Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

TMAA YAKUSANYA SH.BILIONI 79.26 KATIKA KAMPUNI ZA MADINI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA)  kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kipindi cha  Julai mpaka Desemba 2016 zilifanya ukaguzi katika baadhi ya migodi mikubwa nchini na kampuni za uchimbaji madini kulipa kodi na kufanikiwa kukusanya Sh. bilioni 79.26

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari TMAA,  Mhandisi Yisambi Shiwa, amesema fedha zilizopatikana zililipwa serikalini ikiwa ni kodi ya mapato iliyotokana na ukaguzi huo. Amesema katika ukaguzi huo Kampuni ya Geita Gold Mining Limited  imelipa Sh. biliioni 45.76  pamoja na  Kampuni ya North Mara Limited imelipa  sh. bilioni 33.5

Mhandisi Yisambi amesema  ukaguzi wa madini ya ujenzi na viwandani uliofanywa na wakala kwa kushirikiana na Ofisi za Madini Kanda za Kaskazini,Mashariki,Kusini  pamoja na Magharibi umesaidia kuongezeka kwa malipo ya mrabaha serikalini kwa  kiasi cha sh. bilioni 3.8.
‘’Kiasi cha mrabaha huo kimetokana na uzalishaji wa tani milioni 6.8 za madini ya ujenzi na viwandani yenye  thamani ya shilingi bilioni 119.5’’amesema Shiwa.

 Aidha amesema kupitia madawati ya ukaguzi yaliyopo katika Viwanja vya Ndege Nchini Wakala kwa kushirikiana na taasisi za serikali wamekuwa wakiwakamata watu wanaosafarisha madini nje ya nchi kinyume cha sheria walipigwa faini ya  Dola za Kimarekani 91,924.38 katika kipindi cha Julai na Desemba 2016.

‘’Wahusika  waliohusika na sakata la usafirishaji wa madini nje ya nchi walichukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka 2010.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha habari TMAA, Mhandisi Yisambi Shiwa Akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu shughuli mbalilmbali zinazowafanywa na wakala wa ukaguzi wa madini leo jijini Dar es Salaam. Kulia Kaimu Mkurugenzi Uzalishaji na Biashara ya Madini , Migodi ya Kati na Midogo, Mhandisi George Manyama. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

ADEBAYOR KUJIUNGA YANGA ?

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii


Kiungo wa zamani wa Real Madrid, Arsenal na Monaco Emmanuel Adebayor anatajwa kuwa muda wowote kuanzia sasa atajiunga na klabu ya Yanga ya  Dar es salaam kwa mkataba mnono.


Taarifa zilizotufikia zinamtaja nahodha huyo wa timu ya Taifa ya Togo kuwa atajiunga na timu hiyo hili waweze kutetea ubingwa na kujiandaa na michuano ya kimataifa ya klabu bingwa Afrika.


Adebayor anataka kujiunga na wana-Jangwani hao ikiwa ni siku chache baada ya timu yao ya Taifa ya Togo kutolewa katika michuano ya AFCON.

Adebayor kama atajiunga klabu hiyo ya Yanga atakuwa mchezaji wa kwanza kutoka ligi ya mabingwa ulaya kuja kucheza katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.



DIAMOND KUACHIA NGOMA MPYA NA MOHOMBI WA CONGO

$
0
0
Na Humphrey Shao, 
Globu ya Jamii

Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul a.k.a ‘Diamond Platnumz’ anatarajia kuachia video ya wimbo wake mpya uitwao Rockonolo wakati wowote kuanzia sasa, kwa mujibu wa Meneja wa Mwanamuziki huyo Jorge Mendez ambaye ameandika katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter na kuweka kipande cha Video hiyo na kusema inakuja hivi karibuni.
Video ya wimbo huo ambao inamuonesha mwanamuziki wa kimataifa kutoka nchini Congo Muhombi ambaye amefanya vizuri sana kutokana wimbo huo kutajwa kuwa ni remix ya moja ya nyimbo zake. 
Mara baada ya kuweka video hiyo katika mtandao huo Mendez amepokelewa kwa shangwe na wapenzi wa mwanamuziki huyo. Video ya Diamond na Mohombipamoja katika uzinduzi wa AFCON 2017.

