Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

WAFANYABIASHARA WA SIDO MBEYA WATAKA VIBANDA VYA KUDUMU SIDO...


CHAMA CHA MAPINDUZI CHAWAJIBU WAPINZANI WAKE

$
0
0
 Kwa muda sasa kumekuwepo na usambazaji wa taarifa za upotoshaji zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa wakishirikiana na baadhi ya vyombo vya habari zinazolenga kukejeli, kudhihaki, kukatisha tamaa, kubeza na kudhoofisha jitihada zinazofanywa na Chama Cha Mapinduzi na Serikali zake katika kuleta maendeleo kwa Watanzania.

Kumekuwepo na makala zinazoandikwa na magazeti mawili ya nje ambazo hutolewa kila baada ya miezi miwili na ambazo zinapotosha na kuandika habari zisizo za kweli kuhusu Tanzania.
Pia, yapo magazeti mawili ya ndani ambayo yamekuwa yakitoa makala mfululizo kwa kila wiki zinazolenga kumchafua Mheshimiwa Rais na kuichafua taswira ya nchi yetu. Kusoma zaidi BOFYA HAPA

DAWA BANDIA ZAKAMATWA KANDA YA ZIWA, NYANDA ZA JUU KUSINI

$
0
0
DAWA bandia na yasiyo sahihi kwa matumizi ya binadamu yamekamatwa maeneo ya Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kusini baada ya kufanyika ukaguzi maalum wa kutafuta dawa bandia katika maeneo hayo iliyofanyika hivi karibuni.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Bw. Hiiti Sillo wakati wa kutoa Matokeo ya ukaguzi maalum wa dawa uliofanyika katika mikoa ya Kanda za Ziwa na Nyanda za Juu Kusini.
“Kutokana na ukaguzi maalum tulioufanya katika Kanda za Ziwa pamoja na Nyanda za Juu Kusini wa kutafuta dawa bandia na zisizo sahihi kwa matumizi ya binadamu tumefanikiwa kukamata dawa bandia za aina tano ambazo zipo kwenye makundi mawili ya Dawa za malaria na Viua vijasumu(Antibiotics)” alisema Bw. Sillo.

Vijana wasomi 53 wafyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni na nyumba za walimu Shule ya SeKondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani

$
0
0
 Vijana wasomi 53  wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani, umbali wa kilomita 151 kutoka Dar es salaam, na kilomita 53 kutoka makao makuu ya Wilaya. 
Vijana hao ni wahitimu wa vyuo vikuu mbalimbali nchini  na nje ya nchi ambao wamejitolea kufnya kazi hiyo nzito bila malipo.
Vijana hao, ambao wameungana katika  grupu la Whatsapp la WAZALENDO,  leo wamekutwa wakifanya kazi hiyo nzito huku wakihamasika kwa nyimbo wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filbert Sanga (wa pili kulia). 
Vijana hao, 14 wakiwa wanawake na 39 wanaume, walikubaliana kupiga kambi shuleni hapo toka Septemba 27, 2016  na kufanya kazi hiyo ya kujitolea na bila malipo kwa moyo mmoja na kufanikiwa kufyatua matofali hayo. Kambi hiyo inatarajiwa kufungwa kesho Jumamosi Oktoba 29, 2016 na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako.
 Sehemu ya vijana hao wasomi 53 wakichota maji ili kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani
 Vijana hao wasomi 53 wakikamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani.
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filbert Sanga akipungia pamoja  na vijana hao wasomi 53 baada ya kukamilisha kufyatua matofali 45,000 kwa ajili ya mabweni matano na  nyumba tano za walimu Shule ya Sekondari ya Nasibugani wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani.




