasa wateja wa Airtel watafurahi kupiga simu kwa gharama nafuu na kwa muda zaidi kuliko ilivyokuwa awali”.

 “Hii ni ya kwanza na pekee kutoka Airtel, Airtel yatosha itaendelea kuwa suluhisho la mawasiliano ya huduma za simu kwa watuamiaji na wateja wa Airtel nchi nzima ”. aliongeza Mmbando

Airtel yatosha ni huduma iliyoanzishwa ili kuleta kuvunja mipaka kwa watanzania na kuwawezesha kuwasiliana ndani na nje ya mtandaa kwa gharama nafuu. Kujiunga na huduma hii  piga *149*99# na atapata majibu papo hapo achague unataka Yatosha WIKI au Yatosha SIKU au Tosha ya Mwenzi.

TAIFA STARS YAIKABILI MOROCCO UGENINI KESHO

$
0
0
Taifa Stars inatupa karata yake ya pili ugenini kwenye mechi za mchujo za Kombe la Dunia kwa kesho (Juni 8 mwaka huu) kuikabili Morocco (Lions of the Atlas) kwenye Uwanja wa Grand Stade hapa Marrakech, Morocco.

Ilipoteza ya kwanza ugenini dhidi ya Ivory Coast mwaka jana, na kushinda mbili mfululizo nyumbani dhidi ya Gambia na Morocco. 

Mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za Morocco ni ya pili kwa Stars katika uwanja huo ambapo mwaka juzi ilifungwa mabao 3-1.

Washabiki wa Morocco wanaonekana kuikatia tama timu yao yenye pointi mbili tu nyuma ya Ivory Coast inayoongoza kundi hilo la C ikiwa na pointi saba ikifuatiwa na Tanzania yenye sita. Huo ni mtazamo wa washabiki, lakini kwa upande wa timu inaonekana imepania kujichomoa katika nafasi za chini.

Kwa upande wa Kocha wa Stars, Kim Poulsen amesema timu yake imepania mechi hiyo, lengo likiwa ni kuona inapata matokeo mazuri baada ya dakika 90 za mechi hiyo itakayokuwa chini ya refa Daniel Frazier Bennett wa Afrika Kusini.

Amesema timu yake itacheza kwa umakini na uangalifu kwa vile wanajua wapinzani wao wakicheza mbele ya washabiki wao watakuwa katika shinikizo za kushinda, jambo ambalo wamejiandaa kukabiliana nalo.

Kwa upande wa maandalizi, Kim amesema Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na wadhamini wa timu hiyo Kilimanjaro Premium Lager wameiandaa vizuri kwani iko kambini kwa wiki tatu sasa na kupata mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan iliyochezwa wiki iliyopita nchini Ethiopia. 
Stars iliifunga Morocco mabao 3-1 zilipokutana Machi 24 mwaka huu jijini Dar es Salaa. Lakini zilipokutana hapa Marrakech mara ya mwisho mwaka 2011, Morocco iliibuka na ushindi wa mabao 3-1. 

Kim amesisitiza kuwa kikosi chake kimepania kufanya vizuri katika michuano hii ya mchujo ya Kombe la Dunia, ha hiyo inathibitishwa na matokeo ya timu kadri inavyoendelea kucheza mechi za mashindano.

“Moja ya mipango yetu katika mechi hizi za Kombe la Dunia ni kushinda nyumbani, hilo hadi sasa tumelifanya kwa asilimia 100. Lakini ili tukae vizuri zaidi tumekuja hapa Morocco kwa lengo la kupata matokeo mazuri, ingawa tunajua mechi itakuwa ngumi,” amesema kocha huyo raia wa Denmark. 
Kwa hapa Marrakech mechi hiyo imekuwa haizungumzwi mara kwa mara, na kubwa ni kuwa Wamorocco wengi wanaamini kuwa timu yao ambayo hadi sasa ina pointi mbili haina nafasi ya kusonga mbele katika hatua inayofuata ya michuano hiyo.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Marrakech, Morocco

ujumbe wa leo

Viewing all 110000 articles
Browse latest View live


Latest Images