Adebayor kutua Yanga???

$
0
0
Kiungo wa zamani wa Manchester City, Real Madrid, Tottenham Hotspur, Arsenal , Crystal Palace na Monaco ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Togo, Emmanuel Adebayor anatajwa kuwa muda wowote kuanzia sasa ataweza kujiunga na klabu ya Yanga ya Tanzania kwa mkataba mnono.
Taarifa zilizotufikia katika globu ya jamii zinamtaja nahodha huyo wa timu ya Togo kuwa atajiunga na timu hiyo ili waweze kutetea ubingwa na kujianda na michuano ya kimataifa ya klabu bingwa Afrika.

Adebayor anataka kujiunga na wanajangwani hao ikiwa ni siku chache baada ya timu yao ya Taifa ya Togo kutolewa katika michuano ya AFCON.

Adebayor kama atajiunga na klabu hiyo ya Yanga atakuwa mchezaji wa kwanza kutoka ligi ya mabingwa ulaya kuja kucheza katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

TANESCO YAWATOA HOFU WATEJA WAKE KUFUATIA HITALAFU YA UMEME LEO JIJINI DAR, YASEMA GRIDI YA TAIFA IKO SALAMA

$
0
0
Kaimu Meneja Mwandamizi udhibiti mifumo ya umeme TANESCO makao makuu, Mhandisi Abubakar Issa,(katikati), akionyesha kifaa kilicholipika (female connector), cha umeme wa 132kv kutoka Ubungo kwenda Chalinze. Kulia ni KaimunMeneja Uhusiano, Bi. Leila Muhaji na kushoto ni mwangalkizi mkuu wa kituo cha kupoza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam, Bw,Deodatus Ngwanda.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

SHIRIKA la Umeme Tanzania, (TANESCO), limeeleza chanzo cha kukatika umeme leo Januari 25, 2017), ni kulipuka kwa kikata umeme,(Circuit breaker), baada ya kifaa kijulikanacho kama female connector ya umeme wa 132kv kutoka kituo cha kupoza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam kwenda Chalinze mkoani Pwani kupata hitilafu.

Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Mwandamizi udhibiti mifumo ya umeme TANESCO makao makuu, Mhandisi Abubakar Issa,(pichani juu), alisema hitilafu hiyo iliyotokea majira ya saa 12;32 asubuhi, leo Januari 25, 2017 ilileta athari kwenye mfumo mzima wa gridi ya taifa na kufanya wateja wa TANESCO walio kwenye mikoa inayotumia gridi ya taifa kukosa umeme kwa takriban masaa mawili.

"Napenda kuwahakikishia wateja wetu kuwa gridi ya taifa iko salama, hakuna tatizo lolote isipokuwa ilizima baada ya kikata umeme hicho kulipuka, lakini sasa mambo yamewekwa sawa na umeme unazidi kurejea katika hali yake ya kawaida kote nchini" alisema Mhandisi Issa, wakati waandishi wa habari walipopelekwa kujionea wenyewe hitilafu hiyo majira ya mchana leo.

Hata hivyo alisema kifaa kilichoharibika kinasafirishwa kutoka mkoani Tanga, na mara kitakapowasili kitafungwa mahala kilipoharibika kile cha awali.
Hii ndiyo kikata umeme (Circuit breaker) iliyolipuka
Female Connector inayotoa umeme hapo ubunge kupeleka Chalinze mkoani Pwani ambayo ililipuka
Female connector (juu katikati) iliyolipuka
Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO makao makuu, Bi Leila Muhaji, akiwa na baadhi ya waandshi wa habari waliotembelea eneo hilo leo mchana Januari 25, 2017.

