Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109973 articles
Browse latest View live

VODACOM TANZANIA APPOINTS NEW DIRECTOR OF CONSUMER BUSINESS UNIT

$
0
0
Vodacom Tanzania’s Managing Director, Ian Ferrao is pleased to announce the appointment of Hisham Hendi as the new Director of Consumer Business Unit with effect from November 2016.

 Hisham will be leading both Marketing and Sales functions allowing Vodacom to build on its customer centric approach in the market. 

 “We brought Hisham on board due to his expertise and experience. Having worked in various other Vodacom operations in Africa and beyond, he understands the ins and outs of our commercial operations. With his leadership in the commercial area,  our customers can expect more valuable products and services that will address all their communications needs” said Ferrao.    

 Hisham has previously worked with Vodacom Tanzania supporting Vodacom’s International Business as the Managing Executive – Commercial.

Prior to this, Hisham spent 11 years working in various roles across Vodafone’s Consumer Business in Egypt including digital services in Consumer Marketing and Prepaid Sales – Consumer Marketing in 2003 and 2005 respectively. Hisham went on to work in Consumer Proposition in Partner Networks in London, UK in 2007 before moving back to Egypt in 2009 to manage Prepaid Segments and later became Head of Consumer Marketing.

Hisham holds a Bachelor Degree of Commerce from the University of Cairo, Egypt (2001).

RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA MAHAFALI YA 31 YA CHUO KIKUU HURIA KIBAHA LEO.

$
0
0

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania, Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda wakati wakielekea kwenye Viwanja vya Chuo hicho, Bungo Kibaha Mkoani Pwani, katika Mahafali ya 31 ya Chuo hicho. 
 
Sehemu ya Wahitimu wa Kozi mbalimbali wa Chuo Kikuu Huria wakiwa katika Mahafali hayo.

Ukosefu wa Ajira ni Matokeo sio Janga barani Afrika-Profesa Ole Gabriel

$
0
0

Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii

Katibu mkuu wa Wizara ya habari  Sanaa na michezo Profesa Elisante Ole Gabriel amesema kuwa tatizo la ukosefu  wa ajira Afrika ni matokeo na sio tatizo kama watu wanavyosema ama dhania.

Profesa Gabriel amesema hayo katika Mdahalo wa wanazuoni  kutoka Afrika Mashariki uliofanyika katika ukumbi wa mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.

"Tatizo kubwa la Afrika ni soko na kubadilisha fikra za vijana katika bara letu kwa  kupata ellimu juu ya namna   Watakavyoweza kujikwamua kiuchumi  hali itakayosadia kuondokana na umaskini uliokithiri hivyo ifike hatua watu wasiwe wanahitaji kupewa pesa pindi inapohitaji kupewa elimu "amesema Profesa Gabriel

Amewataka wakufunzi wa vyuo kurudi vyuoni na kubadilisha mawazo ya vijana kurudi katika mtazamo chanya wa kujipatia maendeleo kuliko kusubiri kusukumwa na watu juu ya kupata ajira.
 Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza katika Mjadala huo
washiriki wakimsikiliza Profesa Ole Gabriel

Muungano wa wapiga kura Tanzania waandaa matembezi ya hiyari ya upandaji mti kwa lengo la kuunga mkono serikali awamu ya tano

$
0
0

Na Amina Kibwana,Glabu ya Jamii

  Muungano wa wapiga kura Tanzania (TANVU) umeandaa matembezi ya Hiayari ya upandaji mti kwa lengo la kuunga mkono  Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya Awamu ya tano.

  Matembezi hayo yanatarajiwa kuanza rasmi Novemba 26 hadi 30,2016, ambayo yataanzia Mkoani Singida wilaya ya Ikungi hadi Mkoa wa Dodoma ambapo zaidi ya wazalendo 600 wnatarajiwa kuhudhuria katika matembezi hayo.

  Akizungumza na waandishi wa habari Mratibu Msaidizi na Katibu mwenezi,Habari na Mawasiliano Barrynice Mayunga amesema kuwa katika matembezi hayo kutakuwa na upandaji wa miti ipatayo 12,500 (Elfu kumi na mbili na miatano)  kwa ajili ya utunzaji wa mazingira na misingi endelevu kwa viwanda.

  Amesema Mayunga, kwa kufanya hivyo pia itasaidia kujenga na kudumisha uzalendo ndani ya mioyo ya watanzania pamoja na kufanya kazi kwa kutumia kauli mbiu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli wa Hapa kazi tu.

  "Sisi kama wazalendo tumeamua kujitoa kwa kufanya mate mbezi ya hiyari ili tuweze kukamilisha shughuli za upandaji miti kwa kuisaidia serikali ya awamu ya tano katika kuzisimamia rasilimali za nchi yetu."

  Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mipango na Uwezeshaji John Meena amesema kuwa miti ni pamoja na mikakati ya utunzaji wa mazingira kwani bila kuwa na miti kunaweza kusababisha madhara mbalimbali katika nchi ikiwemo, kuharibika kwa mifugo, kusababisha ukame nchini, Kupotea kwa mazao ya asili kama mbao,asali na matunda pamoja na kushuka kwa uzalishaji wa mazao na kuharibika kwa miundombinu ya hali ya hewa.
 
