Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110090 articles
Browse latest View live

MSIKITI WACHOMWA MOTO KITONGOJI CHA BELLEVUE, MAREKANI

$
0
0
Taharuki imetamalaki jijini Seattle, Marekani, kufuatia kuchomwa moto kwa msikiti wa Bellevue, WA,  (angalia picha) ambao huwa unatumiwa na jumuiya ya Waislamu jijini humo, wengi wao wakiwa Watanzania.
Kwa mujibu wa taarifa za polisi, moto huo ulizuka alfajiri ya Jumamosi na mtu mmoja mwanaume mwenye umri wa miaka 37 ametiwa mbaroni kwa kutuhumiwa kuhusika na hujuma hiyo baada ya kukutwa eneo la tukio.
Kikosi cha zimamoto cha Bellevue kinasema kilifika msikitini hapo alfajiri hiyo na kukuta miali ya moto ya futi 40 ikiunguza sehemu za nyuma za msikiti huo, ambapo vikosi 13 vilivyofika vilifanikiwa kuuzia, Hakukuwa na majeruhi walioripotiwa.  
Bellevue ni mji ulio upande wa Mashariki (Eastside) wa  King County, Washington, Marekani, ukiwa upande wa pili wa Ziwa Washington kutoka  Seattle. Ukiwa ni mji wa tatu kwa ukubwa katika eneo la jiji la Seattle metropolitan, Bellevue ambao unajulikana kama mji unaokua pembezoni (satellite city), ulikuwa na wakaazi wapatao 122, 363 katika sensa ya mwaka 2010. Watanzania wengi wanaishi hapo.
Uongozi wa msikiti huo umetoa taarifa katika tovuti yake mapema leo Jumamosi kuhusu moto huo, na kueleza kwamba nyumba hiyo ya ibada imefungwa. "As Salaaam Aleikum. Kulikuwa na mototo sehemu ya nyuma ya msikiti wa Bellevue (Kituo cha Kiislamu cha). Moto ulianza mnamo saa tisa alfajiri Jumamosi (14/1/2017 ) na msikiti huo hauwezimkutumika mpaka itapotangazwa”, ilisema taarifa hiyo.
 “NDUGU WANA WATANZANIA KWA UJUMLA NAOMBA TUUNGANE PAMOJA KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU TENA AMBACHO JAMII YETU YA KIISLAM INAPITIA KWA KULAANI KWA PAMOJA KITENDO CHA WATU KUINGIA MSIKITINI NA KUUCHOMA MOTO. 
" TUWATAKE POLISI, FBI NA VYOMBO VYOTE VYA ULINZI NA USALAMA MAJIBU YA KWANINI MSIKITINI UCHOMWE MOTO? TUWATAKE ULINZI WA KUTOSHA KWA FAMILIA ZETU.
"TUUNGANE PAMOJA KWA SALA NA DUA KUOMBA MWENYEZI MUNGU MOYO WA SUBRA NA KUSAMEHE”, AMSEMA MMOJA WA VIONGOZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA WA SEATTLE BW. DOLA KWENYE UJUMBE WAKE ULIOSAMBAZWA MTANDAONI.

Msanii Mrisho Mpoto afurahia hatua ya china kutaka kupiga marufuku biashara ya pembe za tembo nchini humo

$
0
0
Msanii wa muziki wa asili nchi, Mrisho Mpoto ambaye pia amekuwa mmoja kati ya wasanii ambao wanatoa elimu kwa jamii juu ya kukomesha suala la mauwaji ya tembo nchini, ameipokea kwa furaha hatua ya nchi ya China kutaka kupiga marufuku biashara ya meno ya Tembo nchini humo.


Mapema Jumamosi hii katika matembezi ya amani ya kupinga ujangili hapa nchini, Balozi wa China, Lu Youqing alisema nchi ya China ipo kwenye mkakati wa kupiga marufuku biashara ya meno ya tembo na wanatarajia mwishoni mwa mwaka huu biashara hiyo kufa kabisa.

Akiongea na waandishi wa habari kuhusu kauli hiyo, Mrisho Mpoto alisema hatua hiyo ni nzuri na itasaidia nchi mbalimbali duniani kuiga nyayo zao.
“Mimi ni mmoja kati ya wasanii ambao tumekuwa tukihusika sana katika hizi harakati hasa hasa kimataifa zaidi, nimeshasafiri nchi mbalimbali kama mtanzania kupinga mauwaji ya tembo au ujangili ndio maana hata leo nipo kwa baada ya kualikwa na ubalozi wa China kwamba wameona jitihada zangu,” alisema Mpoto. 
“Kwa hiyo alichokisema balozi kuhusu nchi ya China kupiga marufuku biashara ya meno ya tembo ni kitu kizuri sana kwa sababu huu ni mwanzo kwa China ambao zimekuwa zikisema China ndo vinara wa biashara hiyo kuwa na mtazamo mwingine, lakini pia kupitia maamuzi haya naona sasa biashara hii inaenda ukingoni kama nchi zingine za Ulaya ambazo zimekuwa zikitajwa kufuata msimamo wa China,”
Alisema suala la kupinga ujangili nchini sio suala la mtu mmoja, kila mtanzania ana haki ya kulinda maliasili za nchi kwajili ya kizazi kijacho.

