Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110129 articles
Browse latest View live

MAGUFULI: VYOMBO VYA HABARI SIMAMIENI KUJENGA MAADILI NA UTAMADUNI WA MTANZANIA

$
0
0
Na Daudi Manongi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli ametoa wito kwa vyombo vya Habari nchini kuwa mbele katika kusimamia Maadili na kuutangaza Utamaduni wa Mtanzania.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati wa Mahojiano ya mwaka na waandishi wa habari kwa mara ya kwanza tangu aingie madaraka.

“Jukumu la kulinda Utamaduni na Maadili ya mtanzania ni la kila mzalendo, mtanzania, mzazi na Wizara husika ipo kwa ajili ya kusimamia jambo hili na vyombo vya habari mnatakiwa kuwa mstari wa mbele kulisimamia kwa kuanzia katika vyombo vyenu vya Habari kutokana na kile mnachoonyesha”Alisema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amevitaka vyombo vya Habari kuwa wazalendo katika kutengeneza vipindi vyenye mahadhi ya kitanzania ili kuisaidia jamii kukua katika utamaduni wetu na kusaidia kujenga maadili yaliyo bora.

Mbali na hayo Rais Magufuli amezungumzia mafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika kipindi chake cha mwaka mmoja toka aingie madarakani ikiwemo kuongezeka kwa mapato kutoka bilioni 800 mpaka makusanyo ya shilingi trilioni 1.5 kwa mwezi.

Pia amesema kuwa Bajeti ya mwaka 2016 ya trilioni 29.5 iliyotenga asilimia 40 kwenye miradi ya maendeleo imekuwa yenye mageuzi makubwa ukilinganisha na bajeti ya miradi hapo nyuma mabayo ilikuwa asilimia 26 tu.Pamoja na hayo Rais magufuli amesema kuwa Serikali imeagiza ndege nyingine mbili zinategemewa kufika nchini mwanzoni mwa mwaka 2018 ili kuboresha sekta ya utalii nchini.

Akizungumzia uundwaji wa serikali amesema mategemeo yake katika serikali aliyoiunda imefanikiwa kwa kuwa Baraza aliloliunda la watu wachache limekuwa la mafanikio makubwa na hili limetokana na ushirikiano mkubwa wa mawaziri wake.

Rais Magufuli amevitaka vyombo vya habari nchini kubadili mtazamo wao katika uandishi wao wa habari na kuandika habari ambazo zina maslahi kwa Taifa na kuwahakikishia waandishi wa habari kushirikiana nao kwa kuwa anatambua kazi nzuri wanayoifanya.

KONGAMANO MAALUM LA UWEKEZAJI KUFANYIKA NCHINI ISRAEL

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji ,Clifford Tandari akizungumza na baadhi ya Watumishi wa Kituo hicho pamoja na Waandishi wa Habari wakati walipotembelewa na balozi wa Israel kuzungumzia Kongamano la Biashara na Uwekezaji litakalofanyika Tel Aviv Israel. 
Balozi wa Israel Nchini Tanzania,Yahel Vilan akizungumzia Kongamano hilo ambalo kwa mara ya kwanza litafanyika nchini Israel baada ya kufanyika Tanzania kwa mara ya Tatu mfululizo.
KITUO  cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya nchi za nje na Taasisi za Sekta binafsi Tanzania  kimeandaa kongamano maalum  la kuamasisha na kukuza uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Israel kwa lengo la kuisaidia na kuitangaza tanzania kama ni miongoni mwa maeneo yenye fursa na mazingira mazuri ya kibiashara kwa kampuni  nyingi za Israeli.

Kongamano hilo ambalo kwa mara ya kwanza litafanyika nchini Israel  baada ya kufanyika Tanzania mara tatu mfulilizo  linatarajia kufanyika kuanzia tarehe 28 novemba hadi 30 mwaka huu ambalo litahudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wawekezaji, wafanyabiashara wakubwa na wataalamu mbalimbali huko Tel Aviv Isrel.

Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji , Clifford Tandari amesema kuwa malengo ya Kongamano hilo ni kutoa fursa za biashara na uwekezaji zilizopo hapa nchini kwa wawekezaji wa Isrel ambazo zipo maeneo katika sekta mbalimbali kama vile viwanda, kilimo na Usindikaji wa mazao,Nishati, Afya,Teknologia, Elimu, Maji ,Majengo,Chakula ,Dawa, Utafiti na Maendeleo.

