Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

LUKUVI ATUA MKOANI MARA KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI

$
0
0
Na Hassan Mabuye 
(Kitengo cha Mawasiliano - Wizara ya Ardhi)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi anaendelea na Ziara zake za utatuzi wa Migogoro ya Ardhi nchini, ambayo imejikita zaidi katika kutatua migogoro ya ardhi ya Mikoa ya kanda ya Magharibi, Kaskazini na ile ya Kanda ya Ziwa hapa nchini.
Mhe. Lukuvi kwa siku ya jumatatu tarehe 19 Desemba 2016 atatua migogoro ya ardhi ya wilaya ya Musoma mkoani Mara na siku ya jumanne tarehe 19 Desemba 2016 atatua migogoro ya ardhi ya wilaya ya Bunda mkoani Mara.
Katika ziara hiyo Waziri Lukuvi atakutana na wananchi wa Musoma mjini na wananchi wa Bunda walio na kero za migogoro ya ardhi na kuzitatua pamoja na kutembelea miradi inayosimamiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika wilaya ya Musoma.
Aidha, Mhe. Lukuvi baada ya ziara hiyo anatarajiwa kuwasili mkoani Arusha ambapo pia atatua migogoro ya ardhi inayoukabili mkoa huo.
Hadi sasa Mhe. Lukuvi ndani ya mwezi huu wa Desesmba ameishatatua migogoro ya ardhi ya Mkoa wa Kigoma na wilaya zake za Kigoma mjini, Kasulu na Kibondo na katika Mkoa wa Shinyanga na wilaya zake za Kishapu na Shinyanga mjini na katika mkoa wa Geita amefanya ziara wilayani Chato.
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiongea na wananchi walio na migogoro ya ardhi wakati wa ziara zake mikoani.
Muonekano wa Halmashauri ya Musoma Mjini.

Newz Alert:Msanii Darassa na wenzake wanusurika kifo baada ya kupata ajali kahama,mkoani Shinyanga.

$
0
0


 Baadhi ya Wananchi wakilitazama gari hilo baada ya kupata ajali
Muonekano wa gari alilopata nalo ajali Msanii huyo na Wenzake,
Habari zilizoifikia Globu ya Jamii hivi punde zinaeleza kuwa Mwanamuziki wa Hip Hop Bongo ambaye ametokea kutikisa kwa kiasi kikubwa kupitia ngoma yake kali ya Muziki, Sharrif  Thabit ‘Darassa’ amenusurika kifo baada ya kupata ajali mbaya maeneo ya Ntobo barabara ya kuelekea Mgodi wa Bullyanhulu Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Habari zimeeleza kuwa ndani ya gari hilo aina ya Toyota Harrier yenye namba za usajili T503 DGQ, ambalo dereva hakufahamika mapema, Darassa alikuwa ameambatana na Director wake, Hanscana pamoja na producer wake, Abba Process na wote wametoka salama.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Darassa amethibitisha kupata ajali hiyo, na kama aonekanavyo kwenye hiyo clip ya video sehemu ya tukio ya ajali hiyo akimshukuru Mungu kwa kutoka salama yeye pamoja na wenzake. 

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana mpaka sasa.

MAMA JANETH MAGUFULI AUNGANA NA WANAPAROKIA Wenzake kusali Ibada ya Jumapili Kanisa la Mt. Petro Dar es Salaam

$
0
0
Desemba 18, 2016

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli leo Jumapili ameungana na Wakristo wenzake wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro iliyopo Oysterbay Jijini Dar es Salaam ikiwa ni wiki kadhaa tangu alipougua na kulazwa hospitali.

Akiwa mwenye afya njema na furaha Mama Magufuli aliyekuwa pamoja na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa wamesali ibada ya asubuhi katika kanisa hilo na baadaye kusalimiana na waumini nje ya kanisa.

Baada ya kumalizika kwa Ibada, baadhi ya Waumini wa Kanisa hilo wameelezea furaha yao ya kumuona Muumini mwenzao akiungana nao katika ibada na wamemuombea afya njema.

"Nimejisikia furaha sana kumuona Mama Magufuli amekuja Kanisani akiwa na afya njema na uso wa bashasha, na ninamuombea kwa Mungu aendelee kumsimamia"amesema Mama Mabula.

"Nimeshukuru sana kumuona Mama yangu Mama Magufuli, Mwanajumuiya mwenzangu leo Kanisani, huku afya yake ikiwa imetengemaa zaidi, tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu na tunamuombea aendelee kumpigania afya yake izidi kuwa imara"amesema Thomas Simon.

"Kwa kweli siku ya leo kwangu mimi ninafuraha sana kwa kumuona Mama akiwa kanisani, na zaidi Mama wote wawili kwa sababu pia amekuja Mke wa Mhe. Waziri Mkuu, kwa hiyo kwetu sisi ni furaha sana kama Parokia, tunafurahi sana tunaposhirikiana na viongozi wetu" ameongeza Epifania Ngonyani.