  Hata hivyo Muungano wa wapiga kura Tanzania (TANVU) umetoa wito kwa wanachi wote kujiandikisha na kuungana nao katika matembezi haya ili waweze kufikia lengo kwa pamoja kama wazalendo, Pia wameipomgeza serikali  yaawamu ya tano kwa jitihada inayoionesha katika kusimamia masuala mazima ya uwajibikaji kwa wanachi wake.
  Mratibu Msaidizi na Katibu mwenezi,Habari na Mawasiliano wa Muungano wa wapiga kura Tanzania Berrynice Mayunga akizungumza na waandishi wa habari, kulia ni Mshauri wa Muungano wa wapiga Kura Tanzania Mchungaji Donald Mathew.

MAADHIMISHO KITAIFA YA SIKU YA UTALII DUNIANI NA MAONESHO YA ‘’KARIBU KUSINI’’ KUFANYIKA MKOANI IRINGA

$
0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

TAARIFA KWA UMMA

MAADHIMISHO KITAIFA YA SIKU YA UTALII DUNIANI NA MAONESHO YA ‘’KARIBU KUSINI’’ 2016


Wizara ya Maliasili na Utalii  kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa  Mkoa wa Iringa, Mradi wa kuboresha Mtandao wa Hifadhi za Kusini mwa Tanzania (SPANEST)  pamoja na Wadau wa Sekta ya Utalii nchini watashiriki  katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani   kwa mwaka 2016 sambamba na Sherehe za maadhimisho ya ‘’Karibu Kusini ‘’ Karibu Tanzania Southern Circuit’’  ambayo  Kitaifa yataadhimishwa   Mkoani Iringa kwenye viwanja vya  Kichangani  kuanzia tarehe 25 hadi 29 Novemba, 2016.
Lengo la maadhimisho hayo ni  kuweka uelewa kwa Jamii kuhusu umuhimu wa utalii na thamani yake ikiwa pamoja na  kuutangaza Utalii kwa kuihamasisha jamii kutumia fursa za utalii zilizopo katika kuinua uchumi wa wakazi wa Ukanda wa Kusini mwa Tanzania na Taifa kwa ujumla
Kauli Mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani kwa mwaka  2016  ni “Utalii kwa wote – wote wawezeshe’’ (Tourism for All – Promoting Universal Accessilibity). Kwa kuzingatia Kauli Mbiu hii, Serikali inatambua kuwa kuna watu wenye mahitaji maalumu kama vile walemavu, wazee na watoto ikisisitiza miundombinu rafiki, gharama nafuu kutembelea  vivutio vya utalii na gharama nafuu za usafiri ili kuhakikisha kwamba, utalii unawahusisha watu wengi zaidi kunufaika nao.
Katika Maadhimisho hayo, Wizara itakuwa na washiriki ambao ni Idara pamoja na Taasisi zake mbalimbali. Idara zitakazoshiriki ni Utalii, Wanyamapori, Mambo ya Kale na Misitu na Nyuki.
Kwa upande wa Taasisi zitakazoshiriki  ni Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Chuo cha Taifa cha Utalii, Makumbusho ya Taifa, Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Mamlaka ya Usimamizi ya Wanyamapori (TAWA) Mfuko wa Misitu Tanzania  (TaFF) Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, (TFS)  Taasisi ya Utafiti wa Misitu na Wadau wa Wizara ya Maliasili na Utalii.
Wadau wa Sekta ya Utalii kutoka mikoa  ya Nyanda za Juu Kusini watashiriki kuonesha bidhaa na huduma zao muhimu. Mikoa hiyo ni pamoja na Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya na Songwe
Aidha, Wizara itatoa punguzo kwa watanzania kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Ruaha pamoja na vivutio vya utalii vilivyokaribu na mji wa Iringa ambavyo ni Ismila,Kalenga na Boma la Mkuu wa Wilaya  kwa gharama nafuu.
Kupitia Maadhimisho hayo wito unatolewa kwa kuwaalika wadau wote wa utalii na jamii husika kwa pamoja na kuadhimisha siku hii kama ishara ya jitihada za pamoja za kuufanya utalii nguzo ya kweli ya maendeleo ya jamii na maendeleo ya jamii ni chanzo cha sekta ya utalii endelevu zaidi.
 Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na  Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Maliasili na Utalii.




TPDC yalipiga jeki Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPDC, Prof. Sufian Bukurra (wa pili kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni tano kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, George Salala (wa kwanza kushoto) kwajili ya ukarabati wa Kituo cha Polisi Uwanja wa ndege Mtwara, wengine ni Kaimu Mkurugenzi wa TPDC Mhandisi, Kapuulya Musomba (kwa kwanza kulia), Mkuu wa Mkuu wa Kituo cha Polisi Uwanja wa ndege Mtwara, Inspekta, Moses Moremi (wa pili kushoto) na Kaimu Meneja wa Uwanja wa ndege Mtwara, Vita Majinge (katikati).
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Dkt. Khatibu Kazungu akitoa neno la shukurani mara baada ya kupokea mchango wa shilingi milioni tano za ukarabati wa Kituo cha Uwanja wa Ndege Mtwara kutoka TPDC.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Geroge Salala akizungumza katika wakati wa zoezi la kupokea mchango wa shilingi milioni tano za ukarabati wa Kituo cha Uwanja wa Ndege Mtwara kutoka TPDC.