Bw.Tanadri ametoa two kwa makampuni ya Tanzanania kwenda kushiriki  kongamano hilo ili kuanzisha na kukuza ushirikiano katika nyanja za biashara na uwekezaji kwa kushirikiana na Kampuni na wafanyabiashara wa Israel, kwani kuna uwezekano mkubwa  Tanzania ikaongeza thamani yake.thamani ya mitaji na uwekezaji  kutoka nje iwapo makampuni ya Israel yatakayohudhuria kongamano hilo yataamua kufanya uwekezaji.

"Tunatoa wito kwa makampuni yetu ya Kitanzania yaweze kwenda kushiriki katika kongamano hili maana ni fursa za kipekee sana,” amesema Tandari

Naye Mh.Balozi wa Israel Nchini Tanzania Bw.Yahel Vilan ameeleza kuwa amefurahishwa na  kongamano hilo na anaamini kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zitashiriki vizuri Kongamano hilo.

TANZANIA CIVIL SOCETY STATEMENT TOWARDS THE UNFCCC COP22

$
0
0
ForumCC Project Officer Fazal Issa (left) and Dar es Salaam Program Manager of Oxfam Tanzania Heri Ayubu speaking to journalists during a press conference organized by ForumCC, Care Tanzania and Oxfam Tanzania to brief on the Tanzania Civil Society Statement towards the UNFCCC COP22 which will be held in Marrakesh-Morocco from 7-18th November 2016.
Journalists taking notes during a press conference organized by ForumCC, Care Tanzania and Oxfam Tanzania to brief on the Tanzania Civil Society Statement towards the UNFCCC COP22 which will be held in Marrakesh-Morocco from 7-18th November 2016

Read more in the below attached statement

UN yawapiga msasa wanafunzi wa Chuo cha Tumaini Makumira juu ya SDGs

$
0
0
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu akitoa semina juu ya malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs) katika Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kilichopo mkoani Arusha.(Picha na Ferdinand Shayo).

Maafisa kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wamefanya ziara ya kutembelea Chuo cha Tumaini tawi la Arusha ikiwa ni pamoja na kutoa semina juu ya Malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ikiwemo kufuta umasikini, kuondoa njaa na kuhakikisha upatikanaji wa maji.

Mtaalam wa Programu kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Amon Manyama amesema kuwa wasomi na wanafunzi walioko vyuoni wanapaswa kuelewa vizuri malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) ya Umoja wa Mataifa ili waweze kuyatimiza katika ngazi zao hasa ukizingatia kuwa wanachuo ni wataalamu watarajiwa,na viongozi wa kesho.

Manyama amesema kuwa taasisi,mashirika na jamii pamoja na serikali ina jukumu kubwa la kutekeleza malengo hayo ili kuondoa umasikini, kujenga uchumi endelevu,kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu amesema kuwa vijana hususan wanavyuoni wanapaswa kuwa mambalozi wazuri wa kuyatangaza malengo ya maendeleo endelevu ya UN ili yaweze kutimia na dunia iwe ni sehemu bora zaidi ya kuishi kwa kila mtu.

Temu amesema kuwa UN ina mpango wa kuwafikia vijana walioko vyuoni na mitaani ili waweze kuelewa vizuri juu ya malengo 17 ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa na kujua jukumu walilonalo ndani ya malengo hayo.

Na Ferdinand Shayo, Arusha
Mtaalam wa Programu kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Amon Manyama akiwapiga msasa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira juu ya malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs) katika ukumbi wa chuo hicho jijini Arusha.Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Hoyce Temu (katikati) naRaisi wa Chuo hicho John Maembe (kushoto).
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira wakifuatilia semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyoandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa jijini Arusha.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MUSWADA WA SHERIA YA HUDUMA ZA HABARI WASOMWA MARA YA PILI

$
0
0
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO

Muwada wa Sheria ya Huduma za Habari wa mwaka 2016 umesomwa mara ya pili Bungeni mjini Dodoma ukiwa na lengo la kuifanya tasnia ya habari nchini kuwa taaluma kamili.

Wiziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye amesema hay oleo Bungeni Dodoma alipokuwa akiwasilisha Muswada huo, huku akisisitiza kuwa una sehemu kuu nane ambazo zinaufanya kuleta mageuzi katika tasnia ya habari nchini na kuifanya kuwa taaluma kamili itayowaletea heshima wanahabari na tasnia hiyo kwa ujumla. 

“Hatuwezi kwa na vyombo vya habari makini kama hatutakuwa na wanahabari wenye taaluma ya habari nchini” alisema Nape.

Katika kuonesha ushirikishwaji wa wadau katika kutoa maoni yaliyolenga kuboresha Muswada huo, Waziri Nape amesema kuwa kumekuwa na ushirikishwaji mkubwa wenye wigo mpana kutoka kwa mwananchi mmoja mmoja, wanataaluma wa habari, wanasheria kupitia Chama cha Mawakili Tanzania (TLS), Baraza la Habari Tanzania (MCT), Umoja wa Wamiliki wa vyombo vya habari (MOAT) na Taasisi ya Wanahabari Kusini mwa Afrika, tawi la Tanzania (MISA-TAN).

Wadau wengine walitoa maoni yao ni Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Sikika, Wabunge kupitia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na michango ya Wabunge kupitia Kamati nyingine ambao umesaidia katika kuboresha Muswada huo wenye dhamira ya kuleta ufanisi katika sekta ya habari. 

Miongoni mwa maeneo ambayo wadau hao wameyafanyia maboresho ili Muswada uwe na tija ni pamoja na kuainisha haki na wajibu wa wananhabari ikiwemo uhuru wa kukusanya, kuhariri na kuchapisha au kutangaza habari pamoja na kuainisha haki ya chombo cha habari kukata rufaa kwa kuzingatia mfumo wa wazi na wa kidemokrasia kupitia vyombo vya kutoa haki ikiwemo mahakama huku Jaji Mkuu akiweka utaratibu wa kusikilizwa haraka kwa kesi za masuala ya kihabari.

MADAKTARI BINGWA WA TAASISI YA MOI WAFANYA UPASUAJI WA VICHWA MAJI NA MGONGO WAZI MNAZI MMOJA ZANZIBAR

$
0
0

Dkt. Yassin Juma kutoka Kitengo cha MOI akiwa katika maandalizi ya kumfanyia upasuaji wa kichwa mmoja ya watoto waliofika Hospitali ya Mnazi mmoja kufanyiwa tiba hiyo. 


Daktari bingwa wa upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu ambae pia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya MOI Othman Kiloloma akimueleza Waziri wa Afya Zanzibar (hayupo pichani) jinsi Taasisi hiyo inavyookoa maisha ya watoto wanaokabiliwa na maradhi hayo, (kulia) ni Afisa Habari wa GSM Foundation Khalfani Kiwamba. 
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na ujumbe wa Taasisi ya MOI na GSM Foundation ambao wapo Zanzibar kuwafanyia upasuaji watoto wenye vichwa vikubwa katika Hospitali ya Mnazi mmoja Mjini Zanzibar. 
Dkt. Mohammed Ali Haji wa Kitengo cha upasuaji vichwa maji na mgongo wazi wa Hospitali ya Mnazimmoja akizungumzia ukubwa wa tatizo hilo katika visiwa vya Unguja na Pemba. 

Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo wa nne (kulia) akiwa na Dkt. Othman Kiloloma watatu (kulia)wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wizara na maafisa wa GSM Foundation. Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.

RC NDIKILO ATEMBELEA HIFADHI YA UZIGUA

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo akitembelea hifadhi ya msitu wa Uzigua akiwa ameambatana na kamanda wa polisi mkoani Pwani Boniventure Mushongi, mkuu wa wilaya ya Bagamoyo alhaj Majid Mwanga na viongozi wengine kutoka mkoa,wilaya na wakala wa misitu (TFS)kanda ya Mashariki.
Mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo akizungumza jambo wakati ilipokwenda kutembelea hifadhi ya msitu wa Uzigua na kutoa agizo kwa waliwavamia waondoke Mara moja.

WANAFUNZI ELIMU YA JUU WATENGEWA BILIONI 483 ZA MIKOPO

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma.

Jumla ya wanafunzi 119,012 wa Elimu ya Juu nchini wametengewa kiasi cha shilingi bilioni 483 Katika mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya kupewa mikopo itakayowasaidia kujikimu pindi watakapokuwa vyuoni.

Kiasi hicho cha fedha kimetajwa leo Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako alipokuwa akitoa kauli ya Serikali kuhusu utoaji wa mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2016/2017.

Prof. Ndalichako amesema kuwa mikopo hiyo inatolewa kwa kuzingatia malengo ya Mfuko wa Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu ambapo kigezo kikuu kimekuwa ni uhitaji wa mwanafunzi pamoja na fani za kipaumbele anayosoma mwanafunzi.