Mwezi uliopita Mama Janeth Magufuli aliugua na kulazwa katika wodi ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako alipata matibabu kwa siku mbili na kisha kuruhusiwa.

KARIBU MKULIMA MARKET CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAM KUANZIA ALHAMISI

$
0
0
Karibu katika Soko la Wazi yaani Mkulima Market litakalofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mkabala na UDASA Club. Ufungaji wa mabanda utafanyika Jumatano tarehe 21 Desemba 2016 kuanzia saa 3 asubuhi hadi 12 jioni. Siku ya ufungaji wa mabanda kutakuwa na mauzo ya bidhaa mbalimbali hususani mbogamboga na matunda kutoka Muheza.

Alhamisi, Ijumaa na Jumamosi (22, 24 na 24 Desemba 2016) kuanzia saa 3 asubuhi hadi 12 jioni ndio siku rasmi za maonesho na mauzo ya bidhaa mbalimbali toka kwa wadau wa kilimo, uvuvi, ufugaji na uwindaji. 

Elimu kuhusu biashara, ubora na ufungashaji wa bidhaa za kilimo utatolewa kila siku za maonesho kuanzia saa 5 asubuhi hadi saa 7 mchana kwenye Banda Darasa. Elimu hii ni ya wazi na bure kwa kila mudhuriaji na washiriki wa Mkulima Market.

Mkulima Market ni fursa ya kupata bidhaa bora kabisa kutoka shambani kwa bei ya shambani. Sasa ni wakati muafaka wa kuwapongeza wakulima, wafugaji, wavuvi na wawindaji wa Tanzania kwa kununua bidhaa zao katika msimu huu wa sikukuu

                                Hakuna kiingilio ni BURE kabisa kwa wahudhuriaji.
Kushiriki kuuza, kuonesha, kutoa huduma au kupata taarifa zaidi
Wasiliana na Mwandaaji Vicensia Shule 0767 254 887 
Mratibu Msaidizi (Ushiriki) Steven Peter Mfuko 0718 054 169 au tuandikie kupitia mkulimamarket@gmail.com au tufuate twitter, facebook, instagram na youtube @mkulimamarket kupata updates

WATOTO KLABU YA JWTZ YA LUGALO GOLF CLUB WAPIMANA UWEZO

$
0
0
Na Luteni Selemani Semunyu.

Viwango vya Watoto wanaocheza mchezo wa golf katika klabu ya Jeshi la Ulinzi la  Wananchi wa Tanzania ya Lugalo vinazidi kupanda na kuongeza uwezekano wa  kupata vipaji vipya  na Wawakilishi wa Taifa.

Hayo yalisemwa na Mmoja wa Walimu wa Mchezo huo katika Klabu ya Lugalo Elias Chiundu mara baada ya mashindano ya Watoto yaliyofanyika mwishoni mwa Wiki katika Uwanja wa Golf wa Lugalo Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waaandishi wa habari mwalimu huyo alisema yeye kama Mwalimu anafarijika kwa kuona viwango vya watoto hao vikikua na hivyo ni matarajio yake katika mwaka 2017 watafanya vyema Zaidi.

“Mwaka 2017 tunataraji baadhi ya watoto  waliokuwa wanacheza katika Daraja la Junior kutokana na Umri wao kuongezeka sambamba na kiwango cha uchezaji basi wataingia katika Divisheni Nyingine na kutoa changamoto kwa waliowakuta” Alisema Chiundu.

Aliongeza kuwa kuna Faida kubwa kwa Wachezaji kuandaliwa wangali wadogo kwani wanakuwa na kipindi kirefu cha  mafanikio iwapo wataweka jitihada sambamba na kuungwa mkono na wazazi.

Katika mashindano hayo mshindi wa kwanza  baada ya kucheza Viwanja 18 aliibuka  Habiba Likuli baada ya kupata  mikwaju ya jumla 89 kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 15 na hivyo kuibuka na Mikwaju ya Jumla 72 akifuatiwa na Sophia Juma aliyepiga Mikwaju ya Jumla 74.

 Mbali na Viwanja 18 pia katika kundi la Watoto waliocheza viwanja Tisa mshindi ni Abra Bella aliyepiga mikwaju ya jumla 48 na katika viwanja vitatu mshindi ni Salehe Ramadhani aliyepiga mikwaju ya jumla 17
Kwa upande wake mshindi wa mashindano hayo ya siku moja Habiba Likuli amesema mashindano yalikuwa mazuri licha ya changamoto ya jua kuwa kali na kuomba Wazazi  kuwaruhusu watoto wao kuja kushiriki nao ili kuonyesha vipaji na kutumia muda wao vizuri.