MGODI MAARUFU WA DHAHABU GEITA GGM WATOZWA FAINI YA SH. MILIONI 10 KWA KUKOSA CHOO CHA WAFANYAKAZI.

$
0
0

Na Evelyn Mkokoi, Geita

Mgodi maarufu wa kuchimba dhahabu mjini Geita wa GGM umekumbana na adhabu ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC katika Ziara ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina Mkoani Geita kwa kosa la kukosa vyoo vya wafanyakazi zaidi ya mia tatu (300) katika eneo la chini ya ardhi underground la uchimbaji wa madini ya dhahabu.

Hali hiyo imeipelekea NEMC kuutoza mgodi huo faini ya shilingi milioni 10, zinazotakiwa kulipwa ndani ya siku kumi na nne.

Katika ziara hiyo iliyomlazimu Naibu Waziri Mpina kuvaa vifaa maluum ili kuweza kuingia katika eneo la chini ya ardhi lenye mwamba mkubwa wa mgodi huo, akiambatana na baadhi ya maafisa aliongozana nao katika ziara yake, Naibu Waziri alijionea namna ambavyo eneo lenye idadi kuwa ya wafanyakazi kukosa huduma hiyo muhimu ya choo inayowapelekea kujisaidi vichakani na kuharibu mazingira.

Aidha Naibu Waziri Mpina Pia aliweza kujionea uharibifu mwingine unaofanywa na mgodi huo wa utiririshwaji wa Maji ya mvua yaliyochanganyikana na madawa hatarishi kwa mazingira na viumbe hai kwenda kwenye makazi ya wananchi.Kufuatia hali hiyo, Naibu waziri Mpina alielekeza uongozi wa mgodi huo kujenga miundombinu rafiki kwa mazingira yatakayopelekea maji hayo kwenda katika mkondo sahihi..

Akiongea kwa Niaba ya GGM makamu wa Rais wa Mgodi huo Bw. Simon Mushy, alisema kuwa wapo kwenye mchakato wa kujenga miundombinu kwa kushiriana na Halmashauri ya Mji wa Geita.Kwa upande wa mmoja wa wakazi wa kijiji cha Katoma Bi. Magori James Katoka alisema kuwa vumbi na maji ya mvua vinavyotoka kwenye mgodi huo vimekuwa ni kero na changamoto ya muda mrefu katikma kijiji hicho.

Pamoja na malalamiko mengi ya wakazi wa Katoma Geita kuhusu uharibifu wa mazingira unaofanywa na mgodi wa GGM, Mgodi huo pia umefanya shughuli mbali mbali za kijamii ikiwa ni pamoja na kusambaza maji safi a salama katika mji wa Geita ukishirikiana na mamlaka ya maji safi na maji taka ya Mkoa huo.

Ziara ya Naibu Waziri Mpina Katika Mkoa wa Geita ni muendelezo wa ziara yake ya ukaguzi wa mazingira katika viwanda na migodi nchini.
Mkurugeni mtendaji wa GGM wa pili kulia Bw. Terry Mulpeter akimuonyesha Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina katikati, bwawa linalotumika kusambaza maji safi katika mji wa Geita.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Mungano na Mazingiraa Mhe. Luhaga Mpina akijiandaa kwenda sdehemu ya chini ya ardhi ya mgodi wa GGM 
Sehemu ya chini ya ardhi (underground) yenye dhahabu ya mgodi wa GGM inayosemekaka kukosa huduma ya choo kwa watumishi wanaokadiriwa kuwa zaidi ya mia tatu, ikionekana kwa nje katika katika picha.
Bw. Simon Mushy Makamu wa Rais wa Mgodi wa GGM akijibu maswali ya Naibu Waziri Ofisi ya Maku wa Rais Mungano na Mazingira mhe Luhaga Mpina hayupo pichani kuhusu suala la mgodi kutiririsha maji ya mvua yaliyochanganyikana na sumu kutoka mgoni kwenda katika mazingira na maeneo ya vijiji jirani na Katoma
Sehemu ya kutupia na kutetekeza taka ngumu katika mgodi wa GGM Geita.
Mabwawa Ya majitaka la Mgodi wa dhabu wa Geita wa Geita Gold Mining maarufu kama GGM, ambapo imeelekezwa kuweka mtambo wa kusafisha Majitaka hayo kuingia katika mabwawa.