Pia muimbaji huyo ambaye bado anafanya vizuri na wimbo Sizonje, amesema yeye bado ataendeleza mapambano kwa kuanzisha kampeni mbalimbali ambazo zitawafanya watanzania kufichua majangili kwa kuwa ni watu ambao wanatoka katika jamii zetu. 
Msanii wa muziki wa asili nchi, Mrisho Mpoto akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja.Gen Gaudence Milanzi wakati wa matembezi ya kupinga ujangili unaofanywa dhidi ya Tembo  ya kilometa 5 kutoka Ubalozi wa China mpaka Hoteli ya Sea Cliff  ambapo wageni mashuhuli kama Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe. Benjamini William Mkapa alishiriki.

MAMA SAMIA AFUNGUA MAFUNZO YA VIONGOZI NA WATENDAJI WA CCM MKOA WA KASKAZINI UNGUJA

$
0
0

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa ambaye pia Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi wa CCM katika Mkoa Kaskazini (A) Unguja kuwachukulia hatua stahiki wanachama ambao wanakisaliti na kuhujumu shughuli katika hatua ya kujenga CCM mpya.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduz i(CCM) Taifa SAMIA SULUHU HASSAN ametoa kauli hiyo wakati anafungua mafunzo maalum ya viongozi na watendaji wa CCM na Jumuiya zake wapatao 556 katika ngazi ya matawi, wadi/tarafa na majimbo katika Mkoa wa Kaskazini (A) Unguja.

Samia Suluhu Hassan amesema kuwa hatua hiyo itasaidia chama kuimarisha shughuli zake kwa sababu chama kitakuwa na watu waadilifu na wenye nia ya kukisaidia CCM kusonga mbele na kupata ushindi mkubwa katika chaguzi zijazo.

Amesisitiza wanachama na viongozi wa CCM kote nchini waendelee kuweka mipango na mikakati imara itakayowezesha chama kuendelea kupata ushindi mkubwa na kushika dola.

Mjumbe huyo ambaye pia ni Mlezi wa CCM katika mkoa wa Kaskazini A Unguja amesema Umoja na Mshikamano miongoni mwa wananchama na viongozi ndio silaha madhubuti itakayowezesha chama hicho kuimarisha shughuli zake na kuongeza maradufu idadi ya wanachama nchini.

Amesema kwa sasa Viongozi watakiwa kujielekeza katika kufufua na kuimarisha jumuiya za chama ambazo katika baadhi ya maeneo hazifanyi kazi vizuri ili zianze kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia kanuni na taratibu za chama.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi(CCM) Taifa pia ameendelea kuonya baadhi ya viongozi waache tabia ya kutengeneza makundi ya ndani ya chama kwa ajili ya kusaka madaraka bali wawe mstari wa mbele katika kujenga umoja na mshikamano ndani ya chama.

Kuhusu mafunzo, Samia Suluhu Hassan amewahimiza viongozi wanaopata mafunzo hayo kuyatumia vizuri ili kuhakikisha wanaporudi kwenye maeneo yao wanafanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu mkubwa.

Amesema kwa sababu Serikali iliyopo madarakani inatekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi ni muhimu kwa viongozi wa chama katika ngazi zote washirikiane na viongozi wa Serikali katika maeneo husika ili kuhakikisha miradi ya maendeleo ya wananchi inafanyika kwa ubora unaotakiwa kulingana na thamani ya fedha. 

Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakazi wa mkoa wa Kaskazini A, Unguja wakati wa Kufungua Mafunzo maalum ya Viongozi na watendaji wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake wa ngazi ya Matawi, Wadi na Majimbo 
Wana CCM wa Kaskazini A wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwenye mafunzo ya Uongozi yaliofunguliwa na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. 
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kaskazini A Unguja, Ndugu Juma Haji akihutubia kabla ya kumkaribisha Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kufungua mafunzo maalum ya Uongozi yaliofanyika Mkokotoni Unguja kwenye Chuo cha Amali.

ACHENI KUINGIZA MIFUGO KATIKA HIFADHI ZA TAIFA - MEJA JENERALI MILANZI

$
0
0
Na Daudi Manongi-MAELEZO.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja.Gen Gaudence Milanzi amewaasa wafugaji kuacha kuingiza mifugo katika hifadhi za taifa ili kuzitunza hifadhi hizo.
Katibu Mkuu uyo aitoa wito huo wakati akizungumza baada ya kufanya matembezi ya kupinga ujangili unaofanywa dhidi ya Tembo  ya kilometa 5 kutoka Ubalozi wa China mpaka Hoteli ya Sea Cliff  ambapo wageni mashughuli kama Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe.Benjamini William Mkapa alishiriki.
“Hifadhi za taifa hapa nchini hazina budi kulindwa na kutunzwa ili vizazi vijavyo viweze kuzifaidi kwani maeneo hayo yametengwa kwa ajili ya wanyama pori pekee na siyo kwa mifugo na hivyo kila mwananchi analo jukumu la kuyalinda mazingira haya,”Aliongeza Mej.Gen Milanzi.