MSAADA TUTANI: OMBI LA KUWASILIANA NA WATOTO WALIOPO UINGEREZA KWA ZAIDI YA MIAKA 22 SASA.

$
0
0
Picha za awali za wahusika wa waraka huu ikiwa ni pamoja na watoto Amina na Seleman Kichawela na Bw. Mahmud Hassan Mihile aliyewachukua miaka 22 iliyopita ili kuwasaidia masomo huko Uingereza.

Kutokana na kichwa cha habari hapo juu mimi AZAMA ABBASI KICHAWELE ambae kwa sasa ni mjane, mwenye namba ya simu +255 784 697319 na mkazi wa Majengo Arusha, Tanzania, na ambae ni mama wa nyumbani, nachukua nafasi hii kukutaarifu kama ifuatavyo.
Mume wangu kwa majina ABBASI ALLY KICHAWELE ambaye kwa sasa ni marehemu alikua na rafiki wake wa karibu kwa majina MAHMUD HASSAN MIHILE aliekuwa akitumia namba ya simu +441332270462 wakati huo mwenye asili ya Kisomali na uraia wa Uingereza na Tanzania walikubaliana awachukue watoto wetu ambao ni: SELEMAN ABBASI KICHAWELE aliekuwa na umri wa miaka kumi na AMINA JABIRI KICHAWELE aliekuwa na umri wa miaka saba aende nao Uingereza kwa ajili ya kuwasomesha.
Siku ya kuondoka watoto hawa ilikuwa ni mwaka 1994 na waliondoka na mke wa huyo Msomali kwa majina RAHMA MIHILE.
Mji wa kwanza walioshukia huko UINGEREZA unaitwa LEICESTER.
Baada ya hapo mawasiliano yaliendelea kuwepo kati ya mzazi wa kiume wa watoto na Msomali.
NB: Katika hawa watoto huyu wa kike, Amina Jabiri alikuwa ni wa mdogo wake mume wangu yaani shemeji yangu.
Kwa bahati mbaya mume wangu, aliugua maradhi ya cancer na ilipofika mwaka 1998, nikampoteza (alitangulia mbele ya haki)
Baada ya kifo cha mume wangu hakukua na mawasiliano yoyote kati yangu na huyu bwana aliyechukua watoto wangu. Alikata mawasiliano kabisa na wala hakutaka watoto wajue kuwa baba yao hayupo tena Duniani.
Kwa bahati mbaya sikua na mtu mwingine mbadala wa kuweza kuniunganisha na huyu bwana ikizingatiwa pia mimi ni mama wa nyumbani sikuwa na PR kubwa.
Leo hii ninapoandika barua hii, huu ni mwaka wa ishirini na mbili (22) toka nitengane na watoto wangu. Sisi pamoja na wanafamilia tutaendelea kutoa shukrani zetu kwa serikali ya Uingereza iwapo watoto hawa wapo salama na kwenye ajira zao. Kwetu hilo sio tatizo.
Jambo kubwa linaloniumiza ni kutokua na MAWASILIANO na watoto wangu kwa miaka ishirini na mbili sasa. Wakati mwingine najenga wasiwasi kwamba je, wako hai? Na hali hii nitaendelea nayo mpaka lini? 
Huyu bwana Mahamudu (msomali) nini kimemsukuma kuwa na ujasiri wa kuwaficha watoto wangu hata nisiwe na mawasiliano nao? Ana dhamira gain?
Kutokana na maelezo mafupi hapo juu nimefikia hatua ya kuiomba ofisi yako tukufu kunisaidia kupata namna ya kuwasiliana na watoto wangu wapendwa huko waliko. Jambo hili likifanikiwa litaleta faraja sana kwangu na kwa wana familia kwa ujumla.
Pia itakuwa ni fursa kwa watoto kutambua kuwa baba yao mpendwa alishafariki lakini mimi mama yao bado nipo hai, taarifa ambazo tuna hakika hawajazipata. Naambatanisha picha za watoto ambazo walipigwa wakati wanakaribia kuondoka mwaka 1994.
Pia naambatinisha na picha ya Mahmud Hassan Mihile (Msomali) ya wakati huo aliyewachukua watoto kwa makubaliano na mume wangu.