MKURUGENZI WA ILEJE AWADHIBITI WAKWEPA KODI

$
0
0
 Na Daniel Mwambene, Songwe                           

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje wampongeza Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Haji Mnasi kwa kukuza uchumi wa wilaya hiyo na kufanikiwa kuwadhibiti wafanyabiashara waliokuwa wakikwepa kodi.
Pongezi hizo zilitolewa na madiwani hivi karibuni wakati wa kikao cha Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.
Akizungumza na blog hii diwani wa kata ya Itumba Mohamed Mwala alisema kuwa wanatambua juhudi zilizofanywa na Mkurugenzi Haj Mnasi na wafanyakazi wa halmashauri kukusanya ushuru maeneo mbalimbali na kufanikiwa kuyakamata magari aina ya maroli yaliyokuwa yakikwepa ushuru.
Naye diwani wa kata ya Ibaba Tata Kibona alisema kuwa mkurugenzi na timu yake  wamekuwa wakitembea usiku kuwatafuta wakwepa kodi hasa kwenye kata yake ambapo mara kadhaa mkurugenzi huyo amekuwa akionekana nyakati za usiku.
"mimi sijawahi ona mkurugenzi kama huyu maana anaacha usingizi wake unamkuta kwenye kata nyakati za usiku akipambana nao wakwepa kodi na amefanikiwa kuwadhibiti wafanyabiashara wote wakwepa kodi na ndio maana sasa mapato yameanza kukua kwa kasi katika wilaya yetu"alisema Kibona 
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya ileje Haji Mnasi akiwa kwenye eneo husika la kukagua wakwepa kodi.
 
Hawa ni baadhi ya madiwani wa halmashauri ya wialaya ya Ileje wakifutalia jambo lililokuwa likiongelewa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya ileje haji mnasi
Hili ni moja ya malori yaliyokuwa yakikwepa ushuru kwa kufanya biashara ya kushusha mizigo vichochoroni.
Hili ni moja kati ya gari linalobeba milunda bila kulipia ushuru na mkurugenzi Haji Mnasi kufanikiwa kulikamata wakati wa zoezi maalumu la kuwatafuta wakwepa kodi waliobobea kuikimbia serikali kulipa kodi.




WAZIRI NAPE AKATAA MAMLUKI SHIMMUTA

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye amekemea vikali baadhi ya tabia ya viongozi wa timu zinazoshiriki michezo mbalimbali kutumia wachezaji wasiostahili kutumika katika mashindano husika.

Ameyasema hayo wakati akizindua mashindano ya michezo mbalimbali yanayoandaliwa na Shirikisho la Michezo ya mashirika ya Umma na Binafsi (SHIMMUTA) yanayoendelea Jijini Tanga ambayo yameshirikisha timu mbalimbali kutoka mashirika ya Umma na Binafsi Tanzania.

Mhe. Nnauye amewataka viongozi wa SHIMMUTA kufanya uhakiki upya wa wachezaji wa timu shiriki ili kuondoa lawama zinazoweza kutokea na kupata mshindi anayestahili kwa kufata Sheria na taratibu zote za mashindano.“Nawaomba viongozi muangalie na kupitia upya wachezaji wa timu shiriki ili kusiwe na zengwe lolote katika mashindano haya na mshindi katika kila mchezo apatikane kihalali” alisisitiza Mhe. Nnauye.

Aidha ametoa wito kwa mashirika kutenga muda na fedha ili kuwezesha timu zao kushiriki katika michezo ikiwa ni moja ya kujenga mshikamano na amani kwa watanzania na pia kujenga afya ya mwili na akili.Mashindano ya SHIMMUTA yameshirikisha mashirika ya Umma na Binafsi katika michezo 12 ikiwemo Mpira wa Miguu(Football), Mpira wa Pete(Netball),kuvuta kamba, Riadha, Mchezo wa vishale(Darts),Mchezo wa Pooltable, mchezo wa bao, Karata,kukimbia na magunia.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akikagua timu mbalimbali kabla ya kuanza kwa michezo mbalimbali wakati wa uzinduzi wa mashindano ya SHIMMUTA yanayofanyika Jijini Tanga.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akikagua timu mbalimbali kabla ya kuanza kwa michezo mbalimbali wakati wa uzinduzi wa mashindano ya SHIMMUTA yanayofanyika Jijini Tanga.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akipiga mpira kuashiria uzinduzi rasmi wa mashindano ya SHIMMUTA yanayofanyika Jijini Tanga.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akionesha ufundi wa kupiga danadana wakati wa uzinduzi rasmi wa wa mashindano ya SHIMMUTA yanayofanyika Jijini Tanga, akimshuhudia akipiga danadana hizo ni Mbunge wa Tanga Mjini Mhe.Musa Mbaruk.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WHUSM.

Ujumbe kutoka UNESCO kuhusu siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake,Novemba 25, 2016.

$
0
0
-Usalama wa Wanawake kufuatia Mabadiliko ya Tabia Nchi

Ukatili dhidi ya wanawake ni uvunjaji mkubwa wa haki za msingi za binadamu na tishio kwa mamilioni ya wasichana na wanawake duniani kote. 

Takribani mwanamke mmoja kati ya wanawake watatu duniani amekuwa akipigwa, kulazimishwa kufanya ngono, au kunyanyaswa vinginevyo katika maisha yake. 
 
Jamii nzima imeathiriwa na ukatili ambao unaweza kuwa wa kimwili, kingono (unyanyasaji, kulazimishwa au kubaguliwa) na kisaikolojia (kunyanyaswa kwa maneno au kwa hisia, kama vile kuonewa au kutengwa).