Fani za kipaumbele kwa mujibu wa Wizara hiyo ni pamoja na Sayansi za Tiba na Afya, Ualimu wa Sayansi na Hisabati, Mafuta na Gesi Asilia, Sayansi Asilia na Mifugo, Uhandisi wa Viwanda pamoja na Kilimo na Umwagiliaji.

Prof. Ndalichako ameongeza kuwa kuna baadhi ya wanafunzi ambao wamedahiliwa kwenye fani za kipaumbele lakini hawana vigezo vya kupewa mikopo kutokana na tathmini ya uhitaji kuonesha kuwa wanaweza kusomeshwa na wazazi au walezi wao. 

“Kwa mwaka huu wa fedha, Serikali imeongeza kiasi cha fedha zinazotakiwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu waliochaguliwa na wanaondelea na masomo katika vyuo mbalimbali nchini kutoka shilingi bilioni 473 hadi bilioni 483 ambayo itaweza kugharamia wanafunzi wanaoanza 25,717 na wanaoendelea na masomo 93, 295”, alisema Prof. Ndalichako.


ULANGA YAPOKEA MSAADA WA MADAWATI KUTOKA KWA WAKAL WA MISITU

$
0
0

Na Sekela Mwasubila 
Afisa habari, halmashauri ya wilaya ya ulanga

Mkuu wa wilaya ya Ulanga mh. Jacob Kassema amewaomba wakala wa misitu na wadau wengine wa elimu kuchangia ujenzi wa madarasa na upatikanaji wa madawati katika shule ya sekondari ulanga.

Aliyasema hayo wakati wa akipokea msaada wa madawati kutoka kwa wakala wamisitu wilayani ulanga ikiwa ni mchango wao wa kuunga mkono agizo la rais la kuhakikisha kila mwanafunzi anakaa kwenye dawati.

Alisema kuwa anawashukuru wadau hao kwa msaada wao mkubwa walioutoa kwaniutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo la madawati ndani ya wilaya nakuongezea kuwa wasiishie hapo kwani bado kuna mahitaji ya ukamilishaji wamadarasa katika shule ya sekondari ya ulanga ili kuhakikisha wanafunzi wakidato cha kwanza wanapata mahali pa kusomea kwani kuna upungufu wamadawati na madarasa.

Aidha amesema kuwa pamoja na serikali kutenga fedha kwa ajili ya
ukamilishaji wa madarasa hayo lakini pia kama wadau wa maendeleo
wasichokekuchangia katika shule hiyo kwani maendeleo ya ulanga
yateletwa na wadau wamaendeleo.

Pia kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya
Ulanga bwana Yusuf Semuguruka aliongeza kwa kuwashukuru wadau hao kwa mchango wao na kusema kuwa msaada huo utaelekezwa katika shule ya
sekondari ulanga ilikuhakikisha wanafunzi wa kidato cha kwanza
wanakaa kwenye madawati.

Hata hivyo diwani wa kata ya mahenge mjini mh. nassoro kihiyo
aliwashukuruwadau hao kwa msaada huo na kusema kuwa kwa kushirikiana na madiwani wengine watahakikisha wanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule yasekondari ulanga wataanza kidato cha kwanza na wote watakaa kwenye madawatikwa kushirikiana na wadau wengine.

Wakala wa misitu wilaya ya ulanga wametoa madawati themanini kwa ajili
yashule za sekondari na msingi ili kukabiliana na tatizo la upungufu
wamadawati na kutimiza agizo la rais wa jamuhuri wa muungano wa
tanzania lakuhakikisha kila mwanafunzi anakaa kwenye dawati.
Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Kulia Mh. Jacob Kassema akipokea
madawati kwa kaimu Meneja Misitu Wilaya ya Ulanga Bwana Fredrick Lohay katika viwanja vya Shule ya Msingi Mahenge Mjini.

RAIS MAGUFULI AWATAKA WATANZANIA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO

$
0
0

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amewataka watanzania kutumia fursa zilizopo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) kwa ajili ya kuliletea maendeleo ya taifa.

Aliyasema hayo leo Jijini Dar es Saalam wakati wa mkutano wake na Wahariri wa vyombo vya habari nchini katika kuadhimisha mwaka mmoja wa Utawala wake, ambapo alisema kuwa ipo haja ya kuzungumza na kuelimisha watanzania juu ya fursa zilizopo katika taasisi hizo.

