Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

Mwana FA awataka wanaume kubadili mtazamo kuhusu fistula

$
0
0
Msanii mahiri wa kizazi kipya Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA (pichani) ambae ni Balozi wa Chapa Vodacom amesema hadhi na heshima ya mwanaume katika jamii itakuwa na uzito mbele ya uso wa jamii kwa wao kuwa tayari kutafuta suluhu ya changamoto zinazoikabili jamii na wala si vinginevyo.
Mwana FA ametoa kauli hiyo mjini Dodoma wakati wa kampeni ya kuelimisha jamii kuhusu fistula iliyofanyika katika viwanja vya Nyerere Square kuelekea siku ya fistula dunaini Mei 23. 
Kampeni hiyo inadhaminiwa na kampuni ya Vodacom na Vodafone ya Uingereza ikiihusisha mikoa mbalimbali. 
Balozi huyo amesema ni wazi kwamba wanaume wamekuwa wamiliki wa maamuzi katika jamii huku wakitajwa kuwa nguzo ya familia lakini sifa hizo na mamlaka hayo yatakuwa na dosari kubwa iwapo hawatokuwa pia mstari wa mbele katika kuhakikisha jamii inapata suluhisho la matatizo.

UHURU WA VYOMBO VYA HABARI UWE NA MIPAKA

$
0
0
Na Zawadi Msalla-MAELEZO Dodoma

Vyombo vya Habari nchini vimeaswa kutumia uhuru wake vizuri bila kusababisha madhara ndani ya nchi kama ilivyotokea katika baadhi ya nchi za Afrika.

Akichangia hotuba ya wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Mhe.Jaddy Simayi Jaddy mbunge wa Mkwajuni alisema baadhi ya vyombo vya habari vilivyopo hapa nchini vinaweza kuchangia machafuko ndani ya nchi kwani mwelekeo wa mambo yanayoandikwa yana dalili ya uchochezi.

Alisisitiza kuwa hata kama wananchi wanavihitaji vyombo vya habari lakini vikiachiwa vifanye vinavyotaka vitaipeleka nchi pabaya. “Ni kweli tunavihitaji sana vyombo hivyo ila kwa sasa inabidi viangaliwe kwa umakini sana” Alisema mchangiaji.

Aliiomba Serikali iwasilishe sheria ya vyombo vya habari kama ilivyo ahidi ili kuweza kudhibiti baadhi ya mambo yasiyo sahihi yanayoonekana kwa sasa kwenye vyombo vya habari.

Akielezea uwezo wa vyombo vya habari alisema vyombo hivyo vina nguvu kubwa katika kujenga nchi na kuleta maendeleo ya nchi yeyote ile duniani.

Naye Mbunge wa Bunda Mh. Stephen Wasira akichangia hoja hiyo alisema uhuru lazima uwe na mipaka . Kama hakuna nidhamu ya vyombo vya habari uwepo wa demokrasia inapotea.

Alisema Tanzania ni kati ya nchi inayojali uhuru wa vyombo vya habari kwani mpaka sasa ni nchi pekee Afrika Mashariki iliyo na vyombo vingi vya habari. Takwimu zinaonesha mpaka sasa kuna jumla ya magazeti na majarida 781, magazeti yanayotoka kila siku 13 na magazeti na majarida yanayotoka kwa wiki 62 na kuongeza kuwa hiyo ni moja ya mafanikio makubwa ya kutekeleza uhuru wa Vyombo vya Habari nchini.

Hata hivyo aliwaomba waandishi wa habari waache kuandika habari zisizo na ukweli ndani yake kwani wanao athirika na hilo ni wengi. Alisema uandishi wa habari ni taaluma hivyo wanaoitumikia taaluma hiyo inawapasa kufanya kazi kwa weledi na kufuata kanuni na taratibu za taaluma hiyo.

