Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110031 articles
Browse latest View live

TPSF NA DEIK ZAUNDA BARAZA LA KIBIASHARA BAINA YA UTURUKI NA TANZANIA

$
0
0
Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) na Bodi ya Mahusiano ya Kigeni kwenye masuala ya Kiuchumi nchini Uturuki (DEIK) wameingia makubaliano kuanzisha Baraza la Kibiashara baina ya nchi mbili,makubaliano hayo yalifikiwa tarehe 23 Januari 2017 jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF),Godfrey Simbeye amesema Baraza hilo litakuwa na majukumu na shughuli mbalimbali kama kusaidia kukuza biashara kati ya nchi hizo mbili,kutoa mchango katika kuanzisha kukuza Viwanda kupitia ushirikiano wa Teknolojia wa mashirika na Taasisi za Kiuchumi za nchini Uturuki.

Pia amesema kuratibu juhudi za pamoja kukusanya,kuunganisha,
kuniambia,kutathmini na kieneza taarifa zinazohusu biashara.Amesema Baraza hilo litasaidia kutambua changamoto za kibiashara baina ya nchi hizo mbili na kwenye ushirikiano Kiuchumi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF),Reginald Mengi amesema kuwa Baraza hilo la Kibiashara baina ya Uturuki na Tanzania litagawa katika kamati za Kitaifa mbili.Kila kundi litakuwa na Wanachama wake na Taasisi  za Kiuchumi au za Kibiashara.

Amesema kuwa Kamati hizo ndogo za Baraza zinatarajiwa kukutana angalau Mara moja kwa Mwaka,kutazama na kujadili mafanikio ya Baraza kwenye masuala ya Kibiashara,Uwekezaji,
Teknolojia baina ya nchi hizo mbili.
 Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini,Reginald Mengi akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Uundwaji wa Baraza la Kibiashara baina na Tanzania na Uturuki.
Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF,Godfrey Simbeye akizungumzia majukumu ya Baraza lilioundwa kati ya nchi mbili za Tanzania na Uturuki.Kushoto ni Mwenyekiti wa TPSF,Reginald Mengi.

NAIBU WAZIRI MASAUNI AWASILI MKOA WA SONGWE AFANYA MAZUNGUMZO NA WAKUU WA IDARA ZA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

$
0
0
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisalimiana maafisa wa Jeshi la Polisi baada ya kuwasili mkoani Songwe kwa ziara ya kikazi na kutembelea idara zilizopo chini ya wizara yake kwa lengo la kufuatilia utendaji kazi wa idara hizo na kuzishauri.( Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, ACP Mathias Nyange(kulia), akimuongoza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni kutembelea makao makuu ya Jeshi la Polisi mkoani Songwe wakati wa ziara ya naibu waziri yenye lengo la kufuatilia utendaji kazi wa idara za wizara yake  na kuzishauri ili kuweza kudhibiti hali ya uhalifu mkoani hapo.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wakuu wa Idara zilizopo chini ya wizara yake, alipowasili mkoani Songwe kwa ziara ya kikazi ikiwepo kufuatilia utendaji wa idara hizo katika kukabiliana na hali ya usalama kwa mikoa iliyopo mipakani.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia), akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Mkoa wa Songwe, Coletha Peter, alipofanya ziara katika ofisi hizo kwa lengo la kujua zoezi la kuandikisha wafanyakazi wa umma lilipofikia.
 Naibu Waziri wa Wizara ya  Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza  baada ya kupata maelezo ya mradi wa Ujenzi wa ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe unaojengwa kwa ushrikiano wa wadau wa mkoa huo na jeshi la polisi.Wapili kushoto ni Kamanda wa Polisi wa mkoa huo ACP Mathias Nyange.
Naibu Waziri wa Wizara ya   Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(watano kulia), akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa idara zilizopo chini ya wizara yake katika mkoa wa Songwe  mara baada ya kufanya mazungumzo na wafungwa katika gereza la wilaya ya Mbozi ambapo aliwataka kufanya kazi wanazopangiwa ili wawe rasilimali watu katika dhana ya kulipeleka Taifa katika uchumi wa kati.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI –WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI


WAZIRI MAKAMBA AKUTANA NA KAMATI YA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR YA KUSHUGHULIKIA VIONGOZI WAKUU WA KITAIFA

$
0
0
Evelyn Mkokoi na Lulu Mussa.



Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar (SMZ) ambao pia ni wajumbe wa kamati ya Kusimamia viongozi wakuu wa kitaifa wamekutana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Masuala ya Muungano na Mazingira Mh. January Makamba, Jijini Dar es Salaam wakiwa na lengo la kuzungumzia baadhi ya changamoto za Muungano na kubadilishana mawazo katika maeneo ya Muungano.



