Mashindano ya Mitumbwi Musoma Vijiji yaliyoshirikisha Kata 12 yamemalizika kwa Kata ya Etaro kuibuka na ushindi na hivyo kujinyakulia fedha tasilimu milioni moja pamoja na kombe.
Mashindano hayo yaliandaliwa hivi karibuni na Mbunge wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo kwa ajili ya kuuaga mwaka 2016 na kuukaribisha mwaka 2017 ambapo washindi wa pili ambao ni Kata ya Nyakatende walijinyakulia shilingi 750,000 na washindi wa tatu ambao ni Kata ya Suguti kujinyakulia shilingi 500,000 na huku wanaofuatia walipata shilingi 20,000 kwa kila Kata.
Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma Vijijini na Diwani wa Kata ya Mugango, Charles Magoma, alimpongeza Profesa Muhongo kwa kuanzisha mashindano ya namna hiyo jimboni humo kwani yamekutanisha wananchi wa Musoma Vijijini kutoka pande mbalimbali za jimbo hilo.
Aliongeza kwamba mashindano hayo yameleta mwamko mkubwa miongoni mwa vijana hasa ikizingatiwa kuwa hakuna mashindano ambayo huwakutanisha vijana kwa wingi kama ilivyokuwa kwa mashindano hayo ya mtumbwi.
Mbunge wa Musoma Vijijini na muandaaji wa Mashindano ya mitumbwi Musoma vijijini, Profesa Sospeter Muhongo akizungumza baada ya mashindano.
Washindani wakiendelea na mashindano ndani ya ziwa Victoria katika kata ya Etaro, Musoma Vijijini
Wananchi wa Musoma Vijijini wakishangilia wakati wa mashindano ya Mitumbwi
Timu ya International iliyoshika nafasi ya mwisho ikiwasili
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma Vijijini na Diwani wa Kata ya Mugango, Charles Magoma (kushoto) akikabidhi zawadi kwa washindi wa kwanza.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA