Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

FIFA YAAGIZA YANGA KUMLIPA BRANDITS, HATIHATI KUPOKWA POINTI

$
0
0
Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA), limeitaka Klabuya Yanga  kulipa  deni la aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, Ernest Wilhelmus Johannes Brandts - Raia wa Uholanzi waliyevunja naye mkataba miaka miwili iliyopita.


Klabu ya Yanga imetakiwa kulipa dola 11,000 za Marekani kama ambavyo iliamriwa Juni 30, 2015 na Kamati ya Hadhi ya Wachezaji ya FIFA. Kwa kuchelewa kulipa fedha hizo tangu Juni, 2015 Klabu ya Young Africans imeamliwa pia ilipe fidia ya asilimia tano ya deni halisi.

Yanga  wametakiwa kulipa fedha hizo na kutuma nakala ya malipo hayo, kabla ya shauri hilo halijapelekwa Kamati ya Nidhamu. Kutolipa deni hilo kwa wakati, imetafsiriwa kwamba Klabu ya Yanga imevunja Kanuni ya 64 inayozungumzia Nidhamu katika FIFA yaani FDC (FIFA Disciplinary Committee).



Kama Yanga watashindwa kulipa kwa wakati watakabiliwa na  adhabu za kupigwa faini zaidi ya awali, kukatwa pointi katika Ligi Kuu ya Vodacom inayoendelea kwa sasa au kushushwa daraja. Kamati hiyo ya Nidhamu inatarajiwa kukutana wakati wowote wiki ijayo na suala la Nidhamu ya Yanga  litakuwa ajenda ili kama Young Africans hawakulipa, watachukua hatua kama adhabu zinavyojieleza hapo juu

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limeagizwa haraka kufuatilia suala la deni hilo katika Klabu ya Yanga na kurudisha majibu FIFA. TFF kupitia Katibu Mkuu, imeagizwa kupeleka barua ya FIFA katika Makao makuu ya Klabu hiyo.

TFF wameliweka  wazi suala hilo kama ‘Tahadhari kabla ya hatari’, kwani tungeweza kufanya mawasiliano kati ya shirikisho (TFF) na klabu  kwa siri tu, lakini ikitokea huko mbele klabu inakutana na adhabu mojawapo, lawama hushuka TFF kwa madai kwamba tumekalia taarifa muhimu ya kuchukuliwa hatua haraka.

MKURUGENZI AMVUA MADARAKA MWALIMU MKUU WA BUNDA B KWA UDAGANYIFU.

$
0
0
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Bi. Janeth Mayanja amemvua madaraka Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Bunda B, Bw. Laurent Agustino kwa tuhuma za kushiriki kusaidia mwanafunzi mmoja kufanya udanganyifu katika mtihani wa darasa la nne.

Mwalimu huyo anatuhumiwa kumruhusu mwanafunzi wa darasa la tano kufanyia mtihani wa mwanafunzi wa darasa nne kwa lengo la kumsaidia mwanafunzi huyo ambaye hajui kusoma wala kuandika ili aweze kufaulu.

Mkurugenzi huyo ametoa kauli hiyo leo wakati wa mahojiano na mwandishi wa habari hizi.

Kufuatia tukio hilo Bi. Janeth ametoa onyo kwa walimu wote wa shule zilizofanya vibaya na kuwataka kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani kwa mwaka 2017 na kuahidi kuwavua madaraka walimu wa shule zitakazofanya vibaya.

Aidha, Mkurugenzi huyo wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda amewataka walimu wakuu, waratibu na walimu wote kutekeleza kutekeleza majukumu yao kulingana na sheria na kanun9 a utumishi wa Umma.

Mkurugenzi huyo amezizawadia shule kumi za Msingi zilizofanya vizuri katika mtihani wa kumaliza Darasa la saba kwa mwaka 2016 kwa ajili ya kuboresha kiwango cha elimu katika eneo hilo.

Utaratibu huo ulenga kutoa hamasa kwa wanafunzi na walimu wilayani humo na kuongeza juhudi katika kufundisha na kujifunza kwa ajili ya kuongeza kiwango cha ufaulu katika Halmashauri hiyo.

Amezitaja shule zilizoingia kumi bora ni pamoja na Olympus, Daystar, St. Paul, Mzuma, Kabarimu B, Bigutu, Bukore, Kung’ombe, Kabarimu A na Bitaraguru ambazo zote zimetunukiwa vyeti vya kutambua mchango na juhudi wanazofanya.

Mayanja alisema kuwa kati ya shule hizo nne ni shule binafsi na sita za Serikali ambazo ambapo pamoja na zimekabidhiwa hundi za fedha.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Bi. Janeth Mayanja

MAKONDA ATAJA LIST YA WAUZA MADAWA YA KULEVYA,WEMA SEPETU,TID,MR BLUE WATAKIWA KUJISALIMISHA POLISI

$
0
0
Na Anthony John, Globu Jamii.