Jumla ya wachezaji 32 wameshiriki katika mashindano hayo yenye lengo la kupima ukuaji wa vipaji vyao.
 Mwalimu wa mchezo wa golf wa klabu  ya JWTZ  ya  Lugalo  Elias Chiundu akitoa maelekezo kwa watoto walioshiriki mashindano maalum ya mchezo huo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam. (Picha na Luteni Selemani Semunyu)
 Mshindi wa mashindano maalum ya watoto yaliyoandaliwa na klabu ya golf ya JWTZ ya Lugalo Habiba Likuli akipiga mpira huku wachezaji wenzie wakimuangalia katika hekaheka za mashindano hayo yaliyofanyika mwisho wa wiki  jijini Dar es salaam. 
 Washiriki wa mashindano maalum ya watoto wakihakiki matokeo yao mara baada ya kumaliza viwanja 18  ambapo Habiba Likuli aliibuka mshindi katika mashindano hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Lugalo jijini Dar es salaam.

Mshindi wapili wa mashindano maalum ya watoto yaliyoandaliwa na klabu ya golf ya JWTZ ya Lugalo, Sophia Juma  akipiga mpira huku wachezaji wenzie wakimuangalia katika hekaheka za mashindano hayo yaliyofanyika mwisho wa  wiki jijini Dar es salaam.

YATAMBUE MAMBO 10 YA KUKUSAIDIA KUPERUZI KWA USALAMA MTANDAONI

$
0
0

Sababu ya mtandao, Dunia ni kama kijiji kimoja.Mtandao umekuwa kitu cha muhimu kwenye maisha ya watu wengi sana,mitandao inatufanya tuwasiliane kwa urahisi na ndugu jamaa na marafiki mbalimbali,inatufanya kupata taarifa mapema zaidi kuliko vyanzo vingi vya taarifa vya ‘kizamani’ kama runinga, redio na magazeti,mitandao pia ni chanzo cha ajira kwa watu wengine.

Hapa chini nakupa dondoo kadhaa za kukusaidia walau kujihadhari na hatari ndogondogo ukiwa kama mtumiaji wa kawaida wa mtandao

1.Usisambaze taarifa zako ovyo.

Kuwa makini unapowasiliana na watu katika mitandao ya kijamii,na kuwa makini zaidi linapokuja suala la kumpa mtu taarifa zako nyeti kama akaunti za benki,au password,usidangaanyike na jumbe za kilaghai kama zinazokutaarifu kushinda bahati nasibu,kupata mkopo au mtu anayetaka kukupa dili lakini anataka taarifa hizo akuwekee kiasi fulani cha fedha,asilimia 99 huwa ni matapeli wa mtandaoni

2. Epuka malumbano yasiyo na maana mtandaoni

Moja ya sababu ya kuwa na mitandao,haswa ya kijamii ni kubadilishana mawazo na mijadala mbalimbali lakini kama ilivyo kwa imani tofauti tulizonazo,wakati mwingi mawazo huwa tofauti-wasilisha mawazo yako kwa hoja na sio mihemko,jifunze kukubali kutokubaliana na mawazo ya wengine kama hamjafikia tamati inayoendana,ni sawa kila mtu kuamua kuamini anachoamini.

La pili ni kukaa mbali na wazinguaji wa mtandaoni(Trolls) hawa ni watu ambao aidha hukataa kila kitu kwa ajili ya ubishi tu au hufanya hivyo kutafuta sifa na ‘likes’ kwa kuonekana wanaenda tofauti na mawazo ya wengine,hapa hata ukiwa na hoja za maana ni kazi bure kwani kwao ubishi wa mtandaoni ni kama mchezona zaidi ya yote epuka matusi,kumbuka kuna sheria za mitandao hivyo unaweza kujikuta mikononi mwa dola kwa sababu ya malumbano yasiyo na mantiki.

3. Usisambaze taarifa usizojua chanzo chake.

Umeamka asubuhi umekutana na taarifa kwenye kundi la WhatsApp mtu fulani maarufu amekufa,bila kuwa na uhakika sana unasambaza kwa makundi yako mengine 8 na jamaa zako kadhaa kwenye simu yako.Unakosea,mtandao ni kama bahari kubwa sana ya taarifa zipo taarifa za ukweli,za uongo za utanina kadharika,na kwa kukusaidia tu kama hujui kuna baadhi ya blogu na tovuti ambazo ni maalumu kwa ajili ya kuchapisha taarifa za utani/uongo(Mfano huzzlers.com)-NDIO,yaani taarifa zote utakazosoma humo ni za kutunga na kufikirika hivyo unapoona taarifa mpya jiridhishe kuhusu chanzo chake kabla ya kusambaza kwa wengine na kuendeleza upotoshaji.

4. Chunguza mtu unayewasiliana naye.

Kweli mitandao ya kijamii imetengenezwa kwa ajili ya kukutanishwa na marafiki,wale tunaowajua toka zamani mashuleni au wapya,lakini kuwa na utaratibu wa kumfahamu mtu unaejuana nae mara ya kwanza mtandaoni kabla ya kuanza kubadilishana nae taarifa zako muhimu na nyeti,kumtumia picha zako au za familia,kuna akaunti nyingine za mitandao ya kijamii ni za watu wanaotumia taarifa za uongo kuonyesha ni mtu au jinsia fulani kumbe sio hivyo inabidi utumie akili ya kuzaliwa katika kujiridhisha na uhalisia wa mtu unayewasiliana naye.