Awali akizungumza katibu mkuu huyo alisema kuwa Serikali ina mkakati mkubwa wa kuhakikisha inashirikiana na nchi zingine katika kutokomeza kabisa Ujangili wa pembe za ndovu nchini.
Aidha aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya watu wa China kwa kuwa mstari wa mbele katika kupambana na ujangili wa pembe za ndovu ikiwemo upigaji  marufuku biashara ya pembe za ndovu na viwanda vya kuchonga pembe hizo ifikapo mwezi machi Mwaka huu.
 Rais Msataafu wa Awamu ya Tatu wa Tanzania, Benjamin William Mkapa akizungumza mara baada ya kupokea Matembezi kwa ajili ya kupinga ujangili ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yameratibiwa na Asasi ya Tanzania – China Promotion Association (TCFPA) na Ubolozi wa China ambapo yalianzia Ofisi za Ubalozi wa China na kuishia katika Hotel ya Sea Cliff.

 Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing, akizungumza kabla ya kuanza matembezi  ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yana lengo la kuhamasisha upingaji wa ujangili na mauaji ya Tembo.
 Katibu Mkuu wa Asasi ya Tanzania – China Promotion Association (TCFPA) akitoa maelekezo kuhusu matembezi ya  Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yameratibiwa na asasi hiyo kwa kushirikiana na Ubolozi wa China ambapo yalianzia Ofisi za Ubalozi wa China na kuishia katika Hotel ya Sea Cliff.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi (kushoto) akisalimiana na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu Youqing wakati wa matembezi ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Lengo la matembezi hayo ni kuhamasisha jamii kupinga ujangili na mauaji ya Tembo.
 Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing, akiwaongoza mamia ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam kufanya mazoezi kabla ya kuanza matembezi  ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yana lengo la kuhamasisha upingaji wa ujangili na mauaji ya Tembo. Kwa habari kamili BOFYA HAPA

KUTOKANA NA HALI YA HEWA MBAYA.DMV SASA KISOMO CHA AROBAINI YA MAREHEMU ALHAJI PROFESSOR IDRIS ALI MTULIA KUFANYIKA KESHO JUMAPILI

$
0
0
Asalaam Aleykum. 
Kwa niaba ya familia ya Marehemu baba yetu mpenzi, Alhaji Professor Idris Ali Mtulia Tunapenda kuwatangazia kisomo cha Hitma ya baba yetu kitakachofanyika siku ya JUMAPILI January 15, 2017.

Alhaji Professor Idris Ali Mtulia aliyefariki dunia ghafla siku ya Jumatatu Desemba 5, 2016 Nyumbani Kwake Upanga, Dar-es-salaam Na kuzikwa Jumanne Desemba 06, katika makaburi ya Kisutu, Dar-es-salaam.
Nyote mnakaribishwa.
Anuani: Indian Spring Terrace Local park
9717 Lawndale Drive
Silver Spring, Md 20901
Muda: 12 jioni - 4 usiku

Kama ilivyo mila Na desturi yetu Wana DMV tunaomba ushirikiano wenu. Kina mama msaada wa vyakula Na kina baba vinywaji, tafadhali wasiliana Na hawa wafuatao Katika maandalizi ya shughuli hii..
Iddi Sandaly (301) 613-5165
Mohamed Matope 301-655-0409
Saidi Mchumo (850) 339 6783
Asha Nyang'anyi (301) 793-2833
Jasmine Rubama (410) 371-9966
Mwasi Marijani (301) 256-8902
Joha Nyang'anyi (240) 813-5563
Dr. Rukia Marijani (850) 980-6633
Tunatanguliza Shukrani..

MUHIMU KWA KINA MAMA

DIAMOND ALIVYOPAISHA BENDERA YA TANZANIA GABON

MWANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO GAZETI LA UHURU AMINA ATHUMAN AFARIKI DUNIA

$
0
0

Mwandishi wa habari za Michezo wa Gazeti la Uhuru na Mzalendo, Amina Athuman (pichani) amefariki Dunia leo asubuhi katika Hosptali ya Mnazi Mmoja mjini Zanzibar alikokuwa amelazwa.

Amina alilazwa Hospitalini hapo baada ya kuzidiwa (kushikwa na uchungu) kutokana na ujauzito na kukimbizwa kupata huduma katika hospitali hiyo ambpo alijifungua mtoto wa Kiume (bahati mbaya) na yeye akaendelea kupatiwa matibabu hadi ulipomkuta umauti leo asubuhi.

Amina alikuwa mjini Zanzibar kikazi alipokwenda kuripoti mashindano ya Kombe la Mapinduzi, ambapo alikuwa arejee jijini Dar es Salaam jana. Tutaendelea kupeata taarifa, ikiwa ni pamoja na mipngo ya mazishi, kwa kadri tutavyozipata.