Waziri Makamba aliwapongeza wajumbe wa Kamati hiyo, na  kusema kuwa ujio wao unaonyesha dhamira nzuri ya kuwawakilisha wananchi wa Zanzibar na kuimarisha Muungano uliodumu kwa miaka hamsini na saba (53) sasa.



Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Omary Seif Abeid ambaye pia ni Muwakilishi wa Jimbo la Konde Pemba, alisema kuwa, pande hizi mbili za Muungano hazina Budi kuwakumbuka waasisi wa Muungano huo Hayati Mzee Abeid Amani Karume na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kuunganisha pande mbili hizi na kupatikana kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusema  kuwa anaeubeza Muungano anajibeza mwenyewe.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba  (katikati) akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wa Kuu wa Kitaifa. Wajumbe wa Kamati walifanya ziara ya kikazi katika Ofisi ya Makamu wa Rais Mtaa wa Luthuli Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw. Omary Seif Abeid na Bw. Mihayo Juma N'hunga Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba  (aliyesimama) akiwakaribisha wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wa Kuu wa Kitaifa mara baada ya kumtembelea Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora  (aliyesimama) akiongea na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wa Kuu wa Kitaifa, mara baada ya kufanya ziara ya kikazi. Kushoto ni Mkurugenzi wa Muungano Bw. Baraka Rajab Baraka.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi wa Kuu wa Kitaifa wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba.

Recycling of waste, discovering of gas should foster progress in Tanzania

$
0
0
Speaking to reporters in Dar es Salaam on his first visit to the country, UN Environment Programme (UNEP), Executive Director, Erik Solheim said that UNEP is the leading global environment authority that sets the global environment agenda.

“The discovering of gas reserved in Tanzania should be use as stepping stone to employment, business opportunity and as a tool to alleviate poverty,” he noted.

He commended that the efforts taken by the government through local municipalities for setting an area in the outskirt of city center Pugu Dampo as a permanently place for cabbage without destructing the environment of the Dar es Salaam city.

Solheim added that the UN environment works with a wide range of partners, including United Nations entities, international organizations, national governments, non-governmental organizations, the private sector and civil society.

He added hope that “other leaders will be inspired to pick up the baton and ensure that Africa’s rich natural resources can be conserved, and thus serve as the foundation for a sustainable future and food security for all on the continent.”
 United Nations Environment Programme, Executive Director, Erik Solheim (right) speaks to reporters at the news conference held in Dar es Salaam on his official visit to Tanzania on Global environmental agenda, on his right, UN Resident Coordinator, Alvaro Rodriguez.
United Nations Environment Programme (UNEP), National Coordination Officer, Ms Clara Makenya (right) when she stressed a point to reporters during the press conference held in Dar es Salaam on the official visit to UN Environment Head Erik Solheim to Tanzania. Second left is UNEP, Executive Director, Erik Solheim, far left, UN Resident Coordinator, Alvaro Rodriguez. 

TANZANIA should adapt recycling waste policy, increasing uses of gas instead of charcoal for cooking as a long term solution on ensuring sustainable environmental protection to tape the pressing challenge of climate change.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWASILI MAKAMBAKO KUENDELEA NA ZIARA YA MKOA WA NJOMBE

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Iringa mjini, Richard Kasesela baada ya kuwali kwenye uwanja wa Nduli  mjini  IringaKulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Amina Masenza. akiwa njiani  kuelekea Njombe kuendelea na ziara ya kazi Januari 25, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiakaribiwahwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka baada ya kuwasili Makambako kuendelea na ziara ya mkoa huo, Januari 25, 2017.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Njombe, Deo Sanga baada ya kuwasili Makambako kuendelea na ziara ya mkoa huo, Januari 25, 2017.  Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WITO KWA WALIOKUWA WAFANYAKAZI WA MGODI WA DHAHABU BULYANHULU WALIOPIMWA AFYA KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI

$
0
0

WITO KWA WALIOKUWA WAFANYAKAZI WA ULIOKUWA MGODI WA DHAHABU BULYANHULU

UPIMAJI ULIOFANYIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI .


Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) unawakaribisha walioorodheshwa hapo chini kufika katika ofisi za OSHA zilizopo Kinondoni Manyanya karibu na mahakama kati ya tarehe 26 na 27 Januari ili waweze kupewa majibu yao. Tangazo hili linawahusu waliopimwa Muhimbili tu. Waliopimwa Bugando wanaombwa kusubiri tangazo jingine.