MKUU wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amewataja baadhi ya Maafisa wa Jeshi la polisi wanao shirikiana na watu wanaojihusisha na uuzwaji wa dawa za kulevya.

 Akizungumza na waandishi wa Habari mapema leo hii jijini hapa amesema Serikali ya awamu ya Tano haito vumilia vitendo vya uuzwaji wa dawa za kulevya na kutoa agizo kwa jeshi la polisi kuwakamata Maafisa wote wa jeshi la polisi waliotajwa kushirikiana na wauza madawa ya kulevya mpaka pale uchunguzi utakapo kamilika.

 "nimepata taarifa kuwa baadhi ya Askari wa Jeshi polisi wanajihusisha na uuzwaji wa madawa ya kulevya na wengine wamekuwa na utaratibu wa kwenda kuchukua pesa kila jumamosi kwa wauzaji wa madawa ya kulevya na ndio maana biashara hii inaendelea kuwepo kwakuwa wanashirikiana na wauzaji" amesema Makonda.

 Wakati huo huo Makonda amewataka wale wote waliotajwa kuhusika na kuuza dawa za kulevya wanatakiwa kufika katika kituo cha polisi  kati kwaajili ya mahojiano.
 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akipitia orodha ya majina ya maafisa wa wanaotuhumiwa kujihusisha ya biashara ya madawa ya kulevya.

KAMATI YA UTENDAJI, BARAZA LA WADHAMINI SIMBA LAMALIZA TOFAUTI ZAO

$
0
0

Mwenyekiti wa Baraza La Wadhamini wa Simba Mzee Hamis Kilomoni (katikati) akiwa ameshikana mikono na viongozi wa kamati ya utendaji wa Simba, Rais wa Klabu ya Simba Evance Aveva, Mkuu wa kitengo wa habari na mawasiliano Haji Manara, Mjumbe wa kamati ya utendaji na mwenyekiti wa kamati ya usajili Zacharia Hanspope.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii



Baraza la Wadhamini wa Klabu ya Simba limekubali yaishe baada ya kukutana leo na na Kamati ya utendaji ya Klabu hiyo na kuwataka wapeleke mpango kazi wa mabadiliko ili kufikia maamuzi yatakayokuwa na manufaa ndani ya klabu hiyo kongwe hapa nchini.

Mwenyekiti wa Baraza hilo, Mzee Hamis Kilomoni alisema wanatambua kila binadamu anafanya makosa na kama mtu akifanya kosa hakuna budi kumsamehe na kushirikiana kufanya mambo mbalimbali ambayo yataleta maendeleo.

Alisema Kamati hiyo ilifanya vikao vyake na kugundua Uongozi wa Simba kwa ujumla ulikosea kufanya maamuzi yake na kuamua kuwasamehe kwa yote waliyoyakosea ili kukamilisha mchakato wa mabadiliko ya uendeshaji wa klabu hiyo kutoka kumilikiwa na wanachama na kuelekea kwa mwekezaji mmoja. Ikumbukwe kuwa baraza hilo liligomea hatua za mabadiliko ya uendeshaji wa klabu hiyo yaliyotangazwa kufanywa na kamati tendaji tangu mwaka jana kwa madai ya kutotimiza matakwa mbalimbali ya kisheria ikiwemo kupuuzia baraza hilo linalotambulika kisheria.

"Niwajulishe mashabiki wa Simba kwa ujumla kwamba sisi hatuna ugomvi na Kamati tendaji ya Simba lakini kilichokuwa kikifanyika ni kuwashtua watekeleze matakwa yale tuliyokuwa tukiwaeleza kwa muda mrefu na wao walikuwa hawajayatekeleza kikubwa zaidi hakuna mtu anayekataa mabadiliko na sisi kama bodi ya wadhamini ya Simba SC ambao tunapenda kuona mafanikio ya klabu tumewaagiza hawa viongozi watuletee mpango kazi ili tujue ni namna gani mabadiliko hayo yatakavyokuwa na msaada kwa klabu kiujumla," alisema Kilomoni.

Kilomoni aliendelea kusisitiza kuwa licha ya kuwataka viongozi wa klabu hiyo kupeleka mpango kazi ili wafanye mabadiliko, Viongozi hao wanapaswa kutambua mali zilizopo katika klabu hiyo ni za Simba hazitokwenda kwa yeyote badala yake zitaendelea kubaki chini ya baraza la wadhamini kama ilivyokuwa kipindi chote na mali za klabu hiyo sio za mchezo wa mpira wa miguu pekee bali zinauhusiano na michezo mingine licha ya kuwa kwa sasa haipo katika klabu hiyo.

Wakati huo huo, Rais wa Klabu hiyo, Evans Aveva alisema kumekuwa na taarifa za kutokuwepo kwa maelewano chanya kati ya Uongozi wa klabu hiyo na baraza la wadhamini jambo ambalo limemsukuma na kujitokeza kulizungumzia ili kuwajuza watanzania kwamba hakuna tatizo lolote.