NB: Kwa mawasiliano tumia namba hizi za barua pepe
Au Athuman Rashid Mfinanga
Box 2614, - Arusha Tanzania
Ph: 0754375602/0784375602

 
Wako,
Katika ujenzi wa Taifa
Azama Abbasi Kichawele

MAJALIWA ATEMBELEA KIWANDA CHA CHAI CHA LUPEMBE NA KUZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu Mzee Philemon Luhanjo wakati alipowasili kwenye kiwanda cha chai cha Lupembe kukagua kiwanda na kuzungumza na wafanyakazi  akiwa katika ziara ya mkoa wa Njombe Januari 25, 2017. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa kiwanda cha chai cha Lupembe, Mussa Kefa   (kushoto kwake) wakati alipotembelea kiwanda hicho akiwa katika ziara ya mkoa wa Njombe Januari 25, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama ngoma  kutoka kijiji cha Kanitelele mkoani Njombe  ikicheza ngoma ya Limdoya wakati alipowasili kwenye kiwanda cha chai cha Lupembe  akiwa katika ziara ya mkoa wa Njombe Januari 25, 2017.  Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka
 Wasanii  kutoka kijiji cha  Kanitelele mkoani Njombe wakicheza ngoma  ya Limdoya wakati  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa   alipowasili kwenye kiwanda cha chai cha Lupembe  kukagua kiwanda na kuzungumza na wanyakazi  Januari 25, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha chai cha Lupembe akiwa katika ziara ya mkoa wa Njombe Januari 25, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

SEND OFF PARTY OF EVA AMOS BUJIKU LIVE FROM MRINA HALL DAR ES SALAAM, TANZANIA

$
0
0
Brought to you by Kelvin Kongojole

VETA YATOA MAFUNZO KATIKA MAKUNDI MBALIMBALI ILI KUJENGA UCHUMI WA NCHI

$
0
0
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Renatus Mpatili (mwenye tai)akiangalia vitu mbalimbali vilivyoandaliwa na wahitimu wa mafunzo ya VETA katika mahafali yaliyofanyika katika Kanisa la Christian Center Tabata jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
KUKUA kwa uchumi wa nchi kunatokana na kuwa watu wenye ujuzi mbalimbali na ukatumika katika kuleta maendeleo ya ukuaji wa uchumi huo.

Akizungumza katika mahafali ya Watu waliopata ujuzi kupitia mafunzo ya VETA yanayoendeshwa nchini, Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Renatus Mpatili amesema kuwa ujuzi walioupata kupitia VETA ufanye kazi ya kuzalisha na kuanzisha biashara itakayoleta manufaa.

Amesema kuwa VETA ina mipango mizuri ya kuhakikisha wananchi wanakuwa na ujuzi ambao utafanya watambulike katika kuendesha shughuli mbalimbali ikiwe ya kujiajiri au kuajiriwa.

Mpatili amesema kuwa nchi ya viwanda ya awamu ya tano inahitaji wajuzi mbalilmbali watakaotumikia katika viwanda hivyo VETA wanawajibu wa kuendelea kutoa ujuzi kwa makundi mbalimbali.

Nae Mkurugenzi wa Kanda ya Dar es Salaam, Habib Bukko amesema VETA inafanya kazi yake katika kuwafikia wananchi kwa kutoa mafunzo mbalimbali ili wawe sehemu ya nguvu kazi ya tifa.