“Katika Jumuiya hizo zipo fursa nyingi kwa ajili ya maendeleo ingawa inahitajika elimu ya kutosha kwa watanzania kuona fursa zilizopo ikiwemo ufundishaji wa lugha ya Kiswahili nchi za nje” alisema Rais Magufuli.

Mbali na hayo, akizungumza kuhusu suala la kupambana na Rushwa nchini Rais Magufuli ametoa wito kwa vyombo vinavyohusika na kupambana na rushwa kufichua watu wotw wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Rais Magufuli alisema kuwa vita ya Rushwa ni ya kila mwananchi, ambapo alitoa wito kwa watanzania wote kwa ujumla kujiepisha na masuala ya rushwa kwani rushwa ni kansa ya maendeleo nchini.

“Taifa litakwama tukiacha suala la rushwa liendelee, tumeumia kweli kweli katika hili hivyo nitoe wito kwa watanzania wote kwa ujumla kujiepusha na masuala haya kwa ajili ya maendeleo ya nchi kwani kesi ya rushwa ni yetu sote” alifafanua Rais Magufuli.

TBS WATOA ZAWADI KWA WAANDISHI BORA WA INSHA ZA MAZINGIRA KWA WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
SHIRIKA la Viwango Nchini (TBS) limewatangaza washindi wa shindano la uandikaji wa insha lililoandaliwa na Shirika la Mazingira Duniani (UNEP) lililoshirikisha shule za msingi na sekondari Tanzania nzima.

Akizungumza kabla ya utoaji tuzo hizo,Kaimu mkurugenzi mkuu wa TBS Egid Mubofu amesema hatua hii itasaidia sana kuweza kutoa elimu kwa wananchi hasa baada ya wanafunzi hawa kuonesha jitihada kubwa za kuondokana na suala zima la uchafuzi wa mazingira.



Katika shindano hilo lililoshirikisha takribani wanafunzi 75 kutoka sehemu mbalimbali nchini lilianza rasmi mwezi Septemba na kumalizika mwishoni mwa mwezi Oktoba na kufanikiwa kupatikana kwa washiriki nane kwa shule za Msingi na 10 kutoka shule za Sekondari.



Mshindi wa kwanza kwa upande wa shule ya msingi ilichukuliwa na Nairath Ngururu kutoka shule ya Wasichana Almutanzir huku nafasi ya pili ikiendelea Eldred Medard kutoka shule ya Valentine na nafasi ya tatu kwenda kwa Shiluni Laizer kutoka shule ya Havard zote za Jijini Dar es salaam.

kwa upande wa sekondari,wasichana waliendelea kutamba baada ya Zainab Kambi kutoka Academic Internaational kushika nafasi ya kwanza, Frank Kapinga kutoka Kibaha Sekondari kushika nafasi ya pili na nafasi ya tau kuchukuliwa na Pius Mollel kutoka St Jude
 ya Jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa mradi huo, Mary Meela amesema kuwa washiriki wote ni washindi kwani waliweza kuingia kwenye hatua ya mwisho ya mchujo na wanatakiwa kuja kuwa mabalozi wakubwa katika suala zima la mazingira.

Afisa mwakilishi wa UNEP, Clara Nakenya amesema kuwa hatua hii ni moja ya malengo 12 yaliyofikiwa kwa ajili ya kupambana na masuala ya mazingira kwani insha hizi zina elimu ya kutosha kwa rika zote husuani watoto, vijana na wazee katika kufanya maamuzi kuhusiana na mazingira.
Kaimu mkurugenzi mkuu wa TBS Egid Mubofu akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa shindano hilo walioingia fainali pamoja na majaji wa shindano hilo.
Kaimu mkurugenzi mkuu wa Shirika la Viwango Nchini (TBS) Egid Mubofu akizungumza wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano uandishi wa insha wa mazingira lililoratibiwa na Shirika la Mazingira Duniani (UNEP) kushirikiana na shirika hilo.
Afisa mwakilishi wa Shirika la Mazingira Duniani (UNEP), Clara Nakenya akizungumza wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano uandishi wa insha wa mazingira lililoratibiwa na Shirika la Mazingira Duniani (UNEP) kushirikiana na shirika hilo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

SHERIA YA MUSWADA WA HUDUMA ZA HABARI IMECHELEWA” RAIS MAGUFULI

$
0
0
Rais Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza na wahariri pamoja na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari leo, Ikulu jijini Dar es Salaam 


Na. Immaculate Makilika - MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Magufuli amesema kuwa huu ni wakati mwafaka kwa muswada wa sheria ya huduma za vyombo vya habari kukubaliwa na kuwa sheria kwa vile tasnia ya habari inakumbwa na changamoto nyingi zitakazotatuliwa na sheria hiyo.