Akichangia hoja ya vijana alisema vijana ni Taifa la leo. Iwapo Serikali itatoa kipaumbele kwa vijana ajira itapatikana. Hata hivyo aliisifu Serikali kwa jitihada inazochukua za kusaidia vijana katika mikopo inayo wanyanyua, mpango mkakati wa maendeleo ya vijana ni moja ya njia ya kuinua vijana nchini.

UTAMBULISHO WA USIKU WA HIP HOP & FAINALI ZA VODACOM MIC KING KWA WANAHABARI

$
0
0
Meneja Matukio wa Dar Live, Abdallah Mrisho (wa pili kushoto) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho huo. Wengine pichani kutoka kushoto ni DJ John Dilinga (JD), Prodyuza Ally Baucha na Prodyuza Tudd Thomas.
Kutoka kushoto waliokaa ni msanii Stamina, DJ John Dilinga, Abdallah Mrisho, Ally Baucha na Tudd Thomas katika picha ya pamoja na washiriki wa The Vodacom Mic King waliosimama nyuma.
Wakali wa MIC wanaowania gari wakiwa katika pozi na gari hilo.
Wanahabari wakichukua baadhi ya matukio.
...Wakimsikiliza Abdallah Mrisho.
Hawa ndiyo wakali tisa wanaowania gari aina ya Toyota Funcargo (New Model).

Uongozi wa Dar Live Co. Ltd leo umetambulisha tamasha kubwa la kila mwaka la Usiku wa Hip Hop na fainali za kumtafuta Mkali wa Mic zijulikano kama 'The Vodacom Mic King' kwa wanahabari. Tamasha hili litafanyika Jumamosi hii, Mei 25, 2013 katika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar. 

Jumla ya vijana tisa wenye vipaji watapanda stejini kuchuana na mshindi ataondoka na gari aina ya Toyota Funcargo (New Model) yenye thamani ya shilingi milioni 15. 

Mbali na zawadi ya gari, mshindi wa kwanza, pili na watatu, watapata fursa ya kurekodi wimbo mmoja chini ya Prodyuza mahiri nchini, Tudd Thomas, aliyerekodi wimbo maarufu wa Leka Dutigite wa Kigoma All Stars na nyingine nyingi. Majaji katika shindano hili ni mwandishi mkongwe wa habari za muziki na wasanii, Abdallah Mrisho, DJ John Dilinga (JD) na Prodyuza Ally Baucha.

Tamasha hilo litapambwa na burudani kutoka kwa wakali wa Hip Hop nchini ambao ni Fid Q, Joh Makini, Stamina, Kala Jeremiah, Nay wa Mitego pamoja na shoo kali kutoka kundi la Wakali Dancers. Katika usiku huo, zitatolewa tuzo kwa wasanii wa Hip Hop na kwa wimbo bora wa Hip Hop uliofanya vizuri mwaka 2012/13. 

Kutakuwa na Tuzo kwa Msanii Mkongwe Bora wa Hip Hop na Msanii Chipukizi Bora wa Hip Hop pamoja na Wimbo Bora wa Hip Hop.(PICHA NA MUSA MATEJA / GPL)

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA 14 WA BARAZA LA USIMAMIZI WA MAWASILIANO AFRIKA, JIJINI DAR LEO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongoza na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Prof. John Mkoma, wakati akiondoka kwenye chumba cha mkutano baada ya kufungu rasmi mkutano huo wa 14 wa baraza la usimamizi wa Mawasiliano Afrika, uliofunguliwa leo Mei 21, 2013 kwenye Hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya washiriki wa mkutano huo, baada ya ufunguzi. Picha na OMR.

Mkurugenzi Mkuu wa Helvetic Solar Eng. Patrick Ngowi atembelea IPP media

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Helvetic Solar Contractors Eng. Patrick Ngowi akiwa na mwenyeji wake Mkurugenzi Mkuu wa IPP Media Bi. Joyce Mhavile alipofika katika ofisi hizo mapema leo kwa ajili ya mazungumzo na kuhojiwa katika kipindi cha Business Edition, kitakachorushwa Ijumaa hii saa 2 na dakika 45 usiku, Capital TV.