WAENDESHA PIKIPIKI ZINGATIEA KANUNI ZA BARABARANI NA KUFUATA SHERIA ZA BARABARANI.

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga  Firbato Sanga akizungumza na vijana wa Umoja wa  endesha piikipiki (Bodaboda) zaidi ya 1580 juu ya kuwataka waendesha Pikipiki hao kuzingatia mafunzo waliyoyapata ikiwamo kufuata sheria za barabarani na kuzingatia sheria za  barabarani na kanuni, katika hafla ya kuwapa vyeti na leseni iliyofanyika  mkoani Pwani. Picha zote na Emmanuel Massaka, Globu ya jamii.
 Mbunge wa  Jimbo la  Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na vijana wa Umoja wa  waendesha piikipiki (Bodaboda) zaidi ya 1580 na kuwataka kufanya Kazi hiyo Kwa uaminifu mkubwa na zaidi kuona ndio sehemu yao ya ajira kama zilivyo ajira zingine, katika hafla ya kuwapa vyeti na leseni mkoani Pwani.
 Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Mkuu wa Usalama barabarani Wilaya ya Mkuranga,Hamidu Mtianjola juu ya kufanya Kazi zao kihalali,ambapo aliwapongeza kwakuweza kuhitimu mafunzo hayo ya uendeshaji wa Pikipiki na miongoni mwao kupata leseni.
 Waendesha piikipiki (Bodaboda) Wakichangai damu katika hafla ya kuwapa vyeti na leseni mkoani Pwani.Picha na Emmanuel Massaka Globu ya Jamii.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

UJUMBE MWANANA


HIZI NDIZO ATHARI ZA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

$
0
0
Ng'ombe na mbuzi wakiwa wamesongamana chini ya mti pekee uliokuwepo katika eneo lililopo karibu na Shule ya sekondari ya Oljoro mkoani Arusha wakifuata kivuli ili kujikinga na jua Desemba 17, 2016. Uharibifu wa mazingira unaosabishwa na shughuli za binadamu hasa ukataji miti hovyo unaathiri hata viumbe wengine kama picha inavyoonyesha.
Mwendesha pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda akiwa amejipumzisha katika eneo lililoathiriwa na uharibifu wa mazingira unaofanywa na binadamu katika kijiji cha Ormapinu, Arusha Desemba 17, 2016.
Wananchi wakiwa wamebeba bango lenye maneno yanayoeleza suala la uharibifu wa mazingira kuwa ni tatizo kwao katika mkutano uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye kijiji cha Ondenderet, Arusha Desemba 17, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

JESHI LA MAGEREZA NA WAKALA WA MAJENGO - TBA WAINGIA MAKUBALIANO UJENZI WA NYUMBA 320 ZA ASKARI MAGEREZA MKOA WA DAR ES SALAAM

$
0
0
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo – TBA, Arch. Elius Mwakalinga akimkabidhi Mkataba wa Makubaliano ya mradi wa ujenzi wa nyumba 320 Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa. Hafla hiyo ya uwekaji saini makubaliano hayo ya ujenzi wa nyumba za askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dar es Salaam imefanyika leo Desemba 19, 2016 Jijini, Dar es Salaam katika Ukumbi wa TBA. Ujenzi wa nyumba hizo ni agizo la Rais Magufuli kufuatia ziara yake hivi karibuni ambapo alitoa kiasi cha bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za makazi ya askari wa Jeshi hilo.
  Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo – TBA, Arch. Elius Mwakalinga (kushoto) na Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) kwa pamoja wakisaini Mkataba wa Makubaliano ya ujenzi wa nyumba 320 za Askari wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa TBA, leo Desemba 19, 2016 Jijini, Dar es Salaam.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo – TBA, Arch. Elius Mwakalinga na Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) wakionesha nyaraka mbalimbali baada ya hafla fupi ya uwekaji saini wa Mkataba wa Makubaliano ya mradi wa ujenzi wa nyumba 320 za askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dar es Salaam.
 Maafisa Waandamizi wa Wakala wa Majengo - TBA wakifuatilia majadiliano kabla ya uwekaji saini wa Mkataba wa Makubaliano ya ujenzi wa nyumba 320 za Askari wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa TBA, leo 19 Desemba, 2016 Jijini Dar es Salaam.
 Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga(wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakishuhudia uwekaji saini wa Makubaliano ya ujenzi wa nyumba 320 za Askari wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa TBA, leo 19 Desemba, 2016 Jijini Dar es Salaam (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