Akizungumza na wahariri pamoja na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari leo, Ikulu jijini Dar es Salaam Rais Magufuli alisema kuwa muswada huo ni wa muda mrefu na sasa ni wakati mwafaka kwa vile tansia ya habari inakumbwa na changamoto nyingi zinazoweza kutatuliwa na muswada huo.

“Hii sheria ya huduma za vyombo vya habari imechelewa kwa vile mchakato wake ulianza tangu mwaka 2011 hadi sasa mwaka 2016 wadau walikuwa na muda wa kutosha wa kujiandaa na kutoa maoni yao ambayo yangeweza kuboresha muswada huo” alisema Rais Magufuli

Ameongeza kuwa, Sheria hii italeta mabadiliko katika tasnia ya habari kwa vile kutakuwepo na Bodi ambayo itashughulikia masuala ya taaluma ya habari, pamoja na mambo mengine yaliyoanishwa katika muswada huo ambayo ni maslahi ya waandishi wa habari nchini.

Muswada huu unatazamiwa kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili waweze kufanyakazi kitaalamu kwa kuandika na kutangaza habari zenye ukweli zitakazochangia katika harakati za kuleta maendeleo kwa nia ya kuwasaidia watanzania na serikali kwa ujumla katika kufikia malengo yake.

Muswada wa Sheria ya huduma za habari umesomwa leo Novemba 4, 2016 katika kikao cha tano cha Bunge na mkutano wa 11, ambapo utajadiliwa na kufuata taratibu zingine kabla ya kuwa sheria.

ISRAEL YAZINDUA KITUO CHA VIZA

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Prof. Jumanne Maghembe na Balozi wa Israel nchini mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Yahel Vilan wakikata utepe kuashiria kituo cha kutoa viza cha Israel kimefunguliwa rasmi. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (Mb) ambaye alikuwa Mgeni Rasmi kwenye sherehe za kufungua Kituo cha Kutoa viza za kwenda nchini Israel akiwasilisha hotuba katika ufunguzi huo. Prof. Maghembe alipongeza uamuzi wa Israel kufungua kituo hicho hapa nchini kwa kuwa kitarahisisha ziara za kwenda Israel kwa Watanzania. Aidha, alirejea kauli ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu dhamira ya Serikali ya kufungua Ubalozi nchini Israel. 

Prof. Maghembe alieleza kuwa idadi ya watalii kutoka Israel kuja Tanzania inaendelea kuongezeka na jana alikutana na wakala wa usafirishaji kutoka nchi hiyo ambao wana nia ya kuanza safari za ndege za kila wiki kutoka Israel hadi mkoani Katavi (charter flights) kutembelea maoeneo ya utalii. Ndege aina kama hiyo inafanya safari za kuja Tanzania katika mikoa ya kaskazini mara mbili kwa mwaka. Prof. Maghembe alisisitiza umuhimu wa Tanzania kushirikiana na Israel katika sekta ya teknolojia hususan mbinu za kitaalamu za kukabiliana na ujangili wa wanayamapori nchini.Kituo cha viza kitakuwa na ofisi za muda kwenye Hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. 
Balozi wa Israel nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Yahel Vilan akitoa neno la ukaribisho wakati wa sherehe za ufunguzi. Alisema anashukuru Mungu ametimiza ombi alilotoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipokutana naye Ikuku, Dar es Salaam. Mhe. Rais aliomba Serikali ya Israel ifungue Kituo cha Viza hapa nchini jambo ambalo limetia leo hii. Aliongeza kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi maarufu nchini Israel, hivyo anatarajia ahadi ya kufungua Ubalozi wa Tanzania nchini humo litatekelezwa hivi karibuni. 
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Abdallah Kilima (kushoto) akifuatilia hotuba za sherehe za ufunguzi wa kituo cha viza cha Israel .

MKUU WA WILAYA YA CHUNYA AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

$
0
0
Ziara hiyo iliambatana na ukaguzi wa Scheme ya umwagiliaji ya Ifumbo ambapo katika mradi huo kuna zaidi ya hekta 1,000 (alfu moja) zinazotumia Scheme hiyo. Mara baada ya kutembelea Scheme hiyo Mkuu huyo wa Wilaya ameonesha kuridhishwa na namna ambavyo wananchi wanatumia fursa hiyo katika kujiongezea kipato chao . 