Dar es Salaam. 21 Mei, 2013.Mkurugenzi Mkuu wa Helvetic Solar Contractors Eng. Patrick Ngowi ameendelea kutoa rai kwa vijana nchini Tanzania kuwa na moyo na bidii ili kuweza kutimiza ndoto zao za maendeleo na kujikwamua kiuchumi.

Eng. Ngowi ambaye pia ni mshindi wa ‘Forbes 2013: 30 under 30: Africa’s Best Young Entrepreneurs’ alisema maneno hayo mapema leo katika mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa IPP media Bi. Joyce Mhavile alipofika kufanya ziara na mahojiano maalum katika kituo hicho.

“Vijana wa kitanzania wanafursa nyingi sana katika nchi yetu, imefika wakati sasa vijana wajitambue kwamba wanaweza kutimiza ndoto zao kadiri bidii zao zitakavyowatuma. Kwa mfano, mi nilianza na mtaji wa shilingi milioni mbili, lakini hivi sasa nilipofikia biashara yangu imekua na nimeweza kufanya maajabu makubwa katika soko ukizungumzia swala ya nishati ya jua,” alisema Eng. Ngowi.

Aliongeza, “Kinachotakiwa ni kuwa mbunifu katika biashara unayofanya, kuwa na ujasiri pamoja na umakini wa kile unachokipenda na pale unapotaka kufika. Yote yanawezekana na kijana yeyote anaweza fanikiwa.”

Pamoja na hayo Eng. Ngowi aliwapongeza sana IPP media kwa mafanikio yao waliyopata katika kipindi chote tangu kianzishwe, ikiwemo tuzo ya ‘Number 1 Super Brand’ katika Afrika Mashariki hivi karibuni.

Aidha, Mkurugenzi Mkuu wa IPP Media Bi. Joyce Mhavile alimpongeza kwa mafanikio yake na kumshukuru sana Eng. Ngowi kwa ugeni wake.

Picha na habari na Amani Nkurlu.

Afande mpinga kazi kwako

$
0
0
Kamanda Mpinga unaiona hii ya leo karibu na New Msasani Club Barabara ya Mwai Kibaki Road jijini Dar es salaam? Huyo dereva sio tu aliamua kupita katikati ya foleni bali pia alikuwa katika mwendo wa kasi na fujo huku akipiga honi. Mie mwenyewe kanikosa kunipiga pasi Kitetenesi changu....Wanaomjua wanasema dereva huyo hizo ndio zake na  hakuna wa kumgusa (ati hata wewe) kwa kuwa yuko 'Connected'. Je ni kweli jamaa yuko juu ya sheria??
Mdau Msasani Kwa Mwalimu

Bandari ya Dar es Salaam ni kichocheo cha uchumi – Benki ya Dunia

$
0
0

Na VOA

Tanzania na mataifa jirani ya Afrika Mashariki yanatajwa kuwa yanaweza kuboresha pato la ndani la mwaka – GDP – kama yatachukua hatua za kuboresha ubora wa bandari ya Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa ripoti mpya iliyopewa kichwa cha ‘Opening the Gates: How the port of Dar es Salaam can transform Tanzania’ iliyoandikwa na Jacques Morisset, mchumi mkuu wa Benki ya Dunia kwa Tanzania, Uganda na Burundi, Tanzania na majirani zake wanaweza kuongeza pato lao la ndani kwa kiwango kikubwa.
Ripoti hiyo inasema Tanzania inaweza kuongeza pato lake la ndani kwa kiasi cha dola bilioni 1.8  na nchi jirani zinaweza kupandisha pato la ndani kwa dola milioni 830 kwa mwaka, kiwango ambacho kinaelezewa ni hasara iliyotokea mwaka 2012.

Ripoti hiyo inasema kuwa bandari ya Dar es Salaam iko katika njia kuu ya biashara ya Tanzania kwa asilimia 90, na inashughulikia bidhaa zinazogharimu dola bilioni 15 kwa mwaka, sawa na asilimia 60 ya pato la ndani la Tanzania kwa mwaka 2012.