Katika siku hii ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake, UNESCO inaangazia mabadiliko ya tabia nchi na uhaba wa rasilimali kama sababu za kuchochea ukatili dhidi ya wanawake – nyumbani, mitaani, wakati wa majanga asilia yanayosababishwa na tabia nchi.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

BALOZI DK ASHA ROSE MIGIRO ALIPOHUTUBIA KIKAO CHA JUMUIYA YA WAINGEREZA NA WATANZANIA – BTS

$
0
0
Picha na Habari za Freddy Macha, London 
Balozi wetu Uingereza, mheshimiwa Dk Asha Rose Migiro alihutubia  jumuiya ya Watanzania na Waingereza (British Tanzania Society- BTS)  Jumamosi iliyopita. 
Hotuba hiyo iliyofanyika ukumbi wa Central Hall Westminster, London ni mara ya pili kwa balozi huyu mgeni kukutana na BTS. Mwezi Julai alikaribishwa rasmi akiwa na Balozi mpya Uingereza Tanzania Bi Sarah Cooke na aliyestaafu, Bi Diana Melrose. 

Mada hiyo iliyoitwa “Maendeleo ya Sasa Tanzania”  Ilikuwa sehemu ya mkutano wa 41 wa mwaka wa BTS na kuhudhuriwa na Watanzania na Waingereza wakazi hapa.

Wajumbe wa BTS wanaipenda Tanzania na kusimamia miradi tele kwa kujitolea bila hata senti moja. Mwaka 2015-2016 BTS imeendeleza mipango 46 ya maendeleo haya.

Mama Balozi alizungumza kifupi akisisitiza masuala muhimu ya maendeleo ya elimu, uongozi  mpya wa Rais John Magufuli unaosisitiza “Hapa Kazi Tu” katika kipindi cha mwaka mzima. Baada ya hapo alitumia muda mwingi kujibu maswali ya wajumbe. Aidha masuala yalijibiwa  au kupewa ahadi ya kufuatiliwa kivitendo. 

Wajumbe wa BTS wanaipenda Tanzania na kusimamia miradi tele kwa kujitolea bila hata senti moja. Mwaka 2015-2016 BTS imeendeleza mipango 46 ya maendeleo haya. Mama Balozi alizungumza kifupi akisisitiza masuala muhimu ya maendeleo ya elimu, uongozi mpya wa Rais John Magufuli unaosisitiza “Hapa Kazi Tu” katika kipindi cha mwaka mzima. Baada ya hapo alitumia muda mwingi kujibu maswali ya wajumbe. Aidha masuala yalijibiwa au kupewa ahadi ya kufuatiliwa kivitendo.

1-balozi-migiro-akihutubia-jumuiya-ya-watanzania-na-waingereza-pic-by-f-machaBalozi wetu Uingereza, mheshimiwa Dk Asha Rose Migiro alihutubia jumuiya ya Watanzania na Waingereza (British Tanzania Society- BTS) Jumamosi iliyopita. Hotuba hiyo iliyofanyika ukumbi wa Central Hall Westminster, London ni mara ya pili kwa balozi huyu mgeni kukutana na BTS. Mwezi Julai alikaribishwa rasmi akiwa na Balozi mpya Uingereza Tanzania Bi Sarah Cooke na aliyestaafu, Bi Diana Melrose.8-bango-la-bts-pic-by-f-macha-2016Mada hiyo iliyoitwa “Maendeleo ya Sasa Tanzania” Ilikuwa sehemu ya mkutano wa 41 wa mwaka wa BTS na kuhudhuriwa na Watanzania na Waingereza wakazi hapa.
2-petronilla-mwakaluma-akiuliza-swali-pic-by-f-macha-2016Mtanzania na mwanachama wa BTS, 
Bi. Petronilla Mwakaluma akiuliza swali3-balozi-migiro-akijadiliana-na-wataalamu-hapa-dk-gideon-mlawa-pic-by-f-machaBalozi Migiro akijadiliana na baadhi ya wataalamu Watanzania waliokuja kumsikiliza. Aliye naye “maso kwa maso” ni mganga shupavu wa kisukari Dk. Gideon Mlawa. Kulia kwake ni mwanafunzi chuo kikuu Wales, Fadhili Maghiya. Kwa habari zaidi BOFYA HAPA

TAMASHA LA MUZIKI LA SAUTI ZA BUSARA ZANZIBAR 2017

RAIS DKT MAGUFULI MGENI RASMI MAHAFALI YA 31 YA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA (OUT)

$
0
0
  Serikali itaendelea kusimamia ubora wa elimu kwa kuhakikisha shule na taasisi zinadahili wanafunzi wenye sifa stahiki za kujiunga na kozi wanazoomba.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 24 Novemba, 2016 katika sherehe za mahafali ya 31 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania zilizofanyika Bungo, Kibaha Mkoani Pwani.

Kabla ya Rais Magufuli kutoa kauli hiyo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Prof. Elifas Tozo Bisanda alieleza kuwa chuo hicho kimeshindwa kudahili idadi kubwa ya wanafunzi baada ya Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) kuzuia udahili wa wanafunzi wanaotaka kujiunga na masomo ya elimu ya juu kwa kutumia sifa ya kupatiwa kozi ya awali (Foundation Course) ambayo imekuwa ikitumiwa na wanafunzi wasio na sifa za kujiunga vyuo vikuu kwa vigezo vya TCU.