RIPHAT HAMIS AKABIDHIWA HUNDI YAKE YA MCHEZAJI BORA WA MWEZI LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA

$
0
0
Mkuu wa Masoko na Usambazaji wa Vodacom Tanzania Kanda ya Pwani, Harrieth Koka (Kushoto) akimkabidhi hundi ya Tsh. Milioni 1/- kwa mchezaji wa Ndanda FC, Riphat Hamis aliyeibuka mchezaji bora wa ligi kuu mwezi uliopita kabla ya kuanza kwa mchezo wa timu yake na Simba SC hapo jana.Simba ilishinda 2-0(Na Mpiga picha wetu)

MABONDIA VICENT MBILINYI NA IDD MKWELA WAENDELEA KUJIFUA KWA SUPER D COACH

$
0
0
Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini, Rajabu Mhamila 'Super D' (kulia) akimnowa bondia Vicent Mbilinyi kwa ajili ya mpambano wake dhidi ya Mrisho Adamu, wa raundi kumi unaotarajiwa kufanyika Desemba 31, 2016 katika ukumbi wa Manyara Park, Jijini Dar es salaam.
Bondia Vicent Mbilinyi (kushoto) akionyeshana umwamba wa kutupiana makonde na Bondia Iddi Mkwela, wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Super D Coach Uhuru GYM, Kariakoo Jijini Dar es salaam. Mbilinyi anajiandaa na mpambano wake na dhidi ya Mrisho Adamu utakaofanyika Desemba 31 katika ukumbi wa Manyara Park Manzese, Jijini Dar es salaam.
Mabondia Iddi Mkwela (kushoto) na Vicent Mbilinyi wakioneshana umwamba wa kutupiana makonde. Picha na SUPER D BOXING NEWS

WANANCHI WAVAMIA KITUO CHA POLISI CHUNYA, MKOANI MBEYA

$
0
0
 Na Ripota wa Globu ya Jamii, Mbeya

Wananchi wa Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya wamevamia kituo cha Polisi Jeshi la Polisi  cha makongolosi kwa kufanya fujo na uwarushia mawe polisi wa kituo hicho kwa lengo la kuwatoa watuhumiwa wa kituo hicho wanaokabiliwa na mashtaka ya mauaji.

Akizungumza   baada ya tukio hilo , Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Naibu Kamishna wa Polisi Dhahiri Kidavashari, amesema kuwa  mnamo desemba 18, mwaka huu Kundi la wananchi  Mkoani Mbeyilaya ya Chunya, Tarafa ya Kiwanja, Kata ya makongolosi Wananchi waliamua kujichukulia sheria mkononi kwa kuvamia kituo cha Polisi Makongolosi na kufanya fujo kwa kuwarushia mawe askari wa Kituo hicho kwa  lengo la kuwatoa watuhumiwa wawili waliokuwa katika kituo hicho.

"mkoa wa Mbeya   kwa kushirikiana na wananchi na wadau wengine limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu  ili kuhakikisha matukio ya namna hiyo kuisha kabisa."


Aidha amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Erasto Robert, [28] mkazi wa Kilombero na Basil Linus [24] mkazi wa Makongolosi wanaodaiwa kukabiliwa na kosa la mauaji kwa RB namba [MKI/IR/1249/2016] kwa lengo la kuwatoa nje na kuwauawa kwa kuwachoma moto.  
Amesema kuwa  inadaiwa wananchi hao walifika Kituoni hapo kwa lengo la kuwatoa nje watuhumiwa hao wawili lakini, Diwani wa Kata ya Makongolosi Bwana Lusajo Ntofyo  aliweza kuongea na wananchi hao na kisha kutawanyika, Hata hivyo wananchi hao walifunga barabara ya Chunya-Makongolosi kwa kuweka mawe makubwa na magogo hali iliyosababisha usumbufu mkubwa wa watumiaji wengine wa barabara hiyo. 

Aidha katika vurugu hizo watu wanne walijeruhiwa ambao ni Dimita Mwangabula [24] fundi uashi, mkazi wa Makongolosi [aliumia miguuni na mikononi] 2. Amosi Kandonga [16] mkazi wa Kasumulu Wilaya ya Kyela [aliumia puani] 3. Hawa Masumbuko [21] mkazi wa Makongolisi [aliumia mkononi wa kulia] na 4. Amoke Mbilinyi [25] mkazi wa Makongolisi ambao walikimbizwa hospitali ya Wilaya ya Chunya kwa matibabu.
Hata Hivyo mbali Matukio hayo Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya pia linaongeza jitihada za kuzuia na kupunguza ajali za barabarani kwa kuhakikisha madereva na watumiaji wengine wa barabara wanatii sheria za usalama barabarani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishna wa Polisi Dhahiri Kidavashari ametoa wito kwa wananchi kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mkononi kwani vinasababisha madhara makubwa kwa watu wasiokuwa na hatia na usumbufu kwa wengine.
Sehemu ya Askari Polisi wa Mkoa wa Mbeya wakifanya ulinzi katika eneo la tukio.