Mungu ilaze roho ya Marehemu 
Amina Athuman mahala pema peponi
- Amina

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 15, 2017

MASHINDANO YA NAGE MAPINDUZI CUP YAFIKIA TAMATI, NAIBU WAZIRI NGONYANI, MASAUNI WAMWAGA ZAWADI KWA WASHINDI

$
0
0
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani akiwasalimia wachezaji wa Karakana City wakati akikagua timu za mchezo wa Nage zilizoingia Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017. Aliyevaa kofia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, ambaye ndiyo mwandaaji wa Mashindano hayo. Ngonyani aliyafunga Mashindano hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani akizungumza na mamia ya wananchi waliouhudhuria katika Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Katikati ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, ambaye ndiyo mwandaaji wa Mashindano hayo. Ngonyani aliyafunga Mashindano hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Kulia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala. Katika mashindano hayo, timu ya Six Centre iliibuka mshindi dhidi ya timu ya Karakana City zote za mjini Unguja. Picha na Felix Mwagara.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani (wapili kulia) kuja kufunga Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017 katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Katika hotuba yake Masauni ambaye ndiyo aliyeandaa msahindano hayo alisema, mchezo huo utazidi kuthaminiwa ili kuwaweka vijana pamoja. Picha na Felix Mwagara.
Mchezaji wa timu ya Six Centre ya Mwera ambayo imepata ushindi, akikwepa mpira katika mchezo wa Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017, kati ya timu hiyo na Karakana City ya Chumbuni, katika viwanja vya Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Picha na Felix Mwagara.
Msanii wa kizazi kipya, Kheri Sameer Rajab (Mr. Blue), akitoa burudani huku akishangiliwa na Waheshimiwa Wabunge pamoja na Wawakilishi wakati wa Fainali za Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017 yaliyofanyika katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. , Watatu kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akifuatiwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala. Picha na Felix Mwagara.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiwa katika picha ya pozi na Msanii wa nyimbo za Singeli, Manfongo kabla ya msanii huyo kupanda jukwaa kutoa burudani katika
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, (watatu kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na wasanii maarufu wa kizazi kipya kutoka Tanzania Bara na Visiwani kabla ya Wasanii hao kupanda jukwaani kutoa burudani katika Fainali ya Mashindano ya Nage Mapinduzi CUP 2016-2017 yaliyofanyika katika Uwanja wa Amani, mjini Unguja, Zanzibar. Mashindano hayo yaliandaliwa na Mhandisi Masauni ili kukuza vipaji vya vijana. Picha zote na Felix Mwagara.

ZIARA YA KAMISHNA MSAIDIZI NISHATI, KWENYE MRADI WA UMEME JUA UKEREWE

$
0
0
Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Styden Rwebangila (wa kwanza kulia) pamoja na wataalam kutoka Idara ya Nishati, Wizara ya Nishati na Madini wakiwa katika kivuko cha kuelekea katika Wilaya ya Ukerewe, Mwanza kwa ajili ya kukagua miradi ya umeme jua inayotekelezwa na kampuni ya Rex Energy.
Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Styden Rwebangila (kushoto) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mtendaji kutoka kampuni ya Rex Energy, Francis Kibhisa (kulia) katika ziara hiyo.
Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Styden Rwebangila (kulia nyuma) pamoja na wajumbe wengine wakielekea katika kisiwa kidogo cha Ghana/Siza kwa ajili ya kukagua miradi ya umeme jua inayotekelezwa na kampuni ya Rex Energy.
Mkurugenzi Mtendaji kutoka kampuni ya Rex Energy, Francis Kibhisa (kulia) akielezea hatua ya utekelezaji ya miradi ya kusambaza umeme katika kisiwa cha Ghana/Siza wilayani Ukerewe kwa Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Styden Rwebangila (kushoto).

MAKOSA MAKUBWA IKIWEMO UNYANG’ANYI WA KUTUMIA NGUVU/SILAHA NA MAUAJI YAONGEZEKA PWANI

$
0
0

Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

MKOA wa Pwani,umekuwa na ongezeko la makosa makubwa 4,208 yaliyoripotiwa katika mwaka 2016 ambapo makosa ya yaliyochukua nafasi kubwa ni unyang’anyi wa kutumia nguvu,kupatikana silaha na mauaji.

Ongezeko hilo ni la makosa 419 ukilinganisha na makosa yaliyoripotiwa mwaka 2015 yaliyokuwa 3,784 .Aidha makosa madogo 16,332 yaliripotiwa katika kipindi hicho cha mwaka 2016 ambapo kuna ongezeko la makosa 2,396 ikilinganishwa na mwaka 2015 uliokuwa na makosa 13,936.

Akitoa taarifa ya mwaka uliopita kwa waandishi wa habari,ofisini kwake,kamanda wa polisi mkoani Pwani Boniventure Mushongi ,alisema ,hali hiyo inawapa nguvu ya kuongeza kasi ya kupambana/kudhibiti njia za panya na njama wanazotumia wahalifu.