BONDIA DULLAH MBABE AMPA KICHAPO 'HEAVY' BONDIA CHENGBO ZHENG WA CHINA, AMTOA KWA 'KNOCKOUT' RAUNDI YA KWANZA

$
0
0
Bondia Abdallah  Pazi a.k.a Dullah Mbabe (78.2KG) akitangazwa mshindi mara baada ya kumpiga kwa 'KnockOut' Bondia Chengbo Zheng (77.9KG) kutoka nchini China katika raundi kwanza kabisa ya mpambano wao usiokuwa wa Ubingwa uliomalizika usiku huu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini Dar es salaam.
Bondia Abdallah  Pazi a.k.a Dullah Mbabe akimsukumia makonde mazito Bondia Chengbo Zheng kutoka nchini China na kupelekea mpambano huo kuisha ndani ya dakika mbili na sekunde kadhaa kwa 'KnockOut' ya kiufundi, katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini Dar es salaam.
Bondia Abdallah  Pazi a.k.a Dullah Mbabe akiendelea kumsukumia makonde mazito Bondia Chengbo Zheng yaliyompelekea kwenda chini na kuomba kutoendelea na mpambani huo.
Katika mambano ya utangulizi, kulikuwa na pambano hili la raundi nane lililokuwa na mvuto wa aina yake lililowakutanisha mabondia Said Mbelwa (nyeupe) na Shaban Kaoneka. hili lilikuwa na pambano la rusha nirushe, ambapo Bondia Said Mbelwa alifanikiwa kushinda kwa 'KnockOut' ya kiufundi dakika ya saba ya mpambano huo.
Bondia Paul Kamata (nyeupe) akimsukumia makonde mithili ya mvua Bondia Buta Obed katika mpambano wao usio na ubingwa wa raundi nani, ulichezwa usiku wa leo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini Dar es salaam. Bondia Paul Kamata alishinda kwa 'KnockOut' ya kiufundi, katika raundi ya tano ya mchezo hio.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 29

UKAGUZI WA MAZINGIRA UFANYIKE KATIKA KAMBI YA NYARUGUSU – MAKAMBA

$
0
0

Na Lulu Mussa -Kasulu

Imebainika kuwa ongezeko kubwa la idadi ya wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu inachangia kwa kiasi kubwa la uharibifu wa mazingira kwa kuongeza matumizi ya rasilimali za asili.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu Bw. Peter Bulugu wakati wa kuwasilisha taarifa ya hali mazingira katika kambi hiyo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba

Kaimu Mkuu wa Kambi wa Nyarugusu Bw. Peter Bulugu amesema kuwa hali ya mazingira katika kambi si nzuri na inakabiliwa na tatizo la uharibufu wa mazingira kwakuwa wengi wa wakimbizi hao hutumia kuni kama nishati ya kupikia.

Hata hivyo Bw. Bulugu amebainisha kuwa Ofisi yake imeeanda mkakati wa upandaji miti ili kunusuru maeneo yanayozunguka, na kwakuanzia jumla ya miche 900,000 imeoteshwa katika vitalu. Pia Kambi imedhamiria kugawa majiko banifu ambayo yatatumia nishati kidogo na uzalishaji wa nishati kwa kutumia takataka za mashambani unatarajiwa kuanza mwezi Novemba.

Aidha, mkakati mwingine ni ujenzi wa nyumba za tofali mbichi na kuezeka kwa mabati badala ya miti ambapo jumla ya nyumba 800 zimekamilika na nyumba 542 ziko katika hatua mbalimbali za ujenzi. Alisema Bw. Bulugu

Akiwa katika Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma, Waziri Makamba ametembelea kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu na kupata fursa ya kuongea na wawakilishi wa mashirika mbalimbali yanayotoa huduma katika kambi hiyo.

Waziri Makamba amesema kuwa ni vema uongozi na mashirika yanayotoa misaada katika kambi hiyo kuandaa mpango mzuri wa namna ya kuwapokea na kuwahifadhi wakimbizi ili ujio wao usiathiri watanzania wanaozunguka kambi ili shughuli zao za uzalishaji mali kila siku ziwe na tija.

Waziri Makamba aliuagiza Ungozi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na wakimbizi kutafuta pesa zaidi ili mpango wa kugawa majiko banifu uwafikie wakimbizi wote. “Kaya zilizopo hapa ni 30,000 ninyi mnataka kugawa majiko hayo kwa kaya 3000 tu, nashauri muangalie uwezekano wa kugawa kwa kaya zote” Makamba alisisitiza.

Waziri Makamba pia ameagiza kufanyika kwa Ukaguzi wa Mazingira (Environment Audit) ndani ya wiki mbili kwakuwa ni takwa la kisheria. Na kuwataka na kupanda miti kwa wingi. ” Pandeni miti ya aina mbalimbali mfao miti ya matunda, kuni na mbao ili kunusuru mazingira yetu”.

Waziri Makamba pia alitembelea msitu wa Makere wenye takriban ekari 75,000 ambao kwa upande wa Makere kusini kumekuwa na uharibufu mkubwa wa mazingira na kuagiza doria za mara kwa mara ili kudhibiti wananchi wanaofanya kilimo cha kuhamahama, kukata na kuchoma miti pia kudhibiti ongezeko la mifugo kwa kuiandikisha ili mgogoro uliopo baina ya hifadhi na wananchi uweze kupatiwa ufumbuzi kwa kujenga hoja madhubuti.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba hii leo ameendelea na ziara ya kukagua hali ya mazingira katika Mikoa 10 hapa nchini ambapo leo ni siku ya 13. Waziri Makamba pia atatembelea Mkoa wa Tabora.
Mbunge wa Kasulu vijijini Mhe Augustine Vuma (Kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba wakati viongozi hao walipotembelea kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu. (Katikati ni Bw. Peter Bulugu Kaimu Mkuu wa Kambi – Nyarugusu 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba akihutubia katika Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kagera Nkanda, Wilayani Kasulu 
Sehemu ya wawakilishi wa mashirika mbalimbali yanayotoa huduma katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba (hayupo pichani) mara baada ya kutembelea kutembelea kambi ya Nyarugusu na kutoa maelezo katika sekta ya mazingira
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Martin Mkisi wakikagua uharibifu wa mazingira katika msitu wa Makere katika Wilaya ya Kasulu .

Maabara ya Mkemia Mkuu Zanzibar ina nafasi kubwa ya kufanya uchunguzi unasaidia kutatua matatizo mbalimbali kiafya - Kombo

$
0
0
Na Fatma Kassim, Zanzibar.

Waziri wa Afya Zanzibar, Mahmuod Thabit Kombo amesema kuwa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ina nafasi kubwa ya kufanya uchunguzi ambao unasaidia kutatua matatizo mbalimbali kiafya katika jamii.

Amesema kutokana na kuwa Bodi hiyo inawalinda wananchi na mambo mbalimbali yanapelekea madhara ni vyema kufanya kazi kwa uwadilifu na kuishauri Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kufanya kazi kwa jitihada zote ili kuepusha matatizo ya kiafya kwa jamii.

Akizindua Bodi ya Ushauri ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Waziri wa Afya ameitaka bodi hiyo  kuandaa mipango madhubuti itakayosaidia kuondosha mapungufu inayowakabili Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

Amesema kutokana na kuwa maabara hiyo inafanya uchunguzi wa mambo mbalimbali ikiwemo vyakula,vinywaji na dawa za binaadamu pamoja na kudhibiti kemikali zinatumiwa viwandani na majumbani hivyo amewataka kufanya kazi kwa mashirikiano na taasisi mbalimbali ikiwemo bodi ya chakula dawa na vipodozi na shirika la viwango.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dk Yussuf Nuhu  Pandu amesema watahakikisha wanafakazi  kwa mujibu wa sheria zilizowekwa ili kuweza kufanikisha maabara ya Mkemia Mkuu  wa Serikali kufanyakazi zake kwa uadilifu.

Amesema kutokana na kazi za Maabara ni kulinda afya za Wazanzibar pamoja na mazingira yao kwa kuchunguza ubora wa chakula na kemikali watafanya kila jitihada kuona mambo hayo yanafanyika .

Nae Mkemia Mkuu  wa Maabara ya Serikali Dk Slim Rashid Juma amesema wameweza kupata mafanikio mbalimbali ikiwemo kuwa na sheria ya maabara namba 10 ya mwaka 2011 inayoipa maabara hadhi ya wakala wa Serikali.

Mafanikio  mengine ni Serikali kuwapatia majengo matatu katika eneo la Maruhubi Unguja  na jengo jengine eneo la Madungu Pemba kwa matumizi ya maabara.

Amesema licha ya mafanikio hayo pia wanakabiliwa na changamoto na uchakavu na uchache wa vifaa na mashine za kufanyia uchunguzi pamoja na uchache wa kemikali ambalo linashusha utendaji wa kazi za maabara.

TAASISI YA OCEAN ROAD YAFANYA MATEMBEZI YA HISANI KUCHANGIA SARATANI YA MATITI JIJINI DAR

$
0
0
TAASISI ya Saratani ya Hospital ya Ocean Road leo imefanya matembezi ya hisani kwa lengo la Kuhamasisha na kuchangia zaidi ya milioni 120 zinazohitajika kwa ajili ya kununua vifaa tiba vya chemotherapy.

Matembezi hayo yalianzia Hospitali ya Ocean road na kumalizika hapo hapo huku wakizunguka moja ya barabara za jiji la Dar es Salaam huku Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Hamis Kigwangala akiwa ni mgeni rasmi.
Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Hamis Kigwangala akizungumza mara baada ya kumaliza matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa saratani ya matiti yaliyoandaliwa na Taasisi ya Saratani ya Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam ambapo huu ni mwaka wa nne tokea yameanzishwa. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Mmoja ya wagonjwa ambaye amepona saratani ya matiti akitoa ushuhuda mbele ya wageni.

BBC DIRA YA DUNIA IJUMAA 28.10.2016

Happy Birthday Mr.President!

$
0
0
Leo 29 Oktoba ndio siku ya Kuzaliwa Rais wetu Dkt.John Pombe Joseph Magufuli. Inawezekana mheshimiwa Rais wetu labda siku hii anaichukulia ya kawaida tu au ya kifamilia tu, kwa kuwanmuheshimiwa si mtu wa kupenda penda ufahari na masherehe. Sikushangaa kumuona leo kavamia Wizara ya Maliasili na Utalii kushuhudia meno ya tembo 50 yaliyokamatwa na kikosi kazi cha kuzuia ujandili. Pia akamtumbua Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya Jinai (DCI) Athumani Diwani badala ya kukata keki. Lakini pamoja na hayo sisi Watanzania ni lazima tumtakie na kumuombea kila la heri, afya njema Rais wetu  mpendwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika siku ya kuzaliwa - Happy Birthday Mr. President!! YOU ROCK!!
- From Ngoma Africa Band in Germany

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA OFISI YA RAIS MENEJIMENT YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA

RC SINGIDA: MASHINDANO YA IKUNGI HALF MARATHON 2016 YAMEUPA HESHIMA MKOA WA SINGIDA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi Mathew Mtigumwe akiwapongeza washiriki waliomaliza kwa wastani mzuri wa muda, kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu
Bi Zaibabu Ramadhani mwenye umri wa miaka 47 akiwasili Katika uwanja wa Shule ya Sekondari Ikungi kumalizia kilomita 21
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi Mathew Mtigumwe akisalimia na Felix Simbu kijana wa Kitanzania aliyeshika nafasi ya tano katika mashindano ya Olimpiki nchini Brazil mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Ikungi kwa ajili ya kuhamasisha Ikungi Half Marathon 2016
Washiriki wa mbio fupi za Mita 100 wakipokea maelekezo ya Mkufunzi wa Ikungi Half Marathon 2016.

MCHAPALO WA MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA SERENGETI PREMIUM LAGER WAFANA

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa SBL Helene Weesie akitoa hotuba ya  ufunguzi kwa wageni waliohudhuria tafrija mchapalo ya maadhimisho ya miaka 20  tangu kuanzishwa kwa bia ya Serengeti Premium Lager (SPL)  mwaka 1996.Pia kulizinduliwa chapa mpya ya Bia hiyo  .hafla hiyo ilifanyika siku ya alhamisi  katikahoteli ya Kilimanjaro  Hyatt Regency Jijini Dar es salaam

Mgeni Rasmi Waziri Wa Viwanda, Biashara  Na Uwekezaji, Mh. Charles Mwijage (Mb) akitoa hotuba kwa wageni waliohudhuria hafla ya kutimiza miaka 20 ya bia ya Serengeti premium lager .Hafla ilifanyika katika Hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar Es salaam.


Mwenyekiti wa Bodi ya SBL Nehemiah Mchechu akitoa hotuba yake katika hafla ya kutimiza miaka 20 ya Bia ya Serengeti Premium Lager na pia kuzinduliwa kwa muonekano mupyaa wa bia hiyo mapema siku ya alhamisi.

Wageni waalikwa katika hafla hiyo wakifurahia jambo

Mkurugenzi Mkuu wa SBL Helene Weesie (katikati) akijadiliana jambo na Mkurungezi wa Mawasiliano wa SBL John Wanyacha na Mkurungezi wa Masoko wa SBL Ceasar Mloka katka tafrija mchapalo ya kutimiza miaka 20 ya bia ya Serengeti Premium Lager
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

SHIWATA yandaa mashindano

$
0
0

MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA)umeandaa mashindano ya Sanaa na Michezo litakalofanyika kuanzia Novemba 12,2016 katika viwanja
mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa SHIWATA,Cassim Taalib alisema jana kuwa michezo
itakayoshindaniwa ni soka,mpira wa kikapu,ngoma za asili, muziki wa
dansi, sarakasi, Karate na kaswida.

Alisema mashindano hayo yatafanyika kuwapata washindi ambao kwa pamoja watakwenda kukabidhiwa zawadi zao kwenye kijiji cha wasanii
Mwanzega,Mkuranga.

Mwenyekiti Taalib aliwataja wajumbe wa Kamati ya tamasha hilo kuwa ni
Deo Kway, na mchezaji wa zamani wa Simba, Kureshi Ufunguo na mchezaji
wa zamani wa Yanga, Salvatory Edward watakaosimamia mashindano ya
soka.

Wengine ni Selemani Pembe, Athumani Bakari maarufu kama Mbegeja katika mchezo wa sarakasi,Abdul Salvador kamati ya muziki wa dansi na Kocha wa timu ya Taifa ya Mpira wa Kikapu, Manase Zablon katika mchezo wa mpira wa kikapu.

Wajumbe wengine ni Ismail Kambangwa, Kashindye Fundikira na Mariam
Ismail maarufu kama mama Mipango watakaosimamia ngoma za asili.

KAMATI YA BUNGE YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII YAENDELEA KUUJADILI MUSWADA WA SHERIA YA HABARI YA MWAKA 2016

PROGRAMU YA JIANDALIE AJIRA YAZINDULIWA RASMI

$
0
0

Na Ally Daud-MAELEZO. 

Mfuko wa Kimataifa wa Vijana( Interanational Youth Foundation) imezindua rasmi programu mpya ya miaka mitano wa JIANDALIE AJIRA unaowalenga vijana hapa nchini kama moja ya jitihaha za kukuwajengea vijana mafunzo ya ufundi stadi na ujasiriamali kuondokana na tatizo la ajira . 

Akizindua programu hiyo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Technolojia ,Mhandisi Stella Manyanya alisema program hiyo ni ukombozi mkubwa kwa vijana hapa nchini kwa kuwa itawawezeshae kutengEneza ajira na kukuza uchumi. 

“Programu hii imekuja kutengneza vijana kuwa wabunifu na kutengneza ajira ikiwa ni pamoja na kuajiri wengine na siyo kuwa wasaka ajira,”na kwa kufanya hivyo taifa litapiga hatua kiuchumi,aliongeza kusema,Mhandisi huyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nyasa” alisema Mhandisi Manyanya 

Aidha Mhandisi Manyanya aliupongeza mfuko huo wa IYF kwa kuja na mradi ambao utatekelezwa kwa ushirikiano na Taasisi ya Ujasirimali na Ushindani (TECC), Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) na Shirika lisilokuwa la kiserikali la The MasterCard Foundation. 

Mhandisi Manyanya alisema pia programu hiyo itawezesha kuwaandaa wakufunzi wa chuo cha VETA ili waweze tumika katika kuwafundisha vijana ambao ndio walengwa katika mradi mzima na ambao wanachangamoto kubwa ya ajira. 

Mbali na hayo Mhandisi Manyanya alikitaka chuo hicho kuendeleza na kupanua wigo wa ushirikiano na waajiri ili kujenga nguvu kazi kukidhi matwakwa ya soko la ajira kwenda sambana na dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025. 

Naibu Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya (kulia) akikata utepe wakati uzinduzi wa program ya JIANDALIE AJIRA inayolenga kupunguza tatizo la ajira nchini. Wengine katika picha ni Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Kimataifa wa Vijana (IYF), Bw. William Reese (wa pili kulia), Mwenyekiti wa bodi wa Taasisi ya Ujasiriamali na Ushindani TECC Bi. Beng’I Issa (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ujasiriamali na Ushindani, Bw. Sosthenes Sambua (wa pili kushoto) na Ahmed Makbel Mkurugenzi Msaidizi wa Ajira kutoka ofisi ya Waziri Mkuu (katikati).
Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa wa Mfuko wa Kimataifa wa Vijana (IYF), Bw. William Reese, akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa program ya Jiandalie Ajira jana jijini Dar es Salaam, wengine katika picha ni Mwenyekiti wa bodi wa Taasisi ya Ujasiriamali na Ushindani (TECC) Bi. Beng’I Issa (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa (TECC) Sosthenes Sambua katikati, program hiyo ili zinduliwa na Naibu Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya kwenye ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam jana.