BELLE 9 KUFUNGA MWAKA 2016 NA "GIVE IT TO ME"

$
0
0
Mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Fleva) hapa nchini, Abelnego Damian maarufu kama Belle 9 ameachia wimbo wake wimbo mpya unaoitwa ‘Give it to me’ aliomshirikisha G Nako kutoka Weusi Kundi la Weusi. 

Katibu Mpya wa NEC, Itikadi na Uwenezi CCM, Humphrey Polepole katika Mizani ya Wiki ndani ya Azam TV


WIZARA YA AFYA KUANZA KUDHIBITI VILAINISHI VYA MITAMBO

$
0
0
Na Amina Kibwana, Globu ya Jamii.

Waziri ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Dkt Khamis Kigwangalla  ametangaza kuwa wizara  yake kupitia Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imepewa dhamana ya kusimamia sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali za Viwandani na Majumbani ni kuhakikisha nchi inalindwa ili isiwe soko la bidhaa hafifu.

Akizungumza na waandishi wa habari Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na watoto,  Dkt Kigwangalla amesema kuwa sheria hiyo pia itasaidia kuchunguza vilainishi pamoja na Kemikali zinazoingia na kutumika nchini ziwe zenye kukidhi ubora na salama katika kulinda afya na mazingira ya Taifa letu. 

"Katika karne hii ya “Utandawazi” yenye maendeleo makubwa ya Sayansi na Teknolojia, wananchi na wawekezaji wanahitaji kuhakiki ubora na usalama wa bidhaa zao ili ziweze kukubalika katika soko la kitaifa na kimataifa".

 Amesema kuwa kutokana na kuongezeka kwa mizigo ya bidhaa za vilainishi nchini, kumekuwepo na taarifa za uwepo wa bidhaa za vilainishi visivyo na ubora katika matumizi mbalimbali.

Aidha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto ametoa agizo kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kuaendelea na uchunguzi wa kimaabara wa bidhaa za vilainishi vilivyo sokoni, kwa kushirikiana na makampuni yenye nembo halisi “trade-marks” ili kubaini na kutambua bidhaa za vilainishi halisi na visivyokidhi viwango vya ubora. 

Kwa upande wake Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele amesema kuwa wataendelea na uchunguzi wa kimaabara kwa kuchukua sampo kutoka sokoni ili waweze kuona vilainishi vilivyopo sokoni kama vinaendana na viwango, ambapo katika zoezi hilo pia watawapata watu ambao wanafanya biashara isiyokubalika ambao watapewa onyo na kuendelea kufanya biashara zao na ikiwa bado wataendelea sheria itafuata nkondo wake. 

Hata hivyo Serikali imepiga marufuku uuzaji wa vilainishi vya kupima unaofanyika mtaani na sokoni kwa sababu vifungashio vya vilainishi hivyo havikidhi ubora na pia bidhaa hizo zinaharibu ubora wa vilainishi na hivyo kuathiri utendaji wa mitambo inayotumia vilainishi.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamis Kigwangalla akizungumza  wakati akitoa tamko kuhusu ubora wa bidhaa za vilainishi nchini. Leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mohamed Ali Mohamed

UTAMADUNI WETU AFRIKA YETU AFCON YETU, NANI ASIYEPENDA NGOMA ZA KWAO

$
0
0


Na Ripota wa Globu ya Jamii.

Kati ya mambo ambayo tumekuwa tukipewa sifa waafrika bila kujali sifa nzuri au mbaya ni pale tunavyokua tunaenzi tamaduni zetu ambazo tangu wazungu wanaingia karne ya kumi na tisa bara la Afrika wakaona kama tusiostarabika na akuna taifa au bara lisilo na utamaduni na likafuata. 

Afrika tuna mambo mengi ndani ya utamaduni ambayo yanajumuisha michezo,lugha,vyakula,mavazi. Katika mashindano ya mpira wa miguu kwa Mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON yamebakiza siku zipatazo 26 ili yaanze katika ardhi ya nchi ya Gaboni. Ni tarehe 14/1/2017 yanaanza na ni kipindi ambacho waafrika tunakipenda na kufurahia sana tena sana kwasababu ya kutangaza utamaduni na vivutio mbalimbali kutoka nchi shiriki wawapo mashindanoni. 

Msimu wa kuangalia singeli za mataifa ya afrika umewadia kwani kila shabiki atakuwa na mtindo wake, sisi ni ngoma mwanzo mwisho huku wachezaji wakitusapot kucheza nao wafungapo magoli hapo ndo utakapo ona umahili wa Asamoah, Adebayor na wengine katika ngoma wachezazo. 

Afrika yetu ngoma yetu kombe letu sisi ni kusasambua tu wakati Ulaya wakilalamikia wachezaji kwenye vilabu vyao. Asili haachi asili ndiyo maana hata magoli yatakayo fungwa na wachezaji wenye asili ya Afrika yana ushangiliaji mzuri na wakunogesha kuliko wazungu . 