Bukko amesema kwa mafunzo walioyapata wahitimu hao wakatumie vyeti vyao katika kzalisha kila ambacho wamekisomea na kuweza kubadili maisha yao na taifa kwa ujumla.
Wahitimu wakiwa wameandaa vitu mblimbali katika mafunzo ya siku 10 waliopewa na VETA katika mahafali yaliyofanyika katika Kanisa la Christian Center Tabata jijini Dar es Salaam.
Mhitimu akisonga ugali wa lishe kwa mafunzo waliopata na VETA katika mahafali yaliyofanyika katika Kanisa la Christian Center Tabata jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wahitimu katika mahafali katika mahafali yaliyofanyika katika Kanisa la Christian Center Tabata jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Renatus Mpatili (mwenye tai)akiangalia katika mahafali yaliyofanyika katika Kanisa la Christian Center Tabata jijini Dar es Salaam.

TEASER JOTO LA ASUBUHI ALHAMISI JANUARY 26, 2017

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

$
0
0

SIMU.TV: Benki ya Dunia imeiahidi Tanzania kuharakisha baadhi ya miradi inayofadhiliwa na benki hiyo ili kutimiza lengo la kuifanya Tanzania ya viwanda; https://youtu.be/XxAUudPcRbs

SIMU.TV: Kampuni ya bia ya Serengeti SBL imewapatia watanzania zaidi ya milioni 2 maji safi na salama baada ya kuwachimbia visima 17 nchi nzima; https://youtu.be/49-RBXzouZo

SIMU.TV: Kijana Elisha Selvestre mwenye umri wa miaka 26 amepigwa na kujeruhiwa sehemu za siri na mwajiri wake raia wa China baada ya kunywa maji yake ya chupa; https://youtu.be/hwHEi5cFsC8

SIMU.TV: Kampuni ya TCCIA imeanza kuuza hisa zake katika soko la hisa Dar Es salaam DSE kwa kipindi cha wiki sita; https://youtu.be/2KXw6L0I8S0

SIMU.TV: Naibu waziri wa Fedha Dkt Ashantu Kijaji amewataka wahitimu nchini kuachana na fikra za kuajiriwa na badala yake wafikirie zaidi kujiajiri; https://youtu.be/Y1IaL8ZH8-s

SIMU.TV: Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Mbeya Angela Maganga ameisimamisha kazi bodi ya Madibila Saccos kwa ubadhirifu wa fedha; https://youtu.be/QXgaQQ0Bn1g

SIMU.TV: Maandalizi kuelekea mashindano maalumu ya Gofu yaliyoandaliwa na klabu ya jeshi ya Lugalo yamezidi kupamba moto baada ya timu alikwa kuanza kuwasili; https://youtu.be/PSAK5tZo8dk

SIMU.TV: Ligi kuu Tanzania bara inatarajia kuendelea tena wikiendi ijayo kwa kuzikutanisha timu za Simba na Azam Fc uwanja wa Uhuru jijini Dar Es salaam; https://youtu.be/O1whY0ncw0U

SIMU.TV: Bondia Mwankemwa anatarajia kupanda ulingoni February 5 mwaka huu kumkabili Ramadhani Shauri kuwania ubingwa wa Afrika mashariki; https://youtu.be/y9idZbZkoYQ

WAZIRI MWAKYEMBE AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA NORWAY

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akimsikiliza mmoja wa wataalam walioambatana na Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe. Hanne Marie Kaarstad (wa tatun kulia) walipomtembelea ofisini kwake leo
 
 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria Prof. sifuni Mchome (wa pili kulia) akifafanua jambo wakati wa kikao na Balozi wa Norway na ujumbe wake (hawapo pichani) walipotembelea Wizara hiyo leo ili kujadili namna wataalam hao wanavyoweza kusaidia kiteknolojia katika kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiagana na  Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe. Hanne Marie Kaarstad na ujumbe wake baada ya kumaliza kikao leo jijini Dar es salaam. 
(Picha na Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria)