"Kwa vile mnachukuliwa sawa na vyuo vingine ni lazima mzingatie vigezo vya mtu kuitwa mhitimu wa Chuo Kikuu, kwa hiyo nasema kwa dhati nakubaliana sana tena kwa asilimia 100 na yale yaliyozungumzwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Ufundi Prof. Joyce Ndalichako.

"Kwa hiyo ni lazima hili suala la kuweka viwango vya ubora wa elimu yetu tulizingatie, ni mara kumi tuwe na wanafunzi hata 10 wanaohitimu elimu ya juu kuliko kuwa na wanafunzi 20,000 wakati hawana sifa, kwa sababu tutakapokwenda kwenye ajira hatutauliza kama huyu ametoka Chuo Kikuu Huria, huyu ametoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ama huyu ametoka Chuo Kikuu cha Dodoma, wote tutawaangalia kwa usawa.

"Tusitafute njia ya mkato, njia ya mkato ni mbaya, kwa hiyo kwa hili kwa kweli Mhe. Prof. Ndalichako nakubaliana na wewe, nafikiri ndio maana umekuwa Waziri wa Elimu, tunataka kulinda hadhi ya elimu yetu"amesema Dkt. Magufuli.

Hata hivyo, Rais Magufuli amekipongeza Chuo Kikuu Huria kwa kazi nzuri ya kutoa elimu ya juu kwa Watanzania wengi na kuanzisha matawi katika nchi mbalimbali za Afrika na ameahidi kuwa Serikali yake itaendelea kuunga mkono juhudi hizo ikiwa ni pamoja na kukabiliana na changamoto za miundombinu na mahitaji mengine.

Aidha, Rais Magufuli amewaonya viongozi na watendaji wa taasisi mbalimbali za Serikali ambao wamekuwa wakitumia vibaya fedha za umma ikiwemo kuweka fedha nyingi za Serikali katika akaunti za muda maalum (Fixed Deposit Account) kwenye benki za biashara ambako hujipatia fedha kupitia faida ya akiba bila kujali kuwa vitendo hivyo husababisha Serikali kukosa fedha na kulazimika kukopa kutoka benki za biashara ambako hutozwa riba kubwa.

"Sasa sifahamu kama Chuo Kikuu Huria na nyinyi mmekuwa mkiweka fedha za maendeleo katika Fixed Deposit Account, lakini huo ndio umekuwa ni mchezo, juzi hapa tumekuta fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 26 zilizokuwa zimetolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa ajili ya matumizi ya TRA, zikapelekwa kwenye benki tatu kama Fixed Deposit Account na Bodi ya TRA ikapitisha, ndio maana nilipozipata hizo taarifa, fedha nikachukua na Bodi kwa heri.

"Hata kwa sasa hivi Waziri upo hapa, Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ambayo ilianzishwa kwa sababu maalum, inachangiwa fedha wakati kuna fedha zao wameziweka kwenye Fixed Deposit Account, Waziri hiyo ni message sent and Delivered"amesisitiza Rais Magufuli.

Katika Mahafali hayo, Mkuu wa Chuo Kikuu Huria na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda amewatunuku shahada na vyeti jumla ya wahitimu 4038, wakiwemo wahitimu 8 wa shahada ya Uzamivu, 217 wa shahada ya Uzamili, 111 wa Stashahada ya Uzamili, 1,186 wa Shahada ya Kwanza, 484 wa Stashahada na 1,421 wa vyeti mbalimbali.
  
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

24 Novemba, 2016.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya wahitimu wa  Shahada ya Uzamivu ya Udaktari wa Falsafa  wakati wa mahafali ya 31 ya  Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye kampasi ya chuo hicho huko huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na  baadhi ya wahadhiri wakati wa mahafali ya 31 ya  Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye kampasi ya chuo hicho huko huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipiga makofi wakati Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akimtunuku Shahada ya Uzamivu ya Udaktari wa Falsafa mhitimu Hebson Opiyo Andala kutoka Rwanda wakati wa mahafali ya 31 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye kampasi ya OUT huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa mahafali ya 31 ya  Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye kampasi ya chuo hicho huko huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
 Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa, Joyce  Ndalichako  akihutubia wakati wa mahafali ya 31 ya  Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye kampasi ya chuo hicho huko huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016.
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akimtunuku Shahada ya Uzamivu ya Udaktari wa Falsafa mhitimu Philip Filikunjombe wakati wa mahafali ya 31 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye kampasi ya OUT huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBER 25, 2016

VIJANA KUONESHA VIPAJI VYAO HADHARANI MASHINDANO YA ULEGA CUP MKURANGA

$
0
0
VIJANA wa Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani wamesema kuwa kitendo cha Mbunge wa Jimbo hilo Abdallah Ulega kupiga marufuku kukodi wachezaji Kutoka Nje ya Wilaya hiyo imeleta changamoto kwao kuonesha vipaji vyao Kwenye ligi ya mbunge inayoendelea.