Unamkumbuka Bafetimbi Gomis unamkumbuka Junior Agogo unamkumbuka Muntari ile 2006 kule Ujerumani ,unazikumbuka mbwembwe za kucheza Kiplanonga kwa style ya Azonto hii ndo Afrika . Kwangu kombe la dunia naweza nikaikosa mechi halafu ikawa poa lakini sio Afcon hapa ndo unaposema Hadithi njoo mangoma njoo utamu kolea sijui Uganda watatusapraizi na ngoma zipi isije ikawa kama wenzao Rwanda 2004 kule Tunisia ila kama Tanzania ingekuwepo najua jukwaa lingeshikwa na sholomwamba na manifongo asingekaa shabiki. 

Klabu nyingi barani ulaya zimekuwa zikilalamikia ratiba yetu na kuwaomba FIFA waishinikize CAF kubadili kalenda yake kwasababu muda huo zile timu zenye wachezaji wenye asili ya Afrika na timu zao zikiwa zimefudhu mashindano hayo hutakiwa katika nchi zao na kutumikia vikosi vya nchi zao kitu ambacho huacha pengo kwenye vilabu vyao ulaya. 

Hakuna asiyefahamu nyakati walizokua wakipitia Klabu kama Manchester City, Chelsea, Arsenal kwa nyakati tofauti pale wachezaji wao muhimu wakitumikia mataifa yao.

Katika uhalisia wa uafrika ulivyo hakuna mchezaji ambaye hapendi kujumuishwa kwenye nchi yake ila wako wanaingia katika mitego ya vilabu vyao kutoa taarifa za ugonjwa huku ikiwa tofauti kwa mchezaji husika ,lilitokea kwa Michael Essieni mwaka 2008 katika mashindano yaliyoandaliwa Ghana Chelsea .

Wakitoa taarifa za ugonjwa yaani majeruhi kumbe ilikua udanganyifu kitu ambacho kilimharibia Essien kwao Ghana akaja kurejea 2010 pale Angola na hakuwa fiti kwani alikuja kuumizwa na Didier Drogba kwenye mechi ya robo fainali, mtego huo umewahi pia kuteguka kwa Sadio Mane na Kouyatte mwaka 2015 lakini ukweli toka kwa baadhi ya wakongwe waafrika kama Bernard McCarthy anasema hakuna mwafrika asiyetaka kuja kutumikia taifa lake ila ni ujanja unaofanywa na maboss. 

Tuleteeni Afcon yetu. 

TPDC YATOA SHILIONI MILIONI 10 WAKAZI WA PUGU-MAJOHE

$
0
0

Na Daudi Manongi-MAELEZO.

SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) limeipatia shilingi milioni 10 Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa mji Mpya iliyopo Pugu Majohe Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Serikali hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo leo Jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi wa Shirikahilo, Mhandisi Kapulya Musomba alisema wakazi wa Pugu-Majohe wameamua kutoa fedha hizo kutokana na wakazi wa eneo hilo kupitiwa na bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.

“TPDC hatuwezi kulinda bomba hili la Gesi kila mahali linapopita, wadau hawa wamekuwa ni sehemu ya kulinda bomba hili wanalinda pia uchumi wa nchi kwa sababu gesi hii pia inatumika kuzalisha umeme wa viwanda” Alisema Musomba.

Aidha Mhandisi Musomba ametoa wito kwa wananchi wa Pugu Majohe kuacha kuchimba mchanga karibu na bomba hilo kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wanaharibu miundombinu ya bomba hilo.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas ameishukuru TPDC kwa kuwawezesha kupata kiasi hicho kwani kitawasaidia katika ujenzi wa Ofisi hizo na pia katika maendeleo ya Pugu Majohe na kuwaomba kuendelea kusaidia katika maeneo tofauti ya Wilaya ya Ilala.

Nae Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa mji Mpya-Majohe Bw.Geofrey Chacha amesema kuwa wamejiskia faraja sana kwa kupata msaada huo kutoka TPDC kwani utaweza kusaidia kumalizia ujenzi wa Ofisi zao.


Mchango huu umetupa nguvu katika kuwahamasisha wananchi katika eneo hili kuweza kuwa walinzi wazuri wa miundombinu hii ambayo inagusa maslahi ya Taifa letu” alisema Chacha.
Kaimu Mkurugenzi Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Mhandisi Kapulya Musomba akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 10 kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Serikali ya Mtaa,katikati ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas. Wakazi wa Majohe ni wadau wa Bomba la Gesi linalotokea Mtwara hadi Dar es Salaam.