Imetolewa na:
MTENDAJI MKUU
WAKALA WA USALAMA NA AFYA MAHALI PA KAZI (OSHA)
S.L.P 519, MAHAKAMA ROAD KINONDONI
DAR ES SALAAM.

NEC YATOLEA UFAFANUZI TAARIFA ZA UPOTOSHAJI MATOKEO UCHAGUZI MDOGO WA JIMBO LA DIMANI –ZANZIBAR.

$
0
0
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Ramadhan Kailima

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeeleza  kuwa Kura 234 ziliharibika katika Uchaguzi mdogo wa Ubunge katika jimbo la Dimani, Zanzibar Januari 22, 2017.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Ramadhan Kailima amesema kuwa Wapiga Kura walioandikishwa katika jimbo la Dimani, Zanzibar ni 9,275.
Amesema kati ya hao wapiga Kura 6,406 walijitokeza kupiga Kura siku hiyo ambapo Kura halali zilikuwa 6,172 na Kura zilizoharibika zilikuwa 234.
“Napenda kuwafahamisha wananchi wote kuwa taarifa sahihi za matokeo ya Kura katika Uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo la Dimani ni kama ifuatavyo; Wapiga Kura walioandikishwa jimbo la Dimani ni 9,275, Waliopiga Kura walikuwa 6,406, Kura halali 6,172 na Kura zilizoharibika ni 234” Amesisitiza.
Mkurugenzi Kailima ameeleza kuwa katika Uchaguzi huo vyama 11 vilikuwa na wagombea wa Ubunge ambapo Chama cha ACT-Wazalendo kilipata Kura 8, Chama cha ADC Kura 42, Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kura 4860, CHAUMA Kura 10, Chama Cha Wananchi CUF Kura 1234, Chama cha DP Kura 8.
Vingine ni Chama cha NRA kura 1, SAU Kura 4, TLP kura 2, Chama Cha UMD Kura 2 na Chama Cha UPDP Kura 1 na kufanya jumla ya Kura za Vyama vyote kuwa 6172. 

BEI YA MADAFU LEO


SERIKALI YA AWAMU YA TANO INAWAPENDA WAFANYABIASHARA - RAIS MAGUFULI

TPSF NA DEIK ZAUNDA BARAZA LA KIBIASHARA BAINA YA UTURUKI NA TANZANIA

sherehe za ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya mabasi ya mwendo kasi

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba kwa Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop kwenye sherehe za  ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam leo Jumatano Januari 25, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na meza kuu wakimshangilia  Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop kwenye sherehe za  ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam leo Jumatano Januari 25, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop pamoja na viongozi wengine meza kuu wakifurahia nyimbo za msanii Mrisho Mpoto na Banana Zorro kwenye sherehe za  ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam leo Jumatano Januari 25, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop pamoja na viongozi wengine meza kuu wakifurahia nyimbo na kwenda kumtuza msanii Mrisho Mpoto na Banana Zorro kwenye sherehe za  ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam leo Jumatano Januari 25, 2017
Mungu ampe nini Msanii Mrisho Mpoto baada ya kuambulia burungutu la noti baada ya kutumbuiza kwenye sherehe za  ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam leo Jumatano Januari 25, 2017

Papa amtimua kiongozi wa dini kwa kusambaza kondomu

$
0
0
Kiongozi wa kanisa katoliki anayewasaidia raia wa Malta amejiuzulu kufuatia mgogoro na Vatican kuhusu mpango wa kusambaza mipira ya kondomu kulingana na kanisa hilo.
Mathew Festing mwenye umri wa miaka 67 alijiuzulu baada ya papa Francis kumtaka kufanya hivyo katika mkutano siku ya Alhamisi. Hatua hiyo inafuatia ufichuzi kwamba tawi la hisani la kanisa hilo huko Malta lilisambaza maelfu ya mipira ya kondomu katika taifa la Myanmar.
Kanisa katoliki linakataza utumizi wa mipira ya kondomu. Papa Francis ilimtaka ajiuzulu na alikubali. Tawi hilo la Malta lina uwezo mwingi kama ule wa taifa zima. Hutoa pasipoti, stampu na leseni na pia lina uhusiano wa kidiplomasia na mataifa 106 ,ikiwemo Vatican.
Ijapokuwa tawi hilo linaonekana kuwa na wanaume pekee, viongozi wake sio wanaume pekee.Kufikia 2013 wanawake walikuwa asilimia 30 wakijulikana kama Dames.Kundi hilo lilo katika kuondoa sura yake ya kibwenyenye na kuvutia vipaji ili kuendelea kazi zake za kibinaadamu. Chanzo:BC
Papa Francis akiwa na kiongozi wa
kanisa katoliki anayewasaidia raia wa Malta