Hata hivyo alieleza,katika kipindi cha Jan hadi desemba 2016 ,kumekuwepo na baadhi ya matukio yaliyovuta hisia za watu ikiwemo tukio kupatikana kwa miili ya watu saba kwa nyakati tofauti wilayani Bagamoyo.Alitaja matukio mengine ni yaliyosababisha vifo vya viongozi wa serikali za za vijiji kwa Mkuranga ,Rufiji na Kibiti ambapo watu 11 walikamatwa na wameshafikishwa mahakamani.

Mushongi alisema kati ya makosa yaliyoripotiwa katika vituo vya polisi ni pamoja na unyang’anyi wa kutumia nguvu makosa 294 ukilinganisha na makosa 197 yaliyoripotiwa 2015 hivyo kuwa na ongezekjo la makosa 57.Makosa mengine ni kupatikana kwa silaha makosa 25 ambapo 2015 yalikuwa 20 ongezeko 5 na makosa ya mauaji kwa mwaka 2016 ni 126 huku 2015 yakiwa 107 tofauti 19.

Makosa mengine ni unyang’anyi wa kutumia silaha ,uvunjaji,magendo makosa 52,na makosa ya kubaka yameongezeka kutoka 340 hadi kufikia 416 mwaka 2016.Mushongi alieleza kuwa,ongezeko la makosa hayo imetokana na misako iliyofanywa, doria na oparesheni zilizokuwa zikifanywa kwenye maeneo mbalimbali na kushirikisha jamii.

“Tunawashukuru wananchi ,wasamaria wema,kwa ushirikainao wao na jeshi letu,tunawaomba waendelee na ushirikiano huo wa kutoa taarifa mbalimbali ambazo zinasaidia kukabiliana na uhalifu ““Uwiano wa askari na raia bado hautoshi kwani askari mmoja anahudumia raia zaidi 1,000 hivyo ulinzi shirikishi ni muhimu ndani ya jamii,” alisema Mushongi.

Alisema katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita walifikisha mahakamani makosa 1,439 sambamba na hilo watuhumiwa wa makosa 159 walikutwa na hatia na kuhukumiwa kifungo wakati makosa 29 watuhumiwa walishindwa kutiwa hatiani na kuachiwa huru.

Jeshi hilo licha ya kukabiliana na wahalifu mbalimbali lakini linakabiliwa na changamoto ya upungufu wa vitendea kazi ikiwa ni pamoja na uchache wa magari,Jiografia ya mkoa kwenye mipango miji ni ngumu kumpata mhalifu kwa haraka pindi uhalifu unapotokea.

Muingiliano na mkoa wa Dar es Salaam unafanya wahalifu kuweza kuingia kirahisi na kufanya makosa na uuwepo wa ukanda wa mkubwa katika bahari unaosababisha kuwepo kwa bandari bubu nyingi za kupitisha wahamiaji haramu na biashara za magendo.

KAMANDA wa polisi mkoani Pwani, Boniventure Mushongi, akitoa taarifa ya matukio ya mwaka 2016 ,yaliyotokea mkoani hapo kwa waandishi wa habari. (Picha na Mwamvua Mwinyi)

NAIBU WAZIRI KIGWANGALA AWAKABIDHI WAZEE 200 KADI ZA BIMA ZA AFYA JIMBO LA MASAUNI, UNGUJA ZANZIBAR

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala, akimkabidhi Bi. Salma Salum kadi ya bima ya Afya katika viwanja vya Mnarani, Mwembe Kisonge, Mjini Unguja, Zanzibar. Kadi zaidi ya 200 walikabidhiwa wazee wa Jimbo la Kikwajuni ambapo anatoka Mbunge wa Jimbo hilo ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto). Picha zote na Felix Mwagara
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimkaribisha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala, katika Sherehe za Kukabidhi Bima ya Afya kwa Wazee wa Jimbo la Kikwajuni, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnarani, Mwembe Kisonge, Mjini Unguja, Zanzibar. Picha na Felix Mwagara.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala akizungumza na wananchi wa Jimbo la Kikwajuni (hawapo pichani), kabla ya kukabidhi kadi za Bima ya Afya kwa wazee zaidi ya 200 wa jimbo hilo ambalo anatoka Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto). Kulia ni Mwakilishi wa Jimbo hilo, Nassor Salim Jazeera. Tukio hilo lilifanyika katika Viwanja vya Mnarani, Mwembe Kisonge, Mjini Unguja, Zanzibar. Picha na Felix Mwagara.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akuzungumza na wananchi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala (wapili kulia), kukabidhi kadi za Bima ya Afya kwa Wazee zaidi ya 200 wa Jimbo la Kikwajuni. Kulia ni Mwakilishi wa Jimbo hilo, Nassor Salum Jazeera. Tukio hilo lilifanyika katika Viwanja vya Mnarani, Mwembe Kisonge, Mjini Unguja, Zanzibar. Picha na Felix Mwagara.
Naibu Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapindiuzi, Zanzibar, Bi Harusi Said akizungumza na wananchi katika Sherehe za kukabidhi Bima ya Afya kwa Wazee zaidi ya 200 wa Jimbo la Kikwajuni ambapo anatoka Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) ambaye ni Mbunge wa Jimbo hilo. Tukio hilo lilifanyika katika viwanja vya Mnarani, Mwembe Kisonge, Mjini Unguja, Zanzibar. Picha na Felix Mwagara.