Bandari hiyo pia inaelezewa kuwa inatumiwa na majirani sita wa Tanzania, ambao nchi zao hazina bandari, nchi hizo ni Malawi, Zambia, Burundi, Rwanda, Uganda na mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Mwaka 2012 pekee, ripoti inasema hasara ya jumla inayoelezewa ambayo imetokea katika bandari hiyo imefikia dola bilioni 1.8 kwa uchumi wa Tanzania na dola milioni 830 kwa nchi jirani. Hasara ambayo ni sawa na asilimia saba ya pato la ndani la mwaka la Tanzania, na kwa kiasi kikubwa imeathiri wanunuzi wa ndani, biashara na mashirika ya serikali.

Moja ya sababu ambazo inaelezewa zimechangia katika hasara hii ni utendaji mbaya wa bandari ya Dar es Salaam ambao umezigharimu nchi nyingine jirani nazo kupata hasara, na hivyo kulazimika kulipa fedha zaidi kwa bidhaa zinazoagiwa kutoka nje, ikiwemo bidhaa za msingi kama vile mafuta ghafi, simenti, mbolea na madawa.

Moja ya vigezo  vilivyoelezewa katika ripoti ambavyo vinachangia katika kusababisha  hasara ni pamoja na uchelewesho unaozikabili meli ambazo zinafika katika bandari ya Dar es Salaam.  Katikati ya mwaka 2012, meli zilisubiri kwa takriban siku 10 ili kuweza kuruhusiwa kutia nagan na siku 10 nyingine za ziada ili kuweza kushusha mizigo. 

Rushwa pia imetajwa kuwa ni kigezo kingine kinachochangia katika utendaji mbaya wa Bandar, kama chanzo cha utendaji mbaya na kusababisha hasara kubwa.

SERENGETI FREIGHT FORWARDERS LTD WAZEE WA KAZI: GOOD NEWS FOR TANZANIA

$
0
0


HUDUMA MPYA YA KIFURUSHI 
NEW DOOR TO DOOR SERVICE
TUNACHUKUA MZIGO MLANGONI KWAKO UK NA TUTAUFIKISHA MLANGONI KWAKO DAR
UKILIPA HAPA UK HAULIPI TENA DAR, SISI TUTAKULETEA MZIGO NYUMBANI KWAKO!
Baada ya kushughilikia kwa kina mapungufu yaliyojitokeza mwanzo, 
sasa tumerudi na huduma ya kifurushi tena ikiwa imeboreshwa zaidi.
BEI ZETU KAMA KAWAIDA HAZINA KIGUGUMIZI NA SI ZA KUUMIZA

AIR CARGO TO DAR NOW £3.50 INCLUSIVE CLEARANCE!
AIR CARGO TO ZANZIBAR NOW £3.00 INCLUSIVE CLEARANCE!
AIR CARGO TO NAIROBI/MOMBASA NOW £2.80 INCLUSIVE CLEARANCE!
KIFURUSHI KWA KONTENA DAR/ZANZIBAR NOW £2.20 INCLUSIVE CLEARANCE!

NDEGE ZINAONDOKA KILA WIKI MARA MBILI
TUNAFUATA MZIGO KUTOKA POPOTE UK
MINIMUM WEIGHT IS 40KILOS
KAMA UNATAKA KUAGIZA KITU AU KUFANYA BOOKINGS TUWASILIANE KWA NAMBA HAPA CHINI
CHRIS LUKOSI +44 07903828119  & 07404279633 
SIMON LOUIS (MOHSIN) +44 07950689243

HQ -  UNIT 92 THAMES INDUSTRIAL PARK, PRINCESS MARGARET ROAD, EAST TILBURY, RM18 8RHRH
Tell (+44) 01375 855917  Fax (+44) 01708202477