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA RASMI AWAMU YA KWANZA YA MIUNDOMBINU NA UTOAJI HUDUMA YA MABASI YAENDAYO HARAKA (BRT) JIJINI DAR

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop pamoja na viongozi wengine wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop wa kwanza kulia wavivuta kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene pamoja na  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka kadi ya Kieletroniki katika Mashine ya UDART ilikuweza kupita kama ishara ya Ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam. Pembeni yake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene akimuelekeza jambo katika mashine hizo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipita kwenye mashine hizo mara baada ya uzinduzi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

BREAKING NYUZZZZ.....: JENGO LAPOROMOKA MJI MKONGWE ZANZIBAR MCHANA HUU

$
0
0
Watu wanne akiwemo mama na mtoto wanashukiwa kufukiwa na kifusi kufuatia kubomoka kwa ukuta wa upande wa jengo la ghorofa 3 huko Mji Mkongwe, Zanzibar. juhudi za kuokoa waliofukiwa na kifusi hicho yaendelea.Chanzo cha kuporomoka kwa ukuta huo bado hakijafahamika.
Juhudi za kuokoa watu waliofunikwa na kifusi baada ya kuanguka kwa ukuta wa jengo hilo zikiendelea, Mji Mkongwe Zanzibar mchana huu.
Muonekano wa Jengo hilo baada ya kuporomoka.

TRUMP AANZA KUWABANA WAHAMIAJI KUINGIA MAREKANI, AAMURU UJENZI WA UKUTA MPAKANI MWA MEXICO

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump atia saini amri kuu kuweka masharti juu ya wahamiaji wanaoingia nchini humo. Taarifa kutoka Ikulu ya Marekani zinasema kuwa, Rais Trump ameanza kwa hatua ya kuimarisha usalama katika mpaka wa nchi hiyo na Mexico baada ya kuzuru makao makuu ya wizara ya usalama wa ndani nchini humo.

Aidha, anatarajiwa pia kutoa tangazo la kuidhinisha sheria kali zaidi za kupata visa kwa wageni kutoka maeneo ya Mashariki ya Kati na Afrika ambayo yana Waislamu wengi.

Miongoni mwa nchi zitakazoathiriwa na agizo la Trump ni Syria, Yemen, Iran, Sudan , Somalia na Iraq.

Rais Trump ameandika kwenye Twitter kwamba leo itakuwa siku muhimu sana kwa usalama wa taifa la Marekani. Mwandishi wa BBC David Willis kutoka Washington anasema hatua hiyo huenda ikayaudhi mashirika ya kibinadamu na yale ya kutoa misaada ikizingatiwa mzozo unaoendelea kwa sasa kuhusu hali ya wakimbizi wa Syria.
Wakati wa kampeni yake ya urais, Donald Trump aliahidi kufanyia mageuzi suala la uhamiaji Marekani. Aligusia ujenzi wa ukuta kati ya Mexico na Marekani kuzuia wahamiaji haramu na kuwapiga marufuku Waislamu kuingia katika taifa hilo kama sehemu ya vita dhidi ya ugaidi. Baadaye alibadili msimamo kidogo na kufafanua kwamba watakachofanyiwa Waislamu ni kufanyiwa ukaguzi mkali kabla ya kuruhusiwa kuingia Marekani.

Anatarajiwa kufika katika wizara ya usalama wa ndani baadaye leo na anatarajiwa kusaini maagizo hayo ya kuimarisha usalama katika mpaka wa Mexico na taifa lake na baadaye wiki hii taarifa zinaashiria atawajibikia ahadi yake ya kupunguza idadi ya wakimbizi wanaoingia Marekani.

Na hiyo ni hadi pale ukaguzi mkali utakapoanzishwa na kuzuia raia wa mataifa saba ya Afrika na kutoka eneo la Mashariki ya Kati yote yalio na idadi kubwa ya waumini wa Kiislamu.

Ubaguzi wa kidini unapigwa marufuku kwa mujibu wa katiba ya Marekani lakini inadhaniwa utawala wa Trump utaidhinisha marufuku hiyo kwa misingi kwamba ni hatua za dharura kukabiliana na tishio lililopo la ugaidi.

Awali, Trump aliandika kwenye Twitter kueleza kusikitishwa kwake na kiwango cha juu cha ghasia na mauaji katika jiji la Chicago.

Vyombo vya habari wiki hii viliripoti kwamba tayari watu 228 wamepigwa risasi na wengine zaidi ya 40 kuuawa mwaka huu.