BENKI YA DUNIA YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KUKUZA UCHUMI

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Bw. Makhtar Diop, akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), walipokutana kwaajili ya mazungumzo Makao makuu ya Wizara hiyo, Jijini Dar es salaam. Wanao shuhudia ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anaye hudumia nchi za Tanzania, Malawi, Burundi, Bella Bird na Msaidizi wa Waziri wa Fedha na Mipango, Bw. Edwin Makamba (aliyesimama)

 Baadhi ya Watendaji wakuu wa Serikali kutoka Wizara ya Fedha na Mipango na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) wakiwa katika Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb) na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Bw. Makhtar Diop ( hawapo Pichani), Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es salaam.

 Ujumbe wa Tanzania na Benki ya Dunia, ukiwa katika kikao kilichojadili masuala mbalimbali yanayogusa Serikali na Benki hiyo, wakiongozwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Bw. Makhtar Diop, pamoja na Mwenyeji wake,  Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango,Jijini Dar es salaam,
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (wa Pili kutoka kulia) akisisitiza jambo wakati wa alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia ukanda wa Afrika Bw. Makhtar Diop, makao makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar salaam.
 Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Bw. Makhtar Diop, (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watendaji wa Wizara na Taasisi zake baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati yake na mwenyeji wake, Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), Makao Makuu ya Wizara hiyo, Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiagana na Mgeni wake, Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Bw. Makhtar Diop, mara baada ya kumalizika kwamazungumzo kati yao, ambapo Benki hiyo imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania kwa kuipatia Mikopo yenye mashari Nafuu kwaajili ya miradi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii. Picha na Ben Mwaipaja - WFM

WAZIRI JAFO AWASHANGAA WANASHERIA WA HALMASHAURI KUSHINDWA KESI

$
0
0
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jafo, amefungua mafunzo ya siku tatu ya wanasheria kwenye Halmashauri zote nchini huku akioneshwa kukerwa na tabia ya wanasheria hao kushindwa kesi na kuisababishia hasara serikali kwa kuwalipa fidia washindi.

Akifungua mafunzo hay oleo mkoani Dodoma, Jafo amesema zipo kesi nyingi zinazohusu halmashauri mbalimbali, lakini zinashindwa kutetewa na kusababisha serikali kulipa fidia.

Amebainisha pamoja na kuwepo wanasheria ndani ya halmashauri hizo, lakini wanashindwa kusimamia kesi zinazowakabili hali inayochangia serikali kulipa gharama kubwa kwa washindi wakati fedha hizo zingetumika kwa maendeleo ya wananchi.

“Fedha zinazolipwa na serikali mara baada ya kushindwa kesi, zingeweza kusaidia maendeleo ya wananchi ndani ya halmashauri hizi kutokana na wanasheria kutokuwa makini,”amesema Jafo.

Amewataka kuhakikisha wanasimamia vyema kesi za ardhi zinazowakabili wananchi wa chini ambao wengi wao hudhurumiwa na wenye uwezo na kusababisha malalamiko kwa wasimamizi wa sheria.

Mbali na hilo, pia Jafo amesema sheria nyingi za halmashauri zinatofautiana na maeneo husika ma kuwa na matatizo makubwa ya kimaandishi kutokana na kukinzana na sheria mama.