Wakazi wa Tanga sasa kulipia maji kupitia Vodacom M-Pesa na Airtel Money

$
0
0
Zaidi ya wananchi 700,000 waishio katika manispaa ya Tanga sasa hawatahitaji tena kupanga foleni ili kulipia ankara za maji. Hii inafuatia ushirikiano baina ya Vodacom Tanzania na mamlaka ya maji safi na maji taka ya Tanga (UWASA) utakaowezesha malipo hayo kufanyika kupitia huduma ya M-Pesa na Airtel Money. 
(UWASA) ni mamlaka iliyoundwa kisheria chini ya sheria ya utoaji maji kifungu cha 272 ili kuendesha shughuli za upatikanaji wa maji safi na kusimamia maji taka mjini Tanga.(UWASA) ilianza kufanya kazi zake kama taasisi huru mwezi Januari, 1998.
 Huduma ya M-Pesa ina mawakala zaidi ya 40,000 nchi nzima, hivyo kuwezesha urahisi wa malipo ya huduma ya maji kama hii mahala popote pale nchini. Katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa UWASA,Injinia Joshua Mgenyekwa, alizungumzia jinsi ambavyo kwa kiwango kikubwa wakazi wa Tanga wataepuka usumbufu wa kutumia muda mrefu kwenye foleni za kulipia huduma ya maji na kusema: 
"Huduma hizi ni hatua ya kipekee hasa ikizingatiwa kuwa kuanzia sasa muda ambao mteja angeutumia kusubiri kwenye foleni, badala yake atauingiza katika shughuli nyingine za kila siku kama kazi au biashara. Pia kufanya malipo kupitia M-Pesa au Airtel Money kutarahisisha ufanyaji kazi wa mamlaka na kutoa nafasi ya kuongeza ubora wa huduma." 
Mkuu wa kitengo cha biashara cha M-pesa Vodacom Tanzania,Bw.Jackson Kiswaga alisema: "Nawahimiza wakazi wa Tanga watumie huduma ya M-Pesa kulipia ankara za maji kutokana na kuwa ni huduma ya haraka na salama. Hii ni njia ya uhakika ya kuokoa muda malighafi muhimu wa muda, na hivyo ni vyema sote kuitumia."
 Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya maji safi Mkoa wa Tanga,(UWASA) Injinia Joshua Mgenyekwa(katikati)akimshuhudia Mkuu wa kitengo cha biashara cha M-pesa Vodacom Tanzania,Bw.Jackson Kiswaga kushoto akisaini mkataba kwa ajili ya kutoa huduma ya M-pesa kwa wakazi wa mkoa wa Tanga,ambapo watakuwa wakilipia Ankara za maji kwa mara ya kwanza  kupitia huduma hiyo na Airtel Money,kulia ni Meneja wa kanda ya kaskazini wa Airtel Bw.Stephen Kimea.
 Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya maji safi(UWASA) Mkoa wa Tanga,Injinia Joshua Mgenyekwa(katikati)akibadilishana nyaraka walizosainiana zinazohusu makubaliano ya kutoa huduma ya M-PESA na Mkuu wa kitengo cha biashara cha M-pesa Vodacom Tanzania,Bw.Jackson Kiswaga.Ambapo wakazi wa mkoa huo watakuwa wakilipia Ankara za maji kwa mara ya kwanza  kupitia huduma hiyo na Airtel Money,kulia ni Meneja wa kanda ya kaskazini wa Airtel Bw.Stephen Kimea.
Baadhi ya wafanyakazi wa taasisi ya maji safi Mkoa wa Tanga,(UWASA)wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania na Airtel,mara baada ya kusainiana mkataba wa kampuni hizo mbili kutoa huduma ya malipo ya Ankara za maji kupitia huduma ya M-PESA NA Airtel Money.

OBAMA KUTEMBELEA TANZANIA MWEZI UJAO

$
0
0
Rais wa Marekani,Mh. Barack Obama.

Kuanzia tarehe 26 Juni hadi 3 Julai, Rais Obama na Mkewe wanatarajia kutembelea nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania. 

Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.

Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa. 

Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla.

TAARIFA TOKA WHITE HOUSE, MAREKANI

safu mpya ya globu ya jamii: Miondoko ya kumeremeta kwenye mnuso

$
0
0
Tegemea kupata makala hii kila saa mbili asubuhi kila siku..

Article 24

Article 23

changamoto za magari ya zimamoto kufika maeneo ya tukio jijini Dar

Africa Center and U.S. Embassy Sponsor Symposium on Natural Resources and Conflict Prevention in Tanzania

$
0
0
Program Manager at the Africa Center for Strategic Studies (ACSS) Regional Office for East Africa Mr. Bradley Anderson, giving remarks when recently attended a full-day program discussing Natural Resources and Conflict Prevention event which was co-hosted by the ACSS, the ACSS Tanzania Community Chapter, and the United States Embassy in Tanzania. The symposium is part of the Washington, D.C.-based Africa Center’s Topical Outreach Program Series (TOPS), designed to increase the quality and quantity of communications and networking among ACSS alumni, ACSS faculty and staff, and U.S. stakeholders and policymakers.
In the picture seated is; President of the Africa Center for Strategic Studies (ACSS) Tanzania Community Chapter and Associate Professor at St. John's University of Tanzania, Professor Egnald P. Mihanjo, (2nd from left); Member of Parliament for Kahama and Chairman Natural Resources Parliamentary Committee, Natural Resources and Conflict Prevention, Honorable James Lembeli, (3rd from left); ACSS Professor of National Security Studies, Dr. John Kelly, (3rd from right); and Program Manager at the ACSS Regional Office for East Africa Mr. Bradley Anderson, (right); with other participants who recently attended a full-day program discussing Natural Resources and Conflict Prevention event which was co-hosted by the ACSS, the ACSS Tanzania Community Chapter, and the United States Embassy in Tanzania. The symposium is part of the Washington, D.C.-based Africa Center’s Topical Outreach Program Series (TOPS), designed to increase the quality and quantity of communications and networking among ACSS alumni, ACSS faculty and staff, and U.S. stakeholders and policymakers. (Photo courtesy of the U.S. Embassy).

MESSAGE ON THE INTERNATIONAL DAY FOR BIOLOGICAL DIVERSITY

$
0
0
Secretary-General of the United Nations,Ban Ki-moon 
As the international community strives to accelerate its efforts to achieve the Millennium Development Goals and define a post-2015 agenda, including a set of goals for sustainable development, water and biodiversity are important streams in the discussion.

Although seemingly abundant, only a tiny amount of the water on our planet is easily available as freshwater. We live in an increasingly water insecure world where demand often outstrips supply and where water quality often fails to meet minimum standards. Under current trends, future demands for water will not be met.

Biodiversity and the ecosystem services it provides are central to achieving the vision of a water secure world. Ecosystems influence the local, regional and global availability and quality of water. Forests help regulate soil erosion and protect water quality and supply.

Wetlands can reduce flood risks. Soil biodiversity helps maintain water for crops. Integrating nature-based solutions into urban planning can also help us build better water futures for cities, where water stresses may be especially acute given the rapid pace of urbanization.

Recognizing the importance of biodiversity, the United Nations General Assembly has encouraged the use of the Convention on Biological Diversity’s Strategic Plan for Biodiversity 2011-2020 and its Aichi Targets in the elaboration of the post-2015 development agenda. Last year’s Rio+20 Conference on Sustainable Development also recognized the role of ecosystems in maintaining water quantity and quality. Where once the focus was on trade-offs between water use and biodiversity, today we are coming to understand how biodiversity and water security are mutually reinforcing.

This shift from conflict to synergy is particularly welcome in this, the International Year of Water Cooperation.

On the International Day for Biological Diversity, I also call on all Parties to the Convention on Biological Diversity who have not already done so, to ratify the Nagoya Protocol on Access to Genetic Resources and the Fair and Equitable Sharing of Benefits Arising from their Utilization, and therefore help us all to work toward the future we want.