MAMA SAMIA ATOA DARASA KUBWA LA SIASA KWA WANA CCM KASKAZINI B UNGUJA

$
0
0

Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakazi wa mkoa wa Kaskazini B, Unguja wakati wa Kufungua Mafunzo maalum ya Viongozi na watendaji wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake wa ngazi ya Matawi, Wadi na Majimbo

Wana CCM wa Kaskazini B wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwenye mafunzo ya Uongozi yaliofunguliwa na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifundisha kwa vitendo masuala ya Uongozi kwa wakazi wa mkoa wa Kaskazini B, Unguja wakati wa Kufungua Mafunzo maalum ya Viongozi na watendaji wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake wa ngazi ya Matawi, Wadi na Majimbo.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kaskazini ,Unguja, Ndugu Juma Haji akihutubia kabla ya kumkaribisha Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Kaskazini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kufungua mafunzo maalum ya Uongozi yaliofanyika Mkokotoni Kaskazini B,Unguja kwenye Chuo cha Amali.





Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimjulia hali Waziri wa Mambo ya Ndani wa zamani Mzee Ali Ameir nyumbani kwake Donge Kichavyani, Zanzibar.

Msiba wa Marehemu Amina Athumani Mwandishi wa Habari za Michezo Gazeti la Uhuru na Mzalendo Kisiwani Zanzibar.

$
0
0
Katibu wa Kamati ya Kombe la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Zanzibar Ndg Khamis Said akimfariji Mume wa Marehemu Amina Athumani Ndg Toufik Majaliwa alipofika nyumbani kwa jamaa wa marehemu katika mtaa wa kariakoo unguja leo. kutowa mkono wa pole akiwa na waandishi wa habari za michezo Zanzibar ZASWA.

Kwa taarifa za msemaji wa familia Ndg Nurdin Ramadhani amesema mwili wa marehemu tasafirishwa kesho asubuhi na Boti ya Kampuni ya Azam Marine saa moja asubuhi kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika Kijiji kwao Lushoto siku ya Jumanne mchana. 

Mwili wa marehemu utawasili jijini Dar es Salaam saa tatu asubuhi ukitokea Zanzibar baada ya kuwasili katika bandari ya Dar es Salaam utasafirishwa kuelekea kijiji kwao Wilaya ya Lushoto Mkoano Tanga kwa ajili ya mazishi.
Katibu wa Kamati ya Kombe la Mapinduzi Zanzibar Ndg Khamis Said akizungumza na waandishi wa habari za michezo Zanzibar Zaswa alipofika nyumbani kwa ndugu wa marehemu katika mtaa wa kariakoo zanzibar.
Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa  Habari za Michezo Zanzibar Ndg Mwinyimvua Mnzuki akizungumza na waandishi wa habari kwa kupokea kwa masikitiko kifo cha mwandishi mwezao mrehemu amani athuman kilichotokea leo asubuhi katika hopspitali ya mnazi mmoja.
Ndugu wa marehemu wakiwa msibari wakisubiri taratibu za kusafirisha mwili wa marehemu kuelekea Wilayani Lushoto Mkoani Tanga.
Wanafamilia wa marehemu Amina Athumani wakiwa katika msiba huo katika mtaa wa kariakoo Zanzibar.
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot 
Zanzinews.com.
0777424152 Or 0715424152., 


MO Dewji akanusha kuzungumza kuhusu pesa za tetemeko la ardhi Kagera

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group), Mohammed Dewji amekanusha taarifa ambazo zimesambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa amefanya mahojiano na kituo cha Redio cha Times FM kuhusu pesa zilizochangishwa katika Tetemeko la Ardhi la Kagera lililotokea mwezi Septemba, 2016.


Dewji amesema hajafanya mahojiano na kituo chochote cha habari kuhusu tetemeko la Kagera na habari hiyo haina ukweli wowote zaidi ni mbinu ambayo imetumiwa na baadhi ya watu kwa ajili ya kuchafua jina lake na kampuni yake ya MeTL Group ambayo mpaka sasa ina wafanyakazi zaidi ya watu 28,000.

Aidha Dewji amesema ana imani na Serikali ya awamu ya tano na kuwatoa hofu Watanzania kuwa ataendelea kushirikiana na Serikali kusaidia jamii yenye uhitaji ikiwa ni sehemu ya ahadi yake ya kutumia nusu ya utajiri wake kusaidia watu wenye uhitaji.