TAREHE 21,OCTOBER 2016 KIPINDI CHA RAIS MAGUFULI KWENYE SIKU YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI

WANASHINYANGA WAOMBA KIWANDA CHA KUTENGENEZA MKAA RAFIKI KWA MAZINGIRA KATIKA SIKU YA USAFI KITAIFA

$
0
0

EVELYN MKOKOI-SHINYANGA

Uongozi wa mkoa wa Shinyanga kupitia Mkuu wa Wilaya yake Bi Josephine Matiru umeiomba serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais Kujenga kiwanda kitakacho tengeneza mkaa utokanao na mabaki ya miti ambao ni rafiki kwa mazingira ili kunusuru hali ya mkoa huo kuendelea kuwa jangwa kutokana na ukataji miti ovyo kwa matumizi ya makaa manyumbani, matumizi mengine na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.

Mkuu wa wilaya hiyo ametoa ombi hilo leo mbele ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina aliposhiriki siku ya usafi kitaifa ya mwisho wa mwezi October ambapo zoezi hilo lilizinduliwa rasmi na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania December Mwaka jana na kuendelea kutekelezwa kila jumamosi ya mwisho wa mwezi kama siku maalum ya usafi nchini.

Bi Materu aliendelea kusema kuwa, Mkoa wa shinyanga unakumbana na changamoto kubwa ya ukataji miti ovyo ambayo ingeweza kukabiliwa kwa kutumia mabaki ya miti, taka na maranda ya mbao kutengeneza mkaa rafiki kwa mazingira na kusema kuwa mkoa na wilaya ya shinyanga imebarikiwa kuwa na miti ya aina mbali mbali ambazo mazingira yangetunzwa vizuri na kutumia malighafi hiyo ya taka kutengeneza mkaa banifu akitolea mfano kiwanda cha kutengeneza mkaa rafiki wa mazingira cha Zanzibar.
 Baadhi ya wakazi wa Mji wa Shinyanga wakishiriki katika zoezi la usafi wa mazingira leo, Mjini Shinyanga. 
 Katikati Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, Kushoto Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Bi Josephine Matiru,  na Bwana Daniel Sagata Pamoja wakijiandaa kuanza zoezi la usafi wa mazingira katika eneo la Binzatana Mjini Shinyanga mapema leo. 
 Naibu Waziri Ofisi ya makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luahaga Mpina akishiriki katika zoezi la kupanda miti Mjini Shinyanga leo

WORLD BANK LAUNCHES HIGHER EDUCATION CENTERS OF EXCELLENCE IN EIGHT EASTERN AND SOUTHERN AFRICAN COUNTRIES

$
0
0




The $140 million project will help raise quality and relevance of the region’s post-graduate education in five priority sectors

Inter-University Council for East Africa; Nairobi, Kenya; 26 October 2016: The Eastern and Southern Africa Higher Education Centers of Excellence Project (ACE II) – which seeks to strengthen 24 competitively selected centers to deliver quality, market-relevant post-graduate education in Eastern and Southern Africa – was launched in Nairobi by the Inter University Council for East Africa (IUCEA) and the World Bank.

The five-year project will work to build collaborative research capacity in five regional priority areas: industry (Science, Technology, Engineering and Mathematics), agriculture, health, education and applied statistics. The $140 million project is financed by the World Bank in form of credit to eight participating countries. These include Ethiopia, Kenya, Malawi, Mozambique, Rwanda, Tanzania, Uganda, and Zambia. IUCEA, an East African Community institution responsible for coordinating the development of higher education will facilitate and coordinate the project.

Hon. Fred Matiangi, Kenya’s Cabinet Secretary for Education, in his remarks to the participating country delegates, thanked the World Bank for its support for the education sector. He also called on all governments to end bureaucratic delays that slow project implementation. 

“We don’t get any useful results from being bureaucratic. Governments should not be a hurdle; they should be a facilitating entity.” Dr. Sajitha Bashir, World Bank’s Practice Manager for its Education Global Practice, said that the Bank sees this as a broader effort to build technical and scientific capability for Africa’s socio-economic transformation. “Without these highly specialized professional skills and without that critical mass, we don’t think that Africa can transform itself,” she said. 

Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images