Amesema Wananchi wa Ifumbo wanatumia kwa mazao mbalimbali yakiwemo mahindi, ufuta, kunde, mtama, alizeti, kunde pamoja na matunda. 

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya pamoja na Kamati hiyo ya Ulinzi na Usalama wamebaini kuwepo kwa changamoto kubwa ya maeneo katika mradi huo wa umwagiliwaji kukodishwa kwa watu wengine badala ya wananchi wenyewe kulitumia eneo hilo kwa ajili ya kilimo huku hekta 100 tu kati ya 1000 ndizo zinazolimwa . 

Kutokana na hali hiyo Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wananchi hao kuhakikisha wanaongeza kiwango cha Kilimo kwa kuongeza mazao kama viazi lishe ambayo yatawasaidia katika kupunguza tatizo la macho kutokana na uwingi wa vitamin A iliyomo katika viazi. 

Pia ametumia fursa hiyo kuwataka wananchi hao kutekeleze mpango wa ufyatuaji tofali kwa kila Kitongoji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati na matundu ya vyoo.
Mkuu wa Wilaya ya Chunya Rehema Madusa pamoja na kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani humo wamefanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo katika halmasahuri hiyo . 

RAIS DKT MAGUFULI AFANYA MAHOJIANO NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 04 Novemba, 2016 kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani mwaka mmoja uliopita, amefanya mahojiano na Wahariri na Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi katika ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mahojiano hayo yaliyorushwa moja kwa moja (Live) kupitia vyombo vya habari vya Redio, Televisheni na Mitandao yamechukua muda wa saa 2 na dakika 40 ambapo Rais Magufuli ametumia nafasi hiyo kujibu maswali yote yaliyoulizwa na wahariri na waandishi wa habari na ambayo yalilenga kujua utendaji kazi wa Serikali ya awamu ya tano katika kipindi cha mwaka mmoja tangu iingie madarakani.

Katika majibu yake Rais Magufuli amesema katika kipindi cha mwaka mmoja Serikali yake imehakikisha nchi inaendelea kuwa na amani, utulivu na umoja na pia imechukua hatua madhubuti za kuchochea kasi ya maendeleo zikiwemo kuongeza ukusanyaji wa mapato kutoka Shilingi Bilioni 800 hadi kufikia wastani wa Shilingi Trilioni 1.2, Kununua ndege kwa ajili ya kurahisisha usafiri na kukuza sekta ya utalii, kuongeza bajeti ya maendeleo katika bajeti ya Serikali kutoka asilimia 26 hadi kufikia asilimia 40 na kujenga miundombinu ya barabara na madaraja.

Dkt. Magufuli amezielezea hatua nyingine kuwa ni kulipa madeni ya ndani na nje ya nchi, kuongeza mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu, kuongeza fedha za kununulia dawa na chanjo, kubana matumizi kwa kuelekeza fedha nyingi katika utatuzi wa kero za wananchi na kuimarisha uhusiano na ushirikiana na nchi mbalimbali duniani kwa lengo la kuvutia uwekezaji katika viwanda, utalii, miundombinu na huduma za kijamii.

Aidha, ameongeza kuwa Serikali imeweza kutoa fedha za ruzuku kwa shule za msingi na sekondari kiasi cha shilingi Bilioni 18.77 kila Mwezi kwa ajili ya kuwezesha utoaji wa elimu bila malipo, imetoa fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 148 kwa ajili ya upanuzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa Kinyerezi I na uanzishaji wa mradi wa umeme wa Kinyerezi II.

Kufuatia hatua hizo na nyingine nyingi, Rais Magufuli amesema katika mwaka mmoja wa uongozi wake nchi imeshuhudia ukuaji mzuri wa uchumi wa wastani wa asilimia 7.9 katika robo ya pili ikilinganishwa na asilimia 7 ya mwaka jana na kupunguza mfumuko wa bei kutoka zaidi ya asilimia 7 hadi kufikia asilimia 4.5 hivi sasa.

Dkt. Magufuli amesema amedhamiria kuhakikisha Serikali inarekebisha kasoro zilizokuwa zikisababisha upotevu wa mali ya umma, vitendo vya ulaji rushwa na uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuijenga Tanzania mpya ambayo kila Mtanzania atanufaika na rasilimali za nchi yake.