“Nitumie nafasi hii kuwajulisha Watanzania wenzangu kuwa hii habari ambayo inasambazwa na watu katika mitandao ni ya uongo na haina ukweli wowote, sijafanya mazungumzo na media yoyote na mimi nilichangia pesa kwa nia nzuri, nina imani na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli kuwa inafanya kazi kwa faida ya watu wote bila kufanya ubaguzi,” amesema Dewji.

Katika ujumbe ambao unaonekana kusambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwepo Facebook, Instagram na WhatsApp imeandikwa kuwa MO Dewji amefanya mahojiano na Redio Times FM na kusema kama angejua mapema kuwa wahanga hawatopatiwa pesa hizo asingechangia

TAARIFA RUZUKU KWA WACHIMBAJI MADINI WADOGO AWAMU YA TATU

$
0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA NISHATI NA MADINI



 UTOAJI RUZUKU AWAMU YA TATU KWA WACHIMBAJI MADINI WADOGO, TAREHE 17 JANUARI 2017, MPANDA.

Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, kwa kushirikiana na Benki ya Dunia (WB) itatoa Ruzuku ya jumla ya Shilingi Bilioni 7.481 kwa Wachimbaji Madini Wadogo 59 waliokidhi vigezo vya kupata ruzuku hiyo kati ya 592 walioshindanishwa.


Hafla ya utoaji wa Ruzuku hiyo itafanyika siku ya Jumanne, tarehe 17 Januari 2017, Mjini Mpanda katika Uwanja wa Shule ya Msingi, 

KASHAULILI.

Mgeni Rasmi atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim  M. Majaliwa(Mb.).


Taarifa zaidi kuhusu  Ruzuku hiyo inapatikana katika Tovuti ya Wizara ya Nishati na Madini, www.mem.go.tzna Ofisi za Madini za Kanda.

Imetolewa na,

                                        

Prof. Justin W. Ntalikwa

KATIBU MKUU



Wakulima viazi Njombe waishukuru SAGCOT kuwawezesha

$
0
0
WAKULIMA wa viazi Mkoani Njombe wameushukuru Mpango wa kuendeleza Kilimo Ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT) kwa kuwaletea mradi wa uzalishaji na usambazaji mbegu bora za viazi pamoja elimu juu ya zao hilo ambapo sasa uzalishaji wake umeongezeka.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakulima wa viazi mkoani hapa wamewaambia waandishi habari jana kuwa kuwepo kwa mradi huu toka SAGCOT umetusaidia kutoka katika kilimo cha mazoea na kuingia kwenye kilimo biashara.

Mchungaji Michael Nyagawa toka kijiji cha Lunguya, kata ya Mtwango Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ni mmoja wa wakulima waliofaidika na mradi wa uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora za viazi toka SAGCOT alisema wakulima wa viazi walikuwa na mazingira magumu katika uzalishaji.

“Tulifika kipindi hekali moja ya viazi unavuna gunia 20 tu, lakini sasa tunapata gunia 60 mpaka 80 kwa hekali,” alisema MchungajiNyagawa na kufafanua kuwa kupitia mafunzo na mbegu mpya toka SAGCOT uzalishaji wa viazi umeongezeka na kuinua vipato kwa wakulima,” alisema.

Mchungaji huyo hakusita kusema kuwa kutokuwa na elimu ya kutosha kuhusu zao hilo vilichangia uzalishaji kuwa mdogo kama vile uandaaji wa shamba, namna ya kupanda mbegu, uhifadhi wa mbegu katika maghala na pia mbegu ilikuwa ya zamani sana.

“SAGCOT imetupatia mbegu za aina nne ambazo ni Tengeru,Sherekea,Asante na Meru ambazo zimetolewa bure kwa sisi wakulima” alisema Mchungaji Nyagawa na kuongezea kuwa hata pale tunapovuna mazao yote yanakuwa mali yetu.
Mtaalam na Mratibu wa Mradi wa kuzalisha na kusambaza mbegu bora za viazi mviringo kwa wakulima – Njombe toka SAGCOT, Bw.Owekisha Kwigizile akitoa mafunzo kwa wanakikundi cha Matunda group katika kata ya Mhaji, halmashauri ya Wilaya ya wanging’ombe Mkoani Njombe hivi karibu alipowatembelea na kuwaelimisha juu y Mradi wa kuzalisha na kusambaza mbegu bora za viazi mviringo unaoratibiwa na Mpango wa kuendeleza kilimo ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT). Chini ya unafadhiliwa na Serikali ya watu wa Marekani(USAID) kupitia Shirika la Kimataifa la kusimamia mapinduzi ya kijani barani Afrika(AGRA).
Mkulima Bi Sara Martin akimwonesha kitu Mtaalam na Mratibu wa Mradi wa kuzalisha na kusambaza mbegu bora za viazi mviringo kwa wakulima – Njombe toka SAGCOT, Bw.Owekisha Kwigizile alimpomtembelea shambani kwake katika kijiji cha Maduma kata ya Kichiwa ,Halmashauri ya wilaya ya Njombe na kuona maendeleo ya kilimo cha zao hilo. Mradi huo unafadhiliwa na Serikali ya watu wa Marekani(USAID) kupitia Shirika la Kimataifa la kusimamia mapinduzi ya kijani barani Afrika(AGRA)na kuratibiwa na Mpango wa kuendeleza kilimo ukanda wa kusini mwa Tanzania(SAGCOT).
Mkulima Bi. Agusta Madembwe wa kijiji cha Nyanga, kata ya Ikuna, Halmashauri ya wilaya ya Njombe akikagua shamba lake alilipanda mbegu mpya za viazi mviringo alizozipata kupitia Mradi wa kuzalisha na kusambaza mbegu bora za viazi mviringo kwa wakulima – Njombe unaoratibiwa na Mpango wa kuendeleza kilimo ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT). Akiwa na matumaini makubwa ya uzalishaji kwani amelima kwa njia ya kisasa.