Wamesema kuwa wao kama vijana ndio wakati muafaka kwao kuonesha vipaji vyao na uwezo ili mwisho wa siku wapate nafasi ya kushiriki Kwenye ligi mbalimbali.Mbunge Ulega ameazisha Ligi ya mbunge ambapo hivi sasa timu Kutoka kila kijiji zinapambana na baadae zitatoa timu moja ya Kata ambayo itakwenda kushindana na Kata zingine zilizopo ndani ya Wilaya ya Mkuranga.

Akizungumzia ligi hiyo jana wilayani humo Kijana khatibu Dadi alisema kuwa mbunge Ulega amedhamiria kuinua vipaji vya vijana wa Mkuranga na hiyo nikutokana na wito wake wakutaka ligi hiyo ishirikishe vijana wa maeneo husika tofauti na wanavyofanya kungineko.

"Kwa kifupi kila mtu anampongeza Mh.Mbunge Kwa uamuzi wake kwani lazima ifike wakati sisi kama vijana wa Mkuranga tuoneshe wenyewe uwezo na vipaji vyetu na tunaamini kupitia ligi hii ya Mbunge tutapata timu kabambe ya Wilaya."alisema Dadi
 Katibu wa mbunge wa Mkuranga Bw Omar Kisatu akipeana mikono na baadhi ya wachezaji wa timu shiriki mashindano ya Ulega Cup yanayoendelea kutimua vumbi Wilayani Mkuranga.

 Diwani wa Kata ya Panzua Bw Juma Magaila akiongea na waandishi wa habari kuhusu ligi ya Ulega Cup  inayoendelea  Wilayani Mkuranga.
Katibu wa mbunge wa mkuranga Bw Omar Kisatu Akiongea na waandishi wa habari kuhusu mashindano hayo ya Ulega Cup yanayoendelea kutimua vumbi Wilayani Mkuranga.
 Diwani wa Kata ya Mkamba Wilayani Mkuranga Bw Hassan Dunda Akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na Mtiririko mzima wa ligi ya Ulega Cup unaondelea huko Wilayani Mkuranga.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


CoST TO BECOME AN INDEPENDENT INSTITUTION

$
0
0
Jacquiline Mrisho – MAELEZO

The Construction Sector Transparency Initiative (CoST-Tanzania) has begun to review its institutional structure in order to give it the legal mandate on implementing its activities.

The statement for implementation was released today in a meeting involving various stakeholders in the construction industry held in the the Blue pearl auditorium  in Dar es Salaam and opened by Guest  of Honor, the Permanent Secretary Ministry of Works, Transport and Communications (Works), Eng. Joseph Nyamuhanga.
 
The Permanent Secretary Ministry of Works, Transport and Communications (Works), Eng. Joseph Nyamuhanga opening one-day stakeholders meeting of the construction industry organised by The Construction Sector Transparency Initiative (CoST-Tanzania) held today in Dar es Salaam.

Eng. Nyamuhanga said that, the meeting took place in order to coordinate various stakeholders to discuss and give out constructive opinions that will focus on how CoST – Tanzania will shift from dependent institution to independent.

“Construction sector is perceived to be one of the most corrupt sectors in the world because mostly of 10 – 30% of its budget being wasted through corruption and mismanagement so, if we want to control those problems we must have legal mandate,” Eng. Nyamuhanga said. 
The Chairman of Construction Sector Transparency Initiative (Cost- Tanzania), Eng. Kazungu Magili speaking to stakeholders in the construction industry (not pictured) on how CoST-Tanzania will shift from dependent to independent institution held today in Dar es Salaam.

Eng. Nyamuhanga added that, the Construction Sector Transparency Initiative aims at becoming the leading promoter of transparency and accountability in the construction sector so this will be initiated by having legal mandate.

Meanwhile, CoST’s Chairman Eng. Kazungu Magili explained that it is estimated that by 2030 Global adoption of CoST will have the potential to save about US 5 trillion annually through savings and reduced corruption also it will build confidence among supporters especially in private sectors and donors who finance those programs. 
Manager of the Construction Sector Transparency Initiative (Cost- Tanzania), Clement Mworia giving definition to the stakeholders of the construction industry on the procedure for comment on the stakeholders meeting held today in Dar es Salaam.

“The objective of this Global Multi-Stakeholder Initiative whose aim of promoting data disclosure on infrastructure projects is to achieve better value for money and better quality infrastructure thus increasing the quality of life for all citizens,” Eng. Magili said.

He added that CoST helps the process by building the capacity of procuring entities to comply with legal disclosure requirements and building the capacity of oversight institutions and Non – State actors to undertake scrutiny of disclosed data, raise issues and engage with the Government to deal with the issues.

The Government has supported the Initiative since its inception in 2007 first by hosting the Initiative under the National Construction Council (NCC) and championing it through the Ministry responsible for Good Governance.
The Permanent Secretary, Ministry of Works, Transport and Communications (Works), Eng. Joseph Nyamuhanga in a group picture with the stakeholders of the construction industry who attended a one- day conference organized by The Construction Sector Transparency Initiative (Cost-Tanzania) held today in Dar es Salaam.

RC MAKONDA AANZA ZIARA WILAYA MPYA YA UBUNGO LEO.

