Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

MASHINDANO YA MITUMBWI MUSOMA VIJIJINI YAMALIZIKA

$
0
0
Mashindano ya Mitumbwi Musoma Vijiji yaliyoshirikisha Kata 12 yamemalizika kwa Kata ya Etaro kuibuka na ushindi na hivyo kujinyakulia fedha tasilimu milioni moja pamoja na kombe.

Mashindano hayo yaliandaliwa hivi karibuni na Mbunge wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo kwa ajili ya kuuaga mwaka 2016 na kuukaribisha mwaka 2017 ambapo washindi wa pili ambao ni Kata ya Nyakatende walijinyakulia shilingi 750,000 na washindi wa tatu ambao ni Kata ya Suguti kujinyakulia shilingi 500,000 na huku wanaofuatia walipata shilingi 20,000 kwa kila Kata.



Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma Vijijini na Diwani wa Kata ya Mugango, Charles Magoma, alimpongeza Profesa Muhongo kwa kuanzisha mashindano ya namna hiyo jimboni humo kwani yamekutanisha wananchi wa Musoma Vijijini kutoka pande mbalimbali za jimbo hilo.



Aliongeza kwamba mashindano hayo yameleta mwamko mkubwa miongoni mwa vijana hasa ikizingatiwa kuwa hakuna mashindano ambayo huwakutanisha vijana kwa wingi kama ilivyokuwa kwa mashindano hayo ya mtumbwi.


 Mbunge wa Musoma Vijijini na muandaaji wa Mashindano ya mitumbwi Musoma vijijini, Profesa Sospeter Muhongo akizungumza baada ya mashindano.
 Washindani wakiendelea na mashindano ndani ya ziwa Victoria katika kata ya Etaro, Musoma Vijijini
 Wananchi wa Musoma Vijijini wakishangilia wakati wa mashindano ya Mitumbwi
 Timu ya International iliyoshika nafasi ya mwisho ikiwasili
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma Vijijini na Diwani wa Kata ya Mugango, Charles Magoma (kushoto) akikabidhi zawadi kwa washindi wa kwanza.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AUPONGEZA UONGOZI WA UBALOZI MDOGO CHINA,ZANZIBAR

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameupongeza Uongozi wa Ubalozi Mdogo wa Jamuhuri ya Watu wa China uliopo Zanzibar kwa maandalizi mazuri iliyofanya kuratibu ratiba ya ziara yake ya Siku Tano aliyoifanya hivi karibuni Nchini China.

Alisema ziara hiyo ya Kiserikali ilimuwezesha na kumpa fursa ya kukutana na Uongozi wa Kampuni na Taasisi mbali mbali za China zilizoonyesha nia ya kutaka kuwekeza vitega uchumi vyao Visiwani Zanzibar.

Balozi Seif Ali Iddi alieleza hayo hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar wakati wa mazungumzo yake na Balozi Mdogo wa Jamuhuri ya Watu wa China hapa Zanzibar Bwana Xie Xiaolon akimshukuru kwa kukamilisha ziara hiyo kwa mafanikio makubwa.

Alisema Mikutano ya pamoja kati ya Ujumbe wa Zanzibar na Uongozi na Makampuni mbali mbali waliyokutana nayo yalikuwa na muelekeo mwema wa ushirikiano kati ya pande hizo mbili.

“ Ratiba yote iliyopangwa ndani ya ziara hiyo imetekelezwa kwa asilimia kubwa na kuonyesha matumaini mapya ya ushirikiano na uhusiano uliopo kati ya China na Zanzibar na Tanzania kwa ujumla”. Alisema Balozi Seif.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alimueleza Balozi mdogo wa China aliyepo Zanzibar kwamba Makampuni ya Umeme ya TBEA, Uvuvi ya Hongdong, ile inayotoa huduma za Kijamii ya Avic pamoja na Kampuni ya MCC – Oversease tayari wataalamu wake wameshaangalia mazingira ya Zanzibar na kujiandaa namna ya kuanzisha miradi yao Zanzibar.

Naye Balozi Mdogo wa Jamuhuri ya Watu wa China Bwana Xie Xiaolon alisema Zanzibar na China daima zitaendelea kushirikiana katika njia ya uanzishwaji wa miradi ya pamoja itakayosaidia kuleta ustawi wa wananchi wa sehemu hizo mbili.

Bwana Xie alimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba juhudi zitaendelea kuchukuliwa katika kuona miradi ya maendeleo iliyoanzishwa kupitia msaada au udhamini wa Serikali ya China itatekelezwa na kukamilika kama ilivyokusidiwa.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Kulia akizungumza na Balozi Mdogo wa Jamuhuri ya Watu wa China aliyepo Zanzibar Bwana Xie Xiaolon Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.Mazungumzo hayo yalikuwa na lengo la kuushukuru Ubalozi wa Ubalozi huo kwa kufanikisha uratibu wa Ziara ya Kiserikali ya Balozi Seif aliyoifanya hivi karibuni Nchini China.

Picha na – OMPR – ZNZ.

RAIS DKT. MAGUFULI ATEMBELEA MAENEO YALIOATHIRIKA NA TETEMEKO NA KUWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI IHUNGO MKOANI KAGERA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na balozi wa Uingereza hapa nchini Sarah Cooke (kushoto) wakiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihungo mkoani Kagera. Shule hiyo inajengwa upya kufatia kuathirika na tetemeko la Ardhi lililotokea mkoani humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitazama wakati Balozi wa Uingereza hapa nchini Sarah Cooke alipokuwa akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihungo mkoani Kagera. Wakwanza kushoto ni Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Balozi wa uingereza hapa nchi Sarah Cooke wakikagua ujenzi wa majengo ya Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihungo mkoani Kagera.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo nchini (TBA) Elius Mwakalinga akitoa maelezo ya mradi huo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa ukaguzi.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo nchini Elius Mwakalinga akitoa maelezo ya mradi huo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa ukaguzi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Charles Masinde mmoja wa wanachi mkoani Kagera aliyeamua kujenga nyumba yake mwenyewe mara baada ya tetemeko. Rais Dkt. Magufuli amemuahidi mwananchi huyo kuwa atampatia mabati 30 kwa ajili ya kuezekea nyumba yake.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifafanua jambo wakati alipokuwa akikagua majengo ya shule ya Sekonadri ya Wavulana Ihungo ambayo yanajengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).

RAIS DKT MAGUFULI AMALIZA ZIARA YA SIKU MBILI MKOANI KAGERA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Jumatatu  Januari mbili, 2017 amemaliza ziara yake ya siku mbili Mkoani Kagera kwa kuwatembelea baadhi ya wananchi walioathiriwa na tetemeko la ardhi pamoja na kukagua baadhi ya miundo mbinu iliyoathiriwa na tetemeko hilo na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa majengo ya shule ya sekondari ya Ihungo  Omumwani iliyobomolewa na tetemeko la ardhi la Septemba 10,2016.
Mara baada ya ukaguzi huo Rais Dkt Magufuli akazungumza na wananchi wa Mkoa huo wa Kagera katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Ihungo na kuagiza kuvunjwa kwa kamati ya maafa ya Mkoa huo iliyokuwa ikiratibu utoaji wa misaaada na kufanya tathmini ya athari ya tetemeko hilo.
”Kila kitu huwa kina mwanzo na mwisho wake ukiwa na harusi huwa kuna kamati ya harusi,ukishamaliza kufunga ndoa kamati ya harusi huwa inavunjwa,na ukiwa kwenye msiba huwa kuna kamati ya msiba na msiba  mkishazika kamati ya mazishi huvunjwa,kamati ya maafa ya Kagera huu ni mwezi wa tano na inawezekana hata kwenye kamati huwa wanalipana posho,sasa nataka hii kamati nayo iishe,yalishapita yamepita”
Aidha Dkt Magufuli amewataka wote walioahidi kuchangia katika kamati ya tetemeko la ardhi ya mkoa wa Kagera ambao bado hawajatekeleza ahadi zao ambazo ni jumla ya shilingi bilioni nne nukta tano wakamilishe ahadi hizo ili ziweze kumalizia miundombinu ya Serikali iliyoathiriwa na tetemeko hilo.
Ameongeza kuwa wale wote wanaoendelea kuguswa kusaidia wapeleke michango yao moja kwa moja kwa wananchi badala ya kuipeleka serikalini kwa kuwa hakuna mchango mwingine utakaopokelewa katika Ofisi ya Waziri Mkuu.
Pia Rais Dkt Magufuli ameagiza shule ya Sekondari ya Omumwani iliyokuwa inamilikiwa na Jumuia ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi CCM imilikiwe na Serikali kutaka wanafunzi wote wanaosoma katika shule hiyo kutolipa ada kama zilivyo shule nyingine za serikali.
Dkt Magufuli ameuagiza uongozi wa Mkoa wa Kagera kupunguza utitiri wa kodi katika zao la kahawa ili bei ya zao hilo ipande na kuwanufaisha wakulima
Balozi wa Uingereza hapa Nchini Bi Sarah Cooke ambaye nchi yake imechangia kiasi cha shilingi bilioni sita kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Sekondari ya Ihungo, amempongeza Rais Dkt Magufuli na serikali yake kwa jitihada za kupambana na rushwa suala ambalo nchi yake ya Uingereza inalipa kipaumbele sambamba na kutoa elimu bila malipo jambo linalowawezesha watoto wengi wa kitanzania kupata elimu bure

Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Kagera.
02 Januari, 2017

My farewell address - President Barack Obama

$
0
0
The White House, Washington

In 1796, as George Washington set the precedent for a peaceful, democratic transfer of power, he also set a precedent by penning a farewell address to the American people. And over the 220 years since, many American presidents have followed his lead.
I'm just beginning to write my remarks. But I'm thinking about them as a chance to say thank you for this amazing journey, to celebrate the ways you've changed this country for the better these past eight years, and to offer some thoughts on where we all go from here.
Since 2009, we've faced our fair share of challenges, and come through them stronger. That's because we have never let go of a belief that has guided us ever since our founding -- our conviction that, together, we can change this country for the better.

Because, for me, it's always been about you.
President Barack Obama

MKASA MZIMA WA KIJANA ANAYESHIKILIWA NA JESHI LA POLISI RUVUMA KWA KUSADIKIWA KUMUUA BABA YAKE MZAZI

$
0
0

Kijana anayejulikana kwa jiana la Patrick Malindisa ( 29 ) mkazi wa Namanyigu kata ya mshangano Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma,anashikiliwa na jeshi kwa kusadikiwa kumuua baba yake mzazi anitwaye Atanasi Malindisa. Mkasa Mzima huu hapa. 

TANZIA: MAZISHI YA BIBI CATHERINE MARWA (89) YAFANYIKA KENYAMANYORI TARIME MKOANI MARA.

$
0
0
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Anglikana Jimbo la Tarime mkoani Mara, akiongoza ibada ya mazishi ya marehemu, bibi Catherine Seba Marwa (89). Mazishi yamefanyika hii leo katika Kata ya Kenyamanyori wilayani Tarime.
Na BMG
Ndugu, jamaa na marafiki wakiuaga mwili wa marehemu
Mtoto wa marehemu (kushoto) akiwa na shemeji yake, wakiweka shada
Viongozi wa dini wakiweka mashada
 Marehemu, bibi Catherine Seba Marwa (89), enzi za uhai wake. Mola aipumzishe roho ya marehemu, mahala pema, peponi, Amina!

News Alert: Salum Mayanga ndiye kocha wa muda wa ‘Taifa Stars’, mkataba wa Mkwasa wamalizika March mwaka huu

$
0
0
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limemteua Salum Mayanga (kulia) kuwa kocha wa muda  (Interim coach), wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’.

Kocha Salum Mayanga, ambaye alikuwa kocha msaidizi wa Taifa Stars, anachukua nafasi ya Kocha Charles Boniface Mkwasa (pichani chini) ambaye mkataba wake unafikia mwisho mwezi Machi, mwaka huu - 2017.

Kati ya majukumu yake yatakuwa ni kuandaa kikosi cha timu ya Taifa kwa ajili ya hatua ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2019 ambazo mechi za awali zitanza mapema mwaka huu.

Pia Kocha Mayanga atakuwa na jukumu la kuandaa kikosi cha wachezaji wa ndani kwa ajili ya hatua ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi ya ndani (CHAN).

TFF inamshukuru Kocha Charles Boniface Mkwasa kwa utumishi katika nafasi hiyo ulioanza Julai, 2015 na kumtakia mafanikio katika mipango yake inayofuata.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA 
MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)





RAIS DKT. MAGUFULI AWASALIMIA WAKAZI WA BUKOBA MJINI, MULEBA NA MUGANZA MKOANI GEITA

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wakazi wa Bukoba mjini mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili mkoani Kagera.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wakazi wa Muleba mkoani Kagera mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili mkoani humo.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wakazi wa Muganza Wilayani Chato mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili mkoani Kagera. PICHA NA IKULU

RAIS WA ZANZIBAR DK.SHEIN ATEMBELEA KARAKANA YA MATREKTA MBWENI

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) pamoja na Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na watendaji  mbali mbali  wa Serikali wakipata maelezo kutoka kwa Fundi Mkuu  wa Kiwanda cha Matrekta Nd,Haji Haji Makame (Mtumbatu) kuhusu mashine zinavyofanyakazi kutokana na uchakavu wake,  wakati alipofika kutembelea Kiwanda hicho leo, Mbweni Wilaya ya Magharibi "B" Unguja,(wa pili kulia) Waziri wa Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Mhe. Hamad Rashid Mohamed.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) pamoja na Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na Viongozi mbali mbali  wakipata maelezo kutoka kwa Fundi Mkuu  wa  Kiwanda cha  Matrekta Mbweni Nd,Haji Haji Makame (Mtumbatu) walipofika kuangalia mashine   zinavyofanyakazi kutokana na uchakavu wake,  wakati walipofika kutembelea Kiwanda hicho leo huko Mbweni Wilaya ya Magharibi "B" Unguja,(wa pili kulia)Waziri wa Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Mhe,Hamad Rashid Mohamed
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na watendaji  mbali mbali wa Serikali  wakati walipotembelea  Kiwanda cha  Matrekta Mbweni  Wilaya ya Magharibi "B" Unguja. Kushoto ni mkuu wa Kiwanda Ndg. Mohamed Omar
 Waziri wa Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Mhe Hamad Rashid Mohamed  akitoa maelezo mafupi na kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) kuzungumza na wafayakazi wa Kiwanda cha  Matrekta Mbweni  Wilaya ya Magharibi "B" Unguja leo,baada ya kukitembelea akiwa na Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na watendaji mbali mbali Serikali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kushoto) alipokuwa akizungumza na Wafanyakazi wa Kiwanda cha  Matrekta Mbweni  Wilaya ya Magharibi "B" Unguja leo,alipofayna ziara maalum ya kukitembelea kiwanda hicho akiwa na ujumbe wa Baraza la Mapinduzi na watendaji  mbali mbali wa serikali. Picha na IKULU.
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 02/01/2017

RAIS DKT. MAGUFULI ATEMBELEA MAENEO YALIOATHIRIKA NA TETEMEKO NA KUWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI IHUNGO MKOANI KAGERA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na balozi wa Uingereza hapa nchini Sarah Cooke (kushoto) wakiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihungo mkoani Kagera. Shule hiyo inajengwa upya kufatia kuathirika na tetemeko la Ardhi lililotokea mkoani humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitazama wakati Balozi wa Uingereza hapa nchini Sarah Cooke alipokuwa akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihungo mkoani Kagera. Wa kwanza kushoto ni Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Balozi wa uingereza hapa nchi Sarah Cooke wakikagua ujenzi wa majengo ya Shule ya Sekondari ya Wavulana Ihungo mkoani Kagera.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo nchini (TBA) Elius Mwakalinga akitoa maelezo ya mradi huo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa ukaguzi.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo nchini Elius Mwakalinga akitoa maelezo ya mradi huo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa ukaguzi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mbunge wa Bukoba mjini(CHADEMA) Wilfred Lwakatare mara baada ya kuwasili katika shule ya Sekondari Ihungo mkoani Kagera. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Rc Gambo akabidhi Tsh. Mil 624 Kama Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake na Vijana mkoani Arusha

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (katikati) akizungumza na vikundi vya wanawake na vijana kutoka katika Jiji la Arusha kabla ya Kukabidhi hundi za Mikopo ya robo ya kwanza na ya Pili kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Nteghenjwa Hosseah, Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo amefungua mafunzo ya ujasiriamali kwa vikundi vinavyokopeshwa na kutoa mikopo kwa vikundi 85 vya wanawake na vikundi 40 vya vijana kutoka katika kata zote za Jiji la Arusha.

Akikabidhi hundi zenye thamani ya Sh Mil 624 kwa vikundi hivyo ikiwa ni mikopo ya robo ya kwanza na ya pili kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Mhe. Gambo amewataka kinamama na vijana kutumia fedha hizo kwa shughuli zilizokusudiwa ili ziweze kuleta manufaa na kuwatoa katika lindi la umasikini.

 “Mikopo hii inatolewa ili kuendeleza shughuli za kijasiriamali ambazo ndizo zilizopelekea mkidhi vigezo vya kupata Fedha; Nimatumaini yangu fedha hizi zitawawezesha kuongeza mitaji yenu na kuwapa ari ya kujituma zaidi huku mkizingatia nidhamu ya pesa ili muweze kuzirejesha kwa wakati na makundi mengine waweze kupata fedha hizo”Alisema Rc Gambo.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo(Katikati) akikabidhi hundi ya Tsh Mil 425 kwa wawakilishi wa Wanawake Bi. Mariamu Okash(Kata ya Kati) na Rose Charles(Kata ya Olorieni).

Aliongeza kuwa tofauti na mikopo hii ya halmashauri baada ya kuwawezesha vijana waendesha boda boda kwa kuwapatia Pikipiki 200 kundi litakalofuata ni wakinamama ambao watanufaika na Fedha zitakazorejeshwa na vijana hao kwa kupewa mitaji midogomidogo kadiri ya uhitaji.

Aidha Rc Gambo alimuagiza Mkurugenzi wa Jiji kuunda timu maalumu ya kuchunguza utoaji wa Mikopo kwa Kipindi cha Miaka mitatu kama ilifuata taratibu, vikundi vilivyonufaika kama ni hai  na hali ya urejeshaji.

Naye Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Mhe. Kalisti Lazaro Bukhay ambaye alishiriki katika zoezi  la utoaji mafunzo na kukabidhi hundi amesema Kikundi ambacho hakitarejesha fedha zote za mkopo ama kuchelewesha marejesho kwa namna yeyote ile hakitapatiwa mkopo katika mwaka unaofuata ila wale watakaofanya vizuri katika biashara zao na kukuza mitaji wataongezewa kiasi cha kukopa kulingana na hali ya shughuli zao.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.Mrisho Gambo akikabidhi hundi ya Tsh Mil 199 kwa wawakilishi wa Vijana Amos Kosani (Daraja II) na Janeth Prosper (Kata ya Unga Ltd).

CHUPU CHUPU KATIKA BARABARA YA MANDELA ASUBUHI HII

$
0
0
 Gari ndogo aina ya Toyota Ruxi yenye nambari za usajili T 530 DHT imenusurika kupiga mzinga asubuhi hii katika barabara ya Mandela jijini Dar es salaam, baada ya tairi moja ya mbele kulia kupasuka wakati ikiwa kwenye mwendo. hakuna madhara yaliyotokea katika tukio hilo.

Trump aupuuzilia mbali mkwara wa Korea Kaskazini

$
0
0
Rais mteule wa Marekani, Donald Trump, amepuuzilia mbali madai ya Korea Kaskazini kuwa imeunda Kombora linaloweza kuwasilisha zana za nyuklia hadi Marekani.

Katika mawasiliano kupitia mtandao wa Twitter, Trump aligusia majigambo ya kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, katika ujumbe wake wa mwaka mpya ambapo alisema kuwa maandalizi ya kombora la aina hiyo yamefikia hatua ya mwisho.

Trump alisema katika ujumbe wake kuwa "Haitawezekana." Tamko lake la haiwezekani, halikueleweka vizuri kwa sababu wachanganuzi hawajui iwapo alimaanisha kuwa Korea Kaskazini haina uwezo huo au alikuwa akiandaa hatua ya kujikinga.
Trump pia alishutumu Uchina kwa kushindwa kumdhibiti mshirika wake Korea Kaskazini na pia akailaumu Beijing kwa kupokea pesa kiasi kikubwa cha pesa na mali kutoka Marekani. CHANZO: BBC SWAHILI

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 3, 2017

KATIBU MKUU MPYA WA UMOJA WA MATAIFA ATOA WITO KWA DUNIA KULIPA KIPAUMBELE SUALA YA AMANI

$
0
0
Katibu mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ametoa wito kwa dunia kulipa kipaumbele suala la amani, ikiwa ni kauli yake ya kwanza baada ya kuchukua madaraka kutoka kwa mtangulizi wake Ban Ki-moon.

Guterres ambaye amewahi kuwa waziri mkuu wa Ureno na pia amewahi kufanya kazi kama mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, ameapa kufanya mabadiliko muhimu yanayohitajika ili kurejesha hadhi ya taasisi hiyo kwa kufanya marekebisho ya jinsi Umoja wa Mataifa unavyofanya kazi.
Katibu mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres
Katika siku za nyuma Guterres alinukuliwa akisema kuwa anachukua nafasi wakati ambapo watu duniani kote wakiwa hawana imani na viongozi wao, pamoja na taasisi nyingine za kimataifa ikiwemo Umoja wa Mataifa, na kuongeza kuwa anakusudia kutilia mkazo uboreshaji wa maeneo matatu ya kimkakati ambayo yanahitaji mabadiliko. 

Maeneo hayo ni pamoja na kujenga na kudumisha amani, kufikia maendeleo endelevu na kurekebisha utendaji kazi wa ndani wa umoja huo.

"Katika siku ya kwanza, nina swali moja zito katika moyo wangu, jinsi gani naweza kuwasadia mamilioni ya watu walionaswa katika migogoro na kuhangaishwa kwa kiasi kikubwa na vita visivyo na mwisho. Wanawake, watoto na wanaume wanauwawa, misafara ya misaada nayo inalengwa. Ninawaomba mniunge mkono kujitoa kwa ajili ya amani sasa na siku zote. Tuufanye mwaka 2017 uwe mwaka wa amani" alisema Guterres.

Guterres anaanza awamu ya kwanza ya miaka mitano ya uongozi wake akiwa anakabiliwa na migogoro nchini Syria, Yemen, Sudani Kusini na Libya huku kukiwa na majanga mengine duniani kama vile ugaidi na mabadiliko ya tabia nchi.
Amina Mohammed naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa
Kwa upande wake katibu mkuu ambaye amemaliza muda wake Ban Ki- moon, wakati akiwaaga wafanyakazi wa umoja huo, aliwashukuru kwa ushirikiano walioonyesha kwa kipindi chote ambacho amekuwa madarakani.

Suala la Marekani kuunga mkono umoja huo likibaki kuwa ni swali la kujiuliza kutokana na kuwa Marekani ni moja kati ya wanachama wa kudumu  wenye kura ya turufu katika baraza la usalama na inachangia asilimia 22 ya bajeti ya kawaida ya umoja wa mataifa, na asilimia 25 ya bajeti ya vikosi vya kulinda amani.

Guterres anatarajiwa kuanza kazi rasmi leo Jumanne (03.01.2017) ambapo atazungumza na wafanyakazi wengine wa Umoja wa Mataifa.CHANZO: DW

2017 UWE MWAKA WA KULIPA KODI KWA HIARI

$
0
0
Na Beatrice Lyimo- MAELEZO

MOJA ya malengo makuu ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuongeza nguvu katika ukusanyaji wa mapato nchini kwa lengo la kupanua wigo katika ukusanyanyi wa kodi ili kuimarisha mfumo wa utoaji huduma kwa wananchi.

Akifungua mkutano wa Bunge la 11 la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania mwaka jana mjini Dodoma, Rais Dkt. John Pombe Magufuli alisema Serikali yake itaongeza nguvu katika upanuzi wa wigo wa kodi na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato.

Rais Magufuli alisema, Serikali yake itahakikisha kila mtu anayestahili kulipa kodi analipa kodi stahiki kwa maendeleo ya nchi. 

“Hatutasita kumchukulia hatua mtu yoyote atakayekwepa kulipa kodi, tunawaomba wananchi mhakikishe mnapewa risiti kila mnaponunua bidhaa au huduma. Kodi ni kitu muhimu kila mtu anayestahili kulipa kodi alipe” alifafanua Rais Magufuli.

Aidha, alisema kuwa Serikali yake itahakikisha kila senti inayoongezeka katika mapato ya Serikali inaelekezwa katika kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi na kuziba mianya ya upotevu wa fedha za Serikali ambayo inapunguzia uwezo wa kuhudumia wananchi. 

Taarifa ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inamtaka kila Mfanyabiashara anayetumia mashine ya EFD anayekwepa kutoa risiti ni kosa la kisheria ambapo adhabu yake ni kulipa faini isiyopungua sarafu ya pointi 100 hadi pointi 150 ya thamani halisi ya fedha au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichozidi miaka mitatu au vyote kwa pamoja.

Aidha kwa mtu yeyote atakayeshindwa kudai au kutoa taarifa ya kukataliwa kupewa risiti au ankara ya malipo ya bidhaa au huduma atakuwa ametenda kosa na ikithibitika atatozwa faini isiyopungua sarafu ya pointi 2 na zisizozidi sarafu ya pointi 100.

Hata hivyo kila mfanyabiashara aliyesajiliwa na kodi ya Ongezeko la la Thamani anatakiwa kuzingatia kutumia mashine za kodi za kielektroniki (EFD).

Hivyo basi Utii wa Sheria bila shuruti  katika masuala ya kutoa na kudai risiti pindi tununuapo bidhaa ni jukumu letu sote na hivyo kupelekea ongezeko la mapato kwa maendeleo ya Taifa letu.

Aidha dira ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ni kuongeza mapato ya ndani kwa kuimarisha ulipaji wa kodi kwa hiari, hivyo watanzania wenzangu tushirikiane na Mamlaka hiyo katika kuongeza mapato ya ndani kwa maendeleo ya Taifa.

TUNAFARIJIKA NA KAZI KUBWA UNAYOIFANYA YA KUUJENGA UCHUMI WA TANZANIA-MH.LWAKATARE

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mbunge wa Bukoba mjini(CHADEMA) Wilfred Lwakatare mara baada ya kuwasili katika shule ya Sekondari Ihungo mkoani Kagera.

MWENYEKITI WA MTAA WA OYSTERBAY ATOA TAARIFA YA UTEKELEZAJI KWA MWAKA MZIMA 2016

$
0
0
Serikali ya Mtaa wa Oysterbay imeendelea kutekeleza maagizo na maadhimio mbalimbali yaliyoafikiwa ikiwamo kutatua changamoto na kero zinazowakabili Wananchi. Mtiririko wa Taarifa hiyo umejikita zaidi  kwenye maeneo ya ulinzi na Usalama wa Mazingira,mapato na matumizi na maendeleo kwa ujumla wake.                                                
 Mwenyekiti wa Mtaa serikali ya Mtaa Oysterbay Bw Zefrin Lubuva akizungumza na wajumbe pamoja na wananchi wa mtaa wa oysterbay kuhusubTaarifa hio ya Mwaka wa 2016 jijini Dar es salaam.
  Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Kinondoni Bw Abubakar Kunga akiongea na wananchi wa Mtaa huo kihusu amani na usalama kuelekea Mwaka mpya Unaoanza na kuwasihi wananchi kuwa makini wao wenyewe na mali zao kwa ujumla. Picha na Yassir Adam.                        
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images