Alisema kilichokuwa kikitokea katika klabu hiyo ni changamoto za kufanya kazi kwa pamoja na sehemu zote zinazowakutanisha watu mbalimbali kutokea kwa baadhi ya watu kukubali jambo fulani na wengine kutokubali ni lakawaida na halishangazi sana kwa kuwa Simba sio ya kwanza kupitia hilo.

Alisema uongozi wa Simba umekuwa ukifanya kazi kwa ushirikiano na mamlaka zote zilizopo katika klabu hiyo ili kuhakikisha inapata mafanikio yale waliyoyapata kwa wakati waliojipangia na kuahidi kufanyia kazi kwa wakati maelezo yaliyotolewa na baraza la wadhamini.
Rais wa Klabu ya Simba Evance Aveva akizungumza na waandishi wa habari juu ya mustakabali wa uhalali wa Simba na bodi ya wadhamini na kukubaliana kuweka wazi michakato yote ya mabadiliko ya klabu hiyo, kulia ni Mwenyekiti wa Baraza La Wadhamini wa Simba Mzee Hamis Kilomoni.
Mwenyekiti wa Baraza La Wadhamini wa Simba Mzee Hamis Kilomoni akizungumza na waandishi wa habari juu ya mustakabali wa uhalali wa Simba na bodi ya wadhamini na kukubaliana kuweka wazi michakato yote ya mabadiliko ya klabu hiyo.

Dawasco kinondoni yaendelea kubadilisha mita za maji

$
0
0
Meneja wa DAWASCO Mkoa wa Kinondoni Judith Singinika (Aliyesimama) akiwa na fundi kutoka DAWASCO wakibadilisha mita chakavu na kuweka mita mpya ya Maji katika maeneo ya Barabara ya Dunga Mtaa wa Isere, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt Magufuli ateua Mkuu wa Majeshi na Mnadhimu Mkuu

$
0
0





Luteni Jenerali Venance Mabeyo ambaye ameteuliwa na Rais Dkt Magufuli kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania




BBC DIRA YA DUNIA ALHAMISI 02/02/2017

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI


Taarifa ya Mauaji ya Kondakta Tanga

$
0
0

 


JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA

KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO


Simu ya Upepo  : “N G O M E”        Makao Makuu ya Jeshi,

Simu ya Mdomo: DSM 22150463     Sanduku la Posta 9203,

Telex                   : 41051                       DAR ESSALAAM, 31 Januari, 2017.

Tele Fax              : 2153426

Barua pepe       : ulinzimagazine@yahoo.co.uk

Tovuti                  : www.tpdf.mil.tz


Taarifa kwa Vyombo vya Habari


Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania limesikitishwa na taarifa iliyotolewa na gazeti la Tanzania Daima toleoNambari 4438 la tarehe 28 Januari 2017, Habari leo   la tarehe 29 Januari 2017 na baadhi ya vyombo vya habari vikihusisha mauaji ya kondakta wa daladala na Wanajeshi Mkoani Tanga.


Tunapenda  kuwataarifu wananchi kwamba kwa mujibu wa jeshi la polisi watuhumiwa wanaoshikiliwa na Jeshi hilo ni wanne (4),mmoja kati yao ni Mwanajeshi ambaye ni mzazi wa msichana anayetuhumiwa kusababisha tukio hilo. 

Hivyo Mwanajeshi huyo anashikiliwa kwa ajili ya kulisaidia Jeshi la Polisi katika uchunguzi kwa kuwa tukio hilo lilifanyika nyumbani kwake. Hakuna Wanajeshi waliohusika katika tukio hilo kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari, kambi za Jeshi wanaishi Wanajeshi pamoja na familia zao hivyo kuhusisha moja kwa moja mauaji hayo na Wanajeshi  mkoani Tanga ni kuupotosha umma.

Wito unatolewa kwa vyombo vya habari kuripoti habari zenye ukweli.Habari zisizo za kweli zinapotosha umma na kujenga taswira potofu kwa wananchi dhidi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.  


Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano

Makao Makuu ya Jeshi, Upanga

S.L.P  9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.


Kwa Mawasiliano zaidi: 0756-716085

AVEVA AWATAKA WANACHAMA 71 WA SIMBA KUFUTA KESI MAHAKAMANI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Raisi wa klabu ya Simba Evance Aveva amewataka wanachama 71 wa klabu hiyo waliofungiwa kushiriki shughuli mbalimbali za klabu hiyo kutokana na kosa la kupeleka mahakamani masuala ya soka, kwenda kuifuta kesi hiyo mahakamani ili waweze kuruhusiwa kuendelea kuwa wanachama halali.

Aveva aliyasema hayo wakati wakizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam, kitendo kilichofanywa na wanachama hao kilikuwa na kinyume na katiba ya klabu hiyo, TFF pamoja na katiba ya FIFA, hivyo kupelekea kamati tendaji kwa pamoja kuchukua maamuzi ya kuwafungia ili kuwakumbusha kanuni wanachama wa klabu hiyo ambao walikuwa na lengo la kufanya kama walivyofanya wao.

"Kila mmoja natumaini sio mgeni wa kanuni zinazoendesha soka letu na tumeamua kuchukua maamuzi ya kuwataka wafute shitaka walilolifungua ili warudi kundini kwa sababu tumetambua ili tufanye vyema ni lazima tuwe na umoja na mshikamano kwani bila hivyo kupata mafanikio ni vigumu," alisema Aveva.

Wakati wa uongoozi wa Rais huyo wakiingia madarakani wanachama 71 waliamua kufungua kesi mahakamani na kwenye mkutano mkuu wa wanachama kwa pamoja walikubaliana kuwavua uanachama.

Aveva alisisitiza kuwa katika kuijenga Simba, wanachama kwa pamoja wanatakiwa kuwa wamoja na kushirikiana kuhakikisha inasimamia malengo na mikakati ya klabu hiyo.

Raisi wa klabu ya Simba Evance Aveva

BARAZA LA TATU LA WAFANYAKAZI MOI LAFUNGULIWA

$
0
0
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MOI Profesa Bakari Lembariti leo amezindua vikao vya Baraza la Tatu la Wafanyakazi wa MOI katika ukumbi wa IDDI NYUNDO katika halmashauri ya Temeke jijini Dar es Salaam. Vikao vimehudhuriwa na zaidi ya wajumbe 50 kutoka katika kila idara, vitengo na chama cha wafanyakazi wa MOI (TUGHE) na wajumbe wa TUGHE mkoa.

Akizindua Baraza hilo Profesa Lembariti alisema anampongeza Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli. Alisema ” Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini MOI Mh Zakia Meghji natumia Fursa hii kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa uongozi wake uliotukuka na jitihada zake za kuboresha huduma za afya hapa nchini, sote ni mashahidi“.

Aidha, Profesa Lembariti aliwakumbusha wafanyakazi wa MOI kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia maadili ya utumishi wa Umma ili kujenga imani kwa watanzania walio wengi ambao wanaitegemea MOI kama Taasisi pekee inayotoa Tiba ya kiwango cha juu cha rufaa kwenye Tiba ya Mifupa, upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu.

Pia Profesa Lembariti alisema ni vyema wajumbe wa Baraza la MOI wakatumia vikao vya Baraza kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili Taasisi ya MOI na kutafuta muarobaini ili Taasisi ya MOI iendelee kutoa huduma bora

Kwa upande mwingine Profesa Lembariti aliwakabidhi zawadi wafanyakazi Bora wa MOI kwa mwaka 2015/2016 ambapo Bwana Robert Sere aliibuka kidedea na kuwa mfanyakazi Bora wa MOI na kujipatia cheti na fedha taslimu kiasi cha Tshs Milioni 4, nafasi ya pili ikishikwa na Bwana Lucas Machage akijipatia cheti na kiasi cha Tshs Milioni 2 na nafasi ya tatu ikishikwa na Bi Betty Shila ambaye alijipatia cheti na kiasi cha Tshs Milioni 1.5

Kwa upande wake ,akiwasilisha ripoti ya utendaji wa Taasisi ya Kaimu Mkurugenzi wa MOI Dkt Othman Kiloloma alisema kutokana na ongezeko kubwa la ajali ambazo zimepelekea ongezeko kubwa la wagonjwa MOI, Taasisi ya MOI iko kwenye mpango mkakati kabambe wa kushirikiana na baadhi ya hospitali za rufaa za pembezoni kwa kuwapeleka wataalamu kutoa huduma katika hospitali hizo na kupunguza kama si kuondoa kabisa wimbi la wagonjwa wanaopokelewa MOI

Dkt Kiloloma alisema kwamba Taasisi ya MOI imeendelea kuwa Kitovu cha Weledi katika matibabu ya Mifupa ,Ajali ,Ubongo na Mishipa ya Fahamu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati ambapo mwaka 2015 MOI ilitoa utafiti bora wa mfupa mrefu wa paja duniani ,ambapo utafiti uliwasilishwa katika Taasisi ya kimataifa ya upasuaji wa mifupa duniani ya Marekani (AOTA)

Vilevile, Dkt Kiloloma aliwaomba wajumbe wa Baraza la MOI kutoa michango yenye tija ili kupata matibabu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili Taasisi ili Taasisi iendelee kutoa huduma bora kwa watanzania.

Makamu mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MOI Prof Bakari Lembariti akihutubia wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa MOI wakati wa Uzinduzi wa Kikao cha Tatu cha Baraza Hilo.
Kaimu Mkurugenzi wa MOI Dkt Othman Kiloloma akiwasilisha ripoti ya Utendaji ya Mwaka 2015/2016.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa MOI wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi Prof Bakari Lembariti
Makamu mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi MOI Prof Bakari Lembariti akimkabidhi cheti Mfanyakazi bora wa MOI kwa Mwaka 2015/2016 Bwana Robert Sere

SERIKALI ITAOKOA SH.BILIONI 900 KWA MWAKA ENDAPO IKIFANIKIWA KUTEKELEZA MKAKATI WA UWAZI KATIKA UJENZI NCHINI.

$
0
0
SERIKALI itaokoa angalau Sh.bilioni 900 kwa mwaka endapo itafanikiwa katika utekelezaji wa Mkakati Uwazi katika Ujenzi (CoST).

Aidha kupitia mkakati huo, miradi mbalimbali ya mashirika ya umma 10 inatarajiwa kufanyiwa tathmini itakayokamilika ifikapo Julai mwaka huu.

Akizungumza katika mkutano wa mashauriano ya utoaji wa taarifa za miradi ya ujenzi wa miundombinu ya umma wa baraza la wajenzi, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu, Peter Ilomo alisema kuwa mkakati huo utapunguza rushwa na upotevu wa fedha za Serikali.

Ilomo alisema CoST itaisaidia Serikali na umma kujua fedha zinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu, kuokoa fedha za umma kwa kupunguza rushwa na kuboresha usimamiaji wa utekelezaji wa miundombinu.

Mwenyekiti wa CoST, Kazungu Magili alitaja mashirika yatakayofanyiwa tathmini na kuweka wazi miradi yake kuwa ni, Wakala wa Majengo (TBA), Wakala wa Barabara (Tanroads) na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)/.

Mashirika mengine ni mifuko wa Taifa wa hifadhi ya jamii ya NSSF, GEPF, LAPF, Wizara ya Elimu na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii jinsia Wazee na Watoto na kutoa taarifa kwa umma ambapo utaweza kuitumia kufuatilia utekelezaji wa miradi husika.

Alisema kupitia tathmini hiyo, CoST itapata fursa ya kutambua majengo yaliyojengwa kwa mujibu wa vigezo ama chini ya kiwango halisi cha fedha zilizotolewa na thamani ya jengo husika.

Magili alisema ikitokea kuna baadhi ya miradi imejengwa chini ya kiwango itafikishwa katika mamlaka mbalimbali ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) ili hatua mbalimbali zichukuliwe.

Aidha alisema kuwa awali kabla ya kuanzishwa mkakati huo mambo mengi yalikuwa hayawekwi wazi hali ambayo imekuwa ikisababisha upotevu wa fedha.
Kaimu Mtendaji Mkuu Baraza la Taifa la Ujenzi,Elias Kissamo akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa mchakato wa utoaji wa taarifa za miradi ya ujenzi wa miundombinu ya umma katika ukumbi wa Holiday Inn jijini Dar es Salaam jana. (PICHA NA ELISA SHUNDA)
Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Ikulu,Peter Ilomo,akifungua mkutano wa mchakato wa utoaji wa taarifa za miradi ya ujenzi wa miundombinu ya umma katika ukumbi wa Holiday Inn jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mwenyekiti wa Sekta ya Uwazi na Uwajibikaji katika Ujenzi (Cost Tanzania),Mhandisi Kazungu Magili na Kaimu Mtendaji Mkuu Baraza la Taifa la Ujenzi,Elias Kissamo.
Wadau wa masuala ya ujenzi wakifuatilia kwa umakini wakati mkutano huo ukiendelea.


Mwenyekiti wa Baraza la Ujenzi la Taifa (Cost Tanzania),Mhandisi Kazungu Magili,akizungumza katika mkutano huo. 
Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Ikulu,Peter Ilomo akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Baraza la Taifa la Ujenzi Tanzania na wadau wa masuala ya ujenzi nchini.(www.elisashunda.blogspot.com)

SIKU YA SHERIA NI SIKU AMBAYO WANANCHI HUPATA MSAADA WA KISHERIA - Mruma

$
0
0
Na Pamela Mollel,Arusha 
 Imeelezwa kuwa siku ya sheria ni siku ambayo wananchi wanapata fursa ya kupata msaada wa kisheria ambayo kila mwananchi anapaswa kuwa chini ya shieria na sio juu ya sheria. 
 Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakili wa kujitegemea Mruma aShabibu kutoka kampuni IRM Legal alisema kuwa siku hii ni maalum kwa mawakili kutoa huduma za kisheria kwa jamii bila malipo yeyote. 
 Alisema kuwa kwa siku hii watu wengi ufaidika kwa kutatuliwa baadhi ya matatizo yao bila kutozwa gharama yeyote ikiwa ni pamoja na kupata elimu ya kisheria sanjari na kupata fursa ya kubadilishana mawazo na mawakili. 
 Alidai kuwa wananchi wanapaswa kuheshimu katiba lakini pia na kukaa chini ya sheria ili haki iweze kutendekea kwani baadhi ya wananchi wanakaa juu ya sheria hali ambayo inawafanya kujiona hawatendewi haki. 
 Hata hivyo alifafanua kuwa lengo la kuanzishwa kwa siku hii ni kuangalia umuhimu wa sheria katika jamii na kuona jinsi inavyofanya kazi katika kukuza uchumi wa nchi
Wakili wa kujitegemea Mhe. Mruma aShabibu kutoka kampuni  IRM Legal  anasema kuwa siku hii ni maalum kwa mawakili kutoa huduma za kisheria kwa jamii bila malipo yeyote.

CAMEROON KUKIPIGA NA MISRI FAINALI YA AFCON, WAICHAPA GHANA BAO 2-0

$
0
0
Timu ya Taifa ya Cameroon imefanikiwa kutinga fainali ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) yanaoendelea kufanyika kule nchini Gabon, baada ya kufunga timu ya Ghana goli 2-0 yaliyowekwa mikiani na Ngadeu Ngadjui (dakika ya 72) na Christian Bassogog (dakika ya 90). kwa matokeo hayo, Timu ya Cameroon itakutana na Timu ya Misri katika mchezo wa fainali utakachezwa Februari 5, 2016 katika dimba la Libreville, nchini Gabon.

DC MUFINDI: UKATAJI MITI OVYO NI CHANZO CHA MVUA CHACHE NCHINI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Mufindi amewataka wananchi Wilayani Mufindi, kujenga utamaduni wa kupanda miti na kuacha tabia ya kuharibu miti na misitu kwa kuichoma moto na kuikata ovyo sanjari  na tabia ya kuishi ndani ya misitu kwani kwa kufanya hivyo ni kutenda kosa la jinai kwa mujibu wa sheria za misitu.

Tarifa ya kitengo cha habari na mawasiliano cha halmshauri ya Wilaya ya Mufindi, imebainisha kuwa, Mkuu huyo wa wilaya ameyasema hayo kupitia hotuba  iliyosomwa kwa niaba yake na katibu tawala wa Wilaya Bw. Aberdi Mwela wakati wa uzinduzi wa siku ya upandaji miti kiwilaya iliyofanyika kwenye eneo la Jeshi la Magereza katika kijiji cha Ikongosi juu Wilayani Mufindi.

Mkuu huyo wa Wilaya ameongeza kuwa, serikali iliamua kutunga  sheria hiyo baada ya kuona kumekuwa na uharibifu mkubwa wa misitu na mazingira tabia ambayo husababisha mabadiliko ya hali ya hewa , kuongezeka kwa hewa ya ukaa, kupungua kwa kiasi cha mvua na kubadilika kwa majira yake, kupungua kwa mazao mashambani pamoja na kuongezeka kwa joto duniani.

Aidha, ameongeza kuwa, siku ya upandaji miti nchini, inawakumbusha wakazi wote wa Mufindi, Mkoa wa Iringa na hata Taifa kwa ujumla wake, kuzingatia utunzaji wa miti, misitu na mazingira kwa kupunguza ukataji miti ovyo na kuongeza kasi ya upandaji miti ili kupunguza uharibifu wa mazingira kwani ukwasi tunaoweza kuwanao sanjari na uhai tulionao unategemea sana uwepo wa mazingira rafiki kwa mwanadamu na kuongeza kuwa viumbe vyote chini ya dunia vinategemea miti ili kuishi.

Halmahauri ya Wilaya ya Mufindi ni moja kati ya halmshauri zinazo shika nafasi za juu nchini kwa sifa ya kupanda miti ikiwa na misitu mikubwa huku baadhi ya vijiji vyake vikinufaika na mamilioni ya fedha kupitia  mradi wa kiduni wa kupambana na  hewa ukaa duniani.
katibu tawala wa Wilaya ya Mufindi Bw. Aberd Mwela akipanda mti wakati wa uzinduzi alipomwakilisha Mkuu wa Wilaya.
Wananchi wa kata ya Ikongosi wakiwa wamejitokeza kwa wingi kumsikiliza mgeni wa heshima na kushiriki upandaji miti uliokuwa ukifanyika katika shamba la Magereza kama sehemu teule ya uzinduzi.

VEROSSA LAINGIA MTARONI USIKU HUU

$
0
0
 Gari ndogo aina ya Toyota Verossa yenye namba za usajili T 957 CPB likiwa ndani ya mtaro ulipo kando ya barabara ya Mandela, eneo la Tabata Relini jijini Dar es salaam usiku huu, baada ya kupiga mweleka. haikufahamika kwa haraka chanzo cha gari hiyo kupiga huo mweleka huo. hakuna alieripotiwa kupoteza maisha katika ajali hiyo.
Lori lenye "winch" likiwa eneo la tukio ili kuweza kuichomoa gari hiyo mtaroni. 

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 3,2017

Wafanyabiashara wa Tanzania tupo tayari kwa ubia- Dkt Mengi

$
0
0

Wafanyabiashara wa Tanzania wamesema wapo tayari kwa kufanya ushirikiano wa kibiashara wa ubia na wafanyabiashara kutoka nje ili kukuza diplomasia ya kiuchumi na mataifa mengine.