KIASI CHA DOLA ZA MAREKANI BILIONI MOJA ZATENGWA KUIMARISHA ZAO LA MUHOGO NCHINI

$
0
0
KIASI cha Dola za Marekani bilioni moja kimetengwa kwa ajili ya kuimarisha zao la muhogo nchini kupitia mkataba wa kibiashara baina ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya Tanzania Agricultural Export Processing Zone Limited and Epoch Agriculture (TAEPZ) kutoka China.

Akizungumza wakati wa utiaji saini makubaliano hayo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda Dk. Adelhelm Meru, alisema huu ni wakati wa wakulima kunufaika na Kilimo cha muhogo baada ya kulima kimazoea.

Alisema, kwa muda mrefu Watanzania wamekua wakilima muhogo kwa ajili ya chakula tu huku wakisafirisha muhogo ghafi hali inayokosesha serikali mapato na kunufaisha mataifa ya nje kupitia zao hilo lenye manufaa mengi.

“Lengo la serikali kuwa na uchumi wa viwanda linaanza kutimia, huu ni uwekezaji mkubwa katika sekta ya kilimo cha biashara. Kutakuwa na shamba kubwa la mihogo, kutajengwa viwanda mbalimbali vya kuzalisha unga wa mihogo, makopa, chakula cha mifugo, sukari ya viwandani na mbolea.

“Hii fursa tusiiache, kama mlikua mkilima mihogo kwa kiwango kidogo ongezeni mashamba kwa sababu soko la uhakika lipo, pia tunashauri mnunue hisa katika kampuni hii ili ikiwezekana tuimiliki kwa kiwango kikubwa,” alisema Dk. Meru.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda Dk. Adelhelm Meru (kushoto), akiwa na Mwenyekiti wa TAEPZ, Dior Feng wakati wa kutia saini makubaliano ya mradi wa zao la muhogo nchini utakaogharimu Dola za Marekani bilioni 1. Waliosimama kutoka kushoto ni balozi wa China nchini, Dk. Lu Youqing na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF), Godfrey Simbeye. Mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda Dk. Adelhelm Meru (kushoto), akibadilishana nyaraka na Mwenyekiti wa TAEPZ, Dior Feng baada ya kusaini mradi wa zao la muhogo nchini utakaogharimu Dola za Marekani bilioni 1. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni balozi wa China nchini, Dk. Lu Youqing na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF), Godfrey Simbeye. Mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda Dk. Adelhelm Meru, akizungumza katika hafla ya utiaji saini makubaliano ya mradi wa kusindika muhogo nchini utakaogharimu Dola za Marekani bilioni 1, wengine katika picha ni Mwenyekiti wa TAEPZ, Dior Feng na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF), Godfrey Simbeye. Mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

.RC MAKALA AAGIZA WANAFUNZI 214 WALIOKOSA MADARASA WAANZE MASOMO KESHO JUMATATU

$
0
0
Image may contain: 6 people, people smiling, crowd and outdoor
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mh.Amos Makala leo amekagua ukamilishaji wa madarasa kwa wanafunzi 406 waliokuwa wamekwama kuanza masomo kutokana na upungufu wa Madarasa.

Kati ya wanafunzi 406 waliokosa nafasi kuanza masomo ni 192,madarasa yao yamekamilika na wanafunzi 214 madarasa yao yatakamilika ndani ya siku 14.


"Hivyo ili wanafunzi 214 wasiendelee kuchelewa kuanza masomo yao,nimeagiza kuwa maabara ambazo zipo na hazijaanza kutumika kwa kukosa Vifaa, sasa zitumike kama madarasa kuanzia kesho Jumatatu, na baada ya madarasa kukamilika Januari 30 2017,Wanafunzi hao watatumia madarasa hayo",alisema Mh.Makala.


Rc.Makala amezipongeza halmashauri za jiji la Mbeya na Mbeya vijijini kwa kuchangia ukamilishaji wa madarasa na amewashukuru wananchi na wadau kwa kuchangia ujenzi wa madarasa.Habari Picha na Mr Pendo-MMG.
Viewing all 110090 articles
Browse latest View live




Latest Images