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Manispaa Ubungo leo jijini Dar es Salaam kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Humphrey Polepole. Mhe Makonda yupo katika ziara ya siku 10 jijini Dar es Salaam kwaajili ya kusikiliza kero za wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Humphrey akimkaribisha Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kuzungumza na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Manispaa Ubungo leo jijini Dar es Salaam

Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Manispaa Ubungo wakimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA KATIBU MKUU WA CCM ,NDUGU KINANA JIJINI DAR LEO

$
0
0



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikarishwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipofika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam, kwa ajili ya mazungumzo na Katibu mkuu huyo wa CCM, leo.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwenda eneo la kufanyia mazungumzo, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam, kwa ajili ya mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungmza na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, leo katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO- theNkoromo Blog

SERIKALI YASHAURIWA KUANDAA SERA BORA KUKUZA UJASIRIAMALI NA UBUNIFU

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Uwekezaji, Profesa Adolf Mkenda (kulia) akifungua majadiliano yaliyohusu kuongeza kasi ya ubunifu na ukuaji wa wajasiriamali kupitia sera wezeshi zenye kutekelezeka, (wa pili kulia) Meneja Mradi wa BEST-DIALOGUE, Bw.Hans Determeyer , (katikati) ni Mkurugenzi wa Program ya Kimataifa ya SEPT, Profesa Utz Donberger, (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF),Bw. Godfrey Simbeye na (kushoto) ni Mkuu wa Kitivo cha Biashara Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDBS),Dk. Ulingeta Mbamba.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF),Bw. Godfrey Simbeye (kulia) akitoa taarifa juu ya maendeleo ya sekta binafsi nchini, wakati wa majadiliano yaliyohusu kuongeza kasi ya ubunifu na ukuaji wa wajasiriamali kupitia sera wezeshi zenye kutekelezeka, wa pili kulia Meneja Mradi wa BEST-DIALOGUE, Bw.Hans Determeyer , katikati ni Mkurugenzi wa Program ya Kimataifa ya SEPT,Profesa Utz Donberger, (wa pili kushoto) ni Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Uwekezaji ,Profesa Adolf Mkenda na kushoto ni Mkuu wa Kitivo cha Biashara Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDBS) ,Dk. Ulingeta Mbamba.
Wadau wa masuala ya biashara wa ndani na nje ya nchi wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa majadiliano iliyotolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Uwekezaji ,Profesa Adolf Mkenda (hayupo pichani), wakati wa majadiliano yaliyohusu kuongeza kasi ya ubunifu na ukuaji wa wajasiriamali kupitia sera wezeshi zenye kutekelezeka.

IJUE LULU-KITO, PAMBO, DAWA NA CHAKULA CHA THAMANI KUBWA

$
0
0
Inaitwa Lulu kwa lugha ya Kiswahili. Kwa lugha ya Kiingereza ni Pearl. Hicho ni kito cha thamani ambacho mara nyingi kinakatwa, kusuguliwa na kung'arishwa kwa namna mbalimbali na kutumiwa pamoja na madini mengine kama dhahabu au fedha na kutengenezwa mapambo kama pete, hereni, mikufu au vikuku.

Lulu inatajwa siku nyingi kuanzia katika misahafu ambavyo ni vitabu vitakatifu kwa waumini wa dini ya Kiislamu hadi katika Bibilia na hadithi nyingine za kale. Nchini kuna utajiri mkubwa wa Lulu, lakini hakuna jitihada zozote za kuvuna kito hicho cha thamani ambacho moja ya sifa yake kuu ni kutobadilika rangi yake kwa namna yoyote katika kipindi chote cha kudumu kwake labda iharibiwe kwa tindikali.
Lulu ni nini?

Kito hicho ni tofauti na madini ya almasi, dhahabu, Tanzanite, Ruby na madini mengine ambayo yanachimbwa, lakini Lulu inatokana na wanyama (katika viumbe hai aina ya chaza/Oyster) jambo ambalo huenda watu wengi hawalifahamu.

CHAZA NI VIUMBE WA PEKEE SANA DUNIANI KWANI HUZALIWA WOTE WAKIWA MADUME NA KUBADILIKA KUWA MAJIKE MIAKA MITATU BAADA YA KUWAPO DUNIANI NA WANAWEZA KUJIGEUZA TENA KUWA MADUME BAADA YA KUTOTOA MAYAI......
(All pearl oysters are born male and transform into females at around three years of age. Even more remarkably, after releasing her eggs, the female oyster may turn male again! This change can happen in under a month!)

Lulu ni moja kati ya mazao ya bahari ambayo kama yangetumika vizuri yangewanufaisha wakazi wa Pwani na Taifa kwa ujumla kuliko sasa. Kwa kawaida chaza ana magamba na chakula chake hukipata baada ya kuyachuja maji ambayo mintaarafu anayavuta baada ya kufungua na kufunga magamba yake na wakati wa tendo hilo kuna mabaki ambayo ni chakula kwake hubakia.

Nyama yake inahusishwa na kuongeza virutubisho mwilini na kuchochea ongezeko la homoni ambazo zinaongeza nguvu za kiume kwa wanaume na upande mwingine gamba la mnyama huyo hutumika kama mapambo majumbani na kwingineko.

​Geofrey Chambua Kutoka Vyanzo Mbalimbali ​
Viewing all 109973 articles
Browse latest View live


Latest Images