Rais Magufuli ametoa wito kwa vyombo vya habari kufanya kazi zake kwa kutanguliza uzalendo, kuepuka kutumiwa na watu wenye nia ya kutetea maslai yao binafsi, kuepuka kuchochea vurugu na uvunjifu wa amani na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali kurekebisha kasoro zilizokuwa zikisababisha nchi kwenda vibaya.

Dkt. Magufuli amewapongeza Wahariri na Waandishi wa Habari kwa kazi kubwa wanayoifanya na amewaahidi kuwa Serikali yake itaendelea kushirikiana nao ili kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu utendaji kazi wa Serikali na maendeleo ya nchi yao.
  
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
04 Novemba, 2016
 






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akijibu maswali kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dkt. Ayoub Rioba wakati wa kupokea  maswali kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza mwanahabari Sammy Awami wa BBC wakati akiuliza maswali kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi w3a mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Jim Yonazi wakati akiuliza maswali kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi w3a mikutano wa Ikulu jijini Dar es  salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Mtangazaji Tido Mhando wakati akiuliza maswali kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi w3a mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Msanii Mrisho Mpoto akiimbwa wimbo wa "SIJONZE" wakati alipokutana na wahariri kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi w3a mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam.PICHA NA IKULU.



KUTOKA MAKTABA: KUAPISHWA RAIS MAGUFULI MWAKA MMOJA ULIOPITA SIKU KAMA HII

KAMBI YA UPINZANI YAUKUBALI MUSWADA WA HABARI KWA KUWEKA BIMA YA AFYA KWA WANAHABARI

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Dodoma

Kambi Rasmi ya upinzani Bungeni yaikubali Bodi ya Ithibati, Baraza Huru la Habari pamoja na Bima ya Afya kwa waandishi wa habari nchini.

Akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni mjini Dodoma, Msemaji Mkuu wa Kambi hiyo katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Joseph Mbilinyi amesema kuwa Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa 2016 unamaufaa kwa wanahabari nchini

“Kifungu cha 58 kinatoa jukumu na kuwataka waajiri wa waandishi wa habarikuhakikisha kuwa waandishi wa habari wanakuwa na bima ya afya pamoja na kuhakikisha kuwa wanachangia katika mifuko ya hifadhi za jamii” alisema Mbilimnyi.Msemaji huyo aliendelea kusema “Jambo hili ni jema sana na Kambi Rasmi ya Upinzani inaliunga mkono”.

Kuanzishwa kwa Bodi ya Ithibati pamoja na Baraza Huru la Habari ni jambo jema vitu ambavyo vitalinda maslahi ya mwandishi wa habari kwa kuzingatia kuwa moja ya kazi Baraza na Bodi ni kuweka viwango vya uangalizi pamoja na utaratibu wa kitaaluma katika kuratibu tasnia ya habari nchini.

Mbilinyi ametoa rai kwa Wabunge wote bila kujali itikadi za vyama kutambua kuwa jukumu la kutunga sheria ni wajibu wao wa kikatiba ambayo wanawajibika wakiwa sehemu ya Bunge kufanya kazi kwa maslahi mapana ya taifa.
 
Msemaji Mkuu wa Kambi Bungeni katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Joseph Mbilinyi akiwasilisha hotuba ya kambi hiyo kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa 2016.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOV 5

AGA KHAN YAWAPIGA MSASA WABUNGE, WADAU UBORESHAJI ELIMU NCHINI

$
0
0
 Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Kitilya Mkumbo akielezea kwenye mkutano wa wadau wa elimu mjini Dodoma, mambo mbalimbali yanayokwamisha maendeloeo ya elimu na jinsi ya kuiboresha. Mkutano huo ambao pia walishirikisha wabunge umeandaliwa na  Chuo Kikuu cha Aga khan (AKU).PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG.
 Mwenyekiti wa Bunge ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Zungu na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi wakisikiliza kwa makini mada kuhusu uboreshaji wa elimu nchini.

KUMBUKUMBU ZA SHEREHE YA KUAPISHWA KWA RAIS WA AWAMU YA TANO DKT JOHN POMBE MAGUFULI UWANJA WA UHURU

$
0
0

Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akila kiapo.
Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akila kiapo.
 
Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akikagua gwaride rasmi likiwa katika muundo wa Alpha kuashiria kushika madaraka ya Amiri Jeshi Mkuu.
Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akikagua gwaride rasmi likiwa katika muundo wa Alpha kuashiria kushika madaraka ya Amiri Jeshi Mkuu.

Viewing all 110129 articles
Browse latest View live




Latest Images