Airtel yazindua ofa kabambe kupiga simu kwenda nje ya nchi

$
0
0

 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano (kushoto) na Meneja Biashara za Kimataifa wa Kampuni hiyo, Prisca Tembo (wa pili kutoka kulia) wakizindua huduma mpya ya kupiga simu kwenda India kwa gharama nafuu. Wengine ni Balozi wa India hapa nchini, Debnath Shaw (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Sunil Colaso.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa pili kutoka kulia), akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya kupiga simu kwenda India kwa gharama nafuu. Wengine ni Meneja Biashara za Kimataifa wa Kampuni hiyo, Prisca Tembo (kulia), Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni hiyo, Beatrice Singano na Balozi wa India hapa nchini, Debnath Shaw.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya kupiga simu kwenda India kwa gharama nafuu. Wengine wanaofuatia ni Balozi wa India hapa nchini, Debnath Shaw, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Sunil Colaso na Meneja Biashara za Kimataifa wa Kampuni hiyo, Prisca Tembo.

HAYAWIHAYAWI, SASA YAMEKUWA! USIKU WA HIP HOP, THE VODACOM MIC KING KURINDIMA J’MOSI HII DAR LIVE

$
0
0
Wakali tisa wa Hip Hop wanaowania gari aina ya Toyota FunCargo (new model), katika pozi mbele ya gari lao.

ILIPANGWA, ikapangika. Baada ya kusubiririwa kwa muda mrefu, hatimaye msimu mpya wa shoo ya Usiku wa Hip Hop (2013) unachukuwa nafasi Jumamosi hii ndani ya Ukumbi wa Dar live, Mbagala-Zakhem, jijini Dar.

Wasanii wanaotamba kwenye gemu la Hip Hop, Kala Jeremiah, Fid Q, Nay wa Mitego, Joh Makini, Stamina na wengine kibao pamoja na washiriki wa Shindano la The Vodacom Mic King watakamua shoo baab’kubwa kuweka historia mpya ya burudani.

Meneja Matukio wa Ukumbi wa Dar Live, Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’ amewahakikishia mashabiki wote wa muziki wa Hip Hop kuwa Jumamosi kutasheheni matukio kibao, ulinzi mzito utakuwepo pamoja na parking kubwa ya magari hivyo watu wafike kwa wingi watainjoi kwa nafasi na kuondoka salama ukumbini.

“Vijana tisa waliosalia katika Shindano la The Vodacom Mic King watapanda jukwaani na kushusha mistari ambapo mshiriki mmoja anatarajiwa kuondoka na gari jipya aina ya Toyota FunCargo (new model),” alisema Abby Cool na kuongeza:“Mashabiki wanaweza kulifuatilia shindano hilo kupitia Runinga ya DTV kuweza kujua jinsi ya kuwapigia kura.”

Washiriki hao na namba zao za ushiriki kwenye mabano ni Ally (MK 02), Anold (MK 03), Bahati (MK 05), Boniface (MK 07), Emmanuel (MK 10), Ibrahim (MK 12), Karrys (MK 13), Lusajo (MK 14) na Martin (MK15). Jinsi ya kuwapigia kura, wasomaji wanatakiwa kuandika neno MK wakiambatanisha na namba ya mshiriki kisha kutuma ujumbe huo kwenda namba 15564.

OFA ZAIDI KWA MSHINDI
Mbali na mshindi kuondoka na gari, Mrisho aliongeza kuwa washindi watatu wa nafasi za juu watajipatia dili la kurekodi singo mojamoja kutoka kwa prodyuza kiwango aliyezalisha ngoma kali Bongo ikiwemo ya Kundi la Kigoma All Stars iitwayo Leka Dutigite, Tudd Thomas.

TUZO KUTOLEWA
Mrisho alitiririka na mistari kuwa, mbali na shoo kali kutoka kwa wakali hao wa Hip Hop, kutakuwa na kipengele cha kutoa tuzo za muziki wa Hip Hop katika vipengele tofauti hivyo mashabiki pia waendelee kuwapigia kura wasanii wanaowapenda.