Akizungumza katika hafla ya chakula cha mchana na mabalozi wa Tanzania nje ya nchi kilichoandaliwa na Taasisi ya sekta binafsi (TPSF) nchini, Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Dkt. Reginald Mengi amesema wafanyabiashara watanzania si omba omba na wapo tayari kwa kufanya biashara ya ubia na wenzao.

“Napenda kusisitiza kwamba sisi watanzania si omba omba kwa wafanyabishara wa nje, tuna nia uwezo, ujuzi na tunajiamini kwa kufanya biashara za kimataifa kwa ubia ili kukuza uchumi wa nchini zetu,” amesema Dkt. Mengi.

Amesema kwamba fursa za uwekezaji zipo nchini kwenye sekta za kilimo, mafuta, gesi, usindikaji na mawasiliano ila ni muhimu kuunganisha nguvu za wafanyabiashara ili kuweza kupata matokeo chanya.

Dkt. Mengi alilisisitiza kwamba sekta binafsi nchini ina imani kubwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli katika adhma yake ya kukuza sekta ya viwanda ili kutatua tatizo la ajira na kuongeza mapato ya nchini.

“Ni muhimu kuimarisha sekta binafsi ili iweze kutoa mchango mkubwa katika uanzishwaji wa viwanda hapa nchini, kwa vyovyote vile sekta hii binafsi ndio itakayojenga viwanda hapa Tanzania,” aliongeza

Kwa Upande wa Mabalozi, Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye anakwenda kuiwakilisha nchi huko Brazil, amesema kwamba mabalozi ni kiungo muhimu kati ya wananchi wa mataifa husika katika kukuza mahusiano na ushirikiano wa kimataifa.

“Sisi ni wawakilishi wenu huko kwenye mataifa ya nje na zaidi na kukuza mahusiano au diplomasia ya kiuchumi kwa maslahi ya wananchi wetu,” amesema Dkt. Nchimbi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Bw. Godfrey Simbeye akiwasilisha 'presentation' iliyoainisha maeneo muhimu ya fursa za kibiashara kwenye masoko ya kimataifa kwa mabalozi wapya wa Tanzania nje ya nchi walioapishwa hivi karibuni wakati wa hafla ya chakula cha mchana kwa mabalozi hao iliyoandaliwa na TPSF jijini Dar es Salaam
 Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Dkt. Reginald Mengi akisisitiza jambo kwa mabalozi wapya watakaoiwakilisha Tanzania kwenye nchi za Uturuki, Italy, China, Brazil na UN Geneva (hawapo pichani) katika hafla ya chakula cha mchana na kuwapongeza mabalozi hao iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda nchini–CTI Dr. Samwel Nyantahe akisisitiza umuhimu wa ushirikiano katika uwekezaji, kutafuta masoko mapya, kubadilishana bidhaa na utafutaji fursa za biashara kwenye masoko ya kimataifa kwa wafanyabiashara katika hafla ya chakula cha mchana na kuwapongeza mabalozi wapya watakaoiwakilisha Tanzania kwenye nchi za Uturuki, Italy, China, Brazil na UN Geneva iliyoandaliwa na TPSF katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
 Balozi mpya wa Tanzania nchini Uturuki, Prof Elizabeth Kiondo  akitoa shukrani kwa TPSF kwa kuandaa hafla fupi kama hiyo ya kubadilishana mawazo kwa jinsi gani wanaweza kukuza diplomasia ya kiuchumi katika vituo vyao vya kazi walipopangiwa.
 Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki, akizungumza kwenye hafla hiyo  ambapo amesisitiza wafanyabiashara kutoka Tanzania watumie fursa adimu ambayo ipo kati ya Tanzania na China ambapo mahusiano na ushirikiano ulianza tangu enzi za Mao na Mwalimu Nyerere.
 Balozi wa Tanzania, Geneva, Dkt. James Msekela akisisitiza jambo kwa bodi ya TPSF kwenye hafla ya chakula cha mchana kwa mabalozi hao wapya iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

FEMINA HIP YAWAJENGEA VIJANA NCHINI UWEZO WA UONGOZI NA KUJIAMINI.

$
0
0

Na: Frank Shija – MAELEZO

FEMINA Hip yatoa tuzo tano za mwaka kwa Klabu za Fema ambazo zimefanya vizuri katika Nyanja mbalimbali.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la Kiserikali la Femina Hip Dkt. Minou Fuglesang wakati wa Kongamano la mwaka la Vijana leo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa tuzo hizo zinatolewa ili kutia chachu kwa vijana kuongeza bidi katika kutatua changamoto zao kwa kujiamnini huku wakiwa na ujuzi mwepesi utakaowaomgezea umakini katika shughuli zao.

“Tmezigawa tuzo hizi katika makundi makuu matano ambayo ni Mtandao Bora wa Klabu ya Fema ambayo imekwenda kwa Mwanza Federation Fema Clubs, Mshindi wa Pili wa Mtandao Bora wa Klabu za Fema iliyochukuliwa na Dodoma Students and Teachers”.Alisema Fuhlesang.