Rais Trump ameandika kwamba iwapo watawala wa Chicago hawatatatua tatizo hilo la mauaji, basi atawatuma 'Feds' akimaanisha maafisa wa FBI.

BARAZA LA WATOTO LATAKA WANAOLAWITI KUTOFICHWA

JKCI KWA KUSHIRIKIANA NA MADAKTARI AFRIKA WA NCHINI MAREKANI WATOA HUDUMA YA KUZIBUA MISHIPA YA MOYO ILIYOZIBA

$
0
0
 Madaktari Bingwa wa Moyo wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Madaktari Afrika wa nchini Marekani wakitoa huduma kwa mgonjwa ya kuzibua mshipa wa moyo uliokuwa umeziba  bila ya kupasua kifua (Catheterization). Kulia ni Dkt. Peter Kisenge, akifuatiwa na Dkt. Peter O’brien na kushoto ni Afisa Muuguzi Ayoub Mchau.
 Daktari Bingwa wa Moyo kutoka Madaktari Afrika wa nchini Marekani Dkt. Peter O’brien na Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ayoub Mchau wakitoa huduma kwa mgonjwa ya kuzibua mshipa wa moyo uliokuwa umeziba  bila ya kupasua kifua (Catheterization).
 Madaktari Bingwa wa Moyo wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Madaktari Afrika wa nchini Marekani wakiendelea na kazi ya kutoa  huduma kwa mgonjwa ya kuzibua mshipa wa moyo uliokuwa umeziba  bila ya kupasua kifua (Catheterization).
Madaktari Bingwa wa Moyo wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Madaktari Afrika wa nchini Marekani wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizi kutoa  huduma kwa mgonjwa ya kuzibua mshipa wa moyo uliokuwa umeziba  bila ya kupasua kifua (Catheterization). Picha na Anna Nkinda – JKCI

TANZIA

BENKI YA DUINIA KUIKOPESHA TANZANI DOLA MILIONI 350 KUPANUA BANDARI YA DAR

$
0
0
BEN MWAIPAJA -WFM
 BENKI ya Dunia imekubali kuikopesha Tanzania fedha kwaajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo mkopo wa Dola Milioni 350 kwa ajili ya Mradi wa Upanuzi wa Bandari ya Dar es salam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dokta Philip Mpango, amewaambia waandishi wa Habari mara baada ya kumalizika kwa Mazungumzo kati yake na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anaye shughulikia Kanda ya Afrika, Mhe. Makhtar Diop, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es salaam.
Amesema kuwa kukamilika kwa upanuzi wa Babdari hiyo kutasaidia kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa na Bandari hiyo hatua itakayo chochea ukuaji wa  uchumi wa nchi.
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika Mhe. Makhtar Diop, amesema kuwa Benki yake imefurahishwa na hatua zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya tano katika kukuza uchumi na kwamba Benki hiyo itaendelea kushirikiana na serikali kuhakikisha kuwa malengo yaliyokusudiwa yana fikiwa kwa haraka
Ameishauri Serikali kuongeza ushirikiano kati yake na Sekta Binafsi katika kuchochea  biashara na uwekezaji pamoja na kutupia jicho sekta ya kilimo kwa kuboresha uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo pamoja na kuongeza thamani ya mazao hayo ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kuondokana na umasikini na kuchochea uwekezaji katika sekta hiyo

POLEPOLEA ATEMBELEA MAGAZETI YA UHURU, MTANZANIA NA UHURU FM, LEO

$
0
0
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole, leo amefanya ziara ya kikazi katika Vyombo vitatu vya Habari vya Kampuni za Uhuru Publications Ltd, Wachapishajiwa Magazeti ya Uhuru,Mzalendo na Burudani, Peoples Media ya Uhuru FM na New Habari Corporation, Wachapishaji wa Magazeti ya Mtanzania, Rai na Dimba. Pichani, Polepole akizungumza na Wafanyakazi na viongozi wa kampuni ya Uhuru Publications Ltd, wakati wa ziara hiyo.
 Polepole akimsalimia Suleiman Jongo alipokuwa akisalimia wafanyakazi wa Uhuru Publications Ltd, baada ya kuwasili kwenye Ofisi za Kampuni hiyo leo
 Mhariti Mtendaji wa New Habari Corporation Absalom Kibanda akimkaribisha Polepole katika Ofisi za Kampuni hiyo, Sinza jijini Dar es Salaam
 Polepole akizungumza na wafanyakazi na viongozi wa New Habari Corporation.

Viewing all 110031 articles
Browse latest View live




Latest Images