Vipengele vitakavyotolewa tuzo ni Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Legendary) ambapo yamepita majina matatu; Fid Q, Joh Makini na Profesa Jay. Pia kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Chipukizi) ambacho kina majina kama Young Killer, P The Mc na Tabla huku akianisha kipengele cha mwisho ambacho ni Wimbo Bora wa Hip Hop (2012/13) chenye nyimbo kali za Dear God (Kala Jeremiah), Sihitaji Marafiki (Fid Q) na Najuta Kubalehe (Stamina).

“Ili kuwapigia kura, mashabiki wanatakiwa kuandika neno BHL wakiambatanisha na jina la msanii husika kwenda namba 15564 katika kipengele cha Msanii Bora wa Hip Hop (Legendary).
“Kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Chipukizi), mashabiki waandike neno BUA na kufuatiwa na jina la msanii wanayempenda kwenda namba 15564,” alisema Abby Cool na kuongeza:“Kipengele cha Wimbo Bora wa Mwaka, mashabiki waandike neno BHS likifuatiwa na jina la msanii wanayempenda kisha watume ujumbe huo kwenda namba 15564.”


KUWAENZI WASANII/SOKA KWENYE SKRINI KUBWA

Abby Cool aliweka bayana kuwa katika shoo hiyo kutakuwepo na documentary maalumu ya kuwakumbuka wasanii wa Hip Hop waliotangulia mbele za haki kupitia skrini kubwa bila kusahau mashabiki wa soka watapata fursa ya kushuhudia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (Uefa) kati ya Bayern Munich na Borrusia Dortmund. Twendeni Dar Live J’mosi!

bei ya madafu leo

Nyerere remembered as pioneer of democracy in Africa

$
0
0
By Hassan Abbas, Addis Ababa

As the African Union (AU) celebrates its 50 Years Golden Anniversary and its brain child, the governance assessment Mechanism (APRM), marks 10 Years of its existence, African leaders have been challenged to promote democracy and good governance.

The call was issued by two African governance activists, the CEO of the APRM Continental office, Assefa Shifa and the former Mozambican President, Joachim. Opening during the opening of a two days colloquium to reflect on the 10th Anniversary of the APRM.

In his presentation on progress in improving governance in Africa, Mr. Shifa cited Mwalimu Julius Kambarage Nyerere of Tanzania as one of the few African leaders who could descend from power from their own volition.

He added that others leaders like Joachim Chissano of Mozambique and Nelson Mandela of South Africa who followed Nyerere’s footsteps by stepping down from leadership position at a time nobody their people were still in quest of their services.

On his part, President Chissano who was invited to offer a key note address to the gathering of more than 100 African experts and political leaders’, said the African continent once accused for having imperial presidents was now making significant strides in democratization and respect to constitutional and term limits.

He argued that term limit and respect for good governance values were the heart of the AU and APRM cherished values but situation in some countries caused the whole of the Continent to be accused. He reminisced how his own people protested when he announced to step down.

“My personal view of the state of governance and democratization in Africa is that against the backdrop of imperial presidents and hegemony leaders, the wave of democratization is now too high for such practices,” said Mr. Chissano a recipient of the prestigious Mo Ibrahim Governance Award.

He expressed his optimism that with the APRM, Africa has now a unique opportunity to address governance issues with a Pan-African solidarity. He said the design of the APRM makes it possible for African countries to treat each others like members of the same family and that has helped incidents of leaders being overthrown from power to diminish.

“With democratization in Africa and APRM advocacy among other interventions, Africans today must act and feel like brothers and sisters…military coups are now sporadic as those who continue to ascend to power unconstitutionally are clearly aware that they will be denounced,” he said.

The former leader called upon African leaders to strengthen the Mechanism to become a premier assessment Mechanism for governance in Africa so as to cherish the dream of AU founders who longed for a more prosperous Africa.
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images