Amesema kutokana na sheria hizo kutoeleweka, inasababisha mikataba mingi ndani ya halmashauri hizo kutokuwa na umakini kwa kutoipendelea serikali na kuwapa kipaumbele walioingia mikataba hiyo, hali inayoonyesha kama hawapo wanasheria.
Naibu Waziri wa Nchi TAMISEMI Mhe. Suleimani Jafo (Mb) akitoa hotuba katika kikao cha kazi katika ukumbi wa mikutano Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini mjini Dodoma akiwaasa wanasheria kuhakikisha sheria ndogo hazikinzani na sheria mama kwa kuzingatia uandishi wa taaluma ya sheria kwani katika baadhi ya ziara zake amebaini kuwepo mogogoro ya wakulima na wafugaji, kesi nyingi za halmashauri kushindwa mahakamani na uandishi mbovu wa mikataba inayoingia halmashauri
Naibu Katibu Mkuu OR TAMISEMI Bw. Benard Makali akisisitiza jambo juu ya makosa yanayofanywa na Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini kama ukiukwaji wa utendaji kazi wa kisheria ambapo wanasheria wanapaswa kusimamia masuala yote ya kisheria katika utendaji wa kazi za Serikali
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kishapu (Shinyanga) ambaye pia ni Mwanasheria Bw. Stephen M.Magoiga akimshukuru Naibu Waziri OR TAMISEMI Mhe. Suleimani Jafo (Mb) kwa niaba ya Wanasheria ambapo amewaasa Wanasheria wenzake kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kuzifanyia kazi sheria ndogo kwa ustawi wa Mamlaka za Serikali nchini.
Baadhi ya Wanasheria wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi TAMISEMI Mhe. Suleimani Jafo (Mb) wakati akitoa hotuba katika kikao cha kazi katika ukumbi wa mikutano  Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini mjini Dodoma ambapo amewaasa kufanya kazi kwa bidii na umuhimu wa sheria ndogo katika uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.

BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 25/01/2017


NEWS ALERT: MOTO WAZUKA KATIKA MOJA YA JENGO LA POLISI MKOANI KILIMANJARO USIKU HUU, ZAIDI YA FAMILIA ZA ASKARI 20 ZAKOSA MAKAZI

$
0
0
Moto umezuka katika moja ya jengo la ghorofa mbili ambalo ni makazi ya askari Polisi, Moshi mkoani Kilimanjaro usiku huu na kuteketeza baadhi ya vyumba na Mali za familia za askari waliokuwa wakiishi katika jengo hilo.

Moto huo unadaiwa unaodaiwa kuanza kuwaka majira ya saa mbili za usiku, umepelekea zaidi ya familia za askari 20 kukosa makazi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo, wamemedai kuwa chanzo cha moto huo huenda kikawa ni mshumaa uliokuwa ukiwaka katika moja ya vyumba hivyo kufuatia kukatika kwa umeme.

Taarifa kamili za tukio hilo tutawaleteeni.Picha na Dixon Busagaga, Globu ya Jamii, Moshi.
Moto ulipokuwa ukiendelea kuwaka katika Jengo hilo, kabla vikosi vya Zimamoto na Uokoaji kufika katika eneo la tukio.
Sehemu ya Familia za Askari waliokuwa wakikaa katika Jengo hilo pamoja na mashuhuda wakiangalia tukio hilo wakati vikosi vya Zimamoto na Uokoaji vikiendelea na jitihada za kuudhibiti moto huo.
Sehemu ya mali zilizoteketea kwa moto huo.
Jitihada za kuuzima moto huo kwa baadhi ya maeneo ndani ya jengi hilo zikiendelea.

MSIKILIZE MSANII WA BONGO FLEVA LAMECK DITTO KATIKA KIPINDI CHA THE AVENUE

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JANUARI 26,2017

MKUU WA WILAYA YA BUHIGWE KANALI GAGUTI AKUTANA NA UONGOZI WA BURUNDI KUJADILI WIMBI LA WAKIMBIZI WANAOINGIA NCHINI KWA KASI BILA UTARATIBU

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

MKUU wa wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma kanali Marco Gaguti amewaonya wakimbizi wenye historia ya uhalifu nchini Burundi  wanaoingia Nchini  Tanzania, kwa kigezo cha kuomba hifadhi ya ukimbizi kwa kuhofia wasikamatwe kwa uhalifu walioufanya Nchini mwao, kuwa ikibainika  hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Aidha, Gaguti aliuomba uongozi wa Nchi ya Burundi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya   Wilaya hiyo iliyopo Mpakani, kuwabaini waomba hifadhi  hao wanaoingia Nchini kwa kukimbia uhalifu walioufanya Nchini mwao na kuja kuendeleza vitendo hivyo wanapo ingia Nchini.