Tuzo zingine kuwa ni Mhamasishaji Bora wa Mtandao wa Klabu za Fema wa mwaka iliyokwenda kwa Mwalimu Christopher Mavunde, Mhamasishaji Bora wa Klabu za Fema wa mwaka iliyochukuliwa na Mwalimu Bryson Paul kutoka Ngweli FEMA Klabu – Shule ya Sekondari Ngweli wilayani Sengerema pamoja na Klabu bora ya FEMA kwa mwaka ambayo ni Kisihigh Fema Club kutoka Shule ya Sekondari Kisimiri mkoani Arusha.

Akizungumza katika mkutano huo Mkurugenzi huyo amesema kuwa FEMINA Hip imekuwa ikiendesha program za kuwakutanisha vijana ili kuwajengea uwezo katika Nyanja za mabalimabali ikiwemo uongozi kwa manufaa ya sasa na baadae. Ujuzi ambaa vijana wamekuwa wakipatiwa kutoka kwa wataalamu wa Shirika hilo ni pamoja na mawasiliano,

Kwa upande wake mshindi wa tuzo Mhamasishaji Bora wa Klabu za Fema wa mwaka 2017 Mwalimu Bryson Paul amesema kuwa Klabu za FEMA zimekuwa msingi imara wa kuwajengea uwezo wa kujitambua vijana wengi nchini hivyo ni vyema watanzania wakatambua umuhimu wa vijana wao kushiriki katika vikundi hivyo ambavyo vimekuwa na lengo la kuwajengea uwezo kwa kuwapa elimu na ujuzi mbalimbali ikiwemo stadi za maisha.

Aliongeza kuwa binafsi amefarijika kwa kuibuka kuwa mshindi katika kipengele hicho na kusisitiza kuwa siri pekee ni nidhamu na moyo wa kujifunza Zaidi kwa kushirikiana na wenzako.

FEMINA Hip imewakutanisha vijana walikatika Klabu za FEMA kutoka pande zote za nchi katika Kongamono lililofanyika katika hoteli ya Belinda Jijini Dar es Salaam, ambalo pamoja na utoaji wa tuzo pia vijana walipata fursa ya kujadiliana mambo mbalimbali kuhusu elimu na masuala mtambuka kwa vijana.  

Mkurugenzi na mwanzilishi wa FeminaHip Dr. Minou Fuglesanga kizungumza wakati wa Kongamano la mwaka la Vijana leo jijini Dar es Salaam.
Jopo la washiriki wa mjadala katika kongamano la vijana wa FeminaHip 2017 (Kushoto: Lyen Charles-Kiongozi wa Team ya Feminahip Nguvu ya binti, Mwakilishi wa One UN Tanzania –Alvaro Rodriguez, Mkurugenzi na mwanzilishi wa FeminaHip Dr. Minou Fuglesang, Naibu Kamishna wa elimu Tz (Nicholaus Burreta), Balozi wa Denmark Tanzania (Einar Jensen) na Mwakilishi kutoka ubalozi wa Sweden-Helena Reutersward . Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii. 
Mshindi wa tuzo ya mlezi bora wa Fema Club Network – Christopher Mavunde akipokkea tuzo kutoka kwa Mkurugenzi na mwanzilishi wa FeminaHip Dr. Minou Fuglesang na Balozi wa Denmark Tanzania (Einar Jensen) leo jijini Dar es Salaam. 

WABUNGE WANAWAKE WAJUMUIKA KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA JAMHURI MJINI DODOMA

$
0
0

Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiongea na Wabunge (hawapo pichani) pamoja na Waandishi wa Habari kuhusu umuhimu wa kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya leo katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma.
Naibu Waziri, Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Anastazia Wambura (Mb) akiongea na Wabunge wenzake (hawapo pichani) kuhusu umuhimu wa kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya ya miili pamoja na matarajio ya Uzinduzi wa Mazoezi yanayotarajiwa kuzinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo yatatangazwa hivi karibuni.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mhe. Ritta Kabati akiongea na Wabunge wenzake pamoja na Waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya ya miili wakati wa mazoezi ya pamoja kwa Wabunge hao wanawake yaliyofanyika leo 03/02/2017 Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. 
Mbunge wa Jimbo la Ilemela Jijini Mwanza (CCM), Mhe. Angeline Mabula akiongea na Wabunge wenzake pamoja na Waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya ya miili wakati wa mazoezi ya pamoja kwa Wabunge hao wanawake yaliyofanyika leo 03/02/2017 Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Baadhi ya Wabunge wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa wameongozana na Spika wa Bunge (wa pili kushoto) wakifanya mazoezi (Jogging) ikiwa ni sehemu ya kufanya mazoezi ya pamoja kwa ajili ya kuweka sawa miili, mazoezi hayo yamefanyika leo 03/02/2017 katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. 






Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images