Wakazi wa Pugu Majohe wakifurahi kupatiwa hundi ya shilingi milioni 10 kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Serikali ya Mtaa . Wakazi wa Majohe ni wadau wa Bomba la Gesi linalotokea Mtwara hadi Dar es Salaam. Picha na Daudi Manongi-MAELEZO.
Diwani wa kata ya Majohe Bw.Waziri Mwanavyale akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiwa msaada wa shilingi milioni 10 toka kwa Shirika la Petroli Nchini (TPDC) kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Serikali ya Mtaa.Kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Mhandisi Kapulya Musomba na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas.
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi.Elizabeth Thomas akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiwa msaada wa shilingi milioni 10 toka kwa Shirika la Petroli Nchini(TPDC) kwa ajili ya Ulinzi mzuri wa Bomba la Gesi linalopita jirani yao.
Kaimu Mkurugenzi Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) Mhandisi Kapulya Musomba akizungumza na wananchi wa Pugu Majohe kabla ya kuwakabidhi shilingi milioni 10 kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Serikali ya Mtaa.

AZAM YAPANGWA KUNDI B NA YANGA, YAJIZATITI KUCHUKUA KOMBE

$
0
0


KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imepangwa Kundi B kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, inayotarajia kufanyika ndani ya Uwanja wa Amaan, Visiwani Zanzibar kuanzia Desemba 30 hadi Januari 13 mwakani.


Uongozi wa Azam FC umeweka wazi mikakati yao ya kutaka kuuchukua ubingwa wa msimu huu  ambapo kwa mwaka huu iliishia hatua ya makundi huku ikiwa  imepangwa pamoja na Yanga kwa mara ya pili mfululizo na timu nyingine zikiwa ni Jamhuri na Zimamoto, zote za visiwani humo.

Timu hiyo pia iliwahi kupangwa na Yanga kwenye hatua hiyo mwaka 2012 na kuifunga mabao 3-0, ushindi ulioitupa nje ya michuano Yanga, kabla ya Azam FC kutinga nusu fainali na kwenda kutwaa ubingwa mbele ya Jamhuri kwa kuwachapa 3-1.

Mabingwa hao mara mbili wa michuano hiyo (2012, 2013), wataanza kufungua dimba Januari 2 kwa kuchuana na Zimamoto saa 10.15 jioni kabla ya kuvaana na Jamhuri Januari 4 saa 2.15 usiku.

Wakazi wa visiwani humo wanatarajia kushuhudia mpambano wa aina yake Januari 7, pale mahasimu Azam FC na Yanga watakapochuana kwenye mchezo wa kufunga hatua ya makundi utakaofanyika saa 2.15 usiku.

Washindi wawili wa juu kwenye kundi hilo wanatarajia kutinga hatua ya nusu fainali na kuungana na timu nyingine mbili zilizofanya vizuri Kundi A, linaloundwa na timu za Simba, Taifa ya Jang’ombe, Jang’ombe Boys, KVZ na mabingwa watetezi wa michuano hiyo, URA, ambao waalikwa kutoka Uganda.

Michuano ya mwaka huu mwanzoni, Azam FC ilishindwa kuingia hatua ya nusu fainali baada ya kulazimishwa sare mechi mbili dhidi ya Yanga (1-1), Mtibwa Sugar (1-1) na kupoteza dhidi ya Mafunzo mabao 2-1.

BINTI WA KITANZANIA ANYAKUA TUZO YA MJASIRIAMALI BORA AFRIKA

$
0
0
Na Anthony John Globu Jamii.

Binti wa Kitanzania, Jennifer Shigholi ameibuka kuwa Mjasiriamali katika Bara la Afrika(African Enterprenuership Awards) katika Mashindano yaliyofanyika Desemba 5 Nchini Morroco.

Shigholi amewahasa Vijana  kuendelea kudhubutu na kutumia fursa mbalimbali zilizopo nchini ilikuweza kujikomboa kichumia na badala yake kuacha kulalamika na kuchukua hatua za uthubutu kwa kuwa kila kitu kinawezekana kama mtu akimua.

Pia amesema kuwa Serikali imempatia eneo la kujenga Kiwanda kikubwa zaidi ilikuweza kutoa ajira kwa vijana hapa Nchini.

Hivyo hivyo Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania TPSF Salum Shamte, amesema Mjasiliamali huyo ameleta heshima kubwa  katika nchini yetu na sisi kama Sekta binafsi tutafanya naye kazi bega kwa bega ilikumsaidia  kuweza kuendeleza biashara zake.

" Jennifer ni Mfano wa kuigwa na Vijana wengine kwa Ujasiliamali wake Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania inampongeza kwa Ushindi wake kwenye tuzo za Ujasiliamali barani Afrika na kuiletea nchi yetu heshima kubwa haswa wanawake" amesema 

Mshindi wa  tuzo ya African entrepreneurship, Jennifer Shigholi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, kulia ni makamu Mwenyekiti wa bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania Salum Shamte. 
Makamu Mwenyekiti wa TPSF,Salum Shamte akitoa shukrani kwa  Mshindi wa Jennifer Shigholi.
Makamu Mwenyekiti wa TPSF,Salum Shamte akimkabidhi Mshindi wa Tuzo ya Mjasiliamali Bora Afrika, Jennifer Shigholi cheti cha kumtambua katika Taasisi hiyo ya TPSF kama Mjasiriamali Mahiri
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live




Latest Images