Hayo yalibainika jana wakati wa Kikao cha majadiliano baina ya Mkuu huyo na Mkuu wa Wilaya ya Mabanda Mkoa wa Makamba Nchini Burundi, alipokuwa akihoji ni kwanini wahamiaji wengi wanaongezeka Nchini wakidai wanakimbia vurugu zinazo endelea Nchini mwao ambapo kwa Mwezi january  waliingia waomba hifadhi 2230, ambapo ilibainika wengi wao wanadai wanakimbia kukamatwa kwa kujihusisha na uhalifu na wengine kukimbia njaa iliyopo majumbani kwao.

Gaguti alisema kumekuwa na ongezeko kubwa la wahamiaji wanaoingia Nchini wakidai kukimbia vitisho wanavyo pewa na kikundi cha Vijana wa chama tawala kinacho julikana kama  ( IMBONELAKULE),  ambapo wanakuja kuomba hifadhi katika Nchi ya Tanzania ilihali Nchi yao ina amani ya kutosha  na wengine kukimbilia kambini kupata huduma za bure kwa kuhofia njaa nchini mwao . 


Hali iliyopelekea Waziri wa Mambo ya ndani kusitisha zoezi la Waomba hifadhi kuingia Nchini kwa kigezo cha kukimbia njaa Nchini mwao na kukimbilia Tanzania ili waweze kupata Msaada wa chakula , ni lazima Afanyiwe mahojiano na atoe sababu zilizo mfanya akimbie iliaweze kupatiwa kibali cha kuwa mkimbizi.

Hata hivyo Kanali Gaguti aliwaomba viongozi hao kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuwabaini wahalifu hao waweze kurudishwa Nchini mwao kuepukana na vitendo vinavyo endelea na ongezeko la waomba hifadhi kuingia Nchini bila kufuata utaratibu.

'' leo nilikuwa natembelea vituo na kuona ongezeko la wahamiaji lakini serikali imetoa maelekezo mapya ikiwemo kuwatambua na kujua sababu za kukimbia Nchini mwao, lakini kama atakuwa na sababu za Msingi hata pata fursa ya kuwa mkimbizi, lakini pia nikuombe ushirikiano kama kuna taarifa za watu ambao ni wahalifu upewe taarifa mapema kabla ya mambo kubadilika ili tuweze kuchukua tahadhari mapema kwa pande zote mbili" alisema kanali Gaguti. 
 MKUU wa wilaya ya Buhigwe mkoa wa Kigoma kanali Marco Gaguti   akifafanua jambo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Mabanda Mkoa wa Makamba nchini Burundi,(Musitanteri) Niyonkuru Laetitia, pamoja na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Tanzania na Burundi katika kujadiliana sakata la Wahamiaji wengi wengi kuanza kuingia nchini Tanzania kwa kasi tangu Januari,2017.
MKUU wa wilaya ya Buhigwe mkoa wa Kigoma kanali Marco Gaguti  akisalimiana na  Mkuu wa Wilaya ya Mabanda Mkoa wa Makamba nchini Burundi,(Musitanteri) Niyonkuru Laetitia
 Mkuu wa Wilaya Ya Buhigwe akisalimiana Na Wanajeshi wa Burundi mpakani mwa Tanzania na Burundi
 Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe akiongozana na kamati ya ulinzi na usalama kuingia mpakani mwa Burundi na Tanzania.

UZINDUZI WA AWAMU YA KWANZA YA MRADI WA MABASI YA MWENDO KASI JIJINI DAR ES SALAAM

Viewing all 110028 articles
Browse latest View live




Latest Images